Riwaya: Nitakupata tu

Riwaya: Nitakupata tu

******NITAKUFA NA WEWE*******

*******SEHEMU YA 080*******

Wakati Akielekea barabarani ili kuangalia usafiri wa kumpeleka bunju.. Akashtuliwa na msururu wa magari yakija na usawa ule aliyosimama Yeye... Kabla hajajua kipi akifanye akashangazwa na Mtindo wa kikomando kutoka kwa Askari wale. Walikuwa wakishuka katika aina fulani ambayo ungekuwa mtu wa kitengo ungefurahi Kuutazama ule mtindo. Kila askari Aliyekuwa Akishuka Ndani ya Gari alikuwa Akichupa katika aina fulani na hata walipokuwa wakitua chini walikuwa wakiruka tena katika aina fulani ambayo ilimuweka Jenifer katika Woga, woga ambao hakuutarajia kumjia katika Hali ile.. Makomandoo wale wenye kofia Nyekundu huku wakiwa na Alama ya Bawa kwenye mavazi Yao walimtisha kwa Mara ya kwanza na kumfanya atamani kujisalimisha, lakini kila alipokumbuka vifo vya Wazazi Wake alipuuza mpango wa kujisalimisha. Chuki ikaongezeka na Nguvu kumjia kwa nguvu upya... Mkono wake uliokuwa Ukivuja damu Haukumzuia Kufanya kitu kibaya kwa Makomandoo wale... Akaupeleka mkono wake katika kiuno chake alipomuhifadhi mwanawe, mwanawe ambaye alipenda kumtumia katika mikasa mizito kama Huu... Akaishika bastola Sawa sawia katika Mikono yake..... Kisha akaanza kukimbia kuelekea kwenye mashimo ya michanga huku masikio yake yakiwa yananusa kila Aina ya Michakato Hata kama ni ya wadudu...

Alijua maisha yake yapo mikononi mwake hivyo alikuwa makini katika kuruhusu mtu kumuona au kumgundua... Akaendelea kukimbia huku wakati mwingine akilazimika kutambaa kwa kwa tumbo yote ikiwa ni Kukwepa kuingia mikononi kwa Wanajeshi wale na Makachero Wengine. Akiwa amebakisha hatua kama tatu Kukifikia kibarabara ambacho kilikuwa kikitumiwa na Wakazi wa maeneo ya Ununio... Mara Akasikia Mngurumo Wa Pikipiki.. Mngurumo Ambao haukuchukua Muda ukanyamaza,.. Wakati Akiwa Ametulia kusikiliza kile kitakachotokea pale, mara Akasikia Mazungumzo Ya Kunong'ona... Akajiinua taratibu na kunyata mpaka karibu na iliposimama Ile Pikipiki ambapo aliendelea kuwasikiliza Watu wale waliokuwa wakiongea kwa kunong'ona. Sasa akawafikia karibu, ni ukaribu Huo Uliyomfanya akipeleke kidole chake kwenye kitufe cha kuruhusu risasi... Bastola Ikakohoa mara mbili... Risasi kutoka kwenye Bastola Zikaifanya kazi ambayo Zilitumwa. Miili ya Watu wawili akatambarajika Chini katika namna fulani Ilitia Raha kuitazama... Akasogea katika namna ya kipekee huku bastola Akiwa imetazama mbele katika kumziba mdomo Yoyote Ambaye Angeleta Fyoko fyoko......

Akaifikia Ile miili ya Watu Wale, akashangaa kukutana na Miili ya watu wawili ambao mmoja alikuwa mwanamke na mwingine mwanaume... Wote walikuwa wamelaliana wakiwa katikati ya dimbwi la damu... Akaumia sana katika Maisha Yake hakupenda kuua watu wasio na hatia lakini hutokea kufanya Hivyo kwa kutaka ama kuokoa maisha yake au kupoteza Ushahidi..

Hakutaka kuupoteza Muda, Alichokifanya ni Kuiendea ile pikipiki na kupanda kisha kuiondoa Eneo lile katika Mwendo wa Kasi Sana... Ni mwendo na Mngurumo wa Pikipiki ile Kuliko wagutusha makomandoo na Maofisa usalama waliokuwa wamezagaa Katika Eneo lote la Mbweni Jkt.... Mpaka Wanaifikia Sehemu ulipoanzia Mngurumo wa pikipiki... Jenifer Alikuwa Hayupo pale na Alikuwa Tayari Ameshafika mbali...

Wakabaki wakiitazama Miili ya Watu wale wawili Waliolala katika Dimbwi la Damu Huku Vichwa vyao vikiwa vimefumuliwa kwa risasi....

Wote wakaangaliana na Kutikisa Kichwa, Walikuwa wameachwa kwa Mara Nyingine na Jenifer.. Ilikuwa Dharau Kubwa kwa Makomandoo wale... Sasa Wakaamua Kulichukua wao lile Jukumu la Kumsaka Jenifer... Iwe mchana au Usiku, asubuhi au Jioni mpaka pale atakapopatikana.... Wanaume Wakakoki Silaha zao wakaingia Kazini Huku wakisema Ama Zake Ama Zetu.....

UKIITAKA HII UTAIPATA KWA BEI YA 5000 KUPITIA WHATSAP NA KWINGINEKO
 
******NITAKUFA NA WEWE*******

*******SEHEMU YA 080*******

Wakati Akielekea barabarani ili kuangalia usafiri wa kumpeleka bunju.. Akashtuliwa na msururu wa magari yakija na usawa ule aliyosimama Yeye... Kabla hajajua kipi akifanye akashangazwa na Mtindo wa kikomando kutoka kwa Askari wale. Walikuwa wakishuka katika aina fulani ambayo ungekuwa mtu wa kitengo ungefurahi Kuutazama ule mtindo. Kila askari Aliyekuwa Akishuka Ndani ya Gari alikuwa Akichupa katika aina fulani na hata walipokuwa wakitua chini walikuwa wakiruka tena katika aina fulani ambayo ilimuweka Jenifer katika Woga, woga ambao hakuutarajia kumjia katika Hali ile.. Makomandoo wale wenye kofia Nyekundu huku wakiwa na Alama ya Bawa kwenye mavazi Yao walimtisha kwa Mara ya kwanza na kumfanya atamani kujisalimisha, lakini kila alipokumbuka vifo vya Wazazi Wake alipuuza mpango wa kujisalimisha. Chuki ikaongezeka na Nguvu kumjia kwa nguvu upya... Mkono wake uliokuwa Ukivuja damu Haukumzuia Kufanya kitu kibaya kwa Makomandoo wale... Akaupeleka mkono wake katika kiuno chake alipomuhifadhi mwanawe, mwanawe ambaye alipenda kumtumia katika mikasa mizito kama Huu... Akaishika bastola Sawa sawia katika Mikono yake..... Kisha akaanza kukimbia kuelekea kwenye mashimo ya michanga huku masikio yake yakiwa yananusa kila Aina ya Michakato Hata kama ni ya wadudu...

Alijua maisha yake yapo mikononi mwake hivyo alikuwa makini katika kuruhusu mtu kumuona au kumgundua... Akaendelea kukimbia huku wakati mwingine akilazimika kutambaa kwa kwa tumbo yote ikiwa ni Kukwepa kuingia mikononi kwa Wanajeshi wale na Makachero Wengine. Akiwa amebakisha hatua kama tatu Kukifikia kibarabara ambacho kilikuwa kikitumiwa na Wakazi wa maeneo ya Ununio... Mara Akasikia Mngurumo Wa Pikipiki.. Mngurumo Ambao haukuchukua Muda ukanyamaza,.. Wakati Akiwa Ametulia kusikiliza kile kitakachotokea pale, mara Akasikia Mazungumzo Ya Kunong'ona... Akajiinua taratibu na kunyata mpaka karibu na iliposimama Ile Pikipiki ambapo aliendelea kuwasikiliza Watu wale waliokuwa wakiongea kwa kunong'ona. Sasa akawafikia karibu, ni ukaribu Huo Uliyomfanya akipeleke kidole chake kwenye kitufe cha kuruhusu risasi... Bastola Ikakohoa mara mbili... Risasi kutoka kwenye Bastola Zikaifanya kazi ambayo Zilitumwa. Miili ya Watu wawili akatambarajika Chini katika namna fulani Ilitia Raha kuitazama... Akasogea katika namna ya kipekee huku bastola Akiwa imetazama mbele katika kumziba mdomo Yoyote Ambaye Angeleta Fyoko fyoko......

Akaifikia Ile miili ya Watu Wale, akashangaa kukutana na Miili ya watu wawili ambao mmoja alikuwa mwanamke na mwingine mwanaume... Wote walikuwa wamelaliana wakiwa katikati ya dimbwi la damu... Akaumia sana katika Maisha Yake hakupenda kuua watu wasio na hatia lakini hutokea kufanya Hivyo kwa kutaka ama kuokoa maisha yake au kupoteza Ushahidi..

Hakutaka kuupoteza Muda, Alichokifanya ni Kuiendea ile pikipiki na kupanda kisha kuiondoa Eneo lile katika Mwendo wa Kasi Sana... Ni mwendo na Mngurumo wa Pikipiki ile Kuliko wagutusha makomandoo na Maofisa usalama waliokuwa wamezagaa Katika Eneo lote la Mbweni Jkt.... Mpaka Wanaifikia Sehemu ulipoanzia Mngurumo wa pikipiki... Jenifer Alikuwa Hayupo pale na Alikuwa Tayari Ameshafika mbali...

Wakabaki wakiitazama Miili ya Watu wale wawili Waliolala katika Dimbwi la Damu Huku Vichwa vyao vikiwa vimefumuliwa kwa risasi....

Wote wakaangaliana na Kutikisa Kichwa, Walikuwa wameachwa kwa Mara Nyingine na Jenifer.. Ilikuwa Dharau Kubwa kwa Makomandoo wale... Sasa Wakaamua Kulichukua wao lile Jukumu la Kumsaka Jenifer... Iwe mchana au Usiku, asubuhi au Jioni mpaka pale atakapopatikana.... Wanaume Wakakoki Silaha zao wakaingia Kazini Huku wakisema Ama Zake Ama Zetu.....

UKIITAKA HII UTAIPATA KWA BEI YA 5000 KUPITIA WHATSAP NA KWINGINEKO
Nifanyie 3000 mkuu niinunue kesho
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 062

Walikuwa wakitizamana na nyumba husika. Nyumba ya mwanamke anayesadikika kuwa ndio aliyemuua Vicky katika fukwe za mikadi. Ilikuwa nyumba nzuri ambayo ilizungushiwa ukuta wenye urefu wa kawaida. Mbele kulikuwa na geti moja kubwa sambamba na mtu mmoja ambaye alikaa nje akiwa na gongo mkononi kuonyesha kuwa alikuwa mlinzi wa mahala pale. Masimba akamuonyesha ishara yule mpelelezi mwenzie azunguke upande wa nyuma wa nyumba ile. Huku yeye akiamua kupitia getini kuongea na mlinzi yule. Aliondoka pale akitembea katika mwendo wa taratibu. Mwendo ambao ulimuonyesha kama ni mpita njia wa kawaida. Alipofika karibu kabisa ya mlinzi yule akainua mkono kama ishara ya kumtaka kusogea. Mlinzi yule akiwa na rungu mkononi akasogea mpaka pale alipokuwa amesimama Masimba. Lakini wakati akisubiria kusikia chochote kutoka kwa mtu huyu aliyemuita, akashtukia mdomo wa bastola ukiigusa shingo yake. Mlinzi yule akashtuka nusura ya kuanguka. "Naomba unifungulie geti niingie ndani, ukileta ubishi tu naufumua Ubongo wako." Aliongea masimba huku akiukandamiza Mdomo wa bastola shingoni kwa Mlinzi yule. Huku mlinzi yule akitetemeka alitembea taratibu kuelekea getini. Baada ya kufika hapo akainama na kulifungua geti kisha kutangulia ndani. Bado mdomo wa bastola ulikua nyuma yake ukimsindikiza. Macho ya masimba yakapokewa na kiza fulani kuonyesha kuwa mwenye nyumba hakuwa mtu wa kuwasha taa katika nyumba hiyo. Kitendo cha kuingia sambamba na mlinzi kikafuatiwa na pigo la kitako cha bastola kutua kisogoni. Mlinzi yule akaanguka chini taratibu na kupoteza fahamu. Akaondoka hapo akinyata mpaka mlango wa kuingilia ndani. Wakati akitaka kuugusa mlango wa kuingilia ndani, akausikia mngurumo wa gari ukitokea kwa nje kuonyesha kwamba kuna gari ilikuwa imesimama. Akajivuta haraka mpaka nyuma ya geti kisha taratibu akaanza kulifungua geti mpaka usawa unaotakiwa. Punde akaiona gari ikiingia ndani. Ni gari ambayo aliikumbuka kuiona mahali fulani. Akaitizama gari ikitembea mpaka nyuma ya jengo sehemu ambayo ilikuwa na sehemu maalum ya kuegesha magari. Akauona mlango ukifunguliwa kisha mwanadada yule akishuka. Alikuwa yule yule wa kwenye picha aliyopewa, na alikuwa yule yule aliyemuona pale benki siku ile. Baada ya mwanadada yule kushuka akaonekana akiangalia kitu fulani ambacho wao hawakuwa wamekiona wala kukifahamu. Baada ya hapo akaufuata mlango, lakini kabla hajaufikia mlango, mwanamke yule akazimisha mkono mfukoni na kuchomoa bastola kisha kuishikilia mkononi. Macho yake aliyaelekeza getini akitizama kila kitu, geti lilifungwa na mlinzi hakuonekana pale. Mwanadada yule akasogea huku bastola ikiwa mkononi.

Lengo lake ilikuwa kwenda mpaka nje bila kujua kwamba sehemu anayoelekea ndipo sehemu ambayo alisimama MASIMBA. Akaendelea kutembea zaidi na zaidi, akaendelea kutembea akiupita mti ambao ulikuwa umepandwa ndani ya nyumba ile. Kuupita mti akalifikia geti na kutaka kulifungua. Mchakato wa vishindo vya mtu nyuma vikamfanya ageuke mithiri ya mshale. Lakini alikuwa amechelewa, kwani wakati anageuka akakutana na pigo moja lililomlegeza. Pigo lililotua kwenye mishipa ya fahamu. Binti akaanguka chini mithili ya furushi. Masimba akainama ili kumuinua yule mwanamke tayari kwa kuondoka naye. Lakini hakuwahi kufanya hivyo, hakuwahi kwa kuwa muda ule ule akawaona watu wakiingia mithili ya Ninja. Walikuwa wakishuka na ukuta mfano wa Paka. Tayari Masimba alishahama pale nakuuzunguka mti kisha kukaa nyuma yake. Macho yake yalikuwa yakiwaangalia watu hawa walioingia mfano wa Ninja. Aliuangalia utembeaji wao na hata pishana yao. Alikuwa na uwezo wa kutumia risasi lakini hakutaka hilo kutokana na kutaka kuwajua watu hawa. Kila utembeaji wao na namna ya kujipanga kwao akatambua kuwa hawa hawakuwa watu wa kawaida, hawakuwa watu wa nchi hii. Hawa walikuwa wengine kutoka nchi nyingine. Watu hawa wakamjengea maswali, maswali ambayo yalimuweka katika kutokufahamu namna Jimmy na watu wake walivyoota mizizi katika nchi hii ya Tanzania. Bado hakutaka kuiruhusu bastola yake kufanyakazi. Alitaka kuwaangalia watu hawa lakini vile vile alihofia mwanamke yule aliyepoteza fahamu kurudiwa na fahamu.

Wakati hilo likiendelea mara akaiona taa ya sebuleni ikiwashwa, kitendo hicho kikaonyesha kutokutarajiwa na hata hawa watu waliofika hapo. Kwani kuwashwa kwa taa kukawafanya hata wao washangae huku kila mmoja akichupa na kuangukia pembeni katika namna ambayo ulionekana ujuaji wao katika medani hiyo. Ukimya wa ajabu ukatamalaki katikati yao. Kila mmoja alikuwa ametulia katika sehemu yake. Punde taa zikazimwa kwa mara nyingine. Kisha milio ya risasi ikafuatia
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 063

Taa zikazimwa na wakati ule ule risasi zikaanza kuvulumishwa kama njugu. Watu wale walikuwa wakichupa katika aina itiayo raha machoni. Raha ya kuwaangalia na hata kupambana nao. Masimba hakuliona hilo kama ni la kawaida. Bado alikuwa ametulia akimuangakia mwanamke yule aliyemuua Vicky. Hakutaka aondoke na kupotea katika macho yake. Hakutaka aondoke kabla hajatapika ukweli wote. Hilo likamfanya awaangalie watu hawa katika umakini wa hali ya Juu, Umakini wa hatua zao na hata mienendo. Bado risasi zilikuwa zikivurumishwa. Safari hii mpigaji huyo wa risasi alikuwa amebadili uelekeo. Sasa alikuwa akipiga kuelekea pale walipojibanza watu hawa mfano wa ninja. Ni hapo Masimba alipohitaji kufanya kitu, alijua kijana mwenzie ndiye ambaye anaifanya hiyo shughuli. Ukauona ulikuwa muda wake, muda wake kumsaidia. Akajiondoa pale mfano wa kivuli. Akitembea na giza kuelekea upande ule walipo watu wale. Bastola mkononi macho yakiangalia huku na huko. Alikuwa akifuata usawa wa kule zinapotoka Risasi. Kule ambako alihisi kuwepo kwa kijana yule. Wakati anakaribia kwenye mti mmoja nyuma kabisa ya nyumba ile, akamuona mru akiwa amejibanza pembeni kidogo mwa ukuta wa nyumba ile. Mkono wenye bastola ukanyooka kuelekea huko. Punde mlipuko mdogo ukasikika masikioni kwake mwenyewe, mlio ulioambatana na mtu kupiga yowe la uchungu kisha kutulia katika muda huo huo. Masimba akazidi kusonga, bado risasi zilisikika masikioni mwake. Sasa alikuwa amefika pale alipoangukia mtu yule. Risasi ilikuwa imefumua kichwa chake, imekifumua katika aina nayotia Raha. Wakati bado anauangalia mwili wa mtu huyu aliyekuwa amekufa. Akauona mlango wa nyumba kubwa unaotokea nyuma ukifunguliwa. Kufunguliwa kwa mlango wa nyuma ya nyumba kubwa kukafuatana na ukomo wa milio ya Risasi. Hilo likamfanya hata yeye atulie na kutizama nani atatoka ndani katika muda ule. Hazikupita hata sekunde tano akamuona mtu akitoka kisha kuuparamia ukuta na kuangukia upande wa pili. Wakati akilishangaa hilo akamuona mtu wa pili akitokea pia hata yeye alifanya kama alivyofanya mtu huyu aliyetangulia. Lakini kilichomsisimua kwa huyu mtu wa pili ni kule kumjua kwake, alikuwa ni yule msichana. Msichana ambaye muda mfupi uliopita alikuwa amepiteza fahamu.. Hakutaka kuliacha hilo lipite, hakutaka kuliacha liende pasipo kwenda nalo. Wakati akijitayarisha kupiga hatua kusonga pale, akamuona mtu watatu akitoka, mtu ambaye aliruka katika namna fulani ambayo ilikuwa tofauti na hawa. Huyu alikuwa ni yule mpelelezi mwenzake. Hata yeye alichupa lakini wakati huo huo akiupiga mluzi wa ishara ya hatari. Haukuwa mluzi usiofahamika, ulikuwa mlio uliokuwa ukitoa ishara ya kuwa na hatari sehemu husika. Sekunde hii alikuwa amesimama na hata sekunde ya tatu akikuwa akitua Nje lakini ndani ya Sekunde ya Tano Mlipuko mkubwa Ukatamalaki eneo lote. Nyumba ile ilikuwa akiteketea kwa moto. Akasimama mahali kuitizama nyumba ilivyokuwa ikiteketea. Aliitizama kwa Ghadhabu kubwa. Hatimaye alikuwa ameshindwa kumtia nguvuni muuaji Wa Vicky. Hili lilimuuliza sana. Akaondoka Eneo la tukio akiapa kuufanya usiku ule, kuwa usiku wa kufa na kupona. Ulikuwa ni wakati wa kupambana na Jimmy. Watu aliowaona wajiingia pale hawakua watu wa kawaida. Aliiona hatari na ugumu wa kazi hii endapo ataendelea kumuacha Jimmy akipumua. Ilikuwa ni Lazima amsafirishe ili kuizima hii mipango yake. Mipango ya kuchukua watu kutoka sehemu fulani kuwaleta sehemu fulani kwa minajili ya kujilinda asifikiwe. Hilo lilimfanya aipate hamu ya kwenda kuongea na Teddy. Hamu ya kwenda kumtoa kwenye ukataji tamaa na kumjaza nguvu za kupambana. Nguvu za kulipa kisasi kutokana na kifo cha Mdogo wake. Aliondoka Mwananyamala usiku ule akielekea Toangoma kigamboni nyumbani kwa marehemu vicky.

******

Alikuwa amejiinamia machozi yakishuka taratibu machoni. Hakua akiamini kile alichokuwa akikitizama. Mbele ya macho yake ulikuwepo mwili wa mdogo wake ukiwa umelala bila uhai. Aliutizama mwili wa Vicky akishindwa kupambana na maumivu ndani ya moyo wake. Maumivu makali ambayo yaliileta Hasira moyoni mwake juu ya Masimba. Alijikuta akimchukia masimba katika aina ambayo haikuweza kumithilika. Ni kweli alimwambia kuhusu mdogo wake kutokuwa mzoefu katika kile anachotaka kukifanya. Alimtahadharisha masimba kuhusu uhatari wa watu hawa katika kumpeleka vicky. Lakini ubishi wa masimba ukamfanya afanye kile ambacho alikiamini. Ni hilo lililosababisha kumpoteza Vicky. Kumpoteza mdogo wake kipenzi. Mdogo wake aliyekuwa akimpenda sana. Aliinua uso wake kuuangalia tena mwili wa vicky. Machozi yaliendelea kushuka zaidi na zaidi. Mdogo wake alikuwa ametuli sehemu ya mochwari akiwa kama amelala. Alikuwa kama amefumba macho. Vicky alikuwa hapumui tena. Hakujali uwingi wa maiti kule mochwari, alitaka kulala mle ndani na mdogo wake. Alitaka kukaa na mwili wa vicky. "Masimba nimekufanya nini mpaka unifanyie haya? Nimekufanya nini mpaka uniondolee kipenzi changu? Masimba Roho inaniuma na kuniuma. Sitajali wewe ni nani, sitajali ulikuwa nani kwangu nitakuua Masimba, kama sio wewe nitawaua wanao na hata ndugu zako. Damu ya mdogo wangu haiwezi kwenda bure. Masimba nitakuua tu." Aliongea Teddy huki akiendelea kuushika mwili wa Vicky. Wakati akilifanya hivyo akauona mlango wa Mochwari ukifunguliwa kisha akamuona Masimba akiingia taratibu akiwa amechafuka mavazi yake kuonyesha kwamba alitoka kwenye pata shika. Alitembea taratibu mpaka ulipo mwili wa Vicky. Aliutizama kwa Muda kisha kwa sauti ya huzuni akanena. "Vicky najua damu yako ipo mikononi mwangu, najua damu yako inaweza kunigharimu damu za watu wengine kwa ujinga wangu. Lakini nauapia moyo wangu na hata mwili wako. Sitalala wala kula mpaka nimpate muuaji. Sitapumzika popote pale mpaka siku nitakapo waua watu hawa. Pumzika Vicky wangu, siku ya mazishi yako hautazikwa peke yako. Nadhani unaweza kuzukwa sambamba na wanangu. Sambamba na damu yangu." Alipomaliza kusema hayo akamuangalia Teddy usoni. "Teddy najua una hasira na mimi. Najua hata wanangu umepanga kuwaua. Nakupa Ruhusa, nenda kawaue wote harafu tuone kama ukiwaua Vicky atarudi. Kwa heri ya kuonana nitarudi tu pale nitakapo waua Jimmy na vibaraka wake." Baada ya maneno hayo masimba akatoka mle ndani na kutokomea mtaani akimuacha teddy akiangua kilio. Aliondoka akiamua kwenda kumtafuta mwanamke yule. Hakutaka kupumzika mpaka pale atakapompata mwanamke yule aliyeitoa Roho ya Vicky. Safari yake katika usiku huu ilikuwa safari ya kufa na kupona. Ilikuwa safari ya usiku kucha ya kukesha katika mapambano. Usiku wa damu na hata kifo. Aliamua kuibeba kazi hiyo peke yake, aliamua kuifanya kwa kuwa yeye ndiye aliyeianza. Usiku huu aliamua kuanzia kigamboni katika mtaa mmoja uitwao tungi. Ulikuwa mtaa ambao aliishi Mbunge wa kigamboni Bibi Grace Bwahama sambamba na familia yake. Aliamua kuanzia hapo kwanza akiamini ni lazima angemkuta hapo. Alikodi pikipiki ambayo ilimpeleka mpaka mjimwema. Kutoka hapo akachukua tax ambayo ilimpeleka mpaka mtaa maarufu uitwao magengeni. Baada ya kufika hapo akachepuka mpaka kwenye bar maarufu iitwayo kwa chacha. Kufika hapo akaungia ndani ya bar kwa kupitia mlango wa nyuma. Wakati anaingia eneo hilo akamuona kijana mmoja akipita mbele yake. Akamuita na kumvuta pembeni.

"Mambo vipi dogo?. Akasabahi masimba.

"Safi kaka, nikusaidie nini?. Akajibu na kuuliza.

"Nyumba anayoishi mbunge wetu unaijua?. Akauliza tena.

"Yeah naijua sana mkuu, tena mwenyewe yupo hapa hapa ndani." Akajibu kijana yule akinyoosha kidole kumuonyesha Masimba kule ambapo alikaa mbunge yule. Masimba akainua macho kucheki, ni kweli alimuona bibi grace akiwa na vijana sambamba na kina dada wakionyesha kufurahia kitu.

"Chukua hii mwanangu utapata hata supu." Aliongea masimba akimkabidhi kijana yule noti mbili za elfu kumi kumi. Kijana yule huku akionyesha kutokuamini, akapokea pesa ile huku akimuangalia Masimba usoni.

"Ahsante sana kaka, Mungu akupe wepesi na upate zaidi ya hii. Umenifaa sana." Aliongea kijana yule kwa unyenyekevu. "Usijali, lakini nisingependa haya niliokuuliza useme popote." Alionya Masimba. "Usijali kaka sitaongea popote." Baaada ya Kujibu hilo wakaachana kila mmoja akienda na njia yake. Masimba akatafut meza nzuri ambayo ingemuwezesha kuiona meza aliokaa mbunge wa kigamboni. Alikuwa akihitaji kufanya shambulizi akiwa pale pale mezani alipokaaa. Baaada ya kuipata meza iliyotupu akaichoma Bastola yake ambayo ilikuawa ndani ya gazeti na kuiweka juu ya meza. Macho yake yakawa yanautafuta upenyo wa kuipata nafasi kumlipua mbunge yule. Alitaka kumuondoa akiwa pale pale katikati ya watu.
 
JENIPHER

SEHEMU YA 019

******
Ilikuwa lazima wafike, ilikuwa lazima waende katika misitu ya katanga kurudi na watafiti waliotekwa. Ilikuwa kazi ngumu kuifikia misitu hiyo bila kupitia Mjini. Hakukuwa na njia ya gari ama baiskeli ya kuwapeleka huko pale watakapoingia katika nchi ya rwanda. Lakini ilikuwa lazima wafike, ilikuwa lazima watembea ama kutumia usafiri kufika huko. Hapa kuwa salama na hapakuwa sehemu sahihi katika kutembea. Hilo lilikuwa changamoto kwa watu hawa. Ilikuwa lazima waende. Walikuwa wamekaa watatu katika chumba kimoja wakiitizama ramani ya kuwafikisha huko. Kila mmoja kichwa kilikuwa kikimuuma akitafuta jinsi ya kufanikisha azma yao. Kazi waliopewa na taifa ilikuwa kubwa sana, kazi ya kurudi na watafiti wao, kazi ya kurudi na wanasayansi. Kila mmoja aliijua hali ya kiusalama katika nchi ya kongo, kila mmoja alitambua hatari ambayo wangekutana nayo endapo wangeanza kwenda kinshasa. Walitaka kutumia msitu kwa msitu katika kufika huko. Jenipher, Masimba pamoja na Muddy bado walikuwa wamejifungia katika chumba hicho kila mmoja akiichora ramani katika kichwa chake. Ilikuwa safari ya kufa na kupona, safari ya kifo mkononi, safari ambayo ilibeba matumaini yote ya wanasayansi waliotekwa. Ilikuwa ni lazima wote waanze ndani ya misitu.. hilo likapita na kilichobakia ilikuwa ni safari. Wana usalama wengine wawili tayari walikuwa wameshatangulia katika nchi ya congo katika kufanya kile kinachojulikana kama kuisafisha njia. Hawa walipelekwa katika kunusa kile ambacho kingewasaidia wanausalama kuingia nchini humo pasipo kuwepo kwa matatizo. Walihakikisha wananusa katika kila sehemu kuhakikisha kwamba mission ile inafanikiwa katika wakati ambao umepangwa. Kila kitu kilikuwa tayari kwa safari, kila kitu kiliandaliwa ikiwa ni pamoja na watu wakuwapokea katika nchi ya rwanda. Tayari kulikuwa na watu waliowekwa tayari kwa kuwapeleka mpaka katika mpaka wa rwanda na nchi ya Congo. Hayo yote yalifanywa na Spy ambao walipandikizwa katika jeshi la rwanda kwa sababu ya kusaidia pale yatakapotokea mahitaji ama uhitaji wa taarifa Muhimu sana. Yote hiyo ilikuwa ni kulifanya taifa la Tanzania liwe katika usalama. Wakati sisi tukiwa tumelala huku tukila raha, kuna watu katika Tanzania hii wakihatarisha maisha yao. Wakati sisi tukipiga kelele na porojo katika vitu visivyo na msingi, kuna watu ambao maisha yao wameyaweka rehani kwa sababu ya watanzania. Wapo katika mipaka na vikosi vya waasi wakichukua hili na kuchukua lile yote ikiwa ni kwa sababu ya nchi hii.. Kuna watu ambao huitwa Spy katika kitengo fulani nyeti katika nchi hii. Watu hao ndio wanaotufanya Watanzania tuwe na amani. Watu hawa asilimia tisini ya maisha yao ni kifo. Wapo ambao wapo katika kikundi cha Al shababy, wapi ambao wapo katika mataifa yote makubwa wakichukua taarifa sababu ya usalama wetu. Hawa hawalali kwa sababu ya Tanzania. Na kazi yao kubwa ni kuhakikisha tunaishi kwa amani.

Hawa ndio watu ambao walitengeneza njia katika mission na hata katika ziara za viongozi wa nchi. Kila uchwao Tanzania tukiwa na amani tambua hawa wamehusika kwa asilimia mia. Hivyo suala la kufanikisha watu hawa kufika misitu ya katanga ni lazima waifanye wao kazi.

******
Waliingia katika nchi ya rwanda kila mtu kwa njia yake na kwa wakati wake. Wote walikuwa na taarifa moja ya kukutana kwao katika mpaka wa nchi hizo mbili. Kwahiyo nilazima kila mmoja apitie katika njia tofauti ili kutokuhisiwa kuwa ni wamoja katika safari hiyo. Wa kwanza kufika huko alikuwa Jenipher akiwa sambamba na vijana wengine wawili ambao hawa walihakikisha kuwa hakuna chochote kibaya kingeweza kumtokea Jenipher. Waliwasili hapo majira ya jioni wakiwa katika usafiri wa kawaida. Walipofika hapo wakamuacha Jenipher atangulie eneo hilo wao wakimfuata kwa nyuma. Hakuwa Jenipher pekee katika mwili wake, bali alikuwa Jenipher sambamba na watoto wake watatu katika maeneo tofauti ya mwili wake. Umbo lake lilimvutia kila mwanaume ambaye alimtizama, hiyo ilikuwa ni silaha muhimu sana kwake. Silaha ambayo kwa kitaalam huitwa pussypower kutokana na mara nyingi wanausalama wengi wa kike kutumia miili yao ilikupata habari sehemu fulani. Alitembea akiuacha mwili wake ujitingishe, wanaume wengi wakinyarwanda walikuwa wakimtizama katika namna tatu tofauti. Wapo ambao walimtizama kwa matamanio ya kumpata, kuna ambao walimtizama kwa woga wakidhani ni mwanausalama. Wengine walimtizama kwa kuwa alikuwa akivutia kutizama. Hilo likampa Jenipher nguvu ya kuendelea kutembea kwa mwendo ule. Ilikuwa ni lazima wapite hapo na kuingia katika nchi ya congo, ni lazima waitafute njia ambayo ingewapitisha hapo. Akaona ni muda wa kuutumia mwili wake. Muda wa kutafuta mbinu ya kufika katanga pasipo kutokea kwa rabsha zozote zile. Akaifikia meza ambayo haikuwa na mtu akajibweteka katika sehemu hiyo ambayo palikuwa na wamama wanaouza chakula. Muda mfupi akafuatwa na mwanadada mrefu, mzuri wakinyarwandwa. Huyu alikuwa msichana mzuri kama walivyo wasichana wengi wa rwanda.

"Habari yako?" Alisalimia mwanadada yule kwa kiswahili kibovu.

Kusalimiwa katika Lugha ya kiswahili kulimshtua sana Jenipher. Lakini ulikuwa mshtuko wake pekee yake, mshtuko ambao haukufika hata machoni kwa msichana huyo.

'"Nzuri tu, umejuaje kama mimi najua hii lugha? Akajibu Jenipher huku akimuangalia mwanamke yule. "Kuna mtu pale ndio ameniambia kuwa nikuulize una kula nini!" Alijibu mnyarwanda yule huku akinyoosha kidole kumuonyesha Jenipher. Jenipher akageuza macho yake, akajikuta akimuona mtu ambaye hakumuona wakati anaingia hapo. Alikuwa akiangaliana na Masimba. Alikuwa tofauti na masimba yule alietoka Tanzania. Huyu alikuwa amebadilika zaudi na zaidi. Tabasamu likachanua usoni kwake. Lakini wakati anacheka akamuona mwanamke mwingine wa kinyarwanda akisogea pale alipokaa masimba. Tofauti ya huyu na yule, yule alikuwa na sare za jeshi la rwanda lakini uzuri walikuwa wakifanana. Akili ya Jenipher ikafanyakazi kwa haraka sana, huyu alikuwa mmoja kati yao. Huyu alikuwa mmoja kati ya spying anayefanya kazi ndani ya Jeshi la Rwanda. Alikuwa pale kwa kazi maalumu ya kuhakishasha wanavuka na kuingia salama katika nchi ya Congo.

ITAENDELEA

HATA HII UKIITAKA UTAIPATA KUANZIA MWANZO WAKE.
 
  • Thanks
Reactions: ADK
JENIPHER

SEHEMU YA 019

******
Ilikuwa lazima wafike, ilikuwa lazima waende katika misitu ya katanga kurudi na watafiti waliotekwa. Ilikuwa kazi ngumu kuifikia misitu hiyo bila kupitia Mjini. Hakukuwa na njia ya gari ama baiskeli ya kuwapeleka huko pale watakapoingia katika nchi ya rwanda. Lakini ilikuwa lazima wafike, ilikuwa lazima watembea ama kutumia usafiri kufika huko. Hapa kuwa salama na hapakuwa sehemu sahihi katika kutembea. Hilo lilikuwa changamoto kwa watu hawa. Ilikuwa lazima waende. Walikuwa wamekaa watatu katika chumba kimoja wakiitizama ramani ya kuwafikisha huko. Kila mmoja kichwa kilikuwa kikimuuma akitafuta jinsi ya kufanikisha azma yao. Kazi waliopewa na taifa ilikuwa kubwa sana, kazi ya kurudi na watafiti wao, kazi ya kurudi na wanasayansi. Kila mmoja aliijua hali ya kiusalama katika nchi ya kongo, kila mmoja alitambua hatari ambayo wangekutana nayo endapo wangeanza kwenda kinshasa. Walitaka kutumia msitu kwa msitu katika kufika huko. Jenipher, Masimba pamoja na Muddy bado walikuwa wamejifungia katika chumba hicho kila mmoja akiichora ramani katika kichwa chake. Ilikuwa safari ya kufa na kupona, safari ya kifo mkononi, safari ambayo ilibeba matumaini yote ya wanasayansi waliotekwa. Ilikuwa ni lazima wote waanze ndani ya misitu.. hilo likapita na kilichobakia ilikuwa ni safari. Wana usalama wengine wawili tayari walikuwa wameshatangulia katika nchi ya congo katika kufanya kile kinachojulikana kama kuisafisha njia. Hawa walipelekwa katika kunusa kile ambacho kingewasaidia wanausalama kuingia nchini humo pasipo kuwepo kwa matatizo. Walihakikisha wananusa katika kila sehemu kuhakikisha kwamba mission ile inafanikiwa katika wakati ambao umepangwa. Kila kitu kilikuwa tayari kwa safari, kila kitu kiliandaliwa ikiwa ni pamoja na watu wakuwapokea katika nchi ya rwanda. Tayari kulikuwa na watu waliowekwa tayari kwa kuwapeleka mpaka katika mpaka wa rwanda na nchi ya Congo. Hayo yote yalifanywa na Spy ambao walipandikizwa katika jeshi la rwanda kwa sababu ya kusaidia pale yatakapotokea mahitaji ama uhitaji wa taarifa Muhimu sana. Yote hiyo ilikuwa ni kulifanya taifa la Tanzania liwe katika usalama. Wakati sisi tukiwa tumelala huku tukila raha, kuna watu katika Tanzania hii wakihatarisha maisha yao. Wakati sisi tukipiga kelele na porojo katika vitu visivyo na msingi, kuna watu ambao maisha yao wameyaweka rehani kwa sababu ya watanzania. Wapo katika mipaka na vikosi vya waasi wakichukua hili na kuchukua lile yote ikiwa ni kwa sababu ya nchi hii.. Kuna watu ambao huitwa Spy katika kitengo fulani nyeti katika nchi hii. Watu hao ndio wanaotufanya Watanzania tuwe na amani. Watu hawa asilimia tisini ya maisha yao ni kifo. Wapo ambao wapo katika kikundi cha Al shababy, wapi ambao wapo katika mataifa yote makubwa wakichukua taarifa sababu ya usalama wetu. Hawa hawalali kwa sababu ya Tanzania. Na kazi yao kubwa ni kuhakikisha tunaishi kwa amani.

Hawa ndio watu ambao walitengeneza njia katika mission na hata katika ziara za viongozi wa nchi. Kila uchwao Tanzania tukiwa na amani tambua hawa wamehusika kwa asilimia mia. Hivyo suala la kufanikisha watu hawa kufika misitu ya katanga ni lazima waifanye wao kazi.

******
Waliingia katika nchi ya rwanda kila mtu kwa njia yake na kwa wakati wake. Wote walikuwa na taarifa moja ya kukutana kwao katika mpaka wa nchi hizo mbili. Kwahiyo nilazima kila mmoja apitie katika njia tofauti ili kutokuhisiwa kuwa ni wamoja katika safari hiyo. Wa kwanza kufika huko alikuwa Jenipher akiwa sambamba na vijana wengine wawili ambao hawa walihakikisha kuwa hakuna chochote kibaya kingeweza kumtokea Jenipher. Waliwasili hapo majira ya jioni wakiwa katika usafiri wa kawaida. Walipofika hapo wakamuacha Jenipher atangulie eneo hilo wao wakimfuata kwa nyuma. Hakuwa Jenipher pekee katika mwili wake, bali alikuwa Jenipher sambamba na watoto wake watatu katika maeneo tofauti ya mwili wake. Umbo lake lilimvutia kila mwanaume ambaye alimtizama, hiyo ilikuwa ni silaha muhimu sana kwake. Silaha ambayo kwa kitaalam huitwa pussypower kutokana na mara nyingi wanausalama wengi wa kike kutumia miili yao ilikupata habari sehemu fulani. Alitembea akiuacha mwili wake ujitingishe, wanaume wengi wakinyarwanda walikuwa wakimtizama katika namna tatu tofauti. Wapo ambao walimtizama kwa matamanio ya kumpata, kuna ambao walimtizama kwa woga wakidhani ni mwanausalama. Wengine walimtizama kwa kuwa alikuwa akivutia kutizama. Hilo likampa Jenipher nguvu ya kuendelea kutembea kwa mwendo ule. Ilikuwa ni lazima wapite hapo na kuingia katika nchi ya congo, ni lazima waitafute njia ambayo ingewapitisha hapo. Akaona ni muda wa kuutumia mwili wake. Muda wa kutafuta mbinu ya kufika katanga pasipo kutokea kwa rabsha zozote zile. Akaifikia meza ambayo haikuwa na mtu akajibweteka katika sehemu hiyo ambayo palikuwa na wamama wanaouza chakula. Muda mfupi akafuatwa na mwanadada mrefu, mzuri wakinyarwandwa. Huyu alikuwa msichana mzuri kama walivyo wasichana wengi wa rwanda.

"Habari yako?" Alisalimia mwanadada yule kwa kiswahili kibovu.

Kusalimiwa katika Lugha ya kiswahili kulimshtua sana Jenipher. Lakini ulikuwa mshtuko wake pekee yake, mshtuko ambao haukufika hata machoni kwa msichana huyo.

'"Nzuri tu, umejuaje kama mimi najua hii lugha? Akajibu Jenipher huku akimuangalia mwanamke yule. "Kuna mtu pale ndio ameniambia kuwa nikuulize una kula nini!" Alijibu mnyarwanda yule huku akinyoosha kidole kumuonyesha Jenipher. Jenipher akageuza macho yake, akajikuta akimuona mtu ambaye hakumuona wakati anaingia hapo. Alikuwa akiangaliana na Masimba. Alikuwa tofauti na masimba yule alietoka Tanzania. Huyu alikuwa amebadilika zaudi na zaidi. Tabasamu likachanua usoni kwake. Lakini wakati anacheka akamuona mwanamke mwingine wa kinyarwanda akisogea pale alipokaa masimba. Tofauti ya huyu na yule, yule alikuwa na sare za jeshi la rwanda lakini uzuri walikuwa wakifanana. Akili ya Jenipher ikafanyakazi kwa haraka sana, huyu alikuwa mmoja kati yao. Huyu alikuwa mmoja kati ya spying anayefanya kazi ndani ya Jeshi la Rwanda. Alikuwa pale kwa kazi maalumu ya kuhakishasha wanavuka na kuingia salama katika nchi ya Congo.

ITAENDELEA

HATA HII UKIITAKA UTAIPATA KUANZIA MWANZO WAKE.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom