MKE WA RAIS
SEHEMU YA 44
Mwanamke Mweupe akatokea mbele yake tabasamu mdomoni.. Huyu hakuwa mwingine bali Inspekta Ummu Sammy. Alikuwa akisogea kwa mwendo wake wa Madaha.. Alipomfikia Mudy Wakasalimiana kwa kupeana mikono kisha wakaongozana mpaka sehemu ambayo ilikuwa maalumu kwa Maongezi.. Muda wote macho ya Mudy hayakutulia sehemu moja.. Yalikuwa yakitambaa na kuangalia kila kona ya chumba kile. Uwepo wa waziri wa mambo ya ndani kulimpa wasiwasi mkubwa kwa kuwa alifahamu kuwa alikuwa mmoja kati ya wanaopanga mkakati wa kufanya mapinduzi.. Kwahiyo kila alipokuwa akiongea na Inspekta Ummu Sammy macho yake yalikuwa yakitizama kwa hila katika kila dirisha na kila kona.. Alihitaji kufanya mAongezi na Afande Ummu Sammy lakini kila alipokuwa akitizama mazingira hayakumpa Ujasiri wa kufanya hivyo kwa kuwa hapakuwa Salama Zaidi... Wakati akiendelea kuongea hiki na kile bila kuonyesha Chochote cha maana mara simu Ya Inspecta Ummu Samy ikaita kuonyesha kuwa kulikuwa na Sms imeingia.. Mudy Bado alikuwa akiendelea kutizama nje Huku akimtupia jicho la chati Inspekta. Akamuona Inspekta Ummu Akiifungua simu yake na kuanza kuusoma ujumbe Ulioingia.. Punde uso wake ukapoteza Ile furaha.. Alionyesha kuwa na Wasiwasi katika macho Yake... Ingawa alijitahidi sana kujikaza, lakini alikuwa ameshachelewa kwani MUDY tayari alikwisha kigundua kitu kutoka kwake... Lakini Kabla hajaongea naye, akamuona Ummu Sammy akiinuka na kuufungua mlango Kisha kutoka Nje ya Chumba kile.. Mudy akaduwaa karibia dakika moja.. Mabadiliko katika Sura ya Afande Ummu Sammy yalimshangaza.. Hakuwahi kumuona Ummu akiwa na Wasiwasi na Yeye.. Hata walipokutana kule Cuba katika Mafunzo Ya Kijasusi hawakuwahi kufichana kitu, lakini hiki kilichotokea Muda Mfupi uliyopita kilimpa mashaka makubwa sana.
Akainuka na kuchungulia Huku na Huko.. Kwa mbali akamuona Ummu akiongea na Vijana wawili ambao walionyesha kuwa na wasiwasi Sana Huku Ummu Akigeuka kila wakati kutizama ndani Ya Ofisi Zao alipomuacha Mohamedi.. Mudy hakutaka kuchelewa kutoka ndani Ya Chumba kile.. Alichokifanya nikuinuka na kuuendea mlango, akaufungua kisha akatoka nje taratibu kwa kupitia Mlango wa Nyuma Ya Jengo.. Alipotoka Nje akawapita Askari Wawili Watatu kisha akapita uchochoro Huu na Ule Muda Mfupi baadae alikuwa ameshatoweka maeneo Ya polisi.
Alitembea kwa miguu safari hii akitaka kufanya Uchunguzi wake kuhusu kile ambacho kimewaleta Arusha.. Lakini kabla ya kufanya hivyo alichoamua ni Kuelekea Sanawari Eneo ambalo alikuwa akiishi mtu fulani ambaye alimjua Sana Mohamedi huku Mohamedi Akishindwa kumjua ni nani hasa. Hakuna kitu ambacho Mudy alikipenda kama kuitwa Sehemu na mtu ambaye hakumfahamu... Michezo ya Hatari kwake kilikuwa ni kitu cha kawaida na hata ikitokea Akaumizwa basi Yeye Huchukulia kama Bahati Mbaya kazini. Alijikagua hapa na pale.. Bastola Zake Mbili Zilikuwa zimetulia Sehemu husika huku upande Wa pili kukiwa na kisu Chake kikubwa ambacho alipenda sana kukitumia. Aliporidhika kuwa Yupo na kila kitu Chake akaianza Safari kuelekea Sanawari.
*****
upepo mwanana ulikuwa ukivuma na Kuwaburudisha watu waliokuwa wameketi sehemu wakipata moja moto moja Baridi.. Walikuwa watu wachache sana katika ukumbi ule lakini machoni kwa Jenifer Ulionekana ni Ukumbi wenye watu wengi sana.. Aliingia pale akiwa kama wateja Wengine. Leo hii alikuwa katika Jeans Matata Sana iliyoubana mwili wake, huku juu akitupia Tshirt Nyeupe pamoja na Raba nyeupe miguuni. Alipoingia alikwenda kukaa sehemu, akaagiza mishkaki mitano pamoja na Chupa kubwa ya Maji kisha akaomba aletewe na Ugali kidogo. Wakati akiendelea kusubiri Oda yake iletwe.. Akawaona wanaume wawili Wakiingia pale ukumbini.. Walikuwa ni Wanaume Aliyowajua sana.. Wanaume wale walipoingia waliangaza Huku na huko walipoonyesha kuridhika na Alichokuwa wakikitizama.. Wakaamua kuvuta viti na kukaa.. Ingawa walikuwa wamekaa lakini walikuwa hawaonyeshi Utulivu wa Macho yao.. Kila wakati walikuwa wakiangalia upande Fulani Huku wakati mikono Yao ikiwa Mifukoni.. Jenifer akavutiwa na Kilichokuwa kikitokea kwa watu wale.. Kila walipokuwa wakiangalia kule, Jenifer Naye alikuwa akipeleka Macho Yake Kwa Chati... Kila walichokuwa wakikifanya Jenifer alikuwa akitizama lakini muda wote hakufanikiwa kukiona kilichokuwa kikiangaliwa. Akiwa na Shauku ya kuona chochote, akashangaa Kumuona Mohamedy Akiingia akiwa Ametangulizana na Mwanadada Mrembo sana.. Akahamisha Macho Yake kumtizama Mohamedi.. Macho Yao Yakakutana! Wote wakatabasamu, lilikuwa tabasamu na Ishara fulani... Mudy Akazuga kutomuona Jenifer.. Akaendelea na Safari Yake.. Punde walikuwa wakivuta viti na kutaka kukaa lakini kabla hawajafanya Hivyo wakaingia Askari Wakiwa na Bunduki na kuongoza mpaka aliposimama Mohamedi..
'''Unahitajika kituoni Mohamedi, tunaomba tuongozane Muda huu na Usijaribu kufanya lolote kwa kuwa hutaweza Kurudi Dar es salaam Ukiwa hai'' ilikuwa Sauti Ya Inspekta Ummu Akimwambia Mohamedi.. Mohamedi Alimtizama Askari Yule kwa Muda kisha Kwa Kujiamini akamwambia.. NeNda nitakuja