Dotonho
Member
- Jun 25, 2022
- 21
- 92
Habari member wa JamiiForums ningependa kuwaleteeni Riwaya ya ndugu mwandishi Kelvin kagambo ili tuelimike na kubuludika pamoja.
========
RIWAYA: MWANAMKE KAMA MAMA YANGU
MTUNZI: KELVIN DONATUS KAGAMBO
SIMU: 0713 48 28 16
FACEBOOK: KEV CLEVER KAGAMBO
SEHEMU YA KWANZA (1)
"Vuta picha ungelikuwa umezaliwa Mwanaume. Je, ungelithubutu kuoa Mwanamke wa sampuli yako?" Nakumbuka hiyo ndiyo ilikuwa sentensi yangu ya mwisho kwake kabla hajarejea Paradiso.
Pengine anaweza asikumbuke nguvu iliyobebwa na sentesi hiyo yenye maneno 12 tu, lakini binafsi naamini ilikuwa ni sentensi yenye nguvu kuu ndani yake. Sentensi ambayo ilikuwa na uwezo wa kubadili yabisi kuwa kimiminika au hata rangi nyeupe kurudi nyeusi.
Ndiyo; na hiyo ni kwasababu sikuzungumza sentensi hiyo kama jinsi mlevi anavyomtongoza baa medi, husema nakupenda licha ya kwamba neno hilo hutokea kwenye ndimi na si moyoni kama inavyohitajika.
Nilizungumza sentensi ile kwa HISIA kali na mguso wa hali ya juu na ndio maana mara tu baada ya sentensi ile nilitokwa na machozi, nikaingia ndani; chumbani, nikajifungia mlango.
Pengine alidhani labda nitaingia ndani na kuchukua kamba ngumu na madhubuti halafu nitajinyonga, lakini mimi si mpuuzi namna hiyo, nijihukumu kwa makosa ya mwenzangu, ni upuuzi ambao kamwe siwezi kuufanya.
Nakumbuka siku ile ilikuwa Jumatatu, kazi zilinibana haswa kiasi kwamba mpaka kufikia majira ya saa tatu za usiku bado nilikuwa kazini. Kwasababu nilikuwa ni Baba wa familia basi ilikuwapo kila sababu ya kuwajulisha wanafamilia yangu kwamba ningechelewa kurejea nyumbani siku hiyo.
Nilichukua simu na kumpigia Ashura--Mke wangu. Simu yake iliita bila majibu na hata niliporudia tena na tena mambo yakawa yale yale.
Sikuwa na hofu wala yale mawazo potofu juu ya Mke wangu. Na hiyo ilikuwa ni kwasababu naifahamu tabia yake ya kuacha simu chumbani wakati mwenyewe akiwa sebuleni.
Nikaendelea na kazi hadi kufikia saa nne nikamaliza. Nitatoka ofisini kuelekea kwenye maegesho ya magari. Nikiwa mbali nikaipata taswira ya ki-gari changu kidogodogo, Toyota Vitz yenye rangi nyekundu ambayo nilinunuliwa na kampuni na kupewa kama zawadi kwa utendaji wa kazi unaozingatia viwango.
Basi nikakiribia na kutoa funguo ambazo mara zote huzifunga kwenye Lux za suruali. Nikafungua mlango huku nikitabasamu.
"Hakika mimi ni mfanyakazi bora na mwenye mafanikio" nikajisemea moyoni na hiko ndicho kilichonifanya nitabasamu.
Lakini ghafla sura yangu ikabadilika, lile tabasamu likayeyuka na ndita zikachukua nafasi.
"Kila mwanaume mwenye mafanikio kuna mwanamke imara nyuma yake" nikasikia sauti ikinambia hivyo na hiyo ndiyo iliyofuta tabasamu langu.
Sikuwa nikikubaliana na sentensi hiyo kwa asilimia 80. Imani yangu ni kwamba si kila mwanaume mwenye mafaniko yupo Mwanamke imara nyuma yake. Sisemi hayo kwasababu ya Ushabiki au kwasababu mimi ni mwanaume, hapana.
Bali nazungumza kitu ambacho nakiishi mimi mwenyewe. Nina kazi nzuri, nina gari, nyumba na hata kipato changu si cha kulenga kwa manati. Yaani hata ingetokea ile kampuni ninayoitumikia ikafirisika leo hii bado ningeendelea kuishi kwa kujitanua kwa kutegemea miradi mingine niliyoianzisha.
Nina kibanda cha Pesa za mtandao, Kibanda umiza ambacho nimemuweka mtu maalum anaonesha mechi za mpira wa miguu na pia namiliki duka kubwa maeneo ya Tabata.
Lakini mafanikio yote hayo Mke wangu ambaye kimsingi ndiye alitakiwa awe mwanamke wa nyuma yangu wa kuhakikisha nafanikiwa hajachangia hata theluthi.
Labda sina bahati kama aliyokuwa nayo Baba yangu-- Mzee Shomari. Yeye alimuoa Khadija, mwanamke ambaye alijitahidi kadri ya uwezo wake kuhakikisha Mume wake anafanikiwa.
Jitihada zake zilinifanya nitamani kuoa na MWANAMKE KAMA MAMA YANGU.
Sio kwasababu Mama yangu alikuwa mweupe kama mimi, mwanya mdogo mdogo na vishimo mashavuni pindi anapotabasamu, kucheka au hata anapotamka baadhi ya maneno bali ni kwasababu ya jitihada zake za kufanikisha Baba yangu anaitwa Mwanaume hata anapokuwa nje ya nyumba yetu. Na si kuitwa mwanaume kwasababu ya kuvaa suruali na kuota ndevu tu. Hapana, bali kwa kuwa na kipato cha kukidhi mahitaji ya familia na ziada.
Sura yangu ilibadilka na kurudi kawaida baada ya kugundua kuwa nimetumia dakika mbili na sekunde kadhaa kuwaza mambo hayo. Nikafungua mlango wa ki-gari changu na kutumbukia ndani yake. Nikakiwasha na leo kikawaka bila matatizo ingawa hiyo haikuwa kawaida yake.
Mara nyingi kilikuwa kikinisumbua kwenye kuwaka, hakikuwa na tabia ya kuwaka mara moja unapokiwasha. Ilikuwa ni lazima kukilazmisha au hata kukisukuma kwanza. Nikarudi nyuma (kwa kupiga Reverse) kisha safari ya kuelekea yalipo makazi yangu ikaanza.
Niliendesha kwa mwendo wa taratibu sana kwani niliamini mwendo kasi haukuwa ukifanana na umri wangu; Miaka 30 na kadhaa, pia namiliki familia ya Mke na watoto wawili ambao wote bado wananitegemea. Wanangu wanasoma shule zisizo za Serikali na kwa pamoja nawalipia karo ya zaidi ya milioni moja kwa mwaka.
Hakika mwendo kasi haukunifaa, mtindo wa kuendesha gari kama
mwendawazimu uliwafaa vijana ambao hawakuwa na majukumu namna yangu.
Basi taratibu niliendesha gari yangu huku nikila muziki laini kutoka kwa baadhi ya vijana wa kitanzania walioamua kutumia sauti na akili zao kutuburudisha, kutuelimisha na hatimaye kujipatia kipato. Nyimbo mbili tu za dakika tatu na sekunde kadhaa kila moja zilitosha kunifikisha Buguruni.
Lakini mara manyunyu ya mvua yakatoa habari kwamba punde itanyesha mvua mkubwa, hapo nikaona kila mtu akijitahidi kufanya jihtihada za kuikabili mvua hiyo na punde ikaanza kunyesha.
Ilinyesha mvua kubwa na kunilazimisha kufunga vioo vya ki-gari changu japo nilijua hiyo ingelikuwa ni adhabu kwani AC ya gari yangu ilikuwa haifanyi kazi.
Mara taa za barabarani zikawa za kijani na kunirusu nitembee.
Niliendesha gari na dakika kumi na mbili baadaye niliwasili nyumbani, Kitunda. Ile mvua bado iliendelea kunyesha, tena huku nyumbani ndiyo ilikuwa kubwa zaidi. Nikaegesha gari mbele ya nyumba yangu, nikachukua simu tu na kuacha vitu vingine vyote garini ili visije kulowa. Nikateremka na kukimbia mpaka kwenye mlango wa nyumba, nikafungua kwa kuusukuma kwasababu ulikuwa umesindikwa tu na nikapita mpaka ndani.
'KIMYA' kilinikaribisha, sikusikia sauti ya Mke wangu wala watoto wangu. Nikajitupa kwenye sofa huku nikiita majina ya wanangu.
"Khadijaaa? Ally?" lakini sikupata jibu.
"Ashura Mke wangu nimerudi" nikapayuka hivyo baada ya kuona sikupata jibu toka kwa wanangu lakini sikujibiwa pia. Nikachukua simu na kumpigia Mke wangu mara baada ya kutafuta nyumba nzima bila kufanikiwa kumuona mtu yeyote. Simu ya Ashura nayo iliita bila majibu kama kawaida yake, hofu ikanizidi lakini si mawazo ya kwamba huenda mke wangu yupo kwenye michepuko kwasababu asingeweza kwenda huko kwa kubeba watoto wote.
Nilichanganyikiwa siku hiyo pengine zaidi ya siku yoyote ile duniani. Niliwaza kupiga simu kwa wakwe zangu lakini nayo niliona ni mapema sana, nilihitajika kuwatafuta zaidi na zaidi kabla ya kufikia hatua hiyo ambayo ingekuwa ya mwisho kabisa katika Operesheni yangu.
Nikapata wazo la kutoka ndani na kuelekea nyumba ya jirani kuuliliza. Nikachukua mwamvuli pamoja na tochi na kueleka huko. "Khadija alikuwa hapa siku nzima ya leo lakini aliondoka kwenye saa kumi na mbili za jioni" akanijibu Mama Alphonce, jirani yangu nyumba ya pili kutoka nyumbani; nilikimbilia hapo kwasababu ndiye jirani niliyemzoea zaidi na hata wanangu walikuwa wakipenda kucheza hapo haswa huyu mkubwa—Khadija.
Nilizidi kutoelewa nini kilikuwa kikiendelea, na wala sikutaka kumuuliza zaidi habari za Mke wangu kwani nafahamu jinsi wanawake walivyonatabia ya kuteteana. Hata kama angelikuwa amekwenda baa kuchuna buzi lakini Mama Alphonce angenidanya ili nisijue lolote.
Nikarudi nyumbani tena, nikaingia jikoni sehemu ambayo mwanzo sikuikagua. Hofu ilinizidi mara baada ya kuingia huko kwani nilikuta sahani kadhaa za udongo zimevunjwa, nikaogopa sasa. Nikahisi huenda kuna uvamizi umefanyika nyumbani kwangu.
Haraka nikatoka nje na kurudi tena kwa Mama Alphonce kuuliza lakini hata kabla sijabisha hodi mlango wa choo chao cha nje ulifunguliwa na akatoka Alphonce; mtoto wa miaka saba tu.
"Shikamoo Baba Ally" akanisalimu huku akisulubiwa na ile mvua ambayo mimi haikunipata kwasababu nilikuwa nimejikinga kwa mwamvuli.
Nikamshauri asogee barazani ambapo mvua isigemsulubu naye akafanya hivyo. "Unamtafuta Khadija?" akaniuliza lakini kabla hata sijamjibu kwamba ni ndio au hapana alitiririka.
"Khadija kaenda kumtafuta Ally, kasema kapotea tangu "akanambia lakini kabla hata hajanipa maelezo ya kutosha radi kubwa ilipiga, hapo akamsikia Mama yake akimuita naye haraka akakimbilia ndani na kuniacha nimeganda kama sanamu ya
Askari pale Posta.
Sikuona tena sababu ya kumuuliza kitu Mama Alphonce kwani tayari nilishapa picha ya nini kinaendelea. Kumbe mwanangu amepotea na pengine ndio maana hata nilipompigia simu Mke wangu hakutaka kupokea kwasababu alijua kuna hitilafu nyumbani.
Nikarudi kwangu na kuketi nikiwaza nifanye nini. Nilirudia tena kumpigia simu mke wangu lakini hakupokea kama kawaida yake na hapo nikiwa nimeshjua kwanini hapokei simu yangu.
Wazo la kunyanyuka na kwenda kuwasaka lilinijia na sikutaka kujishauri mara mbili, nikanyanyuka nikiwa na tochi pamoja na mwamvuli tu. Nikafunga mlango kwa funguo na safari ya kuitafuta familia yangu ilianza.
Mitaani hakukuwa hata na watu kwasababu mbili. Kwanza ni ile mvua kubwa iliyokuwa ikiendelea kunyesha lakini pia kwetu bado palikuwa ni kitongoji kipya, hakukuwa na watu wengi.
Nilivuka mitaa zaidi ya sita nikiitafuta familia yangu hasa mwananangu Ally ambaye nilipata habari kwamba amepotea. Nikiwa mtaa wa sabu kutoka nyumbani nikamuona mtu mbele yangu, sikumfahamu kwa sura kwasababu sikumuona mtu halisi bali taswira ya mtu kutokana na kule alipokuwako kuwa na giza nene. Lakini pia nilitamani kummulika kwa tochi niliyobeba lakini nikahofia kwamba pengine angechukia kumulikwa kama wengi wachukiavyo.
Lakini kitu nilichogundua kwa haraka ni kwamba mtu yule alikuwa ni mwanamke tena mtoto mdogo, hapo nikatamani awe binti yangu Khadija ingawa ingekuwa ngumu kwasababu niliamini kwamba Khadija ameondoka na Mama yake kumtafuta Ally ambaye inasemekana amepotea.
Mtoto yule alikuwa akitembea kuelekea nilipo, hana mwamvuli japo mvua kubwa ilikuwa ikinyesha. Nilimuonea huruma sana na nikanuwia kumsaidi pindi tutakapokaribiana hata kama si mwanangu.
Taratibu tukakaribiana, akiwa umbali wa mita chache hivi nikapata taswira yake kamili. Ni Khadija, binti yangu; Nikagundua hilo.
Tazama alivyolowana kwa mvua. Nguo chapachapa sambamba na kugongana meno kwa baridi. Usiku huu wa takribani saa sita yu-mwenyewe njiani anatembea, tatizo ni nini?
"Babaaa" alipayuka baada ya kung'amua kuwa aliye mbele ni Baba yake, akanikimbilia na kunikumbatia nami nikampokea huku nikipiga magoti ili kulingana nae, sikujali tope lililotapakaa ardhini, nilipiga magoti na kuchafua suruali yangu ya kitambaa yenye rangi nyeusi lakini yote ilikuwa ni kwasababu ya mwanangu.
"Babaa, Ally kapotea" akanambia Khadija huku sentensi yake ikitoka kwa mtetemeko kutokana na baridi na kilio alichokuwa akikishusha.
Nilijikuta natokwa chozi, na si kwasababu ya kupotea kwa Ally bali ile hali aliyokuwa nayo Mwanangu Khadija, ilinisikitisha kwa kweli. Hana hata viatu, miguu pekua kama Bata ingawa wiki moja tu iliyopita nilimnunulia Yebo-Yebo nzuri za manjano.
Lakini wakati yote hayo yanatokea Mama yao alikuwa wapi? Anafanya nini na mbona hakunijulisha kinachoendelea. Hakunijulisha kwamba mtoto kapotea au hata kupokea simu?
**************************
USIPATE SHIDA YA KUJIBU MASWALI YOTE HAYO, SEHEMU YA PILI ITAKUPA MAJIBU.
UKITAKA KUIPATA RIWAYA HII KWA HALAKA ZAIDI WAWEZA KUWASILIANA NA NDUGU MWANDISHI KWA NAMBA TAJWA HAPO JUU.
========
RIWAYA: MWANAMKE KAMA MAMA YANGU
MTUNZI: KELVIN DONATUS KAGAMBO
SIMU: 0713 48 28 16
FACEBOOK: KEV CLEVER KAGAMBO
SEHEMU YA KWANZA (1)
"Vuta picha ungelikuwa umezaliwa Mwanaume. Je, ungelithubutu kuoa Mwanamke wa sampuli yako?" Nakumbuka hiyo ndiyo ilikuwa sentensi yangu ya mwisho kwake kabla hajarejea Paradiso.
Pengine anaweza asikumbuke nguvu iliyobebwa na sentesi hiyo yenye maneno 12 tu, lakini binafsi naamini ilikuwa ni sentensi yenye nguvu kuu ndani yake. Sentensi ambayo ilikuwa na uwezo wa kubadili yabisi kuwa kimiminika au hata rangi nyeupe kurudi nyeusi.
Ndiyo; na hiyo ni kwasababu sikuzungumza sentensi hiyo kama jinsi mlevi anavyomtongoza baa medi, husema nakupenda licha ya kwamba neno hilo hutokea kwenye ndimi na si moyoni kama inavyohitajika.
Nilizungumza sentensi ile kwa HISIA kali na mguso wa hali ya juu na ndio maana mara tu baada ya sentensi ile nilitokwa na machozi, nikaingia ndani; chumbani, nikajifungia mlango.
Pengine alidhani labda nitaingia ndani na kuchukua kamba ngumu na madhubuti halafu nitajinyonga, lakini mimi si mpuuzi namna hiyo, nijihukumu kwa makosa ya mwenzangu, ni upuuzi ambao kamwe siwezi kuufanya.
Nakumbuka siku ile ilikuwa Jumatatu, kazi zilinibana haswa kiasi kwamba mpaka kufikia majira ya saa tatu za usiku bado nilikuwa kazini. Kwasababu nilikuwa ni Baba wa familia basi ilikuwapo kila sababu ya kuwajulisha wanafamilia yangu kwamba ningechelewa kurejea nyumbani siku hiyo.
Nilichukua simu na kumpigia Ashura--Mke wangu. Simu yake iliita bila majibu na hata niliporudia tena na tena mambo yakawa yale yale.
Sikuwa na hofu wala yale mawazo potofu juu ya Mke wangu. Na hiyo ilikuwa ni kwasababu naifahamu tabia yake ya kuacha simu chumbani wakati mwenyewe akiwa sebuleni.
Nikaendelea na kazi hadi kufikia saa nne nikamaliza. Nitatoka ofisini kuelekea kwenye maegesho ya magari. Nikiwa mbali nikaipata taswira ya ki-gari changu kidogodogo, Toyota Vitz yenye rangi nyekundu ambayo nilinunuliwa na kampuni na kupewa kama zawadi kwa utendaji wa kazi unaozingatia viwango.
Basi nikakiribia na kutoa funguo ambazo mara zote huzifunga kwenye Lux za suruali. Nikafungua mlango huku nikitabasamu.
"Hakika mimi ni mfanyakazi bora na mwenye mafanikio" nikajisemea moyoni na hiko ndicho kilichonifanya nitabasamu.
Lakini ghafla sura yangu ikabadilika, lile tabasamu likayeyuka na ndita zikachukua nafasi.
"Kila mwanaume mwenye mafanikio kuna mwanamke imara nyuma yake" nikasikia sauti ikinambia hivyo na hiyo ndiyo iliyofuta tabasamu langu.
Sikuwa nikikubaliana na sentensi hiyo kwa asilimia 80. Imani yangu ni kwamba si kila mwanaume mwenye mafaniko yupo Mwanamke imara nyuma yake. Sisemi hayo kwasababu ya Ushabiki au kwasababu mimi ni mwanaume, hapana.
Bali nazungumza kitu ambacho nakiishi mimi mwenyewe. Nina kazi nzuri, nina gari, nyumba na hata kipato changu si cha kulenga kwa manati. Yaani hata ingetokea ile kampuni ninayoitumikia ikafirisika leo hii bado ningeendelea kuishi kwa kujitanua kwa kutegemea miradi mingine niliyoianzisha.
Nina kibanda cha Pesa za mtandao, Kibanda umiza ambacho nimemuweka mtu maalum anaonesha mechi za mpira wa miguu na pia namiliki duka kubwa maeneo ya Tabata.
Lakini mafanikio yote hayo Mke wangu ambaye kimsingi ndiye alitakiwa awe mwanamke wa nyuma yangu wa kuhakikisha nafanikiwa hajachangia hata theluthi.
Labda sina bahati kama aliyokuwa nayo Baba yangu-- Mzee Shomari. Yeye alimuoa Khadija, mwanamke ambaye alijitahidi kadri ya uwezo wake kuhakikisha Mume wake anafanikiwa.
Jitihada zake zilinifanya nitamani kuoa na MWANAMKE KAMA MAMA YANGU.
Sio kwasababu Mama yangu alikuwa mweupe kama mimi, mwanya mdogo mdogo na vishimo mashavuni pindi anapotabasamu, kucheka au hata anapotamka baadhi ya maneno bali ni kwasababu ya jitihada zake za kufanikisha Baba yangu anaitwa Mwanaume hata anapokuwa nje ya nyumba yetu. Na si kuitwa mwanaume kwasababu ya kuvaa suruali na kuota ndevu tu. Hapana, bali kwa kuwa na kipato cha kukidhi mahitaji ya familia na ziada.
Sura yangu ilibadilka na kurudi kawaida baada ya kugundua kuwa nimetumia dakika mbili na sekunde kadhaa kuwaza mambo hayo. Nikafungua mlango wa ki-gari changu na kutumbukia ndani yake. Nikakiwasha na leo kikawaka bila matatizo ingawa hiyo haikuwa kawaida yake.
Mara nyingi kilikuwa kikinisumbua kwenye kuwaka, hakikuwa na tabia ya kuwaka mara moja unapokiwasha. Ilikuwa ni lazima kukilazmisha au hata kukisukuma kwanza. Nikarudi nyuma (kwa kupiga Reverse) kisha safari ya kuelekea yalipo makazi yangu ikaanza.
Niliendesha kwa mwendo wa taratibu sana kwani niliamini mwendo kasi haukuwa ukifanana na umri wangu; Miaka 30 na kadhaa, pia namiliki familia ya Mke na watoto wawili ambao wote bado wananitegemea. Wanangu wanasoma shule zisizo za Serikali na kwa pamoja nawalipia karo ya zaidi ya milioni moja kwa mwaka.
Hakika mwendo kasi haukunifaa, mtindo wa kuendesha gari kama
mwendawazimu uliwafaa vijana ambao hawakuwa na majukumu namna yangu.
Basi taratibu niliendesha gari yangu huku nikila muziki laini kutoka kwa baadhi ya vijana wa kitanzania walioamua kutumia sauti na akili zao kutuburudisha, kutuelimisha na hatimaye kujipatia kipato. Nyimbo mbili tu za dakika tatu na sekunde kadhaa kila moja zilitosha kunifikisha Buguruni.
Lakini mara manyunyu ya mvua yakatoa habari kwamba punde itanyesha mvua mkubwa, hapo nikaona kila mtu akijitahidi kufanya jihtihada za kuikabili mvua hiyo na punde ikaanza kunyesha.
Ilinyesha mvua kubwa na kunilazimisha kufunga vioo vya ki-gari changu japo nilijua hiyo ingelikuwa ni adhabu kwani AC ya gari yangu ilikuwa haifanyi kazi.
Mara taa za barabarani zikawa za kijani na kunirusu nitembee.
Niliendesha gari na dakika kumi na mbili baadaye niliwasili nyumbani, Kitunda. Ile mvua bado iliendelea kunyesha, tena huku nyumbani ndiyo ilikuwa kubwa zaidi. Nikaegesha gari mbele ya nyumba yangu, nikachukua simu tu na kuacha vitu vingine vyote garini ili visije kulowa. Nikateremka na kukimbia mpaka kwenye mlango wa nyumba, nikafungua kwa kuusukuma kwasababu ulikuwa umesindikwa tu na nikapita mpaka ndani.
'KIMYA' kilinikaribisha, sikusikia sauti ya Mke wangu wala watoto wangu. Nikajitupa kwenye sofa huku nikiita majina ya wanangu.
"Khadijaaa? Ally?" lakini sikupata jibu.
"Ashura Mke wangu nimerudi" nikapayuka hivyo baada ya kuona sikupata jibu toka kwa wanangu lakini sikujibiwa pia. Nikachukua simu na kumpigia Mke wangu mara baada ya kutafuta nyumba nzima bila kufanikiwa kumuona mtu yeyote. Simu ya Ashura nayo iliita bila majibu kama kawaida yake, hofu ikanizidi lakini si mawazo ya kwamba huenda mke wangu yupo kwenye michepuko kwasababu asingeweza kwenda huko kwa kubeba watoto wote.
Nilichanganyikiwa siku hiyo pengine zaidi ya siku yoyote ile duniani. Niliwaza kupiga simu kwa wakwe zangu lakini nayo niliona ni mapema sana, nilihitajika kuwatafuta zaidi na zaidi kabla ya kufikia hatua hiyo ambayo ingekuwa ya mwisho kabisa katika Operesheni yangu.
Nikapata wazo la kutoka ndani na kuelekea nyumba ya jirani kuuliliza. Nikachukua mwamvuli pamoja na tochi na kueleka huko. "Khadija alikuwa hapa siku nzima ya leo lakini aliondoka kwenye saa kumi na mbili za jioni" akanijibu Mama Alphonce, jirani yangu nyumba ya pili kutoka nyumbani; nilikimbilia hapo kwasababu ndiye jirani niliyemzoea zaidi na hata wanangu walikuwa wakipenda kucheza hapo haswa huyu mkubwa—Khadija.
Nilizidi kutoelewa nini kilikuwa kikiendelea, na wala sikutaka kumuuliza zaidi habari za Mke wangu kwani nafahamu jinsi wanawake walivyonatabia ya kuteteana. Hata kama angelikuwa amekwenda baa kuchuna buzi lakini Mama Alphonce angenidanya ili nisijue lolote.
Nikarudi nyumbani tena, nikaingia jikoni sehemu ambayo mwanzo sikuikagua. Hofu ilinizidi mara baada ya kuingia huko kwani nilikuta sahani kadhaa za udongo zimevunjwa, nikaogopa sasa. Nikahisi huenda kuna uvamizi umefanyika nyumbani kwangu.
Haraka nikatoka nje na kurudi tena kwa Mama Alphonce kuuliza lakini hata kabla sijabisha hodi mlango wa choo chao cha nje ulifunguliwa na akatoka Alphonce; mtoto wa miaka saba tu.
"Shikamoo Baba Ally" akanisalimu huku akisulubiwa na ile mvua ambayo mimi haikunipata kwasababu nilikuwa nimejikinga kwa mwamvuli.
Nikamshauri asogee barazani ambapo mvua isigemsulubu naye akafanya hivyo. "Unamtafuta Khadija?" akaniuliza lakini kabla hata sijamjibu kwamba ni ndio au hapana alitiririka.
"Khadija kaenda kumtafuta Ally, kasema kapotea tangu "akanambia lakini kabla hata hajanipa maelezo ya kutosha radi kubwa ilipiga, hapo akamsikia Mama yake akimuita naye haraka akakimbilia ndani na kuniacha nimeganda kama sanamu ya
Askari pale Posta.
Sikuona tena sababu ya kumuuliza kitu Mama Alphonce kwani tayari nilishapa picha ya nini kinaendelea. Kumbe mwanangu amepotea na pengine ndio maana hata nilipompigia simu Mke wangu hakutaka kupokea kwasababu alijua kuna hitilafu nyumbani.
Nikarudi kwangu na kuketi nikiwaza nifanye nini. Nilirudia tena kumpigia simu mke wangu lakini hakupokea kama kawaida yake na hapo nikiwa nimeshjua kwanini hapokei simu yangu.
Wazo la kunyanyuka na kwenda kuwasaka lilinijia na sikutaka kujishauri mara mbili, nikanyanyuka nikiwa na tochi pamoja na mwamvuli tu. Nikafunga mlango kwa funguo na safari ya kuitafuta familia yangu ilianza.
Mitaani hakukuwa hata na watu kwasababu mbili. Kwanza ni ile mvua kubwa iliyokuwa ikiendelea kunyesha lakini pia kwetu bado palikuwa ni kitongoji kipya, hakukuwa na watu wengi.
Nilivuka mitaa zaidi ya sita nikiitafuta familia yangu hasa mwananangu Ally ambaye nilipata habari kwamba amepotea. Nikiwa mtaa wa sabu kutoka nyumbani nikamuona mtu mbele yangu, sikumfahamu kwa sura kwasababu sikumuona mtu halisi bali taswira ya mtu kutokana na kule alipokuwako kuwa na giza nene. Lakini pia nilitamani kummulika kwa tochi niliyobeba lakini nikahofia kwamba pengine angechukia kumulikwa kama wengi wachukiavyo.
Lakini kitu nilichogundua kwa haraka ni kwamba mtu yule alikuwa ni mwanamke tena mtoto mdogo, hapo nikatamani awe binti yangu Khadija ingawa ingekuwa ngumu kwasababu niliamini kwamba Khadija ameondoka na Mama yake kumtafuta Ally ambaye inasemekana amepotea.
Mtoto yule alikuwa akitembea kuelekea nilipo, hana mwamvuli japo mvua kubwa ilikuwa ikinyesha. Nilimuonea huruma sana na nikanuwia kumsaidi pindi tutakapokaribiana hata kama si mwanangu.
Taratibu tukakaribiana, akiwa umbali wa mita chache hivi nikapata taswira yake kamili. Ni Khadija, binti yangu; Nikagundua hilo.
Tazama alivyolowana kwa mvua. Nguo chapachapa sambamba na kugongana meno kwa baridi. Usiku huu wa takribani saa sita yu-mwenyewe njiani anatembea, tatizo ni nini?
"Babaaa" alipayuka baada ya kung'amua kuwa aliye mbele ni Baba yake, akanikimbilia na kunikumbatia nami nikampokea huku nikipiga magoti ili kulingana nae, sikujali tope lililotapakaa ardhini, nilipiga magoti na kuchafua suruali yangu ya kitambaa yenye rangi nyeusi lakini yote ilikuwa ni kwasababu ya mwanangu.
"Babaa, Ally kapotea" akanambia Khadija huku sentensi yake ikitoka kwa mtetemeko kutokana na baridi na kilio alichokuwa akikishusha.
Nilijikuta natokwa chozi, na si kwasababu ya kupotea kwa Ally bali ile hali aliyokuwa nayo Mwanangu Khadija, ilinisikitisha kwa kweli. Hana hata viatu, miguu pekua kama Bata ingawa wiki moja tu iliyopita nilimnunulia Yebo-Yebo nzuri za manjano.
Lakini wakati yote hayo yanatokea Mama yao alikuwa wapi? Anafanya nini na mbona hakunijulisha kinachoendelea. Hakunijulisha kwamba mtoto kapotea au hata kupokea simu?
**************************
USIPATE SHIDA YA KUJIBU MASWALI YOTE HAYO, SEHEMU YA PILI ITAKUPA MAJIBU.
UKITAKA KUIPATA RIWAYA HII KWA HALAKA ZAIDI WAWEZA KUWASILIANA NA NDUGU MWANDISHI KWA NAMBA TAJWA HAPO JUU.