Riwaya: Nitakupata tu

Riwaya: Nitakupata tu

NITAKUPATA TU

EPISODE NO 050

Mlinzi akaanguka chini huku akiwa ameushikilia upande wa kushoto wa kifua chake. Muda mfupi aliungana na mwamvita kwa safari ya kuzimu. Kwa kuwa bastola ilikuwa na kiwambo cha kuzuia mlio. (Silence )mlio ule haukusikika hata umbali wa hatua kumi. Teddy akaongoza kuelekea ndani ya Jumba lile. Alipoufikia mlango akausukuma, lakini akagundua ulikuwa umefungwa. Akajaribu tena bado ulionyesha kuwa ulikuwa umefungwa. Teddy akaingiza mkono mfukoni na kuchomoa funguo malaya. Akautia kwenye tundu la kitasa, taratibu mlango ukamtii. Akauvuta mguu wake na kuingia ndani taratibu. Punde alikuwa kwenye sebule pana iliyopambwa na vitu kibao. Akaangaza huku na huko lakini bado hakumuona mtu yoyote. Hilo likamuaminisha kuwa hapakuwa na mtu yoyote. Akapiga hatua na kuivuka sebule. Sasa alikuwa akielekea kwenye vyumba vya Jengo lile. Kupita chumba cha kwanza na chumba cha pili, masikio yake yakanasa sauti ya kumwagika kwa maji, maji kutoka kwenye mabafu. Akaubadili uelekeo ule, sasa alikuwa akielekea kule bafuni. Mdomo wa bastola ulikuwa mbele tayari kwa kutoa usafiri kwa mtu yoyote ambaye atakuwa kiherehere. Akavuka na kuufikia mlango wa bafuni. Mlango haukuwa umerudishwa. Ulikuwa waziwazi kabisa. Mdomo wa bastola uliotangulia ndio uliomgutusha mbunge yule na kutaka kukurupuka. Lakini alipoiona sura ya mtu aliyeikamata Bastola akatulia akimuangalia vile vile akiwa mtupu. Teddy naye hakuiona aibu ya kuiangalia ile Manati. Alimtizama huku bastola ikiendelea kuwa mbele. Teddy akaivuta hatua mpaka hatua mbili kutoka pale aliposimama Mbunge Yule. Akaunyoosha mkono mpaka kilipo kitu ya mbunge yule. Bastola ikagusa kwenye shina la mnazi. Mbunge yule hakuwa na kauli tena ya kuongea. Aongee nini wakati alikuwa akikitizama kifo. Kifo ambacho kilikuja kwa njia ya ghafla. Kidole kikavuta trigger na muda ule ule mlipuko mdogo ukasikika. Bastola ilikuwa amefanyakazi ya kuvitenganisha viungo vyote vya uzazi. Teddy akasonya huku akigeuka. Alikuwa tayari ametoa tiketi na hata usafiri wenyewe. Mbunge yule alikuwa njiani akielekea kuzimu muda ule. Teddy akarudi mpaka sehemu ya maktaba katika jumba lile. Hapo akaonekana akiangalia hiki na kuacha kile. Alipekuwa hili na kuliacha. Muda mfupi baadae akaonekana akichukua nyaraka fulani kabla ya kuondoka mle ndani na kurudi tena nyumbani. Mkononi alikuwa amebeba nyaraka zinazoonyesha kuwa ni muhimu. Alitembea kwa machale akiwa amejibadilisha. Huyu hakuwa Teddy yule. Huyu alikuwa teddy yule yule wa Syria na Teddy yule wa Russia. Alirudi katika uteddy wake. Alirudi katika fani aliyoipenda kuliko zote. Fani ambayo hapo mwanzo wazazi wake wakikosa kumuunga mkono kutokana na kumtaka Arudi Shule. Lakini teddy alilikataa hilo kwa kuwa alilipenda Jeshi. Alikwenda hivyo hivyo pasipo sapoti ya wazazi wake. MAMA yake alihitaji mtoto asome, na mtoto alilihitaji Jeshi. Alianza pale Ruvu kabla ya kuhamia kule Ifakara. Leo hii alikuwa amerudi akiwa Teddy. Teddy yule aliyeipenda damu na teddy yule ambaye kuua kwake kilikuwa kitu cha kawaida. Siku zote hakuiogopa Damu na Aliipenda Sana.

Sasa aliamua kurudi rasmi kumsaidia mpenzi wake. Aliamua kuutafuta ushahidi kwa njia ya kuua. Aliua kwanza baadae ndio anautafuta ushahidi. Kwake ilikuwa Risasi kwanza kusha kuhoji baadae. Kanuni ambayo hata Jeshi la polisi huwa wanatumia sana. Kukukamata kwanza, kisha kuhoji baadae. Hata Teddy alikuwa na maamuzi hayo. Alitaka kuua kwanza kisha maswali baadae. Alitaka kumuonyesha masimba kuwa hayupo kwenye mkumbo kama mwanzo. Alitaka kumuonyesha kuwa anajua kona zote na mienendo yote ya watu anaopambana nao. Hakuna kinjia wala kichochoro ambacho hakukijua katika biashara ile. Baada kummaliza mbunge yule na kuchukua ushahidi ambao alidhani utamsaidia. Teddy aliondoka pale akiwaza kurudi nyumbani, lakini mawazo yake ya kurudi huko aliyakatisha baada ya kumuwaza mkurugenzi mmoja wa shirika moja la kigeni ambaye alikuwa ni Mshirika katika biashara hiyo. Huyu alikuwa mtu wa kwanza kumrubuni na kumuingiza katika ushirika wa biashara hiyo kwa mara ya kwanza. Aliona afuate huyu katika kazi yake ya kuwaondosha. Ingawa kulikuwa na ugumu lakini Teddy hakuogopa hilo.

*****

Alishuka Ofisi ya waziri mkuu na kupokewa na maafisa usalama wa Ikulu ambao hawakuongea naye sana zaidi ya kumruhusu aingie katika ofisi ile. Kwa kuwa alitoa maagizo ya kuwakuta watu watatu mle ndani, ni kweli aliwakuta watu wale ambao alikuwa ni mkuu wa Idara ya Mawasiliano Ofisi ya Waziri Mkuu. Katibu Binafsi wa Waziri. Sambamba na Waziri mwenye zamana wa wizara ile. Baada ya kuachana na wana usalama masimba aliingia ofisini na kitendo bila kuchelewa akamuita mkurugenzi wa Mawasiliano. Alikuwa mwanamama wa makamo, mwanamama anayekadiliwa kuwa na Umri wa Miaka 55. Alikuwa mwanamke mwembamba mwenye mvi kidogo kichwani. Huyu aliitwa Nina Mndeme. Alikuwa ni Mwanamke aliyehudumu katika Ofisi hiyo kwa takribani Miaka kumi na Tano. Alikuwa ni mwanamke wa kipare, mcheshi na mwenye bashasha kubwa. Aliingia katika chumba kile na kukutana na kijana huyu ambayr kwa kumtizama tu, akajua walikuwa ni vijana wa Mzee Godliving Kimaro.

"Shikamoo Mama!!" Alisalimia masimba akimuangalia mwanamama yule.

"Marahaba, hujambo baba..? Aliitikia kisha kuuliza. "Sijambo Mama.. nimekuja hapa kuhojiana na wewe katika mambo fulani fulani ambayo yanahusiana na kifo cha mzee hapa ofisi." Aliongea Masimba na kumkazia macho yule mama akihisi labda angekutana na Mshangao wowote, lakini haikuwa hivyo. Mwanamama yule alikuwa akimuangalia Masimba huku tabasamu likichanua mdomoni. Tabasamu ambalo halikuonyesha chochote kile. Yaani halikuwa na Kebehi. "Nipo tayari kutoa ushirikiano kwako ikiwa kila kitu kitakuwa ndani ya mamlaka yangu." Alijibu mama yule. Masimba akamuangalia tena kwa mara nyingine. "Mama huyu unayeongea naye hapa ni kama rais, nina baraka zote mpaka kuwa hapa. Nataka unijibu kila kitu hata kama hakipo kwenye mamlaka yako. Kwa kuwa hata mimi nina mamlaka ya kukupeleka kuzimu endapo utanificha chochote." Akaongea Masimba, safari hii akiuondoa ule ucheshi wake na kuivaa sura ya kazi. Licha ya kubadilika huko na hata kauli yake. Bado mwanamke yule aliendelea kutabasamu pasipo kuwa na wasiwasi. "Nataka kujua mawasiliano ya Hayati. Simu alizokuwa akipigiwa, alizopiga, ujumbe mfupi wa maneno na hata barua pepe. Pia nataka kujua mawasiliano yake binafsi sambamba na Simu yake ambayo inasemekana ilipouawa haikuwepo. Aliongea Masimba huku akimuangalia mwanamama yule. Bado tabasamu lilitamalaki usoni mwake. Hata kabla hajajibu chochote, mwanamama yule akainuka kitini na kuelekea kwenye meza kubwa ambayo ndani yake kulikuwa na makablasha mengi. Akavuta moja na kurudi mpaka pale kitini na kumkabidhi Masimba. "Mawasiliano yote aliyokuwa akiyafanya marehemu utayakuta humo. Lakini kuhusu simu yake hapo ndipo kidogo pana utata. Kwani baaada ya kutangazwa kifo chake tu, wakaja watu fulani ambao walikuwa marafiki wa mheshimiwa na kuiomba wakisema kuwa ilikuwa ikihitajika ofisini kwa chief." Alijibu Mama yule huku akimuangalia masimba safari akiwa sio mtu wa tabasamu. Kengele ya hatari Ikalia kichwani kwake. Hapakuwa na watu waliotumwa na mkurugenzi wa idara kuichukua simu hiyo. Hapa lazima kuna unamna. Hapa lazima kuna siri kubwa imetaka kufichwa." Unaweza kuwakumbuka watu waliokuja kuchukua hiyo simu?" Akauliza Masimba safari hii akionekana ni mwenye mawazo. Yule mama hakukurupuka Kujibu.. alifikiria kwa muda, mara akainuka tena na kuelekea sehemu tofauti. Safari hii akimuita Masimba waingie wote kwenye chumba fulani ndani ya Ofisi ile. Masimba akainuka huku mkono wake mwepesi ukicheZa karibu na sehemu Muhimu alipoihifadhi bastola yake. Akavuta hatua kisha kuingia ndani. Hapo akapokewa na mitambo mingi sana. Hapo akagundua alikuwa chumba cha kuongozea camera za Usalama mle ndani. Akasogea karibu na mama yule ambaye alikuwa akihangaika kufungua kitu fulani. Punde chumba kizima kikawa katika mwanga fulani baada ya screen kadhaa kuwaka. Baada ya mama yule kuwasha, akabonyeza sehemu Fulani, watu wawili wakaonekana wakiingia ndani ya Ofisi ya waziri mkuu. Masimba akamuomba yule mama awavute kwa karibu. Mama akafanya hivyo.. Punde Sura za watu wale zikasogea na kusogea. Macho ya Masimba Hayakuweza kuamini kile alichokuwa akikiona. Mbele ya kioo kulikuwa na sura za watu wawili anaowafahamu sana.
 
Yaweza kuwa ndiyo wanaenda kuuawa na Teddy sijui masimba atafanyaje ikiwa ndivyo
 
Teddy Ndio anafanya unyama tu anataka kulilinda penzi lake kwa gharama yeyote ili amfurahishe Masimba kumbe anatoa watu muhimu kwenye mapambano.
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA O51

*******

Zilikuwa sura za watu ambao aliwafahamu kabisa. Walikuwa watu kutoka kikosi maalum cha kuwalinda viongozi. Hawa huendeshwa ama kuagizwa na Rais, makamu, waziri mkuu sambamba na mkurugezi wa idara ya ujasusi. Hawa wawili walikuwa vijana wale ambao walimkanata na kumpeleka kule kuzimu. Lakini leo hii wameingia ofisi ya waziri mkuu na kuichukua simu ambayo ingeweza kumsaidia yeye kwenye kazi yake. Hilo hakuwa amelitegemea kwa kuwa hapo mwanzo alidhani Simu ipo mikononi mwa Wana usalama. Akaziangalia zile sura kwa muda kisha akageuka tena kumuangalia yule Mama. Akili yake haikuwa pale kabisa. Bado aliuona utata katika kuupata ushahidi wa kuuthitishia ulimwengu kuhusu ubaya wa waziri. "Kuna kingine Mama unachojua ukiondoa hivi vichache.? aliuliza Masimba. Mama yule hakumjibu kwa maneno bali akaondoka pale na kuingia katika kichumba kingine. Akatoka na mfano wa bahasha na kumkabidhi masimba. "unachokitafuta kuhusu waziri vyote viko humo ndani. Humo ndio utamjua waziri. Nimekupa hiyo bahasha nikiwa najua nina hatarisha maisha yangu. Lakini siogopi, hata nikifa leo najua nimekufa sababu ya Nchi yangu." Aliongea mama yule huku tabasamu lake likiyeyuka Usoni. Sasa alikuwa katika Uso wa Hofu. Hofu juu ya kifo, hofu juu ya kutoa siri ambayo hakutakiwa kuijua ama kuitoa. Masimba akamuangalia mwanamke huyu kwa muda mrefu. Alimuona ni kama malaika aliyetumwa kwake. "Mama naitwa Masimba, nadhani ushawahi kunisoma mahala ama kunisikia sehemu nikitajwa. Kama nikiwa hai hakuna ambaye atakugusa." Aliongea masimba akimpiga piga yule mama mgongoni. Mama aliganda kwa mshangao, mshangao wa kutokuamini maneno kutoka kwa kijana yule. Masimba ni Huyu? Anawezekana vipi kuwa huyu? Mbona hafanani na sifa anazopewa? Hapana huyu sio masimba. Huyu ni muongo..!! Yalikuwa maswali yalitiririka kichwani kwake. Hakuamini kuwa mtu yule ni masimba. Ni hapo akataka kurudisha macho kumuangalia tena Usoni. Lakini akaendelea kupigwa na butwaa baada ya kujikuta yuko peke yake. Masimba hakuwepo lakini kilichomshangaza Zaidi milango Ilikuwa bado imefungwa. Atakuwa amepitia wapi? Alijiuliza mama yule akiangaza huku na kule. Bado hakumuona Masimba. Bado hakumuona kijana huyu aliyekuwa akizisikia sifa zake. Akatoka ofisini mle haraka hadi pale alipowaacha wenzake. Akawakuta wamejiinamia wakionyesha kuanza kuchoka . "Amepita hapa, lilikuwa swali la kwanza Bi Nina baada ya kutokea pale. "Nani? Wenzake wote wakamuuliza wakimtizama kwa mshangao. "Yule kijana niliyekuwa naye ndani." Akajibu Huku akipepesa macho yake huku na kule. "Hatuja muona mtu hapa." Nao wakajibu wakitizamana.

*****

Wakati kule ofisi ya waziri mkuu wakimtafuta masimba, yeye ndio kwanza alikuwa anavuka Hotel ya kilimanjaro akielekea posta. Alikuwa akitembea kwa miguu kwa umakini wa hali ya juu. Aliijua sasa vita ndio ilikuwa imeiva. Alitambua wakati huo alikuwa akisakwa na kutafutwa. Lakini hilo halikumtisha wala kumuogopesha. Alijua kucheza na watu hawa, na ukitaka kucheza nao ni lazima uwe muwazi na usiwaogope. Hilo ndilo lililomfanya atembea mpaka ilipo benki ya taifa ya biashara. Wakati anaukaribia mlango akawasikia polisi wawili wakiongea kwa sauti ya chini kuhusu tukio la kuuawa kwa mbunge. Ingawa walikuwa wakiongea kwa sauti ya chini lakini kwenye masikio ya Masimba ilikuwa ni sauti kubwa. Moyoni akajua tayari teddy ameshaianza kazi. Akatawapita huku akitabasamu akiuendea mlango wa kuingia ndani ya Jengo lile lenye Benki. Baada ya masimba kuingia, haikupita dakika gari moja alionekana ikipaki pembezoni mwa Benki ile. Kisha wakashuka wasichana wawili na mvulana mmoja sambamba na mtoto wa kiume mwenye umri wa Miaka Saba. Baada ya kushuka kwa wanawake wale, wakaangaza kidogo kisha akaonekana yule mwenye mtoto wa kiume akiuendea mlango Huku wale wawili wakionyesha kumsubiri. Msichana yule aliingia ndani kisha kuchukua karatasi ya kujaza tayari kwa kutoa pesa. Lakini wakati akijazajaza ile karatasi alionekana akigeuka huku na huko katika aina fulani ambayo kama umtu wa kawaida usingeweza kugundua.

Baada ya masimba kuondoka pale Ofisi ya waziri mkuu, alijua kabisa kuwa lazima alikuwa akifuatiliwa na watu mahali fulani. Hakuwa na wazo la kuingia pale Benki, lakini ilikuhakikisha hisia zake kama ni za kweli ndipo alipoamua kuingia hapo benki. Na hata alipoingia alipanda mpaka ghorofa ya tatu sehemu ambayo ilikuwa na chumba cha kuongozea Camera za usalama ndani ya Jengo lile. Akajitambulisha kisha kuomba kuangalia gari zinazoingia sambamba na watu. Wataalam wakamkaribisha. Ni hapo alipoishuhudia gari ile ikiegeshwa kisha kushuka kw watu watatu sambamba na mtoto mdogo wa kiume. Mwanzo walitaka kumpoteza kutokana na kutowatilia mashaka. Lakini kuingia ndani ya benki kwa mmoja kati ya watu wale walioingia sambamba na mtoto mdogo, kuliyafanya maamuzi yake kubadilika ghafla. Uangaliaji na ugeukaji wa mwanamke yule ilikuwa ni majibu tosha kwamba aliyeingia pale licha ya kuwa na mtoto mdogo, alikuwa mmoja kati yao. Alikuwa mtu wa fani kama yake. Yaani alikuwa ni Shushushu. Akavutiwa na hilo. Macho yake yakaendelea kumtizama mwanadada huyu katika namna ya mshangao. Jimmy alikuwa na watu wangapi nyuma ya biashara hii? Swali hilo likamfanya amkumbuke mwandani wake Teddy. Akamtafuta katika namba yake ya kifucho. Licha ya simu kusikika kuita lakini haikupokewa. Akapiga tena na tena lakini hali ilikuwa ni vile vile. Hakuhisi chochote kile katika hilo. Bali aliamini Teddy alikuwa sehemu akifanya kitu. Akageuza macho kwa tetere huyu, tetere aliyekuja na kifaranga chake. Akaiona hamu na kiu, kiu ambayo ilihitaji glass ama kikombe cha maji katika wakati huu. Huyu alikuwa masimba na alikuwa jasusi. Bado alipendezwa na ule utizamaji na hata uangaliaji wa watu wale. Sasa akaamua kuinuka akiondoka katika chumba kile. Akashuka ngazi mpaka chini kabisa sehemu ya wateja. Hapo akajifanya kuongea na watu wawili wa tatu. Akaiendea karatasi kisha kuijaza na kuelekea kwenye foleni. Sasa alikuwa amesimama nyuma ya msichana yule mrembo. Walitenganishwa kwa umbali wa nusu Hatua tu. Walikuwa wakipumuliana na kila mmoja kuisikia pumzi ya mwenzake. Hilo likaileta Raha katika roho ya masimba. Raha ambayo ilikuja pale yule mtoto mdogo alipokuja na kumkumbatia miguu. Hilo akalipenda. Mikono yake ikashuka na kumuinua mtoto na kumbeba kwa mikono yake. Sasa walikuwa wakicheza na kutaniana katoto kale. Katoto ambako kalitokea kumzoea kabakwamba kalishawahi kumuona mahala fulani. Hapo ndipo alipomuona mwanadada yule akitamani kugeuka. Alitaka kumuangalia masimba, wakati mwingine mikono yake ilikuwa akienda uelekeo ambao masimba alikuwa akiu0na. Zamu ikatembea hatimaye ikafika zamu ya msichana yule. Akasogea kwa mwendo wake wa madawa. Alijikaza asionekane kama anatetemeka, lakini hilo aliliona machoni mwake. Baada ya binti kuhudumiwa na kumaliza shida yake ndipo alipogeuka ili kumchukua mtoto. Wakakutanisha macho yao, wakaangaliana na kuangaliana. Wakajuana na kutambuana. "Nenda kwa mama. Mwambie mama tutaonana siku nyingine. Nitamtafuta kwa muda wangu." Aliongea masimba akimshusha mtoto ili kumruhusu aende kwa mama yake.

*******

Kama lilivyoeneo lote la Oystebay mchana huwa kimya sana. Hata leo hii lilikuwa kimya sana kutokana na wakazi wengi wanaoishi eneo hilo kuwa makazini ama wengine kuwa ndani ya majumba yao. Teddy alikuwa mtu pekee ambaye alionekana akitembea katika barabara moja yenye utulivu. Alionekana kutulia sana katika utembeaji wake. Macho yake madogo hayakuacha kutizama kila upande katika namna impendezayo mtu yoyote yule. Hakuuonyesha wasiwasi na wala hakuonyesha kwamba alikuwa akikifuata kitu. Alitulia na kutulia. Alikuwa njiani kupeleka tiketi ya kifo kwa mkurugenzi fulani wa Shirika la kigeni. Muda wote alikuwa akitabasamu. Na hata pale alipolifikia geti la jumba analoishi mkurugenzi yule akalakiwa na mlinzi wake. Na kwakuwa walikuwa wakifahamiana, waliongea maneno mawili matatu, kisha akalisukuma geti na kuingia ndani. Mlinzi hakujua nini ambacho kinaendelea. Akamfuata Teddy kwa Nyuma. Lakini hatua yake ya tatu akahisi kitu kikipenya kifuani. Ulikuwa kama ubaridi fulani hivi. Lakini punde akaelemewa na kuupiga mweleka. Damu zilikuwa zikishuka kifuani. Teddy hakugeuka nyuma, alikuwa akitembea kuingia ndani ya jumba. Nyuma akiiacha maiti ya mlinzi yule ikiwa imelala pasipokuwepo na Uhai. Baada ya kuufikia mlango wa kuingilia ndani ya Jumba lile, akaibonyeza kengele ya mlangoni. Zilipita sekunde kumi bila mlango kufunguliwa. Akausukuma mlango kujaribu kama uko wazi. Naam! Mlango ulikuwa wazi na mbaya zaidi alipokelewa na dimbwi la damu iliyotapakaa pale sebuleni. Vitu vilikuwa vimetupwa ovyo kuonyesha kwamba kulikuwa na vurugu zilizofanyika. Teddy akaingia sasa akiwa tayari kwa chochote. Akaufunga mlango kwa ndani sasa akiitizama ile damu. Bado ilikuwa mbichi kabisa kuonyesha aliyefanya tukio hilo amelifanya katika muda ule. Lakini mpaka muda ule hakujua nani ambaye aliuawa katika damu ile iliyosambaa. Teddy akaongeza umakini zaidi na zaidi. Hatua kumi mbele juu ya ngazi akaukuta mwili wa mzungu yule ukiwa umelala kifudifudi huku KISU KIKUBWA KIKIWA KIMESIMAMA KATIKATI YA MGONGO.

TEDDY AKAPATWA NA BUMBUWAZI. Nani huyu amefanya hivi? Ni swali pekee alilojiuliza ambalo hakupata JIBU KWA MUDA ULE.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom