RIWAYA; Mapambano

Mpo wadau ,Kama mmemaliza sehemu ya Tisa tuidrop sehemu ya kumi.
 
SEHEMU YA KUMI
Mzee yule alijitahidi kuinuka kutoka sakafuni lakini hakuweza,alijaribu kufumbua macho yake makali lakini hayakuweza kufunguka sawasawa alijiuliza muda gani amefika mahali hapa asipopatambua kama sio kuwepo kabisa katika fikra zake.Aliinua kwa shida mkono wake wa kulia kujishika bega lake la kulia,ndipo alipogundua shimo dogo upande wa juu wa bega lake.Alihamaki,kwanza ni kwa namna gani alifika pale alijiuliza lakini kibaya zaidi Chip ndogo aliyowekewa katika bega lake ilikuwa imeondolewa.Hakujua kijana yule E1 alikuwa na nia gani kumleta mahali hapa.Aliita kwa shida Irene,Irene lakini hakusikia sauti yoyote ya kumjibu akajaribu kuinuka,MAUMIVU makali yaliyoanzia juu ya paja lake na kusambaa mwili mzima yalimzuia kuinuka.Alitoa mguno kama Mbogo aliyejeruhiwa.Hali yake ilitia huruma usingeamini kama mzee huyu usiku uliopita alikuwa na afya njema kabisa.

Sauti za vishindo hafifu vilisikika vikija uelekeo alipokuwepo mzee yule.Vishindo vilikaribia kisha mlango ukafunguliwa.Walionekana vijana wawili na mwanamke mmoja aliyevalia koti jeupe na kila haiba ya udaktari.Alikuwa na kibegi kidogo alichoweka vifaa vyake vya tiba.Katika meza ndogo iliyokuwa katika chumba kile,alilifungua begi lake na kuvipanga vifaa alivyokuja navyo ,Bandages,Madawa aina ya heparin,IV fluids ,TT injection,syringes gloves,Tramadol na vitu vingine tayari kwa kuanza huduma ya kwanza kwa mzee aliyekuwa taabani.

"Hapa ni wapi na mnataka nini" aliuliza mzee yule swali ambalo halikujibiwa na vijana wale waliombeba mzee yule mzegamzega na kumlaza juu ya meza wakatumia baadhi ya nguo zilizokuwa katika chumba hicho kumtegemeza kitandani.Daktari akaendelea na utaratibu wake wa kuhakikisha chupa hizi za IV fluids pamoja na dawa hizo zinaingia katika mwili wa mgonjwa,Alionekana kujiamini na kazi yake akichukua tahadhari kubwa katika kila alichokifanya.Mara mlango ukafunguliwa sasa aliingia E1 akiwa na mfuko mdogo wa saizi ya barua ya A4.Bahasha hii ilionekana kutuna na japo ilikuwa imefungwa lakini kilichokuwa ndani yake hakikuwa karatasi.E1 alitembea kwa kujiamini akiongea kwa kujiamini ungeweza kudhani ni Adolf Hitler aanahutubia wanajeshi wa kinazi.Aliongea maneno ambayo mzee yule hakujishughulisha nayo,maneno pekee aliyoyasikia ni alivyopata kulisikia jina la mpenzi wake wa sasa,Irene.

Alijaribu kunyanyuka na kutulizwa na vijana wale wawili waliokuwa wamejazia haswa,akauliza mmemuweka wapi Irene.Wakati huu hakujibiwa kwa maneno wala ukimya,alijibiwa kwa kofi zito toka kwa kijana E1.Kofi hili lilimuweka katika hali ya utayari wa kusikiliza maneno ambayo yalitamkwa na E1,Nahitaji kupata "package ndani ya saa 72" Failure to do that,nitaanza na Irene.Alisema akifungua bahasha ile na kuzitoa nywele za kike.Zilizoonekana kunyolewa pasipo ridhaa ya mnyolewaji.Nywele hizi ziliweza kujitambulisha yakini kuwa za Irene.Mzee aliingiwa na woga,woga uliochanganyika na hasira na kiapo cha sirisiri alichokuwa akikitamka mzee huyu.Laiti angekuwa na uwezo angewaadhibu vijana hao mara moja.

Daktari aliondoka katika chumba kile na kufuatiwa na E1 akiwa na vijana wawili,hawakufunga mlango walipoondoka.Waliingia katika gari moja nyeusi na kuondoka kwa kasi.Mzee yule alijaribu kuchungulia katika uwazi wa mlango ule,hakuona mtu yeyote akajaribu kutembea na kutoka nje ya jengo lile,hakuona mtu yeyote,akajaribu kujua ilikuwa sehemu gani,hakuonekana kuitambua eneo lile.Mfanano wa jengolile ulikuwa kama stoo za maghala ya kuhifadhia pamba au korosho,hii ikamfanya kujua kuwa kwa vyovyote hapa alipo ni kijijini.Alitoka nje ya jengo lile na alipojishika mfukoni akakuta ujumbe mfupi "You're not dreaming,Deliver the package in next 72 hours".Mzee huyu aliyepitia mikiki mbalimbali hakuonekana kujali,Kilichomuuma hakikuwa kusalitiwa na kijana E1,Bali ilikuwa ni kukaa mbali na Irene tena akihisi anaonewa huko aliko,aliapa kulipiza kisasi.

Watu huyaita mapenzi majina wanayojua,wengine watasema ni upofu,wengine watakwambia ni bahari,wengine watasema hayaulizi,Lakini wote tukubaliane kuwa katika mapenzi watu wengi,wenye nguvu na mamlaka wameshindwa kabisa.Shujaa wa jeshi la Israel Samson,alishindwa na kusalimu amri mbele ya Delila,Adam vilevile kwa Eva,Hata Mfalme Daudi,alijikuta akimpenda mke wa mtu na kumtuma aliyekuwa mume wake katika Frontline yalipo mapigano makali ilimradi apate muda wa kukaa na mke wa askari wake.Haya ndiyo mapenzi,aliyokuwa nayo mzee huyu kwa Irene sio kwakuwa hakuwa na mpenzi,sio kwakuwa Irene amekuwa mzuri sana kuliko wanawake wengine aliokuwa nao-HAPANA-

Ni mapenzi,sijui hii inatokeaje lakini utakuta mtu aliye na wanawake nane,akisikia mke mmoja anatoka na mtu mwingine atalaumu.Ataona wivu,utakuta kijana ana wapenzi tofauti lakini akisalitiwa akajua moto utawaka.kwa mzee huyu Irene aliingia kwa kasi sana,na kizuri kuliko yote ni yeye aliyeutoa usichana wa mwanamke huyu.Pamoja na kuwa siku zote alilala kitanda kimoja na binti huyu hakuwahi kufanya lile aliloliita tendo la ndoa,aliisubiri siku ya ndoa aweze kufaidi matunda ya uvumilivu.Ndoto ambayo kwa karne hizi sio tu kwamba haiwezekani bali piaa si vyema hata kuiota.Kama kijana huyu angehojiwa juu ya vitu anavyojutia bila shaka jambo la kumfaidi binti huyu lisingekosekana katika vipaumbele vyake.

Wanawake wengi huhadaa wapenzi wao kusubiri hadi ndoa lakini wengi wao hawawezi,wengi huvumilia hapa lakini wanaomjua vizuri hujilia kiulaini.Sisemi kuwa kusubiri ni vibaya lakini wengi wetu hatuwezi,kwa kuwa tunakuwa tushaanza vitendo hivyo kabla ya ndoa.Hivyo kusubiri inahitaji moyo wa kipekee,aliokuwa nao Brian akaukosa Irene na kuugawa utamu wote kwa mzee yule aliyepagawa hasa,Japo mahusiano yao yalikuwa ndani ya wiki mbili lakini kwa mzee huyu alimuona kama mke wake waliyedumu naye miaka 30.

KIJIJINI IKUNGU
Usiku waleo ulikuwa mrefu,hakukuwa na vipindi vya TV Vya usiku,wala mechi za UEFA,pengine hata tamthilia mbalimbali na taarifa za habari hapa kwa babu yake Brian.Aliamka akiwa amechoka na uchovu wa jana yake uliochangiwa na safari lakini akili yake ilikuwa na nguvu mpya,Naam,nguvu ya kiakili aliyoipata kutoka kwa babu yake akijaribu kuitumia elimu yake kuyabadili maisha ya pale kijijini.Haswa maisha ya babu yake na kumthibitishia kuwa miaka aliyoipoteza darasani ilikuwa na maana.

Kilikuwa kipindi cha mwishoni mwa masika,wakati ambapo mazao mengi yalivunwa hapa kijijini,babu yake alipata mazao ya kutosha lakini kijana Brian,hakuridhishwa na kiasi kilichopatikana.Akaamua kuitumia elimu yake aliyokuwa nayo kuunganisha na uzoefu wake hapa kijijini.Aliamua kubadili mazao shambani kitu ambacho kinaitwa,Crop rotation.Sasa aliamua kuzilima hekari zote 42 za mzee huyu kilimo cha dengu,Aliuza komputa yake ndogo aina ya Macbook air,akapata kiasi cha milioni tatu,Akafanikiwa kumshauri babu yake kuuza baadhi ya mifugo waliyokuwa nayo na kubakiza idadi ya ng'ombe 20,Fedha zote alizozipata aliziweka katika benki mojawapo iliyokuwa wilayani kwao.

Kijana alisafiri hadi Mkoani mwanza katika chuo cha ukiriguru kinachotoa mafunzo ya kilimo kukutana na mzee mmoja aliyempa namna nzuri ya kulima zao lile la dengu.Kijana alimsafirisha mzee huyu hadi kijijini kwao na akawaelekeza kwa vitendo njia bora za kulima,Kijana pia alikodisha trekta kutoka kwa mzee mmoja aliyekuwa wilaya ya jirani na kufanikiwa kuzilima hekari zote za mzee huyu.Japo mzee huyu mwenye miaka 75 alikuwa na nguvu za kutosha ,na ng'ombe waliokokota jembe la kulimia hakuwahi kuwaza kama kuna siku atazilima hekari zote 42.Kijana huyu alionekana kuwa zaidi ya kiongozi akishiriki kikamilifu katika kilimo.Baadhi ya wanakijiji walimwambia babu yake kuwa anakosea kumsikiliza kijana mdogo na kuuza mifugo yake huku wakitoa sababu zisizo na idadi.Lakini mzee huyu alitambua kuwa binadamu hawakosi la kusema,hivyo ni jambo la busara kuepukana nao.

Zikaja siku palizi na hatimaye,mavuno.Yalikuwa mavuno ya kutosha ,kijana huyu alikishangaza kijiji kile akipata zaidi ya mavuno ya kijiji kile kwa mwaka mzima.Wenye imani za ushirikina walianza kudai kuwa kuna dawa anatumia lakini kwa kijana sasa akili yote ilikuwa katika kuyabadili maisha ya babu yake pale kijijini na kuyaanza upya maisha yake bila Irene.Hatimaye wakaanza kuja wachuuzi wa mazao wakitoa offer ya kununua magunia yale ya dengu kwa kutoa Elfu themanini kwa kila gunia.Babu yake alimshauri kijana yule wayauze kwani mwaka uliopita waliuza kwa Elfu sabini kwa gunia.Kijana yule alishika simu yake na kumpa mzee yule mchanganuo wa gharama walizotumia hadi kuyapata mazao yale na kumueleza babu yake kuwa haridhiki na bei ile.Babu yake aliuliza kuwa tutafanyaje mjukuu wangu,tutazila dengu hizi zote? kijana alimtuliza mzee yule akimuahidi kuwa analifanyia kazi.

Wakulima wengi husahau magumu waliyoyapitia wakati wanalima,husahau gharama walizozitumia.Wachuuzi huja na kuchukua mazao yale kwa bei ya kutupwa ambayo huishia kumnyonya mzalishaji.Hivyo miaka yote wakulima huzunguka palepale.Kijana Brian alilijua hili hivyo alianza mapema kutafuta wateja kutoka makampuni mbalimbali,na wafanya biashara wakubwa.Alifanikiwa kuuza mazao yake kwa kilo na kupata kiasi cha shilingi milioni sitini na saba na laki mbili.Ulikuwa ni mwaka wa faida kwake.

