Riwaya: Nitakupata tu

Riwaya: Nitakupata tu

Ibra naomba nirushie no.yako. kesho nina nafasi nitatuma mchango wangu. Ila utaupata jioni. Simu yangu niliipoteza no.yako ilikuwepo kwenye simu iliyopotea
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 056

Masimba hakujua tena kile kilichoendelea. Akaruhusu giza kuifuta Nuru ya macho yake. Akatulia na kutulia.

*****

Teddy alishangaa muda kakatika bila Masimba kufika nyumbani. Kwani walipoachana usiku ule alimwambia kuwa angerudi katika muda wa usiku ule. Lakini mpaka saa mbili ile hakuwa amemuona Masimba pale nyumbani. Hilo likampa shaka na wasiwasi mkubwa, alihisi masimba alikuwa kwenye hatari ama atakuwa ameshakufa. Kwa kuwa wakati wanaachana alimeambia anaelekea nyumbani kwa Chief.. Teddy Hakuona sababu ya kuendelea kukaa pale ndani. Alitaka kwenda kumtafuta Masimba, alitaka kuinasa habari kuhusu wapi alipo mwanaume wake. Akaondoka mle ndani akipanga kuelekea masaki. Masaki sehemu ambayo ilikuwa ya mwisho Masimba kusema kwamba anaelekea huko. Hakutaka kumuacha France, aliamua kumchukua na kuelekea naye huko. Japo ilikuwa ni hatari lakini asingemuacha mtoto katika jumba lile akiwa peke yake. Alijiandaa na kumuandaa France, muda mfupi baadae walikuwa Njiani akielekea Masaki. Kujua taarifa ya mtu sahihi kwake. Alifika masaki asubuhi ile na kupokelewa na Walinzi wa Chief. Akawasalimia na kuwaambia adhma yake ya kuonana na Chief. Simu ikapigwa moja kwa moja na majibu yalipokuja yakamkuta Teddy tayari yupo ndani akizikwea ngazi. Alihitaji kufahamu wapi alipoelekea Masimba baada ya kuondoka hapo. Alizimaliza ngazi na kutokea katika chumba maalum cha Chief. Aliingia akiwa katika sura yake nzuri lakini isiyokuwa na tabasamu. Macho yake yakakutana na macho ya Chief ambayo yalionyesha kuwa hayakupata mapumziko kwa muda mrefu. "Karibu Sana Mama..." aliongea Chief kwa sauti yake tulivu. "Ahsante Baba Yangu, nimekaribia lakini sikuja kukaa mzee.. nimekuja kukuulizia kuhusu muwendaji wako mkuu hajarudi jana." Aliongea Teddy macho yake yakimuangalia chief usoni kutafuta kitu machoni kwake. Alitaka kuumsoma Chief katika aina na mtindo aujuaye yeye. Lakini akakutana na macho ya chief yasio na hofu. Macho ya chief yaliyo yakawaida kabisa kuonyesha hakuwa na mashaka. "Teddy umepoteza uwezo wako uliokuwa nao mwanzo.. Teddy wa mwanzo anapotokewa na hali hiyo alianza kwanza kuutafuta ukweli.. Teddy yule hakuwa akifunga safari kuja ofisini ama hapa nyumbani. Aliitenda kazi ya kumtafuta kwa mikono yake mwenyewe. Umeingia wapi muwindaji wangu? aliongea Chief kwa sauti yenye umakini wa hali ya juu. Teddy akainua uso na kumtizama mzee kwa mara ya pili. Maneno ya chief yalikuwa na ukweli ndani yake. Hakuwahi kuja ofisini wala nyumbani kwa Chief. Aliutafuta ukweli mwenyewe. Hilo likamfanya ainuke na kumuaga chief. Alitaka kwenda kumtafuta Masimba na kumrudisha akiwa hai ama mfu. Alitambua Masimba atakuwa sehemu ametekwa ama kuuawa. Wakati anakaribia kutoka mlango wa mwisho wa jumba la mkurugenzi akaisikia Sauti ya Chief ikimuita. "Teddy Rudi ndani mara moja!!" Ilikuwa sauti ya Chief, mara hii ikionyesha haipo kwenye ukawaida. Teddy akageuka na kurudi ndani. Akitembea Huku macho yake yakipepesa huku na huko. Tofauti ya Chief ya safari hii ilimuonyesha kuwa chief ameipata habari mbaya. Alipomkaribia Chief, chief akanyoosha mkono na kumpa kikaratasi fulani. "Muwindaji wangu amefungiwa sehemu fulani pembezoni mwa Jiji.. Chukua hiyo namba, nenda kwa watu wa Mamlaka ya Mawasiliano Wakwambie hiyo namba imetuma ujumbe kutoka wapi. Nenda Ofisini waambie wakusaidie kupata taarifa ya namba hiyo." Aliongea Chief huku akigeuka kurudi ndani. Teddy hakusubiri, kile alichokuwa akikifikiria ndicho ambacho kimetokea. Akaliacha jengo la chief. Akatembea mpaka alipoiacha Gari yake. Akaufungua mlango wa gari na kujipakia. Safari yao ikaanza kuelekea kijitonyama.. njiani mawazo yaliendelea kumzonga juu ya kutekwa kwa masimba. Nani atakuwa amemteka? Je wamempeleka wapi? Aliyawaza yote huku akimuangalia France aliyekuwa amekaa pembeni. Akakumbuka kwamba alipewa namba na hakuifungua kuiangalia. Akaichukua karatasi ile na kukifungua. Punde alikuwa akiitizama namba ya mtu anayemfahamu. Mtu ambaye alimtambua na kumjua kiundani Zaidi. Alikuwa akiitizama namba ya suresh. Kengele ya tahadhali ikagonga kichwani.

Alitambua Jimmy na washirika wake ndio wako nyuma ya kutoweka kwa masimba. Hapo ndipo alipoipata hamu ya kuweka laini yake ya zamani. Aliwaza kufanya hivyo kwa kuwa aliamini angetumiwa ujumbe kutakiwa kufanya kitu kwa sababu ya kuachia Huru kwa Mpenzi wake. Akaegesha gari pembeni na kuitoa simu yake kisha kuipachika laini husika. Baada ya kuiweka na kukaa sawa.. Muda ule ule akaiona simu yake ikiita, alipoangalia Jina la mpigaji moyo ulimpiga paa baada ya kuona namba ya Chief. Haraka haraka akaipokea.. "hallow baba!!" Aliita Teddy.

"Umefika ofisini tayari? Aliuliza Chief akionyesha wasiwasi kwa sauti yake.

"Hapana, lakini nishamtambua na kuwatambua wote." Akajibu.

"Umewatambua na kuwajua? Ni kina nani? Wamenitumia ujumbe nikutafute nikwambie uupeleke mzigo wao ili tumchukue Masimba." Aliongea chief.

"Hawapelekewi chochote na Masimba atarudi akiwa hai na Salama. Niachie mzee hii ni vita yangu mimi. Masimba aliingia katika Hili kimakosa. Naomba ukae kimya na usijibu chochote." Aliongea Teddy na kukata simu. Sasa alikuwa akiingia kazini rasmi, alikuwa akiingia katika kazi nzito na ya Hatari. Aliujua ugumu na alitambua hatari yake. Hapo ndipo alipoamua kumpeleka France nyumbani kwa Chief. Alitaka kuwa huru katika kuifanya kazi yake. Alitaka kuwaonyesha kuwa hakuwahi kutishwa na akaogopa. Wakati akiwaza Hayo simu yake Ikaita. Kutizama namba ya mpigaji ilikuwa ni namba ile ile ya Suresh. Akaipokea na kuipeleka Sikioni. "Tunauhitaji Mzigo wetu, la sivyo utaiokota maiti ya mpenzi wako." Aliisikia sauti ya upande wa Pili ikiinguruma. Ilikuwa sauti tofauti na ya Suresh.. hii ilikuwa ngeni masikioni kwake. "Sileti chochote, hampati Chochote, na Masimba nitakuja kumchukua mimi mwenyewe." Alijibu Teddy.

Ukimya wa Ajabu ukatokea, kisha kicheko kikafuata. "Teddy wewe ni mdogo sana.. huwezi kupambana na sisi. Nakuonya usithubutu kufanya lolote utampoteza Masimba na hata wewe mwenyewe utapotea." Bado mtu wa upande wa pili alisikika akinguruma.

"Sijawahi kutishwa kisha nikaogopa. Nakipenda kifo na naipenda Damu pia. Nimeshatoka sehemu hatarishi kuliko. Sasa naomba nikwambie.. sitafanya chochote kile mnachohitaji, lakini ninachokisema ni kwamba Masimba atatoka na mzigo hautatoka. Mwambie Jimmy na Suresh sijawahi kushindwa kile ninachokiamua. Vita ndio imeanza." Aliongea Teddy kisha akakata simu. Aliuona uoga wa adui zake. Aliuona uoga wa kina Jimmy. Hili lilionyesha ni jinsi gani watu hawa walivyo waoga.

******
Alihisi kama yupo kwenye kina cha maji kilichommeza kiwiliwili chote. Kichwa chake pekee ndicho ambacho kilibaki. Hewa nzito na harufu mbaya ni vitu pekee vilivyomfanya aanze kufumbua macho yake taratibu na kutizama. Giza, ndio kitu cha kwanza kukutana nacho pale alipoyafumbua macho yake. Alijaribu kuangaza huku na kule kama ataona kitu chochote, lakini hakukiona chochote kile. Bado giza lilitanda kila kona. Akatulia kwa muda kuipa utulivu akili yake, alitaka kuipa muda wa kufikiria hatimaye kufanya maamuzi sahihi. Chumba alichofungiwa kilimpa majibu ya wapi alipo. Akaendelea kuwaza na kuwazua, akainuka pale chini na kukaa kitako. Akaitizama mikono yake ambayo haikufungwa na chochote kisha akacheka. Ni kosa kubwa kumuacha Jasusi mfano wake katika Uhuru wa aina yake. Kumuacha huru katika namna ile ilikuwa ni kumpa nafasi ya kufanya akitakacho. Aliamini angetoka katika muda wowote na katika namna yoyote. Punde akasikia nyayo za watu zaidi ya mmoja zikisogea kuelekea pale ndani. Masimba akarudi chini katika kuzuga kuwa bado hakurudiwa na fahamu. Kwa aina fulani ya kutizama akawaona watu wawili wakiingia ndani huku watatu waliokamatia bunduki nzito wakibaki mkononi wakiitizama kila hatua huku wakiwa tayari kwa chochote. Akaendelea kutulia wakati watu wale walipombeba na kuanza kutoka naye ndani ya chumba kile kinachoonekana kama kuzimu. Alitulia akiangalia kwa umakini, alilichunguza Jengo lile ili akianzisha Rabsha iwe ni rahisi kutoka.

Bado watu wale waliendelea kusonga mbele ndani ya jengo hilo. Wakaufikia mlango mmoja uliotengenezwa kwa chuma. Mmoja akabonyeza kitufe kimoja mara lango likafunguka. Macho ya masimba yakakutana na chumba ambacho ndani yake damu nzito na mabaki ya Binadamu vilisambaa kila kona. AKAJUA SASA ALIKUWA AKIINGIZWA KWENYE CHUMBA CHA MATESO. AKAUANDAA MWILI WAKE TAYARI KWA KUKABILIANA NA MATESO HAYO
 
Kuna kitu napaswa kukifanya ili ninachokifanya kiheshimike. Nitaanza utaratibu wa kuituma hii riwaya kwa njia ya whatsap kwa wale ambao wanajitolea kila wakati kwa ajili ya kuona ndoto yangu inatimia.
 
Kuna kitu napaswa kukifanya ili ninachokifanya kiheshimike. Nitaanza utaratibu wa kuituma hii riwaya kwa njia ya whatsap kwa wale ambao wanajitolea kila wakati kwa ajili ya kuona ndoto yangu inatimia.
Shngap kuchangia ilii mtuu arushiwe kwa njia ya wasap
 
  • Thanks
Reactions: ADK
NITAKUPA TU

SEHEMU YA 057

********

Chumba kilitapakaa damu sambamba na mabaki ya binadamu. Muonekano wa chumba kile ni mfano wa kuzimu. Harufu ya uozo na hewa nzito ilikuwa mara mia na chumba alichotolewa. Wakamuingiza katika namna ya kutaka kumfunga kwenye kiti. Wakati wao wakilitaka hilo masimba macho yake yalikuwa kwa wale watu watatu waliokuwa wameshikilia bunduki. Alikuwa makini kwa kila hatua ya watu wale. Alihitaji kuliona kosa lao ili autumie muda ule kujiokoa. Macho yalikuwa makini zaidi ya majasusi wa CIA katika mission ya kumsaka Osam Bin Laden. Kila walipopiga hatua hata yeye macho yake yakavutika katika namna ya upigwaji wa hatua. Aliupenda na kuuhusudu utembeaji wa aina ile. Utembeaji uliokuwa ukisadifu utaalam na ujuaji katika tulivu, sikivu na elevu. Walionyesha kwamba ni watu wa aina gani, walionyesha hakuwa wa kawaida na pia walikuwa sio watu wa mchezo. Hilo halikuwa tishio kwa masimba, halikuwa tishio machoni kwa mwanaume huyu. Hakuogopa kwa kuwa hawakuwa maridadi katika kulitafuta na kulimudu lolote. Hakuogopa risasi na hata mapigano ya mikono.. alishapitia katika mission mbalimbali akiwa na nchi washirika. Akatulia chini wakati wanaume wale wawili wakitaka kumfunga kwenye kiti. Alizuga kulegea kama maiti, alionekana kama Mfu. Hawakuonyesha kujali katika hilo. Wakajiweka huru huku watu wale wenye silaha wakiweka silaha zao Chini. Hilo lilikuwa kosa kubwa katika hii kazi ya kijasusi. Lilikuwa kosa kubwa katika sheria na mikakati yakimapambano. Hukupaswa kuiacha nafasi ya namna ile, hawakupaswa kumpa uhuru katika hilo. Kitendo cha wao kuweka silaha zao chini tu, kikafuatiwa na kufyatuka kwa Masimba katika namna ya mshale na kuachia mapigo ambayo yaliwapata sahihi wanaume hawa wawili. Kwa kuwa yalikuwa mapigo makali wanaume wale walupepesuka na kuwaangukia wenzao waliokuwa wakishangaa, wote wakaenda chini. Hapo ndipo Masimba alipocharuka na kupambana kiume. Yalikuwa mapambano magumu kwake, yalikuwa mapambano ya kufa na kupona. Mapambano yaliodumu kwa dakika takribani Kumi. Damu ilikuwa imetapakaa.. wanaume watano walikuwa chini wakiwa wametulia. Hawakuwa wakipumua tena. Hata masimba alikuwa ametapakaa damu mwilini. Nguo zake zilikuwa zimechanika mpaka magotini.

Akainama na kuikota bunduki moja na kuishika mkononi. Akatoka akitembea huku mdomo wa bunduki ukiwa umetangulia mbele. Hakuogopa katika namna ile. Hakuogopa katika kutembea. Lakini kila alipokuwa akitembea alihisi ukimya ukiongezeka ndani ya Jengo lile. Akatembea kwa umakini akiendelea kuangalia huku na huko. Cha ajabu kila alipotembea ndani ya Jengo lile hakufanikiwa kuona mtu yoyote mwingone Zaidi ya Ukimya tu. Alitembea na kutoka ndani ya Jengo lile. Kutoka kwake nje akapokelewa na pori kubwa. Jengo lile lilikuwa katikati ya pori kubwa sana. Hapakuonekana Njia zaidi ya Nyasi ndefu tu. Hilo likamfanya ageuke nyuma kutizama ndani alipotoka. Bado akashangazwa na hilo. Hapakuonyesha uwepo wa watu, wala kuishi kwa watu eneo hilo. Hata ile njia ya kupita hakuijua wala kuiona. Jengo lote lilizungukwa na Nyasi Ndefu. Akaamua kurudi ndani tena kuitafuta simu yake ili awasiliane na Teddy. Alijua Teddy ni lazima anaijua sehemu hii alipo. akarudi mpaka chumba kile cha mwanzo lakuni hakuona chochote. Hata alipokwenda chumba cha pili hakuiona Simu yake isipokuwa simu za watu wale. Akainama na kuichukua Moja, akaiandika namba ya teddy mpya.. lakini Haikupatikana. Alipopiga ile ya zamani Tabasamu likaurudia uso wake baada ya kuona inaita.

"Hallow Dady.." Teddy akaita kwa jina ambalo lingeweza kumjulisha kama aliyepiga ni Masimba au lah.

"Yeah D..aliitika Masimba.

"Uko salama? Uko wapi? Na hii namba ni ipi? Aliuliza Teddy akionyesha kuwa na wasiwasi. "Nilipo sipajua Teddy. Nimekupigia kwa kuwa wewe ulikuwa unawajua hawa. Nipo katikati ya pori fulani lakini sijajua ni wapi. Hii simu nimeichukua kutoka kwa hawa maiti hapa. Tafadhali njoo haraka. Akaongea Masimba.

"Nakuja nishapajua, usiondoke wala kupiga hatua kuitafuta njia mpaka nifike.. Hiyo sehemu sio salama na imetegwa mabomu chini ya Ardhi." Aliongea Teddy .. masimba hakujibu, alichokifanya ni Kukata Simu na Kutulia ili kumsubiri Teddy.

Wakati akiendelea kumsubiri Teddy, akausikia mngurumo kama wa gari. Mngurumo ambao haukuchukua muda mrefu ukapotea katika ngoma za masikio yake. Akatulia akishangaa na kusikilizia. Punde akasikia michakato ya miguu ya mtu ikinjogea ndani ya jumba lile. Bunduki bado ilikuwa mkononi akijibanza akiangalia kule kule zinaposikika hatua. Hazikupita sekunde tano akamuona mtu mmoja akitembea kuingia pale ndani. Mkononi alikuwa amekamatia Bastola. Akamuangalia Vizuri mwanamke huyu. Kuigundua siri yake kukampa tabasamu la kukata na shoka. Alikuwa ni yule mwanamke waliyekutana pale Benki. Mwendo wake aliyoonyesha kutokuja kitu kinachoendelea pale. Hata alipobakiza hatua tano kufika usawa ule ambao masimba alijibanza, ndipo alipoihisi Tofauti. Akataka kugeuka Nyuma kutizama huko. Lakini kabla hajalifanya hilo MDOMO WA BUNDUKI UKATUA SHINGONI. USIJARIBU KUJITINGISHA..... NI SAUTI ILIYOSIKIKA NYUMA YAKE.
 
Umeona mchango Wang ibra, kidogo jina limenichanganya
 
Umeona mchango Wang ibra, kidogo jina limenichanganya
Cheki vizuri namba uliyotuma ndio hiyo kweli? Jina ni Ibrahim Masimba.. but hata mimi sijaona
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom