ibra87
R I P
- Jul 22, 2015
- 5,614
- 5,360
- Thread starter
- #701
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 074
Ilikuwa hivyo na ikawa hivyo. Ndimi zao zikakutana huku chini ya sakafu damu ikichuruzika. Harufu ya damu ilikuwa imetawala eneo hilo, harufu ambayo waliipenda na hata kuwavutia. Hawakuogopa damu wala hawakuziogopa maiti. Bado walikumbatiana wakiburudika na kuburudika. Lakini haikuchukua muda wakaachiana. Walikumbuka kuwa wapo kazini. Wapo katika kazi hii ya kifo. Kazi ambayo ilikuwa ikitembea na vifo vyao mikononi. Naam! Huu ulikuwa muda wa kumfuata mtu huyu, muda wa kumfuata mtu yule ambaye muda mfupi uliopitwa alikuwa akishurutishwa aujue na kuusema ukweli. Nilazima wajue kwa nini Askofu alimtaka Teddy afike pale. Ilikuwa ni lazima wamjue na kutambua hilo. Kila mmoja akapiga hatua kuelekea chumba kile, chumba ambacho sauti ya mtu ulikuwa akisikika. Kuingia hapo wakapokelewa na Dimbwi la damu. Juu yake alikuwa amelala mtu, alilala mtu ambaye kwa kumuangalia tu, ungejua huyu atakuwa ni marehemu. Hatua za umakini zikafuatia, hatua za kuelekea ulipolala mwili. Wakaufikia mwili wa mtu yule ambaye alikuwa uchi wa mnyama. Wakatizamana tena huku kila mmoja akiwa makini. Huku kila mmoja akiwa tayari kwa kuifyatua Risasi. Wakaugeuza mwili wa mtu huyu waweze kuufahamu. Wakafanikiwa kuugeuza, kila mmoja macho yakamtoka baada ya kuiona sura ya huyu Marehemu. Hakuna aliyekiamini kile alichokuwa akikiangalia. Macho yao yalikuwa yakitizama sura ya Sheikh mkuu wa mkoa. Hata huyu kisu kikubwa kilikuwa kimesimama tumboni. Kila mmoja akainua macho. Wakaangaliana kwa muda. Baba Askofu, na sasa alikuwa ameuawa Sheikh Mkuu Wa Mkoa. Kuna nini hapa? Ni swali ambalo lilipenya kichwani kwa Teddy. Swali ambalo lilimfanya amuangalie Masimba kwa Mara nyingine. Akimuangalia akihitaji kupata majibu. Majibu ya kile ambacho kimejificha nyuma ya Vifo vya watu hawa. Alitaka kujua kwa nini aliagizwa na Masimba kwenda kumuondoa mtu nyumbani pale kwa Baba Askofu. Hata Masimba akamuangalia kwa Umakini. "Haya ndiyo malipo ya Tamaa. Kilichofanyika kwa watu hawa ni kuzibwa midomo yao ili wasikutane nasi." Aliongea Masimba akiwa bado anamuangalia yule marehemu. Jibu la masimba lilionekana kumshangaza Teddy. Lilimshangaza kwa kuwa hakuwahi kuwaona watu hawa katika biashara kipindi yupo huku. Sasa hii tamaa anayosema Masimba ni Ipi? Lilikuwa swali lililofanya amtizame tena Masimba. "Najua hujawahi kuwaona watu hawa ndio maana unashangaa, lakini Mengi utayaona kwenye Hiyo bahasha uliopewa. Tunatakiwa kuondoka hapa. Huu mchezo nadhani kuna mtu ndani ya Ikulu anaucheza. Lazima tuwe makini na lazima Tuondoke hapa. Aliongea Masimba huku akiuvuta mkono wa Teddy ili kuondoka hapo. Teddy akafuata kama kondoo. Akili yake ilikuwa imesimama kwa muda kutokana na maneno haya kutoka kwa Masimba, maneno kwamba watu hawa ni wa moja katika biashara hii. Kwamba watu hawa nao walikuwa kundi moja na Jimmy na hata Waziri? Kwamba Baba Askofu alikuwa Mmoja wa wana kikundi? Kwamba Sheikh Mkuu wa mkoa alikuwa ni mmoja katika hili? Akaitamani ndoto. Ndoto ya kumtoa katika hili. Aliiona Dunia Jinsi ilivyokuwa ikiwapoteza watu. Akiwaaangamiza katika Matendo mabaya. Kwa mara nyingine akataka kumuuliza Masimba. Kumuuliza kuhusu ukweli huu. Kuhusu hili linalotokea. Lakini macho ya Masimba yakauziba mdomo wake. Macho ya Masimba yalikuwa yakimzindua kutoka katika hili. Kutoka katika lindi la mawazo alionayo. Alitakiwa katika utimamu wa kimwili na hata kiakili. Alitakiwa katika umakini wake wa siku zote. " Alitakiwa kurudi kuwa Teddy kama Teddy. Ilikuwa hivyo na akawa hivyo.
