SEHEMU-23
️[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji737]
Usiku wa sokomoko katika Bonde la Mzakwe
Majira ya saa tano na nusu usiku, giza likiwa limetanda huku anga ikiwa imepambwa na idadi sufufu ya nyota na kipande kiduchu cha mwezi kilichojikata kuashiria tumeshaingia katika mwanzo wa mwezi mwandamo kwa mahesabu ya mzunguko wa mwezi.
Kachero Manu akiwa peke yake na mateka wake ndani ya gari yake aina ya "Subaru Forester" alikuwa ndio anaiacha taratibu barabara ya lami ya Arusha na kukata kona ya barabara ya kulia kuelekea barabara ya vumbi, yenye mashimo kochokocho yaliyojaza maji tobi kuonyesha mvua kubwa ilinyesha siku za karibuni. Pia njia hiyo inayoelekea kwenye shamba la mizabibu la DODEP ilikuwa na makorongo ya kutosha. Alikuwa anaendesha kwa kufuata maelezo toka kwa watekaji wa mkewe. Ambapo walimtaka asifuatane na mtu yoyote zaidi ya mateka wao Bwana 'Kareem Abdallah' peke yake.
"Simamisha gari hapo hapo ulipo kisha ushuke chini na Bwana Kareem" ilikuwa ni maelezo anayopewa Kachero Manu kupitia kwenye simu yake. Kila amri aliyopewa jibu likawa ni hewala! tu kwa Kachero Manu.
Maadui walikuwa wameshika mpini na yeye kakamata makali, hivyo wangeweza kumgeuza wanavyotaka. Alikuwa hawaoni walipojificha maadui zake. "Itakuwa wamejificha humu porini mapema sana, hivyo wamenichora mpaka namna nilivyoingia humu ndani ya eneo" aliwaza Kachero Manu huku akiwa amezima gari na kushuka na mateka wake ambaye bado alikuwa kwenye hali nzuri ya kiafya.
"Tembea mpaka kwenye ule mti wa mwarobaini uliopo mbele yako ukiwa na Bwana Kareem, hakikisha hauna simu wala silaha yoyote ile mfukoni". Kachero Manu akawa anatii kwa kufuata maelekezo aliyopewa. Alipotembea kwa mwendo wa kama dakika 3 akiwa hana hili wala lile, ghafla bin vuu likajitokeza gari linakuja kutokea pembezoni mwake upande wa kushoto kwa kasi huku limewasha taa zote kwa mwanga mkali.
Akiwa hajajua nini cha kufanya gari likawa tayari limeshafika likiwa limefungua mlango tayari, huku likiwa bado halijazimwa wakamdaka Bwana Kareem na kumtupia nyuma ya gari huku mkewe Kachero Manu nae akitupwa chini kama mzigo. Kisha gari likaondoka kwa mchepuko wa kasi kama gari za mashindano ya mbio kuelekea njia ile ile aliyoweka mtego Kachero Yasmine.
Mara moja bila kuzubaa Kachero Manu akambeba mgongoni mkewe akawa anakimbia nae kurudi kwenye gari yake aliyoiacha meta kadhaa aweze kwenda kumsaidia kachero Yasmine. "Pole sana baby, ndio matatizo ya dunia uliyoyapata hayana mwenyewe, haya uliyoyaonja ni thumuni tu yale ninayoonja mumeo kila siku katika kazi zangu" alisema huku anamuweka sawa kwenye kiti mkewe. Ambaye alijibu kwa ishara ya kutikisa kichwa tu kuashiria wapo pamoja katika shida na raha.
Alikuwa amevishwa vazi la kiislamu la baibui nyeusi lilisitiri mwili wake wote. Akawa analalamika baridi kali, ikabidi akilaze kiti na kuchukua koti lake na kumvika yeye kisha akamlaza kwa upole.
Wakati anajiandaa kuwasha swichi ya gari lake, ghafla akaanza kusikia mirindimo ya risasi mfululizo kutokea upande ule ule walioelekea wale magaidi. "Kazi imeanza Ustaadhati Yasmine anawabatiza magaidi kwa mtutu wa bunduki" alijisemea pole pole Kachero Manu.
Akaanza kulitoa gari taratibu kuelekea upande ule ule walioelekea magaidi. Akaendesha mpaka sehemu fulani yenye kichaka akaiegesha. Kisha akabeba mtutu wake kukimbilia eneo la tukio bila kuaga kwa mkewe, akimuacha anakoroma akiwa ameshonwa na usingizi mzito unaotokana na uchovu wa sulubu za watekaji zilizomkosesha mapumziko ya raha.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji737]
Kachero Yasmine akiwa amejificha kwenye fukutu la nyasi, akiwa amejitandazia nyasi mwili mzima ulikuwa huwezi kudhani kama amejificha mtu kwenye kichaka hicho. Mwili wake ukiwa umevikwa kombati maalumu zilizokuwa zimechafuka matope kutokana na kutuama kwa maji kwenye eneo alilokuwepo.
Alikuwa ameshajichimbia hapo kwenye kichaka kwa karibia saa tatu timilifu, huku akiomba Mungu magaidi wapite njia hiyo. Walijua fika hawawezi kupita njia kuu ya jirani na kambi ya jeshi watapewa kichapo cha mbwa koko. Kuna wakati bonge la joka lenye urefu zaidi ya futi 8 lilimtambaa mwilini kuanzia kwenye buti miguuni, na kutambaa mpaka kuja kutokezea kichwani kwa kupanda kwenye kofia yake na kutokomea zake kwenye kichaka, likiwa kwenye harakati zake za kuwinda mawindo yake. Kwa ujasiri mkubwa bila kujitikisa aliliacha limfanye linavyotaka.
Mbu nao hawakubaki nyuma kumletea kero ya udungaji wa maumivu, lakini hawakuwa kikwazo kwake kutimiza lengo lake. Kuna wakati upepo ulivyokuwa unapuliza na miti kutingishika, huku sauti ya vyura ikirindima kwenye vifereji vidogo vidogo. Popo nao walikuwa katika harakati zao za kujitafutia maisha usiku huo wanahama mti mmoja na kuhamia mwingine. Ulikuwa ni msitu wenye kuogofya hasa nyakati za usiku kwa mtu mwenye roho nyepesi. Ukichanganya sauti ya mvumo wa upepo, kelele za vyura, na mtikiso wa matawi ya miti kulikuwa kunapatikana burudani fulani ya sauti yenye kuvutia inayobembeleza kwa msikilizaji na mwili kupata raha. Hiyo hali ikawa inataka kupelekea kope za macho yake ziwe nzito, usingizi ulikuwa unataka kuanza kumnyemeleza na kumpiga dafrau kipindi cha hatari.
Lakini akikumbuka ukubwa wa nguvu za adui ambaye ana nguvu ya kiuchumi, askari watiifu wanaopiga kwa malengo ya kusimamisha utawala wa kiislamu na waliofuzu mafunzo, usingizi wote ukayeyuka kama samli ndani ya moto. Akashtukizwa na kelele za gari linalokuja kasi huku limewasha taa zote kuashiria kuna hatari. Likiwa kwenye umbali wa kama mita kumi akaikoki vizuri silaha yake aina ya "Submachine Gun" aliyoifanyia utundu kuongeza manjonjo yake.
Bila kujiuliza mara mbili mbili akaanza kuzifyatua risasi kama njugu mfululizo, huku akilenga usawa wa kiti cha dereva na abiria. Kachero Yasmine alikuwa ni mtaalamu wa matumizi ya mkono wa kushoto, hakukosi shabaha kijinga akikuwinda risasi. Lengo la kupiga mfululizo ilikuwa ni kuwachanganya maadui wajue kama wamezingirwa na wapiganaji wengi. Mbinu ilijibu vyema, magaidi walipigwa na taharuki, lilikuwa ni shambulizi la kushtukiza kwao hawakutegemea kuzingirwa kirahisi.
Walianza kupiga risasi mfululizo bila mpangilio wowote. Kachero Yasmine kuzima mzizi wa fitina, akabahatisha kubutua matairi ya mbele yote ya gari lao, kwa kuwa lilikuwa kwenye kasi kubwa likayumba na kwenda kujibamiza kwenye mti mkubwa na kuzalisha kishindo kikubwa, na kupelekea gari kupinduka vibaya zaidi ya mara nne, kisha likatulia tuli.
Akasubirishia kama robo saa kuona labda kuna mtego wametegewa akaona kimya. Akawa anachomoka porini huku anakuja wanguwangu kwa kujiamini, akashtukia risasi mbili zinapigwa uelekeo ule ule anakokwenda, akajitupa chini haraka haraka na kuanza kutambaa. Kachero Manu akaanza kuita kwa sauti ya kupaliza iliyokuwa inasikia vizuri "Yasmiiiinee... njoo game is over...!".
Kachero Yasmine alivyosikia hivyo akasita kujitokeza mpaka alivyoisikia tena na kuhakikisha ni sauti ya Kachero Manu akajitokeza mbele ya gari la maadui na kulakiwa na Kachero Manu ambaye nae ndio alikuwa anafika, wakakutana ndindaninda.
“Kazi zuri Kachero Yasmine, nilivyokuwa nazisikia njugu zinatemwa nikajisemea kazi ipo leo Mpemba kashapandisha maruhani yake, maana anuwai yako ya ufyatuaji wa risasi imejipambanua kwangu, wakasalimu magaidi wenzao huko kuzimu" alitoa pongezi Kachero Manu huku akamkumbatia akisifu umahiri uliomfanya awe kama mtazamaji mpira uwanjani, ambaye anashangilia magoli yaliyofungwa na wachezaji.
"Na wewe ahsante kwa kuokoa uhai wangu nilijua nimewamaliza wote kumbe kuna mmoja alikuwa ananivizia nije anidokoe vizuri" Kachero Yasmine alitoa shukrani kwa mwenzake. Ni ukweli tungerudisha jina tu Pemba maana alikuwa pale pembeni ya mti anakuvizia tu ujilete" alijibu Kachero Manu kiufahari. Mara moja bega kwa bega wakaanza upekuzi mle ndani ya gari aina "Jeep kibanda wazi" la maadui.
Wakakuta kulikuwa na magaidi wapambanaji wa kiume 4 pamoja na dereva wao, na mateka wao waliyemkomboa Bwana Kareem Abdallah wakiwa wote wamepoteza maisha. Huku tafrija ya damu ikiwa imetapakaa kwenye gari. Damu ambayo ilitokana na mipigo ya risasi kutoka kwenye silaha ya Kachero Yasmine na kutokana na majeraha ya ajali mbaya ya gari lao. Wakamkuta pia mwanamke mmoja akiwa bado anapigania roho yake amezimia anapumua kwa mbali lakini ana majeraha makubwa kichwani.
"Huyu tumkimbize hospitalini hapo jeshini, tuombe gari la wagonjwa wampeleke Hospitali ya Mkoa" alitoa ushauri wenye mbolea Kachero Yasmine. "Upo sahihi feli bilahi kupona au kutokupona ni majaliwa ya Mwenyezi Mungu" aliongea Kachero Manu kuonyesha kukubaliana na ushauri wa mwenzake. Wakati wanamuweka nguo zake vizuri ikaonekana bahasha nzito ngumu ya kaki imechimbiwa kwenye nguo ya ndani inachungulia. Ikabidi Kachero Yasmine aitoe, na kuanza kuifungua kwa kuchana gundi yake ngumu iliyogandishwa. Alipofanikiwa kuifungua zikajitokeza pesa za kigeni dola za kimarekani kitita kisichopungua dola $10,000 baada ya kuhesabiwa kwa haraka haraka. Kisha wakakuta na barua imevirigiwa kwenye bahasha ndogo. Akapatwa na udadisi wa kuifungua, alipoifungua tu, Kachero Manu kwa msaada wa tochi akaanza kummulikia Kachero Yasmine asome