NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 065
Alikuwa mwanaume tena mwanaume mwenye mwili uliyojengeka kimazoezi. Hilo hakuwa amelitaraji. Mwanaume? Kumbe huyu hakuwa mwanamke. Hilo likampa mshangao, mshangao ambao ulizidi hasa pale mwanaume yule alipomaliza kuvua mavazi yake. Dakika moja iliyopita alikuwa akionekana kama mwanamke mrembo machoni kwa Masimba, hata pale mikadi beach alimuona kama malaika fulani. Macho yake yalikuwa yakimvutia kila mwanaume amtazamae. Licha ya hivyo kumbe hakuwa mwanamke kama alivyoonekana. Hilo likaongeza hamu ya kumjua huyu alikuwa nani, kwa nini alimuua Vicky? Hilo likamtoa pale alipokuwa amejificha kuelekea pale aliposimama mwanaume yule akijinasibu kama wa fanyavyo wasichana wengine. Bastola mkononi hatua za kunyata mfano wa paka. Bado mwanaume yule hakuwa amemuona, bado mwanaume yule hakuusikia mchakato wa viatu wala hatua. "Niliacha kukuua Mikadi Baada ya kumshuti yule mwansmke nia yangu ikiwa ni kukujua wewe ni nani. Umetoka wapi na umetumwa na nani? Kubwa Zaidi ni uzuri wako na muonekano wako ulinifanya nisite kuchukua maamuzi ili mradi nikukute sehemu niujue uzuri wako kiundani. Lakini kilichonishangaza ni kukuona hapa tena ukiwa umwanaume. Sasa nataka unijibu mwenyewe kwa kinywa chako. Ukileta ujuaji nitakusafirisha ukaungane na Vicky, Yule msichana uliyemuua pasipo na hatia. Sasa nijibu wewe ni nani? Umetoka wapi? Na unayafanya haya kwa kutumwa na nani? Aliongea masimba huku bastola yake ikiwa usawa wa kichwa cha mwanaume yule. Kitendo cha kuisikia sauti ile kutoka nyuma yake kilimshtua na kujikuta akiupoteza umakini katika hili. Kitendo cha kugunduliwa kwamba hakuwa mwanamke bali mwanaume hata hicho pia hakutegemea. Siku zote aliishi kama mwanamke na hata jamii ilitambua hivyo. Aliilinda siri ya muonekano wake kwa gharama kubwa sana. Alimuua kila mtu aliyemgundua na kuiigundua siri yake. Alisafiri katika nchi mbalimbali kufanya kazi za ndani kama mwanamke, kote huko aliua matajiri wake pasipo kugundulika. Lakini leo hii siri yake ilikuwa nje na pia alikuwa akitakiwa kueleza kile anachokifanya. Huyu ni nani? Ni swali lililopita kichwani kwake kwa kasi sana. Kumbe niligundulika wakati nikiua? Kumbe alikuwa na uwezo wa kunishuti na kunifuta hapa Duniani? Huyu ni nani? Yalikuwa mawazo yaliyopishana kichwani. Mawazo ambayo yalimchanganya na kuufanya ujasiri wake kuyeyuka. "Nasubiri majibu yako.." ni sauti kutoka kwa masimba iliyomshtua mwanaume huyu.
"Niambie kwanza wewe ni nani? Nami nitakujibu kila kitu unachohitaji kutoka kwangu." Akajibu yule mwanaume kwa sauti tulivu na kawaida sana. "Hupaswi kuuliza maswali, unachotakiwa ni wewe unijibu maswali yangu." Alisema masimba huku akimuangalia kwa umakini. "Sikiliza ni kwambie, huna sababu ya kukataa kunijibu.. nataka nikujue wewe ni nani kwanza na kwa nini unaniuliza maswali ya namna hiyo." Alizidi kuongea mtu yule akionyesha kutokujali. Akionyesha dharau za waziwazi. Hakujua huyu mtu alikuwa nani, hakujua anaongea na mtu ambaye mzaha kwake haukuwepo kabisa. Punde kidole kikafanya yake, risasi moja ikapenya kwenye paja la mtu huyu... Yowee la maumivu likamtoka. Alikuwa akianza kulalama hovyo. "Nitakuua kwa risasi moja moja ukiendelea kuniletea jeuri. Haya jibu maswali yangu." Aliongea Masimba Huku bastola bado ameielekeza kichwani kwa mtu huyu ambaye aliakuwa akilalama kwa maumivu. "Mimi sijui unachokisema.. wewe niue tu." Alijibu mtu yule akiendelea kuugulia maumivu.
"Kumbe unaniletea utani eeeh? Basi sina muda wa kupoteza." Aliongea masimba wakati huo huo akiachia Risasi tatu mfululizo ambazo zilimtupa mtu yule na kwenda kujibamiza ukutani. Alisogea na kumkuta tayari ni marehemu. Baada ya kujua tayari mtu huyu amekufa, akaanza kupekua sehemu tofauti ndani ya chumba kile. Upekuzi ambao ulimsaidia kupata Passports tatu zenye majina Tofauti. Bastola mbili pamoja na vitambulisho vitatu. Kati ya hizo bastola moja ilikuwa imetengenezwa urusi, huku nyingine ikitengenezwa Jamhuri ya Watu wa Czech. Zamani ikijulikana kama Czechslovakia. Pasipoti zilikuwa na majina ya watu watatu Tofauti. Moja ilikuwa na Jina la Veronica Senka ikionyesha ni Raia Wa Uganda. Nyingine ilikuwa na Jina la Janeth Omondi ambayo ilionekana kutolewa Kenya na passpoti ya tatu ilikuwa na Jina la Nusra Kassi akionekana kuwa ni Raia wa nchini kenya maeneo ya mombasa.
Hata vitamburisho vilikuwa na majina ambayo yalikuwa kwenye passipoti tena yakimuonyesha mtu huyu alikuwa ni mfanyakazi wa mamlaka ya bandari nchini kenya, uganda pamoja na Hapa Tanzania. Passpoti zake zilikuwa zimegongwa mihuri kutoka nchi kadhaa za kiafrika na hata ulaya. Baada ya kuridhika na vitu alivyopata akaamua kutoka hapo kwa kupitia Dirishani tayati kwa safari ya kuelekea Bandarini kuulizia jina la mtu huyu. Kichwani alitambua kuwa Jimmy alikuwa ameweka mizizi katika sehemu zote nyeti za nchi hii. Ilikuwa ni lazima kuing'oa mizizi ilikumuondoa katika Uso huu wa Dunia. Haikuwa kazi rahisi kuifanya lakini aliamini akianza kudili na mtu mmoja moja ni lazima atamuangusha Jimmy.
********
Aliingia bandarini na kulakiwa na msichana mmoja mweupe, mrefu na mwenye sura ya kuvutia. Macho yake makubwa na pua za kinyarwanda ni kitu pekee ambacho kilimfanya Masimba amuangalie mwanamke yule mara mbili mbili. Akavuta hatua mpaka pale kisha kwa sauti yake ya tatu akasabahi. "Habari yako Mrembo"?
"Salama tu kaka angu, karibu sana na sema shida yako nikusaidie. Aliongea msichana yule kwa sauti ambayo iliuburudisha moyo wa masimba.
"Naitwa John Raphael, natokea Hazina, nilikuwa nahitaji kumuona Mr Faudhi Facha Mkurugenzi muajiri wa Bandari. Alijibu Masimba huku akimuonyesha kitambulisho chake kinachoonyesha kweli ni mfanyakazi Wa hazina.
"Una miadi naye? Aliuliza binti yule.
"Sina miadi lakini ukimwambia kuna mtu anatoka hazina anataka kukuona atanielewa." Alijibu Masimba Huku macho yake yaliyozoea kugundua visivyogundulika ikitalii hapa mpaka kule.
"Nenda chumba cha Tano ghorofa ya tatu, hapo utakutana na sekretari wake atakusaidia." Alisema mwanamke huyu akimgandishia masimba macho usoni. "Nashukuru nikirudi nitakupitia nikakupe japo soda." Akaongea Masimba akimuacha mwanamke yule akielekea ghorofa ya tatu kwa mkurugenzi Muajiri. Alitembea kwa makini huku macho yake yakipita kwenye macho ya watu kugundua kama kuna macho yanamtizama kwa ghiliba. Lakini hapakuwa na hicho kitu. Kila mmoja alikuwa akiendelea na kazi kama kawaida. Alizipanda ngazi mpaka ghorofa ya tatu, akaongoza mpaka mlangoni mwa chumba husika. Akaugonga mlango kabla haujafunguliwa na binti mmoja mnene na mfupi mweusi. Kuingia na macho yao kutizamana na mwanamke huyu, akiona kitu machoni kwake. Macho ya Dada huyu yalikuwa yakizungumza hofu na wasiwasi. Kwa nini? Lilikuwa swali lililofuatiwa na Salamu.
"Karibu John.." alisema dada yule huku bado mshangao ukiwa usoni. "Ahsante bibie, bila shaka Taarifa yangu mnayo." Aliongea masimba akimuangalia zaidi mwanadada huyu. "Tumepigiwa simu kutoka mapokezi ndio maana umeona nimekuita Jina lako." Alijibu msichana yule.
"Ni utaratibu wa siku hizi au umeanza kwangu? Akauliza tena safari hii akihamisha macho usoni kwa mwanamke huyu na kuutizama mlango wa chumba cha mkurugenzi.
"Hapa sio kwako tu, hata wengine pia ni hivyo." Akajibu mwanamke yule. Lakini kwa masimba aliuona uongo wa Jibu hili. "Naweza kumuona mzeee? Akauliza Masimba.
"Yeah!, ingia anakusubiri." Alijibu msichana yule. Masimba hakuongea kitu zaidi ya kuongoza ndani kuelekea chumba cha mkurugenzi. Akaugonga mlango.. "pita kijana." Ilikuwa sauti kutoka ndani ya chumba. Masimba akausukuma mlango akaingia. Baada ya kuingia ndani akajikuta akitizama na Ofisi nadhifu iliyopangiliwa vizuri. Kaa hapo bwana masimba. Naona leo nina bahati ya kutembelewa na mtu kama wewe. Kufanya kazi hazina Sio kutu cha kawaida." Aliongee mzee yule akionyesha bashasha usoni. Kwa mtu kama masimba haikuwa bashasha, kwa mtu kama Masimba sauti ile haikuwa ikimaanishe kile ilichokusudia. Sauti ile ilikuwa na kitu ndani yake. Kitu kama dharau na hatakejeli. Hakujali hilo, akavuta kiti na kukaa. "Nashukuru sana mzee wangu, nami nimefarijika kukutana na mtu kama wewe. Naamini kuna mengi ambayo nitajifunza kwako." Naye akaongea Huku akimuangalia mzee yule usoni. Hofu na wasiwasi ni vitu viwili ambavyo vilikuwa ndani ya macho ya mzee huyu. "Okay, nakusikiliza kijana Wangu.." aliongea mzee yule akikaaa sawa.
"Nashukuru, kuna kitu ambacho nimekutana nacho leo hii huko nitokako, nikaamini nikija hapa kwako naweza kupata majibu ya maswali yangu." Aliongea masimba kwa upole huku akimtizama mzee yule. "Endelea Kijana...."
"Mzee kabla sijaendelea popote, naomba kumjua mtu huyu. Aliongea masimba akutoa moja ya kitambulisho kati ya vile vitatu na kumpa mzee.
Mzee yule akakipokea na kuanza kukitizama.. Mshtuko usio wa kawaida ukaonekana machoni mwake. Akainua kichwa kumuangalia Masimba. Akakutana na sura tofauti.. hii haikuwa sura iliyoingia hapa muda mfupi uliopita. Hii ilikuwa sura ya kazi. Sura inayomaanisha kile kinachotakiwa kumaanishwa