Riwaya: Nitakupata tu

Riwaya: Nitakupata tu

NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 058

Mdomo wa bastola ulikuwa shingoni katika namna ya kushindwa hata kuigeuza shingo yake. Binti yule akahamanika na kujikuta akiupoteza umakini na hata uwezo. Punde mlango wa upande mwingine ukafunguliwa. Mwanamke mrefu mwembamba alikuwa akiingia kwa ule mwendo wake wa twiga. Alikuwa akitembea kanakwamba alikuwa akiigopa ardhi. Mkononi alikamatia Bastola yake. Alikuwa Teddy Harry akiingia ndani ya jengo lile.. akasogea taratibu kwa namna ambayo alikuwa tayari kwa chochote. Macho yake yakatua kwenye mwili wa Masimba, mwili ambao ulionekana kutapakaa Damu. Nguo zilizochanika na hata damu kuvilia. Teddy hakumjali msiçhana yule ambaye alikuwa akitizamana na mtutu wa Bunduki iliyoshikiliwa sawa sawia na Masimba. Teddy akasogea tena na tena. Alipofika pale waliposimama akakifanya kitu ambacho hata Masimba hakukitegemea. Kitu ambacho kiliuonyesha ukatili wa hali ya juu. Bastola yake ilifanya kazi ya kukifumua kichwa cha mwanamke yule. Risasi tano zilikuwa zimekigawanyisha kichwa na kuufanya ubongo uliochanganyika na damu kuruka juu na kusambaa chumba kizima. Hakulijali hilo, hakujali teddy akasogea na kujitupa kifuani kwa masimba. Alijilaza huku akilia kwa sauti ndogo. Hali aliyonayo Masimba ni hali ambayo hakuwahi kumuona. Moyo wake uliumia sana kumkuta kwenye hali ile. Moyo wake ulihuzunika sana. "Teddy sio muda wa kulia mama, nilazima tuondoke hapa kwa muda huu. Nilazima tuondoke hapa kwa kuwa kazi bado ni ngumu. Nataka kichwa cha suresh katika usiku wa leo. Nataka wote wanaohusika wapewe usafiri." Aliongea masimba huku akimtoa teddy kifuani. Punde walikuwa wakiondoka katika Jengo lile akiongozwa na Teddy. Walipita katika njia ambazo hakuzielewa. Hakuwahi kuwaza kama katika nchii kulikuwa na vitu vya aina ile. Walipita katika njia ambazo kama asingekuwa Teddy basi angebaki Jina. Mabomu yakutegwa yalikuwa yamepandwa chini ya ardhi. Alitembea akifuata hatua za teddy hakutaka kwenda tofauti kabisa. Kila sehemu ambayo teddy alipita alikuwa akimuonyesha kila kitu ambacho kilikuwepo katika eneo lile. Moyoni masimba alikuwa akifarijika kwa kile alichokuwa akikitizama. Alihitaji kuijua njia kwa kuwa alitaka kurudi akiwa peke yake. Hivyo ilimlazimu kukalili njia ile... wakati wanakaribia kuumaliza ule msitu, teddy akamsimamisha kwanza. Wakasimama hapo kwa muda teddy akionekana ni mwenye kufikiria kitu. Alikaa kimya kwa muda wa dakika mbili, baada ya hapo akamwambia Masimba waondoke katika njia mbili tofauti. Teddy alihitaji kila mmoja apite katika njia yake. Masimba hakutaka kulipinga hilo. Akatembea akimuacha Teddy akimuangalia. Akimuangalia katika namna ambayo hakuilewa. Masimba akatembea akiruhusu miguu yake kutembea kwa tahadhari. Hakugeuka nyuma kumuangalia teddy, aliamini teddy alibaki nyuma kama mlinzi wake. Alitembea kwa umbali mrefu kidogo bila kumuona Teddy. Hata alipotokea sehemu Teddy alipiacha gari bado teddy hakuonekana. Hilo likampa shaka masimba, shaka ya kuhisi kitu kutoka kwa teddy. Akauvuta Muda akisubiri kufika kwa Teddy. Lakini wakati akifikiria hilo akakisikia kishindo, kishindo kilichofuatiwa na Milipuko na moto mkubwa kusambaa angani. Hilo halikutegemewa na Masimba, hilo halikutegemewa kwa kuwa alihitaji kulifanya yeye. Kwa nini Teddy? Yalikuwa mawazo yaliyokuwa yakipingana kichwani mwake. Moto ukaendelea kuwaka huku vishindo vya mabomu vikisikika. Licha ya hilo bado hakumuona teddy, bado teddy wake hakuwa ametokea. Bado Teddy hakuwa amefika. Hilo likampa mashaka makubwa. Mashaka ambayo yalimfanya ahitaji kurudi Tena kule alikomuacha teddy. Ni wakati huo akiutizama moto akashtuliwa na sauti ya mtu ikitokea nyuma yake. Hii ilikuwa sauti ya Teddy. Akageuka akionyesha kutokuamini. Macho yake yakakutana na tabasamu kutoka kwa teddy. "Tuondoke Mume wangu." Aliongea Teddy akiufungua mlango ili Masimba aingie.

******

"Mambo yamesha kuwa mabaya, tayari majina yetu yametua ikulu na ushahidi wote upo mikononi kwa masimba. Abanwe mpaka aongee ukweli tusimuache katika hili." Ilikuwa sauti ya Mbunge wa jimbo la Kigamboni Bibi Grace Bwahama akiongea na wajumbe katika kikao kile kilichoitishwa baada ya kukamatwa kwa Mpelelezi Hatari. "Masimba Bado yupo mikononi mwetu, tutajua nini chakumfanya. Tunachotakiwa kukifanya hivi sasa ni kumtafuta kwanza teddy ili tumfutilie mbali. Hili la majina kufika Ikulu lisikupe shaka tutalishughulikia kwa uhakika na litakwisha. Chakufanya ni kuongea na Mr Jacob John Okoth Atuongezee nguvu katika suala hili. Teddy ameonyesha jeuri kubwa kwa kuwa anatufahamu. Nilazima tutumie huku kutufahamu kwake kumuulia mbali. Tunajua ni lazima aanze kutuwinda katika namna yoyote. Nilazima tumuwahi kabla hatujafanya Rabsha yoyote. Naomba tutulie, nitaongea na Mr Okoth nadhani leo hii vijana wake wata... kabla hajamaliza kauli yake simu yake ikapata uhai. Alipotizama juu ya kioo akakutana na namba maalum wanazo wasiliana wao kwa wao.. Kabla hajaipokea akawatizama wenzake kwanza. Haikuwa kawaida kupigiwa kwa namba ile. Huku moyo ukimdunda na mikono kutetemeka akaipokea simu. "Jimmy Lambert naongea." Akaongea Jimmy huku mapigo ya moyo yakimuenda Kasi. "Bosi Secret Base inawaka moto.. makombora yanalipuka kwa sasa." Ilisikika sauti ya upande wa pili. "Ooh my God!! Nini kimetokea? Na ilikuwaje? Akauliza Jimmy Mshangao ukiupamba Uso wake. "Sijui lakini nahisi mtu wetu ametuzidi ujanja na ameamua kufanya alichokifanya." Alijibu mtu wa upande wa pili. "Wewe unaongelia kutoka wapi kwa sasa?" akauliza Jimmy.

"Nipo mafichoni karibu na Eneo la tukio. Alijibu mtu yule. Mara mlipuko mkubwa ukasikika. Hata jimmy aliusikia kwa kuwa bado simu ilikuwa hewani. Hapo akaamini ni kweli Kambi yao ya Siri ilikuwa ikilipuka. Akaikata simu huku akiigonga meza. "Teddy nitakuua kwa mikono Yangu. Nitakuua mimi mwenyewe." Alifoka jimmy akiendelea kupiga ngumi kwenye meza. Kilikuwa kitu kilichowashangaza wadau wenzake. Kila mmoja alikuwa akimuangalia Jimmy Alivyokuwa akihamanika huku na huko. Kwa nini Teddy? Teddy ana nini? Yalikuwa maswali yaliohitaji majibu kutoka kwa Jimmy. Jimmy ambaye alikuwa akitetemeka. "Secret Base Inateketea kwa Milipuko. Teddy na Masimba wameamua kututia vidole vya machoni. Wameamua kututia Hasira. Ni kosa kubwa tumefanya kuwaamini vijana wale mbele ya mtu kama Masimba. Vijana watakuwa wamefanya kosa. Tena kosa kubwa ndio maana masimba anatuadhibu." Aliongea Jimmy safari hii akiinuka kabisa. Chumba kizima kikatawaliwa na ukimya. Ukimya uliozua maswali vichwani kwa watu hawa. Kila mmoja akiwaza kile alichokiamini. Lakini kwa upande wa jimmy, masimba alikuwepo kwa mbali, alikuwa kwa mbali kwa kuwa masimba hakuijua ile kambi. Hakujua kama Chini yametegwa mabomu. Ni teddy tu ndiye aliujua ukweli. Alijua kila kitu kuhusu kambi ile. Ni teddy aliyefanya tukio hili. Ni Teddy alieamua kuwatia hasira. Jimmy alikuwa akiapa huku akibubujikwa machozi. Hakuamini alichokisikia. Sasa akaamua kutoka ukumbini pasipo kuongea na mtu. Alichanganyikiwa na hata kuvurugwa. Alipotoka nje kabisa alipajipakia ndani ya gari, akawasha na kuliondoa kuelekea sehemu ya Tukio.

********

Baada ya kutoka kule kwenye kambi ya Siri. Masimba na Teddy wakarudi mpaka nyumbani kwao. Walipoingia tu ndani teddy akamuendea masimba kisha kumkumbatia. "Pole sana Mume wangu, mimi ndiye niliyesababisha wewe uumie. Kama sio tamaa yangu haya yote yasingetokea. Ona ulivyoumia kwa ajili ya ujinga Wangu. Nisamehe Mpenzi wangu. Nimeamua kusimama na na wewe. Nimeamua kuwa sambamba na wewe. Nisamehe sana." Aliongea teddy huku akimuangalia masimba usoni katika jicho la aina yake. Jicho legevu lenye kushawishi. "Najua yote, lakini hupaswi kujilaumu kwa sasa. Kama sio wewe na kama sio kifo cha Asteria P Paulo nadhani mpaka leo Nchi yetu ingekuwa katika hatari kubwa sana. Bila wewe nisingeijua biashara hii uliyokuwa ikimhusisha mpaka kiongozi mkuu wa nchi. Teddy mimi kukusamehe sio kwamba nimejilazimisha. Niliamini na kukuamini. Nilijua hiii ni vita yetu mimi na wewe. Nilijua ni hii ni vita ya kuwakomboa vijana wengi wanaoendelea kuharibiwa na madawa ya kulevya. Tusingeligundua hili ama asingeuawa Asteria Basi Taifa lingeendelea kuwa katika kipindi hatari zaidi. SIO WAKATI WA KUJILAUMU MAMA, HUU NI WAKATI WA BASTOLA ZETU KUIFANYA KAZI ILIYOBAKI
 
Jimmy atachanganyikiwa zaidi akikutana na masimba USO Kwa USO
 
Ibra huyo mtu amenitumia risiti. Amekuwekea sh.elfu 24500 tangu jana. Naomba angalia vizuri.kumbukumbu ya malipo no 0675191162. Muamala bp 1705131832
 
Ibra huyo mtu amenitumia risiti. Amekuwekea sh.elfu 24500 tangu jana. Naomba angalia vizuri.kumbukumbu ya malipo no 0675191162. Muamala bp 1705131832
Sijajua tatizo lilipo but ntil now sijapata chochote. That's why nikaomba namba ili Niongee naye. But kama anasema ametuma basi tuchukulie ametuma. Lakini sijapokea kiwango hicho na hata tigo wenyewe wamekataa
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 059

"Sio wakati wa kuomba msamaha, ni wakati wa kuziacha Bastola zetu zifanyekazi. Niwakati wakulipigania taifa. Niwakati wakuliokoa taifa kutoka kwa watu ambao nia yao ilikuwa kuharibu Taifa Zima. Tunejitolea kufa na kupona ili kulizima hili. Unatakiwa kusimama Imara huku bastola tukiiacha Ikifanya kazi yake." Aliongea masimba huku akimuangalia Teddy machoni. Akimuangalia katika namna ya kumjaza nguvu. Muda wote walijua wapo katika vita ya kutetea na kuwapigania Vijana wanaoendelea kuharibiwa kwa madawa ya kulevya. Alikuwa tayari kufa kwa sababu ya Hilo. Wakaangaliana na kuangaliana, midomo ikakutana na menginr kuendelea. Mengine yakuiburudisha miili yao na kuipa nguvu. Kila mmoja alikuwa na hamu na mwenzake.. hamu ya kuweza kuifanya dunia iwahurumie. Hapakuwa na kizuizi hata pale walipoangukia kitandani. Hawakuwa na kizuizi hata pale kitanda kilivyowapokea na kuwapa hifadhi. Burudani ikatendeka katika namna ya ufundi mujarabu. Ufundi ambao ulimuacha teddy akiichanisha miguu zaidi na Zaidi. Akiutoa uhuru katika namna ya kumsusumia mtendaji. Ulikuwa mchezo mzuri sana, ulikuwa mchezo wa kuvutia na kupendeza. Mchezo ambao mwisho wake uliwaacha wote wakitazama kwa muda kila mmoja akiwa pembeni kwa mwenzake.

******

Upepo ulivuma taratibu katika pwani ya bahari ya hindi eneo la kigamboni. Ulikuwa upepo uliovuma katika aina fulani ya kuuongeza uhai katika namna ipendezayo. Pembeni kabisa mwa fukwe maarufu itwayo Mikadi, watu wawili walikuwa wamekaa pembezoni kabisa mwa ufukwe ule huku macho yao yakitizama mlango wa kuingilia katika fukwe hizo. Walionekana ni wenye kusubiri kitu ama kuchunguza kitu. Nyuso zao zisizo hata na tabasamu zilikuwa zikizunguka huku na kule kuonyesha umakini. Hawakutaka kupitwa ama kuachwa na kitu chochote. Mmoja akiwa amevaa kaptura fupi na tishite ya kumbana sambamba na viatu vyepesi chini. Huyu wa pili alikuwa mrefu mweusi, alivaa suruali ya kitambaa, shati la rangi nyekundu, sambamba na Viatu vyeusi. Huyu hakuonekana kama ni Raia wa Tanzania. Watu hawa wawili hawakuwa hapo kwa bahati mbaya. Walikuwa hapo kwa sababu ya kuianza kazi yao. Kazi iliyowatoa nchi kenya na kuwaleta hapa Tanzania. Kazi ya kufuata nyendo za watu watatu ambao walikuwa hatari sana. Leo walikuwa hapa mikadi wakiwa na picha ya Vicky mkononi. Vicky mdogo wa Teddy. Fununu za watu na uchunguzi wao wa awali waligundua kuwa Vicky alipenda sana kutembelea Hapo kila mwisho wa wiki. Hivyo ilikuwa Rahisi kuianza kazi yao mapema ili kumlazimisha teddy afanye kile wanachotaka hasa pale watakapo kuwa wamemteka Vicky. Macho yao yakaendelea yakiangalia kila mtu aliyekuwa akiingia hapo.
Wakati wao wakilifanya hilo la kumsubiria Vicky, kushoto kwao umbali wa hatua ishirini alikaa msichana mmoja mrembo sana akionekana kuchezea simu huku mara moja moja akiwatupia macho wanaume wale wawili. Mkononi alikuwa na camera ndogo ya kirusi yenye ukubwa mfano wa kibiriti. Ilikuwa camera maalum ya kuchukua matukio makubwa katika muda mfupi na kwa siri sana. Safari ya msichana huyu kuja hapa kwenye fukwe hizi ilianza tokea usiku wa Jana pale alipowaona watu hawa wakishuka uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere. Uonekanaji wa watu hawa walipokuwa wakishuka sambamba na wengine watano ndio sababu iliyofanya yeye kuamua kuingia kazini sambamba na wenzake ambao nao walijigawa katika kuwafuatilia watu hawa huku wakiripoti moja kwa moja Makao makuu ya Idara Ya ujasusi. Kila kitu kilifanywa kwa usiri mkubwa sana tokea pale Masimba alipowasilisha Ushahidi baadhi wa kumhusisha hayati waziri mkuu na biashara haram ya madawa sambamba na nyara za serikali. Majasusi wengi walikuwa wakiwafuatilia Jimmy sambamba na washirika wengine. Kila alipokuwa akikanyaga Jimmy, watoto wa makumbusho nao walikuwa wapo nyuma wakinusa na kutafuta wapi kapita. Ulikuwa upepelezi wa kiwango cha hali ya juu. Hata pale Jimmy alipokwenda kuwapokea vijana hawa katika uwanja wa ndege, mbwa wa kunusa harufu yoyote iliyojificha walikuwa nyuma yake wakimtizama. Ingawa vijana wale walishuka tofauti pale uwanjani, lakini haikuwa ngumu majasusi hawa kuwagundua. Hotel walizofikia zikawekwa wahudumu wazuri wakike ambao walikuwa ni undercover. Mienendo yao ikachunguzwa kila walipotoka na hata kurudi. Wana usalama wakike na kiume walikuwa wakipishana kama wafanyakazi wa hotel husika.

Hata leo hii walipotoka na kuja pale kwenye ufukwe , nyuma hawakujua kuwa wapo wa na usalama wakiwafuatilia kwa siri kubwa. Wakiwa wao wamekaa wakichunguza wanaoingia na wanaotoka, watu watatu waliokaa sehemu tofauti macho yao yalikuwa yakiwatizama wao kufuata kile ambacho wao wanakitenda. Macho ya wana usalama wengine yalikuwa yakifuata uelekeo wa macho ya watu wale, huku yule wakike akichukua picha za video na kutuma makao makuu. Wakiwa bado katika hilo wakamuona mtu akiiingia katika namna ya kuvutia. Alikuwa mwanamke mrefu mwembamba, alionekana mfano wa msichana wa kinyarwanda kwa mwendo wake na hata umbile lake. Aliingia akiwa amewashikilia watoto watatu, watoto ambao kwa muonekano walikuwa ni wachangamfu sana. Huyu alikuwa vicky mdogo wa Teddy. Alikuwa sambamba na Abby, Queen na Amanda. Alikuwa akiingia hapo kukutana na mtu ambaye alimpigia simu usiku wa jana na kumuomba wakutane hapo kwa mazungumzo. Vicky alitembea huku akipepesa macho yake huku na huko. Simu ilikuwa sikioni akiipiga namba ya mtu husika ambaye alimwambia yupo hapo mikadi. Watoto nao walikuwa wakimtizama kwa namna fulani ya kusubiri kuambiwa twendeni huku. Wakati wote huo macho ya wanausalama hayakucheza mbali na hapo. Ni wakati wakilitizama hilo wakamuona Vicky akipaaa juu na kuanguka chini. Kilikuw kitendo kilichotendeka ndani ya sekunde tano. Watoto wakapiga mayowe.. wana usalama wakagundua kuchelewa kwao, huyu akatoka hapa na yule kutoka pale.. kila mmoja akiwakimbilia watoto waliokuwa wakilia Juu ya mwili wa vicky ambao ulitapakaa Damu. Ilikuwa taharuki kubwa katika fukwe zile. Macho ya wanausalama wengine yalizama kwenye kutizama mtu ambaye angeonyesha utofauti katika eneo. Wakati watu wakiendelea kukimbia hovyo, watu hawa wawili nao waliinuka na kuanza kuelekea sehemu ya tukio. Huyu msichana naye akainuka kuelekea huko akihakikisha hagunduliki kwa mtu yoyote. Alikuwa akitembea huku macho yake yakitembea huku na huko. Hatua kumi katika mbio hizo akamuona mtu akijiunga katika msafara ule wa watu wawili. Watu ambao yeye alikuwa nyuma yao akiwatizama. Mtu huyu watatu ni mtu ambaye ilimbidi apunguze mwendo kumuangalia vizuri. Mshangao ukatamalaki usoni. Pale alipomgundua mtu huyu. Alikuwa Amemuona Masimba akijiunga na watu hawa. Ni wakati akilishangaa hilo, akaliona Jingine, jingine ambalo lilimuacha mdomo wazi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom