Riwaya: Matanga ya rohoni

Riwaya: Matanga ya rohoni

SEHEMU-30

SURA YA KUMI
Recho nyota yake ilizidi kung'aa kiuchumi. Ngwenje alizokuwa analipwa na Washefa wake kwenye kazi yake mpya kuuza mwili zilikosa kifani. Zilimtosha kupanga nyumba nzima peke yake katika eneo la Sinza na kujipatia usafiri binafsi wa kukata mitaa akiwa Jijini Dar es Salaam. Katika wanawake wa kwanza kwanza Jijini Dar es Salaam kumiliki gari la kifahari zama hizo la aina ya 'Korando' toleo jipya. Mpaka ikafika hatua anawaponda kwa kejeli wale wanaouponda wa fisi au kupanda usafiri wa umma kwenye mizunguko yao ya kila siku ndani ya Jiji. Alishajiapiza kamwe hawezi kupanda daladala hata kama gari yake italeta matatizo, alikuwa yupo tayari akodishe taksi hata kama ni siku nzima. Alishafanikiwa kukata miaka kadhaa Jijini Dar es Salaam huku jina lake likiwa maarufu kwenye kumbi na klabu zote kubwa za starehe Jijini.

Bendi zote kubwa za muziki wa dansi hapa nchini kwenye nyimbo zao wakawa wanatia vionjo vya kulitaja jina lake. Mara kwenye nyimbo anaimbwa "utasikia dadaa Rechooo, una sura nzuri kama malaika" na sifa kedekede za kumpamba mafuta kwa mgongo wa chupa. Nae Recho alivyokuwa mpenda misifa, akitajwa tu alikuwa anacheka na kuterema kisha lazima asimame toka kitini kwenda kuwatuza wanamuziki wote wa bendi.

Katika harakati zake za umalaya, Recho akaibua fursa nyingine nchini Jijini Nairobi. Akafanya maamuzi ya kurudi tena huko kwa mara ya pili baada ya kukatika miaka kadhaa tokea afukuzwe ndani ya masaa 24 na kudhulumiwa Klabu yake ya "Nairobee By Night". Kilichomsukuma arudishe majeshi tena Jijini Nairobi ni fursa ya kuwadaka watalii wa kutokea ughaibuni wanaotua Jijini Nairobi. Kenya ilikuwa na wasaa mkubwa wa kupokea watalii kutokana na kuwa na shirika la ndege lenye nguvu la 'Kenya Airways' kulinganisha na Tanzania ambayo shirika lake la ndege la 'ATC' lilikuwa lipo mahututi linapumulia gesi likiwa na kidege kimoja tu tena chakavu. Maelfu ya watalii kutokana na kutoka nchi za Ulaya walikuwa wanamiminikia Kenya wakiaminishwa na propaganda kuwa Mlima Kilimanjaro upo Kenya. Kisha wakija kutanabahi kuwa Mlima huo, upo Tanzania wanakuwa tayari fedha nyingi za kigeni wamezitumia nchini Kenya na Tanzania kuambulia mabaki tu. Hivyo Recho akaona Nairobi ataweza kuibua madanga ya kizungu yenye pesa sufufu hivyo kuzidi kujiimarisha kiuchumi.

Na kwakuwa Jiji la Nairobi analijua nje ndani, haikumpa ugumu kulizoea tena Jiji hilo kwa haraka. Sasa akawa mtu wa kambi popote, anakaa Nairobi wiki mbili kisha anarejea Jiji Dar es Salaam, anazunguka kama popo baina ya Majiji hayo mawili. Baada ya miezi kadhaa tu akafanikiwa kutengeneza mirija ya kuingiza pesa za kutosha. Katika hangaika yake ya kusaka pesa haramu, akafanikiwa kumnasa kiruka mito wa kizungu, kutoka nchini Italia wa rika lake kabisa ambaye kwa jina alikuwa anajulikana kama Mr.Lorenzo. Huyu mzungu, buzi lake jipya alikuwa ni baba mlezi kabisa wa mtoto wa Recho, Pesambili. Mr.Lorenzo alikuja Afrika Mashariki kwa gia ya utalii lakini kiuhalisia alikuja kuangalia fursa kwa ajili ya kazi haramu maalumu. Kazi ambazo zilikuwa zinamuingizia Mr.Lorenzo mabilioni ya pesa katika nchi mbalimbali za Kiafrika alizowekeza.

Nchini kwao Italia alikuwa anajipambanua kama Mfanyabiashara maarufu mwenye kumiliki kampuni ya kuzalisha na kusambaza filamu za wanyama pori 'Wildlife'. Kampuni hiyo ya Mr. Lorenzo ilikuwa inajulikana kama 'Talking Trees and Animals Creative(TTAC)-Films Company LTD. Baadhi ya serikali za nchi za Kiafrika zilikuwa zimeingia nae mkataba wa kuwatangazia vivutio vyao vya kitalii. TTAC-Films Company Ltd, ilijipambanua kama moja ya kampuni bora kabisa ya filamu Jijini Turin nchini Italia. Lakini sirini kampuni hiyo ilikuwa inazalisha pia filamu za ngono zinazorekodiwa maeneo tofautitofauti katika nchi mbalimbali za Afrika. Nchi nyingi za Afrika zilikuwa zimepiga marufuku kwa raia kushiriki kuandaa filamu za ngono, na zilikuwa zimeweka adhabu kali kwa watakaobainika. Hivyo kampuni ya TTAC-Films Company LTD inayomilikiwa na Mr.Lorenzo ikawa inafanya shughuli hizo kinyemela kinyume na utaratibu. Kwa kuwahadaa washiriki hao kwa kuwapa fedha sufufu ili mradi wasikatae kurekodiwa filamu hizo.

Shughuli hizo walikuwa wanazifanya kwa usiri mkubwa sana. Mr Lorenzo na wahuni wenzake walikuwa wanakwenda kuzuru nchi mbalimbali za Kiafrika kwa kutumia hati feki za kusafiria wakijifanya kama watalii wenye kuvutiwa na mali asili za Afrika kumbe wanafanya pia utalii wa ngono. Mr.Lorenzo kwa Recho alijitambulisha kwa jina bandia la 'Luis Van Odergaard', Mdachi wa Uholanzi, akijifanya ni Mfanyabiashara wa vito vya madini. Hakutaka kabisa Tengo amjue undani wa shughuli yake anayoifanya. Na Recho nae mara tu baada ya kufariki mama yake akajibadilisha jina na kuanza kujiita 'Recho Kavishe', akitumia ubini wa ukoo wa babu yake mzaa mama. Hakutaka kabisa kulisikia jina la baba yake mzazi Mzee 'Francesco' ambaye kwanza alikuwa hajawahi kumtia machoni na wala kupata huduma zake za matumizi. Alikuwa anamchukia baba yake mzazi kupita maelezo hasa kutokana na maamuzi ya kumtelekeza hali ya kuwa mama yake alikuwa anamuambia kuwa baba yake ni mkwasi wa mali huko nchini Italia alipo.

Maisha yao ya usanii na ulaghai yakasababisha ndugu wa baba mmoja wasitambuane na waangukie katika mapenzi motomoto bila kufahamu kuwa wao ni ndugu wa damu kabisa. Mwanzoni Mr.Lorenzo alimchukulia Recho kama walivyo malaya wengine tu aliowahi kupita nao, lakini kadri siku zinavyokwenda akajikuta anazidi kumpenda Recho, amesalitika vilivyo. Tokea aanze kuyajua mapenzi alikuwa hajawahi kustareheshwa kwa ufundi mkubwa kama anavyofanyiwa na Recho. Akakata shauri kuwa lazima Recho awe wake peke ajifaidie anavyotaka yeye. Akampa masharti kuwa akitaka awe mpenzi wake aachane na shughuli ya uchangudoa atamfanyia mambo makubwa maishani mwake.

Recho baada ya kumgundua kuwa Mr.Lorenzo ni pochi nene, sio pangu pakavu tia mchuzi nile hakuwa na shida kutimiza masharti aliyotakiwa kuyatekeleza ya kuachana na biashara ya kujiuza mwili wake. Mr.Lorenzo kuonyesha amekufa na kuoza kwa Recho akamuuliza amfungulie mradi gani wa kujikimu kimaisha. Recho alifurahi sana na kuona wakati wa kulipa kisasi kwa mpenzi wake wa zamani Martin Tenga umetimu. Recho bila kupepesa macho, akataka kufunguliwa biashara ya Hoteli, na kumtaka Mr Lorenzo amnunulie 'Martino Royal Hotel' iliyopo Jijini Dar es Salaam, Hoteli ambayo ilikuwa sokoni inapigwa bei. Baada ya Bwana Martin Tenga kushikiliwa huko nchini Italia, ndugu zake wakashindwa namna ya uendeshaji wa Hoteli hiyo ya kifahari hivyo wakaiweka sokoni kwa mteja yoyote atakayejitokeza.

Hoteli hiyo ya kifahari yenye roshani 10 ilikuwa inauzwa milioni 200 taslimu. Mr.Lorenzo alichofanya ni kutekeleza ombi la kimada wake huyo kwa moyo mmoja kwa kufanya taratibu zote za manunuzi ya Hoteli hiyo. Hati ya manunuzi ya Hoteli hiyo iliandikishwa kuwa Hoteli hiyo inamilikiwa kwa ubia kati ya mzawa Recho na mwekezaji Mr.Lorenzo. Hivyo Recho alikuwa na furaha sheshe kwa kufanikisha kuirudisha Hoteli yake aliyoiasisi kwenye mikono yake mwenyewe kisha akaporwa kilaghai na mpenziwe wa zamani Martin Tenga ambaye alikuwa hataki hata kumsikia wala kumuona. Alitamani sana Recho, Mr.Martin Tenga arudi nchini Tanzania na aone jinsi Hoteli aliyodhulumu ilivyotua tena mikononi mwa Recho.
Kwa upande wake Mr. Lorenzo alikuwa anaendelea na shughuli yake haramu kwa kificho sana, bila Recho kushtukia kazi yake inayomleta mara kwa mara katika nchi za Afrika Mashariki.

Wasichana wa kucheza filamu hizo za ngono alikuwa hapati shida kuwapata, kutokana na tabia ya wasichana wengi wa Majiji hayo makubwa ya Afrika Mashariki kuanzia Nairobi, Kigali, Kampala, Bujumbura na Dar es Salaam kuendekeza utajiri wa mezani. Ule utajiri wa bila kutoka jasho kwa kutumia uzuri wa maumbile yao. Maisha yakawa yanasonga baina ya wapenzi hao wapya ambao ni kaka na dada wasiotambuana.

Lakini kama kawaida yake Recho kwenye pesa huwa ana simile, akili yake inaruka na kuwaza kufanya dhuluma, akaandaa mpango wa kumuondoa kwenye umilki wa Hoteli hiyo Mr.Lorenzo, kabla kibao hakijamgeukia na kufanyima unyama wa kutisha na Mr.Lorenzo. Unyama ambao ulimuacha mgonjwa kitandani maisha yake yote.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Deborah alishaanza kuwa mzoefu wa mitaa ya Kisutu stendi ya Mabasi ya mikoani. Alishakata miezi miwili tokea atue Jijini Mwezi Novemba. Alipata kibarua cha kuuza kioski cha kuuza vitafunwa na vya vinywaji baridi kwa abiria na Wafanyabiashara ndogo ndogo kuzunguka eneo hilo la Kisutu. Haikumchukua muda kuzoea biashara maeneo hayo, hasa ikichukuliwa kuwa ana uzoefu wa biashara hizo kwa zaidi ya miaka 4 kutokea kule Kijiji Mikongeni, Morogoro. Kioski alichokuwa anauza kilikuwa kilikuwa kinamilikiwa na Koplo Marieta, Askari wa kituo cha polisi, Msimbazi, Kariakoo. Deborah alikuwa anamchukulia Koplo Marieta kama malaika mkombozi kwake. Hivyo ni kwa namna alivyomchomoa katika mikono ya polisi wenzake waliotaka kumfungulia kesi ya uzembe na uzururaji kisha wamrudishe kijiji kwao tena. Siku ile aliyotoroka nyumbani kwao alifanikiwa kupata msaada wa usafiri wa kumfikisha Jijini Dar es Salaam kama alivyotarajiwa.

"Sasa mwanangu Deborah tumeingia tayari Jijini Dar es Salaam, tutakushusha hapa Buguruni, tutakupakiza kwenye daladala litakalokushusha stendi ya Mabasi ya Kisutu kama ulivyoelekeza kuwa mwenyeji wako yupo huko" aliongea dereva Babu Juma kwa sauti ya uchovu wa safari, akimuelekeza Deborah kuwa wameshawasili ndani ya Jiji. Babu Juma alikuwa ameendesha gari lake usiku kucha bila kupumzika tena akiwa ameutwika mtindi wa pombe za kienyeji kichwani mwake. "Ahsante sana Babu Juma tutaonana tena Mungu akipenda, nakutakia kazi njema" Deborah alishukuru huku akiunda tabasamu moja matata usoni mwake. Shukrani hiyo ilikuwa ni kutokana na msaada wa bure aliopewa na dereva yule. Baada ya hapo akaanza kukusanya kifurushi chake cha nguo akijiandaa kushuka chini ya gari lile.

Deborah aliwadanganya akina Babu Juma na Taniboi wake kuwa mwenyeji wake anamsubiria kumpokea stendi ya Mabasi ya Mikoani ya Jijini Dar es Salaam. Wakati ukweli wa mambo ni kuwa hakuwa na ndugu wala rafiki katika Jiji hilo la Dar es Salaam. Alichokuwa anajipa moyo ni kuwa Mungu atampa stara asiadhirike ugenini. Aliamini bila kwa yakini isiyo na mashaka kuwa kwa baraka za Mola atapata msamaria mwema atakayemuangalia kwa chakula, mavazi na malazi. Walikuwa wameingia Jijini Dar es Salaam asubuhi asubuhi wakiwa wametoka Morogoro tokea manane ya usiku.

Akawashukuru na kuagana nao, akiwaongopea amekuja Jijini Dar es Salaam kusoma masomo ya ziada 'Tuition' kwa ajili ya kujiandaa na masomo ya kidato cha kwanza kwa mwaka ujao wa 1997. Aliposhuka tu kwenye Lori lile, Taniboi nae akawa nae bega kwa bega kumtafutia Daladala kama alivyoomba. Basi hizo ndogo zilikuwa zinaitwa 'Daladala' kutokana na kutoza nauli ya shilingi 5 kwa safari. Deborah kwa bahati nzuri alipata siti ya dirishani, hivyo macho yake yalikuwa yamekodoka barabarani utasema anakata roho kutokana na kushangazwa na uzuri wa maghorofa na magari yanayopishana barabarani kwa kasi kubwa. Tokea anapata akili timamu mpaka anavunja ungo, alikuwa hajawahi kupata mtoko wowote wa safari hata walau wa kufika Morogoro Mjini. Hivyo hiyo ndio ilikuwa ziara yake ya kwanza kubwa katika maisha yake.

Daladala lile alilopanda bila kuchelewa likamshusha Kisutu kama alivyohitaji huku likiendelea na safari zake kuwafikisha abiria wengine. Aliposhuka tu pale stendi na kuuona umati wa watu stendi pale, moyo wake ukamlipuka kwa uoga. Kilichokuwa kinamshangaza watu wale walikuwa wanaongea Kiswahili cha haraka haraka kama ndege tena chenye kukatisha maneno. Lugha ambayo ilikuwa inampa wakati mgumu sana kuelewa wanaongea kitu gani haswa. Hofu ilimjaa zaidi baada ya kuona kila mtu alikuwa ameshika hamsini zake ametingwa na mambo yake hamna hata mmoja wa kumuuliza hali yake mgeni na anahitaji msaada gani. Alitegemea ukarimu wanaofanyiana kijiji kwao huku Mjini uwe maradufu.

Akaanza kuuchukia Mji huo kuanzia muda huo huo kutokana na watu wake kukosa utu na ubinadamu. Kiu ya maji na njaa ilikuwa imemkamata vilivyo asubuhi hiyo utasema yupo kwenye mfungo. Deborah akaanza kutupa macho yake huku na kule kutafuta walau kisima cha kujichotea maji ya kunywa kama kule kijijini kwao. Pia alitarajia huenda atauona mti wa mchungwa au muembe walau abahatike kuchuma tunda ashibishe minyoo tumboni. Kwa bahati mbaya hakuambulia kiti chochote katika alivyovitamani. Zaidi ya kuziona embe chache na machungwa yamepangwa kwenye meza za wachuuzi wadogo wadogo zinauzwa.

Alishangazwa sana kuona matunda wanayogaiana bure kijijini kwao mpaka wanyama kama nyani na tumbili wanajipocholea bwerere huku Mjini yanauzwa kwa bei ya kuchupa. "Hawa watu wa Mji huu, nimewanyooshea mikono na wana dhambi sana, embe za shamba la Bi. Pembe kule kijijini tunajiokotea bure tu" alinong'ona moyoni mwake. Akawa amejikunyata kwenye banda la wasafiri akiwa amejichanganya na wasafiri wengine wanaosubiri Mabasi ya kuelekea mikoani, huku akizichanga karata zake kichwani mwake kuitafakari hatima yake. Kwenye akiba yake kibindoni alikuwa na shilingi 55 taslimu, alizozipata katika mauzo ya shingo za kuku, ndizi na sinia za kuuzia asusa hizo zote alizipiga bei.

Alijitahidi kuvumilia njaa na kiu ili mradi asikiguse kibubu chake cha akiba lakini ilipofika majira ya adhuhuri, uzalendo ukamshinda. Usicheze na tumbo wewe, ndio maana watu wazima na heshima zao wanapokea rushwa, wanajiingiza kwenye ufisadi, wanawake wanajiuza miili yao, ukiwauliza kisa tumbo. Ikabidi aishiwe ujanja, asije kuanguka njaa bure na pesa anayo. Kiunyonge kabisa ikabidi afungue kibubu chake na kujongea banda la jirani la mama lishe na kuagiza chakula, akala, akashiba na kuendelea kutafakari kitu gani cha kufanya kadri saa zinavyozidi kwenda. Mpaka kufika majira ya magharibi, asilimia kubwa ya abiria walikuwa tayari wameshatawanyika zao mmoja mmoja kuelekea majumbani kwao kupumzika. Mabasi ya kutokea mikoani asilimia kubwa yalikuwa yameshawasili zao.

Kiza kikaanza kutanda angani huku mawingu mekundu yakizidi kupotea kuashiria usiku mbichi unakaribishwa. Hofu ikazidi kushamiri katika moyo wa Deborah huku akianza kujutia kwanini hata alichukua maamuzi magumu na ya hasira ya kuja Jijini Dar es Salaam bila kujipanga. Akazidi kujipa nasaha za majuto ni mjukuu kuwa siku zote hasira ni hasara. Na daima mwanadamu hutakiwa kufanya maamuzi wakati una hasira sana au una furaha sana, lazima utapotoka katika maamuzi yako. Sasa alijiona kabisa anapatwa na fedheha ugenini, sehemu ambayo hamna mtu yoyote anayemfahamu kwa kina. Wasela wa stendi nao hawakutaka kujivunga, tayari wakaanza kuiona fursa ya kujiegesha kwa Deborah usiku huo. Walishazoea kujipatia wasichana wa mahonyo wanaozagaazagaa stendi hapo. Kwao suala la magonjwa ya zinaa kama UKIMWI, sijui Kaswende, Kisonono na mengineyo ilikuwa ni hadithi za alinacha zisizo na mashiko. Walichokuwa wanajali wao ni kuitimizia nafsi hawaa zake inazohitaji.
 
SEHEMU-31



Hofu ikazidi kushamiri katika moyo wa Deborah huku akianza kujutia kwanini hata alichukua maamuzi magumu na ya hasira ya kuja Jijini Dar es Salaam bila kujipanga. Akazidi kujipa nasaha za majuto ni mjukuu kuwa siku zote hasira ni hasara. Na daima mwanadamu hutakiwa kufanya maamuzi wakati una hasira sana au una furaha sana, lazima utapotoka katika maamuzi yako. Sasa alijiona kabisa anapatwa na fedheha ugenini, sehemu ambayo hamna mtu yoyote anayemfahamu kwa kina.

Wasela wa stendi nao hawakutaka kujivunga, tayari wakaanza kuiona fursa ya kujiegesha kwa Deborah usiku huo. Walishazoea kujipatia wasichana wa mahonyo wanaozagaazagaa stendi hapo. Kwao suala la magonjwa ya zinaa kama UKIMWI, sijui Kaswende, Kisonono na mengineyo ilikuwa ni hadithi za alinacha zisizo na mashiko. Walichokuwa wanajali wao ni kuitimizia nafsi hawaa zake inazohitaji. Wakaanza kumsarandia waondoke nae wakafanye yao, kila mmoja anamwaga sera zake na kutupa ndoano yake yenye chambo kwa shauku na mshawasha mkubwa wa kumuingiza mtegoni Deborah.

"Sistery....mambo vipi kama hauna mwenyeji, utaondoka na mimi uskonde, tuliza wahaka na jakamoyo...!" alichombweza mmoja wa vijana hao huku akijichekesha chekesha. "Jimmy..achana nae huyu dada ni wa kwetu kabisa toka Mji kasoro bahari lafudhi zake tu unaziskia kabisa. Naondoka nae mimi huyu, huu mkwaju wa maana haswa, toka Milima Uluguru..." aliongea mhuni mwingine kwa swaga za lafudhi za vijana wa Mjini akibishana na hasimu mwenzie.

Deborah hakujishughulisha nao, anawapiga kijicho pembe akawa amebaki amejikunyata, Amejivika ujasiri wa Simba wakati moyoni alikuwa na uoga wa kunguru huku akisali na kuomba kila aina ya dua wasije kumfanyia vitendo vya kifedhuli. Tayari usiku mbichi ulikuwa umeshaingia, kiza kilisha shamiri mawinguni huku nyota angani zikijitutumua kutoa nuru yake walau kufifisha makali ya giza kadri zinavyoweza. Wale wajuba wa stendi baada ya kumuona Deborah sio anuwai ya wasichana wanaojiokotea, wakaamua kutokomea zao vichwa chini kama kuku mwenye mdondo. Walikwenda kujaribu mawindo mengine, hiyo ndio ikawa salama na pona ya Deborah.

Usiku huo akala tena 'chips dume' za muhogo, na kusukumizia na maji ya kidebe, akarudi tena kwenye majlisi yake. Alikuwa ameshachanganyikiwa hajui hata cha kufanya. Taswira ya Jiji la Dar es Salaam kwa namna alivyokuwa anaisikia kwenye redio na kuisoma kwenye vitabu shuleni, na uhalisia wake ilikuwa ni mbingu na ardhi. Fikra zake zikimtuma kuwa amekuja kwenye Jiji la asali na maziwa kumbe yupo kwenye Jiji la shubiri mwitu. Jiji ambalo ni sehemu ya hatari kwa ustawi wa mwanadamu kuishi. Kadri muda ulivyokuwa unasonga ndio wavulana wadogo wadogo, machokoraa wanaolala kwenye stendi za Mabasi wakavamia banda la abiria. Wengine wakawa wanazidi kumjongelea Deborah, ili mradi tafrani mtindo mmoja.

Wakiwa baadhi yai wanatokwa na udenda wa fisi wa kufuata mkono wa binadamu udondoke ale. Walianza kumjongelea na kumuuliza maswali yasiyo na kichwa wala miguu, mpaka Deborah akaona kabisa dalili zote za kubakwa zipo waziwazi akijilegeza. Akapanga achomoke pale alipo, akajibanze kwenye kibanda chenye ulinzi wa mgambo. Alishakata shauri kuwa kesho jua likichomoza tu anakata tiketi ya kurejea nyumbani kwao Morogoro. Alishapanga atamuomba msamaha Mjomba pindi watakapoonana ana kwa ana. Mawazo yaliwaza kuwa siku akirejea, shangazi yake atamdunda kama paka mwizi. Kwanza alifahamu kuwa kijiji kizima kitakuwa kimeshapata taarifa zake za wizi wa shingo za kuku na sahani yake. Machozi yalianza kumlengalenga Deborah, akijiona kabisa yeye ni fungu la kukosa, na daima wambili havai moja.


Ghafla bin vuu....Deborah akiwa hana hili wala lile akashtukia Difenda la polisi limetua pale Stendi ya Kisutu likiwa na askari wapo kwenye kamatakamata ya wazembe na wazururaji. Wale vijana wahuni walipoiona tu ile gari kila mmoja wao mguu begani, kuhofia kutiwa mbaroni. Wale waliozubaa wote wakakamatwa akiwemo na Deborah. Msemo wa kuku mgeni hakosi kamba mguuni ukatimu kwa Deborah. "Wewe unafanya nini hapa sasa hivi usiku huu msichana mdogo kama wewe..!" alibandikwa swali Deborah na mmoja wa maafande wale, yakifuatiwa na mkururu wa maswali ya kipolisi kutoka kwa maaskari wengine.

Deborah akabakia kujing'ata ulimi tu, hawezi kabisa kujitetea, akiwa pia haamini kama amedakwa na wana usalama. Baada ya kushindwa kujieleza kwa ufasaha nae akasombwa na polisi wale kwenye msako huo wa usiku kwa kutupiwa kwenye Difenda. Kisha moja kwa moja akaenda kutupwa selo ya kituo cha polisi Msimbazi, kusubiria kuwekwa kitimoto cha maswali ya ziada. Deborah alikuwa anamwaga mchozi mithili ya ngamia anayetaka kuchinjwa akiwa katika majuto makubwa juu ya maamuzi yake ya hasira ya kutoroka nyumbani namna yalivyomponza. Kwa akili zake za utoto alijua kukamatwa na polisi ndio tiketi ya kufungwa jela.

Walipofikishwa kituoni, wakatenganishwa, wanawake kwao na wanaume kivyao. Baada ya hapo wakaanza kuhojiwa kila mmoja kivyake vyake sababu ya kukamatiwa huko mitaani. Ilipofika zamu ya Deborah, akaingizwa kwenye chumba cha askari mwanamke. Huko ikabidi autapike ukweli wake wote anaoujua kuhusu yeye mbele ya Koplo Marieta. Alimueleza kinagaubaga bila kuficha kitu mpaka sababu iliyomfanya akimbie nyumbani kwa Mjomba Kobelo kukwepa mateso ya shangazi yake. Koplo Marieta, kama binadamu mwenye moyo wenye nyama, imani ikamuingia akashikwa na uchungu mkubwa kutokana na mateso aliyoyapitia Deborah katika umri mdogo.

Hivyo akafunga nae ahadi ya kumchukua, ataishi nae nyumbani kwake kisha utakapofika muda wa kuripoti shule atampa pesa ya ada aende akasome. Deborah akawa amechomokea kwenye tundu la sindano chupuchupu yamkute mambo. Toka hapo Deborah akahamia rasmi nyumbani kwa Koplo Marieta kwenye kota za polisi hapo hapo Msimbazi maghorofani. Shida, tabu na mateso yote aliyopitia akayazika kwenye kaburi la sahau, kutokana na jinsi Koplo Marieta alivyokuwa anamjali. Akapumzishwa kazi za kipagazi na sulubu alizokuwa anafanyishwa na shangazi yake kule kijijini. Kazi yake mpya katika siku za fadhili wakati anasubiria muda wa shule kufunguliwa ikawa asubuhi na mapema kabisa anadamka kwenda Kisutu kwenye Kioski cha biashara kinachomilikiwa na mfadhili wake Koplo Marieta kusaidia kuuza biashara hiyo.

Deborah alikuwa anakaa hapo kibandani mpaka saa 1 mpaka 2 usiku ndio anarejea nyumbani kwa miguu tu. Kutoka Kisutu mpaka Msimbazi alikuwa anatumia takribani nusu saa, na kwa namna Deborah alivyokulia Kijijini umbali huo ulikuwa ni mfupi sana kwake. Siku za kupelekwa shule zilikuwa inakaribia, huku ada yake akiwa ameshakabidhiwa bado kununuliwa mahitaji madogo madogo ya kujikimu. Kwa jinsi Deborah alivyokuwa makini na pesa yake ya ada alikuwa anatembea nayo kila anapokwenda, akilala na kuamka nayo akiwa ameihifadhi katika nguo yake ya ndani. Akiwa Deborah amejistarehe nafsini mwake akijua muda sio mrefu ndoto yake ya mafanikio kielimu itaanza kutimia, akakumbwa na tukio baya sana maishani mwake.
Matanga ya rohoni ambayo alishaanza kuyasahau yakaibuka upya tena katika wakati usio muafaka, ikiwa ni siku tatu kabla ya shule kufunguliwa.

Deborah akatekwa na mtu asiyejulikana. Mtu huyo, aliyemteka alikuwa ni mrefu wa umbo, ana kifua kipana, akiwa anapenda kuvaa miwani nyeusi machoni mwake na kofia ya pama kichwani mwake. Hiyo yote ilikuwa ni mbinu kabambe ya kuficha wajihi wake usijulikane kisawasawa. Alijizoesha karibia wiki nzima kwenda kwenye kioski kunywa soda baridi kwa sambusa kila inapofika muda wa saa 1 usiku. Alikuwa ni mcheshi haswa atamtania Deborah na muuzaji mwenzake, akiwa ni mtu hadhiri haswa. Siku ingine atajitia kuwapa ofa ya soda na wao wanawe, wakamzoea akawazoea, kumbe ana lake jambo.

"Naona ndio muda wako wa kuondoka huu, nisubirie nimalize soda yangu tuondoke wote na mimi naelekea huko huko unakokwenda wewe..!" alizungumza yule jamaa baada ya kumuona Deborah anaagana na mwenzake ambaye yeye alikuwa anaishi Mbagala. "Mhhhh....kwani mie unajua ninakwenda wapi?" Deborah akauliza swali la kidadisi akiwa amepigwa na bumbuwazi baada kushtushwa na maelezo ya yule mtu kuwa anapajua anapoishi hivyo kupatwa na mshawaha nafsini mwake wa kutaka kumdadisi. "Rafiki yangu mwema na mzuri kama wewe nishindwe kujua unapoishi? Yatakuwa maskhara hayo, wewe unaishi Msimbazi kwenye kota za manjagu, nyumbani kwa Koplo Marieta...!" aliongea kwa kujiamini mtu yule huku akikita chupa yake ya Pepsi juu ya meza kuashiria amemaliza soda yake aliyokuwa ameinywa kwa mtindo wa tarumbeta.

Deborah akawa kama mtu aliyeshikwa na kihoro, akijiuliza maswali lukuki nafsini mwake akishangazwa na mgeni huyu kumjua mpaka anapoishi. Wakawa wanatoka wote kwa pamoja nje ya Kioski, mguu kwa mguu Deborah akiwa mbele. "Lakini mimi sina haja ya lifti nikikatisha hapo katikati natokea soko la Kariakoo tayari nipo nyumbani nimefika hivyo ahsante kwa wema wako, labda siku ingine" ghafla aligeuka nyuma Deborah na kuanza kujieleza kwa kujiamini huku akiwa amemtumbulia macho bila uoga. Deborah aliyakumbuka maneno ya wosia ya mfadhili wake Koplo Marieta ya kuwa, Jiji la Dar es Salaam watu wenye utu ni wachache sana wengi ni mbwa kasoro mkia waliovaa sura za kibinadamu, kutokana na tabia.

Hivyo hakuwa tayari kuambatana na mtu asiyemfahamu kwa kinagaubaga. Walikuwa tayari wawili hao wameshalifikia gari la yule jamaa aina ya 'Toyota Hilux Double Cabin' yenye vioo vya giza aliyokuwa ameiegesha meta chache pembeni ya kioski. "Haya nimekuelewa, hamna noma siku ingine nitakupa lifti utakapopenda wewe, chukua basi hii zawadi yako, uchangamshe kinywa......!" alijibu yule jamaa huku akitoa pipi mbili mfukoni, moja akinyoosha mkono kumpa Deborah na ingine akaifungua haraka haraka na kuitumbukiza kinywaji akianza kuimung'unya mbele ya Deborah. "Ahsante sana,ubarikiwe..!" alijibu Deborah huku akiipokea na kuanza kuimung'unya pipi ile mbele ya yule mgeni. Aliona bora amridhishe mgeni huyo asije kumuona ana madahiro kwa wateja.

Uso wa yule jamaa mwanzoni alipokataliwa lifti uliliwa debe, lakini Deborah alipoanza tu kuimung'unya pipi ile, akaunda tabasamu la ushindi lenye kufu ya furaha. Deborah ghafla akakimbilia tena kwenye Kioski kama mtu aliyegutushwa na kitu cha kuogofya. Mwenzake wa kioski alikuwa nae anajiandaa kufunga anaingiza viti ndani ya kibanda, tayari kwa kurejea sehemu anayoishi. Deborah alipomfikia yule mwenzake akawa anamuongelesha mambo mawili matatu, kama maagizo na maelekezo fulani aliyokuwa amesahau kumpa mwenzake wakati wakaagana. Yule mtu alikuwa ameegemea mlango wa mbele ya siti ya abiria kama vile bado anamsubiria Deborah.

Alikuwa anapiga miluzi huku kidole cha shahada cha mkono wa kulia kinauzungusha ufunguo kwa mbwembwe zote. Deborah akaanza kuja mpaka usawa wa ile gari, akawa ananyanyua mikono kama vile anaomba msaada fulani, huku kipochi chake cha mkononi anataka akitupe. Akaanza kuyumba kama mtu mwenye kisunzu au mlevi aliyezidiwa na pombe. "Naomba msaada wako najiskia vibaya sana, macho yanaishiwa nguvu, nifikishshshsh......!" Deborah alizungumza kwa shida kabla hata hajamaliza maelezo yake akataka aanguke chini.

Jamaa akamdaka hewani kabla hajakita sakafuni na hima hima akamfungulia siti ya mbele na kumbeba akamuweka vizuri na kufunga mlango. Akakimbilia kufungua mlango wake wa dereva na kuwasha gari. Akang'oa nanga kwa mwendo wa kasi, kila mtu aliyeshuhudia tukio lile akabaki amepigwa na butwaa asijue kilichotokea. Kilikuwa ni kitendo cha utekaji kilichotekelezwa ndani ya muda wa kufumba na kufumbua, ikionyesha tukio limefanywa na mtu mzoefu wa kazi hizo.

Deborah akawa ameshatekwa na mtu asiyejulikana na kupelekwa sehemu isiyojulikana kwa madhumuni yasiyojulikana. Sasa mambo yakawa mchafukoge kwa upande wa Deborah, hakuna mtu yoyote aliyeshuhudia tukio akawa na uthubutu wa kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi au kumpasha habari mtumishi mwenza wa Deborah pale kwenye kioski.

Kila mtu aliyeshuhudia tukio alikuwa anaogopa kukamatwa ili kuisaidia polisi kwa kosa lisilo lake. Kama ilivyo tabia za wakati wa Jiji la Dar es Salaam, kila mtu akashika hamsini zake kama vile hamna tukio lililotokea. Giza jeusi likatanda tena katika maisha ya Deborah, matanga ya moyoni mwake yanapiga hodi kila uchao kwa upande wao.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
SURA YA KUMI NA MOJA
"Mwana Side-Boy..... sio mwenzetu tena, kaula mbaya huko South anasukuma E- class Mercedes Benz, aah....hiki kijiwe noma sana" aliongea mmoja wa wanachama wa majlisi ya wahuni wanabadilishana mawazo. "Kweli hata mie nimeletewa hizo habari na Timammy yupo Mtoto wa Mzee Fakii wa Vijibweni, ananiambia mara ya mwisho walivyoonana nae alifikia hatua hadi kumiliki kadi nyeusi ya benki 'FNB Bank'. Hiyo kadi nasikia inamaanisha mtu ana zaidi ya Rand milioni 1 kwenye akaunti yake benki" aliongea kwa uchungu kijana mwingine huku anapuliza hewani moshi wa sigara bwege maarufu kwa jina la bangi.

"Bangi, nipe mabawa unipeperushe hewani mpaka South kwa Mjomba Madiba kama ndege, nikale bata mie..." alizidi kuyasasambua maneno kijana yule kwa hisia kali huku anajinuwizia kwa kutumia moshi wa bangi anaojifukiza nao kichwani. "Kwa hiyo hapa mpango mzima ni kuona namna gani na sisi tumainika, tusibakie kuwa washangiliaji tu wa mafanikio ya wenzetu" Mbweku alichangia mawazo huku nae akigongea kwa ishara ya kidole kuwa apitishiwe sigara bwege asuuze akili yake.

"Hamna kulala dogo Mbweku hapa ni amsha amsha na kesha mpaka che tupo Bondeni kwa Mjomba Madiba, ndio maana nimekuunganisha kwenye ule mchongo wa kazi ya Ubaunsa pale 'Martino Royal Hotel' sasa ukambwelembwele wewe mwenyewe. Pale ukifika "How are you" nyingiii na "Yes Yes Mzungu Kala Mafenesi" za kutosha kwa Watasha na kuwachangamkia, Zali la Mentali likikudondokea haina shanapa wala kwepesha unasanda tu, tutajuana mbele kwa mbele" alijibiwa Mbweku na mmoja wa mtu ambaye aliyeonekana kama ndio kiongozi wa kijiwe chao.

Walikuwa wanajikusanya kijiwe wanapeana michapo ya nchi za ughaibuni yenye sura ya hadaa kwa rangi na hali. Hayo ndio maisha yalikuwa maisha mapya ya kijana Mbweku akiwa Kigamboni. Maisha ya kulala kwenye Meli mbovu, maboti na mitumbwi. Maisha ya kula kwa donesheni ya kupiga ugali wa shirika kwa samaki wa kupora kwa wavuvi. Maisha ya kuvizia usiku abiria wanaoshuka kwenye Pantoni na kuwapora ndio ikawa kazi yao. Vijana hao walikuwa hawajali wala hawabali juu ya mustakabali wao wa maisha ya baadae. Mambo yote haramu mutlaki kama ulevi, unyang'anyi, uzinzi, kupigana na mengineyo yalikuwa ndio matendo yao ya kawaida.

Simulizi zile za kuzamia nchi za ughaibuni "Stowaway" zilikuwa zinamsisimua vilivyo Mbweku, hivyo akaazimia lazima azamie Bondeni na kama fursa ikiruhusu Ulaya kabisa. Miaka hiyo kiu ya vijana kutaka kuikimbia nchi yao ya Tanzania ilikuwa kubwa sana. Wapo waliokuwa wanataka kwenda Ughaibuni kwa malengo ya kutabahari katika fani mbalimbali za elimu katika Vyuo Vikuu bora duniani, wengine kufanya kazi au kutembea. Wengi wao katika vijana hao kilichokuwa kinawasukuma kwenda nje ni mseto wa uchumi mbaya, umaskini na kutaka tu kufahamu mambo. Hali hiyo yote ilichagizwa na ukosefu wa ajira kutokana na serikali kuacha kuajiri kutokana na uchumi mbovu wa nchi.


Sasa rasmi kijana Mbweku, baada ya kuhangaika huku na kule akajikuta amepata bahati ya kibarua rasmi cha ulinzi na kufanya usafi kwenye mazingira ya Hoteli ya 'Martino Royal Hotel'. Akawa amejitapua kwenye kundi la vijana hawana kazi hawana bazi, kazi yao kukaa vibarazani kupiga ubwete tu. Hoteli ambayo waasisi wake Mr.Martin Tenga na Recho ndio waliosababisha baba yake mzazi kijana Mbweku afungwe jela kutokana na pesa walizokwapua nyumbani kwa marehemu Bosi Minja. Hawa Mabosi wake ndio waliosababisha Mbweku na familia yake kwa ujumla waishi maisha yasiyo na mbele wala nyuma.

Kwa tabia za MbwekuJr za kutopenda kudhulumiwa haki zake, kama angetambua kuwa Bosi wake Recho, mmiliki wa hiyo Hoteli ndio chanzo cha yeye kuishi maisha magumu yaliyochangia aachane na shule na kuwa chokoraa mtaani, pangechimbika vilivyo. Sala na matumaini ya MbwekuJr ilikuwa ni siku moja afanikiwe kimaisha ili akawachukue kutoka kijijini mama yake na wadogo zake ili waishi pamoja kama zamani.


Mkasa wake wa mauaji ya Kibopa Mwinyi Fuad uliishia hewani, hata Mbweku mwenyewe hakuamini namna lilivyopotezewa. Alikuwa kila siku asubuhi anadamkia kwenye meza za wauza magazeti kufanya taftishi ya taarifa ya mauaji ya Mwinyi Fuad. Lakini akashangazwa taarifa hiyo haikupewa kipaumbele na vyombo hivyo vya habari. Ndugu wa Mwinyi Fuad walitaka kusitiri aibu ya ndugu yao, ya kukutwa amefariki uchi wa mnyama ufukweni mwa bahari tena usiku. Maana Jiji zima walikuwa wanatambua tabia zake chafu katika jamii.

Wakatembeza chai kwa baadhi ya waandishi wa habari wasio waaminifu ili kuhakikisha hakuna redio wala gazeti lolote litakalotoa taarifa ya msiba huo hadharani. Maiti yake siku ya pili yake tu, ikaenda kuzikwa kwao Pangani, Tanga. Huo ndio ukawa mwisho mbaya wa baradhuli Mwinyi Fuad, katika safari yake ya kurejea jongomeo kwa Mola wake. Kufichwa kwa siri hiyo ya kifo hicho na familia ikawa ni nafuu kwa jeshi la polisi kutokana na ugumu wa kumpata muuaji uliopo.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
 
SEHEMU-31



Hofu ikazidi kushamiri katika moyo wa Deborah huku akianza kujutia kwanini hata alichukua maamuzi magumu na ya hasira ya kuja Jijini Dar es Salaam bila kujipanga. Akazidi kujipa nasaha za majuto ni mjukuu kuwa siku zote hasira ni hasara. Na daima mwanadamu hutakiwa kufanya maamuzi wakati una hasira sana au una furaha sana, lazima utapotoka katika maamuzi yako. Sasa alijiona kabisa anapatwa na fedheha ugenini, sehemu ambayo hamna mtu yoyote anayemfahamu kwa kina.

Wasela wa stendi nao hawakutaka kujivunga, tayari wakaanza kuiona fursa ya kujiegesha kwa Deborah usiku huo. Walishazoea kujipatia wasichana wa mahonyo wanaozagaazagaa stendi hapo. Kwao suala la magonjwa ya zinaa kama UKIMWI, sijui Kaswende, Kisonono na mengineyo ilikuwa ni hadithi za alinacha zisizo na mashiko. Walichokuwa wanajali wao ni kuitimizia nafsi hawaa zake inazohitaji. Wakaanza kumsarandia waondoke nae wakafanye yao, kila mmoja anamwaga sera zake na kutupa ndoano yake yenye chambo kwa shauku na mshawasha mkubwa wa kumuingiza mtegoni Deborah.

"Sistery....mambo vipi kama hauna mwenyeji, utaondoka na mimi uskonde, tuliza wahaka na jakamoyo...!" alichombweza mmoja wa vijana hao huku akijichekesha chekesha. "Jimmy..achana nae huyu dada ni wa kwetu kabisa toka Mji kasoro bahari lafudhi zake tu unaziskia kabisa. Naondoka nae mimi huyu, huu mkwaju wa maana haswa, toka Milima Uluguru..." aliongea mhuni mwingine kwa swaga za lafudhi za vijana wa Mjini akibishana na hasimu mwenzie.

Deborah hakujishughulisha nao, anawapiga kijicho pembe akawa amebaki amejikunyata, Amejivika ujasiri wa Simba wakati moyoni alikuwa na uoga wa kunguru huku akisali na kuomba kila aina ya dua wasije kumfanyia vitendo vya kifedhuli. Tayari usiku mbichi ulikuwa umeshaingia, kiza kilisha shamiri mawinguni huku nyota angani zikijitutumua kutoa nuru yake walau kufifisha makali ya giza kadri zinavyoweza. Wale wajuba wa stendi baada ya kumuona Deborah sio anuwai ya wasichana wanaojiokotea, wakaamua kutokomea zao vichwa chini kama kuku mwenye mdondo. Walikwenda kujaribu mawindo mengine, hiyo ndio ikawa salama na pona ya Deborah.

Usiku huo akala tena 'chips dume' za muhogo, na kusukumizia na maji ya kidebe, akarudi tena kwenye majlisi yake. Alikuwa ameshachanganyikiwa hajui hata cha kufanya. Taswira ya Jiji la Dar es Salaam kwa namna alivyokuwa anaisikia kwenye redio na kuisoma kwenye vitabu shuleni, na uhalisia wake ilikuwa ni mbingu na ardhi. Fikra zake zikimtuma kuwa amekuja kwenye Jiji la asali na maziwa kumbe yupo kwenye Jiji la shubiri mwitu. Jiji ambalo ni sehemu ya hatari kwa ustawi wa mwanadamu kuishi. Kadri muda ulivyokuwa unasonga ndio wavulana wadogo wadogo, machokoraa wanaolala kwenye stendi za Mabasi wakavamia banda la abiria. Wengine wakawa wanazidi kumjongelea Deborah, ili mradi tafrani mtindo mmoja.

Wakiwa baadhi yai wanatokwa na udenda wa fisi wa kufuata mkono wa binadamu udondoke ale. Walianza kumjongelea na kumuuliza maswali yasiyo na kichwa wala miguu, mpaka Deborah akaona kabisa dalili zote za kubakwa zipo waziwazi akijilegeza. Akapanga achomoke pale alipo, akajibanze kwenye kibanda chenye ulinzi wa mgambo. Alishakata shauri kuwa kesho jua likichomoza tu anakata tiketi ya kurejea nyumbani kwao Morogoro. Alishapanga atamuomba msamaha Mjomba pindi watakapoonana ana kwa ana. Mawazo yaliwaza kuwa siku akirejea, shangazi yake atamdunda kama paka mwizi. Kwanza alifahamu kuwa kijiji kizima kitakuwa kimeshapata taarifa zake za wizi wa shingo za kuku na sahani yake. Machozi yalianza kumlengalenga Deborah, akijiona kabisa yeye ni fungu la kukosa, na daima wambili havai moja.


Ghafla bin vuu....Deborah akiwa hana hili wala lile akashtukia Difenda la polisi limetua pale Stendi ya Kisutu likiwa na askari wapo kwenye kamatakamata ya wazembe na wazururaji. Wale vijana wahuni walipoiona tu ile gari kila mmoja wao mguu begani, kuhofia kutiwa mbaroni. Wale waliozubaa wote wakakamatwa akiwemo na Deborah. Msemo wa kuku mgeni hakosi kamba mguuni ukatimu kwa Deborah. "Wewe unafanya nini hapa sasa hivi usiku huu msichana mdogo kama wewe..!" alibandikwa swali Deborah na mmoja wa maafande wale, yakifuatiwa na mkururu wa maswali ya kipolisi kutoka kwa maaskari wengine.

Deborah akabakia kujing'ata ulimi tu, hawezi kabisa kujitetea, akiwa pia haamini kama amedakwa na wana usalama. Baada ya kushindwa kujieleza kwa ufasaha nae akasombwa na polisi wale kwenye msako huo wa usiku kwa kutupiwa kwenye Difenda. Kisha moja kwa moja akaenda kutupwa selo ya kituo cha polisi Msimbazi, kusubiria kuwekwa kitimoto cha maswali ya ziada. Deborah alikuwa anamwaga mchozi mithili ya ngamia anayetaka kuchinjwa akiwa katika majuto makubwa juu ya maamuzi yake ya hasira ya kutoroka nyumbani namna yalivyomponza. Kwa akili zake za utoto alijua kukamatwa na polisi ndio tiketi ya kufungwa jela.

Walipofikishwa kituoni, wakatenganishwa, wanawake kwao na wanaume kivyao. Baada ya hapo wakaanza kuhojiwa kila mmoja kivyake vyake sababu ya kukamatiwa huko mitaani. Ilipofika zamu ya Deborah, akaingizwa kwenye chumba cha askari mwanamke. Huko ikabidi autapike ukweli wake wote anaoujua kuhusu yeye mbele ya Koplo Marieta. Alimueleza kinagaubaga bila kuficha kitu mpaka sababu iliyomfanya akimbie nyumbani kwa Mjomba Kobelo kukwepa mateso ya shangazi yake. Koplo Marieta, kama binadamu mwenye moyo wenye nyama, imani ikamuingia akashikwa na uchungu mkubwa kutokana na mateso aliyoyapitia Deborah katika umri mdogo.

Hivyo akafunga nae ahadi ya kumchukua, ataishi nae nyumbani kwake kisha utakapofika muda wa kuripoti shule atampa pesa ya ada aende akasome. Deborah akawa amechomokea kwenye tundu la sindano chupuchupu yamkute mambo. Toka hapo Deborah akahamia rasmi nyumbani kwa Koplo Marieta kwenye kota za polisi hapo hapo Msimbazi maghorofani. Shida, tabu na mateso yote aliyopitia akayazika kwenye kaburi la sahau, kutokana na jinsi Koplo Marieta alivyokuwa anamjali. Akapumzishwa kazi za kipagazi na sulubu alizokuwa anafanyishwa na shangazi yake kule kijijini. Kazi yake mpya katika siku za fadhili wakati anasubiria muda wa shule kufunguliwa ikawa asubuhi na mapema kabisa anadamka kwenda Kisutu kwenye Kioski cha biashara kinachomilikiwa na mfadhili wake Koplo Marieta kusaidia kuuza biashara hiyo.

Deborah alikuwa anakaa hapo kibandani mpaka saa 1 mpaka 2 usiku ndio anarejea nyumbani kwa miguu tu. Kutoka Kisutu mpaka Msimbazi alikuwa anatumia takribani nusu saa, na kwa namna Deborah alivyokulia Kijijini umbali huo ulikuwa ni mfupi sana kwake. Siku za kupelekwa shule zilikuwa inakaribia, huku ada yake akiwa ameshakabidhiwa bado kununuliwa mahitaji madogo madogo ya kujikimu. Kwa jinsi Deborah alivyokuwa makini na pesa yake ya ada alikuwa anatembea nayo kila anapokwenda, akilala na kuamka nayo akiwa ameihifadhi katika nguo yake ya ndani. Akiwa Deborah amejistarehe nafsini mwake akijua muda sio mrefu ndoto yake ya mafanikio kielimu itaanza kutimia, akakumbwa na tukio baya sana maishani mwake.
Matanga ya rohoni ambayo alishaanza kuyasahau yakaibuka upya tena katika wakati usio muafaka, ikiwa ni siku tatu kabla ya shule kufunguliwa.

Deborah akatekwa na mtu asiyejulikana. Mtu huyo, aliyemteka alikuwa ni mrefu wa umbo, ana kifua kipana, akiwa anapenda kuvaa miwani nyeusi machoni mwake na kofia ya pama kichwani mwake. Hiyo yote ilikuwa ni mbinu kabambe ya kuficha wajihi wake usijulikane kisawasawa. Alijizoesha karibia wiki nzima kwenda kwenye kioski kunywa soda baridi kwa sambusa kila inapofika muda wa saa 1 usiku. Alikuwa ni mcheshi haswa atamtania Deborah na muuzaji mwenzake, akiwa ni mtu hadhiri haswa. Siku ingine atajitia kuwapa ofa ya soda na wao wanawe, wakamzoea akawazoea, kumbe ana lake jambo.

"Naona ndio muda wako wa kuondoka huu, nisubirie nimalize soda yangu tuondoke wote na mimi naelekea huko huko unakokwenda wewe..!" alizungumza yule jamaa baada ya kumuona Deborah anaagana na mwenzake ambaye yeye alikuwa anaishi Mbagala. "Mhhhh....kwani mie unajua ninakwenda wapi?" Deborah akauliza swali la kidadisi akiwa amepigwa na bumbuwazi baada kushtushwa na maelezo ya yule mtu kuwa anapajua anapoishi hivyo kupatwa na mshawaha nafsini mwake wa kutaka kumdadisi. "Rafiki yangu mwema na mzuri kama wewe nishindwe kujua unapoishi? Yatakuwa maskhara hayo, wewe unaishi Msimbazi kwenye kota za manjagu, nyumbani kwa Koplo Marieta...!" aliongea kwa kujiamini mtu yule huku akikita chupa yake ya Pepsi juu ya meza kuashiria amemaliza soda yake aliyokuwa ameinywa kwa mtindo wa tarumbeta.

Deborah akawa kama mtu aliyeshikwa na kihoro, akijiuliza maswali lukuki nafsini mwake akishangazwa na mgeni huyu kumjua mpaka anapoishi. Wakawa wanatoka wote kwa pamoja nje ya Kioski, mguu kwa mguu Deborah akiwa mbele. "Lakini mimi sina haja ya lifti nikikatisha hapo katikati natokea soko la Kariakoo tayari nipo nyumbani nimefika hivyo ahsante kwa wema wako, labda siku ingine" ghafla aligeuka nyuma Deborah na kuanza kujieleza kwa kujiamini huku akiwa amemtumbulia macho bila uoga. Deborah aliyakumbuka maneno ya wosia ya mfadhili wake Koplo Marieta ya kuwa, Jiji la Dar es Salaam watu wenye utu ni wachache sana wengi ni mbwa kasoro mkia waliovaa sura za kibinadamu, kutokana na tabia.

Hivyo hakuwa tayari kuambatana na mtu asiyemfahamu kwa kinagaubaga. Walikuwa tayari wawili hao wameshalifikia gari la yule jamaa aina ya 'Toyota Hilux Double Cabin' yenye vioo vya giza aliyokuwa ameiegesha meta chache pembeni ya kioski. "Haya nimekuelewa, hamna noma siku ingine nitakupa lifti utakapopenda wewe, chukua basi hii zawadi yako, uchangamshe kinywa......!" alijibu yule jamaa huku akitoa pipi mbili mfukoni, moja akinyoosha mkono kumpa Deborah na ingine akaifungua haraka haraka na kuitumbukiza kinywaji akianza kuimung'unya mbele ya Deborah. "Ahsante sana,ubarikiwe..!" alijibu Deborah huku akiipokea na kuanza kuimung'unya pipi ile mbele ya yule mgeni. Aliona bora amridhishe mgeni huyo asije kumuona ana madahiro kwa wateja.

Uso wa yule jamaa mwanzoni alipokataliwa lifti uliliwa debe, lakini Deborah alipoanza tu kuimung'unya pipi ile, akaunda tabasamu la ushindi lenye kufu ya furaha. Deborah ghafla akakimbilia tena kwenye Kioski kama mtu aliyegutushwa na kitu cha kuogofya. Mwenzake wa kioski alikuwa nae anajiandaa kufunga anaingiza viti ndani ya kibanda, tayari kwa kurejea sehemu anayoishi. Deborah alipomfikia yule mwenzake akawa anamuongelesha mambo mawili matatu, kama maagizo na maelekezo fulani aliyokuwa amesahau kumpa mwenzake wakati wakaagana. Yule mtu alikuwa ameegemea mlango wa mbele ya siti ya abiria kama vile bado anamsubiria Deborah.

Alikuwa anapiga miluzi huku kidole cha shahada cha mkono wa kulia kinauzungusha ufunguo kwa mbwembwe zote. Deborah akaanza kuja mpaka usawa wa ile gari, akawa ananyanyua mikono kama vile anaomba msaada fulani, huku kipochi chake cha mkononi anataka akitupe. Akaanza kuyumba kama mtu mwenye kisunzu au mlevi aliyezidiwa na pombe. "Naomba msaada wako najiskia vibaya sana, macho yanaishiwa nguvu, nifikishshshsh......!" Deborah alizungumza kwa shida kabla hata hajamaliza maelezo yake akataka aanguke chini.

Jamaa akamdaka hewani kabla hajakita sakafuni na hima hima akamfungulia siti ya mbele na kumbeba akamuweka vizuri na kufunga mlango. Akakimbilia kufungua mlango wake wa dereva na kuwasha gari. Akang'oa nanga kwa mwendo wa kasi, kila mtu aliyeshuhudia tukio lile akabaki amepigwa na butwaa asijue kilichotokea. Kilikuwa ni kitendo cha utekaji kilichotekelezwa ndani ya muda wa kufumba na kufumbua, ikionyesha tukio limefanywa na mtu mzoefu wa kazi hizo.

Deborah akawa ameshatekwa na mtu asiyejulikana na kupelekwa sehemu isiyojulikana kwa madhumuni yasiyojulikana. Sasa mambo yakawa mchafukoge kwa upande wa Deborah, hakuna mtu yoyote aliyeshuhudia tukio akawa na uthubutu wa kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi au kumpasha habari mtumishi mwenza wa Deborah pale kwenye kioski.

Kila mtu aliyeshuhudia tukio alikuwa anaogopa kukamatwa ili kuisaidia polisi kwa kosa lisilo lake. Kama ilivyo tabia za wakati wa Jiji la Dar es Salaam, kila mtu akashika hamsini zake kama vile hamna tukio lililotokea. Giza jeusi likatanda tena katika maisha ya Deborah, matanga ya moyoni mwake yanapiga hodi kila uchao kwa upande wao.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
SURA YA KUMI NA MOJA
"Mwana Side-Boy..... sio mwenzetu tena, kaula mbaya huko South anasukuma E- class Mercedes Benz, aah....hiki kijiwe noma sana" aliongea mmoja wa wanachama wa majlisi ya wahuni wanabadilishana mawazo. "Kweli hata mie nimeletewa hizo habari na Timammy yupo Mtoto wa Mzee Fakii wa Vijibweni, ananiambia mara ya mwisho walivyoonana nae alifikia hatua hadi kumiliki kadi nyeusi ya benki 'FNB Bank'. Hiyo kadi nasikia inamaanisha mtu ana zaidi ya Rand milioni 1 kwenye akaunti yake benki" aliongea kwa uchungu kijana mwingine huku anapuliza hewani moshi wa sigara bwege maarufu kwa jina la bangi.

"Bangi, nipe mabawa unipeperushe hewani mpaka South kwa Mjomba Madiba kama ndege, nikale bata mie..." alizidi kuyasasambua maneno kijana yule kwa hisia kali huku anajinuwizia kwa kutumia moshi wa bangi anaojifukiza nao kichwani. "Kwa hiyo hapa mpango mzima ni kuona namna gani na sisi tumainika, tusibakie kuwa washangiliaji tu wa mafanikio ya wenzetu" Mbweku alichangia mawazo huku nae akigongea kwa ishara ya kidole kuwa apitishiwe sigara bwege asuuze akili yake.

"Hamna kulala dogo Mbweku hapa ni amsha amsha na kesha mpaka che tupo Bondeni kwa Mjomba Madiba, ndio maana nimekuunganisha kwenye ule mchongo wa kazi ya Ubaunsa pale 'Martino Royal Hotel' sasa ukambwelembwele wewe mwenyewe. Pale ukifika "How are you" nyingiii na "Yes Yes Mzungu Kala Mafenesi" za kutosha kwa Watasha na kuwachangamkia, Zali la Mentali likikudondokea haina shanapa wala kwepesha unasanda tu, tutajuana mbele kwa mbele" alijibiwa Mbweku na mmoja wa mtu ambaye aliyeonekana kama ndio kiongozi wa kijiwe chao.

Walikuwa wanajikusanya kijiwe wanapeana michapo ya nchi za ughaibuni yenye sura ya hadaa kwa rangi na hali. Hayo ndio maisha yalikuwa maisha mapya ya kijana Mbweku akiwa Kigamboni. Maisha ya kulala kwenye Meli mbovu, maboti na mitumbwi. Maisha ya kula kwa donesheni ya kupiga ugali wa shirika kwa samaki wa kupora kwa wavuvi. Maisha ya kuvizia usiku abiria wanaoshuka kwenye Pantoni na kuwapora ndio ikawa kazi yao. Vijana hao walikuwa hawajali wala hawabali juu ya mustakabali wao wa maisha ya baadae. Mambo yote haramu mutlaki kama ulevi, unyang'anyi, uzinzi, kupigana na mengineyo yalikuwa ndio matendo yao ya kawaida.

Simulizi zile za kuzamia nchi za ughaibuni "Stowaway" zilikuwa zinamsisimua vilivyo Mbweku, hivyo akaazimia lazima azamie Bondeni na kama fursa ikiruhusu Ulaya kabisa. Miaka hiyo kiu ya vijana kutaka kuikimbia nchi yao ya Tanzania ilikuwa kubwa sana. Wapo waliokuwa wanataka kwenda Ughaibuni kwa malengo ya kutabahari katika fani mbalimbali za elimu katika Vyuo Vikuu bora duniani, wengine kufanya kazi au kutembea. Wengi wao katika vijana hao kilichokuwa kinawasukuma kwenda nje ni mseto wa uchumi mbaya, umaskini na kutaka tu kufahamu mambo. Hali hiyo yote ilichagizwa na ukosefu wa ajira kutokana na serikali kuacha kuajiri kutokana na uchumi mbovu wa nchi.


Sasa rasmi kijana Mbweku, baada ya kuhangaika huku na kule akajikuta amepata bahati ya kibarua rasmi cha ulinzi na kufanya usafi kwenye mazingira ya Hoteli ya 'Martino Royal Hotel'. Akawa amejitapua kwenye kundi la vijana hawana kazi hawana bazi, kazi yao kukaa vibarazani kupiga ubwete tu. Hoteli ambayo waasisi wake Mr.Martin Tenga na Recho ndio waliosababisha baba yake mzazi kijana Mbweku afungwe jela kutokana na pesa walizokwapua nyumbani kwa marehemu Bosi Minja. Hawa Mabosi wake ndio waliosababisha Mbweku na familia yake kwa ujumla waishi maisha yasiyo na mbele wala nyuma.

Kwa tabia za MbwekuJr za kutopenda kudhulumiwa haki zake, kama angetambua kuwa Bosi wake Recho, mmiliki wa hiyo Hoteli ndio chanzo cha yeye kuishi maisha magumu yaliyochangia aachane na shule na kuwa chokoraa mtaani, pangechimbika vilivyo. Sala na matumaini ya MbwekuJr ilikuwa ni siku moja afanikiwe kimaisha ili akawachukue kutoka kijijini mama yake na wadogo zake ili waishi pamoja kama zamani.


Mkasa wake wa mauaji ya Kibopa Mwinyi Fuad uliishia hewani, hata Mbweku mwenyewe hakuamini namna lilivyopotezewa. Alikuwa kila siku asubuhi anadamkia kwenye meza za wauza magazeti kufanya taftishi ya taarifa ya mauaji ya Mwinyi Fuad. Lakini akashangazwa taarifa hiyo haikupewa kipaumbele na vyombo hivyo vya habari. Ndugu wa Mwinyi Fuad walitaka kusitiri aibu ya ndugu yao, ya kukutwa amefariki uchi wa mnyama ufukweni mwa bahari tena usiku. Maana Jiji zima walikuwa wanatambua tabia zake chafu katika jamii.

Wakatembeza chai kwa baadhi ya waandishi wa habari wasio waaminifu ili kuhakikisha hakuna redio wala gazeti lolote litakalotoa taarifa ya msiba huo hadharani. Maiti yake siku ya pili yake tu, ikaenda kuzikwa kwao Pangani, Tanga. Huo ndio ukawa mwisho mbaya wa baradhuli Mwinyi Fuad, katika safari yake ya kurejea jongomeo kwa Mola wake. Kufichwa kwa siri hiyo ya kifo hicho na familia ikawa ni nafuu kwa jeshi la polisi kutokana na ugumu wa kumpata muuaji uliopo.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Shukran mkuu.
Tuendelee tafadhali kiongozi.
 
SEHEMU-32


️[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Msichana mrembo mweusi mng'avu wa rangi, mrefu mwenye umbo la penseli. Uzuri wake wa sura ni wa shani, alikuwa yupo katika kilele cha milki ya usingizi akiwa ndani ya kasri ya kifahari ya aushi iliyopigwa umaridadi na mafundi waashi bobezi katika fani ya ujenzi. Pandikizi hilo la jumba ambalo kwa mtazamo wake, kila mtu atakayeiona lazima atatamani aishi ndani yake walau kwa saa chache. Alilazwa juu ya samadari ya thamani a'ali. Kiyoyozi kilikuwa kinafanya kazi yake ya kuleta ubaridi ndani ya chumba kile chenye wasaa wa kutosha alicholala kisura huyo mbichi. Juu ya dari kulifungwa bodi zilizopakwa rangi nyeupe huku taa mbili zilizozungushiwa marembo marembo ya kung'ara yaliyotengenezwa na madini ya 'Zabarjad' zikiwa zinawaka. Chini ya sakafu kulitandikwa zulia nene lenye rangi nyekundu mithili ya uwaridi. Ukutani kulikuwa na makabati mawili yaliyofungwa kwa funguo zenye kuning'inizwa. Bila kusahau ala za muziki laini zilizopangiliwa mipigo yake ilikuwa inasikia kwa mbali ndani ya chumba kile.

Kwa jinsi alivyokuwa kwenye usingizi mzito, kwa mtazamo tu hakuwa ni mtu wa kuamka muda mfupi ujao. Ghafla bin vuu mlango wa chumba chake yule msichana ukafunguliwa, akaingia daktari mmoja mrefu wa umbo, amevalia miwani yake, kidevuni amenyoa nywele zake mtindo wa duara huku akiziachia nywele za kionjamchuzi zikiungana na zile za kidevuni. Kwapani alikuwa amefumbata mkoba wake wa rangi nyeusi. Alikuwa amefuatana na mzungu mmoja unyounyo bila kuachiana nafasi kubwa baina yao. Yule daktari akaenda mubashara mpaka pale kitandani akampima mapigo ya moyo na joto la mwili la yule msichana kisha akaandika maelezo mafupi kwenye kidaftari chake kidogo chenye gamba gumu la rangi ya kahawia. Baada ya hapo akamtoa damu kubwa ya mkononi kwa kutumia bomba la sindano akahifadhi damu ile kwenye kichupa maalumu. Kisha akamlegeza nguo yake ya ndani aliyovaa msichana yule, akamtanua miguu yake kidogo kisha akamfanyia vipimo kwenye sehemu zake za siri. Muda wote yule mzungu alikuwa anamuangalia yule msichana kwa jicho la uchu wa huba.

"My God..Black beauty Black beauty....!" aliropoka yule mzungu akishindwa kujizuia hisia zake kwa msichana yule aliyezama katika usingizi wa pono akionekana ana furaha ya kupindukia akiwa ameshikwa na raghba ya kumzimikia kimapenzi. Yule daktari akabaki anatabasamu na kufunga kidaftari chake baada ya kumalizia maelezo yake ya mwisho na kumfuata yule mzungu. Daktari yule akamnong'oneza kitu Mzungu yule kwenye sikio la kushoto kisha wakatoka nje ya chumba kile. Yule mzungu alipotoka nje ya vyumba vile akaingia kwenye gari yake kisha warembo waliojiweka pembeni yake wakilizingira gari lile hawataki kumpa nafasi ya kutoka. Akashusha kioo chini na kuchomoa burungutu la pesa za kigeni kisha akamwaga hewani, akawapiga ukope na kutabasamu. Warembo wale wakawa sasa wanagombaniana ngwenje zile. Ndipo yule mzungu akapiga honi ili afunguliwe geti la kutoka nje ya Kasino hilo la vigogo.

Mlinzi wa Kasino hilo la roshani hima hima akafungua geti kuruhusu gari hilo litoke. Yule daktari nae baada ya muda akaagana na mlinzi yule akaondoka zake kwa kutumia usafiri wake binafsi aliokuja nao usiku huo. Warembo wale walikuwa kama wapo kambini ndani ya kasri lile linalotumika kama danguro. Mapaja yao warembo yalianikwa waziwazi huku chuchu zao zikicheza kifuani pale walipokuwa wakipiga hatua wakitembea kwa madahiro pindi wanapomlaki mteja.

Makalio yao ndio usiseme kwani hizo gauni laini walizovaa ziliwachora vyema hasa kutokana na kuwabana vilivyo. Wengine walikuwa chini wamevalia vichupi vya kuogelea na juu wana viblauzi vyepesi. Visura hao walikuwa wanatamanisha kweli hasa kwa mtu mkware, angeweza hata kufanya maamuzi ya kufuja urathi kwa kuhonga nyumba aliyoachiwa wa wazazi.

Danguro hili la siri la kifahari lililopo eneo la Sinza Kijiweni lilikuwa linamilikiwa na Recho. Vigogo pekee ndio walikuwa wanaweza kumudu gharama zake, mtu fukara fuke hata ajichange kipato chake cha mwaka mzima asingeweza kumudu gharama zake. Mpenzi mpya wa Recho, mzungu Mr.Lorenzo alikuwa hajui kitu juu ya uwepo wa danguro hilo la siri. Alichofanya Recho ni kwenda kuweka poni benki hati ya Hoteli ya Martino Royal Hotel waliyokuwa wanaimiliki kwa pamoja kati yake na mwandani wake Mr.Lorenzo. Kisha akachukua mkopo mkubwa wa mamilioni ya shilingi na kuja kununua nyumba ya roshani maeneo ya Sinza kisha akaifanyia ukarabati wa ngumu kuiongezea hadhi na thamani. Kupitia biashara hiyo ya danguro Recho akajikuta anajiingizia pesa kochokocho ambazo hazitozwi kodi hata chembe tofauti na biashara ya Hoteli ambayo macho ya serikali yote yalikuwa hapo ili kupata pesa za kuendesha nchi.

Sera ya serikali ya awamu ya tatu, chini ya Rais 'Benjamin William Mkapa' ilikuwa na mikakati madhubuti ya kukusanya vizuri maduhuli ya ndani yanayotokana na kodi ili nchi ipunguze utegemezi wa wafadhili toka nchi za ng'ambo. Wafadhili ambao daima misaada yao ilikuwa inaambatana na masharti magumu yenye kuvunja maadili ya utu na uhuru. Recho akausoma mchezo mapema akaamua awekeze nguvu kwenye biashara haramu ya danguro. Nia na malengo yake yalikuwa sio kurejesha mkopo benki. Alitaka benki waipige bei Martino Royal Hotel ili awe amejivua ushirika na Mr.Lorenzo. Kilichomsukuma Recho afanye yote hayo, ni kutokana na kugundua kuwa Mr.Lorenzo anamficha vitu vingi sana, hasa kutokana na tukio la kuzifuma hati za kusafiria za Mr Lorenzo zenye majina tofautitofauti ya bandia. Pia alikuwa anaweza kupotea Tanzania kwa zaidi ya miezi 3 asijulikane alipokwenda akiwa kwenye mishemishe zake za kurekodi filamu. HIvyo usiri wa Mr.Lorenzo ukamfanya Recho achukue tahadhari kabla ya hatari kwa kuamua kumzunguka mwekezaji mwenza wake. Alimuona Mr.Lorenzo ni kama nyoka mwenye mwendo wa mzizimo, anayejificha uhalisia wake.

Akajigeuza panya kuuma huku akipuliza kwa mpenzi wake Mr.Lorenzo. Kumbe mwenzake Mr.Lorenzo hakuwa bunga, ni mtoto wa mjini, kazaliwa Jijini Turin kakulia Turin maujanja yote anayajua. Tabia za Mr.Lorenzo zilikuwa kama samaki kitatange, mjanja kupitiliza ingawa kimuonekano anaonekana ni fala, bwege mtozeni. Alikuwa ana watu wake mawakala sehemu nyeti kama benki, uhamiaji na kwingineko ambao wanamuunga taarifa mbalimbali za harakati zake. Wakamnyetisha mkanda mzima namna Recho alivyoweka bondi benki hati ya Hoteli. Hivyo akajipanga akitua tu Bongo, atampiga tukio la hatari Recho litakalomfanya ajute kuzaliwa. Tukio ambalo alifahamu kwa vyovyote vyombo vya dola vitamuwinda vimtie mbaroni jambo ambalo Mr.Lorenzo hakutaka litokee hivyo alijiandaa kugura kikafiri kurejea kwao nchini Italia.


Recho kwa upande wake, wasichana wa danguro lake wengi wao alikuwa anawapata kwa njia za utekaji. Alikuwa ana vijana wake wa kazi, genge la wahuni wanaozunguka mitaani kusaka vipaji. Hivyo likaanza kuibuka wimbi la matukio ya wasichana kupotea mitaani bila kufahamu kuwa wanaenda kugeuzwa kuwa watumwa wa ngono kwenye danguro la Recho. Walikuwa wanapofikishwa hapo kwenye danguro, wanapimwa afya zao na daktari kisha wanaanza kuzoeshwa matumizi ya pombe na madawa ya kulevya. Pia wanalipwa pesa sufufu zinazowashawishi waendee kubakia kwenye ulingo huo wa uchangudoa ili waweze kumudu kuishi maisha ya anasa.

Yule msichana mrembo aliyekuwa amelazwa kitandani alikuwa ni Deborah. Akiwa ndio kwanza ametekwa mtaani na kuletwa ndani ya danguro hilo. Danguro ambalo kutoroka kwake ingekuwa ni ndoto ya mchana, au ni lenye kustaajabisha mfano wa mbwa kuvaa nguo. Alikuwa amefungiwa katika chumba kilichopo roshani ya tano. Mpaka kuifikia roshani ya tano ulikuwa unakutana kwenye kila korido na mlinzi mmoja mwenye silaha. Walinzi hao namba wani walikuwa na maumbo ya miraba minne na sio vimbaumbau kama mwiko wa pilau. Walishapewa maagizo ya wazi kuwa wasiruhusu mwanamke yoyote au mgeni yoyote kuingia bila kibali kutoka kwa mmiliki Recho.

Uzuri wa mambo vibali hivyo alikuwa anatembea navyo Recho kwenye gari yake, hivyo kuzidi kutengeneza ugumu wa mtu yoyote kutoroka au kuingia humo. Hivyo Deborah alikuwa ana wiki moja tu ya kuachwa arudie kwenye hali ya kawaida baada ya hapo, ndio angeanzwa kuharibiwa kisaikolojia kwa mihadarati na kuwa teja rasmi na mtumishi wa danguro hilo. Bila muujiza wa Mungu wake, asingeweza kamwe kufua dafu kama akiamua kutoroka kwenye jumba lile. Deborah kama angejaribu kutaka kutoroka angefilia mbali kutokana na kipigo angechopokea toka kwa walinzi hao.

[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
"Mwana harashi mkubwa huyu binti ameshafilisi Kioski changu, wema wangu umeniponza kumbe mkora wa kutupwa, msakeni popote alipo, mkimkamata ama zake ama zangu pumbavu zake sana....!" alikuwa anafoka Koplo Marieta mbele ya askari wenzake huku mishipa ya shingo imemsimama, mapovu meupe ya hasira yanamtoka pembezoni mwa kinywa chake, wakati anaripoti kituoni kwa polisi wenzake juu ya tukio la kutoroka kwa Deborah.

Koplo Marieta alikuwa anatetemeka kwa hasira utasema amevumbikwa na homa. "Lakini haonekani kama ni mwana hizaya, anaonekana ni Binti anayejitambua labda kapatwa na jambo baya tusimhukumu kwanza, muda ni mwalimu mzuri....!" alitetewa Deborah na polisi mmoja wa kike jirani yake Koplo Marieta ambaye alikuwa anamfuatialia kwa makini nyendo za Deborah akiwa nyumbani. "Watu wahalifu makini daima ni wapole, wanaficha madhambi yao kwenye upole wao...!" alitia shadda msimamo wake Koplo Marieta akionekana hataki kusikia la muadhini wala la mchota maji msikitini, yeye alisha hesabu kuwa Deborah kamuingiza mjini."Afande nilikutahadharisha mapema siku ile juu ya uamuzi wako wa kumkaribisha nyumbani huyo Binti hukunisikiliza, nilikuambia kinagaubaga kuwa hawa watoto machokoraa ni kama kunguru hawafugiki, wameshazoea maisha ya kubakwa, kulawitiwa, na uporaji huko mitaani, daima mbwa ni mbwa tu hawezi kugeuka mbuzi" Afande mwingine wa kiume nae akiwa amevimba kama mvua ya masika aliongezea chumvi kwenye kidonda cha maumivu ya moyoni cha Koplo Marieta.

Koplo Marieta ilibidi aelezee tukio zima lililotokea, ya kuwa Deborah hajarudi nyumbani jana usiku mpaka ilipofika che hajafika maskamoni. Akaelezea pia kuwa amedamka asubuhi na mapema kwenda Kisutu kwenye Kioski, muuzaji mwenzake Deborah hafahamu kitu chochote kama hajafika nyumbani kwa maana waliagana salama salimini jana yake, huku wakiahidiana kukutana mapema iwezekanavyo asubuhi yake. Baada ya majadiliano ya kina, askari wale wakaafikiana kwa kauli moja, wavunje kikao kile kisha waingie mitaani wamsake Deborah popote alipo kisha akamatwe aje kujibu tuhuma zake za wizi wa kuaminika. Deborah alihesabiwa ametoroka na ngwenje za kutosha, za kulipia ada shuleni na zingine za mauzo ya siku ya kwenye Kioski. Msako ulikuwa unafanyika kwa haraka na umakini mkubwa ili kujaribu kuokoa baadhi ya pesa alizotoroka nazo kabla hajazifuja. Askari wale kwanza walimbinya vilivyo kibarua wa pale kwenye Kioski cha Koplo Marieta, viboko vikimwandama mwilini masikini Binti wa watu, wakiweka dhana huenda ni mchezo walioshirikiana na Deborah. Lakini hawakuambulia kitu baada ya kuonyesha hafahamu chochote katika njama hizo za Deborah. Walipowahoji baadhi ya vijana wa pale Stendi wapo waliotoa shuhuda kuwa walimuona anapanda gari usiku huo lililoegeshwa jirani na Kioski. Maelezo hayo yakazidi kuongeza chachu kuwa tayari Deborah alishaanza kushiriki mambo ya mapenzi mpaka anafuatwa na wenye magari usiku.

Siku zikaanza kuyoyoma, bila kuleta matokeo chanya ya kukamatwa kwa Deborah. Koplo Marieta alijaribu kupekua kwenye begi lake la nguo alilolitelekeza kwa matumaini huenda akambulia picha za Deborah na nyaraka zingine zinazoweza kusaidia taftishi ya kukamatwa kwake, lakini hakuambulia kitu. Deborah maisha yake alikuwa anayaendesha kama mwanajeshi, kila kitu chake muhimu kilikuwa kwenye pochi yake ya mkononi. Ilipofika siku ya 5 tokea atoweke, Koplo Marieta akabwaga manyanga, akakubali matokeo na kuamua kumshukuru Mungu kwa yote yaliyotokea. Lakini kama ujuavyo kanuni asilia inasema dhambi daima haisahauliki na wema hauozi. Uwe mwema kadri utakavyokuwa mwema kwa watu, lakini bado watu watakumbushia dhambi zako za nyuma ulizowahi kuwatendea. Hivyo mazuri yote aliyowahi kuyatenda Deborah kwa muda mfupi alioishi na Koplo Marieta akawa ameyachafua, mema yote Koplo Marieta akayaweka kwenye kaburi la sahau.

Ama kweli usilolijua ni kama usiku wa giza nene, na daima ukipatwa na jambo au kuletewa habari usiyo na uhakika nayo, iweke deke kwanza usikimbilie kuhukumu utakuja kujutia maamuzi yako pindi ukweli ukidhihiri. Polisi wale walichokuwa hawakifahamu ni kuwa Deborah alikuwa yupo mateka ndani ya pandikizi la jumba akiwa haifahamu hatima ya usalama wake. Alikuwa yupo katika msongo mkubwa wa mawazo akiwa halifahamu lengo la watekaji wale kwake.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Mbweku Jr alikuwa ndio anatoka kazini asubuhi yake, akiwa ameshushwa na daladala katika kituo cha Manzese Argentina na mkururu wa mawazo kichwani. Mbweku Je alikuwa amehamishiwa kikazi eneo la Sinza Kijiweni kuwa ni mlinzi wa getini kwenye danguro linalomilikiwa na Bosi wake Recho. Alihamishwa kutoka 'Martino Royal Hotel', Kigamboni na kuletwa huku mjini, hivyo ikambidi apangishe chumba maeneo ya Manzese ili kumuwepesishia kufika kazini kwa haraka, tofauti na kama angeendelea kuishi Kigamboni. Mipaka yake ya kazi ilikuwa ni kuishia getini tu, huko ndani ya nyumba kulikuwa na walinzi wengine mahususi kwa kazi za ndani ya jengo.


Usiku wa kuamkia asubuhi aliyokuwa anatoka kazini, kulitokea jambo zito kwa upande wake jambo ambalo ndilo lilikuwa linampa mawazo lukuki kichwani mwake. Jambo ambalo alijiwekea adhima ya kuelekea gereza la Ukonga kwenda kuonana na baba yake mzazi ampasulie ukweli wa mambo asubuhi ile ile. Kutokana na siri aliyoiona, mawazo ya Mbweku Jr yalikuwa yanamtuma huenda baba yake alikuwa na watoto wengine wa nje ya ndoa ambao hawafahamiki na familia yao. Bahati mbaya sana, baba yake mzazi Mbweku Jr alianza kuugua maradhi tofauti tofauti kule gerezani Arusha, hivyo akahamishiwa gereza la Ukonga lililopo Jijini Dar es Salaam ili kumuweka karibu na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya urahisi wa matibabu.

Mbweku Jr alishapewa taarifa hizo za baba yake kuhamishiwa gereza la Dar es Salaam na mmoja wa wajomba zake aliyekutana nae bila kutarajia katika viunga vya maeneo ya Manzese Darajani. Enzi hizo Manzese Darajani kilikuwa ni moja ya kivutio kikubwa kwa wageni wanaokuja Jijini Dar es Salaam wakitokea mikoani. Wananchi hao wa mikoani wengi wao ilikuwa lazima waje Manzese walipande daraja hilo la kisha kupiga nalo picha za kwenda kuonyesha wenzao huko mikoani kuwa wamekanyaga daraja refu la Jjijini Dar es Salaam. Hivyo siku moja Mbweku Jr akiwa kwenye harakati za kuelekea Sinza kibaruani hana hili wala lile ndipo akagongana uso kwa uso na Mjomba wake huyo. Katika kubadilishana mazungumzo baina yao, ndipo akapata taarifa za baba yake mzazi kuletwa gereza la Ukonga. Hivyo akawa anajipanga siku atakayokuwa yupo mapumziko kazini aende kumtembelea amjulie hali na kumueleza maendeleo yake toka alivyowaacha uraiani.

Lakini kwa tukio alilolishuhudia kazini kwake usiku wake aliamua siku hiyo hiyo lazima aende gereza la Ukonga hasa ukichukulia siku hiyo ilikuwa ndio mwisho wa juma, siku ambayo wafungwa wanaruhusiwa kutembelewa na ndugu, jamaa na marafiki zao. Alipofika chumbani kwake, akawasha jiko lake la stovu kisha akabandika sufuria la maji ya chai, haraka haraka akabadilisha sare zake za kazi, akavaa malapa yake na kubeba bakuli lake chakavu la plastiki kwa ajili ya kwenda kununulia mihogo ya kukaanga kwa mama muuza mtaa wa pili kutokea nyumba anayoishi.

Nakuona tu unachomoka wima kama mlingoti, kwani hujui usafi wa choo ni zamu yako, mwanaume mzima lakini ovyoooo kabisa, masharubu kama paka wa baa vile, nakodi yako ikiisha Billahi wa Rasuli utahama nyumba hii siku hiyo hiyo..…!” alikoroma mama mwenye nyumba akimchamba kijana Mbweku Jr kutokana na kuzembea usafi wa msalani. Narudi mama yangu siondoki, nakumbuka vizuri zamu yangu, nisamehe kama ninakukwaza.! Alijibu Mbweku Jr kiunyenyekevu mkubwa huku anachapa lapa zake kutoka kwenye kizingiti cha mlango.

He..Heeeee.Hallow eeeeeh.mama yako nani hapa, mie naweza kuzaa lidume kama wewe, usinizeeshe babu wewe, ukome kuniita mama yako iwe mwanzo na mwisho mwana halulu mkubwa wewe! alizidi kufoka Bibi Mwazani, ajuza ambaye ni mjane alikuwa hapunguzi miaka 65 kwa haraka haraka lakini alikuwa anaupenda ujana balaa. Kila wiki atanunua dera jipya, mara aweke kigodoro usiku kucha nyumbani kwake na vimbwanga vingine kochokocho ambavyo kiuhalisia vilitakiwa vifanywe na wanawake vijana.

Watoto wake walimsema kwa tabia zake mbovu mpaka wakachoka, wakaamua kumsusia nyumba peke yake, aendeleze ufisadi wake nje ya mboni za macho yao. Kawaida yake alikuwa hapendi wapangaji wanawake, au wana ndoa kwenye nyumba yake ya urithi wa mumewe. Alikuwa anapenda barobaro ili ashiriki nao kwa kuwarubuni kimapenzi. Na kwa jinsi vijana wa kileo wanavyopenda mserereko wa kimaisha walikuwa wepesi tu kuzini na Bi. Mwazani ili mradi mambo yao yawaendee vyema. Sasa ugomvi wao mkubwa na mpangaji wake Mbweku mpaka kufikia kutoleana maneno makali ulianzia kwenye mambo ya kunyimana unyumba. Mbweku Jr alikataa kuwa mpenzi wa Bi.Mwazani, licha ya kufanyiwa vibweka na mitego ya kila ya aina ya kimahaba.

Siku za mwanzoni Mbweku Jr kuhamia hapo, Bi. Mwazani alikuwa anadamka alfajiri, siku akijua Mbweku Jr amelala kazini usiku wake. Basi hapo atajipikilisha chapati za mayai na rosti ya maini kisha anamuandalia Mbweku Jr utasema ni mumewe. Mchana wake atamuita Sheikh wa msikiti wa jirani amchinjie jogoo lililofutwa kodi kwa ajili ya pilau ya Mbweku Jr. Kijana wa watu alikuwa anajilia vinono vyake na penzi hatoi kwa Bibi wa watu. Siku waliyogombana kimoja na kuwa mahasimu wasiopikika chungu kimoja, Bi.Mwazani alileta maigizo kuwa kazidiwa na ugonjwa akiwa kibarazani huku akijua wapangaji wake wote wapo vibaruani kasoro Mbweku Jr ndio kabakia nyumbani. Majirani wakapiga kelele baada ya kumuona anazidiwa na kutoa sauti ya kuweweseka kutokana na tashdidi ya ugonjwa. Mbweku Jr ikabidi atimue mbio kutokea ndani akija wangu wangu kumuwahi mama mwenye nyumba wake. "Msinipeleke hospitali, huyu ni jini Khanziri kanipumzisheni kitandani nitapata nafuu baada ya muda msijali" aliongea kwa tabu Bi.Mwazani huku akiwafanyia kiini macho cha kiwango cha lami bila wao kutambua. Ikabidi wakubaliane na matakwa yake, wakambeba mzobemzobe mpaka chumbani kwake wakambwaga kitandani mwake.

Wale watu baki walipotoka chumbani, Bi.Mwazani akajitia kumuagiza maji ya kunywa ya chupa Mbweku Jr. Alipoyaleta maji yale, wakiwa wawili tu chumbani ndipo alipokutana na kituko cha kufungia mwaka. Bi.Mwazani alibakia mtupu uchi wa mnyama, amesaula nguo zake zote amebakiza lundo la shanga kiunoni. Akawa bibi wa watu anamlalamikia Mbweku Jr kwa sauti ya kimahaba ile inayotokea puani kuwa anamtesa sana kwa kumnyima penzi lake, hasa akiona kifua chake Mbweku Jr kilichotanuka kama mataruma ya reli, hivyo amuonjeshe huba atulize ashki na hawaa ya nafsi yake.

Ikabidi Mbweku Jr atumie akili za kuzaliwa, akazichanga vyema karata zake kuepuka mtego huo ulioenda shule. Maana vinginevyo Bi Mwazani angeweza kumzushia kesi ya ubakaji, kesi ambayo asingechomoka abadani kutokana na kukutwa chumbani kwa Bibi. Jamii yote inayopenda kutenda bila kutafakari, inayopenda kuongea bila kupima, moja kwa moja wangetoa hukumu kuwa Mbweku Jr ni mbakaji. "Ngoja basi nikanywe chai nishibe, ndio tuanze upasuaji unaoutaka, uskonde hata mie nakupenda sana sema nilikuwa nakuogopa kukuambia usije kuniona sina adabu" alijitutumua Mbweku Jr kumuongelesha kimahaba Bibi wa watu huku akimpa matumaini feki, mpaka bibi akaingia kwenye mstari.

Akapewa ruhusa ya kutoka chumbani mule kwenda kunywa chai huku Bi, Mwazani akiwa amejawa na furaha fokofoko anapulizia marashi, utuli na manukato chumba kizima maandalizi ya ujio wa Mbweku Jr chumbani kwake aje kumpagawisha. Yakawa yanakatika masaa, Mbweku Jr kajifungia chumbani kwake habari na mtu hana. Mpaka kufika majira ya alasiri Bi.Mwazani akakata tamaa huku uso wake ukibeba soni na fedheha ya hali ya juu ya kuzidiwa akili na mjukuu wake kabisa kiumri, na kuamua kuzindua vita rasmi vya uhasama na Mbweku Jr. Hiyo ndio ilikuwa sababu ya Mbweku Jr kuandamwa asubuhi asubuhi hata hajapumzika tayari ameanza kumjazia nzi mbele ya majirani.

Mbweku Jr alivumilia kwa sababu siku zake za kuishi Tanzania zilikuwa zinahesabika alishajipangia hana siku tatu mbele lazima atazamia Afrika ya Kusini. Alishajiandaa kwa masurufu ya safarini, kutokana na kudunduliza sehemu ya pesa zake za mshahara. Baada ya kujishibia mihogo yake kwa chai ya mkandaa, akaingia zake bafuni akaanza usafi wa choo na bafu kama mama mwenye nyumba wake Bi.Mwazani alivyoagiza. Alipomaliza akajimwagia maji na kujiandaa kuelekea Ukonga, Gerezani. Akalifunga vizuri geto lake, mkononi akiwa na bahasha nzito ya kaki, ndani yake bahasha hiyo ina jambo zito analotaka kwenda kumuonyesha baba yake gerezani. Kisha akampita Bi.Mwazani kibarazani akiwa amefura kwa hasira dhidi yake, anatamani hata awe na uwezo wa kummeza kama chatu.

Mbweku Jr hakumjali, akampita bila kumuaga, na kuelekea dukani kwa Mangi kununua mazagazaga kama sabuni, nyembe, dawa ya mswaki, mswaki na vikorokoro vingine vya kumbebea baba yake gerezani. Alipofika kituo cha daladala, hakuchelewa sana kabla hajapata gari la kuelekea Ukonga. Njia nzima alikuwa anawaza namna baba yake atakavyomshangaa kwa kumuona mabadiliko yake ya kimwili na kiakili. Pia alikuwa na kimuhemuhe cha kufahamu ukweli na undani wa kilichomo ndani ya bahasha ile.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
 
SEHEMU-33

[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
"Mbweku Wa Mbwekuuuuu.........!" "Naaam Afande.....", aliitwa mfungwa Mbweku na askari magereza wa zamu akaitika haraka haraka, aje kumuona mgeni wake aliyemtembelea magereza siku hiyo ya kutembelea wageni. "Babaa....Babaaa....Babaaaa....nini hasa kinakusibu Babaaa.....!" alijikuta Mbweku Jr anaongea kwa hisia kali mpaka machozi yakaanza kumtiririka na kuyalowesha mashavu yake. Mzee Mbweku alipigwa na pumbao na mzubao wa muda fulani akionekana hayaamini macho yake kumtia machoni tena barobaro wake mkubwa baada ya kutenganishwa nae kwa miaka kadhaa. Bila kujibu kitu akamfuata kijana wake na kumkumbatia kwa nguvu mpaka nae akamwaga mchozi wa nguvu. Eneo lile la makutano ya wafungwa na ndugu zao likageuka kama msibani kwa muda kutokana na vilio vilivyokuwa vimetawala.

Askari magereza alikuwa anawaangalia baba na mwana kwa jicho la huruma na imani, moyoni mwake utasema akitamani awe na mamlaka ya kuwaruhusu waondoke wote kwenda nyumbani, lakini La hasha, mwenye mamlaka hayo ya kuwasamehe wafungwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Mheshimiwa Rais pekee. "Mimi ni mahamumu mwangu, kisukari, shinikizo la damu na matatizo ya moyo yote ni magonjwa yangu. Lakini sasa mimi sijambo, nawashukuru sana madaktari wa hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa huduma wanazonipa...! " alijieleza kitu kinachomsibu mwilini mwake mpaka akakondeana akabakia mifupa tupu, kitu ambacho kilimuogopesha sana mtoto wake Mbweku Jr. Mtoto mtu akabaki kutikisa kichwa tu, kuashiria hakubaliani na maelezo ya baba yake, huku moyoni mwake akitambua fika hiyo nafuu ya baba yake ni ile sijambo ya Kiswahili, ya kuanua ngoma juani.

Wakaongea mambo mengi baina yao, wakikumbushiana hadithi za siku za nyuma huku baba akionyesha kusikitishwa sana na kitendo cha Mbweku Jr kukacha shule na kuingia mtaani. Mbweku Jr alijitetea sana mpaka baba yake akamuelewa kuwa ni kweli hakuwa na jinsi lazima tu angeacha shule. Ila akampa wosia huku Jijini aishi vizuri na watu, aviogope vya watu kama ukoma ndipo watu watampenda vinginevyo ataliacha Jiji kwa fedheha. Pia akamuasa asiache kuwaangalia kijiji mama yake mzazi na wadogo zake kwa jicho la huruma, awainamishie bawa la unyenyekevu walau kwa kuwatumia senti ya sukari na unga.

"Baba nisije nikasahau, hii picha yako ulipiga na watu gani, imechakaa na ni ya siku nyingi sana..! " aliuliza Mbweku Jr wakati akiwa tayari ameikabidhi ile picha kwenye mkono wa baba yake huku moyo wake unadunda kwa nguvu akisubiria jibu la baba yake, alikuwa makini kutazama mabadiliko ya uso wa baba yake. "Mmhhhh.....umeipata wapi hii picha?, daah....hawa ni marehemu Bosi Minja huyu aliyekaa katikati na huyu kulia kwetu alikuwa dereva wetu anaitwa Nicco. Hii picha ilipigwa siku ambayo Bosi wetu huyu Mr.Joseph Minja anaripoti kazini pale katika ofisi za Peace Corps-Tanzania. Umeipata wapi hii picha sikumbuki kama ilikuwa kwangu hii picha...! " aliuliza kwa mara ya pili kwa msisitizo na kiudadisi huku amemkodolea macho mtoto wake.

"Hii nimeikuta kwa msichana mmoja, huko kazini kwangu nikamuibia bila yeye kufahamu, mara tu nilivyoiona sura yako, basi nikajua huenda huyo dada ni mtoto wako wanje ya ndoa" alijibu Mbweku Jr huku anairudisha tena ile picha kwenye milki yake ndani ya bahasha akiwa anatabasamu. "Mhhh.....hapana, sina mtoto nje ya ndoa zaidi ya nyinyi wanangu kipenzi,asije akawa ni binti wa Bosi wangu Minja, maana marehemu aliacha mtoto mmoja wa kike anaitwa Deborah kama sijasahau, maana miaka imepita.

Nimemkumbuka kwa sababu alikuwa anakuja nae kazini mara nyingi tu huyo binti yake. Pia kuna mwanamke mmoja chotara wa kizungu, alikuwa katibu muhtasi wetu pale ofisini akiitwa Recho inasemekana alizaa nae mtoto mmoja wa kiume ingawa tetesi zinasema alibambikiwa tu Bosi hakuwa mtoto wake wa damu..!" aliongea kiunyonge Mzee Mbweku huku akionekana anavusha mawazo yake kuyapelekea mbali sana, akikumbukia matukio ya siku za nyuma kabla hajafungwa. "Unasemaje baba?.., Huyo katibu muhtasi wenu akiitwa Recho..? kama vile namfahamu asije kuwa ndio Bosi wangu ninapofanyia kazi baba....!" aliongea Mbweku Jr kwa tashwishi kubwa huku akisubiria jibu la baba yake, litoe ithibati. Moyoni alikuwa anachekelea, kuwa kama Bosi Recho akiwa ndio mtumishi mwenza wa baba yake enzi wakiwa kazini alipanga kwenda kujitambulisha rasmi kwake. Hisia zikimtuma kuwa huenda Recho akamkabidhi kitengo kizito chenye ulaji, na safari ya kwenda Afrika ya Kusini lazima aioteshe mbawa.

"Huenda akawa ndio huyo, maana huyo Recho, dereva wetu Nicco wakati nipo gerezani Arusha alishawahi kunitembelea siku moja akanieleza kuwa sasa ameuchinja, ni mwanamke tajiri sana, anamiliki Hoteli kubwa Jijini Dar es salaam kwa ushirikiano na mpenzi wake, hiyo Hoteli inaitwa 'Martino Royal Hotel'. Nicco akanieleza vitu vingi sana mpaka tukafikia hitimisho huenda Recho ndio alimuua Bosi wetu Minja kwa ushirikiano na huyo mjuba mwenzako Martin ili wapore pesa ambazo zimesababisha mimi niozee jela...!" aliongea kwa hisia kali huku machozi yanazidi kumtiririka Mzee Mbweku, mpaka Mbweku Jr akawa anajitahidi kumfuta machozi baba yake. Maongezi yao, yaliendelea wakimuongelea Recho, wakifafanuliana wajihi wake mpaka Mbweku Jr akajiridhisha bila mashaka kuwa huyo Bosi wake wa sasa nwanamama ndio Recho huyu aliyekuwa Katibu Muhtasi kazini kwa baba yake.

"Muda umekwisha mmebakiza dakika 2 tu, muagane sasa.." aliongea yule askari magereza huku akiwapitia wafungwa wengine waliotembelewa na ndugu zao akiwakumbushia suala la muda kwisha. "Baba mie nasafiri kwenda nchini Afrika ya Kusini saa na wakati wowote kuanzia sasa, hii ni taarifa tu nakupa sihitaji ushauri wako.. !" aliongea Mbweku Jr akiwa ameshasimama lakini anachemka kwa hasira dhidi ya Recho, amekunja ndita mpaka akajikuta machozi yanamlengalenga. "Safari njema, wewe sasa ni mkubwa upo katika utawala wako binafsi, nakujua wewe ukilazimisha jambo lako lazima liwe unavyotaka ndio tabia yako toka utotoni. Ila kikubwa ni kama nilivyokupa nasaha, usijaribu kufanya chochote cha kulipiza kisasi kwa Recho. Kwanza hatuna ushahidi wa asilimia 100% kuwa yeye ndio mporaji wa pesa zilizoibwa ofisini, pili ana nguvu ya kipesa atakupoteza wewe na kizazi chako chote akikugundua umeijua siri yake kuwa yeye ndio muuaji wa Bosi Minja. Pia nakuomba kabla hujasafiri kwenda huko unakotaka kwenda upite Bagamoyo kwa Sheikh Maarifa akufanyie dua ya safari, wakati tupo kazini enzi zetu watumishi wengi tulikuwa tungongana kwake kunyoosha mambo yetu" aliongea Mzee Mbweku huku akisimama na kuvichukua vitu vya zawadi alivyoletewa na mtoto wake baada ya kuwa vimeshakaguliwa na askari magereza kuhusu usalama wake.

"Sasa huyo Sheikh Maaarifa anaishi Bagamoyo gani maana Bagamoyo ni kubwa baba...! " alizidi kuuliza Mbweku Jr huku akionekana amekubaliana na ushauri wa baba yake, wa kwenda kwa mtaalamu. "Haya ondoka zako, karibu tena siku nyingine…" askari yule akamfukuza Mbweku Jr. Mzee Mbweku akawa anaondoka zake kurejea gerezani huku anampungia mkono wa kwaheri mtoto wake. Mbweku Jr alibakia amesimama kama sanamu, alitamani aondoke na baba yake warudi nyumbani pamoja, wakafanye maisha kama zamani. Mbweku Jr nae hakupoteza muda akatoka nje ya gereza na kuingia zake mtaani.

Alipoangalia saa yake akaona ni saa 6 mchana, hivyo bado anao muda wa kutosha kabla ya kuingia kazini saa 12 jioni. Akaingia mtaani kutafuta penyenye wapi anapopatikana Sheikh Maarifa huko Bagamoyo. Hiyo ndio tabia halisi ya Muafrika kuabudu mizimu na kushinda kwa Waganga, hata asome mpaka Chuo Kikuu, awe Tajiri wa dunia lakini bado mambo yake atayaendesha kwa nguvu za ndumba. Pia akitoka kwa Sheikh Maarifa, kuna vitu vya kazi alitaka kuvinunua kwa ajili ya kumtorosha Deborah usiku wa leo ili na yeye atoroke kimoja. Sasa alihisi kuna hisia kabisa za kumuunganisha yeye na Deborah. Picha ile aliyompelekea gerezani baba yake aliifuma katika makorokoro yaliyomo kwenye mkoba aliokutwa nao Deborah pindi alipoletwa na mtekaji wake pale kwenye danguro. Aliona kabisa wao ni wahanga wa vitendo vya kishetani vya Recho, hivyo akapatwa na pashawa la moyo ya kumsaidia Deborah. Ingekuwa ni dhambi kubwa kwa Mwenyezi Mungu kumtelekeza kwenye jumba lile lenye kila aina ya Ufirauni.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]


SURA YA KUMI NA MBILI


“Youu…fala mkubwa, hanisi wewe unachelewa kufungua geti, unataka kazi au hutaki? “ alifoka na kutoa matusi ya nguoni Bosi Recho kwa mlinzi Mbweku Jr ambaye alikuwa yupo kama hayupo usiku huo kutokana na mawazo kichwani mwake. Recho alikuwa akiutwika mtindi kichwani basi kinywa chake hakikosi kutoa maneno tepetepe yenye matusi ndani yake. Sasa adhabu yako gari tunaliacha nje, ulilinde ole wako kiibiwe kitu utakiona kilichomtoa kanga manyoa, kenge mkubwa wewe..Bebiiii.... Bebiii... shuka kwenye gari tukale raha zetu.. alionge Recho kwa hasira akitoa maagizo mapya kwa Mbweku Jr kisha akimuita dereva wake, ambaye alikuwa ndio mpenzi wake wa siri ambaye Mr.Lorenzo hamfahamu. Walianza kwa kificho lakini kama ujuavyo penzi ni kikohozi halifichiki sasa walikuwa wanajiachia waziwazi dhahiri shahiri.

Nisamehe Bosi sirudii tena, usingizi ulikuwa unataka kunimiliki aliomba msamaha Mbweku Jr kwa sauti ya unyenyekevu huku amefumbata mikono yake kifuani kuonyesha majuto yake kwa uzembe alioufanya kazini. Halafu dogo jiangalie sana, punguza dharau ukiwa kazini, umeskia wewe, utarudi kuwa chokoraa shauri yako.. aliongea maneno ya kukereketa, yenye kukata maini yule dereva mdogo tu kiumri, mchepuko wa Bosi Recho, aliyekuwa anajulikana kwa jina la Beka, halafu akamsogelea kwa karibu kisha akamtemea mate usoni mlinzi Mbweku Jr. "Bebiii...muda unayoyoma achana nae mbwa koko huyo...! " aliongea Recho kwa sauti ya kilevi na dereva wake, wakakumbatiana viuno vyao kimahaba huku wanapigana mabusu motomoto, wanapeana nyama ya ulimi kwa sauti za kunong'ona, wanaelekea zao kwa mwendo wa kinyonga kwenye moja ya chumba kilichopo kwenye roshani hiyo kwenda kujivinjari, wakazamishane kwenye kina cha bahari ya mapenzi.

Mbweku Jr akiwa ameumuka uso kwa hasira na ghaidhi ya kutemewa mate na hawara wa Bosi wake. Alikuwa amepandwa na mori wa kutaka kulipiza kisasi, lakini akawa anajitahidi kutuliza hasira zake asije kuharibu mambo ya msingi. Walivyotoweka mabaradhuli wale kwenye upeo wa macho yake, kabidi amshtue mlinzi mwenzake aliyekuwa anarandaranda nje ya ukuta aje kukaa ndani, wabadilishane ili yeye atoke nje kulinda gari kama alivyoagizwa na Bosi Recho. Amri hiyo ya Mbweku Jr kulinda gari ena nje ya geti, ikawa ni kama kumpa paka kazi ya kulinda maziwa, tena kwenye siku ambayo Mbweku kaipanga ndio siku yake ya kutoroka. Himahima kwa ustadi mkubwa akavunja kioo cha gari upande wa abiria na kuzama ndani ya gari hilo la Recho. Akawasha kurunzi yake ndogo na kuanza kufanya speksheni. Akaona mkoba wa Bosi Recho umetuna ameusahau ndani ya Korando lake, akiwa ameuacha chini ya sehemu ya makanyagio ya miguu yake. Bila ajizi akaufungua mkoba huo na kukutana na pochi nene ya ngozi iliyotuna, akashawishika kuifungua pia kujua kilichomo. Alipoifungua tu, akakodoa macho yake kwa mshangao, yakatamani yasifunge tena. Aliziona noti nyingi sana zimepangwa kiufundi mkubwa ili ziweze kuenea kwenye pochi hiyo. Moyo wa Mbweku Jr ulilipuka kwa furaha sheshe huku akijiona ana bahati ya mtende ya kuua ndege wawili kwa wakati mmoja. Mbele ya pesa kila binadamu ana mate ya fisi, hadiriki tamu na daima hutaka zaidi na zaidi, ndio maana mabilionea duniani kila siku wanaanzisha vitega uchumi vipya hawatosheki.

Malengo sasa yakawa ni kumtorosha Deborah na pia kujilipa nusu hasara kwa pesa alizokwapua Recho nyumbani kwa Bosi Minja. Kwenye hilo fuba la pesa alilolifukutua kwenye pochi zilikuwa ni noti mchanganyiko pesa za kigeni na za madafu. Bila kulazia damu, Mbweku Jr akazichukua zote na kuzisunda vizuri ndani ya chupi yake ya kubana aina ya V. I. P. Akaendelea na upekenyuzi wake kwenye droo za gari mpaka akaliona zigo la vibali vya kuingia ndani ya jengo.

Akachukua vibali viwili vilivyokuwa vimeshasainiwa tayari na Recho himahima akashuka garini, huku akiombea Mungu wasitoke mapema Recho na hawara yake Beka. Kilichokuwa kinampa ujasiri ni kuwa kwa kawaida wakiingia kujivinjari wapendanao hao huwa wanatoka Alfajiri, hivyo atakuwa tayari kishatoroka zake Baada ya kufanikisha zoezi lile. akiwa bado Mbweku Jr anachukua doria kule nje anazunguka huku na kule. Kila wakati akiangalia saa yake ya mkononi kama kuna kitu anakisubiria kwa hamu. Ilimchukua kama dakika 45 kitu alichokuwa anakisubiria kwa hamu kikatokea.

Gari nyeupe aina ya Corolla, ikafika pale kwenye danguro la siri na kusimama nyuma ya gari la Recho. Kabla hajapiga honi, Mbweku Jr akamuwahi pale pale mbio mbio dereva wa lile gari, na kwenda kugonga kioo cha mlango wa dereva. Dereva wa Corolla lile baada ya kumuona Mbweku Jr akiwa ndani ya sare za kazi akatambua ni mlinzi, bila hofu yoyote akashusha kioo cha gari lake na kuongea. "Hellow...habari yako, mimi daktari nimekuja kwa mgonjwa wangu yule dada wa jana, kibali changu hiki hapa...!" aliongea yule daktari kwa kujiamini, akiwa ameuvalisha uso wake tabasamu pana huku akitoa mkono wake wa kulia nje ya dirisha akionyesha kibali chake. Hilo ndio likawa kosa yule daktari, Mbweku Jr alizuga kama anakipokea kibali kile, akafanya shambulizi la ghafla na la kuumiza mno. Daktari akashtukia tu amekabwa kabali nzito ya mbao shingoni mwake. Akajaribu kufurukuta huku na kule kujitoa kwenye mikono ya Mbweku Jr, lakini ikawa ni kazi bure, mpaka akalegea na kutulia.

MBweku Jr alikuwa na mshipa wa nguvu wa kuzaliwa nao, mikono yake imekomaa utasema anakula saruji. Mbweku Jr alipojiridhisha kuwa daktari yule ameshazimia, mbele hayuko na nyuma hayuko, akafungua mlango wa dereva na kutoa koti refu jeupe la kidaktari lililokuwa limetundikwa kwenye siti ya abiria kiti cha mbele. Kisha Mbweku Jr akajongea mafichoni kwa haraka alipoficha begi lake la safari umbali wa kama meta 10 kutoka lilipoegeshwa gari la daktari. Akabadilisha nguo zake za sare za kazi na buti za kazi na kuvaa za nguo zake za kawaida na viatu vyake kisha akatinga juu yake koti la kidaktari aliloiba. Akachukua pia kamba ndefu na ngumu yenye kifundo cha chuma kutoka kwenye begi lake na kuitia kwenye mmoja wa mifuko ya koti lile la kidaktari. Akajirekebisha koti alilovaa na kujiaminisha kuwa yupo vizuri sasa, anaweza kuingia ndani ya geti kuelekea kwenye jengo kumuokoa Deborah.
 
SEHEMU-35


️[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji979][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Mbweku Jr alifanikiwa kuwavuka walinzi wote huku akiwa tayari ameshaelekezwa wapi alipo Deborah. Alikuwa anaisikia sauti ya mbwa kwa mbali akibweka woo woo bila kufahamu kuwa huyo ni mbwa wa Mr.Lorenzo, akapuuzia. Alileta ujanja kwa mmoja wa walinzi kuwa amesahau chumba Ambacho Deborah amehifadhiwa. Mbweku Jr alikuwa amewatangulia kuingia ndani ya mjengo akina Jimmy, Mr.Lorenzo na genge lao kwa mpishano wa kama takribani nusu saa. Alikuwa anazipanda ngazi huku akiwa anakimbia pukutu pukutu mithili ya farasi wa mashindano akiwa na hamu ya kumuokoa dada yake Deborah. Kasheshe jipya likaibuka kwa Mbweku Jr alipokifikia chumba cha Deborah. "Vipi Daktari mbona unahangaika, funguo wako upo wapi? "aliuliza mmoja wa walinzi huku anamfuata Mbweku Jr kwa kasi ya ajabu huku akiiweka silaha yake vizuri. Mbweku Jr kijasho chembamba cha uoga kikaanza kumvuja, alijiona kabisa amekamatika kizembe sana. Mawazo yake yalikuwa huenda mlango utakuwa wazi au funguo upo hapo hapo mlangoni, kumbe daktari alikuwa na ufunguo wake maalumu wa kuingilia. "Kama umeupoteza wako sio shida, twende kwa Bosi Recho tukamgongee chumbani kwake ukamuelezee akuazime wa kwake, maana kiongozi wao hawa wanawake Miriam amerudi nyumbani kwake leo halali hapa, yeye pia ana ufunguo wake" aliongea yule mlinzi baada ya kumfikia Mbweku Jr kwa ukaribu zaidi. Kusikia kuwa anataka kupelekwa kwa Bosi Recho, moyo wa Mbweku Jr ulianza kudunda kwa uoga kama saa kweche ya mezani, akijihesabu kabisa ameshakamatwa. "OK...wazo zuri sana, twende kwa Bosi Recho....!" Mbweku Jr akajitutumua kuongea kiujasiri huku akiuweka mkoba wake vizuri na kumfuata nyuma nyuma yule mlinzi mwenye silaha akijitia kupiga miluzi. Mbweku Jr hakuwa na uthubutu katu wa kumvamia yule mlinzi kwa sababu hakuwa na ujuzi wowote wa kutumia silaha ya moto. Alichopanga ni kuwa kuwa akipata upenyo tu atundike miguu mabegani kuepusha masaibu yatakayomsibu toka kwa Recho pindi akimgundua kuwa sio yule daktari wake aliyemuagiza kumchunguza afya Deborah. Kadri alivyokuwa yule mlinzi anapunguza mwendo kuashiria kama vile wamekaribia chumba alichokuwepo Recho na hawara yake katika roshani ileile aliyohifadhiwa Deborah, matumbo ya Mbweku Jr yalianza kumchezacheza huku akizidi kuzama katika bahari ya luja akiwazia mustakabali wake. Mungu si Athumani, Mbweku akajitia kuweka mkono wake wa kushoto kwenye mfuko wa koti lake la udaktari. Akashtuka mshtuko wa furaha kwa mbali, aligusa kitu kigumu kama chuma mfano wa ufunguo. "Aaaaah....tumehangaika bure kumbe funguo niliusweka ndani ya koti langu bwana...!" aliongea kwa sauti ya juu Mbweku Jr na kujilazimisha kujichekesha. " Basi hamna tatizo kaendelee na kazi maana hapa mwenye nilikuwa naogopa kumsumbua Bosi Recho maana kumuamsha usingizini angekuwa moto balaa" alijibu yule mlinzi huku akianza kushika ngazi za kushuka roshani ya chini kama vile kuna kitu anafuatilia. Mbweku Jr akaanza tena kurudi chumbani kwa Deborah kwa mwendo wa kasi. Kwa upande wake Deborah alikuwa ameshashtuka toka kwenye usingizi wa mang'amung'amu unaotokana na kuzidiwa na kileo pia na ndoto za kutisha za kifo cha baba yake mzazi. Aliposhuka alijikuta amepiga makelele huku akiwa tayari ameshajikojolea kitandani. Ndoto ya kifo cha kikatili cha baba yake alikuwa anaiota mara nyingi akiwa na msongo wa mawazo katika usiku wa Jumamosi kuamkia Jumapili. Haraka haraka akaamka akaenda kubadilisha nguo zake za mikojo msalani na kutoa mashuka kitandani na kutandika mapya. Akavaa nguo zingine alizozichukua kwenye kabati kisha akarudi kitandani pake Kichwa kilikuwa kinambangua vilivyo kwa maumivu makali, huku akiwa anajutia kwa kitendo chake cha kunywa pombe. Hakuwa na uwezo wa kubadili kitu, daima asiyeangalia jambo mwanzoni kwa kulifanyia upembuzi yakinifu kabla ya kulifanya huishia ningalijua. Akaanza kuogopa kutumia kinywaji cha aina yoyote ndani ya chumba kile. Alikuwa ameshafungiwa ndani kama mwari kwa zaidi ya saa 24 bila kuangaziwa na jua la nje ya nyumba. Akiwa nae kichwani kazama kwenye bahari ya luja pale kitandani akiyawazia maisha mapya ya ukahaba anayotarajia kuyaanza muda sio mrefu, ghafla bin vuu akashtukia kelele za ufunguo unaogombana na kitasa cha mlango wa chumba ili kuruhusu mlango kuwa wazi mtu apate kuingia ndani. Akakurupuka haraka haraka na kukaa pembeni ya kitanda, macho yakitazamia kukutana na Miriam, mwanamke aliyejitambulisha kwake kama ni kiongozi ndani ya ule mjengo. Alipanga kutaka kupambana na Miriam kwa hali na mali mpaka aweze kutoka ndani ya jengo lile. Hakuwa tayari kufanywa mboga kirahisi labda awe maiti. Kwa mshangao mkubwa akamuona daktari anaingia ndani ya chumba kisha akaufungua mlango kwa ufunguo. Deborah akazidi kuchanganyikiwa, huku akijiuliza maswali lukuki yasiyo na majibu kuhusu huyu daktari. "Nani kakuambia mie mgonjwa, mie sikubali nataka kutoka humu sitaki kuendelea kukaa humu....!" alijikuta Deborah amepata nguvu za kuongea kwa sauti ya juu huku akianza kulia kilio cha kwikwi. "Shiiiiiii.....! Nyamaza Deborah nimekuja kukuokoa usiwe na hofu hata chembe na mimi, upo sehemu mbaya sana, utapoteza muelekeo wako wote kimaisha ukiendelea kukaa humu...!" aliongea Mbweku Jr akiwa ameuegemea mlango wa chumba kile. Mbweku Jr akaanza kuvua koti lake alilovaa na kulitupa pembeni huku akitoa kamba yake aliyoikusudia kumuokolea Deborah. "Samahani...wewe ni nani kwani, Askari umetumwa na mama Koplo Marieta kuja kuniokoa?" aliuliza Deborah kwa furaha akiwa hayaamini macho na masikio yake. Mbweku Jr hakumjibu kitu, akaanza kupambana na kuvunja dirisha, mpaka akafanikiwa kwa utundu wake. "Njoo haraka, jitahidi kugangamala utakapokuwa unashuka na hii kamba mpaka chini ya jengo, ukicheza tu umevunja miguu au kifo hili jengo ni refu sana" alitoa amri ya kijeshi Mbweku Jr akiwa hana muda wa kupoteza kabisa na kumpa tahadhari Deborah ya usalama wake. Akambeba Deborah na kumpitisha dirishani kisha akamshikisha kamba ya kushukia chini ya jengo. Wakati Deborah anajiandaa kuanza kushuka, zikaanza kusikika sauti za kuogofya. "Paaah.....Paaaah.....Paaaaah....", "Maamaaaaah.....nakufaaaaaaah..." Deborah alipiga kelele yenye sauti kubwa kisha akanyamaza akiwa bado anaserereka na kamba ile, baada ya kusikika kwa vishindo vya sauti za risasi mfululizo ndani ya lile jengo. Mbweku Jr nae hakujivunga kwa kutumia kipande kile kile cha kamba aliyokuwa anaitumia Deborah na yeye akaanza kushuka nayo kabla ya kugundua kuwa kamba hiyo imekatika haijafika mpaka chini, hivyo lakini akashuka hivyo hivyo kabla ya kukutana na janga jipya kabla hajatua chini. Kilisikika kishindo kizito sana cha baadhi ya sehemu za jengo lile la kifahari kubomoka vibaya kutokana na mabomu yaliyolipulika kwenye lile jengo. Vishindo hivyo vya sauti za risasi na mabomu likazusha tafrani na taharuki kubwa isiyotegemewa na wakazi wa Sinza usiku huo wa maneno. Mayowe na makelele ya kuomba msaada yakawa yanasikika kila kona ya kitongoji cha Sinza kilichofikiwa na sauti ile ya kutisha katika pindapinda la usiku wa manane tulivu.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
 
SEHEMU-36


️[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Asubuhi na mapema jua lilipochomoza, watu walikuwa wamejazana pomoni ndani ya nyumba mpaka nje ya ukuta wa fensi, wa danguro la siri lililokuwa likimilikiwa na Recho. Walikuwa wamejikunyata wakiwa na hali ya huzuni na majonzi kutokana na tukio la kutisha lililotokea usiku wake. Maelfu ya watu hao walitoka pande mbalimbali za Jiji la Dar es Salaam, na wengine walikuwa bado wanaendelea kumiminika kama siafu, tokea walipopashwa habari kupitia kwenye redio, televisheni na wale Vidinga popo juu ya kutokea kwa milipuko ya mabomu na milio ya risasi kwenye danguro hilo la siri huko Sinza Kijiweni. Wanajeshi wa jeshi la wananchi "JWTZ" na polisi wote kwa pamoja walikuwa wanashirikiana kuhakikisha hali ya usalama inarejea eneo hilo kwa haraka. Helikopta za jeshi nazo zilikuwa zinaruka angani kujaribu kuchunga na kuimarisha hali ya usalama wa eneo hilo. Kwenye milipuko hiyo iliyotokea usiku wa manane, watu kadhaa walisadikiwa kufariki hapo hapo na wengine kujeruhiwa vibaya. Hakuna mkazi wa Jiji aliyependa kusimuliwa tukio hilo la kihistoria katika nchi ya Tanzania, alitaka akashuhudie mwenyewe kwa macho yake kisanga hicho, ikiwa ndio mara ya kwanza kusikika uhalifu wa kulipua jengo unafanyika. Siku hiyo Sinza kutokana na hekaheka zake iligeuka kama sehemu zenye machafuko huko Darfur nchini Sudani na Kandahar nchini Afghanistani. Wale wakazi wenye roho nyepesi kama karatasi kwa uoga, tayari zamani walishakimbilia Stendi ya Kisutu kwenda kutafuta usafiri wa kurejea kwenye Mikoa yao, huku wakienda kusikilizia hali ya usalama irudi kuwa nzuri. Watu walikuwa wamejikusanya vikundi vikundi vidogo vidogo vya midahalo wakibadilishana mawazo na kuhadithiana namna uhalifu huo ulivyotekelezwa. "Penyenye nilizozipata ni kuwa walinzi 6 wa ndani ya jengo wamefariki, pia mlinzi wa getini mmoja tu ndio kapona mwingine mwili wake haujaonekana inasadikiwa amefariki kwa kufunikwa na kifusi" aliongea Habari kauzwa aliyekuwa anajifanya ana siri nyeti za tukio hilo. Umahiri wake wa kupangilia maneno ukawafanya watu wameguke vipande vipande kutoka kwenye vikundi vyao kwenda kumfuata yeye waweze kupata nyepesi nyepesi. "Inasemekana hili ni danguro la siri linalotumiwa na Vigogo wa nchi, mama mmiliki wa hili danguro nae ni miongoni mwa majeruhi hao wenye hali mbaya. Wasichana wasiopungua 20 nao wameaga dunia, waliosalimika ndio wametoa siri zote za kilichokuwa kinafanyika kuhusu utumwa wa ngono. Polisi mpaka sasa inamshikilia mzungu mmoja anaitwa Mr Lorenzo ikimhusisha na tukio hili ambaye ni hawara wa siku nyingi wa huyo mama mjengo. Haki ikitendeka wataumbuka wengi, kuna wanawake watumishi wa serikali na taasisi zake, watumishi wa Mabenki nao walikuwa wanakuja humu kwenye danguro kujipatia kipato haramu cha ziada. Wote majina yao yametajwa na mkubwa wao anaitwa Miriam ambaye nae mpaka sasa yupo mikononi mwa polisi anasaidia uchunguzi" alizidi kubwabwaja huko jamaa maneno kedekede yenye uzandiki na chumvi ndani yake ili kunogesha simulizi zake kwa dhumuni tu ya kuvutia hadhira yake inayomsikiliza. Ghafla fujo na varangati zikaanza kuibuka tena upya ndani ya eneo lile, watu wakaanza kukanyagana na kuumizana baada polisi ya kuanza kuwatawanya watu waliokuwa ndani ya jengo na kuwataka watoke nje kabisa ya fensi. Kikosi cha uokaji kilikuwa ndio kimefika muda sio mrefu ili kutafuta miili ya waliofunikwa na vifusi, hivyo walihitaji utulivu katika utendaji kazi wao. Waandishi wa habari wa televisheni za 'DTV', ITV zote za Jijini Dar es Salaam na 'TVZ' ya Zanzibar hawakubaki nyuma nao, walitingwa na kazi ya kurekodi video na kupita kufanya mahojiano na watu mbalimbali waliojitokeza kwenye umati ule ili wapate kuwahabarisha watazamaji wao. Wandishi wa habari wa redio na magazeti nao walichakarika huku na kule ili mradi nao wapate habari ya kuihabarisha jamii. Daktari aliyeshambuliwa na Mbweku Jr mpaka kuzimia nae alikuwa anategemewa kuwa msaada mkubwa kwa polisi pindi atakapopata nafuu huko hospitalini alipokimbizwa baada kukutwa yupo mahututi. Makachero wa polisi walikuwa nae bega kwa bega ili akizinduka tu awape habari ya kilichomkuta eneo lile. Mr.Lorenzo alikuwa na moyo wa kitoto sana, ndio aliyewapa mabomu ya kutega vijana wa Jimmy walipoingia ndani ya jengo kuruka ukuta. Lengo lilikuwa iwapo atashindwa lengo lake la kumuadabisha Recho lazima alitie hasara jengo hilo lisiweze kumfaidisha Recho maisha yake yote. Hivyo kilichokea yule mlinzi wa jengo aliyekuwa amefuatana na Mbweku Jr wakaachana karibia na mlango wa chumba alichomo Bosi Recho alipokuwa anashuka chini ya jengo ndio akakutana uso kwa uso na akina Mr.Lorenzo, Jimmy na wenzake. Ndipo mapigano kwa njia ya kurushiana risasi yakaanza kusikika. Beka mpenzi wa siri wa Bosi Recho kusikia milio ile ya risasi akajua majambazi wamevamia jengo nae akatoka nje ya chumba na silaha kwenda kuongeza nguvu. Vurugu mtindo mmoja ya vilio vya wanawake ndani ya jengo lile wakitaka kujiokoa kwa hali na mali vikamfanya Mr.Lorenzo ashikwe na taharuki, akafanya maamuzi ya kulipua mabomu yaliyotegwa kuzunguka jengo kwa kutumia saa yake ya mkononi, akihofia Recho asije kuchurupuka kwenye mtego wake. Polisi wa doria nae kusikia vishindo hivyo nao wakatia timu na kulizingira jengo zima na kufanikiwa kumtia mbaroni Mr.Lorenzo na mshirika mmoja wa Jimmy, huku Jimmy na mwenzake wakipoteza uhai kwenye mashambulizi ya risasi. Kizungumkuti na kitendawili kikabakia kwa Mbweku Jr na Deborah, je walifanikiwa kutoroka nje ya jengo au ni miongoni mwa wahanga waliofunikwa na vifusi. Mbweku Jr alitajwa na mlinzi mwenzake aliyesalimika kuwa walikuwa wanalinda wote, na daktari baada ya kuzinduka hospitalini alimtaja mlinzi wa nje ya jengo ndio aliomkaba shingo nusura kufa. Hivyo Mbweku Jr nae akawekwa katika orodha ya watuhumiwa wanaotafutwa kwa udi na uvumba kama yupo hai ili aunganishwe kwenye kesi hiyo ya mauaji ya halaiki. Mawazo ya polisi ni kuwa Mbweku Jr huenda nae ni mshirika wa Mr.Lorenzo katika uhalifu huo. Recho alikuwa mahututi amepoteza fahamu katika chumba maalumu cha wagonjwa mahututi 'ICU' anapumulia mashine akipigania uhai wake, haja kubwa na ndogo zote anajisaidia hapo hapo.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
SURA YA KUMI NA TATU
Mr.Martin Tenga na vijana wake wabebaji mihadarati walisota kwenye rumande maalumu inayoitwa 'Casa Circondariale' wakiwa wanasubiria hukumu yao. Watuhumiwa wanaoshikilia kwenye 'Casa Circondariale' nchini Italia kwa kawaida huwa wanasongamana, hivyo kila siku Mr.Martin Tenga na vijana wake walikuwa kila siku wanaomba kwa Mungu hukumu yao ipitishwe ili wahamishwe kutoka kwenye jela hizo. Ndani ya 'Casa Circondariale' kila chumba walikuwa wanalazwa kwenye chumba kidogo watu 6. Walikuwa wanachanganywa pamoja na wahamiaji haramu wanaozamia nchi za Ulaya kupitia nchi ya Italia. Baada ya kesi yao kuunguruma kwa muda wa miaka 3 hukumu yao ikatoka. Mr.Martin Tenga akahukumiwa kifungo cha miaka 30 jela, huku vijana wake wakifungwa kila mmoja miaka 20. Baada ya kifungo hicho wakahamishiwa kwenye jela maalumu za wafungwa zinazoitwa 'Carcere Giudiziaro'. Huko kidogo kukawa na unafuu, hamna msongamano wa wafungwa. Gereza alilofungwa Martin na vijana wake lilikuwa linaitwa 'Museo del Carcere "Le Nuove' likiwa lipo Jijini Turin. Ndani ya gereza hilo ilikuwa ruksa kutembelewa na ndugu, jamaa na marafiki kila siku saa 9:00 alasiri. Kwa upande wa chakula walikuwa wanalishwa vyakula vya Kitaliano kama Resotto, Pasta na baadhi ya siku wanapikiwa Lasagna. Mwanzoni ilikuwa ni ngumu sana kuzoea vyakula vya Kitaliano hasa ukichukulia Mchaga alishazoea kula ndizi, mchemsho na nyama za kuchoma. Pia ndani ya gereza hilo kulikuwa na jiko la kupikia la gesi kwenye kila chumba hivyo mfungwa alikuwa anaruhusiwa kujipikia chakula chake anacholetewa na ndugu zake. Hivyo maisha ya jela hayakuwa na ugumu wa maisha kama zilivyo jela za nyumbani Tanzania. Kikubwa walichokuwa wananyimwa ni uhuru wa kufanya mambo yao binafsi. Mr.Martin Tenga kila wakati alikuwa anazama katika lindi la mawazo hasa akifikiria kuwa atakapomaliza kifungo chake atakuwa mzee wa zaidi ya miaka 60, je ataenda kuanzaje maisha ya mtaani huko Tanzania. Alijua fika huko Kenya na Tanzania kila kitu chake katika vitega uchumi vyake vitakuwa vimeshafujwa. Hivyo mawazo makubwa yalikuwa yanamsonga kuwa anaenda kuwa mmoja wa wazee wa mitaani. Mzee ambaye atakuwa hana makazi ya kuishi, hana uhakika wa mlo wake wa siku, pia hana uhakika na matibabu yake pindi atakapougua. Moyoni akawa anaomba siku za kumaliza kifungo chake ziende taratibu kwa mwendo wa kobe, maana huko mbeleni ilikuwa ni giza tu. Kingine kilichokuwa kinampa mawazo ni kitendo cha kukosa mtoto katika maisha yake ambaye angeweza pengine kuwa msaada mkubwa sana katika maisha yake ya uzeeni. Akawa anajutia kitendo chao cha Kifirauni walichokifanya na hawara yake Recho cha kumtelekeza mtoto wao mlemavu, Pesambili kwenye nyumba watoto yatima kule Kenya. Kwa muda waliomtelekeza Pesambili kule Jijini Nairobi, Kenya kwa sasa alikuwa anaweka dhana kuwa sasa atakuwa ghulamu mkubwa aliyebaleghe tayari wa zaidi ya miaka 15. Baada ya kupita miaka 6 tokea afungwe jela, Mr.Martin Tenga akapokea mgeni, mfungwa mwenzake kwenye chumba chake cha gereza. Mfungwa huyo mpya hakuwa mwingine bali ni Mr.Lorenzo. Mr.Lorenzo hukumu yake huko nchini Tanzania kutokana na kosa lake la kulipua jengo la roshani ya Recho na kusababisha mauaji ya watu lukuki, alihukumiwa kifungo cha maisha jela. Pia kosa la pili la kukutwa na filamu za ngono za wasichana mbalimbali wa Afrika alihukumiwa kifungo cha miaka 15. Hivyo adhabu hizo mbili zikawa anazitumikia sambamba. Balozi wa Italia nchini Tanzania akaongea na wizara ya mambo ya ndani kuhusiana na suala ya kumhamisha Mr.Lorenzo akatumikie kifungo chake nchini kwake Italia. Wizara ya Mambo ya Ndani, haikuwa na kipingamizi, ikaruhusu Mr.Lorenzo asafirishwe mpaka nchini Italia. Ndipo Mr.Lorenzo akapelekwa gereza alilofungwa Mr.Martin Tenga, na wakapangiwa chumba kimoja. Hawakuchelewa kujenga uswahiba baina yao hasa baada ya kuwa wote wanaongea kiswahili na pia wameshawahi kuishi Tanzania. Ujio wa Mr.Lorenzo ukawa ni neema kwa Mr.Martin Tenga, kutokana na Mr.Lorenzo kuletewa chakula kila wiki cha kupika toka nyumbani kwao. Hivyo wakawa wanashirikiana katika kupika kwa pamoja na kila kitu wakifanya kwa pamoja. Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza, hawa maswahiba wapya wawili, Mr.Martin Tenga na Mr.Lorenzo walikuwa ni mtu na shemeji yake, kwa maana ya kwamba Mr.Martin amezaa mtoto na Recho ambaye ni dada wa damu wa Mr.Lorenzo. Mtoto mwenyewe wa Mr.Martin na Recho ndio huyu Pesambili ambaye anaishi nyumbani kwa Mr.Lorenzo.
 
Back
Top Bottom