Riwaya: Nitakupata tu

Riwaya: Nitakupata tu

Teddy anawakilisha %kubwa ya jinsia hiyo ilivyokuwa na udugu wa kutukuka na mali.
 
Teddy hastahili kusamehewa tena imetosha sasa.
 
Auliweee tuu manaaa kazidi sema masimba anampndaa atamsamehe kwa mara ingne tena
 
[06-09, 15:30] Ibrahim Masimba: NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 079

Wakati Teddy akisubiri gari ili kuondoka eneo lile, ndio Muda Huo ambao Masimba alikuwa akishuka hapo akiwa katika mawazo sana. Alitembea taratibu akihakikisha hakuna macho ya mtu ama watu yanayomuangalia. Muda wote alikuwa makini kwa Kila Hatua. Wakati anaukaribia mlango wa nyumba ile akauhisi mwili wake ukisisimka. Kitendo hicho kilitokea vbaada ya kuuona mlango wa nyumba ile ukiwa wazi. Haikuwa kawaida kwa mlango wa nyumba kama hizo kuwa wazi, haikuwa kawaida kwa kuwa ni sehemu ambayo haikupaswa kuachwa wazi. Akajikuta akijipapasa mfukoni mahala ambapo aliihifadhi bastola yake. Alipoigusa akaachia tabasamu mwanana. Akaipiga hatua nyingine huku miguu na mikono ikiwa tayari kwa lolote. Akaufikia mlango kisha kuingia moja kwa moja ndani. Kengele za hatari zikalia baada ya kukutana na michirizi ya Damu. Michirizi ambayo iliachwa kutokana na muonekano wa kitu kilichojiburuza. Roho yake ikampaa huku bastola ikiwa mkononi mwake. Miguu ilikuwa ikimtetema kila pale alipohisi kuwa Mtu aliyeiacha damu hapo ni Teddy. Hakuwa Tayari Teddy afe, hakuwa Tayari Teddy auawe. Hakuwa tayati kumpoteza Teddy kutokana na kuwa alimpenda. Alimpenda zaidi ya anavyowaza na Hata kufikiria. Akaufuata mburuziko ule. Hatua tatu mbele akakiokota kitu, kitu kilichomfanya akubali kuwa mtu aliyepigwa Risasi alikuwa Teddy. Chini aliiona bahasha. Bahasha ambayo ilikuwa na Siri kubwa. Akaikota huku mikono ikitetemeka. Moyo ukazidi kumpasuka baada ya kuiona bahasha imefunguliwa huku kile kilichodhaniwa kuwa siri hakikuwepo. Akahisi Dunia ikizunguka. Ni vipi kama Teddy ameuawa na kilichopo ndani ya Bahasha kupitea? Ataishi kweli katika amani wakati kilichopo ndani ya bahasha ndio kilikuwa kitu cha kumuweka kwenye usalama? Akaitupa bahasha na kuzidi kuufuatilia ule mburuziko. Mbele kidogo akamuona mtu ambaye hakuamini kama alikuwa Yeye, Meja Jenerali chomboko alikuwa amelala katikati ya Dimbwi la Damu. Damu ambayo ilikuwa ikitembea sakafuni kuonyesha mauaji haya hayakutendeka muda mrefu. Hilo likamfanya Masimba azidi kuchanganyikiwa. Muda mfupi baadae alikuwa pembeni mwa mwili wa Meje Jenerali Chomboko. Masikio yake yakausikia mkoromo na sauti dhaifu kutoka kwa Mzee huyu. Hii ilimaanisha kuwa hakuwa amekufa, alikuwa katika hatua za mwisho kufa. Akamuinamia na kujaribu kuongea naye.. lakini haikuwezekana, haikuwezekana kwa kuwa mzee hakuwa akiongea chochote. Hakuweza kuongea kwa kuwa hakuwa na muda mrefu wa kuishi. Hakuonyesha kama ni mwenye kupona. Punde akauona mkono wa Mzee Chomboko ukinyooka huku kidole chake kukichofya katikati ya Damu kisha kuandika pale sakafuni. "Teddy ameasi. " yalikuwa maneno makali yalioukata Moyo wa Masimba. Akajikuta akitetemeka huku Hasira juu ya Teddy ikizidi kuchukua nafasi. Akiwa katika Hilo akamuona Mzee chomboko akinyoosha miguu, kisha kutulia. Alikuwa amekufa, alikuwa amekufa katika kifo cha kumpigania yeye. Teddy alikuwa amesababisha kupotea tena kwa mtu muhimu katika Maisha Yake. General chomboko alikuwa ni mtu muhimu kwake akimlinda katika hatari, hatari ambayo ingeshampoteza. Leo hii alikuwa amelala katikati ya dimbwi la damu tena akiwa maiti. Tena akiuawa na Mkono wa Teddy. Teddy aliyekuwa akilia muda mfupi uliopita. Teddy aliyenusurika kuuawa mara kadhaa. Teddy aliyesema alikuwa akimpenda, aliyekuwa akimhitaji na kulia kwa Ajili yake. Lakini leo hii amemuuua Mzee chomboko na kutoroka na bahasha ambayo ndiyo ilikuwa zamana ya Maisha yake. "TEDDY NITAKUPATA TU NA NITAKUUA KWA MIKONO YANGU." Baada ya kutamka hilo akainuka na kutoka katika jengo hilo la Siri. Maandishi ya jenerali chomboko yalikuwa yakijirudia Kichwani "TEDDY AMEASI". Alihisi akili yake haifanyi kazi kwa muda ule. Hakuiona furaha tena. Wakati hilo likiendea kumsumbua kichwani, simu yake ya mkononi ikatoa mlio. Ilikuwa ikiita. Akaichomoa na kukutana na Jina la Chief. Mkurugenzi Wa Idara ya Ujasusi alikuwa akimpigia.

Akaipokea haraka na kuipeleka sikioni. "Naomba wahamishe watoto wangu kutoka hapo walipo. General Chomboko No more. Teddy Ameasi na Bahasha ametoroka nayo." Aliongea masimba kwa Haraka bila kusubiri maelezo. "Nililifahamu hilo mapema, nilimfahamu yule mtoto ni mwenye tamaa. Vijana wangu wamemuona katikati ya Mji. Nadhani anataka kwenda kuonana na Rais. Cha kufanya wewe sasa hivi unatakiwa kushughulikiwa. Kwahiyo unachotakiwa ni kuwa makini na usijionyeshe. Vijana wangu wapo sambamba naye na nataka wamzuie kabla hajaingia lango la Ikulu. Nimehuzunika sana kumpoteza Chomboko. Teddy Hastahili kuachwa Hai. Ukishindwa wewe nitaifanya mimi hiyo kazi." Aliongea Chief kisha kukata simu. Masimba akaganda kwa muda, Teddy ameonekana katikati Ya Mji. Anaonyesha kuwa anaelekea Ikulu. Ni maelezo hayo yaliompa masimba muelekeo sahihi kwa kipindi hicho. Damu ya Asteria P Paulo Damu ya Dee Plus damu ya Mama yake na Sasa Damu ya Mzee chomboko ilikuwa mikononi mwake. Ulikuwa ni muda wa kuilipa Damu Hiyo. Ulikuwa muda wa kuwawahi kabla ya kumuwahi. Ulikuwa muda wa kuelekea Posta, ulikuwa muda wa kutembea kila anapokanya Teddy. Ilikuwa ni lazima ampate. Ilikuwa nilazima Amuue.

******

Alikuwa akitembea bila kujua alikuwa akitembea na watu. Hakujua kuwa vijana wasiopungua wanne walikuwa wakitembea naye kwa kila hatua. Walitakiwa kuhakikisha haiingii katika viunga vya ikulu. Hiyo ndio ilikuwa amri kutoka kwa Chief. Teddy hakujua kuwa wauza urembo wawili, muuza pweza kwenye sinia na hata muuza vitambaa walikuwa vijana ambao walikuwa wakimfuatilia yeye. Aliwachukulia kama wamachinga bila kujua kuwa yupo kwenye tageti. Alitembea Kwa mwendo wa kawaida mpaka eneo la Feri. Akatafuta sehemu nzuri na kutulia kandokando ya bahari. Alikuwa akitizama maji huku mawazo yakimzonga. Kile alichokifanya alijua sio kizuri lakini moyo wake ulikuwa tayari kwa lolote. Kwa kuwa alitambua Kitu alichokichukua Kwenye Bahasha ndio dhamana ya Uhai wa masimba. Alijua Masimba Angeuawa muda wowote kitu ambacho kitasababisha yeye kupata pesa zote. Hilo likamfanya asahau mapenzi na ubinadamu wote. Alikuwa tayari Masimba afe ili mradi yeye achukue mamilioni ya shilingi. Muda wote vijana waliokuwa wakimfuatilia bado hawakumpa nafasi. Lakini wakati wakiendelea na hilo wakamuona Teddy akisimama akitembea taratibu kuelekea soko la samaki feri. Hata wao bado walikuwa nyuma katika namna hiyo hiyo. Wakimuangalia kwa umakini. Teddy akaingia ndani ya Soko la samaki, lakini wakatia akiingia hapo akageuka kwa chati kutizama nyuma. Tabasamu la kugundua kitu fulani likatamalaki. Aligundua kuwa alikuwa akifuatiliwa kwa nyuma na vijana wa usalama wa Taifa. Hapo akaongeza umakini akiitafuta njia ya kuwatoroka watu hawa. Kitendo cha kuwaona watu hawa wakimfuatilia, kulitoa majibu kuwa tayari ameshagundulika kile alichokitenda. Kilichokuwa kikimpa nguvu ni kule kujua kuwa Masimba alikuwa Ikulu na isingeweza kutoka huko. Na mpaka kuja kutoka kwake, yeye tayari alikuwa yupo mbali na hatakuwa hapa nchini. Kwa mara ya kwanza akamkumbuka Jimmy, ilikuwa ni lazima ukutane na Jimmy. Ilikuwa ni lazima aongee na Jimmy ili kufanikisha adhma yake. Alijua kabisa akichelewa na akaingia mikononi kwa masimba basi angeuawa hata kwa kukatwakatwa. Hakuwa tayari kwa hilo. Ilikuwa ni Lazima amtafute Jimmy. Au ilikuwa lazima Atafute njia ya kuonana na Rais Wa Nchi. Alikuwa tayari kuitoa karatasi ile aliyoichukua kwenye bahasha. Ilikuwa tayari kuitoa ili apate pesa za kumuondoa hapa nchini.

**********
[06-09, 16:04] Ibrahim Masimba: Alishuka posta mpya akiwa kwenye utofauti wa sura, mavazi na hata utembeaji. Alikuwa ni kama babu kizee mwenye kutembelea mkongoja. Mvi zilipangana kichwani kuonyesha kuwa mzee huyu alikuwa amekula chumvi nyingi. Baada ya kushuka hapo akasogea pembeni sehemu ambayo hukaa watu. Naye akakaaa hapo. Baada ya kukaa, akatoa kitabu chake na kuanza kusoma taratibu huku macho yake yakizunguka kwa hila yakiitizama sura ya kila apitaye na hata wale ambao walikuwa wakipanda magari. Alikuwa masimba akiwa hapo kwa sababu maalum. Alikuwa hapo akimtafuta Teddy katika Utofauti kama huo. Aliamua kuingia kazini kwa staili hiyo akiamini anaweza kuuepuka mkono wa wana usalama. Pia alitambua angeweza kumpata Teddy kwa urahisi. Muda wote macho yake hayakutulia sehemu moja. Alikichunguza hiki na kukiangalia kile. Hata waliokuwa kwenye bajaj alikuwa akiwatizama katika namn ambayo hakuna hata mmoja mwenye uwezo wa kuligundua Hilo. Muda ukasonga bila kumuona mtu. Kagiza kakaanza kuiingia akiwa bado yupo hapo. Alikuwa ametulia safari hii akionyesha akipuliza kiko. Moshi ulikuwa ukipaa hewani taratibu na kuileta burudani kwenye nafsi yake. Wakati akilifurahia hilo simu yake ikaingia Sms.. "Kuku wako imeshindwa kuingia kwenye banda. Wanao wamemtafuta lakini hawamuoni." Ulikuwa ujumbe ulioandikwa kwa lugha ya mafumbo. Ujumbe ambao ulipokelewa kwa mwili wake kusisimka. Teddy alikuwa amewapotea vijana waliokuwa wakimfuatilia. Ilikuwa taarifa iliyousisimua sana mwili wake. Taarifa ambayo ilimfanya ahisi Teddy alikuwa ameshagundua hilo la kufuatiliwa. Akasimama hapo akitaka kuelekea upande wa pili wa barabara. Wakati ikitaka kulifanya hilo, akamuona mwanamke aliyevaa nguo chakavu huku juu akiwa amebeba kapu lililoonyesha kuwa lilikuwa na samaki. Licha ya uchakavu wa mavazi, licha ya ubebaji wa Kapu lile, licha ya kuonekana kama muuza Samaki, bado hakuweza kumpotea Masimba, bado hakuweza kumpoteza masimba. Alimtambua na alimjua. Lakini kwa nini yuko hivi? Lilikuwa swali ambalo halikujibiwa, lilikuwa swali ambalo halikupata muda wa kuulizwa. Misuguano ya tairi za gari zikaleta mayowe kwa watu waliokuwa karibu na kituo cha daladala posta mpya. Gari aina ya Coaster iliyokuwa ikifanya safari yake kati ya Mbezi na Posta ilikuwa nyang'anyang'a baada ya kugongwa na gari kubwa iliyokuwa akipita kwa mwendo wa kasi. Hilo likaifanya shingo ya Masimba kugeuka, kugeuka kutizama kwenye ajali hiyo. Hata pale alipokuja kugeuza shingo na kukumbuka kuwa alikuwa amemuona Mwanamke Anayemfahamu.. Hakuweza Kumuona Tena, licha ya kutokumuona lakini pia hata lile kapu alilokuwa amelibeba kichwani, lilikuwa limeachwa pale pale chini Watu Wakilishangaa. Hakuamini
 
jamani huku hakuna arostoo...nataka nianze kuisoma hiii riwaya
 
[06-10, 16:51] Ibrahim Masimba: NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 080

Alimuona mwanamke anayemfahamu akiwa kwenye mavazi chakavu, licha ya mavazi hayo lakini pia kichwani alikuwa amebeba kapu chakavu ambalo ndani yake lilionekana kuwa na samaki. Lakini baada ya Ajali hii, ajali ambayo ilionekana kupangwa. Hakumuona tena Veronica Senka. Hakumuona Vero zaidi ya kapu la samaki ambalo lilikuwa chini huku samaki wakitawanyika. Hilo likampa mzubao wa kama sekunde tatu, mzubao ambao uliondoka pale tu aliposikia ving'ora vya magari ya hospitali pamoja na magari ya polisi. Akarudi mpaka pale alipokuwa amekaa; akakaa na kujirudisha kwenye muonekano wa kizee. Muonekano ambao ulimfanya aipate heshima. Alikaa hapo mawazo yake yakiwa kwa Teddy, alikaa hapo mawazo yake yakimuwaza mwanamke huyu. Licha ya wazo hilo lakini hakuacha kujiuliza kuhusu Veronica. Veronica mwenye kapu la samaki. Veronica ambaye aliliacha kapu lake la samaki. Veronica aliyepotea katika aina fulani ya kimaajabu. Kwa nini Baada ya Ajali naye akapotea? Kwa nini baada ya Ajali apotee? Ama ajali ilikuwa ni ya kupangwa? Kama imepangwa nani ambaye ameipanga na kwa nini? Hayo pekee ni maswali yaliomsogeza mpaka sehemu yenye mkusanyiko wa watu waliokuwa wakiwasaidia majeruhi. Nia ilikuwa ni kuwatizama majeruhi hawa na hata madereva wa Gari iliyoligonga hili gari la Abiria. Lakini cha ajabu madereva wa ile gari kubwa hawakuwepo ndani ya gari na hapakuwepo na dalili ya uwepo wao eneo hilo. Nyundo kubwa ya Hatari ikagonga kichwani kwake. Gari igongwe pasipo na sababu kisha madereva wapotee? Mara moja akatambua ajali ile ilipangwa na sababu ya kupangwa kwake ni kutaka kuwapoteza watu kutoka machoni kwa watu. Hata Vero alimshangaa kwa sababu ya Kuzingatia kile kinachoendelea kwenye Ajali. Wakati akiliwaza hilo akaupata ujumbe tena kutoka kwa chief. Ujumbe ulioandikwa wa Lugha ile ile ya Mafumbo. "Ndege anaruka kuelekea Kinondoni akiwa sambamba na tetere katika urafiki wa mashaka. Bado tunampeleka kwenye banda." Ulisomeka ujumbe huo. Ujumbe uliokuwa ukimjulisha kuwa Teddy alikuwa sambamba na Veronica. Hilo likamuondoa hapo mpaka kwenye kituo cha Tax Nje ya Jengo la Benjamin Mkapa. Muda mfupi baadae alikuwa barabara akielekea kinondoni kumchukua Teddy. Alijua Teddy hakuwa na uwezo wa kufika Ikulu. Alijua Teddy hakuwa na nguvu hiyo tena. Alitambua alichokitafuta Teddy ni nguvu ya kumuwezesha kuingia mikononi kwa Ikulu. Muda wote alikuwa Akuwasiliana na Chifu akimwambia kila kitu ambacho kilikuwa kikiendelea kati ya Wana usalama waliokuwa wakimfuatilia Teddy na Veronica. Tax iliendelea kukata mbuga, dereva ikipenya hapa na kupenya pale. Wakati wanaiacha barabara ya Morogoro kuifuata barabara inayoelekea kinondoni mkwajuni, wakapitwa na magari mawili yakiwa kwenye mwendo wa kasi sana. Kwa kuwa Masimba hakuwa na mawazo mengine zaidi ya kumuwaza teddy hakuyafuatilia Magari yale. Bado alikuwa akimhimiza Dereva aendelee kuendesha gari. Mbele kidogo baada ya kukipita kituo cha Kanisani, wakakutana na foleni. Ilikuwa foleni iliyowashangaza yeye na Dereva wa Tax. Kwa kuwa wakati huo wa Usiku hapakuonyesha uwepo wa magari mengi katika barabara hiyo. Muda ukawa unayoyoma bila foleni kusogea. Masimba akajipapasa na kutoa Elfu kumi kisha kumuomba Yule dereva ili yeye ashukie hapo. Dereva hakuwa na hiana. Masimba akashuka akiwa na mkongoja wake mkononi. Baada ya kutembea kama hatua Tano, akavutiwa na umati wa watu uliokusanyika umbali mfupi kutoka pale alipo. Kingine kilichomvutia ni uwepo wa Askari wa Kikosi maalum sambamba na Askari Kanzu waliotapakaa Eneo lote. Masimba akajikongoja na kusogea kwa karibu Sana. Hatua kadhaaa mbele macho yake yakatua kwenye miili ya watu watatu ikiwa imelazwa chini ikiwa haina uhai. Kuwatizama kwake kwa mara moja kulitosha kumfanya agundue kuwa waliouawa walikuwa ni Wana Usalama waliokuwa wakimfuatilia Teddy. Hilo likamfanya aondoke pale kwa haraka sana. Alitaka kutafuta sehemu tulivu ili aweze kuwasiliana na Chief.

*******

Chief hakuwa akipatikana kuonyesha simu yake ilikuwa imezimwa. Hilo nalo pia lilianza kukivuruga kichwa cha Masimba. Ni muda mfupi uliopita alikuwa akiwasiliana na Chifu akimueleza kule ambapo walikuwa wakielekea Teddy na Veronica. Lakini muda huu alikuwa hapatikani Huku Vijana wake wameuawa kinyama. Hakikuwa kitu cha kawaida kwake kutokea kwa hilo. Hakikuwa kitu cha kawaida kwa hilo lililotokea. Akailazimisha akili yake iamini. Akaitaka akili yake iamini kuwa chifu alikuwa katika hatari ama shinikizo kutoka mamlaka iliyomteua. Akauona Muda wa Mapambano umewadia, muda wakujitokeza katika vitendo. Aliamua kurudi kazini kuirudisha heshima ya mtu. Muda mfupi baadae alikuwa Juu ya pikipiki akielekea katikati ya Mji. Alikuwa akielekea mahala fulani kwa sababu ya kitu fulani. Alihitaji kwenda kupumzika hata kwa dakika tano. Ni katika safari hiyo alipomkumbuka Mwanaharamu. Alihitaji kumuita katika hili. Alitambua angekuwa msaada mkubwa sana. Lakini kabla hajamuita Huyu, alitaka kwanza kujua pale ambapo Alihifadhiwa mkurugenzi Wa Idara ya Usalama Wa Taifa. Alifika maeneo yale ya Posta ya Zamani. Akachepuka mpaka maeneo ya kanisa la St Joseph. Hapo akazunguka mpaka nyuma ya Jengo la Kanisa hilo. Hapo nyuma palionekana kibanda kidogo ambacho kilionekana kama ni Chumba kinachotumiwa kwa Shughuli za kanisani. Baada ya kusimama na kuugonga mlango kwa Ishara inayotakiwa. Mlango wa kijumba kile ukafunguliwa kisha masimba akapewa Ishara ya kuingia. Baada ya Masimba Kuingia ndani mlango ukafungwa. Ingawa kwa Nje Kilionekana kama kijumba kidogo lakini kwa ndani ilikuwa ni Jumba kubwa. Mbele yake Alikuwa amesimama mtu mwenye umri usiopungua miaka 60. Alikuwa ni mwanaume mwenye asili ya Bara la Ulaya. Licha ya kuwa mzee lakini bado mwili wake ulionekana kuwa na nguvu sana. "Karibu kijana wangu, na pole kutokana na Hii sintofahamu ambayo unae ndelea kupambana nayo." Aliongea mzee yule wa kizungu kwa kiswahili kizuri sana huku akimpa masimba kikombe cha chai. "Nashukuru Mr Raymond Peterson. " alijibu Masimba kwa Kifupi kisha akapiga Fundo la chai kisha kutulia. Hata mzee Raymond Naye Alikuwa ametulia akimtizama Kijana huyu Jinsi alivyochakaa. "Kijana Mambo yalipofikia ni pagumu. Unatakiwa utumie Ujuzi wako wote usiingie mikononi mwa Mamlaka za Juu. Kuna fununu nimeipata kutoka kwa vijana wangu kuwa kuna uwezekano wa wewe kubebeshwa Tuhuma kwa Kifo Cha Mr Chomboko. Na hapa tunapoongea Tayari Mkurugenzi Amepelekwa kusikojulikana. Na hivi Punde Teddy Atawasili Ikulu kupeleka kile ambacho kitakufanya wewe uwe maiti." Alitoa maelezo mzee yule huku akimuangalia Masimba machoni. Macho yake hayakuonyesha kudanganya, macho yake yalikuwa yakikimaanisha kile ambacho alikuwa akikisema. Chief alikuwa amefichwa mahali fulani huku Teddy akibakisha dakika chache kuwasili ikulu ilikuuwasilisha mzigo kwa Rais. "Sitakubali hili litokee kamwe, nimeshapoteza roho za ndugu zangu. Siwezi kuruhusu kilichotoka kwenye bahasha kimfikie Rais. Nipo tayari kufa. " aliongea masimba huku akitembea ndani ya Sebule hii. Mzee Raymond akamuangalia kijana huyu kwa muda mrefu sana. Akajikuta akiukumbuka mkasa uliomfanya atoroke katika jiji la milan nchin Italy na kuja kuishi Tanzania kama Msimamizi wa masuala ya Kanisa Katoliki Katika Africa ya Mashariki. Alikumbuka kipindi kile akiwa muumini wa kundi la kiharifu Lililoitingisha Italy Katika miaka ya themanini mpaka Tisini. Kundi ambalo lilifahamika kama Mafia. Aliikumbuka Asubuhi moja akiwa katikati ya jiji la milan kwa shughuli za kila siku za kundi hilo la kinyang'anyi. Akiwa katikati ya jiji hilo ndipo hapo ilipotoka oda ya yeye kutakiwa kumuua waziri mkuu wa Nchi hiyo.. Simone Masimiliano Kutoka na Waziri huyo kutenda matendo ambayo yalikuwa kinyume Na maelekezo ya Kanisa Katoliki. Ni tukio hilo lililosababisha yeye kutoroshwa katika usiku huo huo mpaka Jijini Washington Dc kabla hajapanda ndege ya Kumleta katika Nchi Hii aliyopo leo. Muda wote aliheshimiwa na viongozi wa nchi kutoka na busura na ushawishi alionao kwa Wananchi.

"Hutakiwi kuwa na Haraka Masimba. Ukifanya Haraka Hutaweza kulitenda Hili. Hili suala limeshafika sehemu ambayo utulivu unahitajika. Vijana wangu bado wanaangalia uwezekano wa kumzuia Teddy akiwa Hai. Na kama itashindikana Kumkamata Akiwa Hai basi wamlipue Ili asipeleke madhara katika Taifa hili. Kitu kilichomo kwenye ile bahasha ni hatari kwa maisha ya masikini wote. Wenye pesa ndio watakao weza kupona. Ama wale wasio na tamaaa ya kutumia vitu hivyo ndio watapona. La sivyo kila siku tutawachukua kwenda kuwatibu Watu ambao tunawaharibu Wenyewe kwa kutengeneza sumu." Yalikuwa maelezo yalimpa masimba mwanga. Mwanga ambao ulimfanya aanze kuhisi kile ambacho alikihisi hapo mwanzo. Lakini kitu hiki no kitu gani mpaka rais aubadili msimamo wake?
[06-10, 16:52] Ibrahim Masimba: Hiki ni kitu gani ambacho Hakitakiwi kufika kwa Rais? Hapo akageuka kwa mara nyingine kutizama aliposimama mzee Peterson. Akamtizama Kwa macho yake mawili, macho yaliokuwa yakiongea kitu. Kitu ambacho hata mzee Raymond alitanbua umuhimu wake. Ndio maana akaamua kuwatumia Vijana wake katika kulifuatilia hilo suala. "Mr Raymond ningependa kujua alipo Chifu, pia nataka kujua hiki ambacho kilikuwa ndani ya bahasha ile. Kina husiana nini na Biashara hii Ya Madawa ya Kulevya na ni kwa vipi Kiongozi wa Nchi analikingia kifua hili suala? Aliuliza Masimba Huku akiendelea kumuangalia Mzee yule. Mzee Raymond naye akamuangalia kwa muda kisha kwa sauti yake ya upole akamuuliza. "Ina maana unapambana Bila kujua kinachokuweka kwenye Hatari? Akauliza.

"Wakati napambana nilidhani napambana na wauza madawa ya kulevya. Na wakati napigana nilijua napambana kwa kutetea Taifa langu." Akajibu Masimba.

"Unadhani inawezekana Waziri mkuu kutenda kitu bila Rais kujua?" Akauliza tena mzee Raymond. "Unataka kujaribu kusema nini hapa? Ina maana Rais alikuwa akiigiza katika maagizo yske huku akujua yeye ni mmoja wao? Akauliza Masimba huku sasa akimuangalia Vizuri mzee Raymond. "Unadhani nani ambaye alikuwa akiwaua watu fulani katika pitapita zenu? Unadhani nani alikuwa akiwafumba midomo yao? Akauliza Mzee Raymond. Ukimya wa muda ukapita kisha akaendelea. "Sikiliza Masimba, kila kilichokuwa kikifanyika yalikuwa ni maigizo. Rais wenu alikuwa analijua hili. Hata kifo cha waziri mkuu kilipotokea Ulitakiwa wewe uuawe. Na Mtu wa kukuua alipangwa awe Teddy kwa kuwa Teddy alikuwa mmoja kati ya Watiifu wanaomtii mkuu. Kuacha kukuua haikuwa Amri yake, bali aliambiwa akuache ili Waupate mzigo wao wa Bilioni mia mbili ishirini na mbili ambao uliuchukua Nyumbani kwa Jimmy. Kwa Taarifa yako Teddy licha ya kuwa Jasusi wa Idara pia Ni Special Agent wa CIA Ambao wapo Nyuma ya Hiki kitu. Kitu kinachokuweka Hatarini ni betri maalum ya kuundia kemikali fulani zenye sumu ambazo huchanganywa katika madawa na kusababisha madawa kuwa na bei na gharama kubwa. CIA, NSA NA HATA FB ndio wanaosapoti hili. Kwahiyo Hatari ya kukupoteza Ipo. Ndio maana niliamua kumtuma Veronica Awe kama Ngao yako. Yule Sio mmoja kati yao, Yule yupo upande wako. Anakulinda kwa kila hatua. Hata pale posta ulipojibadilisha Ulijulikana. Na ile ajali iliyotokea pale Ilikuwa ni kukulinda na kukuokoa. Bastola ilikuwa Tayari kukumaliza kutoka kwa mtu ambaye aliyekuwa mle ndani ya Daladala. Vero ndiye aliyeifanya kazi ile. Kama sio vero ungeshageuka Maiti."
 
Ebwanaeeeh!!!! Kumbe ndivyo hivyo, ahsante mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom