Riwaya: Nitakupata tu

Riwaya: Nitakupata tu

NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 047

Teddy ametoroka na mtoto na inasemekana wameelekea Arusha. Lakini tulipowasiliana na watu wetu kule hawakumuona Teddy popote pale licha ya kupekuwa viwanja vyote vya ndege sambamba na kuangaliwa kwa umakini kwa kila gari ambayo ilikuwa ikiingia arusha na kutoka. Hivyo basi Jimmy na Ben wameelekea huko kumtafuta Teddy ili wamuue ili wamchukue mtoto wako iwe chamba cha kukufanya wewe urudishe mzigo uliouchukua." Aliongea salha akimtizama masimba kwa umakini. Alitaka kugundua nini ambacho angekishuhudia machoni kwake. Lakini hakukutana na chochote kile, hakukiona alichokuwa anakitafuta. Licha ya masimba kutokushtuka kwa taarifa ile, lakini moyoni na kichwani hakuwa katika usawa. Hakuwa katika utimamu wa kiakili na hata kimwili. Alimuwaza france, alimuwaza mwanaye aliempenda sana. Hakutaka kukubali mwanawe kupotezwa. Alinhitaji mwanawe akiwa hai. Alimuhitaji france akiwa kwenye tabasamu lake alilolizoea. Lakini alipofikiria kuhusu Teddy kutoroka bado mwanamke huyu aliiyumbisha akili yake. Bado mwanamke huyu hakueleweka upi msimamo wake. Alifanya mauaji na usaliti wote sababu ya Kundi lao. Hata kuuawa kwa mama yake, Teddy alikuwa nyuma ya kifo cha mama yake. Lakini leo hii tena Teddy alikuwa akisakwa na Jimmy, teddy leo alikuwa ametoroka tena akiwa kwepa Jimmy na Kundi lake. Kwa nini amekimbia? Kipi kimemfanya akimbie Tena akiwa na france. Akaiona Hatari mbele yake endapo atamuacha Jimmy amfikie Teddy. Alitambua ungekuwa nwisho wake sambamba na mwanawe france. Hapo akaamua kufanya kitu. Akarudisha macho kwa Salha. Wakaangaliana kwa mara nyingine. Kila mmoja akisoma kilicho ndani ya macho ya Mwingine. Kila mmoja alijua yupo na nani. Licha ya salha kudanganya kuwa ni mfanyakazi wa kawaida haikuwa hivyo. Huyu alikuwa Jasusi. Alisomeka na Masimba alilitambua hilo. "Naelekea Arusha kumrudisha Teddy na France, nina kisasi na teddy na nitapenda kumuua kwa mikono yangu. Naomba tuondoke hapa nikakuache sehemu salama. Lakini kukuacha huko itabidi ufumbe na usiufumbue Mdomo wako. Ukifanya hivyo nilichomfanya mwamvita Muda mfupi uliopita ndio nitakachokifanya kwako." Alinguruma masimba huku akianza kutembea kuelekea Nje. Licha ya Masimba kutembea kuelekea nje, lakini Salha bado alikuwa amekaa. Alionyesha kupigwa na bumbuwazi. Maneno yaliyotamkwa na Masimba yalimuingia sawasawa. Kwamba mwamvita amekufa? Kwamba mwanamke yule katili ameuawa? Kilikuwa kitu kigumu kukiamini. Alijikuta akiwa kondoo mbele ya Masimba. Alimfuata kwa nyuma akihitaji kukijua kile alichokisia. Hata alipomkaribia Masimba bado aliilazimisha miguu yake kutembea. Akamuangalia Tena masimba. Lakini kabla hajaongea chochote simu yake ikaonyesha uhai. Kuna mtu alikuwa akimpigia. Akaitoa simu na Kuitizama. Jimmy,neno pekee lililosomeka Juu ya kioo. Akasita kisha kumuangalia Tena Masimba. Kuangaliwa kule akatambua kulikuwa kuna kitu. "Jimmy anapiga.!! Ilikuwa sauti iliyomvuta Masimba karibu na Salha. "Pokea, harafu muulize yuko wapi na wamefikia wapi." Ilikuwa amri kutoka kwa Masimba, amri ambayo ilitekelezwa muda ule ule.

********

Alikuwa juu ya kaburi la mama yake Masimba akilia kwa uchungu katika usiku ule. Moyo wake ulikuwa umepondekapondeka. Alikuwa akijuta na hata kulia kwa sauti. Hakuna baya ambalo alifanyiwa na huyu mama. Siku zote alimpenda kuliko hata mwanawe Masimba. Alikuwa akisuluhisha migogoro yao kwa upendo mkubwa. "Nisamehe mama yangu, bila ujinga wangu leo hii nisingekupoteza. Tamaa ya pesa imenifanya niusahau utu wako. Imenifanya nisahau mapenzi yangu kwako. Nikafanya kitu ambacho sasa nakiwaza. Mama nipo hapa nikishindwa kujua wapi nitakwenda. Masimba ananisaka aniue mama. Masimba anitafuta anilete huko, sina uwezo na ujasiri wa kusimama mbele yake kumuomba msamaha. Sina ujasiri hata wa kumuangalia Machoni. Mama nakisubiri kifo changu hapa hapa Juu ya kaburi lako. Nataka Risasi ya Masimba Inilipue nikiwa hapa. Nitamwambiaje mama na hata baba yangu? Vicky atanielewaje katika hili niliofanya? Ataniacha? Vipi mwanangu patra? Hapana Nastahili kufa." Yalikuwa maneno aliyotamka Teddy akiwa juu ya kaburi. Alikuwa Tanga badala ya Arusha. Alitambua asingeweza kufika arusha bila kutiwa nguvuni. Kitu alichoona ni kushinda juu ya kaburi ya mama yake Masimba. Alishinda hapo huku france akimuacha nyumbani kwao kibugumo Nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

*****
Alishuka Handeni Usiku wa Saa sita kwa Usafiri wa kukodi. Baada ya kushuka hapo akaongoza Moja kwa moja mpaka nyumbani kwao ambapo bado watu walikuwa wanalala Matanga. Aliwakuta wengi wa watu wakiwa wamelala huku wachache tu ndio waliokuwa wakiota moto. Aliwasalimia wachache waliokuwepo na kuanza kuongea nao. Kufika hapo akakutana na vilio kutoka nyumbani kwa mzee First wazo,. Hapo akagundua kuwa tayari taarifa za kifo cha Dee Plus zilikuwa zimefika hapo kijijini. Wakaongea mpaka asubuhi kulipokucha. Watu wakajiandaa kwa sababu ya kwenda kuchimba kaburi la kumhifadhi Dee plus. Wakiwa bado wanajiandaa wakalisikia yowe kutoka kwa mmoja wa watoto ambaye alipita karibu na makaburi. Watu waliokuwepo msibani wakageuka na kutizama huko. Wengine walishaanza kukimbia kuelekea kule wengine wakibeba silaha tayari kwa lolote. Masimba ndio aliyekuwa wa kwanza kufika pale makaburini. Macho yake yakatembea katika sekunde ile ile. Macho yake yakatua juu ya kaburi la mama yake. Akamuona mtu akiwa amelala juu akionyesha kudhoofika mwili. Hakushangazwa na kule kudhoofika, bali alishangazwa na mtu aliyejuu ya kaburi. Teddy alikuwa juu ya kaburi la mama yake. Kaburi la mwanamke ambaye alihusika katika kumuondoa duniani. Alikuwa amelala na alikuwa akionyesha kuchoka sana. Wakati huo watu wengine nao walikuwa wameshafika. Kila mmoja alikuwa akikiangalia kile kinachoendelea pale. Mwanamke wanayemjua alikuwa akilia, akilia juu ya kaburi la mama wa masimba. Kaka yake Masimba aitwaye Samwebondo ndiye aliyepiga hatua kuelekea pale kaburini. Dada zake masimba naye wakaungana naye kuelekea pale. Sekunde hii walikuwa wakimbeba Teddy akiendelea kulia. Licha ya ndugu wote kufanya hivyo lakini kwa Masimba haikuwa hivyo. Bado alisimama akimuangalia Teddy Hasira zikimchemka. Alitamani kuchomoa bastola yake na kumlipua. Alitamani kumuendea pale na kufanya lolote. Lakini hakuweza hilo, kwa kuwa macho ya watu yakaanza kumtizama na minong'ono kuanza taratibu. Watu walianza kuhoji katika hili. Walianza kuhoji ulipo utu wa masimba. Wakamlaumu tena na tena. Masimba hakuwasikiliza. Akaondoka pale akiwaza na kuwazua. Alitaka kumuua Teddy, hakutaka alione Juaa la kesho, lakini angemuuaje wakati tayari teddy alikuwa mikono mwa ndugu zake tena akiwa mwenyewe pasipo mtoto wake? Kwa nini hakuelekea arusha na kuamua kuja huku? Inamaana tokea majuzi alikuwa pale juu ya kaburi. Alijiuliza huku akijilazimisha kutembea kurudi nyumbani. Hapo akakutana na kitu kingine. Dada zake walikuwa wamembadili nguo na sasa walikuwa wakimpeleka bafuni kwa minajili ya kumuogesha. Hapo akatamani kuwaambia ukweli. Alitamani kupaza sauti lakini hakuweza. Hawakuweza kwa kuwa dada zake walimpenda na Hawakujua kama alikuwa nyuma ya kifo cha mama yao. LAITI WANGEJUAA!!@@@??? SIDHANI KAMA KUNGEKUWA NA HATA MMOJA ANGEMGUSA.

ITAENDELEA
 
MATESO YANGU

SEHEMU YA 024

Nikaliona lile ambalo sikulitarajia hapo mwanzo. Sikulitarajia kama lingetokea ndani ya Chumba kile. Sketi ya Rehema ilikuwa magotini, Ilikuwa ikishushwa taratibu huku jicho zuri legevu likinitizama. Jicho ambalo lilionekana kukosa usingizi kwa Muda mrefu sana. Sketi ikafika chini ya miguu na kuliacha umbo lake nusu likiwa nje. Paja nyeupe zilizonona zilikuwa zikionekana Waziwazi. Nikalimeza fundo la mate pale mkono wa Rehema ulipoishika Kufuli na kuanza kuishusha chini. Kuishusha huku akinitizama kwa jicho lake lile lile. Punde nguo ile ilikuwa chini, chini kabisa ya miguu yake. Macho yangu yakapokewa na nyasi ndogo mbichi mbichi zilizokuwa zikichipua. Hizi hazikuwa za bandia kama zile za uwanja wa Uhuru. Hizi zilikuwa ni nyasi asilia katika uwanja Asilia. Ulikuwa uwanja uliokuwa unavutia kwa kutizama, uwanja ambao kila ambaye angefanikiwa kuutizama alikuwa akiumezea mate. Punde nikamuona akikiondoa kile kishati na kumuacha kama alivyozaliwa. Alikuwa kama alivyokuja Duniani. Umbo lake tambu lilishahabiana na umbo la Mishy, hata Chuchu zake zilikuwa ndogo mfano wa Embe Ng'ongo. Jicho lake lilikuwa zuri kama lile la Trisar Brown ama Mishy wa Tabara. Lilikuwa limelegea kanakwamba hakuwa na uhai. Ibrah nikapigwa na butwaa nisijue nini nifanye. Nilikuwa nimezubaishwa na Uzuri wa Umbo la Rehema. Nikapiga hatua kumfuata pale aliposimama kisha nikamkumbatia. Ulikuwa mkumbatio wenye kuleta faraja ndani yake. Muda mfupi ulimi wangu ulikuwa ukitembea kwenye ncha ya Chuchu zake. Nilikuwa nikiilamba chuchu katika ufundi mtambuka. Mikono ilikuwa akishuka na kupanda katika kuitekenya nyonga. Nikamuona Rehema akishindwa kusimama, akaishiwa nguvu na kutamani kukaa chini.

Sikumpa hiyo nafasi, sikutaka kumfanya ahangaike, nilitaka kumuonyesha ufundi wa kumtoa machozi ya utamu. Bado ulimi wangu uliendelea kushambulia Chuchu za Rehema. Sasa nilikuwa nimeimeza chuchu moja na kuanza kuinyonya. Niliifanya kama mtoto afanyavyo. Punde nikausikia mguno kutoka kWa Rehema. Sikujali hilo, sikulisikia hilo, sasa nilikuwa nimemuinua na kwenda kumlaza katika kitanda kile. Alikuwa amelala kifudifudi akiuacha mgongo Juu. Ibrah nikaanza kukifanya kile ambacho kila mwanamke alihitaji kufanyiwa, nilikuwa nikiutembeza ulimi usawa wa shingo huku nikiufanya kama naupuliza. Kila nilichokuwa nikifanya nilikuwa nikimuona Rehema akipanda juu. Kila nilipokuwa napumua Shingoni na Hata Sikioni bado alikuwa akiweweseka. Alipoteza mawasiliano. Hakuwa anaelewa kile kinachoendelea. Hata nilipomgeuza Hakuwa na Habari. Hakuwa na taarifa kuwa nilikuwa nikitaka kuonja maji ya Chumvi. Nilipogusisha ulimi wangu kisimani nikamuona Rehema akishika mashuka na kuanza kucheza Sebene. Alikuwa akienda kulia na kushoto akifuatia mdundo wa Biti. Nami nilikuwa nikionja maji na wakati mwingine nilikuwa nikinywa kabisa.

Nilipomuona Rehema akinivuta ndipo nami nilipopanda na kuianza safari. Ilikuwa safari salama yenye kuburudisha. Safari ambayo Chombo changu kilipakiwa katika chombo kitulivu. Chombo ambacho kilikuwa kikinibana na kunisababishia joto kali sana. Tukacheka na kufurahi wote, tukashuka bonde kwa taratibu, tulikuwa tukiogopa Ajali, ajali ambayo ingetuharibia. Binti alikuwa akitatarikana kana kwamba kitanda kilikuwa kinasiafu. Alishuka kitandani na kulala chini ya sofa. Tulibadili kila aina ya mitindo. Mpaka Chombo kinafika bandari Ya Zanzibar kila mmoja alikuwa ameifurahia safari kwa kiwango kikubwa sana. Kila mmoja alikuwa alikuwa amelala pembeni akimuangalia mwenzake. ''ahsante'' ilikuwa sauti ya Rehema ambayo ilinifanya nigeuze Shingo kumtizama vizuri. Bado mwili wake ulikuwa Ukiniita, bado mwili wake ulikuwa ukivuta na kunishawishi. Ni kweli ukafanikiwa katika hilo. Muda mfupi baadae Tulikuwa katika safari ya pili. Hii ilikuwa safari ya taratibu katika kupeana nafasi ya kuonyesha ujuzi. Tulikuwa katika burudani timilifu. Kwa Mara Ya kwanza nilikuwa nikimsahau Sheila pamoja na Shamim. Nilihisi Huyu atakuwa mwanamke Wa Maisha Yangu. Macho yalilegea na kiuno alikilegeza. Alikwenda kushoto na hata kulia, alipanda juu na Kushusha. Ulikuwa Mchezo Mtamu, Mchezo ambao ulitufanya tukione kilele kwa pamoja. Nikaapa kuachana na Sheila, nilipanga hata Kuachana na Shamim. Nilitaka kutulia na Rehema Wangu. Sikutaka kumpoteza kwa ujinga wangu. Hakika sikujua. Kama Ningejua nisingejidanganya.
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 048

Hawakujua chochote kuhusu kuhusika kwa teddy katika kifo cha mama yao. Walimpenda Teddy kama wifi yao. Hawakujali hali ambayo alikuwa nayo Masimba. Masimba bado alikuwa amejiinamia mahali akifikiria. Hakuonyesha kujali katika kile ambacho kilikuwa kikiendelea. Alimpoteza Dee plus kwa sababu ya Teddy, kama sio Teddy kumsaliti leo hii mama yake mzazi asingekufa. Lakini usaliti wa teddy umesababisha madhara makubwa sana kwake. Leo hii teddy alikuwa mbele yake katika nyumba ya mwanamke yule yule aliyemuua? Alikuwa amepokewa kama malkia. Mwanamke aliyemuua mama yake alikuwa akifurahiwa na ndugu zake wote. Sasa alikuwa akienda kuogeshwa kama mwali ama mtu maalum. Moyo ukampasuka hasira zikiendelea kupanda. Muda huu alikuwa akijipapasa bastola yake. Ni jana tu aliachana na Dee katika aina ya kazi yao. Ikimpa Dee kazi ya kumtafuta Teddy.. lakini leo hii Dee alikuwa marehemu. Alikuwa amepigwa risasi zisizo na Idadi. Akatamani ainuke ili aondoke zake arudi dar es salaam, lakini angeondoka vipi bila kumzika Rafikiki yake? Kuliwaza hilo kulimfanya Masimba Atulie. Punde akawaona ndugu zake wakimfuata pale alipo wakiwa wameongozana na Teddy. Wamemshika huku na huko. Hilo hakulitegemea na Hata kuliwaza. Hilo hakuliamini na hakutaka iwe. Lakini ulishakuwa. Teddy alikuwa mbele ya miguu yake akiwa amepiga magoti akilia. Alikuwa katika kuuomba msamaha kwa kile kilichotokea. Ingawa asingeweza kurudisha uhai wa mama lakini bado aliliona kosa lake. Akaanguka miguu kwa Masimba akilia na kulia. Masimba bado alikuwa kimya akimtizama. Akimtizama teddy huku fundo kubwa likiwa kooni. Ni teddy huyu huyu aliyemuondoa Asteria, Mwamvua na Hata familia ya Asteria. Ni teddy aliyemleta Mwamvita kwao mpaka kumuua mama yake. Ni Teddy aliyewapiga watoto katika mapigo ambayo haya stahili. Teddy leo alikuwa miguuni mwake akagalagala. Teddy leo alikuwa akihitaji kusamehewa. Ni msamaha gani angeweza kutoa? Je akiutoa huu msamaha roho za watu waliouawa kwa kushiriki kwake zitarudi? Yalikuwa maswali yaliohitaji Majibu, yalikuwa maswali yaliohitaji ufumbuzi kwa wakati ule ule. Ni ufumbuzi gani angeupata pale kwa wakati ule? Hakujua!! Na kamwe asingejua. Alipoinua uso kutizama mbele yake, akakutana na macho ya ndugu zake yakimtizama katika namna ya kuumuuliza. "Hana mbwani hano, mbona hachikuelewa" (kuna nini hapa mbona hatuelewi).. Kila mmoja alikuwa akihitaji Majibu kutoka kwake. Angejibu nini wakati akijibu kutatokea jingine tena kubwa.

"Welewe chigambile ichindeni, mwanangwa kumtenda zeze? Aliuliza mjomba wake aitwae kilango almaarufu kwa Jina la kabanza. Akimaanisha kutaka kujua ukweli nini ambacho amemtenda Mtoto wa watu. Masimba hakuweza kujibu. Bado alikuwa akikumbuka tukio la mwamvita. Mwili wa Mama yake ulipotupwa juu baada kupigwa risasi. Mama anauma na mama anaumiza. Akainama tena kisha kumuangalia mjomba wake. Machozi yakashuka mpaka mashavuni. Masimba alikuwa akilia mbele ya ndugu zake. Wote walikuwa kimya wakiwatizama wapenzi hawa. Hawakuijua siri ambayo ilikuwa mioyoni mwao. Bado alikuwa akilia machozi. Punde mikono yake ilishuka na kushika mabega ya Teddy. Teddy akaacha kulia na kuinua uso kisha kumtizama Masimba. Macho yao yaliojaa machozi yakiangaliana kwa zaidi ya dakika mbili. "Mapenzi" ndio kitu kilichoonekana machoni mwao. Ndio kitu kilichozungumzwa katika macho yao. Punde walikuwa wakikumbatiana kwa nguvu kila mmoja akilia. Teddy ndiye aliyeonekana akilia na kujutia zaidi. Ndugu wakaungana nao katika kilio, kilio ambacho mara hii kikageuka na kuwa msiba. Wote walikuwa wakimkumbuka mama yao.

******

Walikuwa wawili tu chumbani wakitizamana. Safari hapakuonekana mapenzi machoni kwa huyu kijana wa kiume. Uso wake ulikuwa umekunjamana kwa hasira. Alikuwa akimtizama mpenzi wake kwa hasira. Bastola ilikuwa mkononi akimuangalia Teddy. "Kabla ya yote nahitaji kujua alipo mwanangu France. Aliongea Masimba huku macho yake yakimuangalia Teddy. "Yupo Nyumbani Toangoma. Nilimuacha kwa kuwa nilikuwa na maamuzi magumu."alijibu Teddy huku akimuangalia masimba zaidi na Zaidi. "Mpigie Vicky niongee na France, ole wako unidanganye nitakuua kwa mikono Yangu..." teddy hakujibu, alichokifanya nikuchukua Simu ya Masimba na kuingiza namba ya Vicky, kisha akaipeleka sikioni. Muda mfupi simu ilikuwa ikiita. "Hellow Mume mambo?" Alisikika sauti ya upande wa pili kutoka kwa Vicky ambaye ni mdogo wa Teddy. "Safi mke, naomba Kuongea na Mwanao mkubwa.." aliongea Masimba. "Yupi patra au nani? Akauliza Vicky huku akionyesha kushangaa. MASIMBA NA TEDDY wakatizamana. Haikuwa kawaida kwa vicky kutokumjua Mtoto mkubwa.

"Hapana sio Cleopatra, nataka kuzungumza na France." Alijibu masimba. Ukimya wa ghafla ukatokea upande wa pili. Mshangao na kengele za hatari zikagonga vichwani mwao. Ukimya wa ghafla wa Vicky uliwashangaza.

"Vicky bado upo hewani bado?." Akauliza Masimba. "Ndio nipo hewani mume. Lakini nimeshangaa kwa simu yako kumhitaji France. Wakati kuna mtu amekuja hapa akadai mmemtuma amchukue France awaletee? Aliongea Vicky huku naye akianza kuhisi hali kutokuwa sawa. Kengele ya Hatari ikalia. Pale pale Teddy akaichukua simu kisha kwa sauti ya kupagawa akasema. "Ni nani amekuja hapo nyumbani? Niambie Vicky!!" Huku vicky akionyesha kuchanganyikiwa akamjibu "alikuja rafiki yako yule wa kike akaniambia umemtuma mtoto..." jibu hilo likakifanya kichwa cha Teddy kufanyakazi kwa Haraka. "Mwamvita utanikoma nikikukamata." Aliongea teddy bila kujua kuwa mwamvita hakuwa hai. Alishasafirishwa kuzimu. "Mwamvita hawezi kufufuka kwenda kumchukua France. Huyu Atakuwa Salha. Mwamvita nilishaamuua na kilichokuwa kikifuata ni kifo chako." Alijibu Masimba akimuacha teddy kwenye mshangao. "Salha umemjuaje salha?" Akauliza teddy sasa akimuangalia Usoni kwa makini. "Hatuna muda wa kujibizana na kuukizana. Naamini unazijua njia zote wanazopitia watu hawa. Nimekupa hii kama nafasi ya Mwisho. Ukingengeuka na nikahisi chochote nitakuua Teddy. Naomba Ubaki hapa nyumbani. Sitaki uwaambie chochote. Nasikitika kuondoka nikiacha mazishi ya Dee plus. Lakini hakuna namna ngoja niwahi. Tutaonana Dar es salaam." Aliongea masimba huku akisimama na kuanza kupiga hatua. Teddy akamuwahi na kumkumbatia. Punde ndimi zikagusana. Nahitaji tuongozane masimba. Nahitaji kupambana kufidia damu yote nilioshiriki kuimwaga. Nitakupeleka kila ngome ninayoijua na tutafanya kile ambacho unakitaka." Akaongea Teddy huku akimuangalia Masimba. Hata masimba akamtizama. Safari ya Dar es salaam ikaanza huku masimba akiwa makini sana juu ya Teddy.

*******

Kilikuwa kikao kidogo kilichokuwa kikifanyika nje kidogo ya Jiji la Dar es salaam. Kilikuwa kikao kidogo kilichowakutanisha washirika wote wa biashara ya kulevya hapa nchini. Viongozi wa serikali, wabunge na maafisa na wakurugenzi wa mashirika mbalimbali ya kigeni. Ni kati ya watu waliokusanyika katika kikao hiki. Kila mmoja alikuwa kimya akitega sikio kusikia lolote kutoka kwa mwanamkakati wa kuingiza biashara hiyo bwana Jimmy Lambert. Kila mmoja alikuwa akimuangalia mwenyekiti wengi wakishangazwa na ule uonekanaji wake katika siku ya leo. Jimmy alikuwa mpole sana. Alikuwa amejiinamia akiitizama picha ya mwamvita. Picha ya mpiganaji wake alieuawa usiku uliopita. Akainua uso wake na kuwatizama wajumbe wenzake....
 
Hatimae Teddy arudishwa kundini kwa mtego
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom