NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 059
"Sio wakati wa kuomba msamaha, ni wakati wa kuziacha Bastola zetu zifanyekazi. Niwakati wakulipigania taifa. Niwakati wakuliokoa taifa kutoka kwa watu ambao nia yao ilikuwa kuharibu Taifa Zima. Tunejitolea kufa na kupona ili kulizima hili. Unatakiwa kusimama Imara huku bastola tukiiacha Ikifanya kazi yake." Aliongea masimba huku akimuangalia Teddy machoni. Akimuangalia katika namna ya kumjaza nguvu. Muda wote walijua wapo katika vita ya kutetea na kuwapigania Vijana wanaoendelea kuharibiwa kwa madawa ya kulevya. Alikuwa tayari kufa kwa sababu ya Hilo. Wakaangaliana na kuangaliana, midomo ikakutana na menginr kuendelea. Mengine yakuiburudisha miili yao na kuipa nguvu. Kila mmoja alikuwa na hamu na mwenzake.. hamu ya kuweza kuifanya dunia iwahurumie. Hapakuwa na kizuizi hata pale walipoangukia kitandani. Hawakuwa na kizuizi hata pale kitanda kilivyowapokea na kuwapa hifadhi. Burudani ikatendeka katika namna ya ufundi mujarabu. Ufundi ambao ulimuacha teddy akiichanisha miguu zaidi na Zaidi. Akiutoa uhuru katika namna ya kumsusumia mtendaji. Ulikuwa mchezo mzuri sana, ulikuwa mchezo wa kuvutia na kupendeza. Mchezo ambao mwisho wake uliwaacha wote wakitazama kwa muda kila mmoja akiwa pembeni kwa mwenzake.
******
Upepo ulivuma taratibu katika pwani ya bahari ya hindi eneo la kigamboni. Ulikuwa upepo uliovuma katika aina fulani ya kuuongeza uhai katika namna ipendezayo. Pembeni kabisa mwa fukwe maarufu itwayo Mikadi, watu wawili walikuwa wamekaa pembezoni kabisa mwa ufukwe ule huku macho yao yakitizama mlango wa kuingilia katika fukwe hizo. Walionekana ni wenye kusubiri kitu ama kuchunguza kitu. Nyuso zao zisizo hata na tabasamu zilikuwa zikizunguka huku na kule kuonyesha umakini. Hawakutaka kupitwa ama kuachwa na kitu chochote. Mmoja akiwa amevaa kaptura fupi na tishite ya kumbana sambamba na viatu vyepesi chini. Huyu wa pili alikuwa mrefu mweusi, alivaa suruali ya kitambaa, shati la rangi nyekundu, sambamba na Viatu vyeusi. Huyu hakuonekana kama ni Raia wa Tanzania. Watu hawa wawili hawakuwa hapo kwa bahati mbaya. Walikuwa hapo kwa sababu ya kuianza kazi yao. Kazi iliyowatoa nchi kenya na kuwaleta hapa Tanzania. Kazi ya kufuata nyendo za watu watatu ambao walikuwa hatari sana. Leo walikuwa hapa mikadi wakiwa na picha ya Vicky mkononi. Vicky mdogo wa Teddy. Fununu za watu na uchunguzi wao wa awali waligundua kuwa Vicky alipenda sana kutembelea Hapo kila mwisho wa wiki. Hivyo ilikuwa Rahisi kuianza kazi yao mapema ili kumlazimisha teddy afanye kile wanachotaka hasa pale watakapo kuwa wamemteka Vicky. Macho yao yakaendelea yakiangalia kila mtu aliyekuwa akiingia hapo.
Wakati wao wakilifanya hilo la kumsubiria Vicky, kushoto kwao umbali wa hatua ishirini alikaa msichana mmoja mrembo sana akionekana kuchezea simu huku mara moja moja akiwatupia macho wanaume wale wawili. Mkononi alikuwa na camera ndogo ya kirusi yenye ukubwa mfano wa kibiriti. Ilikuwa camera maalum ya kuchukua matukio makubwa katika muda mfupi na kwa siri sana. Safari ya msichana huyu kuja hapa kwenye fukwe hizi ilianza tokea usiku wa Jana pale alipowaona watu hawa wakishuka uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere. Uonekanaji wa watu hawa walipokuwa wakishuka sambamba na wengine watano ndio sababu iliyofanya yeye kuamua kuingia kazini sambamba na wenzake ambao nao walijigawa katika kuwafuatilia watu hawa huku wakiripoti moja kwa moja Makao makuu ya Idara Ya ujasusi. Kila kitu kilifanywa kwa usiri mkubwa sana tokea pale Masimba alipowasilisha Ushahidi baadhi wa kumhusisha hayati waziri mkuu na biashara haram ya madawa sambamba na nyara za serikali. Majasusi wengi walikuwa wakiwafuatilia Jimmy sambamba na washirika wengine. Kila alipokuwa akikanyaga Jimmy, watoto wa makumbusho nao walikuwa wapo nyuma wakinusa na kutafuta wapi kapita. Ulikuwa upepelezi wa kiwango cha hali ya juu. Hata pale Jimmy alipokwenda kuwapokea vijana hawa katika uwanja wa ndege, mbwa wa kunusa harufu yoyote iliyojificha walikuwa nyuma yake wakimtizama. Ingawa vijana wale walishuka tofauti pale uwanjani, lakini haikuwa ngumu majasusi hawa kuwagundua. Hotel walizofikia zikawekwa wahudumu wazuri wakike ambao walikuwa ni undercover. Mienendo yao ikachunguzwa kila walipotoka na hata kurudi. Wana usalama wakike na kiume walikuwa wakipishana kama wafanyakazi wa hotel husika.
Hata leo hii walipotoka na kuja pale kwenye ufukwe , nyuma hawakujua kuwa wapo wa na usalama wakiwafuatilia kwa siri kubwa. Wakiwa wao wamekaa wakichunguza wanaoingia na wanaotoka, watu watatu waliokaa sehemu tofauti macho yao yalikuwa yakiwatizama wao kufuata kile ambacho wao wanakitenda. Macho ya wana usalama wengine yalikuwa yakifuata uelekeo wa macho ya watu wale, huku yule wakike akichukua picha za video na kutuma makao makuu. Wakiwa bado katika hilo wakamuona mtu akiiingia katika namna ya kuvutia. Alikuwa mwanamke mrefu mwembamba, alionekana mfano wa msichana wa kinyarwanda kwa mwendo wake na hata umbile lake. Aliingia akiwa amewashikilia watoto watatu, watoto ambao kwa muonekano walikuwa ni wachangamfu sana. Huyu alikuwa vicky mdogo wa Teddy. Alikuwa sambamba na Abby, Queen na Amanda. Alikuwa akiingia hapo kukutana na mtu ambaye alimpigia simu usiku wa jana na kumuomba wakutane hapo kwa mazungumzo. Vicky alitembea huku akipepesa macho yake huku na huko. Simu ilikuwa sikioni akiipiga namba ya mtu husika ambaye alimwambia yupo hapo mikadi. Watoto nao walikuwa wakimtizama kwa namna fulani ya kusubiri kuambiwa twendeni huku. Wakati wote huo macho ya wanausalama hayakucheza mbali na hapo. Ni wakati wakilitizama hilo wakamuona Vicky akipaaa juu na kuanguka chini. Kilikuw kitendo kilichotendeka ndani ya sekunde tano. Watoto wakapiga mayowe.. wana usalama wakagundua kuchelewa kwao, huyu akatoka hapa na yule kutoka pale.. kila mmoja akiwakimbilia watoto waliokuwa wakilia Juu ya mwili wa vicky ambao ulitapakaa Damu. Ilikuwa taharuki kubwa katika fukwe zile. Macho ya wanausalama wengine yalizama kwenye kutizama mtu ambaye angeonyesha utofauti katika eneo. Wakati watu wakiendelea kukimbia hovyo, watu hawa wawili nao waliinuka na kuanza kuelekea sehemu ya tukio. Huyu msichana naye akainuka kuelekea huko akihakikisha hagunduliki kwa mtu yoyote. Alikuwa akitembea huku macho yake yakitembea huku na huko. Hatua kumi katika mbio hizo akamuona mtu akijiunga katika msafara ule wa watu wawili. Watu ambao yeye alikuwa nyuma yao akiwatizama. Mtu huyu watatu ni mtu ambaye ilimbidi apunguze mwendo kumuangalia vizuri. Mshangao ukatamalaki usoni. Pale alipomgundua mtu huyu. Alikuwa Amemuona Masimba akijiunga na watu hawa. Ni wakati akilishangaa hilo, akaliona Jingine, jingine ambalo lilimuacha mdomo wazi.