********
Walikuwa wawili ndani ya chumba kimoja, walikuwa wamejiinamia kila mmoja akiwaza kile ambacho kiliutawala ubongo wake kwa wakati huo. Wakati Teddy akiwaza mkanganyiko na mambo yanavyozidi kumshangaza. Masimba alikuwa akiwaza kile kilichopo ndani ya Ile Bahasha. Bahasha ambayo Teddy alipewa na Askofu Ibrahim Lexandre Rengima. Ingawa hakuwa ameifungua kwa kipindi kile lakini aliuhisi usiri mzito kuwepo ndani ya bahasha hili. Kama sheikh mkuu wa mkoa na Baba askofu walikuwa washiriki katika biashara ile, alihisi kuwepo kwa watu wengine wazito kupindukia. Kuiona Gari yenye nembo ya Ikulu sehemu zote mbeli, kisha kuwakuta wahusika wameuawa hii ilitoa picha kuwa hata ndani ya Ikulu kuna watu ambao wapo nyuma ya Biashara hii. Kitendo cha Idara ya Ujasusi kubadilika na kutotaka kuwaunga mkono katika hili ilimaanisha kwamba kuna kitu kizito ambacho hatakiweza Peke yake. Alitambua wanaweza kuuawa muda wowote na kushindwa kuimaliza kazi hii. Kama ikulu inatumika katika hili hii ilionyesha kuwa ilikuwa Hatari kubwa sana kwa upande wao. Hilo likamfanya amkumbuke rafiki yake, Rafiki ambaye walikuwa wote katika purukushani za kuchunguza kifo cha mke wa Rais. Mkasa ambao hautakaa usahaurike maishani kwake hasa baada ya kuigundua njama ya kutaka kumpindua Rais alieko madarakani kwa Wakati. Alikuwa amemkumbuka mwanaharamu, alikuwa amemkumbuka Nemisis The Bastard. Mwanausalama mwenzake Raia Wa Africa ya Kusini. Alimkumbuka katika aina fulani ya kuuhitaji msaada zaidi. Msaada wa kiuchunguzi na hata kuwasafirisha watu kuzimu. Hilo akalipitisha kichwani kwake. Lakini kabla hajamwambia alitaka kukijua kile ambacho kilikuwemo ndani ya Bahasha kutoka kwa baba Askofu. Kwa mara ya kwanza Masimba akainua uso wake, macho yake yakamtizama mwandani wake aliyekuwa pembeni yake akionekana kusafiri umbali mrefu kimawazo. Hakuwa hapo na hakuonekana kuwepo Hapo. Teddy alikuwa amesafiri umbali mrefu kimawazo. Akamsogelea na kumkumbatia kwa mapenzi yote. Kwa upendo wote na hata mahaba yote. Taratibu macho yao yakatizamana. Yakaangaliana na kuangsliana. Macho ya Teddy yaliijenga hofu, macho ya Teddy yalionyesha kuhofu kitu. Hilo lilikuwa jipya moyoni kwa masimba na Hata machoni. Teddy alikuwa akiogopa na Teddy alikuwa akihofia. Teddy alikuwa katika hofu, mduao na hata Bumbuwazi. Teddy anaogopa? Teddy ana hofu? Ameianza lini hii? Akajiswali mwenyewe pasipo majibu ya aina yoyote. "Teddy umeanza kuogopa? Umeanza lini kuwa muoga?. Aliuliza