OYSTERBAY
Nyumbani kwa yule mzee ,Irene alikuwa amefungwa huku nywele zake zikiwa zimekatwa kwa mkasi na kumuacha akiwa uchi wa mnyama,katika lango kuu la kuingia katika Jumba lile lilionekana gari likija.

Nani huyo anakuja kwa Irene?,Ni rafiki au adui? Next episode
 
Wapenzi wasomaji wangu,ninapokea zawadi za sikukuu {tukumbukane}, namba ni 0785386036.Kama wote mmefika tushushe sehemu inayofuata
 
SEHEMU YA KUMI NA MOJA
S
arah alikuwa katika lindi la mawazo,alikuwa njiapanda akishindwa kuamua aende ulaya kuonana na Sir McAllison ama abaki nchini kuendelea na kesi ya Nick.Kimaslahi safari ya ulaya ilikuwa kila kitu,Hata katika taaluma yake ya sheria ilikuwa na maana kubwa maana kufanya kazi na kampuni hii kubwa lilikuwa ni tamanio la kila muhitimu wa sheria.Aliendelea kuwaza na kuwazua,mara hii akiyakumbuka maneno ya secretary wa Sir McAllison,ukishindwa kufika nchini wiki ijayo hutapata nafasi nyingine ya kuonana na mzee huyu.Alimhurumia rafiki yake Nick,kesi yake ilikuwa ikimtegemea ,aliwaza kuwaachia ofisi yake waishughulikie lakini hakuona sababu ya kufanya hivyo.Akaamua kuchagua

Ndiyo-Kuchagua ni sifa kubwa aliyopewa mwanadamu,kila wakati mwanadamu hulazimika ama kulaazimishwa kufanya uchaguzi,achilia mbali chaguzi z kisiasa,za mavazi kabatini,chaguzi za kula chakula kipi,chaguzi za nani wa kuongea naye na nini cha kuongea naye,chaguzi za mahali pa kuishi n.k.Chaguzi hizi zimeanza kutoka enzi zamababu wakati fulani Adam alitakiwa kuchagua kati ya matunda mengine na tunda la mti wa katikati,Alichagua la mti wa katikati.Hivyo upatapo fursa hii ni vyema kuchagua kitakachokufaa ili uchaguzi wako uwe na maffanikio,haijalishi unapitia lipi CHAGUA.Ulivyo leo ni kwa sababu ya machaguo uliyochagua maishani.

Sarah alichagua kubaki nchini,ili apate muda mzuri wa kumsaidia Nick,kijana asiye na hatia ambaye alikuwa anateseka gerezani.Aliamua kuyaacha mengine yapite,ili mradi Nick atoke gerezani.Hiyo ndiyo furaha aliyokuwa akiingojea,alijiandaa kuelekea mahakamani kusikiliza kesi hii ya kijana Nick.

GEREZANI
Kijana Nick alipanda katika gari tayari kwa kuelekea,mahakamani ,hatima ya maisha yake aliiacha mikononi mwa Mungu.Maisha tunajifunza vipya kila siku,hapa gerezani kijana Nick alikuwa amejifunza kula kwa muda uliopangwa na gereza,na kula pasi nakubagua chakula,alijifunza pia kuwa sio wote waliopo mahali hapa walikuwa ni wakosaji.Kutokana na simulizi mbalimbali alizozipata hapa,wengine kwa kusingiziwa kesi mbalimbali na wengine kucheleweshewa kesi zao pasipo sababu za msingi.Aliyazoea maisha haya na kuyaona kama nafasi nyingine ya kujifunza,kwa leo alimuomba Mungu ombi moja tu Haki itendeke.

Watu wengi walihudhuria mahakamani hapo,ukiacha mawakili,na mahakimu,ndugu mbalimbali waliohudhuria mahali hapa,waandishi wa habari walijazana kila mmoja akijitahidi kuipata habari hii kwa undani.mahakama ilifurika.

********************************************************************************************************************************
E1 alikuwa katika chumba chake akiwa na kundi la vijana wapatao sita.Vijana wengine 10 walikuwa wamelizunguka jengo hili la kifahari walilokuwa wamelikodi.Walikuwa wakifatilia kwa umakini nyendo za mzee yule,walikuwa wameweka watu wao kila mahali kuhakikisha mzee yule anatii amri zao.Kwao kuipata Package ilimaanisha maana kubwa kwao,package ambayo wamekuwa wakiitafuta kwa muda mrefu sasa.Hawakutaka kuiachia fursa hii muhimu.E1 aliwaita wenzake na kuwagawia majukumu,E2 na E5 hakikisheni mnawareplace ,vijana wanaomfatilia mzee ili kusitokee kosa lolote,E3 hakikisha mawasiliano hayaingiliwi na ripoti ifike kwangu.Mimi nitafanya nini aliuliza E4 ,Be standby tuna kazi ya kuhakikisha tunaipata hiyo package kabla ya kesho alfajiri.

Kazi ya kuzipanga silaha ilimalizika,na kila Eagle kama walivyojiita kwenda katika majukumu waliyokubaliana,watu hawa wote walikuwa wasomi wa shahada ya juu,katika vyuo vikuu mbalimbali.Waliungana na walikuwa kama ndugu wakizifanya kazi walizokubaliana bila kusita,Walikuwa kama ndugu.Waliwashawishi na wengine kujiunga nao, wanafunzi hawa waliitwa Eaglets waliotakiwa kupitia mafunzo ya kimbinu kwa muda wa wiki 12,sawasawa na kipindi ambacho ndege Eagle huhitaji ili kuota manyoya.Eaglets walikuwa wakishirikiana na Eagles wakubwa nao wakipewa namba kulingana na seniority.Kikundi hiki kilikuwa hatari zaidi kwakuwa kilihusisha wataalamu wa kila nyanja.Kwanzia kompyuta,mawasiliano,udaktari,uinjinia,na fani zingine mbalimbali.Waliogopeka kwani hawakuwahi kushindwa katika mission yoyote waliyoipanga.

E1,we have an emergency,i repeat we have an emergency.Ilisikika sauti ya kiongozi wa Eaglet,aliyekabidhiwa jukumu la kufatilia nyendo za mzee yule.Alikuwa ameona kitendo kisicho cha kawaida,naam mzee yule alitwaliwa katika gari nyeusi na kuendesha kwa kasi kuelekea kusikojulikana.E1 aliita kikosi chake kikutane kwa dharura,ili kujadili tukio hili la ghafla.Katika uwanja wa intelijensia ni kosa kukurupuka,na madhara yake huwa makubwa.Eagles walijiamini na kuwaachia Eaglets jukumu la kufatilia nyendo za mzee yule lakini waligundua muda huu kuwa walikurupuka,katika kulifanya hili.Hawakuwa wamefanya uchunguzi wa kutosha kuwajua maadui wa mzee huyu,maana katika vita ni vyema kumjua adui yako,kuwajua maadui zake na marafiki zake ndipo utapanga mashambulizi yako.Uzuri wa kumjua adui wa adui yako ni kukusaidia kufanya urafiki naye,na hivyo kupambana naye bila kutumia nguvu nyingi.Mzee alikuwa ametekwa na kikundi kingine ambacho hawakukijua.Sasa ikaja zamu ya E1 kukifungua kikao hiki,"Eagles and Eaglets,hamjawahi kuniangusha,tumeshindwa kumdhibiti mzee huyu lakini tuna nafasi kubwa ya kuandaa shambulizi kuhakikisha tunaupata mzigo wetu"."Sasa priority ni kumtafuta mzee yule,mipango mingine yote inasitishwa kwa sasa,"Get him alive" aliamuru E1 huku akikifunga kikao hiki.Mara moja magari yakatawanyika,hili likielekea kigamboni,hili likielekea bagamoyo,Lililombeba E1 likielekea kawe na mengine yakizunguka kutafuta uelekeo wa magari yale.

