Riwaya: Nitakupata tu

Riwaya: Nitakupata tu

[05-30, 14:51] Ibrahim Masimba: NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 071

Hakuwa akipumua na hakua hai tena. Alikuwa amekufa akimuacha masimba kwenye giza totoro. Giza la kujua kile ambacho alitaka kukijua kutoka kwake. Kile ambacho kingemsaidia kumjua yule aliyenyuma ya hawa vijana. Hakuamini kama wakina Jimmy wangeweza kuwa wao kama wao. Alihisi uwepo wa watu wengine, alihisi uwepo wawatu wengi katika biashara hii. Hapo ndipo alipoamua kuipekua nyumba ya Suresh. Alianzia kuipekuwa kwa kuangalia kila sehemu. Kila alipoangalia hakuweza kufanikiwa kitu. Licha ya kujitahidi lakini hakupata kitu chochote cha kumsaidia. Baada ya kuuona ugumu huo akaona huu ulikuwa muda wa kufanya kile ambacho kingewapa hasara watu hawa. Alitoka mle chumbani na kutembea mpaka nje sehemu ambayo yaliegeshwa magari. Kufika hapo bado giza lilikuwa totoro. Bado hakumuona mtu yoyote. Jambo hilo lilimfanya agundue kuwa walinzi wa jumba hili walikuwa Nje wa Kilinda. Alichokifanya ni kuelekea kwenye gari moja kati ya zile, akafungua tanki la mafuta kisha kuyaachia yote ya mwagike ardhini. Baada ya kuhakikisha mafuta yamelowesha ardhi na sehemu za magari mengine yalioegeshwa hapo. Masimba akapiga hatua kama kumi kisha kutoa kibiri maalum mfukoni. Akakiwasha na kukitupia katikati ya magari yale. Mlipuko mkubwa ukasikika, moto mkubwa ukawaka.. wakati huo masimba alikuwa ameshachupa akiondoka taratibu sehemu ya tukio akiliacha Jengo lile likiteketea pamoja na vitu vingine vyote vilivyopo ndani. Alikuwa akitabasamu, akitabasamu akifurahishwa na kilichotokea. Muda wote aliyapenda mapambano, alipenda kupambana na hakuogopa hilo. Akaendelea kutembea katika giza akipishana na magari ya zimamoto yakielekea huko.

*******
Alijiinamia akifikiria kile ambacho
[05-30, 14:51] Ibrahim Masimba: Alikuwa ameinama chini akifikiria kile ambacho anatakiwa kukifanya. Kitendo cha kutekwa bandarini kabla ya kuokolewa kilimpa mawazo sana. Alijua kuwa alikuwa akitembea na watu kila sehemu. Alijua kuwa alikuwa akitafutwa kwa udi na uvumba. Hilo likampa tafakuli thabiti katika kulitenda lile ambalo alipaswa kulitenda. Lile ambalo lingemuweka Huru na kumfanya afurahie mapenzi yake na mumewe kipenzi Masimba. Lakini kwa sasa hawakuipata nafasi hata ya kuburudisha miili yao na nafsi zao. Hawakuupata muda wa kumtafuta mtoto wa pili. Watawezaje kufanya hivyo ikiwa wote wanatafutwa? Watawezaje kufanya hivyo wakati kuna macho kila mahali yakimtizama? Hawakuwa na Njia ya kufanya isipokuwa kuwa kabili watu hawa. Ni lazima Jimmy na Suresh wauawe. Hilo akalipitisha. Ni wakati akiliwaza hilo akaisikia sauti ya mtangazaji wa Tv akitangaza habari. Akitangaza habari ambayo iliushtua moyo wake na kuisisimua Damu mwilini mwake. "Mfanyabiashara maarufu nchini Tanzania Suresh Patel Sigh sambamba na mwanamke asiyetambulika. Wameuawa kwa kupigwa risasi kisha nyumba yao kuchomwa moto. Habari kamili itawajia baadae." Ilikuwa habari ile ambayo ilimuacha Teddy kwenye mawazo. Ilimuacha teddy katika tabasamu. Masimba alikuwa ameshaifanya kazi yake. Hilo likampa tumaini jipya. Naye sasa aliamua kumtafuta Jimmy. Aliamua kumtafuta kwa ajili ya kulipa kisasi. Kisasi cha kuuawa kwa mdogo wake.

Ingawa jimmy hakuwa muuajii katika suala la Vicky. Lakini alijua bila Jimmy kila kitu kisingetokea. Akajiinua pale alipokaa na kuiendea droo. Akaifungua na kutoa bastola zake mbili. Baada ya hapo akazipachika mwilini katika sehemu tofauti ambazo haziwezi kufikiwa kirahisi na macho au mikono ya watu. Akatoka mle chumbani sasa akiamua kurudi pale bandarini lengo likiwa ni kumtafuta Veronica Senka. Mwanamke mjuzi na mwenye kujibadilisha kutokana na mazingira. Alitembea taratibu mpaka kituo cha daladala Cha Ubalozi lengo likiwa ni kuangalia kama alikuwa akifuatiliwa ama la. Lakini mpaka anafika hapo na kuvuka upande wa pili kisha kupanda basi hakuweza kumtilia mashaka mtu yeyote anayemfuatilia ama anayemtizama kwa Hila.. kila mmoja alikuwa busy na Shughuli zake. Baada ya gari aliyopanda kufika maeneo ya daraja la salenda, akausikia ujumbe ukiingia kwenye simu yako. Akaitoa simu kwa haraka na kuufungua ujumbe kisha kuusoma. "Shuka kwenye gari uliyopanda. Nenda Magomeni kagera nyumba namba O912 kuna mtu anatakiwa kuondolewa hapa Duniani." Ulisomeka ujumbe huo kutoka kwa Masimba. Ile kujua tu kuwa Masimba yupi katika macho yake kila aendapo kulimburudisha sana. Alitambua sasa alikuwa ameingia kazini Rasmi. Dakika hii alikuwa chini akitembea baada ya kushuka kwenye basi. Akatembea mpaka pembezoni mwa barabara sehemu ambayo kulikuwa na kijiwe cha bodaboda. Teddy akaidandiq moja kisha kumuomba Dereva aendeshe kuelekea magomeni kagera. Sehemu ambayo aliagizwa kwenda kumpa mtu tiketi ya kuzimu. Muda wote damu yake ilikuwa ikimsisimka. Aliupenda mchezo wa kuua kuliko mchezo wowote. Alishuka magomeni mwembechai na kuanza kutembea kwa mguu akielekea kagera. Muda wote macho yake yalihama hapa na kwenda kule yakitizama kile kile ambacho ilikitizama kule mwanzo. Hakuiona hila yoyote kutoka kwa watu aliokuwa akipishana naye. Kila mmoja alikuwa tofauti na kawaida sana. Muda huu alikuwa akiifikia kagera. Akaingia kwenye mitaa miwili mitatu, mtaa wa tano alijikuta akitizamana na Nyumba husika. Nyumba anayotakiwa kuipeleka tiketi ya mtu anayetakiwa kusafirishwa kwenda kuzimu. Mkono wa Teddy ulishika tiketi ya kifo cha mtu huyu asiyemjua. Ilikuwa nyumba ndogo ya wastani ya vyumba visivyopungua vitano kwa kuitizama. Licha ya hivyo pia ilikuwa imejengwa mfano wa gorofa kwa kupandishwa nyumba nyingine kwa juu. Uzio wake haukuwa mrefu wala mfupi sana. Ulikuwa uzio wa wastani na mbele ya Jengo hilo kukiwa na geti kubwa Jekundu. Nyaya za umeme zilikuwa zimepita kuonyesha nyumba hiyo ilikuwa ikilindwa na mitambo maalum. Akaitizama kwa makini mpaka aliporidhika akaamua kupiga hatua kuelekea hapo. Kwa wakati huo ilikuwa yapata saa kumi na moja jioni. Bado watu walikuwa wengi na kwa magomeni unaweza kudhani labda kumekucha.
[05-30, 14:51] Ibrahim Masimba: Kwa kuwa macho ya watu yalikuwa mengi, Teddy akaamua kutembea tararibu akielekea hapo. Bastola zake zilikuwa mahala pale tulivu mahala ambapo hapakufikiwa na macho ya mtu yoyote. Mazingira ya nyumba hii yalianza kumpa mashaka pale tu alipokaribia geti la nyumba ile. Ni kitu cha ajabu sana kuambiwa ukaue mtu kisha uikute nyumba hiyo ikiwa haina ulinzi. Hilo lilimpa hisia fulani, hisia ambazo zilikuja kuamsha kengele za hatari hasa baada ya kuibonyeza kengele. Licha ya kubonyeza mara nyingi zaidi, lakini hapakuwa na majibu kutoka kwa mtu wa ndani. Akaamua kujaribu kulifungua geti. Kitendo cha kulisukuma geti, akaliona likifunguka lenyewe taratibu. Teddy akitizama kwa chati ndani. Lakini hakuweza kumuona mtu. Hakuweza kumuona mtu yeyote ama kitu ambacho kingemthibitishia uwepo wa mtu mahala hapo. Hilo likazidi kumfanya aongeze umakini. Mguu wa kulia ulikuwa Ndani huku wa kushoto ukifuatia. Sekunde nne baadae alikuwa akiingia ndani mwili mzima. Alikuwa akitizamana na uwanja usiokuwa na mtu isipokuwa magari ya kufahari yaliyoegeshwa hapo. Ukimya pia kilikuwa kitu kingine kilichoitawala nyumba hiyo. Teddy akatembea taratibu safari hii bastola yake ikiwa mkononi huku mdomo ukiwa umetangulia mbele. Akaupita uwanja kwa usalama pasipo chochote, akauendea mlango akaugusa.. Hata mlango pia ukafunguka. Kufunguka kuonyesha kuwa haukuwa umefungwa. Hilo likamuongezea umakini. Akaufungua mlango taratibu kisha kujipenyeza ndani. Hapo akaikuta sebule tupu, licha ya utupu huo lakini bado Tv ilikuwa ikifanyakazi kuonyesha kuwa palikuwa na mtu muda mfupi uliopita. Hilo pia halikuwa la kupuuzwa. Wakati akilishangaa hili la Tv, akakiona kipisi cha sigara kikiwa bado kinamoto kuonyesha kuwa mvutaji alikuwa hap0 muda mfupi uli0pita. Hilo pia hakulitaka lipite. Alitambua hapo palikuwa na mtu, alitambua hapo ndani kuna mtu. Lakini mtu huyu atakuwa amejificha mahala fulani. Akaiacha sebule katika namna hii, katika namna ya masikio ya sungura, masikio ya kunasa hiki. Akakifuata chumba ambacho kilikuwa hatua kama kumi kutoka sebuleni. Kukifikia chumba hicho alishangazwa na alichokiona. Licha ya chumba kuwa wazi lakini pia vitu vilionyesha kutupwa tupwa hovyo. Akaingia taratibu macho yake yakizunguka huku na huko mithili ya Bundi. Kila kitu ndani ya chumba kile kilikuwa kimetupwa huku na huko kuonyesha kuwa palikuwa pakitafutwa kitu muda mfupi uliopita. Mikono yake ikashika hiki huku macho yakitizama kile. Hakuona chochote cha maana. Akakiacha chumba kile huku mdomo wa bastola ukiwa umetangulia mbele. Akaendelea kutembea na kutembea. Hata pale alipotokea kwenye chumba cha pili hali ilikuwa ni ile ile. Alikuta mlango wazi na pia hata vitu vilikuwa vimetupwa Hovyo. Hakutaka kuingia, akapita hapo na kwenda kutokea kwenye sebule nyingine. Mbele ya sebule hii akakutana na kitu kingine kilichomsisimua. Alikutana na matone ya damu. Ukutani na hata sakafuni. Licha ya matone hayo hapakuonekana uwepo wa mwili wa mtu yeyote. Sebule ilikuwa tupu kabisa. Kufika hapo Teddy alikuwa amejua kile kilichotendeka. Alikuwa amewahiwa muda mfupi uliopita. Amewahiwa na watu ambao hakuwatambua. Wakati hilo likimuweka gizani, akayaona matone ya damu yakitokea Juu ya Silling board. Ilikuwa damu ikivuja kutoka Juu kuonyesha kuwa kuna mtu majeruhi yupo huko. Kwa umakini wa Hali ya Juu akaikanyaga meza kisha ufungua mfuniko ambao ulitengeneza sehemu maalum ya kuingilia. Wakati akihisi labda atakutana na giza totoro. Hali ilikuwa tofauti. Kulikuwa na mwanga kama mchana. Akatanguliza kichwa na kuchungulia. Akashangaa baada ya kuuona ukumbi mkubwa kama wa mikutano. Lakini katikati ya Ukumbi huo alilala mtu akiwa katikati ya dimbwi la Damu.

HATARIIIIIIII
 
[05-31, 13:37] Ibrahim Masimba: NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 072

Wakati akidhani macho yake yatakutana na giza, hali ilikuwa tofauti, macho yake yakakutana na mwanga. Na haukuwa mwanga tu bali kulikuwa na ukumbi mkubwa tu. Ni katika ukumbi huo katikati ulilala mwili wa mtu, tena katikati ya dimbwi la damu. Akajivuta kwa juu na kuingia moja kwa moja kupitia sehemu ile. Baada ya kuingia akakiona kingine, kingine ambacho hakukidhania hapo mwanzo. Licha ya mlango mdogo wa kwenye silling board lakini juu ukishaingia kulikuwa na nafasi kubwa ambayo mtu unaweza kutembea pasipo na wasiwasi. Mdomo wa bastola ukiwa umetangulia mbele, kidole kikiwa tayati kuifyatua Risasi. Akatembea kuufuata mwili wa mtu yule, mwili ambao ulilala katikati ya dimbwi. Macho yake yalitizama kwa umakini, masikio yake yaliinasa mivumo yote na sauti ya kitu chochote. Muda mfupi alikuwa pembeni ya mwili wa mtu yule. Mwili ambao sasa aliugundua kuwa ulikuwa wa mwanaume tena. Mwanaume wa makamo mwenye umri wa miaka inayofikia miaka hamsini. Kisu kilikuwa tumboni huku damu ikivuja kama maji. Akamgeuza ili kuutizama mwili wa mwanaume yule. Muda wote mikono ilikuwa tayari kwa chochote. Sura ya mwanaume yule baada ya kumgeuza haikuwa ngeni machoni mwake. Haikuwa ngeni kwake na hata jamii pia. Alikuwa Baba Askofu Ibrahim Lexandre Rengima. Askofu wa kanisa katoriki Jiji dar es salaam. Alikuwa yeye aliyekuwa amelala katikati ya dimbwi la damu. Kisu kikiwa kimesimama tumboni. Akili yake ikasimama kwa muda, ikasimama kutokana na kulikuta hili ambalo hakulitegemea. Baba Askofu Rengima kuuawa. Pili jingine ni Masimba kumtuma kuja kumuua mtu katika Nyumba hiyo. Nyumba ambayo inaonekana ilikuwa ni ya Askofu, askofu anayeheshimika sana hapa nchini na hata Nchi za Jirani. Kwa nini Masimba amtume hapa? Je alimtuma akijua mhusika ni Baba Askofu? Nani amemuua Askofu ikiwa yeye ndiye alitakiwa kufanya hivyo? Yalikuwa maswali ambayo hayakuwa na majibu. Licha ya kutokuwa na Majibu lakini alitambua Masimba pekee ndiye mwenye majibu ya maswali haya. Akaona aichomoe simu yake Aongee na masimba. Wakati akiipeleka simu sikioni, akaisikia sauti ikimuita, sauti dhaifu na sauti iliyokatika hatua za Mwisho. Haikuwa sauti ya mtu mwingine, bali ilikuwa sauti ya Baba Askofu. Teddy akaikata simu haraka kisha kumuinamia Askofu. Akagusa mapigo ya moyo wake. Kwa mbali akausikia moyo ukidunda. Wakati akitaka kujua nini cha kufanya akaisikia sauti ya Askofu ikimwambia. "Chu..chu.chukua ba..hasha pale me..mezani umpelekee ma..masimba. harafu ne..neenda nyumba ...naa namba 123 shekilaaang.... kabla hajamalizia kauli yake. Akashuhudia askofu akinyooka na kutulia. Alikuwa tayari amekata Roho. Teddy akainuka na kuelekea mezani. Meza ambayo aliambiwa kuna bahasha. Bahasha ambayo ilitakiwa kumfikia Masimba kwa wakati ule. Masimba huyu huyu aliyemtuma aje hapa kuitoa roho ya mtu. Hilo lilimshangaza na kumchanganya. Licha ya kuchanganyikiwa huko, lakini alitakiwa kuichukua bahasha kisha kuelekea Shekilango nyumba namba 123. Akaangalia mezani kwa juu hakuona chochote. Lakini alipotizama kwa makini akauona mchoro ukielekeza mahali fulani. Ulikuwa mchoro uliofichwa kwa macho ya kawaida. Mchoro ambao hauwezi kuonekana kwa macho ya watu wengine. Hapo akatambua Askofu alikuwa ni Zaidi ya Askofu. Michoro yake ilisadifu kile kilichopo ndani yake. Kile kilichopo katika ubongo na utaalamu. Kifupi kwa michoro ile alitambua Askofu alikuwa ni Jasusi. Je alikuwa jasusi wa upande upi? Teddy hakulisubiri Jibu. Tayari sekunde hii alishaibeba bahasha na alikuwa akishuka kuelekea Nje. Wakati anakaribia sehemu ile maalum ya kupitia simu yake ikapata uhai. Akaitoa kwa haraka. Kutizama mpigaji alikuwa Masimba.

Akaipokea kwa Haraka. "Usipitie ulipoingilia, pita nyuma ya nyumba kuna mlango wa Siri. Hakikisha unatoka salama." Aliongea masimba na muda ule ule simu ikakatwa. Teddy akashangazwa na hili. Hili la masimba kujua kile ambacho yeye anafanya. Kwa mara ya kwanza tokea wawe wapenzi akakili kuwa hakukosea kuwa na mwanaume huyu. Lakini hili la kujua kile anachokifanya ndani pekee ndicho kilichomsymbua. Kilichomtesa na hata kumshangaza. Akafuata maelezo yote. Muda mfupi alikuwa barabarani akielekea Shekilango. Bado kizungumkuti cha askofu alikuwa nani kilimtatiza. Kutoka magomeni Kagera mpaka Shekilango hapakuwa mbali sana. Hivyo kwa usafiri wa bodaboda alitumia dakika nne tu kufika hapo. Akashuka pembeni mwa ukumbi maarufu kwa Disco Uitwao Sunsiro. Baada ya kushushwa hapo na kumlipa dereva wa pikipiki. Teddy akachepuka mpaka pembezoni mwa Pub fulani iliyokuwa pembeni mwa barabara. Baada ya kukaa na kuagiza kinywaji, teddy akaanza kunywa taratibu huku akitizama kule ilipo barabara ya kuelekea sehemu husika aliyoambiwa na Askofu. Macho yake yalikuwa yakinasa na kufuatilia kila sura ya mtu amba gari iliyokuwa ikitokea kule. Wakati akiendelea kutizama kama ataona chochote, akashangazwa na kuiona gari moja yenye nembo ya Ikulu ikitoka maeneo hayo hayo ya Legho ikielekea barabara iendayo kule. Gari ya ikulu? Ndio swali lililogonga kichwa Cha teddy. Kengele ya Tahadhali ikaendelea kugonga kichwa chake. Gari ya ikulu maeneo haya inafuata nini? Ama kuna kitu ikulu inakijua? Ni maswali yaliyopita kichwani kwake. Akataka kuwasiliana na masimba. Lakini kabla ya kufanya hivyo akamuona mtu ambaye aliufanya moyo wake Upige. Macho yake Yalimuona Veronica Senka, Veronica yule yule aliyemuona kule bandarini. Lakini huyu hakuwa anaelekea kule, bali alikuwa akitoka kule ilipoelekea gari yenye nembo ya Ikulu. Akayaacha macho yake yamuangalie mwanadada huyu. Alikuwa akitembea pasipokuwa na wasiwasi. Hilo pia likamsisimua. Kujiamini kwa veronica kilikuwa kitu kilichomvutia sana Teddy. Aliwataka watu wa aina hii na kuwahusudu. Hilo likamfanya aendelee kumtizama. Kumtizama kulikoishilia kwenye gari moja iliyopaki pembezoni mwa barabara. Hapo akamuona Vero akipanda kisha gari kuwashwa na kuondokewa taratibu. Bado Teddy hakutubutu kuinuka. Bado aliamini uwepo wa watu katika eneo hilo. Watu wanaotizama nani ataifuatilia gari ile. Akaendelea kukausha na kujikausha. Dakika mbili kupita baada ya Vero kuondoka, akaiona ile gari yenye nembo za ikulu ikirudi. Hata ilipopita macho yake yakawanasa watu wanne waliokaa sehemu tofauti tofauti wakiinuka na kila Mmoja kuelekea kwake. Hilo likamfanya atabasamu. Atabasamu kwa kuwa aliutambua uwepo wa watu hawa. Akauvuta muda tena na tena. Aliuvuta muda katika namna ya kuangalia mazingira. Kuangalia endapo kulikuwa na mtu mwingine. Lakini hapakuwepo na dalili hiyo. Kabla hajainuka kuelekea huko akaona amtaarifu Masimba kuhusu kile alichoshuhudia. Kile alichokiona kwa macho yake. Gari yenye nembo ya Ikulu na kumuona veronica. Akautuma ujumbe katika lugha ya mafumbo, lugha ambayo haikuwa rahisi kusomwa na askari ama mtu yeyote. Hata baadhi ya watu wa Idara ya ujasusi hawakuweza kuielewa lugha hiyo. Akavuta muda ili kuyapata majibu, alivuta muda kupata majibu kutoka kwa masimba. Lakini Muda ukasonga pasipo masimba kujibu ujumbe wake. Hilo likamjulisha kuwa inawezekana Masimba hayupo sehemu Husika. Ama alikuwa msambweni. Hilo likamuinua Teddy kutoka sehemu aliyokaa. Sasa alikuwa akielekea kule alipoagizwa na baba Askofu. Akatembea kwa umakini kwa mwendo wa pole pole. Umbo lake la kike kike likamfanya aonekane kama mpita njia. Kwa kuwa hakuwahi kufika maeneo hayo, ilimbidi aanze kuitafuta nyumba husika. Alizunguka mitaa mitatu, mtaa wa nne akafanikiwa kuiona nyumba husika. Hii ilikuwa nyumba ikiyojengwa mfano kama wa nyumba ya baba Askofu.

Lakini tofauti ilikuwa ni uwezekwaji. Wakati ya baba Askofu ikiezekwa kwa Vigae. Hii ilikuwa imeezekwa kwa bati. Lakini ujengajwi ulikuwa wa aina moja. Hilo halikutegemewa na Teddy. Alipiga hatua kuifuata nyumba hii akiwa makini kabisa. Kuiona gari yenye nembo ya ikulu kisha Veronica. Kukampa picha kuwa lolote linaweza kutokea katika Eneo hili. Hakujua kwanini lakini kitendo alichokiona muda mfupi uliopita aliamini kuna kitu kizito sana. Akalifikia geti la nyumba ile. Akafanya kama alikofanya kule kwa Askofu. Lakini hata hapa hali ilikuwa kama ile, hali ikuwa ukimya pia hapakuonekana uwepo wa watu ndani ya nyumba hiyo. Akaligusa geti kwa mara nyingine. Geti lilikuwa wazi kama lilivyokuwa wazi kule kwa askofu. Akalifungua na kuingia ndani pasipo ukelele wowote. Magari manne ya kufahari yaliyoegeshwa ndani uzia wa nyumba ile yalimjulisha kuwa huyu mtu alikuwa ni mwenye uwezo. Akatembea safari hii bastola yake ikiwa tayari mkononi. Nyumba hii ilimpa wasiwasi kutokana na ilivyokuwa katika ukimya. Hata alipoufikia mlango bado hapakuwa na chochote kile. Akausukuma mlango kidogo, akauona mlango ukijifungua. Macho yake yakatembea ndani katika uharaka wa aina yake. Safari hii sebule haikuwa kama kule kwa askofu. Sebule hii ilikuwa hovyo hovyo kabisa kuonyesha hapakuwa na kitu cha Heri. Kila kitu kilikuwa kikizungumzia ushari na unyama. Damu sambamba na Jicho moja la mtu ni vitu vilivyokuwa chini ya sakafu ya sebule. Akaitizama hali ile kwa umakini mkubwa sana. Punde simu yake ikaupata uhai tena. Akaitoa huku bado umakini ukiwa ndani yake. "Ondoka sehemu hiyo upesi." Ulisomeka ujumbe huo. Ujumbe kutoka kwa Masimba. Teddy akaganda kwa muda, akaganda katika namna ya kushangaaa. Kabla hajajua kipi cha kufanya Akalisikia geti likifunguliwa. Kufungukiwa kwa aina fulani ya kutia hamasa. Alipichungulia akawaona watu kama sita wenye silaha
[05-31, 13:37] Ibrahim Masimba: Walikuwa watu sita waliokamatia Bunduki kubwa. Walikuwa wakiingia hapo ndani mfano wa watu wanaokwenda vitani. Teddy akatulia akiwatizama walivyokuwa wakitenbea. Akajiondoa pale taratibu na kusogea mbele kidogo sehemu ambayo palikuwa na kujichumba. Akajibanza hapo bastola yake ikiwa tayari mkononi. Punde akausikia mlango wa sebuleni ukitiwa teke kisha watu wakasikika wakiingia kanakwamba walikuwa katika uwanja wa vita. Bado Teddy akaendelea kutulia akuwasoma watu hawa. Watu ambao walionyesha kuwa kimya baada ya kuingia hapo. Hata yeye hakuwa katika hali hiyo. Kifo cha Askofu, Bahasha aliopewa ikiwa ni pamoja na kuagizwa ni vitu ambavyo hakutaka kuondoka hapo bila kuondoka akiwa na majibu kamili. Hakuogopa kifo kwa kuwa alitamani kuuawa na alipenda kuua. Akasubiri kwa hamu kubwa, kidole chake kilikuwa tayari kuruhusu risasi. Licha ya kutulia kwa muda huo, bado sebule ilikuwa kimya na bado hapakusikika vishindo wala minong'ono. UKIMYA ULITAWALA KANAKWAMBA HAPAKUINGIA WATU
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 073

Walikuwa watu sita wenye silaha nzito. Watu ambao waliingia pale katika namna ambayo hata Teddy mwenyewe alijiuliza. Ukimya ulitawala kanakwamba hapakuwa na watu walioingia hapo sebuleni. Mkononi alikamatia bastola yake aina ya semi automatic pistol huku sehemu fulani ndani ya mavazi yake kukiwa na Sig-sauer p20 nayo ikiwa imetulia ikisubiri kuifanyakazi hiyo. Ukimya, kwa nini ukimya wakati watu wameingia hapa muda mfupi uliopita? Tena watu sita wenye silaha nzito? Huu ukimya ni wa nini? Wameenda wapi watu hawa? Ni maswali aliyojiuliza Teddy huku mikono yake ikiwa tayari. Sekunde, dakika na sasa ilikuwa inafika dakika ya tatu, babo ukimya, bado hapakusikika chochote kutoka sebuleni. Hata nyayo hazikusikika. Sehemu ilikuwa kimya, ukimya ambao ulimaanisha hakuna kitu chochote. Teddy hakutaka kuamini hilo. Bado aliuamini muda, bado aliitambua Subira kama kitu muhimu sana kwenye eneo kama hilo. Semi Automatic pistol Bado haikuondoka mkononi. Bado kidole hakikutoka sehemu ya kufyatulia Risasi. Macho yake yakaanza kulizoea giza lilikilokuwa limeanza kutanda kwenye nyumba ile. Kuanza kuingia kwa giza kukampa uwezo wa kuona kilichokuwa kikiendelea. Kwani ni wakati giza likiingia akahisi kuisikia michakato ya hatua za watu. Michakato ya miguu ikitembea katika aina ya kunyata. Akajiweka tayari, akajiweka akikabiliana na watu waliokuwa wakisogea. Punde akakiona kivuli mtu, mtu ambaye mavazi yake yalifanana kabisa na giza lililopo mle ndani. Mdomo wa bastola ukainuka na kutizama kule kilipo kivuli. Muda mfupi alikuwa akimuona mtu akipita akiwa kimya kabisa. Hakusubiri ainue mguu wa pili. Semi automatic pistol ikakohoa. Ikatoa cheche na kumwaga njugu. Ulikuwa mlio mfano wa chafya ama kuvunjwa kijiti. Risasi ilikuwa imepenya kooni kwa mtu yule. Hakuweza kuongea wala kupiga kelele. Akaporomoka chini akiwa amelishika koo lake. Teddy katulia Tena na kuhama Upande mwingine, akasimama pembeni mwa mlango. Macho yake yalikuwa mbele, macho yake yalikuwa yakitizama mlangoni. Lakini safari hii ukimya ulirejea Tena. Hapakusikika chochote tena. Hata zile hatua za watu zikakoma na nyumba nzima ikawa kimya. Ni wakati huo akiwa ametulia akausikia mngurumo wa gari nje nyumba hiyo. Mngurumo ambao uliishia getini kuonyesha kuwa gari ilikuwa imesimama nje ya geti la nyumba hiyo. Mara akalisikia geti likifunguliwa kisha mngurumo wa gari ukasikika tena. Safari hii gari hii ilikuwa ikiingia ndani ya uzio wa nyumba hii. Teddy akajiuliza huyu ni nani?kabla hajapata jibu. Akausikia mlango wa ndani ukifunguliwa. Kisha michakato ya miguu ya watu ikasikika kusogea. Bado Semi Automatic ilikuwa mkononi akisubiri kutoa hukumu nyingine. Miguu hii sasa ilikuwa ikiukaribia mlango wa chumba alichokuwa ametulia. Miguu ikasikika tena safari hii ikiwa katika usawa wa chumba kile. Lakini cha ajabu hakumuona mtu, hakumuona akipita na hata kivuli chake hakukiona. Huyu ni nani? Mbona kama mzimu? Lilikuwa swali ambalo halikudumu sana akauhisi ukelele wa sauti ya mtu ukitokea mbele kidogo ya pale alipojibanza. Hakuliacha hilo limpite, hakuliacha liondoke na hata kwenda hivi hivi. Akajitoa taratibu, alitaka kwenda kuona na hata kumuangalia huyu mtu. Alitaka kushuhudia na kuona huyu mtu alikuwa nani na kwanini ameingia pasipokuwa na wasiwasi. Bastola mkononi huku macho yakipambana na Giza ndani ya nyumba ile, Teddy alinyata kwa umakini mkubwa mpaka nje ya chumba kile. Licha ya kunyata na kutokea hapo, lakini hakuona chochote zaidi ya ukimya kwa mara nyingine. Hata yule mtu aliyekuwa akipiga ukelele hakusikika tena. Nyumba ikarudi kwenye kimya tena. Hilo halikumbabaisha jasusi huyu wa kike. Bado aliyatembeza macho yake, macho yaliyozoea giza. Hazikupita sekunde tano, akaisikia kelele tena ikitokea juu. Hii ilikuwa sauti ya mtu wa makamo. Mtu ambaye alionyesha kuwa na umri mkubwa. Safari hii sauti ya mtu huyu ilikuwa ikitoka kwa maumivu ya kipigo ama kubanwa na kitu. Alikuwa akilia kama mtoto huku akisema hajui kitu huku akiwataka wauaji wakamuone Baba Askofu Ibrahim Lexandre Rengima. Kutajwa kwa jina la baba Askofu katika mateso ya mtu huyu anayelia kukamfumbua tena kutoka kwenye giza. Alitambua mtu huyo anayepiga kelele ndiye mtu aliyetumwa kuja kumuona na kumuokoa. Lakini kama ni hivyo kwa nini Masimba alimtuma kwenda nyumbani kwa Askofu kumuondoa mtu? Mtu mwenyewe ni nani na kama ni Baba Askofu kwa nini nimemkuta akiwa amejeruhiwa? Ina maaba kulikuwa na mtu mwingine zaidi ya Askofu na mtu huyu anayepiga kelele? Yalikuwa maswali mfululizo, maswali yaliyopita kichwani kwa Teddy. Maswali ambayo hayakuwa na majibu kwa wakati ule wakati sauti ya mteswaji ikizidi kutamalaki.

Akauona upuuzi kuendelea kujiuliza, upuuzi ambao ungemfanya akose kile ambacho alitakiwa kukipata. Akaliacha eneo hilo sasa akielekea sehemu hiyo. Kila alipozidi kusogea ndipo hapo sauti zilipozidi kutanda katika masikio. Akiwa amebakisha hatua kazaa kufika sehemu husika, akawa anakisikia kile ambacho kilikuwa kikitamkwa kutoka ndani. Kikitamkwa na Mteswaji kujibu maswali ya Mtesaji. "Tunaitaka bahasha uliopewa na baba Askofu. La sivyo nitakuua sasa hivi." Aliisikia sauti hiyo ambayo ilipenya mpaka ndani ya moyo wake. Sauti ambayo aliijua. Ilikuwa sauti Ya Ben. Sauti ya mtu katili kuwahi kumuona.

"Sina bahasha yoyote, kama mnaniua niueni tu." Ilisikika sauti hii. Sauti ya mtu aliyetayari kufa sababu ya bahasha ambayo ilikuwa mikononi kwake. Akauona ulikuwa muda wa kufanya kitu, muda wa kufanya kile ambacho kingemuokoa mtu huyu. Ulikuwa wakati wa kumuua Ben. Akatoka hapo sasa akikifuata kile chumba. Lakini kabla ya hapo alitaka kuitafuta swichi ya kuwashia taa. Alitaka kuitumia mbinu hiyo kujua watu hawa wako wapi. Akaendelea kupapasa huku na huko kutafuta anachokitafuta. Baada ya kutafuta sana akaiona swichi hiyo. Huku bastola ikiwa tayari akaifyatua Swichi. Nyumba yote ikawa nyeupe. Watu wanne waliojificha pale ukumbini wakashtushwa na kuduwaa kwa sekunde. Ni wakati wa mduao huo, semi automatic ikakohoa na kumwaga risasi. Watu watatu waliku wamepaa angani kwa Risasi na hata walipokuja kufika chini walikuwa marehemu. Hilo halikutegemewa na watu waliokuwepo hapo ndani. Milio ya risasi ikalindima kutoka kwa wakora hawa waliokuwa wakifyatua risasi hovyo bila kujua hatari mbele yao. Teddy bado alikuwa ametulia, bado alikuwa akiwatizama wakora wale walivyokuwa wamehamanika. Alitamani hata kucheka, alitamani hata kuwaita. Lakini muda huo akamuona mtu akitokea katika aina iburudishayo moyoni na hata machoni. Mtu huyu alikuwa akiyupa kwa wepesi wa karatasi, wepesi wa sisiminzi na hata wepesi wa ubua. Alitoka hapa akienda pale katika namna ambayo ilivutia sana. Alikuwa masimba huku mikono yake yote ikiwa na bastola. Mkono wa kushoto alikuwa na Bastola aina ya PPQ (polizei pistole quick defense) iliyotengenezwa Nchini Italy na mkono wa kulia alikamatia bastola aina ya Springfield XD ambayo hii ilitengenezwa katika nchi ya Marekani. Alitia raha kumtizama na hata kumuangalia, Teddy akapandwa na Mzuka, mzuka wa Kushambulia. Wakati mara ya kwanza alikuwa atumia Bastola moja, Safari hii akaichomoa bastola yake nyingine. Bastola iliyotengenezwa nchini Brazil. Wakati kulia kulia alikuwa na semi automatic, kushoto alikuwa na SIg -sauer p320. Masimba alikuwa akishambulia kutoka mbele, teddy naye alikuwa akimlinda masimba kwa mbele. Ilikuwa burudani katika aini yenye kutoa raha. Kila risasi ilipelekwa sehemu husika, kila ilipotumwa, risasi ilikwenda hapo. Hakufika wala kuchukua Dakika. Zilikuwa sekunde thelathini tu. Kila mkora alikuwa yupo chini akivuja damu.. alikuwa marehemu huku matundu ya Risasi yakionekana Kifuani. Wakatizamana katika macho ya upendo, macho ya kujali na hata kuaminiana. Macho yao yalikuwa yakiongea mapenzi. Hawakujali walikuwa sehemu gani, midomo yao ikakutana katika namna fulani uburishayo nafsi. Lakini hawakufika katika lengo lao, lengo la kuburudika zaidi. Kwani macho ya masimba yakamuona mtu. Mtu ambaye alikuwa ameuinua mdomo wa bunduki yake aina ya combart shotgun akiwa lenga wao. Akiwa lenga pale waliposimama. Hakuwahi kufanya alichotaka kukifanya. Alifanya kile ambacho akukitarajia. Risasi mbili zikatoka mahali apo.. moja ikatua begani kwa Ben na nyingine katikati ya paji la uso. Ben ajayumba na Bunduki yake mkononi na kwenda kujimwaga chini. Alijibwaga tayari akiwa maiti. Wakati huo ndio kwanza Teddy alikuwa akigeuka. Akigeuka kuangalia kile ambacho kilitendwa na kufanywa. Ben alikuwa chini kichwa kikiwa kama chapati. Risasi ilikuwa imefumua kichwa cha ben. Teddy hakulitegemea na hata kuliwaza. Aliporudisha macho Usoni kwa Masimba akakutana na tabasamu. Tabasamu lililomfanya Teddy ajilaze kifuani kwake. Kifua ambacho kilikuwa maalum kwa sababu yake. Ikawa hiyo.

KESHO
 
Dah wadau ibra ni wa tofauti sana,anafanya kazi anayoipenda kwa moyo mmoja,tujitahidi na sisi kutuma michango yetu ili tuzidi kumpa moyo.
Sure, anatupa tunachokihitaji. Tu. Support.
 
Kuna wachache ndio wana kithamini ninachokifanya. Kuna wakati nafikiria kusitisha humu ili niwatumie kwa njia ya whatsap wale wanaojali na kunithamini
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom