Riwaya: Mke wa Rais

Riwaya: Mke wa Rais

MKE WA RAIS

SEHEMU YA 37

Alikuwa na Uwezo wa kuwaua kwa Risasi, lakini Mudy hakupenda kufanya hivyo... Kupita kwa kanali Jamila na luteni Sevenlee.. Kuliirudisha kumbukumbu Mbaya ya kifo cha George katika Kichwa Chake... Akakumbuka kiapo alichokiweka Juu Ya waliohusika na Mauaji ya George. Licha ya kiapo hicho lakini hakutaka kufanya haraka katika kukabiliana na watu wale. Baada ya kupitwa bila kuonekana Mudy alimshika Jenifer Mkono wakaondoka kuelekea katika Hoteli ile ile ambayo walitoka Sevenlee Pamoja na Jamila. Ilikuwa ni faida kubwa sana kupanga sehemu ambayo unajua kabisa Yupo adui yako.. Lakini hapo hapo adui akiwa hafahamu Uwepo Wako. Wakaingia Hotelin kama babu na bibi.. Kufika kwao mapokezi Wakapokewa na mwanadada ambaye hakusita kuonyesha mshangao wake hasa kwa watu ambao alikuwa akiwapokea kwenye Hoteli Yake. Muda mfupi uliyopita alitoka kuwapokea Vikongwe Wawili.. Na muda huu huu tena alikuwa akiwapokea vikongwe wengine tena wakiwa kwenye mavazi kama ya wateja walioingia punde tu.. Hilo lilimshangaza sana.. Lakini mshangao wake haukuwa wake tu, bali ulikuwa mshangao uliogundulika machoni kwa Jenifer na Mohamedi.. Mshtuko ambao hawakuuacha Uende kama ulivyokuja.. Walihitaji kuujua ulikuwa una nini na ulikuja kwa sababu gani... '''vipi mjukuu wangu mbona umeonyesha mshangao baada ya kutuona hapa? Au hatukutakiwa kufika hapa? Lilikuwa swali la Mtego kutoka kwa Mudy...

Mhudumu Yule akamuangalia Mudy Usoni kisha kwa sauti Yake Ya Uchangamfu akajibu.

''Hapana babu, tunawapenda sana watu kama Nyie.. Lakini kuna kitu kimenishangaza na kunishtua Siku Ya leo.''

Mudy akavutiwa na maneno yale .. Akazuga Kuuliza..

''kipi hicho kimekushangaza?''

Mhudumu akacheka tena lakini ndani ya kicheko hicho akanema kitu ambacho kilimvutia Mudy..

''siku ya leo nimepokea wageni wa aina yenu kama sita hivi.. Lakini hawa waliokuja hapa muda mfupi uliyopita ndio walionishangaza''

''Kuku shangaza kivipi mjukuu wangu!?'' hatimaye kwa Mara ya kwanza Jenifer akauliza.

''walikuwa wakionekana kama vijana licha ya mindevu na Mvi walizonazo hasa Yule mwanaume'' akajibu mhudumu wa ile hoteli.

Mudy na Jenifer wakaangaliana kwa sekunde, kisha Jenifer akamshukuru na kumwambia kuwa ilikuwa ni baraka kutembelewa na wazee kama Wao. Baada ya kuupata huo ukweli kutoka kwa Mhudumu yule.. Wakapewa Funguo na kuongozwa mpaka kilipochumba walichochagua.. Wakaingia ndani kwa kuongozwa na Mhudumu.. Baada Ya mhudumu kuondoka Mudy Na Jenifer wakaufunga mlango kisha wakakaa katika sofa ambayo ulikuwa katika chumba kile. Muda mfupi wa kukaa pale.. MUDY akatoa makablasha fulani ambayo alipewa na Mheshimiwa Rais akamkabidhi Jenifer ili ayatazame. Huku Jenifer Akitizama makablasha Yale, Mudy alikuwa ameichomoa simu Aliyopewa na Yule Marehemu kule kibaha. Akaitizama kwa Muda kisha kuiwasha... Muda Mfupi alikuwa akiipekua Simu hapa na pale.. Macho yake yalikuwa Yakiuzingatia Kila Ujumbe anaokutana nao.. Kulikuwa Ujumbe Mwingi Sana kutoka sehemu mbali mbali lakini katika Ujumbe Wote huo alivutiwa na Ujumbe mmoja kutoka kwa Mtu ambaye alikuwa akitumia Jina ambalo kwa kuliangalia tu halikuwa jina Sahihi... Ulikuwa Ujumbe wa kulazimisha kuuawa na kutekwa kwa Baadhi ya Mawaziri Ambao walikuwa wakipinga mpango fulani... Mtumaji Ujumbe Huyo alionekana kuwa na Taarifa nyingi Za Siri..

Hata kuondoka kwa Rais katika makazi Yake na kufichwa sehemu alikuwa akifahamu. Hapo ndipo ambapo Mudy alikuwa na Mashaka napo na pia kuwa na Mashaka na Usalama Wa Rais.. Kila alipokuwa akiendelea kuipekuwa Simu alizidi kukutana na ujumbe ambao uliandikwa kimafumbo.. Mudy hakuwa mgeni wa Maandishi Ya Kijasusi.. Alisoma kama kawaida. Baada ya kumaliza kusoma na Kuridhika Akaizima tena Simu.. Hapo ndipo alipokumbuka kuwa Chumbani mle alikuwa na Jenifer.. Akageuza Shingo kumtizama cha ajabu hakumuona Jenifer.. Alikuwa ametoka bila kumshtua Mohamedi.. Akafika kwenye meza ambapo alikaa Jenifer.. Akakutana na Ujumbe Ulioandikwa.. '''Nimetoka kidogo, nisiporejea tutaonana kesho''' Ulikuwa ni Ujumbe uliyomaanisha kitu.. Kitu ambacho Mohamedi Alikitambua Mapema... Akatabasamu kisha akajisemea Mwenyewe.. Kazi Imeanza... Muda mfupi nae alikuwa akikiacha kile Chumba.. Simu Aliyoipekuwa ilimpa wapi pa kuanzia.. Akatembea kuelekea Mlango wa Nyuma Wa Hotel ile. Hakutaka kusumbuka kuufungua.. Alichokifanya ni kuuruka Ule uzia na kutokea Mtaani.. Akatembea kukifuata kijiwe cha Madereva Wa tax.. Akaingia Kisha Akaomba Apelekwe Triple A... Aliamua kwenda kumsaka Mwanadada Ambaye alihisi atakuwa anaujua ukweli Wote Juu ya mpango wa kumpindua Rais na Yupi mfadhili wa mpango huyo.. Wakati tax ikiendelea kukata Mbuga ndipo akaikumbuka Simu Yake kuwa alitumiwa Sms kipindi alipovamiwa chumbani kwake.. Akaukuta Ujumbe .. Akaufungua na Kuusoma... Kuusoma Ujumbe ule kutoka kusikojulikana kukamfanya Atabasamu.. Ulikuwa Ujumbe Kutoka kwa mwanamke Anayejiita Revina Michael... Akahitaji Kuonana na Mohamedi Katika Hotel Ya Arusha Star Hotel. Mudy akatabasamu.. Gari Ikageuzwa.
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 38

Wakati tax ikikata mbuga kuelekea triple A. Mudy ikaikumbuka simu yake.. Simu ambayo ilikuwa na Ujumbe aliotumiwa kipindi akiwa msambweni kwenye chumba cha hotel aliyokuwa amefikia. Akaichomoa na Kuufungua Ujumbe ule.. Akakutana na Maandishi yaliyousisimua mwili wake.. Maandishi yaliyoandikwa katika namna ya kuwafumba wengine wasijue kilichoandikwa.. Ujumbe kutoka kwa mwanamke Aitwaye Revina Michael... Mwanamke ambaye anamuhitaji Mudy katika Hoteli Ya Arusha Star: muda mfupi tax ilikuwa ikigeuzwa kuelekea Arusha hotel badala Ya Triple A. Kichwa cha Mudy kilikuwa katika utimamu wake.. Bastola Zake mbili zilikuwa zimepachikwa sehemu ambazo zilikuwa Rahisi Kufikiwa na Mikono Yake.. Kila wakati alikuwa akitabasamu.. Hili halikuwa tabasamu la kuvutia watoto Wa kike.. Hili halikuwa tabasamu la utani bali lilikuwa Tabasamu la Mapambano na Uchu wa ushindi.. Hakuwa anamjua mwanamke Aliyemuita.. Lakini hilo halikumfanya Mudy kutokwenda ama kuogopa. Hatari kwake ilikuwa ni michezo Ya kawaida na Aliyoipenda Sana... Ndani Ya Dakika 30 tax ilikuwa ikisimamishwa Sehemu ya Maegesho Ya Magari katika hoteli ya Arusha. Kufungua mlango na kukanyaga Chini.. Akapokelewa na Harufu Ya Damu.. Watu kadhaa Walikuwa wamelaliana Wakiwa Maiti.. Mudy Hakushangaa katika hilo.. Akalipa na kuamuru Dereva kuondoka haraka...

Akaamua kupiga hatua kuingia katika eneo la hoteli.. Kila alipokuwa akipita alikutana na maiti.. Mkono Wake ukashuka mpaka ilipo bastola yake... Akatembea kwa namna ya kuvutia, akitazama na kuangalia hapa na pale... Punde alikuwa akiingia sehemu ambayo hutumiwa na wanywaji.. Hapo akakutana na kile alichokutana nacho Nje.. Watu walikuwa wametambarajika na kulaliana katikati Ya madimbwi Ya damu.. Mudy akavutiwa na kusonga mbele.. Aliupenda mtindo Wa kuangalia maiti.. Alipenda kuangalia damu.. Kila alipokuwa akitizama Damu ndipo alipokuwa akiipata Hamu ya kupambana.. Akauvuka ule ukumbi na kuufuata Uchochoro Ambao ulikuwa ukiingia ndani Zaidi.. Hatua Tano mbele Akakutana na mhudumu wa kike akiwa amechinjwa Shingo.. Kichwa kilikuwa sehemu Yake.. Mzubao ukamkumba Mudy na kuufanya Moyo Wake kuumia.. Kila kilichofanyika katika hotel ile kilikuwa kitendo Cha kinyama kupindukia.. Akampita Mwanamke Yule na kuingia ndani kabisa.. Bastola mkononi, macho Yakitizama huku na Huko.. Alikuwa makini kwa kila kitu, kwani damu bado ilikuwa Mbichi kuonyesha kuwa Mauaji Hayakufanyika muda mrefu.. Wakati anapita kwenye kibaraza ili kuingia Upande wa pili.. Akakiona kivuli Cha mtu. Kivuli ambacho kilipotea ghafla.. Kengele Ya tahadhari ikagonga ... Akaendelea kusonga Huku akielekea Upande Mwingine... Lakini hakuweza kufika popote.. Akapokea mateke matatu mfululizo.. Mateke ambayo Yalimyumbisha Mudy almanusura Kuanguka... Wakati akikaa sawa ili kumkabili Adui Yake.. Mudy Akapokea mvua Ya Ngumi.. Zilikuwa Ngumi Ziliorushwa kwa Ufundi zaidi.. Licha Ya Mudy kuzikwepa lakini kuna ngumi baadhi ziliiingia katika Mwili Wake..

Mudy Akaiona hatari Mbele Yake iwapo hatajipanga. Akarudi katika umiliki na Utimamu wa Akili Yake. Akamuona kiumbe mwenyewe.. Alikuwa mtu ambaye hakuonekana kwa Sura.. Mudy akamsubiri huku akijiandaa kwa mapigo.. Mtu yule akarudi kwa Mara Ya pili Safari Hii akibadilisha mapigo.. Alikuwa kwenye karate akichanganya kidogo na Kung fu.. Pigo la Kwanza Mudy Alilikwepa kwa Ustadi mkubwa.. Pigo la pili Mudy Akalizuia Kisha Akafyatuka pigo moja la Karate likampata na kumtupa Chini yule kiumbe.. Akainuka kwa kuchupa. Lakini bado hakuujua Wepesi Wa Mudy.. Akajivuta Mfano Wa Kinyonga wakati Huo huo akiachia Pigo Moja Aina Ya Tai Chi ambalo lilimtupa Chini yule kiumbe.. Mudy akamuwahi kwa kumrukia kwa Miguu yote Miwili.. Yowe kubwa likamtoka Yule mpiganaji, lakini hapo hapO Mudy Akamvuja Shingo na kumlaza Chini... Akajifuta na kuzidi Kuingia ndani.. Mara akasikia Vishindo Vya Mtu vikitokea Upande Wa pili Huku akiliita Jina la Mwenzake. Mudy Akaitika.. Kuitika kwa Mudy kukamfanya Yule Jambazi kuja Bila Tahadhali.. Akakutana na Mdomo Wa bastola Ukimuangalia kwenye Paji la Uso.. Akataka kupiga kelele.. Lakini Mudy Hakuruhusu Hilo.. Bastola Yenye kiwambo cha kuzuia Mlio ikakohoa.. Risasi Ikapenya Katikati ya Paji la Uso na kumtupa mbali... Alipotua chini alikuwa Maiti.. Mudy akamuwahi huku bastola mkononi... Akampekua hapa na pale.. Akakutana na Vitambulisho pamoja na Pesa kiasi kadhaaa.. Alipoangalia upande wa mifuko Ya Nyuma Akakutana na Bastola Moja pamoja na Kisu.. Mudy akavichukua vyote na kuvisunda katika mifuko yake yake Ya Siri. Akapiga hatua kuelekea ndani zaidi.. Akaupita Ukumbi wa Hoteli ile kwa ndani.. Kuupita ukuta ule Akaisikia Minong'ono kutoka katika Chumba Cha jirani na Aliposimama.. Kwa vile taa Zilikuwa Zimezimwa Ilimpa Mudy Urahisi Wa kusogea Karibu na Inapotokea Minong'ono... Alipoifikia Sehemu Ile akaangaza huku na Huko lakini hakuweza kuona Mtu kutokana na Giza.. Wakati akitafuta Njia ya kupita ili kuwaangalia Watu wanaoongea.. Akashtushwa Taa Kuwashwa kisha, Risasi Kusikika.
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 39

Taa zikawashwa na Risasi kuachiwa.. Mudy akachupa na kuangukia upande wa pili wa Hoteli.. Bado risasi zilikuwa Zikivurumishwa kuelekea kwake.. Alipochupa na kuangukia upande wa pili akachupa tena na tena alipokuja kutua bastola Yake ikakohoa... Lakini risasi zilikwenda patupu bila shabaha.. Ukawa ni mviziano wa hapa na pale.. Mudy wakati amejibanza kwenye ukuta akitizama kule zinapotokea Risasi, akamuona mtu, mtu ambaye alikuwa akihisi ndiye aliyemuita.. Alikuwa Revina.. Alihisi hivyo kwa kuwa alikuwa ni mwanamke aliyemfahamu sana.. Ni msichana aliyewatoroka muda mfupi uliyopita katika Hoteli Fulani.. Ni mwanamke ambaye aliwahi kumuokoa katika mikono Ya Marehemu Kepteni George.. Ni mwanamke Ambaye alipigwa risasi na kuuawa akiwa nae katika kimoja kati ya vyumba vilivyopo katika nyumba moja ya kulala Wageni maeneo Ya Sinza.. Lakini cha ajabu alikuwa akimuona kwa Mara ya Tano akiwa Yu hai na Mwenye Afya.. Hicho ndio kitu pekee kilichomtia hamu Mohamedi ya kumtafuta Binti Yule... Na hata alipotumiwa Ule ujumbe alijua ulitoka kwa mwanamke Huyu.. Lakini hapa akashangaa kumuona akiwa na Watu, tena watu ambao walionekana ni Wa moja katika fani Moja Ya mapigano.. Hilo likampa Ugumu katika ubongo Wake.. Hakutaka kuamini kama ameitwa ili kuingizwa Msambweni.. Bali kulikuwa na kitu ambacho kimejificha kutoka kwa mtu Yule.. Mohamedi Akatulia akitizama kile walichotaka kukifanya... Ghafla taa zikazimwa tena.. Mudy akahama alipo na kusogea pembeni... Mara taa zikawashwa tena... Kuwashwa kwa taa kulifuatiwa na tukio la Macho Ya Mohamedi kutua kwenye Miili miwili iliyolala Chini ikionyesha kutokuwa na Uhai tena. Kilichomchanganya Zaidi ni Watu waliouawa na kitu kingine ni kupotea kwa Yule mwanamke.

Sekunde iliyopita kabla ya Taa kuzimwa walikuwa hai tena wakiwa na mwanamke yule.. Lakini Sekunde ya pili taa kuwashwa walikuwa maiti.. Hiki ni nini? Huyu msichana ni nani? Yalikuwa mawazo kutoka kwa Mohamed.. Mawazo Ambayo Yalikoma Haraka pale alipousikia Mlio wa Ving'ora Vya Magari Ya Polisi.. Akapiga hatua na Kuuruka Uzia Wa Hotel.. Akatua upande wa pili, akaingia Uchochoro huu na ule, alipotokea mtaa Wa tatu akaupunguza mwendo na kuanza kutembea pole pole.. Kichwa chake bado kilikuwa kikiwaza juu ya alichokiona na juu ya wepesi Wa mwanamke Yule... Akatabasamu kama kawaida Yake.. Alitaka kuivuka barabara fulani ili kutokea upande wa pili, lakini akasita baada ya kumuona mtu akimfuata kwa Nyuma....

*******

ukumbi ulikuwa umechangamka huku watu wakiendelea kufurahia kile ambacho kilikuwa kikitendeka. Mwanamke Mrembo sana aliyevaa kigauni kifupi, Chepesi kilichouonyesha mwili wake kwa Asilimia kubwa. Alikuwa akiingia katika Ukumbi ule kwa mwendo wake wa madaha.. Kuingia kwa Mwanamke Yule kulizigeuza Shingo za Wanaume kadhaa.. Kila mmoja alikuwa akimtizama binti Yule kwa Jicho na namna Ya kipekee.. Mwendo na mikogo Ya binti Yule iliwafanya wanaume walikuja na wake Zao kugombana.. Kitendo Cha waume zao kugeuza shingo kumtizama msichana aliyekuwa akiingia kilionekana ni dharau kwao.. Binti Hakujali Hilo.. Alikuwa akitembea kana kwamba hakukuwa na kifo katika Dunia Hii.. Akakiendea kiti ambacho hakikuwa na Watu.. Akakivuta na kujibweteka Huku akiyaacha wazi mapaja Yake mazuri.. Hakujali alichokuwa Akikifanya.. Wanaume wakapagawa... Wakawa kila mmoja anamtupia Jicho Binti.. Jicho la taa na kutamani.. Alipokaa Mhudumu akafika... Akaagiza alichokitaka Huku akiendelea kuchezea Simu Yake... Hakuwa Msichana Mwingine bali Jenifer.. Alikuwa ameianza kazi katika Namna Ya Kipekee... Punde kinywaji Chake kikaletwa.. Akakipokea huku macho Yake mazuri na Yakurembua yakitizama kwa umakini.. Yalikuwa Macho Ya kumfutia kila mwanaume.. Lakini kwa upande mwingine Yalikuwa macho Yakijasusi na Yaliyojaa Utambuzi Wa Hali Ya Juu... Kitu alichokisoma kutoka kwenye makablasha Aliyopewa ni Mohamedi Ambayo Yalitoka kwa Rais Wa Nchi ndio Yaliyomfikisha katika Ukumbi ule akitaka kuonana na Mhudumu Mmoja ambaye ameonekana kutajwa katika Mauaji Ya Mke Wa Rais. Akaendelea kunywa Kinywaji chake huku macho yake yakiendelea kutizama Hapa na pale... Wakati amejuzuka na Kufuatilia kitu fulani akahisi kuguswa bega... Akainua Uso wake na kumtizama Mtu aliyeMgusa.. Macho yake yakakutana na Tabasamu kutoka kwa kijana mmoja mtanashati.. Alikuwa kijana mwenye Umri Usiopungua Miaka kama Ishirini na tano ama Thelathini.. Jenifer akamtizama kwa jicho lake Tamu na zuri sana... Lakini kijana Yule hakuongea kitu, alichofanya ni kumpa Kikaratasi kisha Yeye kuondoka pale... Baada ya kijana Yule Kuondoka Jenifer akakitizama kile kikaratasi na Kwa Mara Nyingine akatabasamu kisha Kuinuka na kuelekea kule alipotakiwa kwenda kwa Mujibu wa kikaratasi kile. Kila alipokuwa akipita wanaume bado hawakuisha kumtizama. Akaingia hapa na kutokea pale.. Akaifikia korido moja ndefu sana.. Akaipita na kukifuata Chumba fulani.. Alipotaka kuufungua Ule mlango akamuona mtu akitoka mle ndani.. Jenifer alimpisha kisha Yeye kuingia... Hamadi!!! Dimbwi la Damu....
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 40

HAMADI!! ALIKUTANA NA DIMBWI LA DAMU!!

Mwanaume alikuwa katikati ya Dimbwi la Damu, kisu kikubwa kikiwa kimesimama katikati ya kifua chake.. Jenifer akaurudisha mlango na kurudi nje.. Kurudi kwake nje ni kutaka kumtizama mtu aliyepishana nae.. Alipoangalia mbele akamuona muuaji Yule akipotelea.. Lakini kupotelea kwake kukafuatiwa na kumgeukia Jenifer kisha kumtizama huku akiachia tabasamu la Dharau. Jenifer hakutaka kujishuhurisha na mtu Yule.. Alichokifanya nikurudi ukumbini Huku akifikiria kile alichokutana nacho kule ndani.. Kuitwa sehemu kisha kukuta sehemu uliyoitwa kumefanyika mauaji.. Ilikuwa ni tafsiri kuwa kila walichokuwa wakikifanya kilikuwa kikijulikana na Inavyoonekana wapo watu ambao walikuwa wakifuatilia Nyendo zake bila Yeye mwenyewe kujua. Hilo sasa akaliona kuwa ni kosa kubwa.. Lakini kingine ambacho kilikuwa kikimtatiza ni kule kuletewa Ujumbe ule.. Kwa nini ameletewa Yeye wakati wakati hakuwahi kufika katika ukumbi ule? Kwa nini hakupelekewa mwingine akapelekewa Yeye? Nina aliyemtumia Ujumbe ule? Ni nani Aliyeuawa? Na kwa nini auliwe? Yalikuwa maswali Tata yaliyopigana Vikumbo katika Kichwa Chake.. Maswali ambayo yalimpa ukweli kuwa alikuwa akifanya kazi huku akifuatiliwa na Watu, watu ambao walikuwa wakimhisi ama Kumshuku kuwa ni Mwanausalama... Mlio wa Meseji kwenye Simu Yake ukamuondoa katika tafakuri Nzito.. Akaichomoa Simu Yake na kuutizama Ujumbe Huo.. Akakutana na Ujumbe kutoka kwa Mohamedy.. Ujumbe ambao Uliandikwa katika Lugha tata.. Katika Lugha ambayo ni lazIma Uwe mbobezi katika mbinu Za Kijasusi ndio unaweza kuitambua '''Kuwa Makini Kuna watu wanakuwinda Mama''' ulikuwa ni Ujumbe mfupi wenye maneno Yaliyousisimua Mwili Wake.. Akauridia Tena Kuusoma Ujumbe ule kwa Mara Ya pili, Akatabasamu na Kucheka.. Hakikuwa Kicheko Cha furaha ama kicheko cha kufurahishwa na Alichokisoma.. Bali kilikuwa kicheko cha kuwapumbaza Watu.. Watu ambao alijua wako maeneo fulani Wakimtizama na kufuatilia kila hatua Yake.

Muda Mfupi baadaye Akasimama tena, lakini safari hii hapa ilikuwa safari Ya bafuni.. Safari ambayo ilikuwa ni mwanzo wa kukipima kile alichoambiwa na Mohamedi.. Bastola Zake mbili zilikuwa sehemu fulani katika mwili wake.. Sehemu ambazo zilikuwa na uhakika wa kufikia na mkono wake pindi atakapobidi kuwa hivyo. Alikuwa akitembea katika Mwendo ule ule, Mwendo ambao uliwafanya wanaume kumgeukia na Kumtupia macho kila apitapo. Wakati Akiungaribia Mlango wakuingia bafuni, Macho Yake yakamuona Kijana mmoja... Kijana ambaye ndiye aliyemletea Ujumbe Muda mfupi uliyopita.. Jenifer hakumuangalia Wala Kumjali.. Aliendelea na Safari Yake huku mwendo wake ukiwa ule ule.. Akaufungua Vizuri Mlango wa Bafuni kisha akaingia... Kitendo Cha kuingia bafuni kikafuatiwa na Mlio wa meseji kwenye Simu yake.. Kwa Haraka Akaufungua..

'''Kuna watu wawili wanakufuata, kuwa makini'' ulikuwa Ujumbe mwingine kutoka kwa Mohamedi.. Jenifer akautizama kisha Akairudisha Simu sehemu Yake.. Sikunde mbili alikuwa akifungua mlango na kutoka Nje ya Bafu... Alipokanyaga mguu mmoja Nje.. Akashangaa Akivamiwa na Vijana Wawili.. Kumvamia kwao kulifuatana na Mapigo kadhaa Ya Kung fu.. Mapigo Ambayo yalikuwa Yakipita Patupu kutokana na Umahiri Wa Jenifer katika kukwepa Mapigo. Kila vijana wale walipokuwa wakibadilisha Mipigo, bado Walikuwa wakipiga patupu.. Punde wakajikuta wapo chini baada ya kupigwa mapigo mawili ya haraka... Wakainuka kwa haraka kukabiliana na Jenifer, lakini walijikuta wamechelewa.. Kwani walipokuwa wakiiinuka, Walimkuta Jenifer tayari Ameshachupa hewani na Mapigo Yake matatu Mfululizo Yakawaingia na kuwavunja Shingo Vijana Wale.. Alipotua Chini akawaruka watu wale na Kurudi ukumbini.. Alitembea kwa Madaha kama Hakukuwa na Tatizo akarudi mpaka alipokuwa Amekaa... Punde Ujumbe Mwingine kutoka kwa Mohamedi Ukaingia..

''''Usitumie kinywaji ulichokiacha'' kwa mara Nyingine Jenifer akacheka. Alitokea kuvutiwa na kile alichokuwa anakifanya Mohamedi, lakini kila alipokuwa akitembeza Macho Yake kwa hila katika Ukumbi ule, bado Hakuweza kumuona Mohamedi.

Akainuka na kuingia katikati ya umati wa watu na kuanza kucheza.. Kucheza kwake kukawavuta wanaume wa kwale kuanza kumzengea.. Ni katika Kucheza Huko ndipo alipomuona Mtu Ambaye alipishana naye kule Chumbani ambapo alimkuta Mtu akiwa Ameuawa. Alikuwa ni Yule Muuaji na Alikuwa akimuangalia Jenifer.. Kila Jenifer alipokuwa Akicheza na kutizama kule, Bado alimuona Yule mtu akiendelea kumtizama.. Akaendelea kucheza huku akimwaga na kujiachia.. Akatupa Macho tena pale alipokuwa Yule mtu.. Akakuta Patupu.. Hapakuwa na Mtu tena.. Yule kijana Waliyekuwa wakitizamana alikuwa Ameondoka kimaajabu.. Taratibu akaondoka katika Umati:. Akapiga hatua kuelekea Nje.. Hatua Ambazo alijua Zilikuwa Zikiangaliwa Na Kila mtu... Ghafla Taa Zikazimwa Ukumbi Mzima, wakati Huo huo Akijikuta AkipAa angani baada ya kupigwa ngwala matata sana na Hata alipokuja kuanguka Chini.. Akajikuta Yupo mikononi kwa mtu Asiyemjua.
 
Jamani, Nashukuru Sana kwa stori hii, cjaimaliza ila naona kama nakuwa mchoyo wa fadhila kutokuappriciate
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 41

Alipoanguka, akajikuta Yupo mikononi kwa mtu huku bastola akigonga kwenye paji lake la Uso.. Jenifer akajua kuwa yupo mikononi kwa mtu.. Akataka kujipindua ili kufanya kile alichotegemea lakini haikuwa Hivyo.. Alijikuta akitulizwa na pigo moja la kisogo akahisi kukiona kizunguzungu na mwisho akalihisi giza likiyaingia macho yake na hakuwa akijua tena kile kilichoendelea.

Wakati Yote hayo yakiendelea kumtokea Jenifer, Mohamedi alikuwa akishuhudia kila kitu. Alikuwa akikiona kitendo kile kupitia macho Yake Ya kijasusi, macho ambayo yalikuwa yakiona kwenye giza mithili ya bundi.. Hata pale Jenifer alipopigwa ngwala na kuanguka mfano wa Furushi kisha kudakwa Juu kwa Juu, Mudy alikuwa akitizama na kukihusudu kile kitendo. Alikiacha kwa muda kitendeke huku akihakikisha haondoi jicho lake katika tukio lile. Akatambaa mfano wa upepo wa asubuhi.. Punde akatokea Karibu na lilipokuwa likitokea tukio la Kutekwa kwa Jenifer.. Punde akalishuhudia pigo la kisogoni likimzimisha Jenifer.. Sekunde Iliyofuata akashuhudia Jenifer akibebwa Begani na watu wawili wakaanza kuuacha ukumbi ule wakitoka nje wakiwa na Jenifer.. Mohamedi hakuliacha hilo lisogee na liondoke machoni mwake.. Sekunde tu ilitosha kujitokeza kama mzimu mbele Ya Watekaji wale.. Kilikuwa kitendo ambacho hakikukusudiwa na wale Vijana.. Wakahamanika na kutetemeka.. Mohamedi Akatamani kucheka.. Hakuwa kumuona adui muoga, wala hakujua kama wapo maadui Waoga.. Siku Zote alizoea kupambana na watu wenye Roho ngumu kupindukia. Lakini hawa aliosimama nao hapa walionyesha kumuogopa kitendo ambacho kilikuwa sio sahihi kwa Jasusi aliyepigwa na Kuivaa kupindukia.

Mudy hakuwa na kitu cha kupoteza, akataka kumchukua Jenifer kutoka mikononi kwa Vijana wale, lakini wakati kitaka kulifanya Hilo, mmoja wa vijana wale akafyatuka mateke mawili mfululizo.. Yote yakapita patupu baada ya Mudy kuyakwepa kwa Ustadi wa Hali ya Juu... Wakati hajakaa sawa akamuona Yule kijana akija tena kwa mapigo mchanganyiko... Alikuwa akipiga karate na kung fu kwa pamoja.. Mudy alikuwa akifanyakazi Ya kukwepa kwa kuruka hapa na pale.. Alipokuja kutua chini, akamuona kijana katika usawa Wake.. Mohamedi Akafyatuka ngumi moja ya maana Ambayo ilimtupa Chini kijana Yule.. Mudy Hakutaka kutoa nafasi kwao, akaanza kumfuata Yule ambaye alikuwa amembeba Jenifer.. Yule kijana Baada ya kuona anafuatwa, alichokifanya ni kumtupa Jenifer Chini, kisha Yeye kuanza kutimua mbio. Mudy hakushughulika naye.. Alichokifanya ni kuwahi alipoangukia Jenifer... Alimuinua Kutoka pale chini na kuanza kumpa huduma ya kwanza ambayo ilikuwa ni mbinu fulani hivi Ya kijasusi.. Punde akamuona Jenifer akipiga Chafya, kisha akamuona Akifumbua Macho Yake Mazuri.. Akakutana na Uso Wa Mudy Ukitabasamu, nae akafanya kama Mudy Akatabasamu.

*****

Ilikuwa ni Asubuhi mbaya Yenye matukio mabaya yaliyolikumba Jiji la Arusha. Kila mtaa kulikuwa na vikundi vikijadili mauaji Yaliyotokea katika Jiji la Arusha na Vitongoji vyake. Kila mmoja alikuwa akiongea lake na Wengine walikuwa wakienda mbali Zaidi kuyahusisha mauaji Ya hapa Arusha na kile kifo Cha Mke Wa Rais. Wengi walisema kuwa walimuona kijana ambaye alikuwa akipambana na Watu wawili.. Kijana Yule alikuwa akipigana kama Mcheza Sinema Wa Kimarekani Garry Daniel.. Wengi walisema kijana alionyesha kuwa alikuwa Akipigana pale kwa sababu ya kumuokoa mwanamke mmoja ambaye alionekana kuingia bar muda mfupi akiwa katika mavazi Ya nusu Uchi. Licha Ya Stori Hizo za mitaani, Lakini Polisi nao na Watu wote wa Usalama walikuwa wamemwaga katika Jiji lote la Arusha Wakinusa hili na kufuatilia lile.. Kila kile walichokuwa wakikisikia mtaani walihakikisha lazima wakifuatilie na kuujua mwisho Wake. Sambamba na wapelelezi kutoka Makao makuu ya Jeshi la Polisi, pia kulikuwa na Maafisa usalama wa Taifa kutoka Makao makuu Jijini Dar Es Salaam na Wengine ambao waliwakuta pale pale jijini Arusha.

Arusha Yote ilikuwa ikipekuliwa Nje ndani, kila Hotel ilikuwa ikichunguzwa kwa Umakini wa Hali Ya Juu.. Vijana Wengi wageni kutoka Usalama wa Taifa walimwaga kila hoteli katika jiji la Arusha.. Wengi walionekana wakiuza Karanga na hata wengine walikuwa ni kama machizi na huku wengine wakionyesha kuwa ni Wateja. Kila kitu kilikuwa kikifanyika kwa Umakini mkubwa..

Majira ya Saa nne Asubuhi Mudy Alikuwa akitoka ndani ya hoteli ili kuingia mtaani kuangalia vitu viwili vitatu ikiwa ni pamoja na kunasa habari pamoja na kukutana na Watu kadhaa ambao alipanga wasaidie kumpa mawili matatu kuhusiana na Kile walichokifuata pale Jijini. Alishuka ngazi Taratibu huku mluzi Mdomoni. ALipofika Chini akaongoza mpaka mapokezi ambapo alikabidhi funguo na kuanza kutoka Nje Ya Hoteli. Alitembea bila wasiwasi Huku macho Yake Yakiangalia kulia, kshoto.. Alipotazama mwanzo kabisa wa mlango wa kutokea akamuona mtu anayemfahamu.. Lakini kwa jinsi Mtu Yule alivyojiweka ilimtajaabisha Sana Mohamedi.. Hakuwahi kusikia ugonjwa wala kurukwa kwa akili kwa mtu Huyu.. Lakini Mbona anaonekana Kichaa?
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 42

Mbele Ya macho Yake karibu na mlango wa kutokea akamuona mtu aliyemfahamu sana.. Alikuwa mtu ambaye alimshangaza kwa muonekano wake.. Hakuwa kusikia popote kuwa ameugua wala hawakuwa kumuona akiwa kichaa.. Sasa mbona huyu ni kichaa? Kengele Ya tahadhali ikagonga katika kichwa Chake. Akaendelea kutembea huku akimwangalia kijana Yule.. Kijana Ambaye Alikuwa kichaa wa kutupwa. Alipomfikia karibu Mudy akampita kwa kumtupia Jicho.. Macho Yao yakakutana.. Mudy Akauona mshtuko kutoka kwa kijana Yule.. Lakini hakumpa nafasi zaidi ya kumshangaa.. Mudy akapotea mfano wa kivuli kwenye chochoro Za Mji wa Arusha. Akaibukia katika meza ya muuza magazeti, akachukua magazeti kadhaa kisha akaondoka na Kurudi Zake Hotelini.. Aliupitia Ufunguo kwa mhudumu yule kisha kuongoza moja kwa moja kuelekea Chumbani kwake. Kitendo cha kukutana na vijana kadhaa kutoka Usalama Wa Taifa wakiwa wamezagaa kwenye jiji la Arusha kulimpa picha kuwa tayari mambo yamekucha hasa kutokana na Mauaji yaliyotokea Usiku Uliyopita. Akafungua mlango na kuingia chumbani kwake.. Alipoingia tu akahisi kuwa chumba chake kiliingiliwa na mtu kwani alikikuta kikiwa kimepekuliwa kwa Utaalam Wa Hali ya Juu, ambao kwa mtu wa kawaida Asingeweza kuligundua hilo. Akachunguza huku na Kule aliporidhika kuwa mpekuaji HakuChukua chochote, akatulia kitandani na kuanza kusoma vichwa vya habari vya Magazeti Yale...

******

alifumbua macho yake kutoka katika usingizi mzito.. Usingizi ambao hakuwahi kulala hata Siku moja.. Baada ya kufumbua macho yake akaanza kutizama Huku na Huko.. Akajikuta Yupo sehemu ngeni machoni mwake.. Sehemu ambayo hakuwahi kufika. Taratibu akaanza kuangalia Huku na Huko.. Alikuwa akitizama ili kukumbuka pale alipo... Alikuwa akitizama kuangalia uwezekano wa kuondoka.. Lakini hapakuonyesha ubaya, wala hapakuonyesha kile ambacho alikitegemea labda. Bado hakuwa katika kukumbuka vizuri.. Hapa niko wapi? Hatimaye akajiuliza.. Alitarajia kuziona pingu mikononi mwake, lakini hakuliona hilo.. Badala Yake alijishangaa baada ya Kujikuta yu Uchi wa Mnyama akiwa kitandani.. Akajikagua sehemu Zake kuangalia kama hajaingiliwa.. Alipokuta kila kitu kipo salama, sasa Akaanza kuvuta kumbukumbu Ya kilichotokea.. Akajaribu kuinua kichwa lakini maumivu Aliyojisikia kutoka nyuma ya kichwa chake Yakaanza kumpa kumbukumbu.. Kumbukumbu Ya kilichotokea katika Ukumbi Ule.. Ghafla mwili ukamsisimka baada ya kulikumbuka pigo alilopigwa wakati pale taa za ukumbi ule Zilipozimwa... Akakumbuka alipokuwa akitizamana na Mdomo wa bastola.. Mwisho akakumbuka pale alipoamshwa na Mtu.. Mtu Ambaye Alimtajua Wakati ule... Mtu ambaye kwa Wakati huu bafo hakuwa Akimkumbuka tena.. Akainuka na Kusimama katikati Ya kioo na kujitizama huku na huko.. Hakuwa mwingine, alikuwa ni Jenifer akiamka kutoka katika Usingizi Mzito.. Akasogea mpaka Sehemu fulani katika nyumba Aliyolazwa.. Akavikuta vitendea kazi Vyake Vyote Vikiwa vipo sawa sawia.. Bastola zake mbili.. Zilikuwa Zimetulia kabisa. Akaichukua na kuitizama.. Ilikuwa bado na Risasi Zake kamili.. Punde Mlango Ukagongwa...

Ulikuwa ukigongaji ambao aliutambua.. Akalitwaa taulo ambalo lilkuwa pale kitandani.. Akalitwaa na Kulitupia Maungoni Mwake.. Akapiga hatua kuelekea Mlangoni huku umbo lake matata likiruka na Kucheza cheza.. Basyola Yake Ilikuwa Imetangulia Mbele Kama Tai... Akaungiza ufunguo mahala pake.. Mlango Ukatii kwa kufunguka.. Akakutana na tabasamu la Mohamedi... Hakujali kama alikuwa na taulo kiunoni wala hakujali kuwa ndani hakuwa na Nguo Yoyote.. Aliufungua mlango Zaidi na Kuruhusu Mudy Kuingia ndani... Baada Ya Mudy Kuingia, Jenifer Aliufunga mlango na Kusogea mpaka karibu na Mohamed. Akasimama huku akinuangalia Mudy kwa Macho Yenye maswali Mengi... Mudy akaendelea kutabasamu huku wakiangaliana. Yalikuwa Macho Ya kazi.. Macho Ambayo Yaliongea kila kitu ambacho kilitokea Usiku Wa Jana.

*****

Kanali jamila na luteni Sevenlee walikuwa ni kati ya wapelelezi ambao walikuja Arusha kwa sababu ya kumdhibiti Mudy.. Wao hawakuwa katika Kile kikosi kilichotumwa kutoka Dar es salaam Ili kuongeza nguvu katika kukabiliana na mauaji ambayo yalianza kuutikisa Mji Wa Arusha..
Kutokana na Hilo na kuogopa kuonekana walikuwa wakijaribu kila wakati Kujibadilisha. Kujibadilisha kwao kulitokana na ukweli kuwa hawakutaka kuonekana wala Kujulikana na wanausalama wenzao.. Muda Mwingi walikuwa wakiutumia kwa kuvaa Sura Za bandia. Mchana Huu Uliwakuta wakiwa katika Hoteli Moja Ya kifahari wakionekana ni Watu tofauti na waliokutana hapo kwa ahadi Zao. Walikuwa wakiongea huku kila wakati Macho Yao yakizunguka katika eneo la Hoteli.. Wana usalama waliozagaa katika Hotel Zote kuliwapa Tahadhali Kubwa Sana.. Hivyo walikuwa wakiishi kwa kuhakikisha kuwa hawashtukiwi kwa Muda wote Ambao watautumia kuwepo Arusha. Lakini Wakati Wakilizungumza na Kulipanga Hilo.. Wakamuona Mudy Akiingia pale Hotelini... Alikuwa peke yake.. Akaongoza Moja kwa Moja mpaka Sehemu Ya Chakula.. Wao wakainuka na kutoweka lakini punde wakarud
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 43

Punde wakamuona Mudy akiingia kwa mwendo wa kawaida na kuelekea upande wa kushoto kwao.. Punde wakatoweka lakini hawakukaa muda mrefu Wakarejea tena. Safari hii waliingia kila mtu kwa wakati wake na kuelekea upande Wake. Macho yao yakimtizama Mudy katika Aina fulani ya kumhusudu.. Walitakiwa kumuondoa Mudy katika Uso wa Dunia kwa kuwa ndio mtu pekee Ambaye alikuwa akizuia Jambo lao kutokea. Jambo ambalo lingewafanya wao kuwa watu wazito katika Serikali Hii.. Lakini wangemuuaje Mohamedi? Ndio swali pekee ambalo liliwaumiza vichwa vyao.. Lakini Leo hii walikuwa wakimuangalia Mohamedi kwa ukaribu Sana.. Ukaribu Ambao ungeruhusu kumuondoa kwa Urahisi Sana..kila mmoja alikuwa na bastola mbili kiunoni kwake.. Bastola Zenye viwambo vya kuthibiti sauti.. Walihitaji sekunde kumi tu kumlipua Mudy.. Lakini wakiwa uelekeo wa macho Yao upo kwa Mohamedi, kikatokea kisanga cha wiki.. Mwanaume na mwanamke walionekana wakigombana huku mwanamke akilalamika kuwa amekopwa na alikuwa akihitaji kulipwa pesa yake. Tukio lile likavuta macho Ya watu.. Watu ambao kanali Jamila na Luteni Sevenlee Walikuwa wamoja kati ya watu waliovutwa na lile Songombingo.. Wakamsahau Mohamedi kwa Sekunde mbili.. Macho Yao wakayaelekeza kule. Lakini Sekunde Ya Tatu waliporudisha Macho Yao alipokuwa amekaa Mohamedi, Wakapokelewa na kiti pamoja na Meza lakini Mohamedi hakuwepo.

Wakaduwaa kwa sekunde wakiangaliana.. Walipotembeza macho yao katika kila kona ya Eneo lile.. Hawakumuona Mohamedi... Na kingine kilichowashangaza na kuwatia hofu ni kule kutoweka kwa mwanaume na Mwanamke Waliokuwa wakigombana Muda Mfupi.. Hapo kengele Za Tahadhari zikagonga vichwani mwao.. Hata vijana wao ambao walikuwa wamezagaa Eneo lote hawakumuona Mudy Wala wale watu waliokuwa wakigombana. Moyoni Wakajiona Kama wajinga kupindukia. Walikuwa wameachwa Solemba bila kutarajia. Wakainuka na kutoka ndani Ya hoteli ile wakionekana wakiwa na wasiwasi mkubwa.

***
Mudy alipoingia pale hotelini, kitu cha kwanza alichokifanya ilikuwa na kutambaza macho yake kona zote kwa namna ambayo asingeweza kushtukiwa na Mtu Yoyote. Wakati akiangalia hilo macho yake yakawaona watu wawili waliokaa pamoja.. Ingawa walikuwa katika Sura Za bandia lakini kwa mpelelezi kama Mohamedi kilikuwa ni kitu kigumu kumdanganya. Alishawajua walio mbele yake walikuwa watu gani.. Alichokifanya ni kuwapita kama hajawaona.. Ni wakati Yupo pale akawaona Watu wale wakiinuka na kutoka nje kisha Kurudi tena.... Waliporudi watu wale, akashangaa kuona vijana Wengine Watano wakiingia kila mtu akionekana ni mwenye safari Yake. Lakini muonekano wa vijana Wale ndio uliomfanya Mudy awatambue Mapema.. Walikuwa Wakitembea mfano wa majasusi Kutoka Shirika la Kijasusi la Urusi (KGB).. Sura zao zikionyesha uwezo walionao katika fani ya mapigano..

Hapo Mudy Akaihisi Hatari. Hakuwahi kuogopa mtu lakini hakupenda kuonekana akipambana mchana kweupe.. Muda Mwingi Alikuwa akiutumia mchana kwa sababu Ya kufanya Uchunguzi.. Hivyo kuwaona Kanali Jamila na Luteni Sevenlee Wakiwa kwenye Sura bandia kisha kuwaona vijana wale watano, kukampa mudy Tahadhali kuwa lolote linaweza kutokea pale. Hivyo akaanza kuwaza jinsi Ya kuondoka pale kuepusha Mapambano.. Lakini Punde akaliona Tukio la Mume na Mke kukwaruzana.. Mudy akawa haangalii tukio lile hasa baada ya kugundua kuwa mwanamke Yule alikuwa Jenifer.. Mawazo Yake yakamwambia Huu ni mpango Wa kukuondoa Hapo.. Sekunde Moja ilitosha kuwatupia macho wale ambao walionyesha kuzama kwenye tukio na Sekunde ya pili alitumia Kujiondoa Sehemu ile bila kuonekana na mtu yoyote.

Baada ya kuondoka pale, Dakika ya kwanza ili mkuta akisimamisha pikipiki na Dakika ya pili alikuwa akiondoka eneo lile. Moyoni Alikuwa amefurahi sana kugundua Njia Mbadala wanayotumia Kanali Jamila na Luteni Sevenlee.. Kwani alitambua kuwa kuigundua Mbinu Ya Adui yako ni Nusu Ya Kushinda Vita.

*****

pikipiki ikasimama mbele ya kituo kikuu cha polesi mkoa wa Arusha. Mudy akashuka, alipomaliza Kumlipa Dereva akaongoza kuingia ndani Ya kituo cha Polisi.. Wakati anaukaribia Mlango Wa kuingilia, Sms ikaingia kwenye Simu Yake.. Mudy hakuijali.. Alipoingia na kuhakikisha Yupo ndani kabisa Ya kituo, akaifungua Sms na kuisoma.. ''KUWA MAKINI, WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YUPO HAPO POLISI. PIA KUNA GARI MOJA AINA YA LAND CRUISER VX LILIKUWA LIKIKIFUATILIA... UKIMALIZA NJOO SANAWARI UTANIKUTA'' ilikuwa sms kutoka kwenye namba ambayo hakuwahi kuiona popote pale. Aliiangalie ile namba kwa Sekunde kama mbili hivi kisha Akairudisha Simu mfukoni.. Akapiga hatua mbili tatu akaifikia sehemu ambayo Ilikuwa ikitumiwa kama Mapokezi. Akasalimia kisha akaomba kuitiwa Afande Ummy Sammy... Kila afande alikuwa akimtizama Mudy Kwani hawakuwahi kumuona popote Zaidi Ya kumsoma tu hivyo kuonekana pale, kili kuwa kitendo ambacho kiliwafanya polisi Wachanganyikiwe kwa Furaha. Mohamedi hakubabaika na sifa na kushangaa kule.. Punde Akamuona Mwanamke Mweupe Mrembo Akitokea kwa Mbele Yake.. Tabasamu mdomoni..

JE ITAKUWAJE?
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 44

Mwanamke Mweupe akatokea mbele yake tabasamu mdomoni.. Huyu hakuwa mwingine bali Inspekta Ummu Sammy. Alikuwa akisogea kwa mwendo wake wa Madaha.. Alipomfikia Mudy Wakasalimiana kwa kupeana mikono kisha wakaongozana mpaka sehemu ambayo ilikuwa maalumu kwa Maongezi.. Muda wote macho ya Mudy hayakutulia sehemu moja.. Yalikuwa yakitambaa na kuangalia kila kona ya chumba kile. Uwepo wa waziri wa mambo ya ndani kulimpa wasiwasi mkubwa kwa kuwa alifahamu kuwa alikuwa mmoja kati ya wanaopanga mkakati wa kufanya mapinduzi.. Kwahiyo kila alipokuwa akiongea na Inspekta Ummu Sammy macho yake yalikuwa yakitizama kwa hila katika kila dirisha na kila kona.. Alihitaji kufanya mAongezi na Afande Ummu Sammy lakini kila alipokuwa akitizama mazingira hayakumpa Ujasiri wa kufanya hivyo kwa kuwa hapakuwa Salama Zaidi... Wakati akiendelea kuongea hiki na kile bila kuonyesha Chochote cha maana mara simu Ya Inspecta Ummu Samy ikaita kuonyesha kuwa kulikuwa na Sms imeingia.. Mudy Bado alikuwa akiendelea kutizama nje Huku akimtupia jicho la chati Inspekta. Akamuona Inspekta Ummu Akiifungua simu yake na kuanza kuusoma ujumbe Ulioingia.. Punde uso wake ukapoteza Ile furaha.. Alionyesha kuwa na Wasiwasi katika macho Yake... Ingawa alijitahidi sana kujikaza, lakini alikuwa ameshachelewa kwani MUDY tayari alikwisha kigundua kitu kutoka kwake... Lakini Kabla hajaongea naye, akamuona Ummu Sammy akiinuka na kuufungua mlango Kisha kutoka Nje ya Chumba kile.. Mudy akaduwaa karibia dakika moja.. Mabadiliko katika Sura ya Afande Ummu Sammy yalimshangaza.. Hakuwahi kumuona Ummu akiwa na Wasiwasi na Yeye.. Hata walipokutana kule Cuba katika Mafunzo Ya Kijasusi hawakuwahi kufichana kitu, lakini hiki kilichotokea Muda Mfupi uliyopita kilimpa mashaka makubwa sana.

Akainuka na kuchungulia Huku na Huko.. Kwa mbali akamuona Ummu akiongea na Vijana wawili ambao walionyesha kuwa na wasiwasi Sana Huku Ummu Akigeuka kila wakati kutizama ndani Ya Ofisi Zao alipomuacha Mohamedi.. Mudy hakutaka kuchelewa kutoka ndani Ya Chumba kile.. Alichokifanya nikuinuka na kuuendea mlango, akaufungua kisha akatoka nje taratibu kwa kupitia Mlango wa Nyuma Ya Jengo.. Alipotoka Nje akawapita Askari Wawili Watatu kisha akapita uchochoro Huu na Ule Muda Mfupi baadae alikuwa ameshatoweka maeneo Ya polisi.

Alitembea kwa miguu safari hii akitaka kufanya Uchunguzi wake kuhusu kile ambacho kimewaleta Arusha.. Lakini kabla ya kufanya hivyo alichoamua ni Kuelekea Sanawari Eneo ambalo alikuwa akiishi mtu fulani ambaye alimjua Sana Mohamedi huku Mohamedi Akishindwa kumjua ni nani hasa. Hakuna kitu ambacho Mudy alikipenda kama kuitwa Sehemu na mtu ambaye hakumfahamu... Michezo ya Hatari kwake kilikuwa ni kitu cha kawaida na hata ikitokea Akaumizwa basi Yeye Huchukulia kama Bahati Mbaya kazini. Alijikagua hapa na pale.. Bastola Zake Mbili Zilikuwa zimetulia Sehemu husika huku upande Wa pili kukiwa na kisu Chake kikubwa ambacho alipenda sana kukitumia. Aliporidhika kuwa Yupo na kila kitu Chake akaianza Safari kuelekea Sanawari.

*****

upepo mwanana ulikuwa ukivuma na Kuwaburudisha watu waliokuwa wameketi sehemu wakipata moja moto moja Baridi.. Walikuwa watu wachache sana katika ukumbi ule lakini machoni kwa Jenifer Ulionekana ni Ukumbi wenye watu wengi sana.. Aliingia pale akiwa kama wateja Wengine. Leo hii alikuwa katika Jeans Matata Sana iliyoubana mwili wake, huku juu akitupia Tshirt Nyeupe pamoja na Raba nyeupe miguuni. Alipoingia alikwenda kukaa sehemu, akaagiza mishkaki mitano pamoja na Chupa kubwa ya Maji kisha akaomba aletewe na Ugali kidogo. Wakati akiendelea kusubiri Oda yake iletwe.. Akawaona wanaume wawili Wakiingia pale ukumbini.. Walikuwa ni Wanaume Aliyowajua sana.. Wanaume wale walipoingia waliangaza Huku na huko walipoonyesha kuridhika na Alichokuwa wakikitizama.. Wakaamua kuvuta viti na kukaa.. Ingawa walikuwa wamekaa lakini walikuwa hawaonyeshi Utulivu wa Macho yao.. Kila wakati walikuwa wakiangalia upande Fulani Huku wakati mikono Yao ikiwa Mifukoni.. Jenifer akavutiwa na Kilichokuwa kikitokea kwa watu wale.. Kila walipokuwa wakiangalia kule, Jenifer Naye alikuwa akipeleka Macho Yake Kwa Chati... Kila walichokuwa wakikifanya Jenifer alikuwa akitizama lakini muda wote hakufanikiwa kukiona kilichokuwa kikiangaliwa. Akiwa na Shauku ya kuona chochote, akashangaa Kumuona Mohamedy Akiingia akiwa Ametangulizana na Mwanadada Mrembo sana.. Akahamisha Macho Yake kumtizama Mohamedi.. Macho Yao Yakakutana! Wote wakatabasamu, lilikuwa tabasamu na Ishara fulani... Mudy Akazuga kutomuona Jenifer.. Akaendelea na Safari Yake.. Punde walikuwa wakivuta viti na kutaka kukaa lakini kabla hawajafanya Hivyo wakaingia Askari Wakiwa na Bunduki na kuongoza mpaka aliposimama Mohamedi..

'''Unahitajika kituoni Mohamedi, tunaomba tuongozane Muda huu na Usijaribu kufanya lolote kwa kuwa hutaweza Kurudi Dar es salaam Ukiwa hai'' ilikuwa Sauti Ya Inspekta Ummu Akimwambia Mohamedi.. Mohamedi Alimtizama Askari Yule kwa Muda kisha Kwa Kujiamini akamwambia.. NeNda nitakuja
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 45

''Tangulia Nitakuja'' alijibu Mudy huku akiendelea kunywa kinywaji chake kwa utulivu mkubwa. Hakuwa akimuangalia tena Ummu.. Muda wote alikuwa akifikiria Kile kilichompeleka pale Arusha.. Alikwenda Arusha kwa Muda Mfupi na wakati akienda kule hakuwa amekusudia kukutana na Ummu Sammy. Bali hilo la kumuona lilikuja tu kama ajali baada ya kuona mambo yanaendelea kuwa ndivyo Sivyo. Lakini kilichokuwa kikimshangaza ni kule kumuona Ummu Sammy akimjia akiwa na lundu la maaskari Utadhani yeye ni kibaka. Bado Inspekta Ummu aliendelea kumtizama Mudy ambaye hakuwa anamtizama.. Alitamani kumuinua Mudy pale kitini alipokaa, lakini kila alipokuwa Akikumbuka kile ambacho alikifanya kule Israel na Hata Mexico pale alipofanikiwa kulisambaratisha kundi la Mafia, ghafla hakuwa na Ujasiri Huo.. Alichofanya ni kuendelea kumuangalia.. Hapo ndipo Mudy Alipoinua Macho Yake na kumuangalia Inspekta.. Macho Yao yalipokutana, Ummu alikiona kile ambacho hakuwahi kukiona hapo mwanzo.. Macho Ya Mohamedi Yalikuwa yamebadilika na kuondoka katika ule ukawaida.. Hakuwa na Ujasiri wa kuangaliana na Macho Yale, Alichokifanya nikuwaambia vijana Wake waondoke..

Aliondoka Akita katika Mshangao Mkubwa.. Aliondoka akijutia kile kilichompeleka pale Ukumbini.. Alimjua na kumfahamu Mohamedi Tokea muda mrefu sana.. Muda Ambao Walikuwa katika Mafunzo Ya kijasusi katika Ghuba Ya uajemi.. Alikumbuka kile ambacho walikuwa wakikifanya katika mapambano na mission Walizokuwa Wote.. Alikumbuka Siku Walipotumwa kwenda Kumkamata Afisa Wa Juu wa Shirika la Kijasusi la Marekani (CIA) Alexandrah panoles ambaye alikuwa ameasi katika shirika hilo. Alikuwa ni Mohamedi aliyefanya kitu cha kuhatarisha maisha Yake.. Alimbidi apambane na kundi kubwa la Watu kutoka Mossad na Hata KGB.. Ilikuwa ni kazi Iliyompa sifa kubwa Mohamedi na Kazi Ambayo ilimpa Nafasi Ya kuendelea kupata Ujuzi Zaidi na Zaidi katika Nchi mbali mbali Duniani. Ni kumbukumbu Hiyo iliyompa Hofu Inspekta Ummu Sammy.. Ni Historia Hiyo Iliyomfanya Ajiulize maswali Mengi Ambayo Hayakuwa na Jibu hata Moja.. Kwa nini apewe Oda ya kumfuatilia Mohamedi? Kwa nini apewe amri ya kumfuata Mohamedi amwambie ajisalimishe kituoni? Kuna kipi Kipo Nyuma ya Uwepo Wa Mohamedi Hapa Arusha? Hawamjui Mohamedi? Hawaitambui Kazi Ya Mohamedi? Kuna nini hapa nyuma mpaka Bosi wetu Aingilie hili? Kwa nini Mudy amekuja Hapa Arusha bila kunambia? Kuna Uhusiano gani Wa Mauaji yanayotokea Hapa Arusha na Uwepo Wake? Lazima ni Ujue ukweli huu... Alijiuliza Ummu Huku Akishuka garini akiingia ndani Ya kituo.. Akapiga hatua kukifuata Chumba ambacho hutumika kama Ofisi Ya Mahojiano. Akakinyonga kitasa mlango ukafunguka.. Akaingia huku akiwa katika mawazo mazito Sana.. Kuingia kwake ndani akakutana na kitu ambacho hakikutegemea kukikuta pale.. Alikuwa ni Mtu.. Mtu ambaye Muda Mfupi alikuwa Amemuacha Bar... Mbele Ya kiti cha Ofisini kwake Alimkuta Mudy akiwa amekaa akimsubiria. Kwanza alitaka kusita kuingia ndani, lakini alipogundua Macho Ya Mudy Yalikuwa yakimtizama, Ummu Sammy akaingia Huku akijilaumu kwanini alilichukua hili jukumu.

Baada Ya kukaa kwa Inspekta akainua mkonGa wa Simu ya ofisini.. Akabonyeza namba Kadhaa, punde Sauti nzito Ya kamanda wa polisi Mkoa Wa Arusha Ikasikika.. Yakafanyika Maongezi Mafupi sana.. Punde mlango wa Ofisi Ya Inspekta Ukafunguliwa.. Wakaingia Askari Wawili ambao walikuwa katika mavazi Ya kiraia.. Wakatoa Heshima kisha Wakampa taarifa Mudy Kuwa alikuwa akihitajika Ghorofa Ya Tatu Sehemu ambayo kulikuwa na Ofisi Ya Kamanda wa Polisi.. Mudy Hakuongea kitu, akainuka na kutangulia Yeye kuelekea Huko.. Alitembea huku akipiga mluzi.. Hakuwa katika Wasiwasi Wowote.. Akaingia kwenye lifti pamoja na Askari Wale waliovaa kiraia.. Punde lifti ilikuwa ikiondoka na baada ya dakika Moja ilikuwa Ikisimama ghorofa Ya tatu... Mudy Akashuka kama kawaida Akiwatangulia wale Askari.. Mwilini alikuwa na bastola mbili na Zilikuwa tayari kufanya Chochote pindi itakapo bidi... Alivyoshuka tu kutoka katika Lifti! Akahisi kengele za Hatari Zikigonga katika Kichwa chake.. Ukimya aliyoukuta pale Ulimaanisha kitu kingine kabisa.. Ulimaanisha hatari.. Akajiandaa Huku macho Yake yakiangalia Nyuma atokapo na mbele aendapo.. Hapo akakiona kitendo ambacho alikitarajia.. Mikono Ya watu waliomsindikiza ilikuwa imeingizwa mifukoni.. Mohamedi Hakuwa mbumbumbu katika hilo.. Hakutaka kusubiri mikono Ya Watu wale itoke katika Mifuko Yake.. Kilikuwa kitendo Kilichofanyika kwa Sekunde kumi tu... Alizuga kutembea kisha Akasimama ghafla.. Kusimama kwake kukafuatia na Samasoti Ya aina Yake.. Punde askari Wale walikuwa wako chini... Tena Sakafuni wakivuja Damu.. Mudy alikuwa amekwisha Achia Risasi ambazo Zilipenya Maungoni mwao wakati alipokuwa hewani.. Alipotua chini akairudisha Bastola sehemu Yake na Kuanza kupiga Hatua Kuelekea Ofisi Ambayo aliambiwa ndipo alipokuwa Akihitajiwa.. Akatembea kwa Ulivu pasipo na Wasiwasi.. Alipoufikia mlango hakuugonga bali alijizungusha mpaka Nyuma Ya Mlango Wa Siri.. Akaufungua....
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 46

Hakuugonga mlango uliombele yake bali alichofanya nikuzunguka kwa upande wa nyuma ambao kulikuwa na mlango wa Siri.. Alikuwa akitembea bila hofu.. Kuondoa mlio katika Bastola Yake kulisaidia kuwanyamazisha Watu wale bila kuwashtua Wengine. Ukimya ulikuwa umetawala.. Bastola ilikuwa mkononi kwa Mara nyingine akiusaka Mlango Wa Kuingilia. Alipoufika mlango akakishika kitasa na kukinyonga.. Sekunde alikuwa ameshazama ndani Baada Ya Mlango Kumtii.. Kuingia kupitia mlango Ule kukamfikisha Mohamedi katika ofisi pana.. Mbele Yake alikuwa akitizamana na Watu wawili ambao waliuonyesha mshangao mkubwa.. Kwani hawakuweza kujua Mohamedi Alipitaje kwa kuwa walikuwa wao wenyewe lakini Sekunde ya pili walikuwa na Mohamedi. Mbele yake palikuwa na kamanda wa Polisi Mkoa pamoja na Waziri Wa Mambo Ya Ndani.. Mudy akawasogelea kwa Utulivu, tabasamu mdomoni na bastola mkononi.. Alikuwa akiwaangalia mabosi wale wa polisi wakitizamana.. Nyuso Zao Zilikuwa zimewashuka huku wakionyesha hofu Ya Waziwazi.. Alipowaona Wamesawajika na hawakuwa wakijiamini.. Mohamedi akajikaribisha mwenyewe kwenye kiti.

Alikuwa amekaa kiti cha mbele kilichokuwa kikitizamana na waheshimiwa wale.. Bado bastola Yake ilikuwa mkononi na Hata tabasamu lake bado liliendelea kuwa pale pale Usoni... Licha ya kukaa na kusubiri kusikiliza Alichoitiwa, bado upande Wa RPC na Waziri Wa Mambo Ya Ndani walibaki kimya... Mudy akaona Auvunje ukimya.. Akajikohoza kisha kwa Sauti Yake tulivu akawaambia... ''Nimeitikia Wito Mheshimiwa Waziri.'' lakini bado hali ya ukimya Ilibaki kuwa pale pale.. Si kamanda wa Polisi mkoa wala Waziri Mwenyewe. Wote Walikuwa kimya kanakwamba hawakuwa wakiambiwa wao.. Mohamedi akawatizama tena na tena.. Kisha kwa Mwendo wake tulivu akainuka na kuwaaga kwa kuwaambia kuwa. '' kuna mizoga Yenu miwili hapo Nje mtaipeleka Mochwari. Akaufungua mlango na kupotea katika aina fulani Ambayo ilitia fora.. Bado Alikuwa ni Mohamedi Yule Yule aliyefanikisha Mission Ya kumchukua Afsa Wa CIA kutoka mikononi mwa KGB na MOSSAd.. Ni Mohamedi Yule yule aliyehatarisha maisha yake kwa kupambana na Kundi hatari la MAFIA Katika Jiji la Milan Kule Italia. Lakini pia Alifanikisha Mission Ya kuwakomboa Askari Wa Tanzania Ambao walitekwa na Kikundi Cha Waislam Wenye msimamo mkali cha ISLAMIC STATE pale walipokwenda kulinda Amani Katika Nchi Ya SYRIA. Ni katika oparesheni hiyo iliyofanya Jina la Mohamedi Kuingizwa katika Wapelelezi Mashuhuri waliowahi kutokea katika Bara la Africa hasa Tanzania.. Alikuwa Nyuma Ya Mtu kama JORAM KIANGO na alikuwa Nyuma Ya WILLY GAMBA... ni Umaarufu Wake Huo ambao ulimfanya Aizimwe na Shirika La kijasusi La Uingereza M16 na Hata Wale Wa SCOTLAND YARD katika mission Ya kwenda Kuwaokoa Raia Wa Uingereza Waliokuwa Wametekwa na Kikundi Cha Wanamgambo wa Alquida Kule katika Nchi Ya Pakistan. Huko
alikutana na Misukosuko na mateso makali ambayo hakuwahi kuyapata popote pale. Licha Ya hayo Yote lakini Risasi Yake Kutoka kwenye Bastola Yake.. Ilitosha kumnyamazisha kiongozi Wa kikundi kile. Alipokelewa na Waingereza kama Shujaa Wao lakini akawatoroka Muda Mfupi kabla Ya Kuhudhuria Sherehe Ya KumShukuru, Sherehe Ambayo Iliandaliwa na Malkia Wa Uingereza.

*****
baada ya kutoka makao makuu ya polisi.. Mohamedi hakutaka Kurudi Hotelini kwake.. Alichokifanya ni kuchukua tax na kumwambia Dereva ampeleke Sanawari.. Nia yake Ili kuwa ni kukamilisha kile ambacho wamekifuata Arusha na kuwahi kurudi Dar es Salaam Katika kumtafuta Muuaji wa Mke Wa Rais na Mpangaji mkubwa wa Mapinduzi. Tax ilitembea kwa Mwendo Wa kawaida Huku kila wakati Mudy akitupa Jicho lake kwenye kioo Kutizama kama alikuwa akifuatiliwa Ama la! Alikuwa na Mashaka ya kufuatiliwa kwa kuwa alimjua Ummu Sammy kuwa ni Mtu ambaye hakubali kupitwa na Kitu.. Alichokiwaza ndicho kilichotokea. Wakati akiendelea kuangalia kupitia vioo Vya Pembeni, Akaiona Gari Moja Aina Ya Toyota Prado ikiwaungia kwa Nyuma.. Ingawa kulikuwa na Magari matatu kabla Ya kuifikia Toyota Prado, Mohamed alilitambua kuwa linawafuata wao kwa kuwa ni Gari Ambayo aliiona pale Makao makuu Ya Polisi. Akamwambia Dereva Aongeze Mwendo.. Dereva Akafanya Hivyo... Punde akaiona Ile gari nayo Ikiongeza Mwendo.. Hapo akajua kuwa mawazo Yake Hayakuwa mbali na Ukweli. Walipofika Sanawari akamwambia Dereva Asimamishe. Dereva Akatii.. Mudy Akalipa Kisha Kuufungua mlango na Kutoka.. Alipo hakikisha tax imeondoka, naye akachepuka na kuingia katika Bar Moja.. Alipoingia Hapo Punde Meseji Ikaingia kwenye Simu Yake.. Akaichomoa Simu na Kuifungua Sms Kisha Kuusoma Ujumbe Ule... -''NIMEKUONA ULIPO LAKINI HAUPO MWENYEWE'' ulikuwa Ujumbe kutoka Kwenye Namba ambayo hakuifahamu lakini kwa Andishi lile akajua ni nani.. Akairudisha Simu mfukoni na kuendelea na Hamsini Zake.. Akaingia ndani Zaidi na kutafuta Sehemu Nzuri.. Alipokaa tu.. Ujumbe Mwingine Ukaingia kwenye Simu Yake. ''CHUMBA NAMBA 14 B . UTANIKUTA HAPO.. HAKIKISHA HUONEKANI NA WATU..

Mudy Akatabasamu Kisha Akainuka na kuelekea Huko.
 
Back
Top Bottom