Riwaya: Nitakupata tu

NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 067

Hata macho ya wana usalama wengine yalikuwa yakimtizama. Mikono mifukoni tayari kwa kufanya chochote. Bado vero alikuwa akitembea katika aina ile ile ya kuwachanganya wanausalama. Alikuwa akionyesha kitu ambacho wana usalama hawakukijua wala kukigundua. Lakini wakati akifanya yote hayo hakujua kama alikuwa akiangaliwa na mtu mwingine ambaye yeye hakumjua na hata kule kugundua kama yeye ndio yule. Hakuwa peke yake katika kutokujua na hata kugunduahuko. Hata watu ambao walikuwa pembeni kidogo hawakumuona mzee huyu ambaye alikuwa akifuatilia kila kitu. Licha veronica kutembea huko akiutupa mkono huku na huko macho yake yakipelekwa sehemu fulani, haikuyasumbua macho ya mwanaume huyu aliyekuwa amesimama pembeni. Wakati wanausalama wakiyumbishwa na uelekeo wa macho yake, hukunyuma bado mtu yule aliuangalia upande ule, upande ambao haukuwa ukitizamwa katika namna fulani ivutiayo. Upande ambao haukutizamwa na veronica. Mtu huyu akajikuta akivutiwa na mwanadada huyu katika kule kutembea, kutenda na hata kudanganya. Hii ilimfanya aamini kuwa huyu ni jasusi wa hali ya Juu. Jasusi mwenye uzoefu wa kutisha. Wakati akiyapa burudani macho yake akamuona Teddy akigeuza kichwa huku na huko. Hata mkono wa teddy ulikuwa umeshuka katika namna ambayo ni ngumu kugundulika kwa macho ya kawaida. Hata naye alikuwa amekinusa kitu, hata huyu alikuwa amegundua uwepo wa hatari mahala hapo. Masimba kubadilika, wana usalama kuhaha huku na huko ni kitu ambacho kilimvutia Teddy. Lakini mpaka watu wanafika nyumbani kwa mama wa marehemu hapakuwa na kilichotokea. Kila mtu alikuwa akihangaika huku na huko. Teddy akahitaji kuongea na masimba katika namna yoyote. Macho yake yakaifanyakazi ya kumuita mwanaume yule. Alihitaji kufahamu nini ambacho kinaendelea. Nini ambacho kinafanyika. Lakini akiwa bado ana mtizama akamuona Masimba akiongea na simu, kilichofuata ni kuondoka katika eneo lile akumuacha Teddy akishangaa.

*****
Ulikuwa ukumbi tulivu wenye ustarabu wa hali ya juu tofauti na kumbi nyingi za burudani hapa mjini Dar es salaam. Ulikuwa ukumbia uliopo kando kando mwa bahari ya Hindi maeneo ya Kawe. Watu walikuwa wengi wakiburudika kwa vinywaji na hata kucheza muziki. Wengi waliokuwepo ukumbini hapo walikuwa ni askari wa jeshi la wananchi kutokana na ukumbi huo kuwa karibu na kambi ya jeshi ya Lugalo. (LUGALO MILITARY BASE). Pembeni kabisa mwa ukumbi ule alionekana mtu mzima wamakamo akiwa amekaa kwenye kiti akionyesha kuendelea na kinywaji huku wakati mwingine akionyesha kutingisha kichwa kufuatia mziki uliokuwa ukiporomoshwa hapo. Muda wote huo hakuacha kuutizama mlango wa mbele na hata ile milango ya siri ambayo waliitumia wao kama wao. Huyu alikuwa mzee Godliving Kimaro Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa. Alikuwa hapo kwa miadi ya kukutana na mzee mwingine ambaye alkuwa mmoja kati ya wale watu watano wanaosemekana ndio wanaoiendesha nchi hii na kumpangia mkuu wa nchi nini cha kufanya. Huyu alikuwa ni mtu mkubwa katika Jeshi la wananchi akiwa na Cheo cha meja jenerali.Yalikuwa maongezi ya siri kuitishwa katika eneo hilo licha ya uwazi huo. Siku zote wao waliamini mazungumzo ya Siri hufanyika hadharani ili kuondoa mashaka na kutokutiliwa wasiwasi. Hawakutaka kukutana kwenye maofisi ama mahotel makubwa kuhofia kumulikwa na watu. Hivyo waliiona sehemu ile kuwa ni zuri na yenye usalama. Askari kadhaa waliomuona mzee huyu akiingia hapa walimtupia macho bila kuhisi chochote kwa kuwa ilikuwa kawaida kwa mtu huyu kuingia hapa kila siku. Meje Jenerali Louis Chomboko alitembea taratibu kwa mwendo wake wa kikakamavu mpaka sehemu ambayo amekaa Chief. Alipomkuta alimsalimia katika nidhamu zote za kijeshi, na baada ya hapo wakakaa. "Ndio bwana kimaro naona safari hii unapata muda sana wa kupumua. Nimesikia unavijana wako wamekufanya utulie kabisa licha ya hili tukio la kuuawa kwa Waziri Mkuu.," alianza meja jenerali Chomboko huku akimtizama Chief kwa makini. Chief hakuongea kwa haraka, alichokifanya nikukaa kwa muda akifikiria kisha kwa sauti ya upole akanena.

"Ni kweli unayosema bwana Chomboko, lakini ni vijana hao ambao wanaufanya ofisi yangu niione chungu.".... " Uione chungu wakati kuna ushahidi Ikulu? Aliongea Mej-jenerali huku akimtizama Chief kwa mshangao. Mshangao ambao haukuwa na kikomo. "Najua hilo, lakini kuna jingine limetokea leo. Siamini kama hujalisikia. Hilo ndio limenfanya mkuu anipigie simu kuniuliza kulikoni. Aliongea Chief huku akiipeleka Glass ya p0mbe kinywani.

"Lipi hilo? La kuuawa kwa Mkurugenzi muajiri wa Bandari na sekretari wake? Sasa Mr Chomboko akauliza huku umakini ukiongezeka.

"Yeah ni hicho kitu.. Rais amenipigia na kuniuliza inakuwaje kijana wako anaua watu hovyo.. Anachotaka yeye hawa watu ambao ushahidi upo wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria. Hivyo ameagiza niongee na Kijana wangu ili aachane na hili suala. Aviachie vyombo vya usalama viifanyekazi yake." Alijibu Chief huku uso wake ukionyesha kukata tamaa. Ukimya wa Ajabu ukapita kati yao. Kila mmoja alikuwa akitafakari kitu chake. "Anaposema awaachie wana usalama wafanye kazi yao, kwani Masimba ni mtu gani? Ina maana yeye hatoki ndani ya usalama? Ni nani angejua mabaya ya huyu bwana kama sio masimba kuyaibua? Hapaswi kufanya hivi.. Idara za usalama lazima zifanyekazi zao kwa uhuru. Sioni Tatizo la masimba hapo. Na kukwambia ukweli ni kwamba Masimba hakuuwa yeye, bali watu wale waliuliwa na watu wengine ili kufumbwa mdomo wasiropoke. Masimba alishagundua baada ya kumuua mkora mmoja pale hotelini, aligundua kuwa mtu yule alikuwa mmoja kati yao na alikuwa akipitisha vitu vingi na kuajiri watu ambao hawafahamiki. Sasa sidhani kama Rais anajua haya mambo." Aliongea meja jenerali Chomboko kwa kirefu akionyesha kufahamu kila kitu ambacho kilikuwa kikiendelea. Maelezo ya Mr Chomboko yalionyesha kumburudisha sana Chief, sasa alikuwa akianza kutabasamu kwa mbali. Kutabasamu hasa baada ya kujua kumbe watu hawa nao wanafahamu kile kinachoendelea. "Kumbe ndiyo hivyo? Sasa mbona hamuongei naye kumueleza hili? Hii hii kazi anayoifanya Masimva ni Ngumu.. ni kazi ambayo inalibeba Taifa. Amepoteza mama kwa sababu ya nchi yake. Aaachwe asafishe hiki alichokianza. Ndio maana nimekuja kuongea nawe ili umwambie hili. Kijana aachwe afanyekazi asichanganywe." Akasema Chief huku akionyesha kuchoshwa na kauli ya mkuu wa nchi. "Haina Sababu ya kuchoka, ujumbe nitaupeleka baada ya kutoka hapa tu. Na ninaamini ataelewa na kijana ataendelea kuifanya kazi hii." Aliongea Meja Gen. Chomboko. Wote wakatabasamu na kucheka kwa pamoja.

*****

Alitakiwa aiache kazi ya kuwafuatilia kina Jimmy, alitakiwa kuviachia vyombo vya ulinzi na usalama viifanye kazi hiyo. Kichwa chake alikiinamisha chini akifikiria watu waliouawa kwa sababu ya kazi ambayo leo alikuwa akiambiwa aiache. Asteria, Mwamvua, Dada wa Asteria, mumewe na hata mtoto wao. Dee plus na Vicky kisha mama yake Mzazi. Nani anaweza kurudisha roho hizi? Nani anaweza kuwarudisha watu hawa? Je nani ataurudisha utimamu wa mateja waliotopea kwenye matumizi? Yalikuwa maswali yaliyokisumbua kuchwa chake. Alichokifanya ni kuinuka na kuendea mlango ili kutoka nje akaanze kazi ya kumfuatilia mwanadada Veronica. Wakati akiufungua mlango ili atokea, akakutana uso kwa uso na Teddy aliyekuwa amesimama hapo mlangoni. Wakatizamana kwa muda wa sekunde tano. Kutizamana kuliko mfanya Masimba Arudi chumbani akifuatiwa na Teddy. Mlango ukafungwa wakisimama na kutizamana. "Nimekuja kuongea na wewe, nataka nimjue aliyemuua mdogo wangu Vicky." Aliongea Teddy Taratibu Akimuangalia Masimba Usoni. "Hayupo tena hapa Duniani. Naona Roho yake inakaribia kufika mbinguni. Nimeshamuua." Alijibu masimba akimtizama Teddy. Hata Teddy naye akamtizama. Wakatizamana na kutizamana. "Rais Ametoa amri kuwa niachane na kazi hii ya upelelezi juu ya haya yote yanayoendelea. Ameniambia niviachie vyombo ya usalama." Aliongea Masimba safari akijibweteka Chini. Teddy hakujibu kwa haraka. Bali alimuangalia kwa muda kisha kwa sauti ya Uchungu akanena. "Kama anaweza kurudisha roho za walipotea katika mapambano haya tutaacha. Kama hawezi basi mpaka nihakikishe Risasi zangu zinapasua kichwa cha Jimmy. Watu wameharibu vijana harafu waachwe. Hata sisi ni wana usalama siwezi kutii wala kukubali. Nitaacha kwa mdomo lakini nitafanya kwa vitendo." Aliongea Teddy akionyesha kutokuwa na masihara. Masimba alimuangalia kwa muda kisha kwa sauti ile ile ya kuonyesha kuwa hakuna masihara akanena. "Ningeomba hii kazi uniachie mwenyewe, sitaki kukupoteza Teddy.. nataka nikutengeneze uwe mwanamke wa maisha yangu." .. Teddy akamuangalia Masimba kwa Muda. Alimtizama kanakwamba alikuwa hamfahamu. "Masimba hii ni kazi yangu sio yako. Ulipoifanya panatosha. Leo nitaanza kukuletea Kichwa cha Ben, sitaki mdogo wangu asindikizwe na muuaji wake nataka aende na watu wengine wengi tu."
 
[05-25, 13:52] Masimba Wa Teddy: NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 068

Yalikuwa maneno ya Teddy akionyesha hakuwa na masihara katika hilo. Suala la kuanbiwa wao waachane na suala lile lilikuwa ni tusi kubwa kwao. Ni siku ile tu amemzika mdogo wake kutokana na suala hilo. Kumwambia aliache lilikuwa ni tusi kubwa, tusi ambalo kamwe wasingelivumilia. "Ni kweli hatuhitaji kuingiliwa katika hili, hatuhitaji kufundishwa nini cha kufanya. Nimemuomba Chief akaonane na Mzee Louis Chomboko wazungumze ili iwe rahisi kwetu kuifanya hii kazi. Pia nataka wewe uende bandarini ukaonane na yule binti wa leo pale makaburini. Yeye ni mfanyakazi wa pale na siku ambayo waliuawa watu wawili yeye ndiye niliemkuta mapokezi. Tukimfuatilia huyu tunaweza kupata mengi kuhusu Jimmy na Suresh. Mimi nitakwenda pale kwenye mazishi ya mbunge wa kigamboni siku ya kesho. Naweza nikanusa na kupata mawili matatu. Lakini pia umakini unatakiwa kuna vijana wenzetu wanakesha wakinusa hili ili kuijua mizizi ya watu hawa. Na ili kulimaliza hili nilazima tujue kila kitu kinachohusiana na hii biashara ya madawa sambamba na Nyara za serikali. Narudia tena hawa watu ni hatari, kwa jinsi walivyojibadilisha na kumuua Vicky kisha kuondoka pasipo kujulikana ni wazi watu hawa ni hatari sana. Kuwa makini na sihitaji kukupoteza tena." Aliongea Masimba akimuangalia Teddy usoni. "Nimekuelewa Masimba, nimejeruhiwa na kifo cha Vicky, nataka nikuonyeshe kuwa serikali haikukosea kunipeleka Urusi na hata Cuba katika mafunzo ya juu ya ujasusi. Nisamehe kwa kauli zangu za pale mwanzo. Hasira zilinizidi.. naomba unisamehe mpenzi." Aliongea Teddy huku akisigea na kumkumbatia masimba.

******

Pilika pilika zilikuwa nyingi katikati ya jiji la Dar es salaam kwa asubuhi hii, watu wenye haraka walikuwa wakihaha wakishika hiki na kushika kile. Walikuwa wakitoka hapa na kutoka pale. Vibaka na wezi wa mifukoni nao hawakukosekana hapo katika kuitafuta riziki yao. Ndani ya jengo moja lililopo mtaa wa mkwepu pale posta mpya. Watu sita walikuwa wameizunguka meza tokea asubuhi hiyo mpaka muda huo pasipikupata muafaka. Kila mmoja alikuwa akipingana na huyu kwa hoja ambazo ukizisikiliza zinaweza kukuvutia na kukufanya ukisikilize kile ambacho kinazungumzwa. Watu sita hao ambao walikuwa wamiliki na waanzilishi wa mtandao wa kuuza na kununua madawa ya nchini Tanzania, walikutana asubuhi hiyo kuzungumzia kile kinachoendelea katika mapambano yao dhidi ya wana usalama. Kitendo cha kuuawa watu wao wawili siku ya jana katika ofisi za bandari lilikuwa ni pengo la tatu kupata katika kundi hili ambalo lilitaka kuifanya Tanzania kuwa katika Himaya na Utawala wao. Tukio la kuuawa kwa Waziri mkuu, kulipuliwa kwa kambi yao ya Siri na kuuawa kwa mkurugenzi Muajiri wa mamlaka ya Bandari ni matukio ambayo yaliwafedhesha na kuwaumiza sana. Kwani waziri mkuu alikuwa ndiye mhimili mkubwa katika masuala yote ya usalama na upitishwaji wa mizigo yao popote pale katika mipaka ya nchi hii. Tukio la kulipuliwa kwa Secret Base ambayo ndio ilikuwa kambi ya kuhifadhia mizigo yao nalo lilikuwa tukio baya ambalo liliwatingisha kwa namna moja ama nyingine. Mzigo ulioteketea kwa moto katika kambi hiyo ya siri ulikuwa ni mara tatu ya mzigo ambao ulitoroshwa airport kabla ya kuibiwa na Masimba. Tukio la tatu ni la kuuawa kwa mkurugenzi muajiri .. hili pia ni tukio ambalo liliwashtua sana. Watu wao wengi katika kazi yao waliajiriwa hapo kwa nguvu ya mkurugenzi huyu. Mizigo yao mingi ya magendo ilikuwa ikipitishwa hapo kutokana na nguvu ya mtu huyu. Vijana wengi wenye mbinu zote waliingia nchini na kupandikizwa hapo kama wafanyakazi kutokanana nguvu za mtu huyu aliyeuawa. Hilo ndilo lililowafanya leo hii wawepo katika Jengo hili wakikutana hapo katika kulitafutia muafaka suala hili. Suala la mtu huyu aitwaye masimba sambamba na mwandani wake aitwaye Teddy. Watu wawili hao ndio watu ambao walikuwa wakiwakosesha Raha. Hawakuwa wakila na kulala usingizi sababu ya watu hawa wawili. Hawa wamekuwa ni mwiba mchungu kwao, mwiba ambao ulikuwa ukiwachoma huku ukiwaacha na Alama kama sio Vidonda. "Tumeshindwa Kumdhibiti Huyu Masimba na mwandani wake? Tuna vijana wangapi wenye ujuzi katika medani lakini mbona hawaonyeshi kile tunachokitambua.

Licha ya kumkamata masimba kwa mara mbili nzima lakini tumeshindwa kufanya maamuzu. Mamuzi ya kumuua. Hili ndio kosa ambalo tumlifanya. Tukio la vijana wetu kumuua Mkurugenzi mchana wa jana pia ilikuwa ni mbinu ya kuificha siri iliyofichika hapo. Lakini ukiondoa hilo ni kwamba pale pataandamwa. Wana usalama watapageuza Njia ya kupita. Njia ya kufika kila wakati ili kuutafuta ukweli. Ukweli wa kile kilichofichwa kwa risasi ya vijana wetu. Kumbukeni Bandarini na Airport ni sehemu ambayo kuna watu wetu wengi. Kujulikana kwa hili la Bandarini ni kutaka kujulikana kwa haya mengine. Ni wajibu wetu kuwaambia vijana wetu ni wajibu wao kuwa makini katika kuwafuatilia hawa watu. Hatuwezi kushindwa na mtoto huyu ambaye tulimlea wenyewe." Aliongea mjumbe mmoja uso wake ukionyesha kukosa raha kabisa.

"Ni kweli ulichokisema mwenyekiti. Hapa nilazima Bandarini na Airport wana usalama watapafanya ndio kwao. Kitendo cha mtu huyu kuuawa mbele ya masimba ndicho kitakachoamsha hisia za Masimba kuwa bandarini hapana usalama. Vijana wetu wamelikosea hili. Wamefanya haraka sana.
[05-25, 13:53] Masimba Wa Teddy: Alisema mjumbe mwingine ambaye wazo lake liliungwa mkono na wajumbe wengine. "Ni kweli tunahitaji kulifanya hili lisijirudie Tena. Nilazima wenzetu waliopo pale bandarini na hata pale Airport ni lazima tuwaondoe kwa kificho. Tukumbuke wote hapa tunadhamana na vyeo vya juu katika Serikali ya Nchi hii. Kumbukeni tukiliacha hili liendelee vitanzi vitakuwa halali yetu. Mimi naomba tufanye kazi moja ya kuwauwa watu hawa. Tuwaue watu wa bandarini Airport na hata wenzetu wa pale uhamiaji. Mauaji haya yafanywe na vijana wetu wakiongozwa Jimmy. Hili suala ni zito na ili kujiepusha ni lazima tuendelee kuwafumba watu midomo yao kabla huyu masimba na Teddy hawajawafikiq. Pia kuna suala ambalo nililisahau. Ni kwamba majira ya Saa nne usiku kuna kikao kilifanyika katika ufukwe wa Kawe. Kikao hicho kilikuwa cha watu wawili tu. Watu hao si wengine bali walikuwa ni Meje Generali Louis Chomboko sambamba na Mr Godliving Kimato Director General wa Tanzania Intelligence and Security Services (TISS). aliyenipa habari hizo hakuniambia kikao hicho cha watu wawili kilikuwa kikizungumzia masuala yapi. Sasa ni wajibu wetu kumpata Major General Chomboko ili tupate kujua kile ambacho kimezungumzwa." Aliongeza mjumbe wa tatu ambaye suala lake liliwafanya wajumbe wote sita wakae kimya kwa muda wakitafakari hilo. Wengi walimjua na kumtambua mzee Chomboko kutokana na wadhifa wake aliowahi kuushika akiwa Jeshi la wananchi wa Tanzania. Lakini pia walijua bado alikuwa afisa Usalama mwandamizi sambamba na ushauri wa kiulinzi na kiusalama anaoutoa ama kuwajibika kuutoa katika Serikali na hata vyombo vya kiusalama. Licha ya kujua hilo lakini hawakujua hili la kuwa kwake katika kitendo kile cha watu watano ambacho kilijulikana kama Finally system in the decisions. (Kitengo cha Mwisho katika Maamuzi). Hawakujua kuwa Meja jenerali Chomboko hakuwa mtu wa kufuatiliwa kwa urahisi kutokana na kutembea kwake na watu maalum ambao huwezi kuwaona katika namna yoyote. Watu ambao walikuwa mfano wa giza hata katika mwanga wa Jua la mchana. Watu ambao walikuwa hatari katika aina yoyote ya Mapigano ya mikono, silaha na hata mateke. "Hili lako limekuja katika Muda ule Muafaka. Muda ambao tunatakiwa tumlazimishe General chomboko aifanye kazi yetu. Lakini kabla hatujamuendea ni lazima tutekeleza mara moja katika kuwaondoa watu hawa katika maeneo tulioambiana hapa. Kwa kumalizia Naomba vijana waambiwe mara moja wawe macho na wawe tayari kwa Mapambano." Aliongea mwenyekiti wa mkutano ule, kisha kuufunga wakiahidiana kukutana jioni hiyo katika Jengo hilo hilo.

******
Macho yake yalikuwa yameelekezwa kwenye lango la ofisi za bandari akitizama kila mtu atokaye na aingiaye. Ushungi na baibui vilimfanya Teddy aonekane kama mwanamke wa kiislam anayefuata misingi yote ya Dini yake. Macho yake yalikuwa kule kumuangalia Veronica Senka. Msichana ambaye alianza kazi ya kumfuatilia tokea pale alipokabidhiwa na masimba. Alifika hapo mapema sana akitaka awe wa kwanza kuingia katika eneo hilo la bandari. Hata alipofanikiwa kuingia na kukaa kwa muda mrefu hakuwa amemuona mwanamke huyo. Alivumilia kwa muda mpaka pale alipomuona mwanamke yule akishuka kutoka kwenye gari moja ya kifahari aina ya Ranger Rover. Akatulia hapo akimwangalia mwanadada yule alivyokuwa akitembea. Mwendo wa mwanadada huyu haukuwa mwendo kama wa wanawake wengine. Mwendo wake ulisadifu ufedhuli. Ulisadifu roho mbaya na hata ukatili. Kwa mara ya kwanza akashangaa bandari kuajili mtu wa aina hiyo. Mtu ambaye muonekano wake pekee ulionyesha kule ambacho kimefichika ndani yake. Hilo likamfanya ahisi uwepo wa kitu kisichoeleweka hapo bandarini. Akatuliza macho yake kumuangalia kiumbe huyu. Wakati kiumbe huyu akiukaribia mlango wa ofisi ile, vijana wawili wakatokea kwa mbele yake kisha kumpa kitu kama kikaratasi. Baada ya kupewa kikaratasi hicho wale vijana wakapita wakimuacha mwanamke yule akiingia ndani ya ofisi. Hilo akaamua kuliacha. Punde akainuka tayari kwa kuanza na vijana wawili walioonekana wakimpa Vero kikaratasi. Aliondoka pale akihakikisha hatiliwi Shaka na Macho ya watu waliojazana Hapo. Macho ya upekuzi na hata udakuzi. Akafanikiwa kutoka nje ya eneo la bandari sambamba na vijana wale. Baada ya kutoka hapo akawaona wale vijana wakijipakia kwenye Ranger Rover ambayo muda mfupi ilitoka kumshusha Vero. Baada ya vijana wale kuingia ndani ya Gari, Teddy akazuga kama anavuka barabara, mbele kidogo akaifika gari aliyokuja nayo. Bila hata dereva kuambiwa wapi pa kwenda, gari iliwashwa na kuanza kuifuatilia gari ile. Hilo kwa Teddy lilikuwa sio jambo la kawaida, jambo ambalo hakulitarajia, hakuwa amemuacha dereva kwenye hii gari, hakuwa amemuacha mtu mwingine ndani ya gari hii. Kwa nini hakuingia upande wa Dereva akaingia upande wa Abiria? Amekosea na kupanda gari isiyo ya kwake ama ilikuwaje Hapa? Wakati akijiuliza maswali hayo akakisikia chuma kikigota kwenye kichwa chake. Kisha sauti tulivu ya kike ikitamalaki katika ngoma za masikio yake. "Tulia Teddy,. Uliona umjanja sana kufuatilia mambo yasiokuhusu. Sasa naamini leo ni Mwisho wako. Nakuapia hutaliona Jua la Kesho." Kufikia hapo Teddy akagundua kuwa alikuwa ameingia katika mikono ya kina Jimmy. Lakini kukumbuka kuwa Masimba alikuwa Eneo hilo kulimpa nguvu na kuamini hata kutekwa kwake Masimba alishuhudia na kuliona hilo. Teddy akatulia tuli kama alivyoambiwa.
 
[05-26, 18:25] Ibrahim Masimba: NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 069

Teddy akatulia kama alivyoambiwa. Akaiacha gari iendelee kutembea huku akiamini uwepo wa macho ya masimba kung'amua kilichotokea hapo. Bado mdomo wa bastola haukuondoka kisogoni, bado mdomo wa bastola haukushushwa. Bado uliachwa pale pale, kikubwa zaidi ni ukimya ndani ya gari. Hakuna aliyeinua mdomo kuongea chochote. Kwa Teddy hilo lilikuwa tukio ambalo hakulitaraji, tukio ambalo hakujua kama lingetokea mahala hapo na kwa staili hiyo. Kwa mara ya kwanza aliusifu uwezo wa kiuchungizi wa watu hawa. Alijulikana mapema licha ya kujibadili. Alitambukiwa mapema tokea akiingia hapo na pia alichukuliwa kirahisi mfano wa kuku wa mdondo. Gari ikaendelea kutembea pasipokujua wapi anaelekea. Muda wote alijitahidi kuangalia nje, lakini kila alipokuwa akilitenda hilo mdomo wa bastola ulizigandamizwa kichwani. Wakati anaendelea kuliwaza hilo wakashtuliwa na kishindo kikubwa kilichotokea, kishindo ambacho kilisababisha gari yao kuyumba na kwenda kuyavaa magari mengine yaliokuwa yameegeshwa pembeni mwa barabara. Kitebdo hicho kikasababisha Dereva kutupwa nje kwa kupitia kwenye kioo.. huku mwanamke aliyekuwa amemuweka Teddy bastola akichupa na kuangukia kwa Nje.. hilo lilikuwa ni jambo ambalo Teddy aliliona mapema hasa kutokana na kuiona gari ambayo ilikuwa nyuma yao kwa tofauti ya magari matatu. Kwahiyo iliposikia kile kishindo alijua nini ambacho anatakiwa kufanya. Ni muda huo akiliwaza hilo akamuona mwanamke aliyekuwa nyuma yake akichupa na kuangukia nje.. Hata yeye akalifanya hilo. Muda mfupi alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakikimbizana huku na huko wakipiga kelele. Licha ya kukimbia huko lakini macho yake yalikuwa yakimtafuta mwanamke yule aliyetoka ndani ya gari na kukimbia. Aliendelea kukimbia akiangalia kila upande. Licha ya kuangalia huko hakumuona msichana yule akata kusimama ili arudi kule alipotoka. Lakini hilo alililipinga, hapakuwa na sababu ya kurudi pale. Lakini akaona kusimama pembeni kutizama mienendo ya watu katika tukio lile kilikuwa ni kitu muhimu. Alisimana pembeni mwa jengo moja la Ghorofa. Macho yake yalikuwa yakitizama mkimbizano wa watu. Mkimbizano ambao alihitaji sana kukiona kitu ndani yake. Macho yake hayakutulia kutizama huku na kule. Punde akaiona ile gari aina ya ranger rover iliomshusha veronica kule bandarini ikisogea taratibu. Macho yake yakaongeza umakini kuitizama. Gari ile ikapita eneo la tukio na kuongoza kama inakwenda posta mpya. Teddy akaona ulikuwa muda wa kufanya hivyo. Muda mfupi alikuwa ndani ya Tax akiifuatilia ile gari kwa nyuma. Muda wote alikuwa akimsisitizia dereva kutokuipoteza ile Ranger Rover machoni mwake. Dereva alikuwa akitii kila alichokuwa akielekezwa ama kuambiwa na teddy. Gari ikaendelea kuhama barabara kutoka hapa na kwenda kule. Walipofika kwenye mnara wa Askari posta mpya, gari ile ikachukua barabara iendayo kivukoni. Lakini mbele kidogo wakaiona ikisimama mbele ya New Africa Hotel. Dereva tax naye akaisimamisha pembeni mwa kituo cha tax palepale hotelini. Mlango wa Ranger Rover ukafunguliwa, watu wawili wakashuka na kuingia ndani. Hawa hawakuwa watu anaowafahamu, wote walikuwa wageni machoni mwake. Wakati akiwashangaa watu wale mara akaiona bajaji ikisimama mbele kidogo na sehemu iliposimama gari. Akashuka Veronica akionyesha ni mwenye wasiwasi. Baada ya Vero kushuka alisimama Nje kidogo na kuzungumza mawili na watu ambao walikuwa ndani ya ranger rover, kisha akaongoza na kuingia ndani. Teddy bado alikuwa Ndani akishuhudia kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Muda wote alikuwa akichunguza kila upande kama angefanikiwa kuona mtu yeyote anayewafuatilia. Lakini hakuona chochote. Akaingizs mkono mfukoni na kutoka na noti mbili za elfu tano tano na kumlipa dereva. Baada ya hapo akaufungua mlango wa tax na kushuka atembea kuelekea njia tofauti. Kufuka mbele kidogo akasimama sehemu ambayo huuzwa vitabu. Baada ya kupekua hiki na kile Teddy akatoa pesa na kuchukua kitabu kiitwacho MIKATABA YA KISHETANI kilichoandikwa na Hayati Ben Mtobwa. Baada ya kukinunua akakitia ndani ya baibui na kuridi tena kule hotelini. Muda wote macho yake yalitembea na sura ya kila mtu. Alihitaji kujua hakuna jicho lolote linalomtizama kwa uchu. Alihitaji kufahamu kama alikuwa akifuatiliwa ama la!. Hilo akaligundua katika namna ya kipekee. Mbele ya jengo fulani upande wa pili mwa barabara akakiona kitoto. Kitoto kidogo kikicheza kanakwamba mama yake alikuwepo karibu. Macho yake yakavutiwa na yule mtoto, sio kuvutiwa kwa upendo. La hasha!! Bali muonekano na jinsi mtoto yule alivyokuwa akizungusha macho kanakwamba kuna kitu ambacho anakiangalia.

Macho ya mtoto yule yalikuwa yakizunguka katika aina ambayo kama ungekuwa mtu wa kawaida usingeweza kugundua wala kung'amua chochote. Kila wakati macho yake yalitizama huku na hata kuangalia upande wapili wa barabara. Hilo kwa teddy halikuwa jambo la kawaida. Alihisi mtoto huyu hakuwa mtu wa kawaida. "Aliyemuua Vicky ni mwanaume aliyejibadili na kuwa na muonekano wa kike. Pia hupenda kutembea na kitoto cha kiume." Hatimaye Teddy Alikuwa amekumbuka maneno ambayo aliambiwa na masimba usiku uliopita. Moja kwa moja akatambua kuwa mtoto mwenyewe alikuwa huyu. Je alikuwa na nani? Lilikuwa swali ambalo lilipita kichwani kwake. Alihisi uwepo wa mtu mahala akimwangalia yule mtoto. Wakati analiwaza hilo akamuona mtu akitokea kule kule alipotokea yeye wakati anakuja na tax. Huyu alikuwa masimba akitembea kwa mwendo wa kawaida, hata pale walipokutanisha macho yao hapakuwa na chochote zaidi ya macho yao kusema "huyu ndio mtoto mwenyewe". Kisha kila mmoja akiendelea na Hamsini zake. Wakati masimba akitembea akielekea ndani ya new afrika hotel, Teddy alikuwa akiivuka barabara akielekea kule ambapo anacheza yule mtoto. Alitembea kama mtu mwingine mwenye haraka zake. Hatua ya kwanza mpaka ya tano ikapita pasipo kutokea kwa rabsha. Hatua ya Sita haikupita hivi hivi.
[05-26, 18:26] Ibrahim Masimba: MHatua ya sita haikupita hivi, haikupita kwa kuwa tayari kitu kikasikika na pia kuonekana. Mlio wa risasi, naam mli0 ambao ulitoa burudani ya kuogofya katika macho na hata masikio. Wakati Teddy akichupa huku na kule katika aina fulani hivi. Mtoto aliyekuwa akicheza mbele yake tayari alikuwa amepaaa na tayari alikuwa ameanguka chini damu zikivuja kifuani. Lilikuwa tukio lililofanyika ndani ya dakika moja. Mtoto alikuwa akicheza muda mfupi akionyesha kufurahi, mtoto huyu muda huu roho yake ilikuwa ikipaa ikirudi kwa muumba wake. Hata wakati Teddy akichupa na kutua sehemu nyingine hakufikiria kama mtoto yule angekuwa maiti katika muda huo. Ni hilo lililomfanya atupe macho yake katika ghorofa zote. Ni muda huo katika jengo la Hoteli ya New Afrika akakiona kioo kikirudishwa kuonyesha muuaji alikuwa hapo. Lakini hakuinuka katika muda huo. Bado aliuona ni kama mtego. Hakuna muuaji mwenye kuweza kufanya kile ambacho kimefanywa muda mfupi. Mauaji kutokea kisha dirisha kufungwa katika muda huo huo.. akapuuza na kutulia pasipo kufanya chochote. Akaendelea kutulia akitafuta namna ya kuondoka Eneo la tukio pasipo kuonekana. Alitaka kuondoka kwa kuwa alijua ameonekana na pia alihisi mtoto yule kauawa kutokana na kule kuonekana kwake akimfuata. Muda mfupi baadae alikuwa akiondoka hapo akielekea upande wa pili wa kituo cha daladala posta. Kila kitu kilichokuwa kikiendelea kilionyesha kuuvuruga akili yake. Kujulikana kwa urahisi machoni kwa watu wanaowapeleleza ni ishara mbaya katika masuala yote ya kijasusi. Kuuawa kwa mtoto yule mbele ya macho yake ni kitu ambacho kiasi fulani kilimpa hofu na kumtetemesha. Ina maana muuaji angeamua angemuondoa yeye katika namna fulani aipendayo. Hapakuwa na ugumu wa kuuawa ikiwa mtu aliyembele yake ameuawa. Kufikia hapo akaona ndio muda muafaka wakumtafuta Masimba ili aongee.. ili afahamu kama yeye ndiye aliyetumbukiza Risasi kifuani kwa mtoto. Alitaka kufahamu yule mtoto alikuwa nani na amefikaje katika himaya ya watu hawa. Ikabidi asogee pembeni mwa jengo la Benjamin Mkapa. Akaichomoa simu yake tayari kumpigia Masimba. Lakini kabla hajafanya hivyo Ujumbe mfupi ukaingia katika simu yake. "Unaandamwa Kuwa makini ". Ulikuwa ujumbe kutoka kwa namba ngeni, namba ambayo hakumjua mmiliki. Hakutaka kujiuliza zaidi ya kuondoka hapo akiingia katika mkusanyiko wa watu na kupenya kwenye Magari. Alipofika mbele kidogo akatulia pembeni mwa Jengo la Posta ili kuangalia kama alichoambiwa ni kweli. Haikupita hata dakika akawaona watu wawili ambao ni wale walioshuka kwenye Ranger Rover pale New Afrika Hoteli. Walikuwa wakihaha kutafuta huku na huko. TEDDY akatamani kucheka Jinsi watu wale walivyokuwa wakihangaika na kuhaha huku na Huko. Aliendelea kuwaaangalia watu wale kwa muda mpaka pale walipoondoka hata yeye akaamua kuondoka.

*****

Giza totoro liliupamba mtaa huu na kusababisha kutokuonekana kwa mtu yoyote isipokuwa sauti pekee za mbwa ndizo zilizosikika. Masimba alikuwa amesimama sehemu katikati ya giza macho yake yakiwa barabarani kuiangalia gari ya Suresh. Yalikuwa makazi mapya ya Suresh tokea kutokea kwa tukio la kuuawa kwa Waziri mkuu. Hata kule Mbagala hakuwa akiishi. Ilimchukua Masimba siku tano katika uchunguzi wake kugundua sehemu ya Makazi ya Suresh. Usiku huu aliamua uwe usiku wa kumuondoa Suresh katika Ulimwengu huu. Alisubiri kwa muda wa dakika tano, ndipo alipovuta hatua kusogea katika Jengo analoishi Suresh. Alitaka Suresh amkute katika himaya yake, amkute akiwa ndani akimsubiri kama sio kumngojea. Alitembea katika kiza kile akitembea sambamba na vivuli vya miti, alipokaribia karibu na uzio uliozungushiwa nyumba ile, akaisikia minong'ono huku Harufu ya Bangi ikipita katika matundu ya pua yake. Vijana walikuwa wakiuvuta mmea. Hilo likampa imani kuwa walinzi hawa hawawezi kuwa katika kiwango cha kupambana naye. Akavuta tena hatua kwa umakini. Bastola ilikuwa kiunoni lakini hakupenda kuitumia. Akaendea kunyata mpaka umbali wa hatua kumi kutoka pale walipo. Akasimama akafikiria kipi cha kufanya ili kuingia ndani ya jengo pasipo kuleta Rabsha. Hapo ndipo alipoamua kuuparamia mti kwa umakini mkubwa na alipofikia usawa wa uzio ule alijitupa na kutua ndani kwa wepesi kama Bua.
 
Unapoambiwa umchangie mwandishi kufika pale anapopataka siamini kama inashindikana. Wengi tunasifia bila kujua watu wanatumia muda na pesa kuandaa. Bora uwatumie wachache wanao kuunga mkono kuliko sifa hizi. Katika watu 78000 wanaotoa mchango hawazidi sita hii ni aibu.
 
[05-28, 13:44] Ibrahim Masimba: NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 070

Akatua chini mfano wa ubua. Akatoka hapo akitembea na tumbo mpaka nyuma ya kibanda ambacho kimejengwa kwa ndani. Akatulia hapo kwa muda akitizama kama atamuona mtu yoyote yule. Mtu ambaye atatokea ama yule ambaye atahisi uwepo wake. Hapakuwa na mtu na hapakuwa na dalili yoyote ya uwepo wa mtu. Akasogea tena na tena akiitafuta njia ya kuingilia kwa ndani. Wakati anakaribia kuufikia mlango, akausikia mngurumo wa gari ukitokea kwa nje, kisha akalisikia lango likifunguliwa kisha ule mngurumo wa gari ukaendelea kusikika. Sekunde mbili baadae akahisi gari ikisimama. Hapo akatambua kuwa Suresh ndiye aliyekuwa ameingia hapo. Akaufuata mlango na kukinyonga kitasa. Mlango ukafunguka, akaingia ndani kwa mwendo wa Taratibu, mwendo ambao haukusikika hata kwa mtu ambaye yuko mbele kwa umbali wa hatua mbili. Wakati akiifikia sehemu fulani ndani ya jumba hilo akaisikia sauti yenye lafudhi ya kihindi kutokea nje. Hapo akajua kuwa huyo lazima atakuwa ni suresh. Akaendelea kusubiri, ndani ya sekunde akauhisi mlango ukifunguliwa kisha kusikia hatua za mtu zikitembea. Kwa kuwa kulikuwa na giza Masimba Hakujua mtu huyu alikuwa nani. Akaendelea kutulia akimngojea apite. Manukato mazuri puani na hatua za taratibu zilitosha kumfahamisha masimba na kumueleza kuwa mtu huyu alikuwa ni mwanamke. Mtu huyu alikuwa ni mwanadada. Wakati akiliona hilo mwanamke yule alikuwa amefika usawa wa pale mahali aliposimama. Masimba akamuacha apite kwanza kisha akaanza kumfuatilia nyuma nyuma. Bado hatua zake zilikuwa zile Zile ambazo hazikusikika. Lakini kwa nini jumba lote hili limejengwa huku na lipo giZa? Ni swali alilojiuliza wakati mwanamke yule akiufungua mlango wa chumba kilicho mbele yao. Kabla mlango haujajifunga masimba akawahi na kujitumbukiza. Hata hapa walipoingia bado kiza kiliwapokea, licha ya ukimya huo lakini pia sehemu hii iliuonekana kama stoo ama chumba kinachotumiwa kwa shughuli ambayo haikutakiwa kuonekana. Mabox sambamba na mifuko mikubwa ambayo ilionekana kujazwa vitu ilikuwa imehifadhiwa vizuri sana. Macho yake bado yalikuwa yakimtizama mtu yule. Kumtizama mwanamke yule. Kumtizama katika utimamu wa kiakili na kimwili. Mikono yake ilikuwa tayari kuichomoa bastola na kumuulia mbali, lakini hakutaka kufanya hivyo kwa kuwa alitaka kujua kule aliko suresh na wapi anapoelekea mwanamke huyu. Wakaipita ile sehemu na kutokea sehemu nyingine. Bado giza liliendelea kutawala katika jengo hilo. Mbele kidogo akauona ukuta, ukuta ambao ulikuwa ukionyesha ulikuw mwisho wa ile safari yao. Mwisho kwa kuwa haapa kuonyesha kama mbele kuna mlango uliokuwa ukiendelea. Lakini uelekeo wa mwanamke huyu ulionyesha uwepo wa kitu fulani. Akaona ulikuwa muda wa kumuwahi. Muda wa kumzuia kusogea ama kusonga mbele. Ilikuwa sekunde tu iliyotosha kuufanya mdomo wa bastola kumtekenya mwanamke yule ubavuni. "Tulia dada na usijaribu kufanya chochote.. " aliongea masimba huku mdomo wa bastola akizidi kuugandamiza.

"Wewe nani kwani? Na utanataka nini? Umeingiaje humu ndani?." Aliuliza mwanamke maswali mfululizo akionyesha kutetemeka. "Sio shughuli yako kujua nimeingiaje, ilaunapaswa kujua kile ninachokitaka. Sasa ninachokitaka ni roho ya Suresh. Na nataka unisaidie kumpata. Ukikaidi hata wewe roho yako nitaiweka katika orodha ya roho zile ambazo zimepangwa kupelekwa kuzimu. Naomba uongoze ulipokuwa unakwenda bila kufungua mdomo wako, la sivyo hutaliona Jua la kesho." Alinguruma masimba huku akiendelea kuugandamiza mdomo wa bastola mgongoni kwa binti. "Kaka mbona unanionea? Mbona suresh simfahamu na sijui unachoongea.!!.." aliongea binti akionyesha kutokujua kitu. "Binti usinilazimishe nikuue. Usinilazimishe niufumbe mdomo wako kwa risasi. Unafanya ninachotaka hufanyi? Alisema Masimba huku akimuangalia msichana. "Fanya kwa kuwa unaongea kitu nisicho... uwiiii nakufa... " hakuimaliza kauli yake, risasi kutoka kwenye bastola ya masimba yenye kiwambo cha kuzuia mlio ikapenya kwenye paja lake la mguu wa kushoto. Binti akalalama kwa maumivu. Hakujua kama Masimba alikiwa hatanii. "Naona sasa umekipata kile ambacho ulikuwa ukikihitaji. Naomba ufanye kama nilivyokwambia, nataka unionyesha alipo Suresh kabla sijakumaliza." Alisema Masimba huku sasa akimuonyesha Ishara ya kumtaka abonyeze kitufe kimoja kati ya vitatu vilivyopo ukutani. Msichana huyu akigugumia kwa maumivu akabonyeza kitufe, punde ukuta ukajifungua na kuacha uwazi kama mlango. Masimba akamtaka aongoze kuingia ndani. Binti hakuwa mbishi tena. Akaongoza ndani huku akigugumia kwa maumivu. Muda wote bastola ilikuwa mkononi tena mgongoni kwa mwanamke huyu. Walipopita kwenye ule uwazi binti akabonyeza vitufe kwa ndani sehemu ikajifunga tena wote wakajikuta ndani ya chumba kizuri na kilichopambwa sana. Kilionekana kuwa ni chumba cha kulala.

"Msubiri suresh atakuja hapa muda mfupi.." aliongea yule msichana huku akimuangalia Masimba Usoni. Macho yake yakurembua yalikuwa usoni kwa masimba. Ingawa macho yalikuwa usoni kwa Masimba, lakini mkono wake ulikuwa ukishuka taratibu sehemu ambapo palihifadhiwa bastola. Lakini hakujua kuwa macho ya masimba yalishamuona zamani, yalishamuona wakati mkono ukielekea sehemu hiyo. Mkono wa mwanamke yule haukufika hapo, haukufika sehemu husika. Risasi mbili zilitosha kuumaliza uhai wa binti huyu. Akajilaza taratibu kitandani akiwa maiti. Baada ya kugundua ameshakufa akamuweka vizuri na kumfunika na shuka, kisha yeye akatulia pembeni ili kumsubiri suresh akiwa katika giza lile lile. Aliona ulikuwa ni mpango bora na kurahisisha kazi kuanza na watu hawa ambao walikuwa kama matawi katika biashara hii.
[05-28, 13:44] Ibrahim Masimba: Ulikuwa ni mpango mzuri kuanza na watu hawa. Ulikuwa mpango mzuri wa kulimaliza hili suala katika aina kama hii. Jimmy na Suresh ndio chanzo cha kuharibika kwa watoto wengi. Vijana wengi walitopea katika utumiaji wa madawa ya kulevya kutokana na hawa watu wawili wakishirikiana na viongozi wa serikali. Ni aibu kuwaacha wakiendelea kuishi wakati huku mtaani vijana wengi walikuwa wameharibika na kuharibikiwa. Alioona hukumu sahihi ya Watu hawa ni Risasi, risasi ya kichwa ndio hukumu sahihi kwa watu hawa. Leo hii alikuwa chumbani kwa suresh akimsubiri huku pembeni yake kukiwa na maiti ya mwanamke ambaye alionyesha kuwa ni kimada wa Suresh. Alikuwa ametulia vilevile na giza bastola yake ya Kirusi Revolver colt 48 ilikuwa mkononi ikisubiri kuitoa roho ya suresh na kuisafirisha. Alitaka kuipeleka kuzimu, alitaka kuipeleka ikakutane na watu wote waliouawa na waliokufa kutokana na Matumizi ya Madawa ya Kulevya. Akaivuta subira katika aina ya kutokukata tamaa. Punde ukuta ule ukajifungua kisha akaonekana mwanaume wa kihindi akiingia taratibu. Baada ya kuingia mtu huyu akabonyeza vitufe mlangoni na ukuta ule kujifunga tena. Baada ya kufanya hivyo akatembea kwa madaha mpaka iliposwichi ya kuwashia Taa katika Chumba kile. Akaupeleka mkono na kuwasha.. nusura azimie kwa mshtuko baada ya kumuona Masimba akiwa ametulia pembeni huku Bastola yake ikiwa anamtizama yeye. "Karibu sana Mr Suresh.. Pia nisamehe kwa kukuingilia kwa Njia hii. Sikuwa na budi isipokuwa kufanya hivi." Aliongea Masimba akitizamana na Suresh katika aina fulani iliyompendeza machoni kwake. Masimba akainuka na kusimama Bastola Ikiwa mkononi bado. "Suresh leo nimeamua kuja mwenyewe kukuuliza machache ambayo nadhani utanijibu pasipo kuleta purukushani." Aliongea Masimba sasa akisogea karibu kabisa na Suresh. Suresh bado hakuinua mdomo wala macho kutizama. Alikuwa muoga kupindukia, alikuwa akitetemeka na hata midomo kukutana. "Suresh sasa naomba kaa pale ujibu maswali yangu. Naomba ujibu nitakavyo usije ukaniacha nikakupoteza kama huyo malaya wako." Bado aliongea Masimba huku akimuonyesha Suresh sehemu sahihi ya kukaa. Suresh bila kubisha akaongoza mfano wa kondoo. Akajibweteka chini akionyesha kuwaza kitu. Kitu ambacho hakujua ni vipi angeweza kukipata. Mwili wa mwanamke uliolala ukiwa hauna uhai ulimtisha na kumtia Hofu. Sasa alikuwa akikiangalia kifo mbele ya macho yake. Kifo ambacho alipenda kukitenda kwa watu wengine. Leo Ilikuwa zamu yake, leo ilikuwa zamu ya kifo chake. Akainua macho kumtizama masimba na hata kuuangalia unbali sahihi. Umbali kutoka alipo masimba na hata kutaka kujaribu kumvamia. Bado macho ya Masimba yalimuangalia kwa umakini na upole. Bado macho ya Masimba yalikuwa yametulia usoni kwake. Hakupepesa na hata kuangalia sehemu Tofauti. Alimtizama akikisoma kilicho katika akili yake. "Mbona ananitizama hivi? Mbona haonyeshi kuogopa? Yalikuwa maswali yaliogonga kichwani kwa Suresh. Akaamua kutulia na kuitafuta mbinu nyingine. "Suresh nahitaji kujua ukimuondoa Hayati waziri mkuu, ni nani mwingine yupo nyuma ya biashara hii mnayoifanya? Akauliza masimba kwa sauti tulivu. Suresh akakaa kimya kana kwamba hakuwa amelisikia swali hilo. "Suresh naongea na wewe, nani yupo nyuma ya hii biashara? Akauliza tena Masimba. Lakini bado Suresh hakutaka kujibu. Bado suresh alikuwa kimya. "Suresh usitake nitumie nguvu katika hili utajuta.." alilisisitiza Masimba. "Sijui unachozungumzia Ndio maana sina majibu ya maswali yako. Pia huwezi kuvamia nyumba za watu na kuua watu hovyo. Hata kama wewe ni mpelelezi hatuendi hivyo." Akajibu Suresh kwa sauti yenye kejeli ndani yake. "Suresh naomba unijibu maswali yangu. Narudia tena sitaki kutumia nguvu.. tambua ukinilazimisha na nikatumia utaumia." Narudia mara ya mwisho, ni nani yupo nyuma ya Biashara Yenu ukimtoa Waziri mkuu.? Akarudia tena.

"Sijui unachozungumzia na sielewi unachosema. Kama unaona una hofu na mimi nipeleke kwenye vyombo vya dora." Akajibu Suresh kwa kejeli tena.

"Sawa nimekuelewa. Lakini nikwambie kuwa sitakupeleka kwenye chombo chochote cha dora, bali nitakusafirisha kukupeleka Kuzimu. Sasa pokea hiyo kwanza." Aliongea Masimba huku bastola ikikohoa na risasi kwenda kupenya kwenye mkono wa kushoto... "haapana haapaana utanionea bure mimi sijui chochote." Aliongea Suresh huku akihamanika. Muda ule ule akakurupuka na kutaka kwenda kumvaa Masimba. Hakuujua Wepesi wa Masimba. Hakuujua wepesi wa mtu huyu. Kwani muda ule ule akajikuta akipokelewa na mateke matatu mfululizo. Mateke yaliyomrudisha chini na kumuacha akitweta. "Inuka upambane, wewe si mwanaume? Inuka tena nikumalizie." Aliongea masimba huku akimuangalia Suresh aliyekuwa akitweta pale chini. "Sasa naomba unijibu kabla sijakipasua kichwa chako kwa risasi. Huwa nawachukia sana watu wa aina yako. Mmeniharibu mamilioni ya vijana kwa uroho wenu wa pesa. Sasa niambie nani yupo nyuma yenu." Alifoka masimba. "Unajisumbua na kupoteza muda wako. Niue tu maana hutapata chochote kutoka kwangu." Aliongea Suresh huku akionyesha hana masihara. Haikupita sekunde Suresh alionekana kuilaza Shingo Yake pembeni huku mapovu meupe ya kimtoka mdomoni. Kilikuwa kitu ambacho hakikutarajiwa kabisa. Suresh alikuwa amejiua kwa kumeza vidonge fulani ambavyo hutumiwa Sana na majasusi wengi duniani kuepusha kutoa siri hasa pale unapobanwa. Suresh aliamua kuifuata njia hiyo. Alikuwa amekufa bila kutoa siri ama kitu chochote ambacho kingeweza kumsaidia masimba.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom