mpasta
JF-Expert Member
- Jan 17, 2011
- 919
- 2,007
SEHEMU-24
Ilikuwa ni barua iliyoandikwa kwa maandishi ya lugha ya kiarabu. Akaisoma mpaka akafika mwisho, kisha akavuta pumzi kubwa Kachero Yasmine. "Ina nini hiyo barua?" alishindwa kuvumilia Kachero Manu maana alikuwa haelewi chochote kutoka kwenye ile barua, kwake ilikuwa ni makorokocho tu kama ya watoto wa chekechea.
"Usijali Bosi wangu, huyu tumuombee azinduke ana mengi ya kutuelezea tena atatufikisha mpaka kwa mama yake "Maso Maso", maana hii ni barua ya kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Huenda huyu ni posta wao. Wakafanya haraka kumuingiza kwenye gari kisha Kachero Yasmine akalikimbiza mpaka hospitali ya jeshi. Baada ya hapo Kachero Manu akapiga simu kwa askari wa kikosi maalumu waje kuondosha mizoga kimya kimya kabla hakujakucha na kuvuta hisia za waandishi wa habari.
Hii ilikuwa ni operesheni chinjachinja adui kimya kimya, mpaka gaidi wa mwisho atiwe mbaroni. Baada ya hapo akarejea kwenye gari lake na kumpeleka hospitali mkewe wamcheki afya yake kisha baada ya hapo ndio warejee nyumbani. Alikuwa anaonekana amesakarika kutokana na uchovu na njaa.














SURA YA KUMI NA MBILI
Ngome ya Al-shabaab ndani ya Wilaya ya Kilindi - Tanga
Watu 4 kwa idadi ambao ni wafuasi wa "Al-Shabaab" walifika Wilayani Kilindi tokea mwaka 2008. Walikuwa wametokea Somalia wakiwa wameiva vilivyo mafunzo ya ugaidi. Malengo ya Al-shaaab yalikuwa ni kusimamisha ngome zao imara katika maeneo mbalimbali ya Afrika Mashariki. Kuanzia Mombasa-Kenya, Tanga, Zanzibari, Rufiji-Tanzania na Pemba ya Msumbiji. Wageni hao walifikia katika Kijiji cha Lwande, kwa muda waliishi na wanakijiji wa Lwande, na wanakijiji wakawa wamewapokea kama waislamu wenzao.
Walikuwa ni watu rahimu na wenye tabia zenye kunukia mauwaridi kijiji kizima. Kila mtu alitamani awafanye kuwa ni marafiki wa familia yake au kama wakitaka kuoa au kuongeza wake basi waje kuolea kwenye mji wao. Walikuwa ni mahodari wa kazi mbalimbali kama kilimo na ujenzi majumba.
Kizuri zaidi walikuwa wanaonekana ni watu wanaomshiriki Mwenyezi Mungu kupita maelezo. Msikitini nako wakaaminiwa kuendesha baadhi ya vipindi vya swala. Walionekana wanasoma Kurani kwa kuipendezesha masikioni mwa msikilizaji.
Wakaanza kusambaza fitina za chini kwa chini kuwagombanisha waislamu wa kijijini wenyewe kwa wenyewe na viongozi wao bila wenyewe kujua kuwa wanapigwa majungu na wageni hao. Wanapita huku na kuzusha uwongo huu na wataenda kule na kuzusha zogo jipya.
Waislamu wa kijijini pale wakaanza kupoteza umoja wao, vurumai na kitimutimu mtindo mmoja kikaibuka, ikawa mwendawazimu kaingia nyumba ya shetani. Waumini wakawafurusha viongozi wao wa msikiti wakiwatuhumu kuwa hawana elimu ya dini, wanawasomea Qur'ani majaka na kuisoma kimakosa kwa kuimong'onyoa. Rungu la uongozi sasa wakakabidhiwa vijana hao wageni wa "Al-shabaab".
Ikawa ni kama kumpa paka kazi ya kulinda maziwa. Wakaanza sasa vibweka vyao baada ya kudhibiti uongozi. Baada ya muda walianza kutoa mafundisho ambayo hayaendani na utamaduni wa Kitanzania. Mfano wakaanza kufundisha elimu ya mazingira ni haramu mutlaki. Hivyo watoto wa Kiislamu wasome Madrasa pekee wasipelekwe shule za elimu dunia.
Wakaanza kupandikiza chuki dhidi ya waislamu wanaofanya kazi serikalini kuwa wamesharitadi. Wakifa wasizikwe kiislamu kwa sababu wanaitumikia serikali ya Kisekula isiyoamini dini. Kutokana na mafundisho hayo butu, yaliyojaa shonde. Baadhi ya wananchi wakang'amua wanapoelekea sipo. Wakaanza kuwahoji wapi wanatoa mafundisho hayo ya ajabu. Wakafarakana na wanakijiji wakajitenga na kununua eneo lao kisha wakajenga msikiti unaitwa "Madina".
Lengo kuupa msikiti wao jina hilo ilikuwa ni kufananiza kitendo cha Kiongozi wa dini ya Kiislamu Ulimwenguni, Mtume Muhammad (S.A.W) kufanya hijra kutoka Mji wa Makkah kuelekea Mji Madina alipofanikiwa kuisimamisha Dola ya Kiislamu.
Wafuasi wao sasa waliendelea kuongezeka na wengi wakitokea Jijini Dar es Salaam, Kigoma na Singida. Wengine walitokea nchi za jirani kama Kenya na Somalia. Kiongozi Mkuu wa msikiti huo akijulikana kwa jina la "Master" ambalo lilikuwa maarufu Kilindi nzima. Huyu alipachikwa jina la "Master" baada ya kuanza kuutumia msikiti wa Madina kama sehemu ya kufanyia mazoezi na mbinu za kigaidi.
Walifahamika kuwa ni magaidi walipoanza kunyanyasa wenyeji kwa kupora mashamba ya wenyeji bila fidia. Maelezo yao kwa wenyeji ilikuwa ni kwamba ardhi ni mali ya Allah, na wao wametumwa na Allah kusimamisha utawala wake duniani hivyo ni haki kwao kuichukua bila fidia. Idadi ya wageni katika kambi hii ikaanza kuongezeka zaidi kadri miezi inavyozidi kusonga. Baadae wakajitanua hadi katika msitu wa Dibungo, katikati ya Kilindi na Bagamoyo.
Katika msitu huo walihodhi ardhi yenye ukubwa wa ekari 500 iliyonunuliwa na Bwana Kareem Abdallah, Meneja wa "Chops Carwash & Garage". Katikati ya eneo hili wakajenga uwanja wa mazoezi. Kwa nje walijenga vibanda kuzunguka eneo hili, na hakuna mtu aliyeruhusiwa kuingia katikati ya msitu huu. Pia walijenga msikiti katika msitu huu, na walikuwa wanafanya mazoezi mara mbili kwa siku. Walikuwa wanafanya mazoezi saa 11 alfajiri baada ya kumaliza swala ya asubuhi na saa 11 jioni baada ya kumaliza shughuli zao za kilimo na ufugaji.
Uhusiano kati ya wafuasi hawa wa "Al-Shabaab" na wanakijiji wa maeneo yaliyozunguka kambi yao hii ulizidi kuzorota siku hadi siku. Wenyeji wengi ni wafugaji, lakini wafuasi hawa wa "Al-Shabaab" walianzisha utaratibu wa kutoza kodi ya mifugo au faini ya mifugo kwa ngombe wanaoingia kwenye msitu huu. Hatari iliyo kubwa zaidi, kambi hii ikawa inatumika kutoa mafunzo kwa vijana ambao wakionekana wameiva tayari wanasafirishwa kutoka Kilindi, kupitia Mombasa na kwenda Somalia kujiunga na kundi la al-Shabaab, wao na wake zao waliotafutiwa kupitia mtandao 'Facebook' kupitia akaunti ya 'NUSRA COMMITEE'.
Usiku walikuwa wanajiliwaza kwa kuangalia video, mikanda ya vita vya Jihadi sehemu mbalimbali duniani. Kulikuwa na mikanda yenye mafundisho ya "Al-Shabaab", yenye kusisitiza kuwa Afrika Mashariki imekamatwa na makafiri, hivyo wanafundishwa namna ya kuikomboa kijeshi. Mpaka kufikia mwaka 2013 ikawa ni kambi ya siri iliyojiimarisha vilivyo yenye zana za kivita toshelevu.
Hivyo "Maso Square The Duduman" baada ya kukamilisha kazi aliyotumwa Tanzania ya kulipua jengo la Wizara ya Mambo ya Ndani na kuua vigogo kadhaa na kuifanikisha vizuri aliteuliwa kwenda kuiongoza kambi hiyo kubwa ya Kilindi akitoa amri zote kutoka mafichoni. "Maso Maso" alikuwa anaishi katika mapango ya Amboni, yeye na wateule wake wachache na wanamgambo wao wachache.
Huku ndiko alikuwa akiletewa ripoti zote za kinachoendelea kwa njia ya maandishi tu. Alikuwa hatumii simu wala kompyuta wala chombo chochote cha elektroniki. Ilikuwa ni kama kujaribu kumpitisha ngamia kwenye tundu la sindano kama utataka kumkamata "Maso Square The Duduman". Mpaka kumfikia yeye ilitakiwa upambane na "Makomandoo" zaidi ya 25 ndio uwafikie kundi la "Wasagaliwa" 10 mgambo waaminifu. Wasagaliwa hao toka nchini Somalia walikuwa ni wanaume mahanithi ambao hawatamani mwanamke kimaumbile kwa namna walivyozaliwa, hivyo huwezi kuwashawishi wamsaliti "Maso Square The Duduman" kwa pesa kwa sababu wanalipwa vizuri wala kwa wanawake kwa sababu hawana matamanio.












Ilikuwa ni barua iliyoandikwa kwa maandishi ya lugha ya kiarabu. Akaisoma mpaka akafika mwisho, kisha akavuta pumzi kubwa Kachero Yasmine. "Ina nini hiyo barua?" alishindwa kuvumilia Kachero Manu maana alikuwa haelewi chochote kutoka kwenye ile barua, kwake ilikuwa ni makorokocho tu kama ya watoto wa chekechea.
"Usijali Bosi wangu, huyu tumuombee azinduke ana mengi ya kutuelezea tena atatufikisha mpaka kwa mama yake "Maso Maso", maana hii ni barua ya kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Huenda huyu ni posta wao. Wakafanya haraka kumuingiza kwenye gari kisha Kachero Yasmine akalikimbiza mpaka hospitali ya jeshi. Baada ya hapo Kachero Manu akapiga simu kwa askari wa kikosi maalumu waje kuondosha mizoga kimya kimya kabla hakujakucha na kuvuta hisia za waandishi wa habari.
Hii ilikuwa ni operesheni chinjachinja adui kimya kimya, mpaka gaidi wa mwisho atiwe mbaroni. Baada ya hapo akarejea kwenye gari lake na kumpeleka hospitali mkewe wamcheki afya yake kisha baada ya hapo ndio warejee nyumbani. Alikuwa anaonekana amesakarika kutokana na uchovu na njaa.














SURA YA KUMI NA MBILI
Ngome ya Al-shabaab ndani ya Wilaya ya Kilindi - Tanga
Watu 4 kwa idadi ambao ni wafuasi wa "Al-Shabaab" walifika Wilayani Kilindi tokea mwaka 2008. Walikuwa wametokea Somalia wakiwa wameiva vilivyo mafunzo ya ugaidi. Malengo ya Al-shaaab yalikuwa ni kusimamisha ngome zao imara katika maeneo mbalimbali ya Afrika Mashariki. Kuanzia Mombasa-Kenya, Tanga, Zanzibari, Rufiji-Tanzania na Pemba ya Msumbiji. Wageni hao walifikia katika Kijiji cha Lwande, kwa muda waliishi na wanakijiji wa Lwande, na wanakijiji wakawa wamewapokea kama waislamu wenzao.
