mpasta
JF-Expert Member
- Jan 17, 2011
- 919
- 2,007
- Thread starter
- #81
Sehemu-37
Ujio wa Mr.Lorenzo ukawa ni neema kwa Mr.Martin Tenga, kutokana na Mr.Lorenzo kuletewa chakula kila wiki cha kupika toka nyumbani kwao. Hivyo wakawa wanashirikiana katika kupika kwa pamoja na kila kitu wakifanya kwa pamoja. Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza, hawa maswahiba wapya wawili, Mr.Martin Tenga na Mr.Lorenzo walikuwa ni mtu na shemeji yake, kwa maana ya kwamba Mr.Martin amezaa mtoto na Recho ambaye ni dada wa damu wa Mr.Lorenzo. Mtoto mwenyewe wa Mr.Martin na Recho ndio huyu Pesambili ambaye anaishi nyumbani kwa Mr.Lorenzo.
Wakati Pesambili anasubiria kujiunga na masomo ya Chuo Kikuu baada ya kumaliza elimu ya kidato cha sita, akakabidhiwa na babu yake jukumu rasmi la kupeleka mahitaji ya baba mlezi wake, Mr.Lorenzo. Hapo ndio kwa mara ya kwanza tokea kuzaliwa kwake, Pesambili akaanza kuonana na baba yake mzazi uso kwa uso bila kutambuana.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Pesambili, tayari majibu yake ya mitihani ya kidato cha sita yalishatoka. Alifaulu kujiunga na masomo Utabibu katika Chuo Kikuu cha Turin, 'University of Turin', alikuwa anasubiria tu muhula mpya wa masomo uanze2 akaanze maisha mapya ya Chuo Kikuu. Alichaguliwa kujiunga na kitivo cha 'Medicine and Surgery' akiwa mmoja wa wanafunzi waliofanya vizuri zaidi katika mitihani ya kumaliza kidato cha 6. Pesambili alikuwa na furaha sana kufanikiwa lengo lake la kusomea Udaktari likiwa linakaribia kutimia.
Pesambili alikuwa na ndoto kubwa ya kuwa Daktari Bingwa wa Upasuaji, kutokana na huduma aliyopewa yeye utotoni ya upasuaji mpaka akaweza kutembea. Akaweka adhima na nia ya kuwa akiwa mkubwa nae atasomea Udaktari wa Binadamu ili nae aje kutoa huduma kwa wahitaji mbalimbali kama alivyosaidiwa yeye. Alipanga akimaliza Chuo Kikuu akafanye kazi katika nchi yoyote ya Afrika, hiyo ndio iwe sadaka yake kwa Mungu, aliyemtoa kwenye kituo cha watoto yatima na kumleta Ulaya. Nchi aliyoipanga kwenda kujitolea kufanya kazi, ni ile ambayo itakuwa ni ya ni ya asili ya wazazi wako. Kitu ambacho kilikuwa kinamuumiza kichwa ni kuwafahamu ndugu zake kwa upande wa baba na mama.
Taarifa aliyowahi kupewa na Babu yake wa kuasili, baba mzazi wa Mr. Lorenzo ni kuwa alichukuliwa kwenye kituo cha yatima katika moja ya nchi za Afrika, hivyo moja kwa moja mawazo yake yakampa kuwa wazazi wake wameaga dunia ndio maana alipelekwa kwenye kituo cha yatima. Bahati mbaya zaidi, Pesambili alikuwa hajijui jina lake hilo la Pesambili alilopewa na Bibi yake mzaa mama. Mr.Lorenzo alipomuasili tu, akambatiza tena upya na kumpa jina jipya la 'Trezguet Lorenzo', na hilo ndio jina alilolitumia kusomea shule. Hakuwa analipenda kabisa jina hilo la kizungu kwa asilimia 100%, ila hakuwa na jinsi. Alizidi kuchukia kuishi nchini Italia hasa kutokana na kuibuka wimbi jipya la ubaguzi wa rangi lililoanza kuibuka kwa kasi. Kuna wakati alikuwa akiingia kwenye Daladala, abiria wazungu wanampisha siti aketi peke yake.
Akikatisha mitaa ya wahuni wanambwekea sauti za nyani. Hali ambayo haikumkatisha tamaa bali ilimjenga kisaikolojia na kumshajiisha afanye bidii katika masomo ili akaungane na Waafrika wenzake kujiletea maendeleo yao binafsi hasa katika uboreshaji wa sekta ya Afya.
Kitendo cha kwenda mara kwa mara kule gerezani kumtembelea baba mlezi wake Mr.Lorenzo, Pesambili akajikuta anajenga mazoea na Mr.Martin Tenga pia. Kama waswahili wasemavyo damu ni nzito kuliko maji, alijikuta tu katokea kumpenda kwa kumsafishia nia bila kufahamu kuwa huyo ndio baba yake mzazi, huku yeye akijua ni rafiki wa Mr.Lorenzo.
Lakini kabla hawajazoeana vya kutosha na baba yake kidudu mtu kikaingilia kati. Wafungwa wote wa gereza lile la 'Museo del Carcere "Le Nuove' wakasambaratishwa kwa kutawanywa magereza mbalimbali ya nchini Italia. Hiyo ilitokana na taarifa za kiintelijinsia toka kwa mashushushu wa serikali kunusa harufu ya mpango wa kundi la Kimafia 'Ndrangheta' kutaka kutorosha gerezani baadhi ya washirika wao. Na kwa kuwa Mr.Martin Tenga alikuwa ni mshirika wao, akahisiwa nae alikuwa kwenye orodha ya wafungwa waliokuwa wanahitaji kutoroshwa gerezani, hivyo akahamishiwa gereza la siri lenye ulinzi mkali saa 24.
Pesambili nae kwa upande wake muda wa kujiiunga na Chuo Kikuu tayari kwa kuanza masomo yake ya Udaktari ukatimu. Ndio ikawa kimoja haonekani tena mitaani Jijini Turin, ametingwa na shule huku mwenyewe akitaka asijiingize kwenye jambo lolote litakalomtoa nje ya masomo. Darasa lao wanaosomea fani ya Utabibu lilikuwa lina wanafunzi 100, huku ngozi nyeusi ni Pesambili peke yake. Mwanzoni wanafunzi wenzake na baadhi ya Wahadhiri walikuwa wanamdharau wakichukulia kuwa mtu mweusi hana anachokiweza zaidi ya kupenda ngoma na starehe. Hakuwajali yeye akawa anajipanga kuwaonyesha kazi darasani.
Masomo yalivyoanza kuchanganya vizuri na kuanza Mitihani kila Mwanachuo alimheshimu na kumhusudu Pesambili. Kila Mtihani alikuwa anapata maksi kuanzia asilimia 90% kwenda juu kwenye masomo yote muhimu kwa daktari kama Anatomia 'Anatomy', Fiziolojia 'Physiology' na mengineyo. Umahiri wake kwenye masomo ukamfanya awe maarufu Chuo kizima kuanzia Wanachuo mpaka Wahadhiri wote.
Chuo tayari kilishaanza kumtongoza Pesambili kwa kumpa ahadi za mshahara mnono na marupurupu ya kutosha kama atakubali kubakia Chuoni hapo awe Mhadhiri pindi akimaliza masomo yake. Pia hospitali mbalimbali kubwa barani Ulaya walishaanza kusikia sifa zake nao wakaingia kwenye mkumbo wa kumgombea Pesambili. Wote hao Pesambili aliwaruka kimanga na kuwakatalia kuwa hayupo tayari kuingia makubaliano na mtu yoyote mpaka atakapomaliza masomo yake.
Maajabu ya kipekee kwa Pesambili ni kuwa usiku alikuwa kwa baadhi ya siku lazima amuote usingizi baba yake mzazi Mr. Martin Tenga, huku akilini akijiaminisha kabisa kuwa sio sura ngeni kabisa machoni mwake. Alikuwa kila akijaribu kuvuta hisia za kumbukumbu zake kuwa wapi alishawahi kuonana na mfungwa mwenzake wa baba yake mlezi, akili ilikuwa inagoma kabisa kukumbuka. Lakini pia bado suala la kutokujua asili yake na ya wazazi bado lilikuwa linamtafuna Pesambili. Siku alikuwa anaona zinachelewa za yeye kumaliza Chuo ili alishughulikie rasmi suala la kuitafuta asili yake na pia kuulizia ni gereza gani Mr.Martin Tenga amefungwa akamtembelee na kumdadisi vyema, huenda akafahamu walionana wapi kwa mara ya mwisho kabla ya kukutana tena gerezani.
Chambilecho siku hazigandi, miaka 5 ya kumaliza masomo kwa Pesambili ikawa imetimu, akachaguwa kwenda kufanya mazoezi vitendo katika Jiji la 'Barletta', moja ya Jiji lenye wakazi masikini nchini Italia. Hayo ndio yalikuwa mapenzi ya Dr. Pesambili au ukipenda Dr.Trezguet Lorenzo kwenda kutoa huduma kwa watu masikini, ambao shukrani yao kwake itakuwa ni kumuombea dua kwa Mungu.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Gandhi Square, eneo maarufu hapa mitaa ya Carlton Centre ndani ya Jiji la Johanesburg ndio ulikuwa moja ya mtaa maarufu sana kwa Mbweku Jr akiwa ameshakata miaka ndani ya Jiji hilo tokea atue nchini Afrika ya Kusini. Ulikuwa ni mtaa ambao Watanzania wengi utawaona wanazurura mitaani. Si ajabu ukakuta kwenye mtaa mzima watu wote wanaongea kiswahili. Haya yalikua maeneo duni sana, machafu, yananuka kila aina ya harufu. Wabongo wengi walikua ni vibaka, wanategeshea barabarani kwenye alama za pundamilia 'zebra cross' ambapo msongamano wa watu ni mkubwa sana. Kisha wanawazonga watu, na kuwakwapulia mali zao. Wadada na wamama walikua wanalizwa sana vitu vyao vya thamani kama simu za mkononi, fedha na vipochi vyao. Wengi wa hawa wabongo walikua kama mateja, wamechoka sana wanapolala ndio hapo hapo wanapokojoa.
Mbweku Jr alikuwa ameshatua nchini Afrika ya Kusini kiwepesi kabisa kuliko matarajio yake. Aliponea kifo kwenye tundu la sindano yeye na Deborah kwenye mlipuko wa mabomu katika jumba la Recho kule Sinza Kijiweni. Pia wakafanikiwa kuruka viunzi vya walinda usalama ambao walikuwa wanamsaka Deborah kwa kosa la kumuibia mfadhili wake Koplo Marieta. Usiku ule walikuwa wanawapita bila kusimamishwa barabarani tena wakiwa wanatembea mashimashi bila usafiri wowote tena kifua mbele bila kuogopa kitu. Deborah alikuwa anashangazwa sana kwanini watu wengine wanasimamishwa na kuhojiwa ila wao wanapita bila kuulizwa kitu chochote. Mbweku Jr alikuwa anatabasamu tu hana hata chembe cha hofu wala uoga wowote. Moyoni mwake mwake alikuwa anajua kila kitu kwanini inatokea vile hawakamatwi na wana usalama, mpaka akafanikisha mpango wake kabambe wa kutorokea nchini Afrika ya Kusini salama salimini huku akimuacha Deborah mikononi mwa rafiki yake kipenzi Timammy kwa ajili ya uangalizi wake wa kila kitu.
Mbweku Jr nae alikuwa ni miongoni mwa vijana hao vibaka wa mitaani, akiishi maisha ya kuungaunga na kubangaiza yasiyo na mbele wala nyuma. Nyumba ya kuishi alikuwa anakaa gheto na vijana wenzake kwenye chumba walichopangisha katika mtaa wa 'Polly Street', kulikuwa na jengo moja limechakaa kiasi, ndipo hapo maskamoni pake. Maamuzi yake ya kuja nchini Afrika ya Kusini licha ya ugumu wa maisha anayoishi hakuyajutia sana hasa kutokana na taarifa zake za msako kusambaa mpaka Afrika ya Kusini. Habari zilimfikia kuwa anasakwa kama nyara ya taifa na wana usalama kutokana na mlipuko wa jengo kule Sinza, na picha zake zimesambaa kila kona ya nchi kuanzia kwenye magazeti na mitaani, akituhumiwa kuwa ni mmoja wa walipuaji wa hilo jengo.
Aliishia kusononeka moyoni kutokana na kusingiziwa kitu asichohusika nacho kabisa hali ya kuwa ukweli wote alikuwa anaujua kinagaubaga kuwa sio mhusika wa tukio hilo. Moyoni alikuwa anahuzunika kuhusu yule daktari aliyemshushia kipigo, hakuwa na taarifa zake kama alisalimika au alipoteza uhai. Pia alikuwa hajui kama Bosi wake Recho aliokoka kwenye milipuko ile au nae alikuwa ni mhanga wa tukio hilo. Alichokuwa anajutia sana ni kitendo chake cha kukubali kuziacha pesa zote sufufu alizopora kwenye gari la Bosi wake Recho kwa rafiki yake aliyekuwa nae kijiwe kule Kigamboni, Timmamy.
Huyu ndio alimlaghai na kumtia ndimu vilivyo Mbweku Jr kuwa aache pesa zote atoroke yeye kama yeye bila kitu chochote huku akimtisha kuwa mpakani mwa Tanzania na Msumbiji, askari wa uhamiaji wa Msumbiji ni wakatili na wababe, watampora kila kitu chake na kumuacha patupu. Wakaweka makubaliano ya mdomo na Timmamy kuwa hizo pesa awekeze kwenye biashara ya pamoja, na mwaka wowote atakaorudi salama watagawa mali nusu kwa nusu. Pia katika makubaliano alimuomba Timmamy kila akipata muda asikose kumtembea baba yake mzazi gerezani na kumpelekea mahitaji mbalimbali hasa ukichukulia ni mgonjwa hivyo anahitaji uangalizi wa karibu.
Timmamy ndio aliyemuelekeza Mbweku Jr afikie 'Polly Street' Jijini Johanesburg. Kwa jinsi Timmamy alivyokuwa anajinadi kijiweni na kujimwambafai kuwa anaishi maisha mazuri huko nchini Afrika ya Kusini, alichokikuta Mbweku Jr ni tofauti kabisa, ni kama mbingu na ardhi. Gheto moja walikuwa wanaishi watu 15 chumba kimoja, wakiwa wamepanga magodoro chini utasema wanalala matanga msibani. Alichokuwa hafahamu Mbweku Jr ni kuwa kuna ujanja na udanganyifu hali ya juu sana, katika uwanda huu wa kidigitari unaofanywa na Watanzania wanaoishi Ughaibuni. Kwa mfano kijana anayeishi nchi za Ulaya au Afrika ya Kusini anaweka picha zake nyingi kwenye mitandao kama Facebook, Instagram au Twitter akijionyesha mwenye tabasamu, afya murua, mavazi ya kisasa na vilevile mazingira safi na mandhari za kuvutia, akiwa ameegemea gari la kisasa ili tu kuwakoga vijana wenzake ambao kwa bahati nzuri kwake wapo nchini Tanzania, ambako mazingira ya Ughaibuni wanayaona kama mazingaombwe kwao. Mpaka wengine wanafikia hatua ya kujutia kuzaliwa nchini Tanzania na kutamani hata kama wangekuwa mbwa huko Ughaibuni lakini sio kuishi Tanzania. Lakini, ndani ya picha hizo kuna matatizo makubwa ambayo hakuna anayeweza kuyajua bila kusafiri na kwenda kuishi huko japo kwa muda mfupi.
Hayo ndio yaliyomkuta Mbweku Jr kwa jinsi alivyokuwa anatamani maisha ya Ughaibuni kutokana na hadithi za paukwa pakawa za kijiweni kule Kigamboni sasa zilikuwa hadithi hizo zinamtokea puani, anaula wa chuya. Akakuta maisha ya Ughaibuni yamejaa msongo wa mawazo ambao siyo wa kawaida na kuna wakati hasa wageni wanaingia katika majaribu mbalimbali hata ya kutaka kujinyonga kwa msongo wa mawazo. Ndipo alipojikuta Mbweku Jr na vijana wenzake toka Mataifa mbalimbali ya Afrika ambao wamezamia nchini Afrika ya Kusini na maisha kukuta yanakwenda mchafukoge na kujikuta wakijiingiza katika biashara hatari ya kuuza dawa za kulevya katika mitaa mbalimbalimbali ya nchi hiyo ili wapate kipato cha kujikimu.
Kwa wanaopenda maisha ya bwerere ili kukabiliana na ugumu wa maisha ya huko Ughaibuni haishangazi kumkuta kijana wa kiume wa Kitanzania akijivinjari na mke wake mwenye umri ambao ni sawa na bibi wa kumzaa mama au baba yake, hivyohivyo kwa msichana kumkuta akiwa na babu yake ukiuliza utaambiwa maisha na makaratasi. Makaratasi ni nyaraka za kukuwezesha kuishi kama raia wa ukiwa katika nchi za Ughaibuni na kupata mahitaji yote ambayo ni ya lazima kwa raia wa nchi hiyo, hasa unapokosa kazi kwa hiyo wengi huona kama wamepata aina fulani ya ushindi.
Ujio wa Mr.Lorenzo ukawa ni neema kwa Mr.Martin Tenga, kutokana na Mr.Lorenzo kuletewa chakula kila wiki cha kupika toka nyumbani kwao. Hivyo wakawa wanashirikiana katika kupika kwa pamoja na kila kitu wakifanya kwa pamoja. Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza, hawa maswahiba wapya wawili, Mr.Martin Tenga na Mr.Lorenzo walikuwa ni mtu na shemeji yake, kwa maana ya kwamba Mr.Martin amezaa mtoto na Recho ambaye ni dada wa damu wa Mr.Lorenzo. Mtoto mwenyewe wa Mr.Martin na Recho ndio huyu Pesambili ambaye anaishi nyumbani kwa Mr.Lorenzo.
Wakati Pesambili anasubiria kujiunga na masomo ya Chuo Kikuu baada ya kumaliza elimu ya kidato cha sita, akakabidhiwa na babu yake jukumu rasmi la kupeleka mahitaji ya baba mlezi wake, Mr.Lorenzo. Hapo ndio kwa mara ya kwanza tokea kuzaliwa kwake, Pesambili akaanza kuonana na baba yake mzazi uso kwa uso bila kutambuana.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Pesambili, tayari majibu yake ya mitihani ya kidato cha sita yalishatoka. Alifaulu kujiunga na masomo Utabibu katika Chuo Kikuu cha Turin, 'University of Turin', alikuwa anasubiria tu muhula mpya wa masomo uanze2 akaanze maisha mapya ya Chuo Kikuu. Alichaguliwa kujiunga na kitivo cha 'Medicine and Surgery' akiwa mmoja wa wanafunzi waliofanya vizuri zaidi katika mitihani ya kumaliza kidato cha 6. Pesambili alikuwa na furaha sana kufanikiwa lengo lake la kusomea Udaktari likiwa linakaribia kutimia.
Pesambili alikuwa na ndoto kubwa ya kuwa Daktari Bingwa wa Upasuaji, kutokana na huduma aliyopewa yeye utotoni ya upasuaji mpaka akaweza kutembea. Akaweka adhima na nia ya kuwa akiwa mkubwa nae atasomea Udaktari wa Binadamu ili nae aje kutoa huduma kwa wahitaji mbalimbali kama alivyosaidiwa yeye. Alipanga akimaliza Chuo Kikuu akafanye kazi katika nchi yoyote ya Afrika, hiyo ndio iwe sadaka yake kwa Mungu, aliyemtoa kwenye kituo cha watoto yatima na kumleta Ulaya. Nchi aliyoipanga kwenda kujitolea kufanya kazi, ni ile ambayo itakuwa ni ya ni ya asili ya wazazi wako. Kitu ambacho kilikuwa kinamuumiza kichwa ni kuwafahamu ndugu zake kwa upande wa baba na mama.
Taarifa aliyowahi kupewa na Babu yake wa kuasili, baba mzazi wa Mr. Lorenzo ni kuwa alichukuliwa kwenye kituo cha yatima katika moja ya nchi za Afrika, hivyo moja kwa moja mawazo yake yakampa kuwa wazazi wake wameaga dunia ndio maana alipelekwa kwenye kituo cha yatima. Bahati mbaya zaidi, Pesambili alikuwa hajijui jina lake hilo la Pesambili alilopewa na Bibi yake mzaa mama. Mr.Lorenzo alipomuasili tu, akambatiza tena upya na kumpa jina jipya la 'Trezguet Lorenzo', na hilo ndio jina alilolitumia kusomea shule. Hakuwa analipenda kabisa jina hilo la kizungu kwa asilimia 100%, ila hakuwa na jinsi. Alizidi kuchukia kuishi nchini Italia hasa kutokana na kuibuka wimbi jipya la ubaguzi wa rangi lililoanza kuibuka kwa kasi. Kuna wakati alikuwa akiingia kwenye Daladala, abiria wazungu wanampisha siti aketi peke yake.
Akikatisha mitaa ya wahuni wanambwekea sauti za nyani. Hali ambayo haikumkatisha tamaa bali ilimjenga kisaikolojia na kumshajiisha afanye bidii katika masomo ili akaungane na Waafrika wenzake kujiletea maendeleo yao binafsi hasa katika uboreshaji wa sekta ya Afya.
Kitendo cha kwenda mara kwa mara kule gerezani kumtembelea baba mlezi wake Mr.Lorenzo, Pesambili akajikuta anajenga mazoea na Mr.Martin Tenga pia. Kama waswahili wasemavyo damu ni nzito kuliko maji, alijikuta tu katokea kumpenda kwa kumsafishia nia bila kufahamu kuwa huyo ndio baba yake mzazi, huku yeye akijua ni rafiki wa Mr.Lorenzo.
Lakini kabla hawajazoeana vya kutosha na baba yake kidudu mtu kikaingilia kati. Wafungwa wote wa gereza lile la 'Museo del Carcere "Le Nuove' wakasambaratishwa kwa kutawanywa magereza mbalimbali ya nchini Italia. Hiyo ilitokana na taarifa za kiintelijinsia toka kwa mashushushu wa serikali kunusa harufu ya mpango wa kundi la Kimafia 'Ndrangheta' kutaka kutorosha gerezani baadhi ya washirika wao. Na kwa kuwa Mr.Martin Tenga alikuwa ni mshirika wao, akahisiwa nae alikuwa kwenye orodha ya wafungwa waliokuwa wanahitaji kutoroshwa gerezani, hivyo akahamishiwa gereza la siri lenye ulinzi mkali saa 24.
Pesambili nae kwa upande wake muda wa kujiiunga na Chuo Kikuu tayari kwa kuanza masomo yake ya Udaktari ukatimu. Ndio ikawa kimoja haonekani tena mitaani Jijini Turin, ametingwa na shule huku mwenyewe akitaka asijiingize kwenye jambo lolote litakalomtoa nje ya masomo. Darasa lao wanaosomea fani ya Utabibu lilikuwa lina wanafunzi 100, huku ngozi nyeusi ni Pesambili peke yake. Mwanzoni wanafunzi wenzake na baadhi ya Wahadhiri walikuwa wanamdharau wakichukulia kuwa mtu mweusi hana anachokiweza zaidi ya kupenda ngoma na starehe. Hakuwajali yeye akawa anajipanga kuwaonyesha kazi darasani.
Masomo yalivyoanza kuchanganya vizuri na kuanza Mitihani kila Mwanachuo alimheshimu na kumhusudu Pesambili. Kila Mtihani alikuwa anapata maksi kuanzia asilimia 90% kwenda juu kwenye masomo yote muhimu kwa daktari kama Anatomia 'Anatomy', Fiziolojia 'Physiology' na mengineyo. Umahiri wake kwenye masomo ukamfanya awe maarufu Chuo kizima kuanzia Wanachuo mpaka Wahadhiri wote.
Chuo tayari kilishaanza kumtongoza Pesambili kwa kumpa ahadi za mshahara mnono na marupurupu ya kutosha kama atakubali kubakia Chuoni hapo awe Mhadhiri pindi akimaliza masomo yake. Pia hospitali mbalimbali kubwa barani Ulaya walishaanza kusikia sifa zake nao wakaingia kwenye mkumbo wa kumgombea Pesambili. Wote hao Pesambili aliwaruka kimanga na kuwakatalia kuwa hayupo tayari kuingia makubaliano na mtu yoyote mpaka atakapomaliza masomo yake.
Maajabu ya kipekee kwa Pesambili ni kuwa usiku alikuwa kwa baadhi ya siku lazima amuote usingizi baba yake mzazi Mr. Martin Tenga, huku akilini akijiaminisha kabisa kuwa sio sura ngeni kabisa machoni mwake. Alikuwa kila akijaribu kuvuta hisia za kumbukumbu zake kuwa wapi alishawahi kuonana na mfungwa mwenzake wa baba yake mlezi, akili ilikuwa inagoma kabisa kukumbuka. Lakini pia bado suala la kutokujua asili yake na ya wazazi bado lilikuwa linamtafuna Pesambili. Siku alikuwa anaona zinachelewa za yeye kumaliza Chuo ili alishughulikie rasmi suala la kuitafuta asili yake na pia kuulizia ni gereza gani Mr.Martin Tenga amefungwa akamtembelee na kumdadisi vyema, huenda akafahamu walionana wapi kwa mara ya mwisho kabla ya kukutana tena gerezani.
Chambilecho siku hazigandi, miaka 5 ya kumaliza masomo kwa Pesambili ikawa imetimu, akachaguwa kwenda kufanya mazoezi vitendo katika Jiji la 'Barletta', moja ya Jiji lenye wakazi masikini nchini Italia. Hayo ndio yalikuwa mapenzi ya Dr. Pesambili au ukipenda Dr.Trezguet Lorenzo kwenda kutoa huduma kwa watu masikini, ambao shukrani yao kwake itakuwa ni kumuombea dua kwa Mungu.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Gandhi Square, eneo maarufu hapa mitaa ya Carlton Centre ndani ya Jiji la Johanesburg ndio ulikuwa moja ya mtaa maarufu sana kwa Mbweku Jr akiwa ameshakata miaka ndani ya Jiji hilo tokea atue nchini Afrika ya Kusini. Ulikuwa ni mtaa ambao Watanzania wengi utawaona wanazurura mitaani. Si ajabu ukakuta kwenye mtaa mzima watu wote wanaongea kiswahili. Haya yalikua maeneo duni sana, machafu, yananuka kila aina ya harufu. Wabongo wengi walikua ni vibaka, wanategeshea barabarani kwenye alama za pundamilia 'zebra cross' ambapo msongamano wa watu ni mkubwa sana. Kisha wanawazonga watu, na kuwakwapulia mali zao. Wadada na wamama walikua wanalizwa sana vitu vyao vya thamani kama simu za mkononi, fedha na vipochi vyao. Wengi wa hawa wabongo walikua kama mateja, wamechoka sana wanapolala ndio hapo hapo wanapokojoa.
Mbweku Jr alikuwa ameshatua nchini Afrika ya Kusini kiwepesi kabisa kuliko matarajio yake. Aliponea kifo kwenye tundu la sindano yeye na Deborah kwenye mlipuko wa mabomu katika jumba la Recho kule Sinza Kijiweni. Pia wakafanikiwa kuruka viunzi vya walinda usalama ambao walikuwa wanamsaka Deborah kwa kosa la kumuibia mfadhili wake Koplo Marieta. Usiku ule walikuwa wanawapita bila kusimamishwa barabarani tena wakiwa wanatembea mashimashi bila usafiri wowote tena kifua mbele bila kuogopa kitu. Deborah alikuwa anashangazwa sana kwanini watu wengine wanasimamishwa na kuhojiwa ila wao wanapita bila kuulizwa kitu chochote. Mbweku Jr alikuwa anatabasamu tu hana hata chembe cha hofu wala uoga wowote. Moyoni mwake mwake alikuwa anajua kila kitu kwanini inatokea vile hawakamatwi na wana usalama, mpaka akafanikisha mpango wake kabambe wa kutorokea nchini Afrika ya Kusini salama salimini huku akimuacha Deborah mikononi mwa rafiki yake kipenzi Timammy kwa ajili ya uangalizi wake wa kila kitu.
Mbweku Jr nae alikuwa ni miongoni mwa vijana hao vibaka wa mitaani, akiishi maisha ya kuungaunga na kubangaiza yasiyo na mbele wala nyuma. Nyumba ya kuishi alikuwa anakaa gheto na vijana wenzake kwenye chumba walichopangisha katika mtaa wa 'Polly Street', kulikuwa na jengo moja limechakaa kiasi, ndipo hapo maskamoni pake. Maamuzi yake ya kuja nchini Afrika ya Kusini licha ya ugumu wa maisha anayoishi hakuyajutia sana hasa kutokana na taarifa zake za msako kusambaa mpaka Afrika ya Kusini. Habari zilimfikia kuwa anasakwa kama nyara ya taifa na wana usalama kutokana na mlipuko wa jengo kule Sinza, na picha zake zimesambaa kila kona ya nchi kuanzia kwenye magazeti na mitaani, akituhumiwa kuwa ni mmoja wa walipuaji wa hilo jengo.
Aliishia kusononeka moyoni kutokana na kusingiziwa kitu asichohusika nacho kabisa hali ya kuwa ukweli wote alikuwa anaujua kinagaubaga kuwa sio mhusika wa tukio hilo. Moyoni alikuwa anahuzunika kuhusu yule daktari aliyemshushia kipigo, hakuwa na taarifa zake kama alisalimika au alipoteza uhai. Pia alikuwa hajui kama Bosi wake Recho aliokoka kwenye milipuko ile au nae alikuwa ni mhanga wa tukio hilo. Alichokuwa anajutia sana ni kitendo chake cha kukubali kuziacha pesa zote sufufu alizopora kwenye gari la Bosi wake Recho kwa rafiki yake aliyekuwa nae kijiwe kule Kigamboni, Timmamy.
Huyu ndio alimlaghai na kumtia ndimu vilivyo Mbweku Jr kuwa aache pesa zote atoroke yeye kama yeye bila kitu chochote huku akimtisha kuwa mpakani mwa Tanzania na Msumbiji, askari wa uhamiaji wa Msumbiji ni wakatili na wababe, watampora kila kitu chake na kumuacha patupu. Wakaweka makubaliano ya mdomo na Timmamy kuwa hizo pesa awekeze kwenye biashara ya pamoja, na mwaka wowote atakaorudi salama watagawa mali nusu kwa nusu. Pia katika makubaliano alimuomba Timmamy kila akipata muda asikose kumtembea baba yake mzazi gerezani na kumpelekea mahitaji mbalimbali hasa ukichukulia ni mgonjwa hivyo anahitaji uangalizi wa karibu.
Timmamy ndio aliyemuelekeza Mbweku Jr afikie 'Polly Street' Jijini Johanesburg. Kwa jinsi Timmamy alivyokuwa anajinadi kijiweni na kujimwambafai kuwa anaishi maisha mazuri huko nchini Afrika ya Kusini, alichokikuta Mbweku Jr ni tofauti kabisa, ni kama mbingu na ardhi. Gheto moja walikuwa wanaishi watu 15 chumba kimoja, wakiwa wamepanga magodoro chini utasema wanalala matanga msibani. Alichokuwa hafahamu Mbweku Jr ni kuwa kuna ujanja na udanganyifu hali ya juu sana, katika uwanda huu wa kidigitari unaofanywa na Watanzania wanaoishi Ughaibuni. Kwa mfano kijana anayeishi nchi za Ulaya au Afrika ya Kusini anaweka picha zake nyingi kwenye mitandao kama Facebook, Instagram au Twitter akijionyesha mwenye tabasamu, afya murua, mavazi ya kisasa na vilevile mazingira safi na mandhari za kuvutia, akiwa ameegemea gari la kisasa ili tu kuwakoga vijana wenzake ambao kwa bahati nzuri kwake wapo nchini Tanzania, ambako mazingira ya Ughaibuni wanayaona kama mazingaombwe kwao. Mpaka wengine wanafikia hatua ya kujutia kuzaliwa nchini Tanzania na kutamani hata kama wangekuwa mbwa huko Ughaibuni lakini sio kuishi Tanzania. Lakini, ndani ya picha hizo kuna matatizo makubwa ambayo hakuna anayeweza kuyajua bila kusafiri na kwenda kuishi huko japo kwa muda mfupi.
Hayo ndio yaliyomkuta Mbweku Jr kwa jinsi alivyokuwa anatamani maisha ya Ughaibuni kutokana na hadithi za paukwa pakawa za kijiweni kule Kigamboni sasa zilikuwa hadithi hizo zinamtokea puani, anaula wa chuya. Akakuta maisha ya Ughaibuni yamejaa msongo wa mawazo ambao siyo wa kawaida na kuna wakati hasa wageni wanaingia katika majaribu mbalimbali hata ya kutaka kujinyonga kwa msongo wa mawazo. Ndipo alipojikuta Mbweku Jr na vijana wenzake toka Mataifa mbalimbali ya Afrika ambao wamezamia nchini Afrika ya Kusini na maisha kukuta yanakwenda mchafukoge na kujikuta wakijiingiza katika biashara hatari ya kuuza dawa za kulevya katika mitaa mbalimbalimbali ya nchi hiyo ili wapate kipato cha kujikimu.
Kwa wanaopenda maisha ya bwerere ili kukabiliana na ugumu wa maisha ya huko Ughaibuni haishangazi kumkuta kijana wa kiume wa Kitanzania akijivinjari na mke wake mwenye umri ambao ni sawa na bibi wa kumzaa mama au baba yake, hivyohivyo kwa msichana kumkuta akiwa na babu yake ukiuliza utaambiwa maisha na makaratasi. Makaratasi ni nyaraka za kukuwezesha kuishi kama raia wa ukiwa katika nchi za Ughaibuni na kupata mahitaji yote ambayo ni ya lazima kwa raia wa nchi hiyo, hasa unapokosa kazi kwa hiyo wengi huona kama wamepata aina fulani ya ushindi.