SEHEMU YA KUMI NA TATU
Maisha yana changamoto nyingi,hivyo kila wakati binadamu huwa katika mapambano tatizo ni kwamba sio wote wanajua wapo kwenye mapambano na hata wanaojua hawajui muda upi wa kupambana.Wahenga wanasema mwenye hekima anajua muda upi wa kupambana au kukaa kimya.
Walikaa zaidi ya saa moja bila dalili zozote za gari kujitokeza ,wasiwasi ulianza kumuingia mrembo huyu.Alihisi uoga uliouondoa ukimya aliokuwa nao kwanzia mwanzo wa safari,alijikaza kisabuni na kumueleza E1 ,Alisema tumsubiri hapa sasa amechelewa?E1 alijibu kwa kichwa kushangazwa na kuchelewa kwa kiumbe huyu.Aliyemkosesha usingizi kwa siku kadhaa zilizopita.Kuna wakati unakisubiria kitu kwa hamu hadi inakuwa sababu yako ya kuishi,ndiyo tunaishi kwa sababu tuna sababu ya kufanya hivyo.Aliendelea kusubiri na mwisho E1 akatoa maelekezo ,nakuomba ushuke kwenye gari alisema E1 akiondoa lock ya mlango wa gari.Alimuelekeza kusimama nje kidogoya gari kisha akalipaki gari pembeni.
Hapa nusu saa nyingine ilikatika mwisho ikaonekana gari moja ikija taratibu na kupakiwa mahali aliposimama binti Irene,walishuka vijana wawili na kumsogelea ,Akawauliza yuko wapi Mzee,wakacheka kana kwamba wanamdhihaki kisha wakasema ameshaondoka muda mrefu,binti aliogopa,vijana sasa walitoa bastola zao kumnyooshea binti yule na kumuamuru aingie kwenye gari walilokuja nalo.
Kuna nafasi ya udhaifu kwa kila mtu,kwa E1 udhaifu wake ni kumuona mtu mnyonge tena asiye na silaha akinyooshewa bastola kana kwamba wanamteka gaidi maarufu,kwa ustadi mkubwa aliwanyunyizia mvua ya risasi bila kumgusa Irene.Akamsogelea na kumuambia waingie kwenye gari. E1 aliiweka miili ya vijana wale kwenye gari lao na kuliendesha hadi pembeni kidogo akatelekeza gari lile na kulimwagia mafuta ya petroli,kisha akapanda gari na kuendesha.
Aliendesha na kuifuata barabara iendayo kivukoni,aliwahi pantoni iliyokuwa ikivuka na kwenda upande wa kigamboni akiwa na mrembo Irene.Kuna wakati unatazama nyuma na kujuta kwanini ulichukua maamuzi kama hayo,wakati huu unakuwa ni majuto makubwa,Bahati mbaya ni kwamba unakuwa huwezi kurudi nyuma na kubadili kilichotokea.Irene alikuwa akijuta kumtelekeza Brian,alimkumbuka sana,aliukumbuka usaliti aliomfanyia,alikumbuka mpaka idadi ya siku alizolala na mzee yule, 23 ndiyo,baada ya kutumika kwa siku hizi amemtelekeza,tena akimtumia watu wa kumuua.
LONDON ,UK
Wakati Irene akilia na kujilaumu,mzee huyu alikuwa katika jumba kubwa alilokodi siku moja iliyopita,baada ya kufikisha document ile salama mikononi mwa mtu hatari kabisa,alipewa kiasi kikubwa cha pesa na kilichobaki kwake ilikuwa ni kufurahia maisha.Alikuwa na wanawake wanne kila mmoja akijibidiisha kumridhisha.Wote wamezivua nguo na kubaki kam walivyozaliwa,katika kitanda hiki cha king size bed.Ilikuwa tu miguno ya mzee huyu akifurahia maisha,kwa raha alizozipata alikuwa anaelekea kupagawa.Ama kweli pesa ni sabuni ya roho.Alishasahau hata habari za Tanzania,alikuwa akiwaza ahamie nchi gani nyingine kuendeleza starehe,Amandaaaaa.....
Aliita akaingia mrembo mwingine,akiwa na bikini huku kifuani hana chochote cha kuzuia chuchu zenye ustahimilivu wa kusimama,aliingia akiwa na tablet ndogo akauliza kama amepata location ya kula bata? BAHAMAS boss,alijibu Amanda huku akiutia ulimi wake masikioni kwa mzee yule.
KIGAMBONI, TANZANIA
Mbele ya jumba kubwa gari iliyowabeba Irene na E1 iliingia taratibu katika jumba hili la kisasa,baada ya kushuka kijana aliyekuwa mmoja wa Eaglets alimkaribia boss wake kupata maelekezo,akashangazwa na uwepo wa bini Irene,This is Irene,alimkatiza E1,Kisha akamwambia tell everyone to meet me in my study, alimaliza E1 akauchukua mkono wa Irene na kupandisha ngazi taratibu,walipanda mpaka ghorofa ya pili,kisha akamwonyesha Irene,chumba atakachopumzika.Irene alikuwa akilia tu.E1 akafungua mlango na kumwambia Irene,be free kama kuna kitu unahitaji piga simu hiyo mezani kitaletwa.Akatoka na kumpa nafasi Irene.
Katika chumba hiki cha chini kabisa ambacho Eagles hukiita Study,walikaa vijana wote alikosekana E2 na Eaglet mmoja ,E1 alipofika wote walisimama na kuinua mikono yao kutengeneza mfano wa mabawa,E1 Alijibu kwa kufanya vile,akaketi kisha wote wakaketi,kisha mara mlango wa geti ukafunguliwa akaingia Eaglet akiwa amebeba mkufu uliobeba kidani kilichoandikwa E2 ,Alilia na kupiga magoti, akakitupa chini na kusema,I betrayed the brotherhood ,I could not protect the Eagle,Machozi yalikuwa yakimtiririka na kuufunika uso wake.
Eagles,today we lost a brother,aliongea E1,Katika kipindi hiki hatupaswi kukurupuka,visasi vitalipwa kwa utaratibu mzuri.Na kuhusu Eaglet asante kwa kutuletea medani ya ndugu yetu afadhali,hatujawapoteza wote kwanzia sasa E3 unakaimu nafasi ya E2, Eagles,waliinua mikono tena na kukaa.Hivyo kwa sasa mwili uko wapi,Umehifadhiwa mochwari japo umeharibika vibaya sana,alijibu Eaglet yule,akiwa bado kapiga magoti,Tunatawanyika kila mtu aendelee kukusanya taarifa zitakazotusaidia.kikao kimefungwa alimaliza E1.
CHUMBANI
Irene alimaliza chupa tatu za Robertson wine zilizokuwa kwenye jokofu la mle chumbani,alikuwa mtupu,akiwa kalewa akilia pasipo kituo.E1 alimhurumia baada ya kumtazama akiwa Study,alipanda kule ghorofani na kufungua mlango,Irene alikuwa kaanguka akiwa kalewa chakari,E1 akatumia nguvu alizokuwa nao akamnyanyua Irene na kumpeleka kwenye Jacuzzi lililokuwa mle ndani,akafungulia na bomba la maji ya mvua kumuelekea,maji yale angalau yalimpa nguvu.Alianza kutapika,E1 akampa maji kidogo hakuweza hata kunyanyua glasi E1 akambeba tena baada ya kumkausha maji,na kumrudisha kitandani,kuna wakati unampinga shetani na kufanikiwa,E1 alifanikiwa muda huu bila kuwa na tamaa ya mapenzi japo aliona kila kiungo cha mrembo huyo.Alimuweka kitandani na kumfunika shuka kisha akamuacha apumzike,alirudi kule bafuni na kusafisha pale chini alipotapika,mrembo huyu.Alimaliza na kuubamiza mlango akaelekea chumbani kwake kupumzika.
E1 aliamka mapema na kufanya mazoezi,baada ya kumaliza akaoga na kuelekea jikoni hapa aliandaa uji mwepesi na kuiweka chupa katika meza iliyokuwa mle chumbani,Drink me aliiandika na kuiweka mezani.kisha akarudi chumbani kwake kuendelea na kazi zake.Irene aliamka akiwa mchovu hakuwa akikumbuka vizuri kilichotokea lakini alikumbuka kuwa alikunywa sana jana yake,hakukumbuka pia kama alilala na alishangaa kujikuta kafunikwa vizuri shuka.kwanza alijishika "kuhakiki usalama" alipotibitisha kuwa yuko sawa aliamka na kukuta kawekewa uji aliuweka kwenye kikombe na kuanza kunywa,akajifunga taulo lililokuwa pale kitandani alijisikia ahueni.Sasa E1 akapanda tena na muda huu alibisha hodi akiwa na sinia la matunda.
Habari mrembo,aliulza E1 akitabasamu
Salama alijibu Irene akiangalia chini,alikuwa akiona aibu,alianza kumpenda kaka huyu aliyeyaokoa maisha yake mara mbili sasa.
Je nini kitaendelea tukutane sehemu ya 14