Riwaya: Nitakupata tu

Riwaya: Nitakupata tu

NITAKUPA TU

SEHEMU YA 044

Punde akamuona Mwamvita Akiingia tena akiwa mtupu. Alikuwa kama alivyozaliwa. Hilo halikumfanya masimba ashtuke. Bado alitulia huku bastola yake aina ya Revolver colt 48 ikiwa mkononi. Akamuacha mwamvita aingie kwanza. Na alipohakikisha ameingia Masimba akaufunga mlango kwa ndani. Mwamvita hakukitegemea kitendo hicho. Kwani baada ya kuusikia mlango ukifungwa akageuka akiwa mtupu vile vile. Akakutana na Mdomo wa bastola ukimtizama. Alikuwa akiangalia na masimba. Alikuwa akiangaliana na mtu ambaye alijua na kuhisi labda alikuwa Tanga kwenye mzima. Masimba hakuongea wala hakuwa anafanya chovhote. Bado alimuangalia Mwamvita kwa utulivu huku macho yake yakicheza pande zote. Kidole kikashuka taratibu kwenye kitufe cha kufyatulia Risasi. Rukia alikuwa akitokwa jasho jingi, alikuwa akikiogopa kifo. Akatamani kuongea kitu lakini akashindwa. Punde risasi ya kwanza akafyatuka na kutua kwenye kifua cha mwamvita. Risasi ya pili ikatua kichwani na kukifumua kichwa cha Mwamvita. Risasi ya tatu na nne zilitua kwenye matiti yake yote. Kila ilipokuwa akiifyatua risasi alikuwa akikumbuka kifo cha mama yake. Alikuwa akipiga risasi kwa Hasira, mwili mzima wa mwamvita ulikuwa umetapakaa damu. "Wasalimie kuzimu.. waambie bado naendelea kuwakusanya wote tayari kwa kuwapeleka huko." Aliongea Masimba huku akiuangalia mwili wa mwamvita. Baada ya kuhakikisha mwamvita amekwishakukata roho akauacha mwili pale pale kitandani kisha yeye akatoka Nje kupitia pale pale Dirishani. Safari hii aliamua kurudi Sinza kumekucha tayari kukijua kile ambacho kinaendelea ndani ya Saloon ile kilichosababisha mpaka Teja yule kuuawa. Alifanikiwa kutoka pasipokuonekana. Akaanza kuutafuta usafiri katika eneo lile ambalo bado hakujua ni wapi. Alitembea usiku usiku pasipokupata usafiri mpaka karibu na kijimji fulani Hivi. Hapo akafanikiwa kuiona pikipiki ambayo ilikuwa akipita. Alichokifanya ni kuisimamisha kisha kuwambia Dereva wapi anapoelekea. "Duh Bro mbona Huku ni Mbali sana na Sinza!! Alishangaa Dereva yule huku akianza kuonyesha wasiwasi Juu ya Masimba. Ndio kwanza masimba alikuwa akishtuka kwamba kumbe hakuwa ndani ya Jiji. "Kwani hapa ni wapi ndugu Yangu? Hatimaye Masimba akauliza huku akitabasamy ilikumtoa hofu kijana yule. "Hapa ni Bagamoyo brother, kwani unatokea wapi? Akajibu kijana yule kisha kuuliza tena.

Ikabidi masimba adanganye ili kupata usafiri wa kumrudisha jijini Dar es salaam. Hakutaka kuchelewa kwa kuwa bado kazi ilikuwa ngumu. Bado alikuwa na mission ngumu sana katika usiku. Usiku wa malipo ya damu ya watu wasio na hatia. Alitamani sana kuwamaliza wote kwa usiku ule ili aanze kumtafuta Yule Malaya Teddy. Alitaka kumuua mwisho kabisa. Hapo ndipo alipoona umuhimu wa kumdanganya kijana huyu. Uongo ambao ulimlainisha kijana na kukubali kumbeba Masimba kumpeleka Jiji Dar es salaam. Pikipiki ikaendeshwa usiku kwa usiku kwa mwendo wa kutisha na kuogopesha. Ilikuwa ni lazima aimalize mission katika muda wa masaa mawili yaliobaki, kwani saa yake ya mkononi ilikuwa ikimwambia ilikuwa saa saba na nusu usiku. Wakati wanaikaribia Bunju wakaiona gari ikija kwa mbele yao. Dereva akaupunguza mwendo kwa kuogopa kukamatwa. Masimba alimsisitiza aendelee kuendesha na Asiogope. Dereva akatii na kuanza kuendesha. Mbele kidogo kuikaribie ile gari wakapigwa mkono. Masimba akamwambia kijana yule asimame na Asiogope chochote. Kijana yule akasimamisha pikipiki na kutulia. Punde wakawaona watu watano wenye makoti makubwa wakisogea. Mkono wa Masimba Ukashuka taratibu alipoihifadhi bastola. Lakini watu wale waliposogea sans akagundua kwamba ni Askari. Akautoa mkono kisha akashuka. Polisi nao Wakawasogelea mpaka pale.

"Naomba Leseni yako ya udereva." Polisi mmoja akaamuru. Dereva yule hakuwa na leseni ya udereva. Baada ya Masimba kuona dereva wake ana hangaika. Akasogea karibu na kumuita askari mmoja pembeni. Askari yule akasogea kwa umakini sana huku SMG ikiwa mkononi. Kumfikia masimba tu akapewa kitanbulisho kimoja kati ya vingi alivyonavyo masimba. Baada ya kukipokea na kukiangalia, askari yule akakamaa kwa Saluti. Kitambulisho kikarudishwa kwa mwenyewe kisha wakaruhusiwa waendelee na Safari yao. Askari wote walikuwa wakintizama Masimba kwa mshangao. Hawakuwahi kumuona Zaidi ya kumsikia. Hawakuwahi kumuona Zaidi Ya kuona na kusoma sifa zake. Wakaendelea kumuangalia mpaka anatokomea. Hawakuwa wameamini na licha ya kutokuamini macho yao lakini walifarijika sana kumuoba mtu huyu.

*********

Kama ilivyo kwa maeneo mengi ya Jiji la dar es salaam kutokukosa watu hata iwe usiku wa maneno, ndio hali ambayo aliikuta Masimba Baada ya kufika hapo. Bado madada poa walikuwa kwenye biashara za kuuza miili yao. Mateja wengi bado walikuwa barabarani wakipiga debe na hata usafiri wa kukupeleka popote bado ulikuwa ni wakumwaga. Alishuka kumekucha na kumlipa dereva wa pikipiki pesa yake. Basda ya hapo akamwambia anaweza kurudi na asiwe na wasiwasi. Baada ya kuachana na dereva yule, masimba akatembea kama mtu wa kawaida mpaka nyuma ya Jengo ambalo kwa mbele ndio kulikuwa na Ile flemu yenye saloon. Cha ajabu lilikuwa jengo kubwa sana. Jengo ambalo lilikuwa na vyumba vingi sana. Na kingine kilichokuwa kikimshangaza ni miguno ya watu wanaofanya mapenzi kila pale alipokuwa anasogea. Hilo likampa shaka na kuamini labda jumba hili lilikuwa na danguro ama ni gesti bubu. Akaendelea kutembea na ukuta wa jengo lile mpaka alipofika mbeli kidogo ndio akauona mlango wa kuingilia. Kuuona mlangoni huo kuliendana na kuwaona walinzi watatu waliokuwa wakizunguka hapo, mikononi wakiwa na Bunduki kubwa. Kuwaona walinzi wale kukampa picha halisi kuwa sehemu ile haikuwa gesti wala danguro bali kulikuwa kukifanyika Biashara nyingine zaidi, tena biashara kubwa na ya hatari. Akaongeza umakini safari hii akiamua kupambana kwa Mikono. Akatafuta njia nzuri ya kuwakabili walinzi wale. Akaendelea kuwatizama kama atawaona walinzi wengine, lakini aligundua walikuwa walewale watatu. Muda huu alikuwa amehama pale na kuhamia huku. Alitaka kuwazunguka na kuwatokea kwa nyuma. Aliwaangalia kwa hatua zao na ukaaji wao. Akahamisha macho kwa kila mmoja aliyekuwa pale. Wote walikuwa wamesimama sehemu moja wakiongea. Alikuwa na uwezo wa kuwachapa Risasi wote lakini hilo akaliacha baada ya kuyaona mazingira. Akatembea na giza mpaka karibu kabisa na walinzi wale. Sekunde hii alikuwa akisogea kwa karibu zaidi. Ulikuwa ni muda wa kuwaonyesha kwa nini Aliaminiwa na Taifa. Akawatokea pale pale kwa kushtukiza. Yaani sekunde hii walikuwa wenyewe wakiongea, lakini sekunde ya pili walijikuta wakiwa wanne. Alikuwa ameongezeka mtu mmoja katikati yao. Mtu ambaye aliwashangaza na hata kuwafanya wababaike. Haiwezekani muda huu waongee watatu, harafu sekunde ile ile aongezeke wa nne. Mikono yao ikataka kushuka kwenye tufe la kuachia Risasi. Ni wakati huo kila mmoja alikuwa akiugulia maumivu. Yalikuwa mapigo yaliompigwa katika namna ambayo hakuna ambaye aliiona. Kila mmoja alikuwa ikigugumia kwa maumivu huku akishika kwenye korodani. Hakutaka kuwapa nafasi ya kujiuliza. Lakini wakati akijiandaa mmoja akarusha teke lakini likapita hewani baada ya kukwepwa kwa ustadi. Akarusha tena ngumi tano mfululizo lakini zilipita hewani. Safari hii akakutana na teke la Taya. Akajikuta mlinzi yule akiisalimia sakafu. Wakati huo walinzi wengine walikuwa wamekaa sawa. Yakafuata mapigano yaliochukua dakika mbili tu. Walinzi wote walikuwa chini wakiwa hawana uhai.

Akawaacha chini wakiwa wamelaliana. Sasa akawa anaingia ndani ya jengo lile kwa kupitia mlango wa ule ule. Bado miguno ya mapenzi ilikuwa ikisikika. Bado malalamiko ya mahaba yalikuwa yakitamalaki katika ngoma za masikio yake. Hapo akahamisha mawazo yake kwa Teddy, alimkumbuka Teddy kwa mengi. Alikuwa msichana wa kipare lakini alikuwa akiyajua mapenzi kama mzaramo ama mngoni. Alikuwa akijua kuutumia mwili wake mwembamba kwa utulivu na ufundi mkubwa. Ukimuona akiwa kwenye uwanja wa fundi seremala ungehisi labda alitokea Tanga yalikozaliwa mapenzi. Akapita akiyalazimisha masikio yake yatii kile ambacho alikwenda kukitenda. Akalifungua geti taratibu na kuchungulia kwa ndani, hapo akakutana na giza totoro. Akalifungua zaidi na zaidi kisha kujipenyeza ndani. Bado utulivu haukuwepo, bado miguno iliendelea. Akatembea sambamba na ukuta mpaka karibu kabisa na kibanda ambacho kilionyesha kilikuwa ni cha walinzi. Akatulia hapo akaangalia kila kona kwa chati. Kwa kuwa alikuwa amezoea giza, kwa kuwa macho yake yalizoea hali hiyo. Akafanikiwa kuwaona watu waanne katika sehemu tofauti. Licha ya uwepo wa watu wale, lakini hawakuonyesha kama walimuona Masimba. Hilo likamfanya masimba asonge mpaka karibu na mlango wa kuingilia ndani. Kufika hapo akaisikia minong'ono ikitokea ndani. Masimba akachomoa bastola kisha kuiweka Tayari. Bado minong'ono iliebdelea tena na tena. Punde akahisi ukimya lakini ukimya huo haukudumu sana, kwani Ndani ya Sekunde kumi miguno ikaanza kusikika kutoka ndani...

ITAENDELEA
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 045

Ukimya ukachukua nafasi maeneo yale. Hakuwa akisikia tena ile minong'ono. Akausogelea mlango katika aina fulani ya ukimya. Hata alipoufikia mlango bado hapakuwa na kizuizi chochote. Masimba akajaribu kutizama huku na huko, lakini bado hapakuwa na kizuizi. Bado hapakuwa na mtu. Mkono wake ukashika kitasa na kukizungusha, mlango ukamtii kama mfano wa mbwa anapomtii chatu. Bastola ilikuwa imetangulia Mbele tayari kumuondoa mtu yoyote. Akaufungua zaidi kisha kuingia. Alipoingia ndani alipokewa na ukimya tena. Kuingia kwake tu hata ile miguno ikapotea. Akaikamata bastola zaidi na zaidi. Kidole bado kilisubiri kuifanya kazi yake. Kazi ya kutoa tiketi na hata usafiri. Usafiri wa kuwapeleka watu kuzimu. Alitaka wakapumzike sambamba na mama yake na hata Dee. Alitaka wakajibu mashtaka yake mbele ya Asteria na Familia yake. Kuingia hapo akapokewa na harufu ya mipira ya kiume. Harufu ya condom ilikuwa imetawala katika nyumba ile. Akaongeza hatua mbele kuwatafuta wasafiri. Akaipita sebule bila kukutana na kizuizi chochote. Aliposogea mbele akasikia vishindo vya mtu vikionyesha mtu kusogea kule alipo. Punde akamuona mwanamume akitokea katika giza lile. Giza ambalo alishindwa kutambua kwa nini limeachwa kutawala pale ndani. Mwanaume yule akatembea na kupita karibu na Masimba bila kumuona. Masimba akamuacha apite, alivyopita akamtokea kwa nyuma na kumkata karate ya Shingo. Mtu yule akaanguka kama mzigo. Baada ya kuhakikisha mtu yule hayupo hai, akamsachi mifukoni. Akamkuta na Bastola mbili sambamba na vitamburisho kadhas. Vyote akavichukua na kuvisunda mifukoni. Baada ya kumaliza vyote akamshika na kumuweka pembeni. Akasogea pale na kuanzs kutembea kuingia ndani alipotokea yule mtu. Wakati anaukaribia mlango akasikia watu wakiongea kwa ndani. Katika mazungumzo yao akahisi walikuwa watatu kutokana na mchanganyiko wa Sauti zao.

"Mbona Fred harudi? Richie hembu muangalie inawezekana amezima. Aliisikia sauti ikitokea ndani. Masimba akajua kuna mtu anakuja. Hivyo akajibanza pembeni. Mara akauona mlango ukifunguliwa kisha mtu tena akatokea. Masimba akamuacha asogee mpaka usawa wake. Hata alipoufika usawa ule akajikuta akiguswa na kitu cha barifi. Kisha sauti nzito ya mwanaume ikanguruma. "Tulia kama Ulivyo, ukifanya chochote sitasita kukusafirisha kuzimu." " mtu yule hakutarajia lile, akahamanika na kutaka kupiga kelele. Masimba akamuwahi kwa pigo moja ya kidogoni, mtu yule akaanguka kama furushi. Masimba akamuwahi na kumshindilia ngumi kama tano. Mtu yule akatepeta kama mlenda. Alimpekuwa mifukoni. Huyu hakuwa na Silaha yoyote zaidi ya paketi tano za condom. Akamuacha sasa alikuwa akizama ndani kuwakabili watu ambao walikuwa ndani. Aliusukuma mlango taratibu na kuchungulia kwa ndani. Watu wawili walikuwa wamepakatana miguuni. Kilichomshangaza huku ndani taa hafifu zilikuwa zikiwaka. Nuru hiyo ndio iliyofanya macho yake kutua kwa watu wale wawili. Mwanaume na mwanamke. Akaufungua mlango tena na kupiga mluzi. Yule mwanaume aliyekuwa amempakata mwanamke akamuomva mwanamke asimame kisha yeye kusogea pale mlangoni huku akiuliza.

"Richie kuna nini? Aliuliza mtu yule huku akiufungua mlango pasipo na tahadgari. Akajikuta akikutana na mapigo matatu ya kung fu. Mtu yule akapepesuka na kwenda kumuangukia mwanamke yule. Masimba hakuitoa nafasi hiyo kwa mtu yule kuinuka. Akawawahi wote pale chini huku mdomo wa Bastola ukiwatizana sawa sawia. Wote walikuwa wakitweta kwa hofu. Kila mmoja alikuwa ameyatoa macho yake akimtizama Masimba. Hofu ilikuwa ikionekana machoni mwao. Hofu ambayo haikufanana na uonekanaji wa watu hawa. "Nimekuja na tiketi zenu za kuzimu, nimekuja na usafiri wa kuwapeleka huko. Lakini mkinijibu maswali yangu naweza kufikiria kuwaacha." Aliongea masimba Akiwatizama watu wale pasipo kuonyesha utani. "Usituue tutakujibu maswali yako." Aliongea mwanamke yule akitetemeka.

"Jimmy na suresh wako wapi? Akauliza masimva.

"Mimi sijui unauliza nini. Alijibu yule mwanaume akimuangalia masimba usoni. "Narudia tena wako wapi Jimmy na Suresh? Aliukiza tena safarii hii akiuinua mkono ulioshika bastola. "Unataka nikujibu mara ngapi? Nimesema sijui.. akajibu tena yule mwanaume. Muda ule ule mlipuko mdogo ukatokea, bastola ya nasimba ilikuwa imekohoa. Risasi ikatua kwenye paja lake la kushoto. Akapiga yoweee kubwa sana. "Utasema hutasema? Akauliza masimba huku bado bastola yake ameielekeza kwa mtu yule aliyekuwa akigumia kwa maumivu. Wakati mtu yule akiharibu kujibu mlango ukasukumwa kwa nguvu huku risasi kama mvua zikimiminwa mle ndani. Masimba akajivingirisha chini kisha kuchupa na kuangukia pembeni. Risasi zikapita muda ule ule akasikia yowee kutoka pale alipowaacha wale majambazi. Baada ya muda wa dakika tano. Risasi zikakoma ukimya ukatawala Eneo lote. Masimba Bado alikuwa amejificha pale akiwaangalia wale watu. Hata wao walionekana wakitafuta kitu. Hapo akajua walikuwa wakimtafuta yeye. Hakutaka kuwachelewesha, bastola yake ikakohoa tena mfululizo. Watu wanne walikuwa wakianguka mithili ya magunia. Walikuwa tayari kwenye safari ya kuzimu. Baada ya kuhakikisha amewamaliza wote akainuka na kusogea pale. Hapo akagundua hata yule mateka wake wakiume alikuwa ameuawa. Lakini kilichomshangaza ni kutokumuona mwanamke yule. Wakati akiendelea kutafuta akasikia kilio kutoka chini ya kiti kikubwa . Punde akamuona msichana yule akiinuka huku akitetemeka. Bastola ya masimba tayari ilikuwa ikimtizama. Lakini alipomuangalia vizuri usoni.. Akajisemea malaika huyu hapaswi kufa. "Nifuate tuondoke hapa kabla polisi hawajaja." Aliongea Masimba Huku akimvuta yule msicgana waondoke mle ndani.

******

Walikuwa wawili tu ndani ya chumba cha hoteli ile. Bastola ilikuwa bado mkononi kwa masimba akuendelea kumuangalia mwanadada yule aliyekuwa akitetemeka kwa hofu.

"Unaitwa nani? Akauliza masimba akiendelea kumtizama.

"Nani.!!!? Mimi au... aliuliza Binti huku akitetemeka.

"Kwani hapa tuko wangapi?" Akauliza Masimba akimuangalia tena.

"Tupo wawili." Akajibu tena Hofu ikionekana machoni.

"Basi tambua nakuuliza wewe.. naomba unijibu kabla sijabadili maamuzi." Aliongea Masimba.

"Naitwa SALHA ....." akajibu msichana yule. "Umefikaje pale kwenye ile nyumba na nani amekufikisha? Aliuliza Masimba akiendelea kumuangalia. "Nimeletwa pale na Jimmy. Wakati ananileta aliniambia kuwa amenitafutia kazi, lakini nilipofika aliniweka pale kama Msimamizi wa Biashara yao. Alijibu yule msichana. "JE ni Biashara gani inafanywa pale? Na kwa nini ulipogundua kazi ulioambiwa haipo, wewe ukaendelea kukaa? Binti yule akamuanglia Masimba kisha kwa sauti yake ya upole akajibu. "Naogopa kukwambia wataniua..... Maana nishatishiwa kupigwa bastola. Baada ya kumuuliza kwa nini ana muogopa mtu mmoja aitwaye masimba.". " kwahiyo una muogopa Jimmy lakini huniogopi mimi? Tambua mimi ni israil nikiamua ufe haufikishi sekunde moja. Naomba nijibu maswali yangu kabla sijakupa tiketi yako." Alinguruma Masimba akimuangalia binti yule. Salha akainua uso na kumwangalia masimba kisha kwa Sauti dhaifu akasema ....

ITAENDELEA KESHO
 
Katika vitu vimenifurahisha ni masimba kumuua mwamvita yaani roho nyeupeeeee
 
MATESO YANGU

SEHEMU YA 022

Niliona mateso makubwa iwapo nitaendelea na Sheila. Mwili wote ulikuwa ukiniuma. Masikio yangu hayakuwa yanasikia vizuri. Niliendelea kujitizama machozi yakinishuka na kuendelea kunilowanisha. Sikuwahi kuona mapenzi yanayonitesa kama haya. Mapenzi yanayoniliza na kuniumiza mfano huu. Kwa nini mimi? Yalikuwa mateso makali sana kwangu. Niliendelea kulazwa pale hospitalini bila kuwa na msaada wa mtu kwa kuwa mama hakuwepo hapa jijini. Hata kula yangu ilitokana na majirani waliokuwa wakiniletea chakula. Mpaka siku ya tano ndipo mama yangu na baba yangu wakiambatana na dada zangu wakafika. Kitendo cha kunikuta katika hali ile kilionyesha kuwaumiza na kuwatesa dada zangu. Walionekana kupaniki na kuanza kuongea maneno makali juu ya Sheila. Waliapa kumshikisha adabu iwapo atakwenda ama kurudi pale nyumbani. Niliwaangalia tu huku nikiendelea kulia, ni ukweli usiofichika kuhusu kupendwa na dada zangu. Kuwa kwangu mtoto wa mwisho kulinifanya dada zangu wanipende na kutotaka kuonewa na mtu yoyote. Nilikuwa nikiendelea kutoa machozi, maneno ya dada zangu yakanipa hasira kali juu ya Sheila. Nikaapa kuwa nikitoka na nikifanikiwa kumtia mikononi mwangu basi ningekwenda kufungwa kwa Kosa la kuua. Nilikuwa nimekasirika kwa kiwango kikubwa sana.

Wakati dada zangu wakiendelea kuongea kwa jazba, ghafla nikamuona mwanadada yule wa Posta akiingia pale ndani. Huyu alikuwa Rehema Ally. Mwanadada ambaye muda wote alionekana kutabasamu hata pale alipokuwa amechukia. Alikuwa akiingia ndani huku akionesha kushangazwa na maneno kutoka kwa dada Zangu. Hata wote walipomuona na kutizamana na kusalimiana, kila mmoja akanyamaza kumtizama malikia yule akitembea. Hata alipowasalimia hakusimama, bali aliendelea kusogea pale kitandani nilipolazwa mimi. Alionekana ni mwenye huzuni na huruma sana, macho yake mazuri yaliobeba kitu kama mapenzi yakanitizama. Kunitizama kwake kukafuatia na kitendo cha kuliona chozi lake. Chozi lililotoka kwenye macho yake. Alionekana kunionea huruma sana. Ila kwa upande wangu sikuwa namuamini na sikuwa natamani kuwa na mwanamke tena, lakini kule kuonyesha kuguswa na matatizo yangu kulinifanya nimfanye kuwa rafiki badala ya mpenzi. Alinishika hapa na kuniachia, akashika pale na kuachia huku. Dada Zangu wote walikuwa katika mshangao na sura zenye maswali.

Kila mmoja alitaka kumjua Rehema, kila mmoja alitaka kujua alikuwa nani kwangu, alitaka kujua ametokea sayari gani mpaka kufika hapa duniani. Walisubiri majibu kutoka kwangu, hata baba na mama walikuwa kwenye mkumbo ule. Wote walikuwa na maswali vichwani vyao. Kila mmoja alikuwa akijiuliza kuhusu Rehema. Huyu ni nani? Nikaona ni muda wa kuwaambia, nikamuita Rehema kwa sauti ya Chini, akaacha kile alichokua anafanya kisha kunitulizia macho usoni, nikakutana na Neno Mapenzi Katika Macho yake.. Neno ambalo sikutaka kulipa nafasi Moyoni mwangu. ''kutana na mama yangu pamoja na Baba. Huyu ndiye Mrs Masimba na Yule ndiye mr Masimba.''Niliongea huku nikiwaangalia Usoni. Nikarudi Upande wa Dada Zangu nao nikafanya kama nilipofanya mwanzo. Binti akainuka na kusogea pale waliposimama Wazazi Wangu. Akainama kwa Heshima na kutoa Salamu.

Alionesha Heshima ambayo nilimuona Mzee Haji Masimba Akitingisha kichwa na tabasamu kutamalaki usoni kwake. Baada ya kutoka kwa wazazi wangu akawaendea Dada Zangu, alianza na dada Yangu Mkubwa Husna, kisha akaenda kwa salama, harafu akafuatia Kwa Khadija. Huko kote alikuwa akipiga magoti na kuonyesha Heshima ya Hali ya Juu. Baada ya kumaliza utamburisho kwa ndugu ikafuata zamu ya kumtambulisha Rehema Ally Kwa wazazi Wangu na Dada Zangu. ''Baba na Mama Yangu pamoja na dada zangu. Nadhani hapa sio mahala pake katika hiki tunachokifanya. Lakini kwa kuwa mna Hamu na Shauku Ya Kumjua Huyu Msichana hapa, basi sina budi kuwatambulisha. Huyu anaitwa Rehema Ally, ni mwanafunzi Wa Chuo Kikuu Cha Dar es salaam akisomea shahada ya Uchumi na Maendeleo. Ni Rafiki Yangu na Dada Yangu.'' nikamaliza huku nikimtizama kila Mmoja Usoni. Hapo nikakutana na maswali lukuki katika nyuso Za Watu Wote. Kila mmoja alitegemea Utambulisho tofauti na ule. Kila mmoja alitarajia niseme labda ni Mpenzi Wangu. Lakini Haikuwa Hivyo, nilisimamia ukweli mtupu bila kupindisha.

******

zilipita wiki tatu tokea litokee lile tukio la kupigwa na polisi. Na sasa nilikuwa nikienda shule huku nikiwa sina mawasiliano na Sheila pamoja na Shamim. Na Hata polisi sikurudishwa tena wala sikuitwa popote pindi nilipotoka hospitalini. Pia nilikuwa sijaonana na hao watu kwa Muda wote Huo. Nilikuwa nikipiga kitabu kwa raha bila bughuza. Kila jioni Rehema alinipitia Chuoni na kwenda nyumbani kwetu. Muda Wote alionekana ni Mwanamke Mpole, msikivu na Mtaratibu. Muda Wote alikuwa akinishauri na kunishirikisha vitu Vingi sana. Kikafikia kipindi kila Alipo REHEMA basi IBRAHIM nami nilikuwepo.. Lakini Sikujua, Kama Ningejua? Mmmhh... KESHO MATESO YANGU

SEHEMU YA 022

Niliona mateso makubwa iwapo nitaendelea na Sheila. Mwili wote ulikuwa ukiniuma. Masikio yangu hayakuwa yanasikia vizuri. Niliendelea kujitizama machozi yakinishuka na kuendelea kunilowanisha. Sikuwahi kuona mapenzi yanayonitesa kama haya. Mapenzi yanayoniliza na kuniumiza mfano huu. Kwa nini mimi? Yalikuwa mateso makali sana kwangu. Niliendelea kulazwa pale hospitalini bila kuwa na msaada wa mtu kwa kuwa mama hakuwepo hapa jijini. Hata kula yangu ilitokana na majirani waliokuwa wakiniletea chakula. Mpaka siku ya tano ndipo mama yangu na baba yangu wakiambatana na dada zangu wakafika. Kitendo cha kunikuta katika hali ile kilionyesha kuwaumiza na kuwatesa dada zangu. Walionekana kupaniki na kuanza kuongea maneno makali juu ya Sheila. Waliapa kumshikisha adabu iwapo atakwenda ama kurudi pale nyumbani. Niliwaangalia tu huku nikiendelea kulia, ni ukweli usiofichika kuhusu kupendwa na dada zangu. Kuwa kwangu mtoto wa mwisho kulinifanya dada zangu wanipende na kutotaka kuonewa na mtu yoyote. Nilikuwa nikiendelea kutoa machozi, maneno ya dada zangu yakanipa hasira kali juu ya Sheila. Nikaapa kuwa nikitoka na nikifanikiwa kumtia mikononi mwangu basi ningekwenda kufungwa kwa Kosa la kuua. Nilikuwa nimekasirika kwa kiwango kikubwa sana.

Wakati dada zangu wakiendelea kuongea kwa jazba, ghafla nikamuona mwanadada yule wa Posta akiingia pale ndani. Huyu alikuwa Rehema Ally. Mwanadada ambaye muda wote alionekana kutabasamu hata pale alipokuwa amechukia. Alikuwa akiingia ndani huku akionesha kushangazwa na maneno kutoka kwa dada Zangu. Hata wote walipomuona na kutizamana na kusalimiana, kila mmoja akanyamaza kumtizama malikia yule akitembea. Hata alipowasalimia hakusimama, bali aliendelea kusogea pale kitandani nilipolazwa mimi. Alionekana ni mwenye huzuni na huruma sana, macho yake mazuri yaliobeba kitu kama mapenzi yakanitizama. Kunitizama kwake kukafuatia na kitendo cha kuliona chozi lake. Chozi lililotoka kwenye macho yake. Alionekana kunionea huruma sana. Ila kwa upande wangu sikuwa namuamini na sikuwa natamani kuwa na mwanamke tena, lakini kule kuonyesha kuguswa na matatizo yangu kulinifanya nimfanye kuwa rafiki badala ya mpenzi. Alinishika hapa na kuniachia, akashika pale na kuachia huku. Dada Zangu wote walikuwa katika mshangao na sura zenye maswali.

Kila mmoja alitaka kumjua Rehema, kila mmoja alitaka kujua alikuwa nani kwangu, alitaka kujua ametokea sayari gani mpaka kufika hapa duniani. Walisubiri majibu kutoka kwangu, hata baba na mama walikuwa kwenye mkumbo ule. Wote walikuwa na maswali vichwani vyao. Kila mmoja alikuwa akijiuliza kuhusu Rehema. Huyu ni nani? Nikaona ni muda wa kuwaambia, nikamuita Rehema kwa sauti ya Chini, akaacha kile alichokua anafanya kisha kunitulizia macho usoni, nikakutana na Neno Mapenzi Katika Macho yake.. Neno ambalo sikutaka kulipa nafasi Moyoni mwangu. ''kutana na mama yangu pamoja na Baba. Huyu ndiye Mrs Masimba na Yule ndiye mr Masimba.''Niliongea huku nikiwaangalia Usoni. Nikarudi Upande wa Dada Zangu nao nikafanya kama nilipofanya mwanzo. Binti akainuka na kusogea pale waliposimama Wazazi Wangu. Akainama kwa Heshima na kutoa Salamu.

Alionesha Heshima ambayo nilimuona Mzee Haji Masimba Akitingisha kichwa na tabasamu kutamalaki usoni kwake. Baada ya kutoka kwa wazazi wangu akawaendea Dada Zangu, alianza na dada Yangu Mkubwa Husna, kisha akaenda kwa salama, harafu akafuatia Kwa Khadija. Huko kote alikuwa akipiga magoti na kuonyesha Heshima ya Hali ya Juu. Baada ya kumaliza utamburisho kwa ndugu ikafuata zamu ya kumtambulisha Rehema Ally Kwa wazazi Wangu na Dada Zangu. ''Baba na Mama Yangu pamoja na dada zangu. Nadhani hapa sio mahala pake katika hiki tunachokifanya. Lakini kwa kuwa mna Hamu na Shauku Ya Kumjua Huyu Msichana hapa, basi sina budi kuwatambulisha. Huyu anaitwa Rehema Ally, ni mwanafunzi Wa Chuo Kikuu Cha Dar es salaam akisomea shahada ya Uchumi na Maendeleo. Ni Rafiki Yangu na Dada Yangu.'' nikamaliza huku nikimtizama kila Mmoja Usoni. Hapo nikakutana na maswali lukuki katika nyuso Za Watu Wote. Kila mmoja alitegemea Utambulisho tofauti na ule. Kila mmoja alitarajia niseme labda ni Mpenzi Wangu. Lakini Haikuwa Hivyo, nilisimamia ukweli mtupu bila kupindisha.

******

zilipita wiki tatu tokea litokee lile tukio la kupigwa na polisi. Na sasa nilikuwa nikienda shule huku nikiwa sina mawasiliano na Sheila pamoja na Shamim. Na Hata polisi sikurudishwa tena wala sikuitwa popote pindi nilipotoka hospitalini. Pia nilikuwa sijaonana na hao watu kwa Muda wote Huo. Nilikuwa nikipiga kitabu kwa raha bila bughuza. Kila jioni Rehema alinipitia Chuoni na kwenda nyumbani kwetu. Muda Wote alionekana ni Mwanamke Mpole, msikivu na Mtaratibu. Muda Wote alikuwa akinishauri na kunishirikisha vitu Vingi sana. Kikafikia kipindi kila Alipo REHEMA basi IBRAHIM nami nilikuwepo.. Lakini Sikujua, Kama Ningejua? Mmmhh... KESHO NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 046

Binti akainua uso kisha kwa sauti dhaifu akasema. "Biashara inayofanyika pale ni uingizaji na usambazaji wa madawa ya kulevya hapa nchini. Kuna viongozi wengi wa serikali, wabunge na mawaziri ni watu wenye hisa kwenye biashara hiyo. Na wafanyakazi wote tuliambiwa kwamba nilazima tufumbe midomo yetu la sivyo tutauawa. Wenzangu wengi wameshauawa kutokana na kuivujisha siri hii. Nadhani hata nami nipo njiani kuwafuata. Kama usiponiua wewe basi wataniua wao." Alijibu msichana yule hofu ikionekana kwenye macho yake. Masimba akamuangalia kwa nukta kisha akamuuliza tena.

"Unaweza kunitajia majina ya mawaziri watatu unaowajua? Swali hilo lilionekana kuwa gumu kwake. Akamuangalia Masimba kisha akaonekana kufikiria kwa muda. Harafu akashtuka kutoka huko na kutingisha kichwa kabla ya kusema. "Hapana siwezi kufanya hivyo, nitauawa.". Hilo likaonyesha kumkwaza masimba. Akamuangalia kwa muda huku mdomo wa bastola ukimlenga msichana yule. "Naomba unijibu maswali yangu, la sivyo nitakusafirisha kuzimu sekunde hii hii. Kama hujui mimi ndiye Masimba ninayeogopewa na mabosi zako. Nina uwezo wa kukufanya chochote. Sitaki unilazimishe kufanya hili." Aliongea huku akiendelea kumiangalia mwanamke yule. Akausoma mshtuko kutoka usoni kwa mwanamke yule. Mshtuko uliotokea baada ya kulitaja jina lake. Sasa akaiona hofu ikiyeyuka katika uso wa mwanamke yule. Tabasamu hafifu likaupamba uso wake. Lakini ghafla akaliona tabasamu likiyeyuka na kupotea ghafla kama mshumaa kwenye upepo mkali. Sura ikagubikwa na hofu tena. Ni hofu hiyo iliyompumbaza masimba. Ni hofu hiyo hiyo iliojenga maswali lukuki kichwani kwa masimba. Tabasamu katika sekunde tatu, lakini tabasamu likapotea katika sekunde ya nne na ya tano. Hofu ikamuingia tena mwanamke huyu. Kwa nini hofu? Kwa nini aogope? Anaogopa Jina langu ama anawahofia watu wake? Yalikuwa maswali, maswali ambayo hayakufanikiwa kupata Jibu katika wakati ule ule. Kwani ni muda ule aliokuwa akiongea na Salha akauona mlango ukitingishwa kisha kukasikika mlango kugongwa. MASIMBA NA SALHA wakatizamana, waliangaliana katika namna ya kuulizana "Huyo ni nani" hakukuwa na mwenye jibu. Lakini hapo hapo akamuona Salha ikisimama na kuufuata mlango. Hata hilo likamshangaza na kumburudisha machoni na hata Moyoni. Hakuburudika kwa utamu wa mtikisiko wa Nyuma wa Binti huyu, hakuburudika kwa kulitamani hilo, bali aliutamani uamuzi wake na kujiamini kwake. Huyu alikuwa kama Teddy Harry Wake. Huyu alikuwa Teddy yule wa kipindi kile. Teddy aliyekuwa haogopi risasi na hata kifo. Hilo likamkumbusha Syria. Kwenye mission ngumu ambayo haikuwahi kutokea. Salha alikuwa ni mfano huo. Licha ya hilo lakini bado alikuwa makini na kila hatua ya binti huyu. Hatua ya mwanamke ambaye alionyesha kuwa na vitu vingi. Hofu ikapotea usoni, hofu ikapotea katika muda huu huu. Alikuwa mfano wa kinyonga, alibadilika kila wakati. Kila hatua yake ilikwenda sambamba na mdomo wa bastola wa Masimba. Hakumuacha ageuke akiwa pekee. Ni pale alipoufikia mlango ndipo likatokea la kutokea. Mlango ukasukumwa wakaingia wanaume katika aina ya kuburudisha na kusisimua. Kila mmoja aliingia akiruka hapa na kutua pale. Ilitia raha na hata kuburudisha pia. Lakini wakati akiliangalia hilo hata yeye alikuwa ameshahama pale na kuangukia pembeni. Ni wakati akitua hapo chini akimuona mwanamke yule akifanya kitu ambacho kilimfanya ashangae. Binti alikuwa akionyesha burudani. Alikuwa akihama hapa katika kuwakabili watu wale. Alikuwa akipiga mateke ngumi na hata vichwa. Alikuwa akichanganya kung fu kareti na hata martial combat. Ilikuwa burudani kumtizama na ilikuwa burudani kumuangalia. Haikupita hata dakika mbili tayari wanaume wale walikuwa wamelaliana wakiwa hawana uhai. Hilo likikuwa jingine kwake. Licha ya uzuri wake, licha ya urembo na muonekano wake lakinikumbe alikuwa ni Hatari. Binti yule akaufunga mlango tena na kurudi pale alipokuwa Masimba amesimama. "Nipo tayari kukujibu maswali yako. Nipo tayari kukujibu chochote kile utakacho." Aliongea Salha akimuangalia Masimba. Masimba naye akamtizama. Wakatizamana na kutizamana. Kulikuwa na sumaku machoni kwa mwanamke huyu wa kichaga. Macho yalikuwa yakiongea vitu vingi sana. "Nadhani lipo swali langu hukunijibu." Akakumbusha, Kisha akaongeza, "nataka kujua majina ya mawaziri na hao wabunge. Pia nataka kufagamu walipo Jimmy na Suresh." Salha akamuangalia Masimba kisha kwa sauti ambayo haikuwa na Hofu Akajibu.

"Mawaziri ni Haji Mvula waziri wa maliasili na utalii. Waziri Utajiju Nyuma wa mambo ya Nje na mwingine Alikuwa Waziri mkuu ambaye amemuua wewe juzi. Wabunge ni Hagare Maro wa jimbo la tarime. Selestine pascal wa ukerewe na bibi Grace Bwahama wa kigamboni. Akajibu Salha.

"Jimmy na Suresh wako wapi?" Akauliza tena Masimba. "Jimmy na Ben Wamemfuatilia Teddy kwani inasemekana ametoroka hapa jijini akiwa na mtoto wako waliemchukua baada ya kumuua mama yako mzazi. Inasemekana Teddy aliomba likizo ya ghafla kazini na alipokubaliwa jana alionekana akitoka Airport na tokea hapo hakuonekana tena mpaka muda huu. Baada ya kufuatilia huku na huko waligundua Teddy alikuwa ameelekea Arusha akiwa na mwanao tayari kwa kuihama Nchi. Wakapiga simu kwa watu wetu kule kuwapa taarifa na kuwataka wafuatilie hilo lakini majibu yaliokuja ni kwanba Teddy hakuonekana Airport wala kwenye barabara yoyote. Ndipo jimmy na Ben walipoamua kwenda arusha kuongeza nguvu."
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom