Hongera mkuu hadithi nzuriMKE WA RAIS
Alikuwa akitizamana na sura ya mwanaume, sura ambayo haikuwa ngeni katika macho yake. Mbele yake Alisimama Mudy Akiwa kwenye mavazi Ya Mazoezi.. Mikononi mwake alikuwa amekamatia Sinia ambalo lilikuwa na Vikombe viwili vya maziwa... Mwanamke Yule akaganda kama sanamu.. Hakuwa akiamini kile alichokuwa akikiona mbele Yake. Licha ya kuishika bastola yake katika mikono yake lakini alikuwa ameshindwa kuitumia.. Muda wote Mudy alikuwa akitabasamu.. Tabasamu ambalo halikuweza kumlewesha mwanamke Yule na kumfanya amuamini Mudy.. Tabasamu ambalo lilikuwa tofauti katika macho Ya mwanamke Yule.. Mudy Hakumjali mwanamke yule.. Akaufungua Zaidi mlango na kwenda kulitua sinia lile katika meza Ile.. Muda wote alikuwa akitembea katika umakini wa hali ya Juu... Aliujua uwezo wa mwanamke Yule.. Ingawa hakuwahi kupambana naye lakini alishuhudia pale alipokuwa akipambana na kepteni George. Alipolitua Sinia lile akageuka Kutaka kumwambia mwanamke Yule asogee pale mezani.. Lakini Akashtuka baada Ya kukutana na midomo miwili ya Bastola Ikimtizama katika kichwa chake. Ingawa alikuwa akijiamini katika mapambano lakini Hakutarajia Kuiona bastola tofauti na Ile ambayo Aliiona pale mwanzo. Mudy Akaendelea kutabasamu kama hakukuwa na kitu cha hatari mbele yake.. Tabasamu ambalo lilivuka na Kuwa kicheko.. Kicheko chake kikaifanya Sura Yake Iwe katika mikunjo... Lakini kwa mwanamke Yule kicheko kile kilimfanya akipeleke kidole Chake katika kiwambo cha kuruhusu kutoka kwa Risasi... Hakuujua Uwezo wa Mudy na Hakumjua Mudy ni nani... Hakuipata nafasi Ya kuifyatua risasi yake... Sekunde mbili alikuwa Chini Ya Sakafu baada ya kupigwa Pigo moja la karate ambalo lilimmaliza nguvu na Kumfanya abaki pale chini Akitweta....
Mudy Hakutaka kumuendea pale na Vile vile hakutaka kumuua kwa kuwa alijua binti Yule alikuwa akijua mambo Mengi sana katika kisanga kile cha kuuawa kwa mke wa Rais.. Akamuendea pale alipoangukia kwa Sura Ya Upole.. Akamuinua na kumkalisha.. Akaanza kumfuta damu Iliyokuwa ikivuja ikitokea Puani...Kumfuta damu Mwanamke Yule kulimfaya Mudy Akumbuke Tukio ambalo Hatokaa Alisahau. Tukio ambalo litaendelea kubaki katika kumbukumbu Zake... Hasa pale aliporudi nyumbani na kuukuta Mwili wa mkewe na mwanawe kipenzi Wakiwa wamechinjwa. Ni Kisa hicho kilichomfanya awahurumie wanawake.. Licha Ya kuwahurumia huko lakini Bado alikuwa katili kwa kila mwanamke ambaye atakuwa kinyume na Sheria.. Akaifuta Ile damu Ya mwanadada Yule na baada ya Muda walikuwa wamekaa katika Meza Moja wakinywa maziwa Huku Waiongea Hili na Lile kama Watu ambao walikuwa wakifahamiana tokea Zamani.
*******
muda wa dakika kumi mbele wakaonekana wanaume wawili wakitoka katika hoteli ile.. Walikuwa wanaume watupu ambao walikuwa katika mavazi ya kanzu huku vichwa vyao vikiwa vimefunikwa kwa baraghashia.. Wakati Watu wake wakiondoka wakapishana na wanaume wengine watano ambao walikuwa Wamevaa mavazi meusi. Kupishana kwa Wanaume wale kukawafanya wanaume waliovalia Kanzu na baraghashia kutabasamu... Watu wale Watano Wakaingia katika Hoteli ile.. Kila mmoja alikuwa ameupeleka mkono wake Mfukoni.. Hawakuuliza mapokezi bali wakaongoza moja kwa Moja mpaka ghorofa Ya pili ambapo kulikuwa ndipo kwenye kitu walichokuwa wakikihitaji. Safari Ya Wanaume wale Ikaishia kwenye mlango Wa Chumba ambacho alikuwemo Mpelelezi mashuhuri Mohamed Pamoja na Mateka wake.. Kuufikia Mlango kukafuatiwa na Kitendo kingine cha Kuburudisha Machoni katika Kuutazama.. Mlango Ulipigwa teke kisha kila Mmoja Akizama ndani Huku akiruka samasoti na Kuangukiwa upande Mwingine.. Ukimya Wa Ajabu ukatawala Mle ndani.... Hata pale wanaume wale kila mmoja alipoingia hawakukuta kitu chochote Cha maana Zaidi Ya damu ambayo Ilionekana kusambaa katika Chumba kile. Wote Wakachoka Huku wakitizamana... Walikuwa wameachwa katika Mazingira Ambayo Kila mmoja akajua kuwa walikuwa wameingia katika Vita na Mtu mmbaya na mwenye mbinu kali Kushinda wao... Mmoja wa Vijana Wale akatoa simu na kuongea maneno mawili matatu Kisha Akakata..
*******
wanaume wale ambao walionekana katika mavazi Ya kanzu hawakuwa wote wanaume bali mmoja alikuwa mwanamke na Mwingine alikuwa mwanaume. Hawakuwa wengine bali alikuwa mohamedi na Yule mwanamke wakiondoka katika staili ambayo Ilikuwa vigumu Kushtukiwa. Na hata walipopishana na Wanaume wale watano walikuwa wamewatambua..
Safari Yao ikaishia maeneo sinza Mori, Wakatafuta Guest moja nzuri Wakalipia kwa kuandikisha MaJina ya Bandia, muda mfupi baadae walikuwa katika chumba kizuri Wakiwa wao wenyewe wawili... Mohamedi akamsaidia mwanamke Yule kulivua lile vazi kisha wakakaa kitandani Wakitizamana Huku kila mmoja Akisoma mawazo Ya Mwenzie... Walitizama kwa muda kisha Mudy akasimama na Kusogea pale ambapo Alikuwa amekaa Yule msichana, lakini hakufanikiwa kumfikia kwani Alishangaa mwanamke Yule Akijirusha na kumsukuma, Hapo hapo Akashangaa kumuona mwanamke Yule akivuja Damu katika Paji La Uso huku ametambalanyika Chini..
HALI ILITISHA SANA...
Mudy kibokoMKE WA RAIS
Mudy alikuwa Nyuma ya pikipiki akiifuatilia gari ya mtu yule aliyeondoka katika makaburi ya Kinondoni kwa wasiwasi mkubwa. Alikuwa amempa nafasi kubwa kwa kumuongoza mbele kwa tofauti ya Magari matatu ili kumfanya asije kushtuka kuwa anafukuzia.. Safari na mfukuzano wao uliishia tamati katika fukwe za bahari ya Hindi maeneo yale Ya masaki. Mudy hakutaka kusimama katika bar Ile bali alichokifanya ni kunyoosha mpaka katika bar ambayo ilikuwa katika eneo lile, akashuka na kuanza kurudi taratibu hasa baada ya kumlipa Dereva Yule. Macho Yake Yalikuwa yakiangaza kila Upande, Alikuwa anaujua mchezo wa watu wale.. Lakini kwa kuwa Alikuwa ameamua kufuatilia tukio la kuuawa kwa mke Wa rais hakujali sana katika lolote ambalo lingetokea. Alikuwa na kila kitu katika mifuko Yake... Akaendelea kulisogelea eneo lile kama Mtu wa Kawaida.. Akaingia katika Hoteli moja ambayo ilikuwa na Bar ndani Yake. Akavuta kiti na kukaa, mara Akamuona Mhudumu akadika haraka na kuuliza kipi ambacho angehitaji Mudy... Huku macho Yake Yakiangalia kwa chati kila mtu katika bar ile, Mudy Akaomba Aletewe Mzinga Wa konyagi... Kuagiza kwake mzinga kukawa kama kumemzubaisha mwanadada Yule... Hata pale Mudy aliporudia tena yule mhudumu alionyesha Kusita.. Lakini kile ambacho hakuna Ambaye amekitarajia kutokea, kikatokea.. Dakika moja mhudumu alikuwa ameduwaa na Ndani Ya Sekunde Ya dakika Ya pili, Mudy Akashangaa kumuona Mhudumu Yule akipaa angani na Kwenda Kuanguka Umbali Mrefu kutoka pale alipokaa Mudy.. Damu Nyingi Ikimvuja katika kifua Chake
Mudy Akaduwaa kwa sekunde na Sekunde Iliyofuata Alikuwa Akichupa na kudondokea upande wa pili wa ukuta wa Bar ile.. Akachomoa bastola Yake tayari Kukabiliana na chochote.. Sehemu Yote Ilikuwa tafrani Huku Wa hudumu wakiangua vilio kupita kiasi... Macho Ya Mudy hayakuwatazama watu waliokuwa wakilia na Kupiga kelele, bali Macho Yake makini Yalikuwa Yakikitazama Chumba ambacho kilikuwa katika Ghorofa Ya nne.. Dirisha Ya Chumba kile lilikuwa limefunguliwa kwa Upenyo Mdogo sana.. Upenyo Ule ungekuwa si Lolote kwa mtu Wa kawaida.. Lakini Kwa Mudy Ulikuwa ni Zaidi Ya Kile ambacho kingedikiriwa na Wengine.. Akajiondoa taratibu na Kuifuata lifti Ya hoteli ile na Muda Mfupi alikuwa katika Korido katika Ghorofa Ya Nne kukifuata kile Chumba Huku mkono wake Ukiwa juu Ya bastola Yake. Akatembea kwa Haraka.. Akakifikia kile Chumba, Akatulia kwa kama Sekunde kuangalia Usalama kwanza kama kutakuwa na Yoyote,,, lakini ukimya Ulikuwa imetawala na Hapakuwa na Mtu Yoyote.. Mudy Akauendea mlango na kujaribu kukinyonga kitasa, akashangaa kuuona Mlango ukifunguka. Macho Yake Yakaangalia kwa Chati na Muda mfupi alikuwa Chumbani huku bastola Mkononi.. Mbele Ya macho Yake Alikuwa Akitizamana na Tukio la Kutisha.. Mtu aliyemfuatilia Kutokea kwenye makaburi Ya kinondoni alikuwa Ameuawa kinyama mle chumbani. Mwili wake Ulikuwa Uchi wa Mnyama Juu Ya kitanda Huku Kisu kikubwa kikiwa katika kifua Chake.. Hali ilikuwa ikitisha sana.. Kwa Mara Ya kwanza Mudy Akahusudu uwezo wa mtu Aliyefanya Mauaji Yale... Akauangalia Mwili wa Marehemu Huku macho Yake Yakizunguka katika Chumba kile.. Hapo Akavutiwa na Kitu Ambacho Alikuiona Pembeni Ya Maiti Yule.. Zilikuwa Picha Za Hayati Mke Wa Rais Akiwa Amepiga na Mwanaume Yule Aliyeuawa Pamoja na Mhudumu ambaye Aliuawa Muda Mfupi uliyopita, Wakati mtu wa Tatu katika Picha Ile alikuwa ni Yule msichana Aliyeuawa kwa Risasi kule Hotelini Sinza lakini akaja kumuona Akiwa Hai... Akainama ili Kuichukua Picha Ile, lakini akasita baada ya Kusikia mtu Akimpigia makofi Kutoka Nyuma Yake... Akageuka Huku tabasamu Usoni... Akajikuta Akitizamana na mdomo Wa bastola kutoka kwa Mtu ambaye Alimjua na Kumtambua... Hakuwa Mwingine Bali Alikuwa Mkurugenzi Mkuu Wa Usalama Wa Taifa Mr Kassim Adnan Kwangay.. Mudy Akahisi Damu Zake Zikimsisimka Kupita kiasi.. Maswali Lukuki Yalikuwa Yakipishanana katika Kichwa Chake.
Akaamua kuyapuuza maswali Na kuitiliza Akili Yake ili kuangalia ni Jinsi gani Anaweza kujiokoa mikononi kwa mtu yule ambaye aliamini ametekwa.. Kukutana uso kwa uso na Mkurugenzi Yule kilikuwa ni Kitu ambacho hakikutegemea kabisaa... Akakiona kiza kinene na Maswali Lukiki katika Mauaji Ya Mke Wa Rais.. Akiwa bado katika tabasamu lile mara Akashangaa kuwaona Watu Wengine Wakiingia pale ndani.. Hawa walikuwa watu Wengine ambao Walimfanya Mudy Auone ugumu katika Kujinasua... Mbele Ya macho Yake alikuwa akiangalia na Waziri wa Ulinzi na Mwenzake Wa Mambo Ya Ndani.. Wote walikuwa wakimtizama mudy Katika Aina Ya hasira na Chuki.. Hapo Mudy Akaiona Hatari Ambayo Ilikuwa Mbele Yake.. Ni Wakati Huo Akiangaliana na Wazito wale ,kitasa kikanyongwa, Wote Wakakosea Kugeuza Sura Zao Kuangalia Nyuma.. Hawakuujua wepesi wa Mudy.. Sekunde Moja ilitosha kufanya Kitu ambacho Kilikuwa hatari katika Maisha Yake... Ni sekunde moja ambayo Ilimkuta Mudy Ikiliparamia dirisha La Kioo na Kuangukia katika Maua Ya Hoteli Ile Kisha akatokomea mitaani Huku Akiwa Amepata mwanga katika uchunguzi Wake Dhidi Ya Mauaji....
Hadithi nzuri mno mkuuMudy kiboko