Walikuwa ni watu rahimu na wenye tabia zenye kunukia mauwaridi kijiji kizima. Kila mtu alitamani awafanye kuwa ni marafiki wa familia yake au kama wakitaka kuoa au kuongeza wake basi waje kuolea kwenye mji wao. Walikuwa ni mahodari wa kazi mbalimbali kama kilimo na ujenzi majumba.
Kizuri zaidi walikuwa wanaonekana ni watu wanaomshiriki Mwenyezi Mungu kupita maelezo. Msikitini nako wakaaminiwa kuendesha baadhi ya vipindi vya swala. Walionekana wanasoma Kurani kwa kuipendezesha masikioni mwa msikilizaji.
Wakaanza kusambaza fitina za chini kwa chini kuwagombanisha waislamu wa kijijini wenyewe kwa wenyewe na viongozi wao bila wenyewe kujua kuwa wanapigwa majungu na wageni hao. Wanapita huku na kuzusha uwongo huu na wataenda kule na kuzusha zogo jipya.
Waislamu wa kijijini pale wakaanza kupoteza umoja wao, vurumai na kitimutimu mtindo mmoja kikaibuka, ikawa mwendawazimu kaingia nyumba ya shetani. Waumini wakawafurusha viongozi wao wa msikiti wakiwatuhumu kuwa hawana elimu ya dini, wanawasomea Qur'ani majaka na kuisoma kimakosa kwa kuimong'onyoa. Rungu la uongozi sasa wakakabidhiwa vijana hao wageni wa "Al-shabaab".
Ikawa ni kama kumpa paka kazi ya kulinda maziwa. Wakaanza sasa vibweka vyao baada ya kudhibiti uongozi. Baada ya muda walianza kutoa mafundisho ambayo hayaendani na utamaduni wa Kitanzania. Mfano wakaanza kufundisha elimu ya mazingira ni haramu mutlaki. Hivyo watoto wa Kiislamu wasome Madrasa pekee wasipelekwe shule za elimu dunia.
Wakaanza kupandikiza chuki dhidi ya waislamu wanaofanya kazi serikalini kuwa wamesharitadi. Wakifa wasizikwe kiislamu kwa sababu wanaitumikia serikali ya Kisekula isiyoamini dini. Kutokana na mafundisho hayo butu, yaliyojaa shonde. Baadhi ya wananchi wakang'amua wanapoelekea sipo. Wakaanza kuwahoji wapi wanatoa mafundisho hayo ya ajabu. Wakafarakana na wanakijiji wakajitenga na kununua eneo lao kisha wakajenga msikiti unaitwa "Madina".
Lengo kuupa msikiti wao jina hilo ilikuwa ni kufananiza kitendo cha Kiongozi wa dini ya Kiislamu Ulimwenguni, Mtume Muhammad (S.A.W) kufanya hijra kutoka Mji wa Makkah kuelekea Mji Madina alipofanikiwa kuisimamisha Dola ya Kiislamu.
Wafuasi wao sasa waliendelea kuongezeka na wengi wakitokea Jijini Dar es Salaam, Kigoma na Singida. Wengine walitokea nchi za jirani kama Kenya na Somalia. Kiongozi Mkuu wa msikiti huo akijulikana kwa jina la "Master" ambalo lilikuwa maarufu Kilindi nzima. Huyu alipachikwa jina la "Master" baada ya kuanza kuutumia msikiti wa Madina kama sehemu ya kufanyia mazoezi na mbinu za kigaidi.
Walifahamika kuwa ni magaidi walipoanza kunyanyasa wenyeji kwa kupora mashamba ya wenyeji bila fidia. Maelezo yao kwa wenyeji ilikuwa ni kwamba ardhi ni mali ya Allah, na wao wametumwa na Allah kusimamisha utawala wake duniani hivyo ni haki kwao kuichukua bila fidia. Idadi ya wageni katika kambi hii ikaanza kuongezeka zaidi kadri miezi inavyozidi kusonga. Baadae wakajitanua hadi katika msitu wa Dibungo, katikati ya Kilindi na Bagamoyo.
Katika msitu huo walihodhi ardhi yenye ukubwa wa ekari 500 iliyonunuliwa na Bwana Kareem Abdallah, Meneja wa "Chops Carwash & Garage". Katikati ya eneo hili wakajenga uwanja wa mazoezi. Kwa nje walijenga vibanda kuzunguka eneo hili, na hakuna mtu aliyeruhusiwa kuingia katikati ya msitu huu. Pia walijenga msikiti katika msitu huu, na walikuwa wanafanya mazoezi mara mbili kwa siku. Walikuwa wanafanya mazoezi saa 11 alfajiri baada ya kumaliza swala ya asubuhi na saa 11 jioni baada ya kumaliza shughuli zao za kilimo na ufugaji.
Uhusiano kati ya wafuasi hawa wa "Al-Shabaab" na wanakijiji wa maeneo yaliyozunguka kambi yao hii ulizidi kuzorota siku hadi siku. Wenyeji wengi ni wafugaji, lakini wafuasi hawa wa "Al-Shabaab" walianzisha utaratibu wa kutoza kodi ya mifugo au faini ya mifugo kwa ngombe wanaoingia kwenye msitu huu. Hatari iliyo kubwa zaidi, kambi hii ikawa inatumika kutoa mafunzo kwa vijana ambao wakionekana wameiva tayari wanasafirishwa kutoka Kilindi, kupitia Mombasa na kwenda Somalia kujiunga na kundi la al-Shabaab, wao na wake zao waliotafutiwa kupitia mtandao 'Facebook' kupitia akaunti ya 'NUSRA COMMITEE'.
Usiku walikuwa wanajiliwaza kwa kuangalia video, mikanda ya vita vya Jihadi sehemu mbalimbali duniani. Kulikuwa na mikanda yenye mafundisho ya "Al-Shabaab", yenye kusisitiza kuwa Afrika Mashariki imekamatwa na makafiri, hivyo wanafundishwa namna ya kuikomboa kijeshi. Mpaka kufikia mwaka 2013 ikawa ni kambi ya siri iliyojiimarisha vilivyo yenye zana za kivita toshelevu.
Hivyo "Maso Square The Duduman" baada ya kukamilisha kazi aliyotumwa Tanzania ya kulipua jengo la Wizara ya Mambo ya Ndani na kuua vigogo kadhaa na kuifanikisha vizuri aliteuliwa kwenda kuiongoza kambi hiyo kubwa ya Kilindi akitoa amri zote kutoka mafichoni. "Maso Maso" alikuwa anaishi katika mapango ya Amboni, yeye na wateule wake wachache na wanamgambo wao wachache.
Huku ndiko alikuwa akiletewa ripoti zote za kinachoendelea kwa njia ya maandishi tu. Alikuwa hatumii simu wala kompyuta wala chombo chochote cha elektroniki. Ilikuwa ni kama kujaribu kumpitisha ngamia kwenye tundu la sindano kama utataka kumkamata "Maso Square The Duduman". Mpaka kumfikia yeye ilitakiwa upambane na "Makomandoo" zaidi ya 25 ndio uwafikie kundi la "Wasagaliwa" 10 mgambo waaminifu. Wasagaliwa hao toka nchini Somalia walikuwa ni wanaume mahanithi ambao hawatamani mwanamke kimaumbile kwa namna walivyozaliwa, hivyo huwezi kuwashawishi wamsaliti "Maso Square The Duduman" kwa pesa kwa sababu wanalipwa vizuri wala kwa wanawake kwa sababu hawana matamanio.














