ibra87
R I P
- Jul 22, 2015
- 5,614
- 5,360
- Thread starter
- #401
NITAKUPA TU
SEHEMU YA 044
Punde akamuona Mwamvita Akiingia tena akiwa mtupu. Alikuwa kama alivyozaliwa. Hilo halikumfanya masimba ashtuke. Bado alitulia huku bastola yake aina ya Revolver colt 48 ikiwa mkononi. Akamuacha mwamvita aingie kwanza. Na alipohakikisha ameingia Masimba akaufunga mlango kwa ndani. Mwamvita hakukitegemea kitendo hicho. Kwani baada ya kuusikia mlango ukifungwa akageuka akiwa mtupu vile vile. Akakutana na Mdomo wa bastola ukimtizama. Alikuwa akiangalia na masimba. Alikuwa akiangaliana na mtu ambaye alijua na kuhisi labda alikuwa Tanga kwenye mzima. Masimba hakuongea wala hakuwa anafanya chovhote. Bado alimuangalia Mwamvita kwa utulivu huku macho yake yakicheza pande zote. Kidole kikashuka taratibu kwenye kitufe cha kufyatulia Risasi. Rukia alikuwa akitokwa jasho jingi, alikuwa akikiogopa kifo. Akatamani kuongea kitu lakini akashindwa. Punde risasi ya kwanza akafyatuka na kutua kwenye kifua cha mwamvita. Risasi ya pili ikatua kichwani na kukifumua kichwa cha Mwamvita. Risasi ya tatu na nne zilitua kwenye matiti yake yote. Kila ilipokuwa akiifyatua risasi alikuwa akikumbuka kifo cha mama yake. Alikuwa akipiga risasi kwa Hasira, mwili mzima wa mwamvita ulikuwa umetapakaa damu. "Wasalimie kuzimu.. waambie bado naendelea kuwakusanya wote tayari kwa kuwapeleka huko." Aliongea Masimba huku akiuangalia mwili wa mwamvita. Baada ya kuhakikisha mwamvita amekwishakukata roho akauacha mwili pale pale kitandani kisha yeye akatoka Nje kupitia pale pale Dirishani. Safari hii aliamua kurudi Sinza kumekucha tayari kukijua kile ambacho kinaendelea ndani ya Saloon ile kilichosababisha mpaka Teja yule kuuawa. Alifanikiwa kutoka pasipokuonekana. Akaanza kuutafuta usafiri katika eneo lile ambalo bado hakujua ni wapi. Alitembea usiku usiku pasipokupata usafiri mpaka karibu na kijimji fulani Hivi. Hapo akafanikiwa kuiona pikipiki ambayo ilikuwa akipita. Alichokifanya ni kuisimamisha kisha kuwambia Dereva wapi anapoelekea. "Duh Bro mbona Huku ni Mbali sana na Sinza!! Alishangaa Dereva yule huku akianza kuonyesha wasiwasi Juu ya Masimba. Ndio kwanza masimba alikuwa akishtuka kwamba kumbe hakuwa ndani ya Jiji. "Kwani hapa ni wapi ndugu Yangu? Hatimaye Masimba akauliza huku akitabasamy ilikumtoa hofu kijana yule. "Hapa ni Bagamoyo brother, kwani unatokea wapi? Akajibu kijana yule kisha kuuliza tena.
Ikabidi masimba adanganye ili kupata usafiri wa kumrudisha jijini Dar es salaam. Hakutaka kuchelewa kwa kuwa bado kazi ilikuwa ngumu. Bado alikuwa na mission ngumu sana katika usiku. Usiku wa malipo ya damu ya watu wasio na hatia. Alitamani sana kuwamaliza wote kwa usiku ule ili aanze kumtafuta Yule Malaya Teddy. Alitaka kumuua mwisho kabisa. Hapo ndipo alipoona umuhimu wa kumdanganya kijana huyu. Uongo ambao ulimlainisha kijana na kukubali kumbeba Masimba kumpeleka Jiji Dar es salaam. Pikipiki ikaendeshwa usiku kwa usiku kwa mwendo wa kutisha na kuogopesha. Ilikuwa ni lazima aimalize mission katika muda wa masaa mawili yaliobaki, kwani saa yake ya mkononi ilikuwa ikimwambia ilikuwa saa saba na nusu usiku. Wakati wanaikaribia Bunju wakaiona gari ikija kwa mbele yao. Dereva akaupunguza mwendo kwa kuogopa kukamatwa. Masimba alimsisitiza aendelee kuendesha na Asiogope. Dereva akatii na kuanza kuendesha. Mbele kidogo kuikaribie ile gari wakapigwa mkono. Masimba akamwambia kijana yule asimame na Asiogope chochote. Kijana yule akasimamisha pikipiki na kutulia. Punde wakawaona watu watano wenye makoti makubwa wakisogea. Mkono wa Masimba Ukashuka taratibu alipoihifadhi bastola. Lakini watu wale waliposogea sans akagundua kwamba ni Askari. Akautoa mkono kisha akashuka. Polisi nao Wakawasogelea mpaka pale.
"Naomba Leseni yako ya udereva." Polisi mmoja akaamuru. Dereva yule hakuwa na leseni ya udereva. Baada ya Masimba kuona dereva wake ana hangaika. Akasogea karibu na kumuita askari mmoja pembeni. Askari yule akasogea kwa umakini sana huku SMG ikiwa mkononi. Kumfikia masimba tu akapewa kitanbulisho kimoja kati ya vingi alivyonavyo masimba. Baada ya kukipokea na kukiangalia, askari yule akakamaa kwa Saluti. Kitambulisho kikarudishwa kwa mwenyewe kisha wakaruhusiwa waendelee na Safari yao. Askari wote walikuwa wakintizama Masimba kwa mshangao. Hawakuwahi kumuona Zaidi ya kumsikia. Hawakuwahi kumuona Zaidi Ya kuona na kusoma sifa zake. Wakaendelea kumuangalia mpaka anatokomea. Hawakuwa wameamini na licha ya kutokuamini macho yao lakini walifarijika sana kumuoba mtu huyu.
*********
Kama ilivyo kwa maeneo mengi ya Jiji la dar es salaam kutokukosa watu hata iwe usiku wa maneno, ndio hali ambayo aliikuta Masimba Baada ya kufika hapo. Bado madada poa walikuwa kwenye biashara za kuuza miili yao. Mateja wengi bado walikuwa barabarani wakipiga debe na hata usafiri wa kukupeleka popote bado ulikuwa ni wakumwaga. Alishuka kumekucha na kumlipa dereva wa pikipiki pesa yake. Basda ya hapo akamwambia anaweza kurudi na asiwe na wasiwasi. Baada ya kuachana na dereva yule, masimba akatembea kama mtu wa kawaida mpaka nyuma ya Jengo ambalo kwa mbele ndio kulikuwa na Ile flemu yenye saloon. Cha ajabu lilikuwa jengo kubwa sana. Jengo ambalo lilikuwa na vyumba vingi sana. Na kingine kilichokuwa kikimshangaza ni miguno ya watu wanaofanya mapenzi kila pale alipokuwa anasogea. Hilo likampa shaka na kuamini labda jumba hili lilikuwa na danguro ama ni gesti bubu. Akaendelea kutembea na ukuta wa jengo lile mpaka alipofika mbeli kidogo ndio akauona mlango wa kuingilia. Kuuona mlangoni huo kuliendana na kuwaona walinzi watatu waliokuwa wakizunguka hapo, mikononi wakiwa na Bunduki kubwa. Kuwaona walinzi wale kukampa picha halisi kuwa sehemu ile haikuwa gesti wala danguro bali kulikuwa kukifanyika Biashara nyingine zaidi, tena biashara kubwa na ya hatari. Akaongeza umakini safari hii akiamua kupambana kwa Mikono. Akatafuta njia nzuri ya kuwakabili walinzi wale. Akaendelea kuwatizama kama atawaona walinzi wengine, lakini aligundua walikuwa walewale watatu. Muda huu alikuwa amehama pale na kuhamia huku. Alitaka kuwazunguka na kuwatokea kwa nyuma. Aliwaangalia kwa hatua zao na ukaaji wao. Akahamisha macho kwa kila mmoja aliyekuwa pale. Wote walikuwa wamesimama sehemu moja wakiongea. Alikuwa na uwezo wa kuwachapa Risasi wote lakini hilo akaliacha baada ya kuyaona mazingira. Akatembea na giza mpaka karibu kabisa na walinzi wale. Sekunde hii alikuwa akisogea kwa karibu zaidi. Ulikuwa ni muda wa kuwaonyesha kwa nini Aliaminiwa na Taifa. Akawatokea pale pale kwa kushtukiza. Yaani sekunde hii walikuwa wenyewe wakiongea, lakini sekunde ya pili walijikuta wakiwa wanne. Alikuwa ameongezeka mtu mmoja katikati yao. Mtu ambaye aliwashangaza na hata kuwafanya wababaike. Haiwezekani muda huu waongee watatu, harafu sekunde ile ile aongezeke wa nne. Mikono yao ikataka kushuka kwenye tufe la kuachia Risasi. Ni wakati huo kila mmoja alikuwa akiugulia maumivu. Yalikuwa mapigo yaliompigwa katika namna ambayo hakuna ambaye aliiona. Kila mmoja alikuwa ikigugumia kwa maumivu huku akishika kwenye korodani. Hakutaka kuwapa nafasi ya kujiuliza. Lakini wakati akijiandaa mmoja akarusha teke lakini likapita hewani baada ya kukwepwa kwa ustadi. Akarusha tena ngumi tano mfululizo lakini zilipita hewani. Safari hii akakutana na teke la Taya. Akajikuta mlinzi yule akiisalimia sakafu. Wakati huo walinzi wengine walikuwa wamekaa sawa. Yakafuata mapigano yaliochukua dakika mbili tu. Walinzi wote walikuwa chini wakiwa hawana uhai.
Akawaacha chini wakiwa wamelaliana. Sasa akawa anaingia ndani ya jengo lile kwa kupitia mlango wa ule ule. Bado miguno ya mapenzi ilikuwa ikisikika. Bado malalamiko ya mahaba yalikuwa yakitamalaki katika ngoma za masikio yake. Hapo akahamisha mawazo yake kwa Teddy, alimkumbuka Teddy kwa mengi. Alikuwa msichana wa kipare lakini alikuwa akiyajua mapenzi kama mzaramo ama mngoni. Alikuwa akijua kuutumia mwili wake mwembamba kwa utulivu na ufundi mkubwa. Ukimuona akiwa kwenye uwanja wa fundi seremala ungehisi labda alitokea Tanga yalikozaliwa mapenzi. Akapita akiyalazimisha masikio yake yatii kile ambacho alikwenda kukitenda. Akalifungua geti taratibu na kuchungulia kwa ndani, hapo akakutana na giza totoro. Akalifungua zaidi na zaidi kisha kujipenyeza ndani. Bado utulivu haukuwepo, bado miguno iliendelea. Akatembea sambamba na ukuta mpaka karibu kabisa na kibanda ambacho kilionyesha kilikuwa ni cha walinzi. Akatulia hapo akaangalia kila kona kwa chati. Kwa kuwa alikuwa amezoea giza, kwa kuwa macho yake yalizoea hali hiyo. Akafanikiwa kuwaona watu waanne katika sehemu tofauti. Licha ya uwepo wa watu wale, lakini hawakuonyesha kama walimuona Masimba. Hilo likamfanya masimba asonge mpaka karibu na mlango wa kuingilia ndani. Kufika hapo akaisikia minong'ono ikitokea ndani. Masimba akachomoa bastola kisha kuiweka Tayari. Bado minong'ono iliebdelea tena na tena. Punde akahisi ukimya lakini ukimya huo haukudumu sana, kwani Ndani ya Sekunde kumi miguno ikaanza kusikika kutoka ndani...
ITAENDELEA
SEHEMU YA 044
Punde akamuona Mwamvita Akiingia tena akiwa mtupu. Alikuwa kama alivyozaliwa. Hilo halikumfanya masimba ashtuke. Bado alitulia huku bastola yake aina ya Revolver colt 48 ikiwa mkononi. Akamuacha mwamvita aingie kwanza. Na alipohakikisha ameingia Masimba akaufunga mlango kwa ndani. Mwamvita hakukitegemea kitendo hicho. Kwani baada ya kuusikia mlango ukifungwa akageuka akiwa mtupu vile vile. Akakutana na Mdomo wa bastola ukimtizama. Alikuwa akiangalia na masimba. Alikuwa akiangaliana na mtu ambaye alijua na kuhisi labda alikuwa Tanga kwenye mzima. Masimba hakuongea wala hakuwa anafanya chovhote. Bado alimuangalia Mwamvita kwa utulivu huku macho yake yakicheza pande zote. Kidole kikashuka taratibu kwenye kitufe cha kufyatulia Risasi. Rukia alikuwa akitokwa jasho jingi, alikuwa akikiogopa kifo. Akatamani kuongea kitu lakini akashindwa. Punde risasi ya kwanza akafyatuka na kutua kwenye kifua cha mwamvita. Risasi ya pili ikatua kichwani na kukifumua kichwa cha Mwamvita. Risasi ya tatu na nne zilitua kwenye matiti yake yote. Kila ilipokuwa akiifyatua risasi alikuwa akikumbuka kifo cha mama yake. Alikuwa akipiga risasi kwa Hasira, mwili mzima wa mwamvita ulikuwa umetapakaa damu. "Wasalimie kuzimu.. waambie bado naendelea kuwakusanya wote tayari kwa kuwapeleka huko." Aliongea Masimba huku akiuangalia mwili wa mwamvita. Baada ya kuhakikisha mwamvita amekwishakukata roho akauacha mwili pale pale kitandani kisha yeye akatoka Nje kupitia pale pale Dirishani. Safari hii aliamua kurudi Sinza kumekucha tayari kukijua kile ambacho kinaendelea ndani ya Saloon ile kilichosababisha mpaka Teja yule kuuawa. Alifanikiwa kutoka pasipokuonekana. Akaanza kuutafuta usafiri katika eneo lile ambalo bado hakujua ni wapi. Alitembea usiku usiku pasipokupata usafiri mpaka karibu na kijimji fulani Hivi. Hapo akafanikiwa kuiona pikipiki ambayo ilikuwa akipita. Alichokifanya ni kuisimamisha kisha kuwambia Dereva wapi anapoelekea. "Duh Bro mbona Huku ni Mbali sana na Sinza!! Alishangaa Dereva yule huku akianza kuonyesha wasiwasi Juu ya Masimba. Ndio kwanza masimba alikuwa akishtuka kwamba kumbe hakuwa ndani ya Jiji. "Kwani hapa ni wapi ndugu Yangu? Hatimaye Masimba akauliza huku akitabasamy ilikumtoa hofu kijana yule. "Hapa ni Bagamoyo brother, kwani unatokea wapi? Akajibu kijana yule kisha kuuliza tena.
Ikabidi masimba adanganye ili kupata usafiri wa kumrudisha jijini Dar es salaam. Hakutaka kuchelewa kwa kuwa bado kazi ilikuwa ngumu. Bado alikuwa na mission ngumu sana katika usiku. Usiku wa malipo ya damu ya watu wasio na hatia. Alitamani sana kuwamaliza wote kwa usiku ule ili aanze kumtafuta Yule Malaya Teddy. Alitaka kumuua mwisho kabisa. Hapo ndipo alipoona umuhimu wa kumdanganya kijana huyu. Uongo ambao ulimlainisha kijana na kukubali kumbeba Masimba kumpeleka Jiji Dar es salaam. Pikipiki ikaendeshwa usiku kwa usiku kwa mwendo wa kutisha na kuogopesha. Ilikuwa ni lazima aimalize mission katika muda wa masaa mawili yaliobaki, kwani saa yake ya mkononi ilikuwa ikimwambia ilikuwa saa saba na nusu usiku. Wakati wanaikaribia Bunju wakaiona gari ikija kwa mbele yao. Dereva akaupunguza mwendo kwa kuogopa kukamatwa. Masimba alimsisitiza aendelee kuendesha na Asiogope. Dereva akatii na kuanza kuendesha. Mbele kidogo kuikaribie ile gari wakapigwa mkono. Masimba akamwambia kijana yule asimame na Asiogope chochote. Kijana yule akasimamisha pikipiki na kutulia. Punde wakawaona watu watano wenye makoti makubwa wakisogea. Mkono wa Masimba Ukashuka taratibu alipoihifadhi bastola. Lakini watu wale waliposogea sans akagundua kwamba ni Askari. Akautoa mkono kisha akashuka. Polisi nao Wakawasogelea mpaka pale.
"Naomba Leseni yako ya udereva." Polisi mmoja akaamuru. Dereva yule hakuwa na leseni ya udereva. Baada ya Masimba kuona dereva wake ana hangaika. Akasogea karibu na kumuita askari mmoja pembeni. Askari yule akasogea kwa umakini sana huku SMG ikiwa mkononi. Kumfikia masimba tu akapewa kitanbulisho kimoja kati ya vingi alivyonavyo masimba. Baada ya kukipokea na kukiangalia, askari yule akakamaa kwa Saluti. Kitambulisho kikarudishwa kwa mwenyewe kisha wakaruhusiwa waendelee na Safari yao. Askari wote walikuwa wakintizama Masimba kwa mshangao. Hawakuwahi kumuona Zaidi ya kumsikia. Hawakuwahi kumuona Zaidi Ya kuona na kusoma sifa zake. Wakaendelea kumuangalia mpaka anatokomea. Hawakuwa wameamini na licha ya kutokuamini macho yao lakini walifarijika sana kumuoba mtu huyu.
*********
Kama ilivyo kwa maeneo mengi ya Jiji la dar es salaam kutokukosa watu hata iwe usiku wa maneno, ndio hali ambayo aliikuta Masimba Baada ya kufika hapo. Bado madada poa walikuwa kwenye biashara za kuuza miili yao. Mateja wengi bado walikuwa barabarani wakipiga debe na hata usafiri wa kukupeleka popote bado ulikuwa ni wakumwaga. Alishuka kumekucha na kumlipa dereva wa pikipiki pesa yake. Basda ya hapo akamwambia anaweza kurudi na asiwe na wasiwasi. Baada ya kuachana na dereva yule, masimba akatembea kama mtu wa kawaida mpaka nyuma ya Jengo ambalo kwa mbele ndio kulikuwa na Ile flemu yenye saloon. Cha ajabu lilikuwa jengo kubwa sana. Jengo ambalo lilikuwa na vyumba vingi sana. Na kingine kilichokuwa kikimshangaza ni miguno ya watu wanaofanya mapenzi kila pale alipokuwa anasogea. Hilo likampa shaka na kuamini labda jumba hili lilikuwa na danguro ama ni gesti bubu. Akaendelea kutembea na ukuta wa jengo lile mpaka alipofika mbeli kidogo ndio akauona mlango wa kuingilia. Kuuona mlangoni huo kuliendana na kuwaona walinzi watatu waliokuwa wakizunguka hapo, mikononi wakiwa na Bunduki kubwa. Kuwaona walinzi wale kukampa picha halisi kuwa sehemu ile haikuwa gesti wala danguro bali kulikuwa kukifanyika Biashara nyingine zaidi, tena biashara kubwa na ya hatari. Akaongeza umakini safari hii akiamua kupambana kwa Mikono. Akatafuta njia nzuri ya kuwakabili walinzi wale. Akaendelea kuwatizama kama atawaona walinzi wengine, lakini aligundua walikuwa walewale watatu. Muda huu alikuwa amehama pale na kuhamia huku. Alitaka kuwazunguka na kuwatokea kwa nyuma. Aliwaangalia kwa hatua zao na ukaaji wao. Akahamisha macho kwa kila mmoja aliyekuwa pale. Wote walikuwa wamesimama sehemu moja wakiongea. Alikuwa na uwezo wa kuwachapa Risasi wote lakini hilo akaliacha baada ya kuyaona mazingira. Akatembea na giza mpaka karibu kabisa na walinzi wale. Sekunde hii alikuwa akisogea kwa karibu zaidi. Ulikuwa ni muda wa kuwaonyesha kwa nini Aliaminiwa na Taifa. Akawatokea pale pale kwa kushtukiza. Yaani sekunde hii walikuwa wenyewe wakiongea, lakini sekunde ya pili walijikuta wakiwa wanne. Alikuwa ameongezeka mtu mmoja katikati yao. Mtu ambaye aliwashangaza na hata kuwafanya wababaike. Haiwezekani muda huu waongee watatu, harafu sekunde ile ile aongezeke wa nne. Mikono yao ikataka kushuka kwenye tufe la kuachia Risasi. Ni wakati huo kila mmoja alikuwa akiugulia maumivu. Yalikuwa mapigo yaliompigwa katika namna ambayo hakuna ambaye aliiona. Kila mmoja alikuwa ikigugumia kwa maumivu huku akishika kwenye korodani. Hakutaka kuwapa nafasi ya kujiuliza. Lakini wakati akijiandaa mmoja akarusha teke lakini likapita hewani baada ya kukwepwa kwa ustadi. Akarusha tena ngumi tano mfululizo lakini zilipita hewani. Safari hii akakutana na teke la Taya. Akajikuta mlinzi yule akiisalimia sakafu. Wakati huo walinzi wengine walikuwa wamekaa sawa. Yakafuata mapigano yaliochukua dakika mbili tu. Walinzi wote walikuwa chini wakiwa hawana uhai.
Akawaacha chini wakiwa wamelaliana. Sasa akawa anaingia ndani ya jengo lile kwa kupitia mlango wa ule ule. Bado miguno ya mapenzi ilikuwa ikisikika. Bado malalamiko ya mahaba yalikuwa yakitamalaki katika ngoma za masikio yake. Hapo akahamisha mawazo yake kwa Teddy, alimkumbuka Teddy kwa mengi. Alikuwa msichana wa kipare lakini alikuwa akiyajua mapenzi kama mzaramo ama mngoni. Alikuwa akijua kuutumia mwili wake mwembamba kwa utulivu na ufundi mkubwa. Ukimuona akiwa kwenye uwanja wa fundi seremala ungehisi labda alitokea Tanga yalikozaliwa mapenzi. Akapita akiyalazimisha masikio yake yatii kile ambacho alikwenda kukitenda. Akalifungua geti taratibu na kuchungulia kwa ndani, hapo akakutana na giza totoro. Akalifungua zaidi na zaidi kisha kujipenyeza ndani. Bado utulivu haukuwepo, bado miguno iliendelea. Akatembea sambamba na ukuta mpaka karibu kabisa na kibanda ambacho kilionyesha kilikuwa ni cha walinzi. Akatulia hapo akaangalia kila kona kwa chati. Kwa kuwa alikuwa amezoea giza, kwa kuwa macho yake yalizoea hali hiyo. Akafanikiwa kuwaona watu waanne katika sehemu tofauti. Licha ya uwepo wa watu wale, lakini hawakuonyesha kama walimuona Masimba. Hilo likamfanya masimba asonge mpaka karibu na mlango wa kuingilia ndani. Kufika hapo akaisikia minong'ono ikitokea ndani. Masimba akachomoa bastola kisha kuiweka Tayari. Bado minong'ono iliebdelea tena na tena. Punde akahisi ukimya lakini ukimya huo haukudumu sana, kwani Ndani ya Sekunde kumi miguno ikaanza kusikika kutoka ndani...
ITAENDELEA