mpasta
JF-Expert Member
- Jan 17, 2011
- 919
- 2,007
- Thread starter
- #61
SEHEMU-30
SURA YA KUMI
Recho nyota yake ilizidi kung'aa kiuchumi. Ngwenje alizokuwa analipwa na Washefa wake kwenye kazi yake mpya kuuza mwili zilikosa kifani. Zilimtosha kupanga nyumba nzima peke yake katika eneo la Sinza na kujipatia usafiri binafsi wa kukata mitaa akiwa Jijini Dar es Salaam. Katika wanawake wa kwanza kwanza Jijini Dar es Salaam kumiliki gari la kifahari zama hizo la aina ya 'Korando' toleo jipya. Mpaka ikafika hatua anawaponda kwa kejeli wale wanaouponda wa fisi au kupanda usafiri wa umma kwenye mizunguko yao ya kila siku ndani ya Jiji. Alishajiapiza kamwe hawezi kupanda daladala hata kama gari yake italeta matatizo, alikuwa yupo tayari akodishe taksi hata kama ni siku nzima. Alishafanikiwa kukata miaka kadhaa Jijini Dar es Salaam huku jina lake likiwa maarufu kwenye kumbi na klabu zote kubwa za starehe Jijini.
Bendi zote kubwa za muziki wa dansi hapa nchini kwenye nyimbo zao wakawa wanatia vionjo vya kulitaja jina lake. Mara kwenye nyimbo anaimbwa "utasikia dadaa Rechooo, una sura nzuri kama malaika" na sifa kedekede za kumpamba mafuta kwa mgongo wa chupa. Nae Recho alivyokuwa mpenda misifa, akitajwa tu alikuwa anacheka na kuterema kisha lazima asimame toka kitini kwenda kuwatuza wanamuziki wote wa bendi.
Katika harakati zake za umalaya, Recho akaibua fursa nyingine nchini Jijini Nairobi. Akafanya maamuzi ya kurudi tena huko kwa mara ya pili baada ya kukatika miaka kadhaa tokea afukuzwe ndani ya masaa 24 na kudhulumiwa Klabu yake ya "Nairobee By Night". Kilichomsukuma arudishe majeshi tena Jijini Nairobi ni fursa ya kuwadaka watalii wa kutokea ughaibuni wanaotua Jijini Nairobi. Kenya ilikuwa na wasaa mkubwa wa kupokea watalii kutokana na kuwa na shirika la ndege lenye nguvu la 'Kenya Airways' kulinganisha na Tanzania ambayo shirika lake la ndege la 'ATC' lilikuwa lipo mahututi linapumulia gesi likiwa na kidege kimoja tu tena chakavu. Maelfu ya watalii kutokana na kutoka nchi za Ulaya walikuwa wanamiminikia Kenya wakiaminishwa na propaganda kuwa Mlima Kilimanjaro upo Kenya. Kisha wakija kutanabahi kuwa Mlima huo, upo Tanzania wanakuwa tayari fedha nyingi za kigeni wamezitumia nchini Kenya na Tanzania kuambulia mabaki tu. Hivyo Recho akaona Nairobi ataweza kuibua madanga ya kizungu yenye pesa sufufu hivyo kuzidi kujiimarisha kiuchumi.
Na kwakuwa Jiji la Nairobi analijua nje ndani, haikumpa ugumu kulizoea tena Jiji hilo kwa haraka. Sasa akawa mtu wa kambi popote, anakaa Nairobi wiki mbili kisha anarejea Jiji Dar es Salaam, anazunguka kama popo baina ya Majiji hayo mawili. Baada ya miezi kadhaa tu akafanikiwa kutengeneza mirija ya kuingiza pesa za kutosha. Katika hangaika yake ya kusaka pesa haramu, akafanikiwa kumnasa kiruka mito wa kizungu, kutoka nchini Italia wa rika lake kabisa ambaye kwa jina alikuwa anajulikana kama Mr.Lorenzo. Huyu mzungu, buzi lake jipya alikuwa ni baba mlezi kabisa wa mtoto wa Recho, Pesambili. Mr.Lorenzo alikuja Afrika Mashariki kwa gia ya utalii lakini kiuhalisia alikuja kuangalia fursa kwa ajili ya kazi haramu maalumu. Kazi ambazo zilikuwa zinamuingizia Mr.Lorenzo mabilioni ya pesa katika nchi mbalimbali za Kiafrika alizowekeza.
Nchini kwao Italia alikuwa anajipambanua kama Mfanyabiashara maarufu mwenye kumiliki kampuni ya kuzalisha na kusambaza filamu za wanyama pori 'Wildlife'. Kampuni hiyo ya Mr. Lorenzo ilikuwa inajulikana kama 'Talking Trees and Animals Creative(TTAC)-Films Company LTD. Baadhi ya serikali za nchi za Kiafrika zilikuwa zimeingia nae mkataba wa kuwatangazia vivutio vyao vya kitalii. TTAC-Films Company Ltd, ilijipambanua kama moja ya kampuni bora kabisa ya filamu Jijini Turin nchini Italia. Lakini sirini kampuni hiyo ilikuwa inazalisha pia filamu za ngono zinazorekodiwa maeneo tofautitofauti katika nchi mbalimbali za Afrika. Nchi nyingi za Afrika zilikuwa zimepiga marufuku kwa raia kushiriki kuandaa filamu za ngono, na zilikuwa zimeweka adhabu kali kwa watakaobainika. Hivyo kampuni ya TTAC-Films Company LTD inayomilikiwa na Mr.Lorenzo ikawa inafanya shughuli hizo kinyemela kinyume na utaratibu. Kwa kuwahadaa washiriki hao kwa kuwapa fedha sufufu ili mradi wasikatae kurekodiwa filamu hizo.
Shughuli hizo walikuwa wanazifanya kwa usiri mkubwa sana. Mr Lorenzo na wahuni wenzake walikuwa wanakwenda kuzuru nchi mbalimbali za Kiafrika kwa kutumia hati feki za kusafiria wakijifanya kama watalii wenye kuvutiwa na mali asili za Afrika kumbe wanafanya pia utalii wa ngono. Mr.Lorenzo kwa Recho alijitambulisha kwa jina bandia la 'Luis Van Odergaard', Mdachi wa Uholanzi, akijifanya ni Mfanyabiashara wa vito vya madini. Hakutaka kabisa Tengo amjue undani wa shughuli yake anayoifanya. Na Recho nae mara tu baada ya kufariki mama yake akajibadilisha jina na kuanza kujiita 'Recho Kavishe', akitumia ubini wa ukoo wa babu yake mzaa mama. Hakutaka kabisa kulisikia jina la baba yake mzazi Mzee 'Francesco' ambaye kwanza alikuwa hajawahi kumtia machoni na wala kupata huduma zake za matumizi. Alikuwa anamchukia baba yake mzazi kupita maelezo hasa kutokana na maamuzi ya kumtelekeza hali ya kuwa mama yake alikuwa anamuambia kuwa baba yake ni mkwasi wa mali huko nchini Italia alipo.
Maisha yao ya usanii na ulaghai yakasababisha ndugu wa baba mmoja wasitambuane na waangukie katika mapenzi motomoto bila kufahamu kuwa wao ni ndugu wa damu kabisa. Mwanzoni Mr.Lorenzo alimchukulia Recho kama walivyo malaya wengine tu aliowahi kupita nao, lakini kadri siku zinavyokwenda akajikuta anazidi kumpenda Recho, amesalitika vilivyo. Tokea aanze kuyajua mapenzi alikuwa hajawahi kustareheshwa kwa ufundi mkubwa kama anavyofanyiwa na Recho. Akakata shauri kuwa lazima Recho awe wake peke ajifaidie anavyotaka yeye. Akampa masharti kuwa akitaka awe mpenzi wake aachane na shughuli ya uchangudoa atamfanyia mambo makubwa maishani mwake.
Recho baada ya kumgundua kuwa Mr.Lorenzo ni pochi nene, sio pangu pakavu tia mchuzi nile hakuwa na shida kutimiza masharti aliyotakiwa kuyatekeleza ya kuachana na biashara ya kujiuza mwili wake. Mr.Lorenzo kuonyesha amekufa na kuoza kwa Recho akamuuliza amfungulie mradi gani wa kujikimu kimaisha. Recho alifurahi sana na kuona wakati wa kulipa kisasi kwa mpenzi wake wa zamani Martin Tenga umetimu. Recho bila kupepesa macho, akataka kufunguliwa biashara ya Hoteli, na kumtaka Mr Lorenzo amnunulie 'Martino Royal Hotel' iliyopo Jijini Dar es Salaam, Hoteli ambayo ilikuwa sokoni inapigwa bei. Baada ya Bwana Martin Tenga kushikiliwa huko nchini Italia, ndugu zake wakashindwa namna ya uendeshaji wa Hoteli hiyo ya kifahari hivyo wakaiweka sokoni kwa mteja yoyote atakayejitokeza.
Hoteli hiyo ya kifahari yenye roshani 10 ilikuwa inauzwa milioni 200 taslimu. Mr.Lorenzo alichofanya ni kutekeleza ombi la kimada wake huyo kwa moyo mmoja kwa kufanya taratibu zote za manunuzi ya Hoteli hiyo. Hati ya manunuzi ya Hoteli hiyo iliandikishwa kuwa Hoteli hiyo inamilikiwa kwa ubia kati ya mzawa Recho na mwekezaji Mr.Lorenzo. Hivyo Recho alikuwa na furaha sheshe kwa kufanikisha kuirudisha Hoteli yake aliyoiasisi kwenye mikono yake mwenyewe kisha akaporwa kilaghai na mpenziwe wa zamani Martin Tenga ambaye alikuwa hataki hata kumsikia wala kumuona. Alitamani sana Recho, Mr.Martin Tenga arudi nchini Tanzania na aone jinsi Hoteli aliyodhulumu ilivyotua tena mikononi mwa Recho.
Kwa upande wake Mr. Lorenzo alikuwa anaendelea na shughuli yake haramu kwa kificho sana, bila Recho kushtukia kazi yake inayomleta mara kwa mara katika nchi za Afrika Mashariki.
Wasichana wa kucheza filamu hizo za ngono alikuwa hapati shida kuwapata, kutokana na tabia ya wasichana wengi wa Majiji hayo makubwa ya Afrika Mashariki kuanzia Nairobi, Kigali, Kampala, Bujumbura na Dar es Salaam kuendekeza utajiri wa mezani. Ule utajiri wa bila kutoka jasho kwa kutumia uzuri wa maumbile yao. Maisha yakawa yanasonga baina ya wapenzi hao wapya ambao ni kaka na dada wasiotambuana.
Lakini kama kawaida yake Recho kwenye pesa huwa ana simile, akili yake inaruka na kuwaza kufanya dhuluma, akaandaa mpango wa kumuondoa kwenye umilki wa Hoteli hiyo Mr.Lorenzo, kabla kibao hakijamgeukia na kufanyima unyama wa kutisha na Mr.Lorenzo. Unyama ambao ulimuacha mgonjwa kitandani maisha yake yote.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Deborah alishaanza kuwa mzoefu wa mitaa ya Kisutu stendi ya Mabasi ya mikoani. Alishakata miezi miwili tokea atue Jijini Mwezi Novemba. Alipata kibarua cha kuuza kioski cha kuuza vitafunwa na vya vinywaji baridi kwa abiria na Wafanyabiashara ndogo ndogo kuzunguka eneo hilo la Kisutu. Haikumchukua muda kuzoea biashara maeneo hayo, hasa ikichukuliwa kuwa ana uzoefu wa biashara hizo kwa zaidi ya miaka 4 kutokea kule Kijiji Mikongeni, Morogoro. Kioski alichokuwa anauza kilikuwa kilikuwa kinamilikiwa na Koplo Marieta, Askari wa kituo cha polisi, Msimbazi, Kariakoo. Deborah alikuwa anamchukulia Koplo Marieta kama malaika mkombozi kwake. Hivyo ni kwa namna alivyomchomoa katika mikono ya polisi wenzake waliotaka kumfungulia kesi ya uzembe na uzururaji kisha wamrudishe kijiji kwao tena. Siku ile aliyotoroka nyumbani kwao alifanikiwa kupata msaada wa usafiri wa kumfikisha Jijini Dar es Salaam kama alivyotarajiwa.
"Sasa mwanangu Deborah tumeingia tayari Jijini Dar es Salaam, tutakushusha hapa Buguruni, tutakupakiza kwenye daladala litakalokushusha stendi ya Mabasi ya Kisutu kama ulivyoelekeza kuwa mwenyeji wako yupo huko" aliongea dereva Babu Juma kwa sauti ya uchovu wa safari, akimuelekeza Deborah kuwa wameshawasili ndani ya Jiji. Babu Juma alikuwa ameendesha gari lake usiku kucha bila kupumzika tena akiwa ameutwika mtindi wa pombe za kienyeji kichwani mwake. "Ahsante sana Babu Juma tutaonana tena Mungu akipenda, nakutakia kazi njema" Deborah alishukuru huku akiunda tabasamu moja matata usoni mwake. Shukrani hiyo ilikuwa ni kutokana na msaada wa bure aliopewa na dereva yule. Baada ya hapo akaanza kukusanya kifurushi chake cha nguo akijiandaa kushuka chini ya gari lile.
Deborah aliwadanganya akina Babu Juma na Taniboi wake kuwa mwenyeji wake anamsubiria kumpokea stendi ya Mabasi ya Mikoani ya Jijini Dar es Salaam. Wakati ukweli wa mambo ni kuwa hakuwa na ndugu wala rafiki katika Jiji hilo la Dar es Salaam. Alichokuwa anajipa moyo ni kuwa Mungu atampa stara asiadhirike ugenini. Aliamini bila kwa yakini isiyo na mashaka kuwa kwa baraka za Mola atapata msamaria mwema atakayemuangalia kwa chakula, mavazi na malazi. Walikuwa wameingia Jijini Dar es Salaam asubuhi asubuhi wakiwa wametoka Morogoro tokea manane ya usiku.
Akawashukuru na kuagana nao, akiwaongopea amekuja Jijini Dar es Salaam kusoma masomo ya ziada 'Tuition' kwa ajili ya kujiandaa na masomo ya kidato cha kwanza kwa mwaka ujao wa 1997. Aliposhuka tu kwenye Lori lile, Taniboi nae akawa nae bega kwa bega kumtafutia Daladala kama alivyoomba. Basi hizo ndogo zilikuwa zinaitwa 'Daladala' kutokana na kutoza nauli ya shilingi 5 kwa safari. Deborah kwa bahati nzuri alipata siti ya dirishani, hivyo macho yake yalikuwa yamekodoka barabarani utasema anakata roho kutokana na kushangazwa na uzuri wa maghorofa na magari yanayopishana barabarani kwa kasi kubwa. Tokea anapata akili timamu mpaka anavunja ungo, alikuwa hajawahi kupata mtoko wowote wa safari hata walau wa kufika Morogoro Mjini. Hivyo hiyo ndio ilikuwa ziara yake ya kwanza kubwa katika maisha yake.
Daladala lile alilopanda bila kuchelewa likamshusha Kisutu kama alivyohitaji huku likiendelea na safari zake kuwafikisha abiria wengine. Aliposhuka tu pale stendi na kuuona umati wa watu stendi pale, moyo wake ukamlipuka kwa uoga. Kilichokuwa kinamshangaza watu wale walikuwa wanaongea Kiswahili cha haraka haraka kama ndege tena chenye kukatisha maneno. Lugha ambayo ilikuwa inampa wakati mgumu sana kuelewa wanaongea kitu gani haswa. Hofu ilimjaa zaidi baada ya kuona kila mtu alikuwa ameshika hamsini zake ametingwa na mambo yake hamna hata mmoja wa kumuuliza hali yake mgeni na anahitaji msaada gani. Alitegemea ukarimu wanaofanyiana kijiji kwao huku Mjini uwe maradufu.
Akaanza kuuchukia Mji huo kuanzia muda huo huo kutokana na watu wake kukosa utu na ubinadamu. Kiu ya maji na njaa ilikuwa imemkamata vilivyo asubuhi hiyo utasema yupo kwenye mfungo. Deborah akaanza kutupa macho yake huku na kule kutafuta walau kisima cha kujichotea maji ya kunywa kama kule kijijini kwao. Pia alitarajia huenda atauona mti wa mchungwa au muembe walau abahatike kuchuma tunda ashibishe minyoo tumboni. Kwa bahati mbaya hakuambulia kiti chochote katika alivyovitamani. Zaidi ya kuziona embe chache na machungwa yamepangwa kwenye meza za wachuuzi wadogo wadogo zinauzwa.
Alishangazwa sana kuona matunda wanayogaiana bure kijijini kwao mpaka wanyama kama nyani na tumbili wanajipocholea bwerere huku Mjini yanauzwa kwa bei ya kuchupa. "Hawa watu wa Mji huu, nimewanyooshea mikono na wana dhambi sana, embe za shamba la Bi. Pembe kule kijijini tunajiokotea bure tu" alinong'ona moyoni mwake. Akawa amejikunyata kwenye banda la wasafiri akiwa amejichanganya na wasafiri wengine wanaosubiri Mabasi ya kuelekea mikoani, huku akizichanga karata zake kichwani mwake kuitafakari hatima yake. Kwenye akiba yake kibindoni alikuwa na shilingi 55 taslimu, alizozipata katika mauzo ya shingo za kuku, ndizi na sinia za kuuzia asusa hizo zote alizipiga bei.
Alijitahidi kuvumilia njaa na kiu ili mradi asikiguse kibubu chake cha akiba lakini ilipofika majira ya adhuhuri, uzalendo ukamshinda. Usicheze na tumbo wewe, ndio maana watu wazima na heshima zao wanapokea rushwa, wanajiingiza kwenye ufisadi, wanawake wanajiuza miili yao, ukiwauliza kisa tumbo. Ikabidi aishiwe ujanja, asije kuanguka njaa bure na pesa anayo. Kiunyonge kabisa ikabidi afungue kibubu chake na kujongea banda la jirani la mama lishe na kuagiza chakula, akala, akashiba na kuendelea kutafakari kitu gani cha kufanya kadri saa zinavyozidi kwenda. Mpaka kufika majira ya magharibi, asilimia kubwa ya abiria walikuwa tayari wameshatawanyika zao mmoja mmoja kuelekea majumbani kwao kupumzika. Mabasi ya kutokea mikoani asilimia kubwa yalikuwa yameshawasili zao.
Kiza kikaanza kutanda angani huku mawingu mekundu yakizidi kupotea kuashiria usiku mbichi unakaribishwa. Hofu ikazidi kushamiri katika moyo wa Deborah huku akianza kujutia kwanini hata alichukua maamuzi magumu na ya hasira ya kuja Jijini Dar es Salaam bila kujipanga. Akazidi kujipa nasaha za majuto ni mjukuu kuwa siku zote hasira ni hasara. Na daima mwanadamu hutakiwa kufanya maamuzi wakati una hasira sana au una furaha sana, lazima utapotoka katika maamuzi yako. Sasa alijiona kabisa anapatwa na fedheha ugenini, sehemu ambayo hamna mtu yoyote anayemfahamu kwa kina. Wasela wa stendi nao hawakutaka kujivunga, tayari wakaanza kuiona fursa ya kujiegesha kwa Deborah usiku huo. Walishazoea kujipatia wasichana wa mahonyo wanaozagaazagaa stendi hapo. Kwao suala la magonjwa ya zinaa kama UKIMWI, sijui Kaswende, Kisonono na mengineyo ilikuwa ni hadithi za alinacha zisizo na mashiko. Walichokuwa wanajali wao ni kuitimizia nafsi hawaa zake inazohitaji.
SURA YA KUMI
Recho nyota yake ilizidi kung'aa kiuchumi. Ngwenje alizokuwa analipwa na Washefa wake kwenye kazi yake mpya kuuza mwili zilikosa kifani. Zilimtosha kupanga nyumba nzima peke yake katika eneo la Sinza na kujipatia usafiri binafsi wa kukata mitaa akiwa Jijini Dar es Salaam. Katika wanawake wa kwanza kwanza Jijini Dar es Salaam kumiliki gari la kifahari zama hizo la aina ya 'Korando' toleo jipya. Mpaka ikafika hatua anawaponda kwa kejeli wale wanaouponda wa fisi au kupanda usafiri wa umma kwenye mizunguko yao ya kila siku ndani ya Jiji. Alishajiapiza kamwe hawezi kupanda daladala hata kama gari yake italeta matatizo, alikuwa yupo tayari akodishe taksi hata kama ni siku nzima. Alishafanikiwa kukata miaka kadhaa Jijini Dar es Salaam huku jina lake likiwa maarufu kwenye kumbi na klabu zote kubwa za starehe Jijini.
Bendi zote kubwa za muziki wa dansi hapa nchini kwenye nyimbo zao wakawa wanatia vionjo vya kulitaja jina lake. Mara kwenye nyimbo anaimbwa "utasikia dadaa Rechooo, una sura nzuri kama malaika" na sifa kedekede za kumpamba mafuta kwa mgongo wa chupa. Nae Recho alivyokuwa mpenda misifa, akitajwa tu alikuwa anacheka na kuterema kisha lazima asimame toka kitini kwenda kuwatuza wanamuziki wote wa bendi.
Katika harakati zake za umalaya, Recho akaibua fursa nyingine nchini Jijini Nairobi. Akafanya maamuzi ya kurudi tena huko kwa mara ya pili baada ya kukatika miaka kadhaa tokea afukuzwe ndani ya masaa 24 na kudhulumiwa Klabu yake ya "Nairobee By Night". Kilichomsukuma arudishe majeshi tena Jijini Nairobi ni fursa ya kuwadaka watalii wa kutokea ughaibuni wanaotua Jijini Nairobi. Kenya ilikuwa na wasaa mkubwa wa kupokea watalii kutokana na kuwa na shirika la ndege lenye nguvu la 'Kenya Airways' kulinganisha na Tanzania ambayo shirika lake la ndege la 'ATC' lilikuwa lipo mahututi linapumulia gesi likiwa na kidege kimoja tu tena chakavu. Maelfu ya watalii kutokana na kutoka nchi za Ulaya walikuwa wanamiminikia Kenya wakiaminishwa na propaganda kuwa Mlima Kilimanjaro upo Kenya. Kisha wakija kutanabahi kuwa Mlima huo, upo Tanzania wanakuwa tayari fedha nyingi za kigeni wamezitumia nchini Kenya na Tanzania kuambulia mabaki tu. Hivyo Recho akaona Nairobi ataweza kuibua madanga ya kizungu yenye pesa sufufu hivyo kuzidi kujiimarisha kiuchumi.
Na kwakuwa Jiji la Nairobi analijua nje ndani, haikumpa ugumu kulizoea tena Jiji hilo kwa haraka. Sasa akawa mtu wa kambi popote, anakaa Nairobi wiki mbili kisha anarejea Jiji Dar es Salaam, anazunguka kama popo baina ya Majiji hayo mawili. Baada ya miezi kadhaa tu akafanikiwa kutengeneza mirija ya kuingiza pesa za kutosha. Katika hangaika yake ya kusaka pesa haramu, akafanikiwa kumnasa kiruka mito wa kizungu, kutoka nchini Italia wa rika lake kabisa ambaye kwa jina alikuwa anajulikana kama Mr.Lorenzo. Huyu mzungu, buzi lake jipya alikuwa ni baba mlezi kabisa wa mtoto wa Recho, Pesambili. Mr.Lorenzo alikuja Afrika Mashariki kwa gia ya utalii lakini kiuhalisia alikuja kuangalia fursa kwa ajili ya kazi haramu maalumu. Kazi ambazo zilikuwa zinamuingizia Mr.Lorenzo mabilioni ya pesa katika nchi mbalimbali za Kiafrika alizowekeza.
Nchini kwao Italia alikuwa anajipambanua kama Mfanyabiashara maarufu mwenye kumiliki kampuni ya kuzalisha na kusambaza filamu za wanyama pori 'Wildlife'. Kampuni hiyo ya Mr. Lorenzo ilikuwa inajulikana kama 'Talking Trees and Animals Creative(TTAC)-Films Company LTD. Baadhi ya serikali za nchi za Kiafrika zilikuwa zimeingia nae mkataba wa kuwatangazia vivutio vyao vya kitalii. TTAC-Films Company Ltd, ilijipambanua kama moja ya kampuni bora kabisa ya filamu Jijini Turin nchini Italia. Lakini sirini kampuni hiyo ilikuwa inazalisha pia filamu za ngono zinazorekodiwa maeneo tofautitofauti katika nchi mbalimbali za Afrika. Nchi nyingi za Afrika zilikuwa zimepiga marufuku kwa raia kushiriki kuandaa filamu za ngono, na zilikuwa zimeweka adhabu kali kwa watakaobainika. Hivyo kampuni ya TTAC-Films Company LTD inayomilikiwa na Mr.Lorenzo ikawa inafanya shughuli hizo kinyemela kinyume na utaratibu. Kwa kuwahadaa washiriki hao kwa kuwapa fedha sufufu ili mradi wasikatae kurekodiwa filamu hizo.
Shughuli hizo walikuwa wanazifanya kwa usiri mkubwa sana. Mr Lorenzo na wahuni wenzake walikuwa wanakwenda kuzuru nchi mbalimbali za Kiafrika kwa kutumia hati feki za kusafiria wakijifanya kama watalii wenye kuvutiwa na mali asili za Afrika kumbe wanafanya pia utalii wa ngono. Mr.Lorenzo kwa Recho alijitambulisha kwa jina bandia la 'Luis Van Odergaard', Mdachi wa Uholanzi, akijifanya ni Mfanyabiashara wa vito vya madini. Hakutaka kabisa Tengo amjue undani wa shughuli yake anayoifanya. Na Recho nae mara tu baada ya kufariki mama yake akajibadilisha jina na kuanza kujiita 'Recho Kavishe', akitumia ubini wa ukoo wa babu yake mzaa mama. Hakutaka kabisa kulisikia jina la baba yake mzazi Mzee 'Francesco' ambaye kwanza alikuwa hajawahi kumtia machoni na wala kupata huduma zake za matumizi. Alikuwa anamchukia baba yake mzazi kupita maelezo hasa kutokana na maamuzi ya kumtelekeza hali ya kuwa mama yake alikuwa anamuambia kuwa baba yake ni mkwasi wa mali huko nchini Italia alipo.
Maisha yao ya usanii na ulaghai yakasababisha ndugu wa baba mmoja wasitambuane na waangukie katika mapenzi motomoto bila kufahamu kuwa wao ni ndugu wa damu kabisa. Mwanzoni Mr.Lorenzo alimchukulia Recho kama walivyo malaya wengine tu aliowahi kupita nao, lakini kadri siku zinavyokwenda akajikuta anazidi kumpenda Recho, amesalitika vilivyo. Tokea aanze kuyajua mapenzi alikuwa hajawahi kustareheshwa kwa ufundi mkubwa kama anavyofanyiwa na Recho. Akakata shauri kuwa lazima Recho awe wake peke ajifaidie anavyotaka yeye. Akampa masharti kuwa akitaka awe mpenzi wake aachane na shughuli ya uchangudoa atamfanyia mambo makubwa maishani mwake.
Recho baada ya kumgundua kuwa Mr.Lorenzo ni pochi nene, sio pangu pakavu tia mchuzi nile hakuwa na shida kutimiza masharti aliyotakiwa kuyatekeleza ya kuachana na biashara ya kujiuza mwili wake. Mr.Lorenzo kuonyesha amekufa na kuoza kwa Recho akamuuliza amfungulie mradi gani wa kujikimu kimaisha. Recho alifurahi sana na kuona wakati wa kulipa kisasi kwa mpenzi wake wa zamani Martin Tenga umetimu. Recho bila kupepesa macho, akataka kufunguliwa biashara ya Hoteli, na kumtaka Mr Lorenzo amnunulie 'Martino Royal Hotel' iliyopo Jijini Dar es Salaam, Hoteli ambayo ilikuwa sokoni inapigwa bei. Baada ya Bwana Martin Tenga kushikiliwa huko nchini Italia, ndugu zake wakashindwa namna ya uendeshaji wa Hoteli hiyo ya kifahari hivyo wakaiweka sokoni kwa mteja yoyote atakayejitokeza.
Hoteli hiyo ya kifahari yenye roshani 10 ilikuwa inauzwa milioni 200 taslimu. Mr.Lorenzo alichofanya ni kutekeleza ombi la kimada wake huyo kwa moyo mmoja kwa kufanya taratibu zote za manunuzi ya Hoteli hiyo. Hati ya manunuzi ya Hoteli hiyo iliandikishwa kuwa Hoteli hiyo inamilikiwa kwa ubia kati ya mzawa Recho na mwekezaji Mr.Lorenzo. Hivyo Recho alikuwa na furaha sheshe kwa kufanikisha kuirudisha Hoteli yake aliyoiasisi kwenye mikono yake mwenyewe kisha akaporwa kilaghai na mpenziwe wa zamani Martin Tenga ambaye alikuwa hataki hata kumsikia wala kumuona. Alitamani sana Recho, Mr.Martin Tenga arudi nchini Tanzania na aone jinsi Hoteli aliyodhulumu ilivyotua tena mikononi mwa Recho.
Kwa upande wake Mr. Lorenzo alikuwa anaendelea na shughuli yake haramu kwa kificho sana, bila Recho kushtukia kazi yake inayomleta mara kwa mara katika nchi za Afrika Mashariki.
Wasichana wa kucheza filamu hizo za ngono alikuwa hapati shida kuwapata, kutokana na tabia ya wasichana wengi wa Majiji hayo makubwa ya Afrika Mashariki kuanzia Nairobi, Kigali, Kampala, Bujumbura na Dar es Salaam kuendekeza utajiri wa mezani. Ule utajiri wa bila kutoka jasho kwa kutumia uzuri wa maumbile yao. Maisha yakawa yanasonga baina ya wapenzi hao wapya ambao ni kaka na dada wasiotambuana.
Lakini kama kawaida yake Recho kwenye pesa huwa ana simile, akili yake inaruka na kuwaza kufanya dhuluma, akaandaa mpango wa kumuondoa kwenye umilki wa Hoteli hiyo Mr.Lorenzo, kabla kibao hakijamgeukia na kufanyima unyama wa kutisha na Mr.Lorenzo. Unyama ambao ulimuacha mgonjwa kitandani maisha yake yote.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Deborah alishaanza kuwa mzoefu wa mitaa ya Kisutu stendi ya Mabasi ya mikoani. Alishakata miezi miwili tokea atue Jijini Mwezi Novemba. Alipata kibarua cha kuuza kioski cha kuuza vitafunwa na vya vinywaji baridi kwa abiria na Wafanyabiashara ndogo ndogo kuzunguka eneo hilo la Kisutu. Haikumchukua muda kuzoea biashara maeneo hayo, hasa ikichukuliwa kuwa ana uzoefu wa biashara hizo kwa zaidi ya miaka 4 kutokea kule Kijiji Mikongeni, Morogoro. Kioski alichokuwa anauza kilikuwa kilikuwa kinamilikiwa na Koplo Marieta, Askari wa kituo cha polisi, Msimbazi, Kariakoo. Deborah alikuwa anamchukulia Koplo Marieta kama malaika mkombozi kwake. Hivyo ni kwa namna alivyomchomoa katika mikono ya polisi wenzake waliotaka kumfungulia kesi ya uzembe na uzururaji kisha wamrudishe kijiji kwao tena. Siku ile aliyotoroka nyumbani kwao alifanikiwa kupata msaada wa usafiri wa kumfikisha Jijini Dar es Salaam kama alivyotarajiwa.
"Sasa mwanangu Deborah tumeingia tayari Jijini Dar es Salaam, tutakushusha hapa Buguruni, tutakupakiza kwenye daladala litakalokushusha stendi ya Mabasi ya Kisutu kama ulivyoelekeza kuwa mwenyeji wako yupo huko" aliongea dereva Babu Juma kwa sauti ya uchovu wa safari, akimuelekeza Deborah kuwa wameshawasili ndani ya Jiji. Babu Juma alikuwa ameendesha gari lake usiku kucha bila kupumzika tena akiwa ameutwika mtindi wa pombe za kienyeji kichwani mwake. "Ahsante sana Babu Juma tutaonana tena Mungu akipenda, nakutakia kazi njema" Deborah alishukuru huku akiunda tabasamu moja matata usoni mwake. Shukrani hiyo ilikuwa ni kutokana na msaada wa bure aliopewa na dereva yule. Baada ya hapo akaanza kukusanya kifurushi chake cha nguo akijiandaa kushuka chini ya gari lile.
Deborah aliwadanganya akina Babu Juma na Taniboi wake kuwa mwenyeji wake anamsubiria kumpokea stendi ya Mabasi ya Mikoani ya Jijini Dar es Salaam. Wakati ukweli wa mambo ni kuwa hakuwa na ndugu wala rafiki katika Jiji hilo la Dar es Salaam. Alichokuwa anajipa moyo ni kuwa Mungu atampa stara asiadhirike ugenini. Aliamini bila kwa yakini isiyo na mashaka kuwa kwa baraka za Mola atapata msamaria mwema atakayemuangalia kwa chakula, mavazi na malazi. Walikuwa wameingia Jijini Dar es Salaam asubuhi asubuhi wakiwa wametoka Morogoro tokea manane ya usiku.
Akawashukuru na kuagana nao, akiwaongopea amekuja Jijini Dar es Salaam kusoma masomo ya ziada 'Tuition' kwa ajili ya kujiandaa na masomo ya kidato cha kwanza kwa mwaka ujao wa 1997. Aliposhuka tu kwenye Lori lile, Taniboi nae akawa nae bega kwa bega kumtafutia Daladala kama alivyoomba. Basi hizo ndogo zilikuwa zinaitwa 'Daladala' kutokana na kutoza nauli ya shilingi 5 kwa safari. Deborah kwa bahati nzuri alipata siti ya dirishani, hivyo macho yake yalikuwa yamekodoka barabarani utasema anakata roho kutokana na kushangazwa na uzuri wa maghorofa na magari yanayopishana barabarani kwa kasi kubwa. Tokea anapata akili timamu mpaka anavunja ungo, alikuwa hajawahi kupata mtoko wowote wa safari hata walau wa kufika Morogoro Mjini. Hivyo hiyo ndio ilikuwa ziara yake ya kwanza kubwa katika maisha yake.
Daladala lile alilopanda bila kuchelewa likamshusha Kisutu kama alivyohitaji huku likiendelea na safari zake kuwafikisha abiria wengine. Aliposhuka tu pale stendi na kuuona umati wa watu stendi pale, moyo wake ukamlipuka kwa uoga. Kilichokuwa kinamshangaza watu wale walikuwa wanaongea Kiswahili cha haraka haraka kama ndege tena chenye kukatisha maneno. Lugha ambayo ilikuwa inampa wakati mgumu sana kuelewa wanaongea kitu gani haswa. Hofu ilimjaa zaidi baada ya kuona kila mtu alikuwa ameshika hamsini zake ametingwa na mambo yake hamna hata mmoja wa kumuuliza hali yake mgeni na anahitaji msaada gani. Alitegemea ukarimu wanaofanyiana kijiji kwao huku Mjini uwe maradufu.
Akaanza kuuchukia Mji huo kuanzia muda huo huo kutokana na watu wake kukosa utu na ubinadamu. Kiu ya maji na njaa ilikuwa imemkamata vilivyo asubuhi hiyo utasema yupo kwenye mfungo. Deborah akaanza kutupa macho yake huku na kule kutafuta walau kisima cha kujichotea maji ya kunywa kama kule kijijini kwao. Pia alitarajia huenda atauona mti wa mchungwa au muembe walau abahatike kuchuma tunda ashibishe minyoo tumboni. Kwa bahati mbaya hakuambulia kiti chochote katika alivyovitamani. Zaidi ya kuziona embe chache na machungwa yamepangwa kwenye meza za wachuuzi wadogo wadogo zinauzwa.
Alishangazwa sana kuona matunda wanayogaiana bure kijijini kwao mpaka wanyama kama nyani na tumbili wanajipocholea bwerere huku Mjini yanauzwa kwa bei ya kuchupa. "Hawa watu wa Mji huu, nimewanyooshea mikono na wana dhambi sana, embe za shamba la Bi. Pembe kule kijijini tunajiokotea bure tu" alinong'ona moyoni mwake. Akawa amejikunyata kwenye banda la wasafiri akiwa amejichanganya na wasafiri wengine wanaosubiri Mabasi ya kuelekea mikoani, huku akizichanga karata zake kichwani mwake kuitafakari hatima yake. Kwenye akiba yake kibindoni alikuwa na shilingi 55 taslimu, alizozipata katika mauzo ya shingo za kuku, ndizi na sinia za kuuzia asusa hizo zote alizipiga bei.
Alijitahidi kuvumilia njaa na kiu ili mradi asikiguse kibubu chake cha akiba lakini ilipofika majira ya adhuhuri, uzalendo ukamshinda. Usicheze na tumbo wewe, ndio maana watu wazima na heshima zao wanapokea rushwa, wanajiingiza kwenye ufisadi, wanawake wanajiuza miili yao, ukiwauliza kisa tumbo. Ikabidi aishiwe ujanja, asije kuanguka njaa bure na pesa anayo. Kiunyonge kabisa ikabidi afungue kibubu chake na kujongea banda la jirani la mama lishe na kuagiza chakula, akala, akashiba na kuendelea kutafakari kitu gani cha kufanya kadri saa zinavyozidi kwenda. Mpaka kufika majira ya magharibi, asilimia kubwa ya abiria walikuwa tayari wameshatawanyika zao mmoja mmoja kuelekea majumbani kwao kupumzika. Mabasi ya kutokea mikoani asilimia kubwa yalikuwa yameshawasili zao.
Kiza kikaanza kutanda angani huku mawingu mekundu yakizidi kupotea kuashiria usiku mbichi unakaribishwa. Hofu ikazidi kushamiri katika moyo wa Deborah huku akianza kujutia kwanini hata alichukua maamuzi magumu na ya hasira ya kuja Jijini Dar es Salaam bila kujipanga. Akazidi kujipa nasaha za majuto ni mjukuu kuwa siku zote hasira ni hasara. Na daima mwanadamu hutakiwa kufanya maamuzi wakati una hasira sana au una furaha sana, lazima utapotoka katika maamuzi yako. Sasa alijiona kabisa anapatwa na fedheha ugenini, sehemu ambayo hamna mtu yoyote anayemfahamu kwa kina. Wasela wa stendi nao hawakutaka kujivunga, tayari wakaanza kuiona fursa ya kujiegesha kwa Deborah usiku huo. Walishazoea kujipatia wasichana wa mahonyo wanaozagaazagaa stendi hapo. Kwao suala la magonjwa ya zinaa kama UKIMWI, sijui Kaswende, Kisonono na mengineyo ilikuwa ni hadithi za alinacha zisizo na mashiko. Walichokuwa wanajali wao ni kuitimizia nafsi hawaa zake inazohitaji.