Masimba huku akimuangalia kwa umakini. Teddy hakujibu bali aliinua macho zaidi na kumuangalia masimba. Midomo yake ilikuwa ikicheza kutaka kuongea kitu lakini haikuwa hivyo. Hakuongea wala hakufumbua mdomo. Hata hili lilimshangaza Masimba, hata hili hakulitegemea. Teddy kushindwa kuongea? Hapana hawezi kuwa Teddy. Alijisemea mwenyewe huku akimtizama Zaidi. "Dady Nahisi Ikulu inahusika katika mapambano haya. Nahisi kuna kitu ikulu ama watu wanaoishi ikulu wapo nyuma ya hii biashara. Na kama ni kweli huioni hatari mbele yetu? Nadhani umeiona gari yenye nembo ya ikulu ikielekea pale nyumbani kwa Sheikh mkuu, na pia nadhani umewaona wana usalama ambao walikuwepo eneo lile tena kwa siri kubwa sana. Hii inaonyesha nini kwetu?" Aliongea Teddy huku akishindwa kuificha hofu. Hofu ambayo ilichukua nafasi kubwa usoni. "Ni kweli nimeona kila kitu, na hata hii gari yenye nembo ya Ikulu ulipishana nayo kidogo tu pale nyumbani kwa Baba Askofu. Hii inaonyesha watu hawa waliouawa ilitakiwa kuwa hivyo kabla hawajaingia mikononi mwetu. Kwahiyo kilichopo sasa hivi ni kutafuta na kujua ni nani ambaye alikuja na ile gari. Na tukishalifahamy hilo tutamtafuta mhusika." Aliongea masimba huku akikilaza kichwa cha Teddy kifuani. "Kwa nini Ulinituma nikamuue Baba Askofu?. Akauliza Teddy kwa mara nyingine huku akiuvaa uso wa kazi. "Nilikutuma kwa kuwa Alikuwa mmoja kati ya wahusika wakuu katika Biashara hii." Akajibu Masimba kwa Utulivu. "Ulijuaje hilo?" Akauliza tena. Ni swali hilo lililoubadirisha uso wa masimba. Sasa alikuwa akimtizama Teddy kwa macho ya sio na utani. Swali lake lilikuwa la kitoto kwa mtu mwenye uzoefu wa kiusalama kama yeye. "Swali gani la kitoto hilo unaloniuliza? Kwa hiyo mimi naweza kubuni tu kuwa mtu fulani anafanya biashara hii? Unajua kwa nini amekupa hiyo bahasha na kukwambia uilete kwangu?" Aliongea masimba kwa kufoka huku akimuangalia teddy. "Sio kwamba ni swali la kitoto, nimeuliza kwa kuwa kuwa kuwa kwangu kule sikuwahi kuwaona hata siku moja katika mikutano yetu." Akajibu Teddy kwa upole huku akikichezea kifua cha Masimba. "Naomba bahasha hiyo tuifungue, lakini tambua hii vita sasa tunapigana Na taasisi ya Urais. Kama gari za Ikulu zinatumika katika haya huku tunakoelekea ni kubaya. Usiikubali hofu ichukue sehemu kubwa katika Maisha yako. Hii ni vita ambayo inaweza kutupoteza na kutufuta katika Dunia hii. Licha ya kutufuta kwenye uso huu, lakini pia hatutokuwa na chochote cha kutukumbuka. Unatakiwa uitoe hofu na kuitokomeza. Ujuzi tulio nao utusaidie kutufikisha katika mwisho wa hii safari." Aliongea masimba kwa kirefu. Maneno yake yakamuingia Teddy na kumsisimua. Ulikuwa wakati wa kupambana, ulikuwa wakati wa kutumia ujuzi wao wote kuhakikisha hili linafika mwisho. Kwa nini awe na Hofu? Kwa nini aogope? Tokea lini yeye akaogopa Risasi? Tokea lini yeye akakiogopa kifo? Akazidi kujilaza kifuani kwa Masimba. "Nipo tayari Kupambana Dady? Nipo tayari kufanya kila kitu kwa sababu yako na sababu ya nchi yangu." Aliongea Teddy katika namna ambayo ilimsisimua. Muda wote huo hakuwa ameitoa Bahasha, hakuwa ameitoa kwa kuwa hakuambiwa afanye hivi. Akapeleka mkono mahali ambapo aliihifadhi Bahasha. Akaitoa na kumkabidhi masimba. Wakati masimba akitaka kuifungua Bahasha, simu yake ya Mkononi ikaita. Akatulia kwanza akimuangalia teddy machoni. Teddy naye akamkazia macho huku wivu ukionekana Shahiri machoni mwake. Alikuwa akihisi labda mpigaji ni Mwanamke. Masimba akaitoa Simu Mfukoni kwake, kabla ya kuipokea akatizama jina la mpigaji.. Major General Chomboko. Haraka akaipokea simu. "Utahitajiwa Ikulu Muda huu, lakini Make sure kabla hujaondoka hapo ulipo unaweka vizuri hiyo Bahasha. Ikipotea Hiyo basi Hata wewe Hutakuwa na Njia ya Kujinasua." Aliongea Major General Chomboko. Kisha pasipo kusubiri chochote. SIMU IKAKATWA.
MASIMBA AKAMTIZAMA TEDDY NA HATA TEDDY AKAMTIZAMA MASIMBA.
BADO KAZI YAO ILIKUWA NGUMU
SEHEMU YA 074
Ilikuwa hivyo na ikawa hivyo. Ndimi zao zikakutana huku chini ya sakafu damu ikichuruzika. Harufu ya damu ilikuwa imetawala eneo hilo, harufu ambayo waliipenda na hata kuwavutia. Hawakuogopa damu wala hawakuziogopa maiti. Bado walikumbatiana wakiburudika na kuburudika. Lakini haikuchukua muda wakaachiana. Walikumbuka kuwa wapo kazini. Wapo katika kazi hii ya kifo. Kazi ambayo ilikuwa ikitembea na vifo vyao mikononi. Naam! Huu ulikuwa muda wa kumfuata mtu huyu, muda wa kumfuata mtu yule ambaye muda mfupi uliopitwa alikuwa akishurutishwa aujue na kuusema ukweli. Nilazima wajue kwa nini Askofu alimtaka Teddy afike pale. Ilikuwa ni lazima wamjue na kutambua hilo. Kila mmoja akapiga hatua kuelekea chumba kile, chumba ambacho sauti ya mtu ulikuwa akisikika. Kuingia hapo wakapokelewa na Dimbwi la damu. Juu yake alikuwa amelala mtu, alilala mtu ambaye kwa kumuangalia tu, ungejua huyu atakuwa ni marehemu. Hatua za umakini zikafuatia, hatua za kuelekea ulipolala mwili. Wakaufikia mwili wa mtu yule ambaye alikuwa uchi wa mnyama. Wakatizamana tena huku kila mmoja akiwa makini. Huku kila mmoja akiwa tayari kwa kuifyatua Risasi. Wakaugeuza mwili wa mtu huyu waweze kuufahamu. Wakafanikiwa kuugeuza, kila mmoja macho yakamtoka baada ya kuiona sura ya huyu Marehemu. Hakuna aliyekiamini kile alichokuwa akikiangalia. Macho yao yalikuwa yakitizama sura ya Sheikh mkuu wa mkoa. Hata huyu kisu kikubwa kilikuwa kimesimama tumboni. Kila mmoja akainua macho. Wakaangaliana kwa muda. Baba Askofu, na sasa alikuwa ameuawa Sheikh Mkuu Wa Mkoa. Kuna nini hapa? Ni swali ambalo lilipenya kichwani kwa Teddy. Swali ambalo lilimfanya amuangalie Masimba kwa Mara nyingine. Akimuangalia akihitaji kupata majibu. Majibu ya kile ambacho kimejificha nyuma ya Vifo vya watu hawa. Alitaka kujua kwa nini aliagizwa na Masimba kwenda kumuondoa mtu nyumbani pale kwa Baba Askofu. Hata Masimba akamuangalia kwa Umakini. "Haya ndiyo malipo ya Tamaa. Kilichofanyika kwa watu hawa ni kuzibwa midomo yao ili wasikutane nasi." Aliongea Masimba akiwa bado anamuangalia yule marehemu. Jibu la masimba lilionekana kumshangaza Teddy. Lilimshangaza kwa kuwa hakuwahi kuwaona watu hawa katika biashara kipindi yupo huku. Sasa hii tamaa anayosema Masimba ni Ipi? Lilikuwa swali lililofanya amtizame tena Masimba. "Najua hujawahi kuwaona watu hawa ndio maana unashangaa, lakini Mengi utayaona kwenye Hiyo bahasha uliopewa. Tunatakiwa kuondoka hapa. Huu mchezo nadhani kuna mtu ndani ya Ikulu anaucheza. Lazima tuwe makini na lazima Tuondoke hapa. Aliongea Masimba huku akiuvuta mkono wa Teddy ili kuondoka hapo. Teddy akafuata kama kondoo. Akili yake ilikuwa imesimama kwa muda kutokana na maneno haya kutoka kwa Masimba, maneno kwamba watu hawa ni wa moja katika biashara hii. Kwamba watu hawa nao walikuwa kundi moja na Jimmy na hata Waziri? Kwamba Baba Askofu alikuwa Mmoja wa wana kikundi? Kwamba Sheikh Mkuu wa mkoa alikuwa ni mmoja katika hili? Akaitamani ndoto. Ndoto ya kumtoa katika hili. Aliiona Dunia Jinsi ilivyokuwa ikiwapoteza watu. Akiwaaangamiza katika Matendo mabaya. Kwa mara nyingine akataka kumuuliza Masimba. Kumuuliza kuhusu ukweli huu. Kuhusu hili linalotokea. Lakini macho ya Masimba yakauziba mdomo wake. Macho ya Masimba yalikuwa yakimzindua kutoka katika hili. Kutoka katika lindi la mawazo alionayo. Alitakiwa katika utimamu wa kimwili na hata kiakili. Alitakiwa katika umakini wake wa siku zote. " Alitakiwa kurudi kuwa Teddy kama Teddy. Ilikuwa hivyo na akawa hivyo.
********
Walikuwa wawili ndani ya chumba kimoja, walikuwa wamejiinamia kila mmoja akiwaza kile ambacho kiliutawala ubongo wake kwa wakati huo. Wakati Teddy akiwaza mkanganyiko na mambo yanavyozidi kumshangaza. Masimba alikuwa akiwaza kile kilichopo ndani ya Ile Bahasha. Bahasha ambayo Teddy alipewa na Askofu Ibrahim Lexandre Rengima. Ingawa hakuwa ameifungua kwa kipindi kile lakini aliuhisi usiri mzito kuwepo ndani ya bahasha hili. Kama sheikh mkuu wa mkoa na Baba askofu walikuwa washiriki katika biashara ile, alihisi kuwepo kwa watu wengine wazito kupindukia. Kuiona Gari yenye nembo ya Ikulu sehemu zote mbeli, kisha kuwakuta wahusika wameuawa hii ilitoa picha kuwa hata ndani ya Ikulu kuna watu ambao wapo nyuma ya Biashara hii. Kitendo cha Idara ya Ujasusi kubadilika na kutotaka kuwaunga mkono katika hili ilimaanisha kwamba kuna kitu kizito ambacho hatakiweza Peke yake. Alitambua wanaweza kuuawa muda wowote na kushindwa kuimaliza kazi hii. Kama ikulu inatumika katika hili hii ilionyesha kuwa ilikuwa Hatari kubwa sana kwa upande wao. Hilo likamfanya amkumbuke rafiki yake, Rafiki ambaye walikuwa wote katika purukushani za kuchunguza kifo cha mke wa Rais. Mkasa ambao hautakaa usahaurike maishani kwake hasa baada ya kuigundua njama ya kutaka kumpindua Rais alieko madarakani kwa Wakati. Alikuwa amemkumbuka mwanaharamu, alikuwa amemkumbuka Nemisis The Bastard. Mwanausalama mwenzake Raia Wa Africa ya Kusini. Alimkumbuka katika aina fulani ya kuuhitaji msaada zaidi. Msaada wa kiuchunguzi na hata kuwasafirisha watu kuzimu. Hilo akalipitisha kichwani kwake. Lakini kabla hajamwambia alitaka kukijua kile ambacho kilikuwemo ndani ya Bahasha kutoka kwa baba Askofu. Kwa mara ya kwanza Masimba akainua uso wake, macho yake yakamtizama mwandani wake aliyekuwa pembeni yake akionekana kusafiri umbali mrefu kimawazo. Hakuwa hapo na hakuonekana kuwepo Hapo. Teddy alikuwa amesafiri umbali mrefu kimawazo. Akamsogelea na kumkumbatia kwa mapenzi yote. Kwa upendo wote na hata mahaba yote. Taratibu macho yao yakatizamana. Yakaangaliana na kuangsliana. Macho ya Teddy yaliijenga hofu, macho ya Teddy yalionyesha kuhofu kitu. Hilo lilikuwa jipya moyoni kwa masimba na Hata machoni. Teddy alikuwa akiogopa na Teddy alikuwa akihofia. Teddy alikuwa katika hofu, mduao na hata Bumbuwazi. Teddy anaogopa? Teddy ana hofu? Ameianza lini hii? Akajiswali mwenyewe pasipo majibu ya aina yoyote. "Teddy umeanza kuogopa? Umeanza lini kuwa muoga?. Aliuliza Masimba huku akimuangalia kwa umakini. Teddy hakujibu bali aliinua macho zaidi na kumuangalia masimba. Midomo yake ilikuwa ikicheza kutaka kuongea kitu lakini haikuwa hivyo. Hakuongea wala hakufumbua mdomo. Hata hili lilimshangaza Masimba, hata hili hakulitegemea. Teddy kushindwa kuongea? Hapana hawezi kuwa Teddy. Alijisemea mwenyewe huku akimtizama Zaidi. "Dady Nahisi Ikulu inahusika katika mapambano haya. Nahisi kuna kitu ikulu ama watu wanaoishi ikulu wapo nyuma ya hii biashara. Na kama ni kweli huioni hatari mbele yetu? Nadhani umeiona gari yenye nembo ya ikulu ikielekea pale nyumbani kwa Sheikh mkuu, na pia nadhani umewaona wana usalama ambao walikuwepo eneo lile tena kwa siri kubwa sana. Hii inaonyesha nini kwetu?" Aliongea Teddy huku akishindwa kuificha hofu. Hofu ambayo ilichukua nafasi kubwa usoni. "Ni kweli nimeona kila kitu, na hata hii gari yenye nembo ya Ikulu ulipishana nayo kidogo tu pale nyumbani kwa Baba Askofu. Hii inaonyesha watu hawa waliouawa ilitakiwa kuwa hivyo kabla hawajaingia mikononi mwetu. Kwahiyo kilichopo sasa hivi ni kutafuta na kujua ni nani ambaye alikuja na ile gari. Na tukishalifahamy hilo tutamtafuta mhusika." Aliongea masimba huku akikilaza kichwa cha Teddy kifuani. "Kwa nini Ulinituma nikamuue Baba Askofu?. Akauliza Teddy kwa mara nyingine huku akiuvaa uso wa kazi. "Nilikutuma kwa kuwa Alikuwa mmoja kati ya wahusika wakuu katika Biashara hii." Akajibu Masimba kwa Utulivu. "Ulijuaje hilo?" Akauliza tena. Ni swali hilo lililoubadirisha uso wa masimba. Sasa alikuwa akimtizama Teddy kwa macho ya sio na utani. Swali lake lilikuwa la kitoto kwa mtu mwenye uzoefu wa kiusalama kama yeye. "Swali gani la kitoto hilo unaloniuliza? Kwa hiyo mimi naweza kubuni tu kuwa mtu fulani anafanya biashara hii? Unajua kwa nini amekupa hiyo bahasha na kukwambia uilete kwangu?" Aliongea masimba kwa kufoka huku akimuangalia teddy. "Sio kwamba ni swali la kitoto, nimeuliza kwa kuwa kuwa kuwa kwangu kule sikuwahi kuwaona hata siku moja katika mikutano yetu." Akajibu Teddy kwa upole huku akikichezea kifua cha Masimba. "Naomba bahasha hiyo tuifungue, lakini tambua hii vita sasa tunapigana Na taasisi ya Urais. Kama gari za Ikulu zinatumika katika haya huku tunakoelekea ni kubaya. Usiikubali hofu ichukue sehemu kubwa katika Maisha yako. Hii ni vita ambayo inaweza kutupoteza na kutufuta katika Dunia hii. Licha ya kutufuta kwenye uso huu, lakini pia hatutokuwa na chochote cha kutukumbuka. Unatakiwa uitoe hofu na kuitokomeza. Ujuzi tulio nao utusaidie kutufikisha katika mwisho wa hii safari." Aliongea masimba kwa kirefu. Maneno yake yakamuingia Teddy na kumsisimua. Ulikuwa wakati wa kupambana, ulikuwa wakati wa kutumia ujuzi wao wote kuhakikisha hili linafika mwisho. Kwa nini awe na Hofu? Kwa nini aogope? Tokea lini yeye akaogopa Risasi? Tokea lini yeye akakiogopa kifo? Akazidi kujilaza kifuani kwa Masimba. "Nipo tayari Kupambana Dady? Nipo tayari kufanya kila kitu kwa sababu yako na sababu ya nchi yangu." Aliongea Teddy katika namna ambayo ilimsisimua. Muda wote huo hakuwa ameitoa Bahasha, hakuwa ameitoa kwa kuwa hakuambiwa afanye hivi. Akapeleka mkono mahali ambapo aliihifadhi Bahasha. Akaitoa na kumkabidhi masimba. Wakati masimba akitaka kuifungua Bahasha, simu yake ya Mkononi ikaita. Akatulia kwanza akimuangalia teddy machoni. Teddy naye akamkazia macho huku wivu ukionekana Shahiri machoni mwake. Alikuwa akihisi labda mpigaji ni Mwanamke. Masimba akaitoa Simu Mfukoni kwake, kabla ya kuipokea akatizama jina la mpigaji.. Major General Chomboko. Haraka akaipokea simu. "Utahitajiwa Ikulu Muda huu, lakini Make sure kabla hujaondoka hapo ulipo unaweka vizuri hiyo Bahasha. Ikipotea Hiyo basi Hata wewe Hutakuwa na Njia ya Kujinasua." Aliongea Major General Chomboko. Kisha pasipo kusubiri chochote. SIMU IKAKATWA.
MASIMBA AKAMTIZAMA TEDDY NA HATA TEDDY AKAMTIZAMA MASIMBA.
BADO KAZI YAO ILIKUWA NGUMU