Hatimaye ukaja wakati uliosubiriwa na kila mtu hapa mahakamani,muda wa kuzijua mbichi na mbivu za kesi hii.Jaji alianza kutoa historia fupi ya kesi hii akielezea jinsi maamuzi yalivyofikiwa na hatimaye kutaja kilichosubiriwa na wengi hukumuya kesi hii."Baada ya kujiridhisha na ushahidi kutoka pande zote mbili mahakama imemkuta Nickson,akiwa bila hatia ya mauaji.Hata hivyo amekutwa na hatia ya kutotoa taarifa polisi ambayo ingeweza kusaidia upelelezi.Alitulia kidogo,hivyo kwa sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura ya ishirini,ninamhukumu mshtakiwa adhabu ya miaka saba gerezani".Alimaliza Jaji yule
Kila mtu alisema lake ,wazazi wa Ben hawakuona kama haki ilitendeka,Hali kadhalika ndugu na jamaa wa Nick waliona kaonewa lakini Jaji yule alimalizakesi ile na kutoa nafasi ya rufaa kama upande wowote hautaridhishwa na hukumu ile.

Kijana alilia,sio kwa sababu aliliogopa gereza,hapana alishakaa zaidi ya miezi sita sasa,sio kwa sababu ya biashara yake ya ushonaji ambayo hakujua inaendelea vipi ila kwa sababu ya wazazi wa Ben alitamani Mungu awaonyeshe kilichotokea na kwamba hakuhusika hata kidogo.Ilikuwa huzuni kubwa kwake.

Uelekeo wa magari mengine ulibadilishwa naam,waligundua uwepo wa idadi kubwa ya walinzi katika jumba hili,Kwa sasa lengo halikuwa kupigana bali ni kumuokoa mzee yule ili awape Package ambayo ilikuwa kipaumbele chao.Waliamua kuingia kivingine kabisa ,kwanza kwa kutumia simu maalum waliyokuwa nayo walijitambulisha kama askari maalum wa kikosi cha zimamoto waliokuja kuangalia miundmbinu ya kisima cha kuzima moto.kilichokuwa katika jengo lile.Msafara huu uliongozwa na E2 na kwa weledi mkubwa wakiwa na sare zao wakawahadaa walinzi na kuingia katika jengo lile.

Je watafanikiwa kumuokoa mzee yule,je ni nani aliye nyuma ya mpango ule wa kumteka ? Tukutane sehemu ijayo heri ya krismasi na mwaka mpya ,TUKUMBUKANE
 
SEHEMU YA KUMI NA MOJA
S
arah alikuwa katika lindi la mawazo,alikuwa njiapanda akishindwa kuamua aende ulaya kuonana na Sir McAllison ama abaki nchini kuendelea na kesi ya Nick.Kimaslahi safari ya ulaya ilikuwa kila kitu,Hata katika taaluma yake ya sheria ilikuwa na maana kubwa maana kufanya kazi na kampuni hii kubwa lilikuwa ni tamanio la kila muhitimu wa sheria.Aliendelea kuwaza na kuwazua,mara hii akiyakumbuka maneno ya secretary wa Sir McAllison,ukishindwa kufika nchini wiki ijayo hutapata nafasi nyingine ya kuonana na mzee huyu.Alimhurumia rafiki yake Nick,kesi yake ilikuwa ikimtegemea ,aliwaza kuwaachia ofisi yake waishughulikie lakini hakuona sababu ya kufanya hivyo.Akaamua kuchagua

Ndiyo-Kuchagua ni sifa kubwa aliyopewa mwanadamu,kila wakati mwanadamu hulazimika ama kulaazimishwa kufanya uchaguzi,achilia mbali chaguzi z kisiasa,za mavazi kabatini,chaguzi za kula chakula kipi,chaguzi za nani wa kuongea naye na nini cha kuongea naye,chaguzi za mahali pa kuishi n.k.Chaguzi hizi zimeanza kutoka enzi zamababu wakati fulani Adam alitakiwa kuchagua kati ya matunda mengine na tunda la mti wa katikati,Alichagua la mti wa katikati.Hivyo upatapo fursa hii ni vyema kuchagua kitakachokufaa ili uchaguzi wako uwe na maffanikio,haijalishi unapitia lipi CHAGUA.Ulivyo leo ni kwa sababu ya machaguo uliyochagua maishani.

Sarah alichagua kubaki nchini,ili apate muda mzuri wa kumsaidia Nick,kijana asiye na hatia ambaye alikuwa anateseka gerezani.Aliamua kuyaacha mengine yapite,ili mradi Nick atoke gerezani.Hiyo ndiyo furaha aliyokuwa akiingojea,alijiandaa kuelekea mahakamani kusikiliza kesi hii ya kijana Nick.

GEREZANI
Kijana Nick alipanda katika gari tayari kwa kuelekea,mahakamani ,hatima ya maisha yake aliiacha mikononi mwa Mungu.Maisha tunajifunza vipya kila siku,hapa gerezani kijana Nick alikuwa amejifunza kula kwa muda uliopangwa na gereza,na kula pasi nakubagua chakula,alijifunza pia kuwa sio wote waliopo mahali hapa walikuwa ni wakosaji.Kutokana na simulizi mbalimbali alizozipata hapa,wengine kwa kusingiziwa kesi mbalimbali na wengine kucheleweshewa kesi zao pasipo sababu za msingi.Aliyazoea maisha haya na kuyaona kama nafasi nyingine ya kujifunza,kwa leo alimuomba Mungu ombi moja tu Haki itendeke.

Watu wengi walihudhuria mahakamani hapo,ukiacha mawakili,na mahakimu,ndugu mbalimbali waliohudhuria mahali hapa,waandishi wa habari walijazana kila mmoja akijitahidi kuipata habari hii kwa undani.mahakama ilifurika.

********************************************************************************************************************************
E1 alikuwa katika chumba chake akiwa na kundi la vijana wapatao sita.Vijana wengine 10 walikuwa wamelizunguka jengo hili la kifahari walilokuwa wamelikodi.Walikuwa wakifatilia kwa umakini nyendo za mzee yule,walikuwa wameweka watu wao kila mahali kuhakikisha mzee yule anatii amri zao.Kwao kuipata Package ilimaanisha maana kubwa kwao,package ambayo wamekuwa wakiitafuta kwa muda mrefu sasa.Hawakutaka kuiachia fursa hii muhimu.E1 aliwaita wenzake na kuwagawia majukumu,E2 na E5 hakikisheni mnawareplace ,vijana wanaomfatilia mzee ili kusitokee kosa lolote,E3 hakikisha mawasiliano hayaingiliwi na ripoti ifike kwangu.Mimi nitafanya nini aliuliza E4 ,Be standby tuna kazi ya kuhakikisha tunaipata hiyo package kabla ya kesho alfajiri.

Kazi ya kuzipanga silaha ilimalizika,na kila Eagle kama walivyojiita kwenda katika majukumu waliyokubaliana,watu hawa wote walikuwa wasomi wa shahada ya juu,katika vyuo vikuu mbalimbali.Waliungana na walikuwa kama ndugu wakizifanya kazi walizokubaliana bila kusita,Walikuwa kama ndugu.Waliwashawishi na wengine kujiunga nao, wanafunzi hawa waliitwa Eaglets waliotakiwa kupitia mafunzo ya kimbinu kwa muda wa wiki 12,sawasawa na kipindi ambacho ndege Eagle huhitaji ili kuota manyoya.Eaglets walikuwa wakishirikiana na Eagles wakubwa nao wakipewa namba kulingana na seniority.Kikundi hiki kilikuwa hatari zaidi kwakuwa kilihusisha wataalamu wa kila nyanja.Kwanzia kompyuta,mawasiliano,udaktari,uinjinia,na fani zingine mbalimbali.Waliogopeka kwani hawakuwahi kushindwa katika mission yoyote waliyoipanga.

E1,we have an emergency,i repeat we have an emergency.Ilisikika sauti ya kiongozi wa Eaglet,aliyekabidhiwa jukumu la kufatilia nyendo za mzee yule.Alikuwa ameona kitendo kisicho cha kawaida,naam mzee yule alitwaliwa katika gari nyeusi na kuendesha kwa kasi kuelekea kusikojulikana.E1 aliita kikosi chake kikutane kwa dharura,ili kujadili tukio hili la ghafla.Katika uwanja wa intelijensia ni kosa kukurupuka,na madhara yake huwa makubwa.Eagles walijiamini na kuwaachia Eaglets jukumu la kufatilia nyendo za mzee yule lakini waligundua muda huu kuwa walikurupuka,katika kulifanya hili.Hawakuwa wamefanya uchunguzi wa kutosha kuwajua maadui wa mzee huyu,maana katika vita ni vyema kumjua adui yako,kuwajua maadui zake na marafiki zake ndipo utapanga mashambulizi yako.Uzuri wa kumjua adui wa adui yako ni kukusaidia kufanya urafiki naye,na hivyo kupambana naye bila kutumia nguvu nyingi.Mzee alikuwa ametekwa na kikundi kingine ambacho hawakukijua.Sasa ikaja zamu ya E1 kukifungua kikao hiki,"Eagles and Eaglets,hamjawahi kuniangusha,tumeshindwa kumdhibiti mzee huyu lakini tuna nafasi kubwa ya kuandaa shambulizi kuhakikisha tunaupata mzigo wetu"."Sasa priority ni kumtafuta mzee yule,mipango mingine yote inasitishwa kwa sasa,"Get him alive" aliamuru E1 huku akikifunga kikao hiki.Mara moja magari yakatawanyika,hili likielekea kigamboni,hili likielekea bagamoyo,Lililombeba E1 likielekea kawe na mengine yakizunguka kutafuta uelekeo wa magari yale.

Hatimaye ukaja wakati uliosubiriwa na kila mtu hapa mahakamani,muda wa kuzijua mbichi na mbivu za kesi hii.Jaji alianza kutoa historia fupi ya kesi hii akielezea jinsi maamuzi yalivyofikiwa na hatimaye kutaja kilichosubiriwa na wengi hukumuya kesi hii."Baada ya kujiridhisha na ushahidi kutoka pande zote mbili mahakama imemkuta Nickson,akiwa bila hatia ya mauaji.Hata hivyo amekutwa na hatia ya kutotoa taarifa polisi ambayo ingeweza kusaidia upelelezi.Alitulia kidogo,hivyo kwa sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura ya ishirini,ninamhukumu mshtakiwa adhabu ya miaka saba gerezani".Alimaliza Jaji yule
Kila mtu alisema lake ,wazazi wa Ben hawakuona kama haki ilitendeka,Hali kadhalika ndugu na jamaa wa Nick waliona kaonewa lakini Jaji yule alimalizakesi ile na kutoa nafasi ya rufaa kama upande wowote hautaridhishwa na hukumu ile.

Kijana alilia,sio kwa sababu aliliogopa gereza,hapana alishakaa zaidi ya miezi sita sasa,sio kwa sababu ya biashara yake ya ushonaji ambayo hakujua inaendelea vipi ila kwa sababu ya wazazi wa Ben alitamani Mungu awaonyeshe kilichotokea na kwamba hakuhusika hata kidogo.Ilikuwa huzuni kubwa kwake.

Uelekeo wa magari mengine ulibadilishwa naam,waligundua uwepo wa idadi kubwa ya walinzi katika jumba hili,Kwa sasa lengo halikuwa kupigana bali ni kumuokoa mzee yule ili awape Package ambayo ilikuwa kipaumbele chao.Waliamua kuingia kivingine kabisa ,kwanza kwa kutumia simu maalum waliyokuwa nayo walijitambulisha kama askari maalum wa kikosi cha zimamoto waliokuja kuangalia miundmbinu ya kisima cha kuzima moto.kilichokuwa katika jengo lile.Msafara huu uliongozwa na E2 na kwa weledi mkubwa wakiwa na sare zao wakawahadaa walinzi na kuingia katika jengo lile.

Je watafanikiwa kumuokoa mzee yule,je ni nani aliye nyuma ya mpango ule wa kumteka ? Tukutane sehemu ijayo heri ya krismasi na mwaka mpya ,TUKUMBUKANE
mkuu, naomba mwendelezo basi
 
Samahani wakuu sina PC hivyo natumia napopata nafasi nashusha uzi na tunaendelea,leo tukijaaliwa tutapandisha sehemu inayofuata
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom