Riwaya: Nitakupata tu

NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 066

Haikuwa sura ile ya mwanzo, hii ilikuwa sura nyingine kabisa. Macho yalikuwa yakimtizama mzee yule pasipo kupepesa kuangalia kando. "Bila shaka unamfahamu huyo mtu, na pia unafahamu kazi zake. Nahitaji kumjua na kujua ni lini alianza kufanyakazi hapa." Akaongeza Masimba. "Mr John nadhani hayo maswali sipaswi kuulizwa na wewe. Muajiri wangu ndiye mwenye mamlaka hiyo pale aonapo kitu hakiendi sawa. Pia hata wanausalama ndiyo wanaweza kufanya hivyo lakini sio mtu wa hazina." Alijibu mzee huku hofu ikiwa imetawala ndani yake. "Mimi ndiye nimekuja badala ya bodi ya mamlaka ya bandari, pia nimekuja kama special Agent.. so nahitaji kupata majibu kuhusu mtu huyo mm0ja mwenye majina matatu tofauti." Alinguruma Masimba huku uso wake ukizidi kuuondoa Uhalisia. "Kijana ya nini tusumbuane, kwanza unaniuliza wewe kama nani? Akabwata yule mzee huku akionyesha kughafilika. "Kama John Raphael kutoka hazina, lakini pia unaongea na Mto roho ambaye ukiendelea kuupoteza muda wangu kesho hutaiona." Aliongea Masimba sasa akilazimisha macho yake yatizamane na macho ya mkurugenzi. "Huyo mtu mimi simfahamu na hata hapa hatuna Jina kama hilo." Akajibu mzee Majibu ambayo kwa kumuangalia tu, alihisi kuwa amedanganywa. "Humjui huyu mtu? Unashindwa kumjua mtu uliyemuajiri mwenyewe? Nikisema unamjua na kumtambua utasema nadanganya? Nikisema nawe ni kibaraka wa Jimmy Na Suresh kama alivyo huyu mtu wako utakataa? Je upo tayari risasi yangu ipenye kichwani kwako kwa sababu ya kuuficha ukweli wa mtu asiyekuhusu? Sasa naomba unijibu kwa umakini, usijaribu kunificha. Nikibadilika nitakupoteza kwa dakika tu." Aliongea Masimba huku akimtizama kwa macho makali. Mshtuko na mfadhaiko vilikuwa dhahri machoni na hata usoni. Mikono ikamtetemeka huku jasho likichuruzika Taratibu licha ya kuwepo kwa mashine za kuleta baridi. Kitendo cha kutajiwa watu hawa wawili kilimvunja nguvu na kumfanya asiwe na la kuongea. Akabaki akimtizama Masimba huku akionekana kutetemeka zaidi. Ni wakati Masimba akilitizama hilo akamuona mzee yule akibadilisha macho na muda ule ule kitu mfano wa damu kikaonekana kifuani kwake. Masimba hakuwa mjinga kiasi hicho asijue kilichotokea. Risasi iliyopitia Dirishani ilikuwa imepenya kwenye kifua cha mkurugenzi. Alikuwa amezibwa mdomo, alikuwa ameondolewa uhai asije kuutapika ukweli wote. Ilikuwa ni njia moja wapo inayotumiwa sana na majasusi kuficha siri husika. Akainua macho kutizama pale ilipotokea Risasi.. akakutana na nafasi ndogo kwenye pazia. Nafasi ambayo alihisi ndio imetumika kumuua Mkurugenzi huyu. Licha ya nafasi hiyo, pia usawa na ukaribu wa alipokaa yeye ilikuwa ni rahisi sana kupigwa yeye Risasi kabla ya mkurugenzi. Kwa nini ameachwa yeye akauliwa mkurugenzi? Lilikuwa swali lililoamsha mashaka. Mtu aliyemuua mkurugenzi alikuwa ni mtu anayemfahamu ama mtu ambaye alipewa oda ya kumuua mkurugenzi na kumuacha yeye. Kilikuwa kitu kigumu kukiamini katika uuaji ule. "Teddy" ndio jina pekee lililopenya kichwani na kuuvuruga ubongo wake. Lakini hilo alilioinga baada ya kutambua Teddy hawezi kuwa pale kutokana na msiba wa Vicky. Ilikuwa ni ngumu Teddy kuiacha maiti ya Vicky kisha aje afanye hivi. Lakini ni nani? Swali hilo alijiuliza wakati ameshaufikia mlango na kutokea ofisi ya sekretari. Kuufungua mlango tu, macho yake yakatua juu ya mwili wa Mwanadada yule ukiwa umelalia juu meza damu ikivuja taratibu na kuilowanisha Sakafu. Naye alikuwa ameuawa katija aina na namna ile ile. Namna ya kufumbwa mdomo asiweze kubweka. Masimba akaiona Hatari, hatari yakuendelea kuwepo ndani ya ofisi zile. Mkurugenzi, kisha sekretari, ilikuwa picha mbaya kwake. Ilikuwa ni lazima aondoke hapo. Aondoke kwa kupitia uelekeo mwingine, alijua alikuwa akitizamwa mahala fulani. Licha ya kutizamwa huko, lakini bado alimhitaji kumuona mwanadada yule wa mapokezi. Mambo kutokea kwa kasi namna hii ni wazi kuwa taarifa ilikuwa imesambaa. Imesambaaa kupitia kwa mtu, mtu ambaye amemuona kwa mara ya kwanza. Nani ameniona kuisambaza Taarifa hii katika muda mfupi huu? Jibu lilikuwa moja tu, veronica Senka Alikuwa msambaza taarifa , ilikuwa ni lazima apatikane kwa njia yoyote ile. Akaondoka akipitia sehemu tofauti na alikoingilia. Wakati akitoka Nje ya jengo, akauona msululu wa magari ya polisi wakikosi maalum ukiingia pale. Kilikuwa kikosi cha kupambana na uharifu wa aina yoyote. Kuuona msafara huo na alipounganisha na matukio ya kuuawa watu wawili katika muda mfupi.. alipata Jibu kuwa ni yeye aliyekuwa akitafutwa, ni yeye aliyetumiwa kikosi kile, ni yeye anayetafutiwa sababu ili wanaomuamini Wasimuamini. Hilo likamfanya azidi kuwa makini katika uondokaji. Uondokaji machoni mwa watu ambao walikuwa hapo.

********
Kwanza alishikwa na kitu kama ganzi, pili akashindwa hata kuongea na kipi akifanye. Butwaa hili lilimfanya mtu huyu aingie pasipo yeye kufanya maamuzi. Uso wake ukatagayari pale macho yake yalipogongana na macho ya mtu huyu aliyeingia kwenye ofisi zao katika mchana huu. Tabasamu mdomoni na uchangamfu wa kuzuga ukauchukua uso wake. Hata kijana huyu alipomsogeleo, bado tabasamu tamu halikuondoka usoni kwake. Hata alipojitambulisha kuwa anaitwa John Raphael, hakuonyesha kushangaa kwa kuwa alishamjua mtu huyu. Hakukuwa na mtu ambaye hakumjua Masimba. Lakini alipohitaji kuonana na mkurugenzi Muajiri, kengele za tahadhali zikalia kichwani kwa binti huyu.. hata pale masimba wakati akielekea kwa mkurugenzi hakuwa na maamuzi yoyote. Hakujua angeamua nini kwa wakati ule. Mpaka anaanza kuzipanda ngazi, bado hakujua nini afanye. Alimuona Masimba kama mtu ambaye anasingiziwa, mtu ambaye hafanani na kile kisemwacho juu yake. Wakati akiyawaza Hayo simu yake ikapata uhai. Simu yake ilikuwa ikiita. Namba ya mpigaji ndio iliomfanya akurupeke. "Jimmy" ndio neno ambalo lilisomeka Juu ya kiio cha simu yake. "Boss wangu.!! Alipokea Veronica.

"Yeah mtoto mzuri uko wapi leo?"aliuliza Jimmy.. "nipo kazini ila tumetembelewa leo." Akajibu Veronica. "Mmetembelewa na nani? Rais au nani?. Akauliza Jimmy safari hii kwa sauti tulivu. "Masimba yupo hapa, ametutembelea na sasa anaelekea kuonana na mkurugenzi muajiri. Nadhani kunatatizo boss maana alivyoingia sio kawaida." Aliongea Veronica. Hata aliposubiri jibu kwa Jimmy hakulipata kwa muda ule. Alipoita tena akagundua simu ilikuwa imekatwa. Baada ya Jimmy kupewa taarifa ya masimba kufika bandarini na kuhitaji kuonana na mkurugenzi ili mshtua sana. Kwa jinsi alivyomjua Masimba, alijua hapakuwa na usalama. Akapiga simu hotelini kwa vijana wake, jibu alilopewa lilimfanya atetemeke. Mmoja wa vijana wake shupavu maarufu kwa Jina la Jike dume alikuwa ameuawa. Akahisi mambo kutokuwa sawa, haraka akapiga simu kwa Ben kisha kumpa maelekezo ya nini cha kufanya. Ndicho ambacho kilitumika kuwaondoa watu walea katika ofisi ile.

******

Alifika msibani kwa mara ya pili tena, aliwakuta watu wapo katika makaburi tayari kwa muhifadhi vicky. Alisogea taratibu akikwepesha macho yake kumuangalia Teddy aliyekuwa ameshikiliwa huku na huko akilia kwa uchungu. Sala ya kumuombea marehemu ikachukua nafasi yake. Baada ya sala mwili wa Vicky ukaanza kushushwa kaburini kuhitimisha safari yake ya mwisho hapa duniani. Ulikuwa wakati mgumu sana. Mama Vicky hakuwa akijua kilichokuwa kikiendelea. Wakati wote huo masimba alikuwa makini akiangalia macho na sura za waliohudhuria mazishi. Hakutaka kuamini kwamba usalama ulikuwepo. Muda wote hakutulua akigeuka huku na kule. Akigeuka katika ya kupendeza. Uvaaji na hata muonekano wake haukuwa kama ule aliotoka nao ofisi za bandari. Hapa alikuwa ni Masimba mwingine. Kila hatua na kila ishara ya waombolezaji ilichunguzwa na kutiliwa mashaka. Vijana walioongezwa kuudumisha ulinzi na kunusa chini kwa chini nao walikuwa makini sana. Hata kama mtu alikuwa akijikuna basi aliangaliwa mara tatu tatu. Aliangaliwa na hata kufuatiliwa. Alichunguzwa kwa ukaribu zaidi na hata kupewa kashkash ambazo hazikuonekana machoni kwa waombolezaji. Macho yao yalikuwa katika sura ya mwanamke fulani ambaye alikuwa ametokea hapo na katika muda huo. Macho ya wanausalama yakamkaribisha katika aina ya tunakushuku. Tunakutuhumu na tutakujua. Akaangalia kila hatua na kila macho yake yalipokuwa yakigeuka kwa kutembea huku na kule. Huyu alikuwa yule mwanamke aliyekuwa pale ofisi za bandari. Huyu alikuwa yule aliyeisambaza taarifa za kufika hapo kwa masimba, taarifa iliyosababisha kuuawa kwa mkurugenzi. Lakini sasa alikuwa hapa makaburini, amekuja kama na nini na amefuata kipi? Hilo ndilo lililojengeka kichwani kwa masimba, hilo ndilo lililojengeka kuwa kuna namna. Mpaka mtu huyu kufika hapa makaburini ni wazi kuwa alikuwa akintafuta yeye. Alikuwa akijua kabisa binti huyu alikuwa hapo kwa kazi maalum. Kazi ya kumpeleleza yeye. Hilo likamvutia kwa kuwa alikuwa anamtaka na kumhitaji. Mazishi yakafika tamati na watu wakaanza kurudi majumbani kwao. Vijana wa usalama walikuwa wakitembea pembeni mwa familia ile kwa karibu sana kuonyesha kuwa walinusa chochote kitu. Masimba bado macho yake yalikuwa kwa Veronica. Bado macho yake yalitaka kujua kile ambacho msichana huyu amekifuata. Kile ambacho angekihisi machoni na hata kupitia mienendo yake. Kumkuta ofisi za bandari, mauaji ya mkurugenzi na sekretari wake, kisha kuja kwenye mazishi ya Vicky ni mambo ambayo yalimuacha katika maswali ambayo hayakupata majibu. Alihisi hata taarifa ya kufika kwake pale Bandari yeye ndiye aliyeisambaza na kisha kutumwa watu wa kuua.

Watu waliendelea kurudi nyumbani kwa wafiwa bila kujua chochote. Bila kutambua kuwa palikuwa na mchezo wa aina yake. Macho kwa mwanamke yule hayakuganduka. Aliitizama miguu yake na kuutizama mwendo wake. Mwende ambao ulimuonyesha kuwa mwanamke yule hakuwa peke yake. Mwili wake ulikuwa ukitoa ishara fulani katika kujulisha watu kitu fulani. Wakati mwili wake ukitembea katika namna ya kutoa taarifa. Macho yake yalikuwa yakitembea kwa aina fulani ya kinyonga ili kuwapoteza waliokuwepo na wale ambao alijua wako mahali na wanamuangalia yeye. Hakujua hilo na pia hakulitambua hilo. Hakutambua kuwa kuna macho mawili ambayo hayajawahi kushindwa kugundua kitu. Macho ambayo hung'aza mpaka ndani. Kila uelekeo wa macho yake hata masimba aliangalia huko. Kila alipokuwa akiuchezesha mguu hata macho ya Masimba yalikuwa yakitizama. Hatua zisizopungua kumi mbele mkono Wa Veronica ukawa unashushwa taratibu kuelekea mahala fulani katika vazi lake.. Hata mkono wa Masimba nao ukafanya hivyo, na Hakuwa masimba pekee, bali Hata wanausalama Wengine mikono ilikuwa Mfukoni tayari kwa tukio la aina yoyote.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom