SITAKUSAHAU RUKIA
SEHEMU YA 022
Na Ibrahim Masimba
Nilitupa macho yangu kitandani na kupokewa na kitu cha kuvutia. Rukia alikuwa amelala kifudifudi kitandani huku akiwa hana hata kipande cha nguo mwilini. Alikuwa kama alivyotoka tumboni kwa mama yake. Ngozi yake ilikuwa ikiwaka na kuvutia kuitizama kwa muda wote. Ulikuwa ulalaji uliovuruga kichwa changu na moyo wangu, damu zilisimama na moyo kushindwa kudunda kwa usahihi. Nilikuwa nikimuangalia mwanamke mrembo akiwa amelala kihasara. Mwanamke mwenye mvuto mubashara. Macho yakatamani kutizama zaidi huku mikono ikitetemeka ikihitaji kwenda kuushika mlima ule. Mlima uliotukuka katika matumizi sahihi ya kutafunwa kama sio kuchemshwa. Miguu ikahitaji kupiga hatua kuelekea pale kitandani. Alifanana kabisa na Kim kardashian ule muinuko wa upande wa pili. Mate yakajaa mdomoni na uchu kuongezeka. Sikuweza kumkumbuka tena Dalillah Adam, sikuweza kumkumbuka kwa wakati ule. Licha ya kutokumkumbuka lakini hilo halikunifanya nipige hatua nielekee pale kitandani, bado nilikuwa nimesimama nikitafakari. Mara nikaliona tukio jingine ambalo lilinishtua na kunifanya nianze kutetemeka. Rukia alijigeuza na kuiachanisha miguu yake huku na huko. Hapo ndipo nilipohisi kuwa ulikuwa mtego, mtego wa kunivuta na kunikamata kabisa. Sikuwa na ujanja zaidi ya kuangalia ule uumbwaji uliotukuka. Uumbwaji ambao haukukosewa hata kidogo. Nikatamani kuuvamia ule uumbwaji lakini niliogopa kwa kuwa Rukia Bado alikuwa ana mshono, bado hakuhitaji kukutana na mtu kimwili. Licha ya kupita miezi tisa lakini bado nilikuwa nikiogopa hilo. Nikasogea taratibu pale kitandani, hofu moyoni tamaa machoni. Mlalo wa rukia haukuwa katika kiwango cha Masters ulikuwa mlalo ambao ulipitiliza. Nikakifikia kitanda kisha nikakaa pembeni yake. Hapo ndipo nilipochanganyikiwa kabisa, hapo ndipo nilipochanganyikiwa nikashindwa pakuanzia. Ni mwanaume gani lijali angeuacha urembo huu? Ni mwanaume gani aliekamilika atakaemuacha Rukia? Hilo lilikuwa gumu kwangu, hilo lilikuwa gumu kwa kuwa nilitambua Rukia Bado anaomshono. Nikaendelea kukaa pale kitandani nikimuangalia kwa matumaini ya kuanguka dhambini. Nam, ilikuwa ni lazima katika hilo. Nikajilaza kitandani nikitizama pembeni, sikutaka kumuangalia tena. Nilitamani kufanya lakini nilihofia kwanza. Sikujua ni muda gani nilipitiwa na usingizi, lakini nilijikuta nikimshtuka saa kumi za usiku tena kwa kuamshwa na Rukia.
Niliinuka huku nikimuuliza kulikoni, lakini bado hakunijibu, bado aliiniangalia usoni mwangu. Bado hakuinua mdomo kunijibu. Alionekana kutafuta maneno ya kusema lakini hakuonyesha kama ameyapata. Nikaendelea kumsubiri aongee, aongee kile ambacho alitaka kukisema.
"Ibu Hivi mimi ni dada yako? Hatimaye aliuliza. Hapo nikahisi uwepo wa tatizo.
"Hapana, wewe sio dada yangu." Nikamjibu.
"Kama unalijua hilo kwa nini unanitendea hivi? Hujui hata mimi nina hisia? Akanipa maswali tena magumu sana. Sauti yake haikuonyesha utani.
"Najua Rukia lakini huoni kama bado wewe ni mgonjwa? Huoni kuwa tunaweza kutafuta tatizo jingine? Nami nilimjibu lakini kwa namna ya kuuliza. Maswali yangu yalimfanya rukia aniangalie usoni kwa muda mrefu bila kuongea kitu. Licha ya Kuniangalia lakini pia mikunjo ya hasira ikatokea usoni.
"Hivi Ibu, wewe na Daktari nani anautaalam kuliko mwenzie? Akauliza.
"Ni daktari. Nikajibu.
"Kama ni Daktari, kwa nini wewe useme sijapona wakati Dk Hamza Kibirige amesema Nipo safi na nina uwezo wa kukutana na mwanaume? Lilikuwa swali ambalo sikupata majibu yake. Nikabaki kimya nikimuangalia tu Rukia. Nilijua nikipi ambacho alikuwa akihitaji.
"Sikiliza Ibrah, hata mimi nina hisia, mwili wangu unahitaji kumbatio. Nimekwambia wewe kwa kuwa tunaishi wote. Lakini kama unaona sikufai niache nikatafute mwanaume mwingine. Wapo wanaume wanapigana vikumbo kwa ajili yangu. Wapo wanaume wanaokosa usingizi kwa ajili yangu. Ninachofanya nikukuheshimu na pia kwa kuwa nimeamua kulipa fadhila kwa kukuonyesha penzi la kweli. Lakini kama hutaki acha nitafute mwanaume tena mwanaume ambaye nitakuja naye hapa ili umuone na nikutambulishe. Naona mimi na wewe tumeshakuwa kaka na dada kwahiyo acha nikuonyeshe shemeji yako." Alipoongea hilo akajilaza kitandani na kujifunika shuka gubigubi. Akaniacha nikianza kutafakari maneno yake, maneno ambayo yaliufanya moyo Wangu Ukose amani. Atamleta mwanaume hapa anitambulishe kwa kuwa mimi ni kaka yake, inawezekana kweli hii? Hapo nikauona wivu ukijaa moyoni. Nikabaki kumuangalia pale alipolala. Wakati mimi nikihangaika mwenzangu ndio kwanza alikuwa akijigeuza huku na huko akionyesha kufurahishwa na maamuzi yake.
******
Ilikuwa wiki ngumu sana kwangu, wiki ambayo haikuwa na kumbukumbu nzuri kwangu. Ilikuwa ni siku ya jumamosi nikiwa nimetulia nyumbani nikijisomea kitabu changu kiitwacho Kikosi cha Kisasi kilichotungwa na kuandikwa na mwandishi nguli wa vitabu vya kipelelezi Hayati ELVIS MUSIBA. Nikausikia mlango ukigongwa huku ukisindikizwa na sauti ya mtu. Kabla sijainuka hapo nikamuona Rukia akiinuka na kuuende mlango kisha kuufungua. Punde nikawaona wazee wawili wakiingia. Walikuwa wamevalia kanzu zao maridadi sana. Nilikiacha kitabu nilichokuwa nikikisoma nikawakaribisha ndani wazee wale. Ulikuwa ni ugeni ambao sikuutegemea. Ulikuwa ugeni ambao ulinipa mashaka sana. Mawazo yangu nikadhani labda ni wazazi wa Dalilah Adam. Lakini nilipoiona ile pilikapilika ya Rukia nikaanza kuhisi uwepo wa kitu. Lakini nikavumilia ili kuuona mwisho wake.
"Samahani Sana bwana Ibrahim, sisi ni washenga tumetumwa hapa kuleta posa kuhusu mdogo wako huyu. Tulipanga tujetokea jumatato lakini kutokana na majukumu mengine tukashindwa na ndio maana tumekuja leo.""alimaliza kuongea mzee mmoja.
Kwanza nilikosa maneno ya kuongea, nikabaki kushikwa na bumbuwazi. Wivu ukanishika kama sio kunishika. Jasho likaanza kunitoka huku mishipa ya hasira ikionekana. Nikaangalia wale washenga kwa muda nikitamani kuwaambia posa hakuna. Lakini watanielewaje...
NIKABAKI KIMYA NIKIUGULIA WIVU MOYONI
******
UKIITAKA YOTE UTATUMIWA KWA BEI NAFUA 3000 YOTE MPAKA MWISHO