Riwaya: Nitakupata tu

Riwaya: Nitakupata tu

NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 049

Jimmy akainua macho yake na kuwatizama wajumbe wote. Akakuta hata wao walikuwa wakimtizama kwa umakini wa hali ya juu. Akarudisha tena macho yake chini na kuitizama picha ya Mwamvita. "Ndugu zangu nimewaita hapa si kwakupongezana kama tulivyozoea. Nafahamu kuwa wote mnafahamu kinachoendelea tokea kufariki kwa Mlinzi wetu mkuu ambaye alikuwa ndio kiongozi wa Serikali Bungeni. Ndugu zangu tokea kufariki kwake tumekuwa tukiishi katika tafakuri na sintofahamu kubwa. Tumekuwa tukishambuliwa na kupelelezwa. Watu wetu wanazidi kuuawa huku ngome zetu nazo zikivamiwa na kuharibiwa. Ndugu wajumbe wakati hayo yote yakiendelea sikuwa nimewahi kuwaita hapa. Tulikuwa kimya tukiiuangalia upepo unapovuma na wapi unapoelekea. Lakini kilichotokea Jana katika ngome yetu ya kumekucha na tukio la kuuawa kwa Mlinzi wetu na muuaji mkuu wa Kitengo chetu. Ni wazi kuwa sasa mambo yameanza kwenda mlama. Mtu mmoja tu anatusumbua anavyotaka! Kwa nini Masimba atambe na kutufanya sisi kama watoto wakike. Kwa nini tunamuacha atambe kama yeye ndiye Mwanaume? Na habari ambazo tunazo mikononi Mwetu ni Kwamba Masimba ameelekea Arusha kumfuata Teddy baada ya kuambiwa kwamba Teddy anataka kuvuka mpaka kuelekea nchini Kenya. Vijana wetu wapo makini lakini cha kushangaza mtu huyu bado hakuonekana popote pale. Hoteli na Nyumba zote za kulala wageni tumepenyeza Watu wetu, kwenye viwanja vya ndege pia tumefanya hivyo na hata katika Njia zile za panya vijana wapo huko. Lakini kama ninavyosema bado Masimba na Hata Teddy hawakuonekana popote. Hilo limetufanya tuamini kuwa watu hawa wapo hapa hapa Dsm ama wapo Arusha na inaonekana wametuzidi ujanja. Ndugu zangu Hii vita ni kubwa vita ambayo itatulazimu sasa tuwe na watu wenye uzoefu mkubwa. Itatulazimu sasa kuitumia tena Idara ya Usalama wa Taifa kwa mara nyingine ili kupambana na Masimba." Wakati akiendelea kueleza mjumbe mmoja akainua mkono kuonyesha kuwa kuna jambo alitaka kulizungumza. Jimmy lambert akamruhusu aongee. "Ndugu mwenyekiti nimekusikiliza kwa makini sana kwenye mazungumzo yako. Lakini nilikuwa na mawili matatu ya kukueleza. Bila shaka unatambua sisi ni wabunge wa bunge la jamhuri. Inawezekana sisi tukawa tunajua mengi kuliko nyie. Tetesi ambazo nimezipata kutoka kwa rafiki yangu ambaye anafanya kazi pale Ikulu ni kwamba. Tayari muuaji wa Waziri mkuu amejulikana lakini kizuizi cha kutangazwa Jina lake kunatoka kwa Mkurugenzi Wa Idara ya Usalama Wa Taifa ambaye alimwambia Rais kuwa asifanye maamuzi yoyote kwa kuwa kuna jambo kubwa lipo nyuma ya mauaji hayo. Hivi ninavyo kwambia ndugu mwenyekiti muuaji ndio amepewa Jukumu la kuleta hilo jambo kubwa lililosababisha kifo cha Waziri na hivi sasa masimba anaripoti Ikulu na Sio kwa DG. Kingine ni kuhusu Masimba na Teddy kusemekana kuwa wameelekea Arusha. Lakini ukweli ni kwamba Masimba na Teddy wapo Tanga. Wapo pamoja na wamerudisha umoja na mapenzi yao. Waambie Vijana waelekee Tanga watoke huko Arusha." Aliongea mjumbe yule akionekana kujiamini. Maneno yale yakaufanya Ujumbe wote kuwa kumya kwa muda. Ukumbi uliingia ubaridi kila mmoja akiwaza lake. Kila mmoja aliuhisi ugumu katika hilo. Rais tayari anamjua muuaji, lakini DG wa Tiss amezuia kutajwa ama kuchukuliwa Hatua kwa Muuaji kwa kile kunachosemekana kuna Jambo kubwa limejificha Nyuma ya Kifo cha Waziri mkuu. Harafu mtu anayetuhumiwa kufanya mauaji ndiye ambaye amepewa Kazi ya kukichunguza kilichopo nyuma ya kifo hicho. Kama suala ni hivyo ni nani atapona katika hili? Kama mtu amemuua Waziri mkuu anayetembea na walinzi maalum wenye mafunzo yote, je atashindwa kuwaua wao? Hilo ndilo lililowatia Hofu na kuupa ukimya Ukumbi wote. Waliijua hatari kama wataliacha hili liendelee. Kwa mara nyingine Jimmy akainua uso na kuwatizama wenzake. Akakutana na Hofu machoni mwao. Yeah! Ilikuwa hofu kubwa sana tena sana. Hata yeye moyoni aliiona hofu moyoni mwake. Alitabasamu mdomoni lakini moyoni alikuwa na hofu. Baada ya kufikiria sana akachukua Simu na kuongea Maneno kadhaa kisha kuirudisha mahala pake. Akawaangalia tena wajumbe akatabasamu. Lilikuwa tabasamu lililopokewa kwa staili tofauti na wajumbe. Hawakujua kile ambacho Mwenyekiti alikujua.

*****

Mume wangu hii ni vita kubwa, vita yangu ambayo inanihusu mimi. Hivi ni vita nilioianzisha, vita ambayo nitaimaliza mimi hata kama nitakufa. Damu ya mama italipwa na mikono yangu. Sitaki uniache kwenye hii mission. Najua mengi sana tena sana. Ni wakati wa kuikusanya nguvu ambayo niliidhoofisha kwa muda mrefu sana." Aliongea teddy akiwa mtupu kama alivyozaliwa pembeni akiwa amelala Masimba. Walikuwa wakitizamana baada ya kuimaliza safari yao ya kupashana miili joto. Teddy alikuwa ameupandisha mguu kwa Masimba akimtizama machoni. Ni muda mrefu ulikuwa umepita pasipo hilo kufanyika. "Tukimaliza hii kazi nahitaji tupate mtoto mwingine wa kike. Si unamuona Amanda jinsi alivyo." Aliongea Teddy huku akisogea zaidi. "Usijali hata mimi natamani tungekuwa na mtoto wa kike. Lakini tumalize hii kazi. Tukishamaliza tutaondoka hapa Tanzania." Iliongea masimba akiichukua Chuchu ya Teddy na Kuitia mdomoni. Kilichofuata hapo ilikuwa ni shuhuli iliyomuacha teddy akigumia kwa Raha.

Ilikuwa ni siku nyingine yenye pilika nyingi, siku ambayo Masimba aliamua kuianza kazi Rasmi ya kuutafuta Uovu wa Waziri mkuu. Leo hii akiwa kwenye Suti kali na kuvutia alikuwa ameamua kutembelea Ofisi ya Waziri mkuu. Alitaka kwenda hapo kwa sababu ya kuianza kazi yake. Kabla ya kwenda hapo aliwasiliana kwanza na Mkurugenzi wa Idara ya Usalama. Taarifa ikatumwa ikulu kueleza safari ya Masimba. Punde majibu yalikuja kwamba ameruhusiwa. Masimba akachukua Gari kutoka mafichoni wanapoishi na Safari ya kuelekea ofisi ya Waziri mkuu ikaanza. Kufika maeneo ya Tabata akakumbuka kuwa alimuacha Salha katika nyumba fulani. Akakata shauri kwenda hapo kumuangalia kwa kuwa aliamini Salha hakuwa amemteka France bali alikuwa amemchukua ki usalama zaidi. Alijua kama Salha angekuwa amemteka France basi mpaka sasa angeshapokea Amri ya kufanya chochote. Gari ikabadili mwelekeo sasa ilikuwa akielekea tabata Matumbi. Muda mfupi gari ilikuwa ikisimamishwa kwenye maegesho fulani ya magari. Masimba akashuka na kutembea kwa miguu mpaka aliposimama mlinzi wa parking ile. Baada ya maneno manne matatu, masimba akaingiza mkono mfukoni na kutoa noti ya elfu kumi na kumpa mlinzi. Sasa akaiacha Parking ile akitembea kuelekea eneo fulani la siri. Wakati anakaribia eneo hilo kuna kitu akakikanyaga, punde ardhi ikafunguka masimba akaingia kisha ardhi kujifunga tena. Kufika ndani akapokelewa na ngazi ambazo zitamshusha moja kwa mmoja mpaka mlangoni mwa nyumba fulani kule chini. Akaufungua mlango na kupokelewa na sebule pana ambayo ilikuwa kimya na tulivu. Baada ya kuingia hapo cha kwanza kukutana nacho ni picha ambayo aliipiga akiwa na Dee plus. Akaitizama kwa uchungu sana. Baada ya kuingalia kwa muda akaiweka na kuufuata mlango unaofuata. Akaufungua na kutokea kwenye sebule nyingine. Hapa akajikuta akitabasamu baada ya kumuona France amelala pembeni mwa Salha. Masimba akawatizama wote kwa kuvutiwa. Akasogea mpaka alipolala France na kumbusu Shavuni. Machozi yalikuwa yakimtoka taratibu. Hakutaka kuwaamsha alijua salha alifanya hivyo kwa kuhakikisha usalama wa mwanawe. Kwa mara ya kwanza alianza kumuamini Salha. Akaufungua mlango na kutoka tena kwa kupitia pale pale. Muda mfupi baadae alikuwa barabarani akielekea ofisini Kwa Waziri Mkuu.

*******

Wakati masimba akielekea nyumbani Kwa waziri mkuu, Teddy alikuwa Barabarani Akielekea nyumbani kwa Mbunge Wa Tarime Maro Hagare. Alitaka kuwaondoa wajumbe wote ambao walikuwa wakihusika katika biashara ile. Bastola zake zilikuwa zimehifadhiwa sehemu tayari kwa kufanya kile kikubwa. Aliwajua na aliwatambua kwa undani zaidi. Hakutishwa na ulinzi wa majumba yao. Alikuwa ameichukua kazi ya mtoa roho. Alikuwa ameibeba Tiketi ya mbunge yule ambaye alikuwa mfanyabiashara mkubwa na mshirika mkubwa wa Biashara ile Haramu. Alifika nyumbani kwa mheshimiwa majira ya saa nne asubuhi. Aliuchagua muda huo kwa kuwa alijua kwa muda huo mbunge huyo alikuwa amelala kutokana na kutokuwepo kwa familia yake. Alipofika nyumbani hapo akaookewa na mlinzi kwa bashasha kwa kuwa walikuwa wakifahamiana. Baada Teddy Kuingia ndani akaona hakuna sababu ya kumuacha hai mlinzi Huyu. Siku zote katika kazi hizi hawakutakiwa kuacha Ushahidi Nyuma. sekunde hii Bastola ilikuwa mkononi na wakati huo huo mlio mithiri ya Chafya ukasikika. Mlinzi akaanguka chini huku akiwa amekishikilia sehemu ya kifua chake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom