RIWAYA; Mapambano

RIWAYA; Mapambano

SEHEMU YA SABA
Leo yalikuwa mazishi Ben,kijana aliyeuawa siku chache zilizopita.Watu wengi walihudhuria kila mmoja akijitahidi kuivaa sura ya huzuni.Sio wanaume,wanawake wote wakiwa wamevalia sare nyeupe tayari kwa kumuaga kijana wao mpendwa,Hata kamanda wa polisi wa wilaya ile alihudhuria na kuahidi kuwatia mbaroni wahalifu huku akiendelea kuiomba halaiki ile kuwa watulivu wakati uchunguzi wa kina ukiendelea.Maneno ambayo waliyatumia kuwafariji waombolezaji.Ilikuwa HUZUNI

Huzuni anayoipata mama kwa kufiwa na mwanae pekee wa kiume,huzuni waliyoipata marafiki kwa kuondokewa na msaada mkubwa kwao katika hali na mali.Huzuni kubwa kwa kijana Nick aliyekuwa gerezani,kwanza kufiwa na rafiki yake wa karibu huku akizuiwa kushiriki mazishi yake na huzuni zaidi kwa kushikiliwa gerezani akituhumiwa kuhusika na mauaji hayo.

Kuna vitu ambavyo ni dhahiri kuwa vitatokea katika maisha,lazima utatokwa jasho ukifanya shughuli fulani,lazima utapumua,lazima utashikwa na usingizi,lazima utahisi njaa na lazima siku moja UTAKUFA.Ndiyo kwakuwa ulizaliwa njia pekee ya kufika mwisho wako ni kufa.Watu hawastaajabishwi na usingizi au njaa,au mwili kutokwa na jasho,lakini mtu akifa kila mmoja huhuzunika,pengine ni kwa sababu tulitegemea aishi milele,au pengine tulitaka akae nasi zaidi lakini huu ndio mwisho wa kila mwenye uhai naam ni kifo.Tukubali au tukatae,kila mmoja kwa wakati wake ataipitia hali hiyo.

Mchungaji na baadhi ya viongozi wa dini waliohudhuria maziko haya waliwaasa watu kumcha Mungu katika siku za maisha yao,wakikumbuka kuwa wapitaji hapa duniani na maneno mengine ilimradi kufariji wafiwa.Watu waliohudhuria walikuwa wakipita kutoa salamu zao za pole kwa familia ile iliyompoteza kijana wao mpendwa.Irene,alikuwepo ,watu mbalimbali kutoka makampuni tofauti walitoa rambirambi zao ,Hata mzee yule alihudhuria!.Alikuwa hapa sio kwa utambulisho wa kificho wa ngozi ya mbwa mwitu,bali kwa utambulisho wa uwazi wa kondoo naam kondoo aliyekuwa alama ya kila upole na huruma eneo hili.Akisaidia na kushauri panapowezekana kutimiza wajibu wa majirani wema na kushiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii.

Upande mwingine kijana alikuwa kwenye basi la wafungwa akielekea mahakamani.Wakili wake Sarah alikuwa kashawahi mahakamani akisubiri muda utimie atoke ndani ya gari lake,kuianza siku hii iliyokuwa na umuhimu katika maisha yake ya uwakili.Kesi nyingi alizowahi kushiriki alikuwa akiwatetea walalamikaji hasa hasa wanawake wanaonyanyaswa na waume zao,ama watoto waliobakwa lakini leo hii alikuwa wakili akijaribu kuishawishi mahakama na pengine ulimwengu wa kisheria kuwa mteja wake hakuwa na hatia.

Kijana alikuwa akiomba kimyakimya ,maombi yasiyoweza kusikiwa na yeyote pengine tuyaite mawazo,naam hii ndio njia iliyowekwa ya kuwasiliana na nguvu zilizo nje ya uwezonwetu wa kufikiri ,Alikuwa akimuomba Mungu amsaidie.

Hatimaye ukaja ule wakati uliosubiriwa na kila mtu katika viunga hivi vya mahakama.Vilivyosubiriwa na majaji,mawakili,mshtakiwa,ofisi ya mwendesha mashitaka,watazamaji na hata waandishi wa habari waliokuwa wakifuatilia mwenendo wa kesi hii.

Mwendesha mashitaka alisoma mashitka mbalimbali kwa kijana huyu ambayo idadi yake ingeweza kufikia tisa,akiiwakilisha Jamhuri katika kesi ya mauaji ya ndugu Ben,na baadaye kuanza kumuhoji shahidi aliyemleta mbele ya mahakama.Ni kawaida kwa upande wa mashitaka kumuhoji shahidi kabla ya kuhojiwa na upande wa mlalamikiwa.

Hatimaye ikaja zamu ya Sarah, LLM graduate kutoka viunga vya New Haven,Connecticut nchini Marekani kilipo chuo kikuu cha Yale kilichoanzishwa mwaka 1824.Kuithibitishia mahakama kuwa yanayosemwa na upande wa mashitaka hayakuwa na mashiko.
Chuo hiki cha Yale huchukua idadi ya wanafunzi 200 tu kwa mwaka idadi ndogo kati ya vyuo vingi vya taaluma ya sheria,pia kibaya zaidi ni kuwa kinachukua wanafunzi kutoka mataifa mbalimbali.Hivyo binti huyu Sarah alikuwa muhitimu wa kwanza kutoka Tanzania katika chuo hiki.

Sarah alianza kwa kusimulia kesi ya Lindbergh ya mwaka 1932,ambapo mtuhumiwa aliendesha gari na kulipaki likiwa na mwili wa marehemu na hatimaye mahakama ilikuja kubaini kuwa ndiye muuaji.Katika kesi hii,naiomba mahakama ifute mashitaka yake dhidi ya mteja wangu kwa sababu hana hatia,kwanza gari liliotumika kumtelekeza marehemu lilipotea na loss report yake nitawapa kama ushahidi,na pia ushahidi wa marehemu kupigiwa simu na mteja wangu hautoshi kuthibitisha kuwa alihusika katika mauaji yake kwa kuwa marehemu alipokea simu nyingi siku ya tukio,nyingine zikiwa hazijasajiliwa.Alimaliza binti yule kwa ufupi kumuachia muda jaji aliyekuwa akiisikiliza kesi ile kuendelea.

Jaji huyu mzoefu alishauriana na jopo la majaji mahakamani pale na kufikia maamuzi ya kuita ushahidi upande wa utetezi na kesi ikaahirishwa kwa mara nyingine.

Magari mbalimbali yalianza kuondoka eneo la mahakama,mojawapo likiwa gari la Sarah,kwa kuwa alikuwa na muda alikuwa amemuomba Irene wakutane katika mkahawa maarufu kwa chakula chenye asili ya Brazil.Sarah alitangulia kufika akaagiza Brazilian lemonade,kinywaji cha asili ya Brazil alichopendelea.Akamsubiri Irene aweze kuja.

Ofisini kazi ziliendelea kama ilivyo ada yake.Leo wageni wengi walifika mahali hapo mmoja wao akiwa Brian mchumba wa Irene mwanaume huyu aliyempenda Irene alikuwa hapa dukani kwao kumletea ua kubwa zuri na ujumbe wenye maneno matamu ambayo yalilenga kumuomba Irene ajifikirie upya kuifuta kauli aliyokwisha kuitoa kauli ambayoo huweka uadui wa pande mbili za wapendanao NAOMBA TUACHANE.Alikuwa kavalia jeans maridadi na shati la rangi ya blue lililokunjwa vyema kuruhusu mikono yake yenye haiba ya urijali kuonekana.

Brian na Irene walikuwa wakipendana sana Irene msaidizi wa Nick dukani na Brian ,kijana ambaye watu humuita "asiye na kazi".Binafsi huwa sikubaliani na neno hili ,maana ya kazi ni shughuli ya kumuingizia mtu kipato,je ukiifanya shughuli hiyo na usiingize kipato utakuwa hauna kazi? Labda hujanielewa,muosha magari au mfanya usafi wa bustani akilipwa tutasema amejiajiri mwenyewe vipi mtu akiliosha gari la mpenzi wake bila kulipwa chochote,ni sahihi kusema hana kazi au pengine kuosha vyombo bila kulipwa je nako ni kukosa kazi? kijana huyu alikuwa akijitahidi kuweka mazingira,katika hali ya usafi,kuliosha gari la mchumba wake Irene na kuzifanya shughuli nyingi mbali na zile zinazohusu mapenzi.

Pamoja na haya yote uhusiano wa Irene na Brian ulikuwa ukilega kila siku,kwa sababu Irene kama walivyo wanawake wengi wa kisasa alikuwa ameanza kuendeshwa na tamaa yake ya kuwa na mwanaume mwenye fedha.Sijui ni fedha kiasi gani-Lakini najua kuwa anatakiwa kuwa na walau gari moja na kuishi maisha ambayo wanawake hawa wanayapenda,ya kujionyesha ,akinywa Hennesy au akiwa Serena,akienda Airport hata kumsindikiza rafiki yake lazima apige picha.Naam ndiyo wanaume wanaowataka wanawake wengi wa sasa.Kwao hawajali kwamba pesa hiyo unaitoa wapi,gari hilo ni mkopo au la kuazima,ilimradi uliendeshe tu tayari umewaweka katika himaya yako.Hata marafiki zake wa karibu walimpa mawazo ya kuachana na Brian.

Ni sahihi,Brian hakuwa na ajira ya kudumu lakini kijana huyu alijitoa kwa moyo wote kuonyesha mapenzi ya dhati kwa Irene.Walikuwa na mipango na ahadi nyingi walizokwishakuahidiana ,Ahadi ambazo zilianza kufifia baada ya kutongozwa na Ben.

Wanasema,"Talk about the devil and he'll appear" ,Ben alikuwa akiingia kwa kasi katika mahusiano haya yaliyoanza kulega,Kwanza alikataa,ili kuvuta hamasa ya Ben.Kama ilivyo imani ya vijana wengi kuwa ,Rome haikujengwa kwa siku moja,yaani wanathamini sana mwanamke anayechukua muda mrefu kuwajibu,akisema anajifikiria,na pengine kutafuta njia nzuri ya kuzipata fedha za kijana huyu.Ben alikuwa "DEVIL" kwenye uchumba huu.

Kuna watu wana matatizo mbalimbali,tatizo la Brian wakati huu lilikuwa ni wasiwasi,wasiwasi wa lini atapata kazi naye ajitegemee na kumridhisha Irene,wasiwasi wa Irene kuwa na mwanaume mwingine zaidi yake na pengine kubwa zaidi wasiwasi wa kutofunga ndoa na mwanamke huyu aliyempenda sana.

Wasiwasi huu ulikuwa unasababishwa na tabia mpya za Irene katika wiki hii,Alhamisi usiku kaenda kwenye sherehe ya kuzaliwa ya rafiki yake.Sehemu linapofanyika tukio hilililitosha kumpa wasiwasi, night club,.Lakini wasiwasi mwingine ulikuwa juu ya kuongozana naye,na jibu la Irene lilimdhihirishia kuwa ataondoka pekeyake.Irene alirudi saa nane usiku......

Moja ya vitu wanavyokumbana navyo wanaume wasio na kazi katika mahusiano yao ni kukosa uhuru wa kuhoji au wa kuzungumza,kwani mazungumzo haya hata kama hayaonyeshi hufunikwa na kujishusha kwa upande mmoja.ndivyo kijana huyu alivyokuwa akijishusha kwa binti Irene.Hata baada ya Irene kutorejea nyumbani jana usiku na kurudi asubuhi yake ,kijana huyu alimuuliza "uko salama"?,swali ambalo halikuwa la msingi,badala ya kuuliza ,like most Africans,ULIKUWA WAPI?

Maisha ya Brian yalitawaliwa na hofu,ya kuikabili hali yake.Na kuamua kujificha katika mapenzi haya na mtu ambaye hakuonekana kulithamini Penzi hilo.Alishindwa hata kuithamini kauli maarufu kwa watu waoga isemayo,In Life Don't be afraid,and if youre afraid about anything don't do it".Aliipoteza kila siku akisubiri kumpata Irene waliyedumu naye kwa miaka miwili sasa,Kipato cha Irene kilikuwa kinaanza kudhihirika na kuibadili hata tabia yake.

Sasa Irene alimuangalia tena kijana huyu,aliyekuwa akimsihi warudiane.Irene alimjibu kuwa ana kazi nyingi na hivyo amtafute jioni yake,kijana huyu alizidi kumsihi na hata kulia,Lakini Irene sasa aliondoka ofisini kwake na kuondoka tayari kwa kuonana na Sarah.

Je Irene yuko sahihi kumuacha mchumba wake ofisini?,je ni mazungumzo yapi yataendelea kati ya Sarah na Irene? USIKOSE SEHEMU YA NANE.
 
SEHEMU YA NANE
Irene alishuka na katika gari lake na kuanza kuzipandisha ngazi fupi za mkahawa huu maarufu kwa chakula chenye asili ya Brazil.Aliangaza macho yake kulia na kushoto,pembeni kabisa ya bustani iliyokuwa imezunguka mkahawa huu alimuona Sarah muda huu akiwa amejiinamia.Alitembea taratibu kumfuata alipokaa,na kumuita Sarah.

"Sarah,Sarah"Aliita Irene

Sarah,aliyekuwa katika lindi la mawazo aligutuliwa na sauti hii ya Irene.Aliinuka na kupiga mafunda kadhaa ya kinywaji chake alichokuwa ameagiza,na kuinua uso wake kumuangalia Irene.Baada ya kukaa,Sarah akaendelea,"Nimekuita hapa niweze kujua hali ya biashara inaendeleaje kwa kipindi hiki ambacho Nick hayupo kazini.Na pia kunieleza upande wako katika habari hizi za mauaji ya Ben ili nijue namna ya kumsaidia Nick".Alimaliza Sarah.

Irene alionekana kuwa na wasiwasi ,Japo alijitahidi kuificha hofu ile aliyokuwa nayo lakini ilidhihirika wazi.Kuhusu kazi order zinaendelea vizuri tu,nimefanikiwa kuwashawishi HYATT,Tuendelee na mkataba kama ilivyokubaliwa awali.Alinyamaza kidogo ,kisha kuhusu hili la mauaji ya Ben siku yalipotokea taarifa nilizipata kazini,hivyo sijui lolote.

Kuna njia rahisi ya kujua uongo,kwa miaka mingi wanasayansi wamethibitisha kuwa uongo ni kutoa sababu isiyo katika kumbukumbu za ubongo hivyo huulazimu ubongo kufikiria zaidi.Hivyo sauti ya mtu anayedanganya,macho yake ,hata vidole kwa baadhi ya watu huweza kuonyesha dhahiri mshtuko anaokuwa nao.Irene alijua fika siri ya mauaji ya Ben japo hakujua sababu iliyonyuma yake lakini,aliamua kuificha kwa shinikizo la mzee yulealiyemtishia kuwa hatarini endapo atajaribu kuusema ukweli.

"Irene unaumwa"? Aliuliza Sarah,
"Hapana,Sarah naumia tu jinsi Ben alivyouawa bila hatia" alijibu Irene akijifuta machozi

Sarah alimtuliza Irene,na kumruhusu aende kupumzika na kumwahidi kumpigia baadaye.

Kijana Brian,alikaa hadi kuchoka pale ofisini kwa Irene,japo AC ya chumba hiki ilikuwa ikiifanya kazi yake vizuri,Jasho jembamba lilikuwa likimtoka,alikuwa haamini kinachomtokea,Irene kumuacha-HAIWEZEKANI-alijisemea.Aliondoka ofisini na Ua lake kubwa,alilolinunua maalum kwa ajili ya mchumba wake Irene,ili kujitahidi kumkumbusha kuwa maisha ya mahusiano yanahitaji uvumilivu lakini binti huyu alionekana kubadilika,sio badiliko la kiumbo ambalo linaweza kurejea katika hali ya kawaida bali la kikemikali.Kemikali hizi zilikuwa zinamwathiri Brian,Alikuwa akilia tu,kijana huyu alikuwa kaupoteza uchangamfu wake kabisa,alihuzunika.

Brian aliamua kurudi nyumbani kwa Irene,alikuwa nafunguo hivyo aliingia ndani,sauti ya mziki ilikuwa ikitoka chumbani kwa Irene,alikuwa akisikia miguno hafifu iliyoambatana na wimbo ule wa mahadhi ya Blues.Haikumuhitaji muhitimu wa shahada ya uzamilivu katika mahusiano,kugundua kwamba zilikuwa sauti za kimapenzi,Chumbani kwao.Ama kweli Irene alikuwa kavuka mipaka,aliutamani ujasiri,sio wa kumuua simba ujasiri wa kusimama mita moja nyuma ya mlango huku ukisikia sauti za miguno ya kidume kitandani kwako ,na mwanamke unayemthamini pengine huu ndio ujasiri alioutaka kijana Brian.

Alifungua mlango na kuingia ndani ndipo alipomkuta mchumba wake akicheza ngoma mfano wa zile za kingoni juu ya Sura ambayo hakuitambua mara moja,Aliinuka na kumkaba mzee yule aliyeonekana kumshangaa kijana Brian.

"wewe nani unakuja kulala nyumbani kwangu" Alifoka Brian
"Kijana sipendi kabisa kuvurugiwa starehe zangu,kama hautaondoka mara moja nitaita polisi waje wakushughulikie"Alisema mzee yule akitabasamu,mzee sasa alionekana kumgeukia Irene na kumuuliza,huyu ni nani?

"my EX,alijibu Irene na kumsogelea mzee yule wakumbatiane.Shuka alilokuwa amejifunika liliuacha mwili wake laini na kudondoka chini.Kijana Brian alikuwa akishuhudia ukatili mkubwa kuwahi kutokea.Pengine ushawahi kusikia mtu akimuua mpenzi wake kwa kinachoitwa "wivu wa kimapenzi".Japo mauaji ni mauaji,ila saikolojia ya watu hawa huathirika.Huchukua maamuzi ya haraka ambayo huathiri maisha yao.

"Kijana,niliambiwa unaitwa Brian.Chukua hii pesa nenda kijijini kamsalimie mama yako" Alimjibu mzee yule huku akimpa laki mbili,Brian,hakuonekana kusikiliza maneno ya mzee yule na badala yake aliamua kuondoka katika nyumba ile.Alilichukua begi lake na kubeba nguo zake na viatu na kuondoka,Alikuwa akilia sana.Machozi yalimfanya kuonekana kama mvuta bangi mashuhuri.Kijana aliondoka kwenye mitaa ile.

Binadamu tuna asili ya kutoridhika,hii ndio hulka yetu.Lakini inawezekana pia kuna wengine hujitahidi kuepukana na hulka hii lakini ndio utamaduni wetu.Hata ungeutoa moyo wako na kuwagawia watu waule kuna mtu atasema hauna chumvi ya kutosha,hivyo mojawapo ya maamuzi ya mabaya kabisa ni kujaribu kuwaridhisha watu wote.Kuna wakati kijana huyu alijiuliza hivi huwezi kuwa masikini ukawa na furaha?,Hivi kwa Irene mapenzi yangu hayakuwa na thamani yoyote?alijiuliza kijana huyu huku akizidi kulia.Mbona babu yangu na bibi wanaishi kwa furaha kijijini ilhali,hawana gari wala nyumba ya kisasa?Kwanini Irene anashindwa kuelewa jinsi gani ninavyompenda? kijana huyu aliendelea kujiuliza maswali mengi.

Sarah aliamua,kwenda mwenyewe ofisini kwa Nick kujiridhisha na utendaji kazi maeneo yale,Shughuli ziliendelea kama kawaida ila aliweza kugundua kukosekana kwa kitu katika wafanyakai wale.FURAHA,japo walijitahidi kuonyesha furaha,nyuso zao zilionyesha wazi kutokuwa na furaha,walimkumbuka kijana yule aliyewajali na kuwathamini aliyeshirikiana nao katika kila kazi.Walimkumbuka sana.Sarah alizungumza na baadhi ya wafanyakazi na kuwapa uelekeo wa kesi ile na kuwafariji kuwa waendelee kumuombea Nick na wapatapo muda wasiache kumtembelea wapatapo nafasi.

Sarah,alielekea nyumbani kwake kujipumzisha na kujiandaa na siku inayofuata.Alifika nyumbani kwake na kubadili nguo zake,sasa alivalia kitenge alichokuwa amejifunga.Alikuwa anajisomea,ulivyoingia ujumbe kwenye simu yake,Hakuusikia wakati ukiingia kwani alielekea katika bafu lake lililokatika chumba chake cha kulala.Baada ya kurejea aliishika simu yake na ndipo akaishika simu yake na kuangalia ujumbe ule.

Oh,My God aliruka juu na kufurahi baada ya kuusoma ujumbe ule,

Ni ujumbe gani katumiwa,je mshiriki gani unapenda au huzipendi tabia zake usiache kucomment tukutane sehemu ijayo
 
Nyandaad upo kamanda ahsante sana tupia nyingine tusonge mbele
 
Mlioniahidi jamani ,mnikumbuke kijana wenu na wanaojiskia kutoa chochote namba yangu ni 0785386036.Sehemu ya Tisa soon
 
SEHEMU YA TISA
Simu ya Sarah ilikuwa ikiita kwa sauti aliinua mkoba wake uliokuwa juu ya meza kuitoa simu yake,akaangalia kioo ili kuliona jina la mpigaji......

MSHANGAO-Sarah alibaki ameduwaa asijue la kufanya.

Ulikuwa ni mshangao uliochanganyika na furaha aliyokuwa nayo.Kuna jambo ambalo hutokea mtu asiamini limetokea vipi,kwa Sarah namba hii yenye code number +44 Ilikuwa na maana kubwa kwake.Alikuwa ni Sir Walters McAllison mmiliki wa kampuni maarufu ya bidhaa za kielektroniki kutoka Uingereza.Sarah alitamani na kuthubutu mara nyingi,kuwa mwanasheria wa kampuni hii lakini mara zote hakuweza kukubaliwa.Sio kwa sababu walikuwa na mashaka naye au taaluma yake ila kwa sababu ya ugumu wa mzee huyu wa cheocha Sir.Mzee Walters,alikuwa mgumu sana kuonana nae kama sio kupata namba zake za simu.

Mshangao huu ulimduwaza mpaka simu ikakata,Alikuwa akifikiria alivyotumia pesa zote alizolipwa katika kesi yake ya kwanza ili apate tiketi za ndege kujaribu kuonana na mzee Walters.Hakufanikiwa na akaamua kuomba walau namba yake ya simu,pia aligonga mwamba,alijaribu tena na tena hakufanikiwa.Hakukata tamaa aliamua kupanda ndege nyingine hadi nchini ufaransa katika jiji la Monaco kujaribu kupata mawasiliano ya mzee huyu,siku hii alimpata msaidizi wake aliyemkatisha tamaa.Alimwambia Simu ya mzee Walters ina namba tatu,moja ya mke wake,ya pili ya bintiye na yatatu ya waziri mkuu wa Uingereza.Hata yeye mlinzi mkuu wa mzee huyu hakuwa na namba zake za simu.Watu wote waliojaribu kumpigia mzee Walters ilikuwa lazima wapitie simu yake ya ofisini na kama kuna dharura yoyote ndipo huelekezwa kwa mzee Walters.


Mlinzi huyu alimuonea huruma Sarah akampa namba za binti yake ikawa bahati yake Sarah.Binti huyu wa Mzee Walters ndiye akaja kumpa namba za baba yake.Lakini akaambiwa habari zilizomkatisha tamaa zaidi.Mzee Walters hapigiwi simu akikuhitaji atakupigia.Hivyo leo ulikuwa mwaka wa nne na miezi tisa,na siku ishirini na saba baada ya tarehe ile jina la Sir Walters kwenye kioo chake alikaribia kuzimia kwa furaha kubwa aliyokuwa nayo.

Akaamua kuipokea,"Hello,Sarah",Sauti nzito ya mzee huyu ilimshtua .I am offering you an opportunity to be my legal representative in one of my cases,My personal secretary will call you for further information".Alimaliza na kukata simu yake bila ya Sarah kujibu,neno pekee alilolitamka ni "YES SIR".

STENDI YA MABASI -UBUNGO
Kijana Brian alilivuta begi lake dogo na kulipandisha katika Basi lililokuwa linaelekea mjini Bariadi,mkoani Simiyu.Huko angepanda lingine tayari kwa kwenda kijijini Ikungu yalipo makazi ya babu na bibi yake.Hakutaka kwenda nyumbani kwao jijini Mwanza ila aliamua kwenda kwa babu yake akiamini itakuwa ni sehemu salama ya kutuliza akili yake kwa kipindi hiki.

Maisha hutufunza mambo mengii,lakini mafunzo haya hutuachia maumivu makubwa.Ili kuyatumia mafunzo haya kufanikiwa tunatakiwa kubadilika,lakini mabadiliko huwa tunayapinga kwani yatabadilisha kila kitu tulichokizoea.Brian aliamua kuanza maisha upya ili ayasahau yaliyojitokeza huko nyuma.Safari iliendelea wakiivuka mikoa ya morogoro na Dodoma,Singida na Tabora,Shinyanga na Mwanza na hatimaye kama kila safari inavyofikia mwisho walifika mjini Bariadi.Alilazimika kulala pale na kusubiri hadi kesho yake ili kupata gari la kwenda kijijini kwa Babu yake.Alifika nyumbani kwa babu yake majira ya asubuhi na kupokelewa kwa shangwe na furaha.Mzee huyu alikuwa na busara nyingi,japo hakufanikiwa kwenda shule lakini alijua mambo mengi na alikuwa maarufu katika kijiji kile.

Baada ya salamu ,zikaanza mbio za hapa na pale kufukuza kitoweo rasmi cha mgeni wa kiafrika,Kuku.Sehemu nyingi za nchi yetu hasahasa maeneo ya vijijini mgeni hukaribishwa kwa kuchinjiwa kuku.Kijana alipewa majukumu hayo akiwasaidia Babu na bibi yake kumkamata.Japo lilikuwa saa la pili tu kwanzia afike mahali hapa aliiona furaha na amani ikiichukua nafasi ya huzuni aliyokuwa nayo.Hadithi za hapa na pale za mzee huyu machachari zilimsahaulisha hata maswahibu aliyokutana nayo.Jikoni nako bibi aliendelea na upishi,harufu nzuri iliwafikia wanaume wawili waliokuwa waki'yajenga'.Kwa kijana Brian ilikuwa ni zaidi ya siku kwake alitamani hata siku zote angekuwa na babu yake.

Watu huamini,au wamelazimishwa kuamini kuwa hela ndiyo kila kitu,hakunatena nafasi ya upendo,kuthaminiana imani,uaminifu.Hata makazini mtu akitumia matumizi inavyopaswa ataitwa anajipendekeza huku anayeiba akijiita anapiga 'dili' bila kujua kuwa bosi wake akifilisika atakosa kazi.Baadhi ya watu wachache wanatambua kuwa hela ipo kwa ajili ya kutimiza mahitaji yao lakini sio kila kitu.Babu yake aliyekuwa na miaka 75 sasa,alikuwa akionekana kama kijana wa miaka 40.Alikuwa mtu mwenye furaha wakati wake,nyumba yake iliyotengenezwa kwa miti imara,kitanda cha wastani ,zizi lenye ng'ombe wengi kiasi,akiishi na mjukuu wake mmoja tu hapa kijijini.Alikuwa na amani na kila mtu akiwa pia kiongozi wa kijiji hiki kwa miaka 15 sasa akipita mara zote bila kupingwa,alikuwa mtu wa watu.

Ukafika wakati wa jioni,kijana alimsaidia babu yake kuwasha moto kwa kutumia kinyesi cha ng'ombe,na baada ya chakula walipiga stori wakiota moto huu.Mzee huyu alimuuliza kijana swali fikirishi,"unajiona wapi katika miaka ijayo"?.Swali hili lililenga kupima ufahamu wa kijana wake.Kijana Brian,hakujua ajibu nini,Japo alikuwa muhitimu wa shahada ya masomo ya Biashara lakini hakujua atakuwa nani miaka ijayo,kwanini?.Kwa sababu hakuwa na uhakika ataajiriwa kama nani kwake yeye aliwaza ije siku apate ajira na hivyo alimjibu mzee yule sijui Babu,Sijui hata nifanye nini.

Babu alijiweka vizuri kwenye kiti na kumtazama kijana Brian,kisha akamwambia."Wakoloni walivyokuja ,walitukuta tukiwa na mfumo wetu wa maisha,waliingiza elimu yao na kuitumia kujinufaisha".Wakati huo watu walilima mazao ya chakula yaliyotosheleza mahitaji yao,walikuwa na elimu iliyosaidia kutatua matatizo yao,Mfano kijana wa kiume alifundishwa ujenzi wa nyumba ya kuishi.Au uhunzi wa kutengeneza,silaha na zana za kutumia katika shughuli mbalimbali.Hivyo,elimu kama haijatumika kusaidia matatizo ya jamii haina maana yoyote.Maneno ya mzee huyu wa miaka 75 yalimuingia barabara kijana Brian.Alizidi kumpenda mzee yule hata akathubutu kumfananisha na gwiji la sayansi Albert Einstein aliyewahi kusema "Kama huwezi kumueleza mtoto wa miaka sita akakuelewa basi hujui hicho unachokieleza".Japo mzee huyu hakusoma lakini aliweza kuiona hekima yake.Aliyahifadhi maneno ya mzee yule.

COLLOSEUM HOTEL
Leo Irene alikuwa na mzee wake,aliyempa "all of her" usiku wa jana,mahali hapa alikuwa akipata chakula cha mchana.Alikuwa amechangamka kwa mara ya kwanza maishani mwake akifanikiwa kunywa glass nzima ya Smirnoff X1.Alikuwa kavalia kaptula fupi na blouse iliyoonyesha sehemu kubwa ya kifua chake.Alionekana kupendeza sana.Wanawake wamejaaliwa upendo,lakini baadh yao hawajui hata mtu wa kupenda,kuna hulka ya watu kuona kilicho mbali kama chenye thamani zaidi kuliko ulichonacho ndiyo iliyomsumbua Irene,akiona Brian hakuwa na maaana yoyote kwake.Kwake yeye muda huu mzee huyu alikuwa ameiteka na kuiweka kusikojulikana akili ya binti huyu mrembo.

Baada ya chakula waliingia katika gari la mzee yule tayari kwa kurejea nyumbani kwa mzee yule maeneo ya Oysterbay.Gari hii ya Volkswagen Amarok,liliwafikisha katika geti kubwa nje ya jengo la ghorofa mbili yalipokuwa makazi ya mzee huyu.Kijana wa kazi alifika na kufungua geti lile,kuipisha gari hii kuingia.Mzee yule alilipaki gari likiungana na mengine matatu na kufikisha idadi ya magari manne yaliyokuwa ndani ya jumba hili kubwa.Walishuka kwenye gari wakiwa wamekumbatiana,japo ungewaangalia walivyotofautiana umri ungefikiri mzee huyu alikuwa na binti yake akimkaribisha kutoka masomoni,lakini alikuwa ni mpenzi wake.Labda tuite mmoja kati ya wapenzi wengi wa mzee huyu.

Walipandisha juu na kuelekea moja kwa moja chumbani kwao,Walivuana nguo kwa kasi ,huku wakitoa miguno ya kimahaba,Sasa mzee huyu alinyanyua mguu wa binti huyu na kuushikilia kwa mguu mmoja.kihisabati tungesema mguu huu ungekuwa umetengeneza angle ya 90 "to the horizontal' mzee huyu aliuvuta mmoja wa miguu yake usiovalishwa viatu kuisherehekea sherehe hii ya dharura.Lakini kabla ya kufanya chochote" mikono juu" ilisikika sauti nzito ya mamlaka ikiamrisha mzee yule.

"E1 nimekukosea nini" alisema mzee yule akitetemeka
"paaaaaaaaaah" Risasi moja kutoka bunduki hii ya kivita hii aina ya Daniel defense AR 15 Semi automatic ilikita katika paja la mzee yule.
Damu zilichuruzika na kukichafua chumba kile,binti Irene sasa alikuwa ameshafanya mojawapo ya sifa za viumbe haiyaani excretion,akitoa mkojo,macho yake yalitoa machozi alikuwa akilia sana.

Nini kimesababisha E1 Kuasi,je nini kitatokea? Nani unampenda katika hadithi hii usiache kucomment.
 
Big up sana mwanzoni sikuielewa vizuri ila sasa hivi nakuelewa vizuri sana, nakutabiria utakuja kuwa mtunzi bora sana, Mungu akubariki sana
SEHEMU YA TISA
Simu ya Sarah ilikuwa ikiita kwa sauti aliinua mkoba wake uliokuwa juu ya meza kuitoa simu yake,akaangalia kioo ili kuliona jina la mpigaji......

MSHANGAO-Sarah alibaki ameduwaa asijue la kufanya.

Ulikuwa ni mshangao uliochanganyika na furaha aliyokuwa nayo.Kuna jambo ambalo hutokea mtu asiamini limetokea vipi,kwa Sarah namba hii yenye code number +44 Ilikuwa na maana kubwa kwake.Alikuwa ni Sir Walters McAllison mmiliki wa kampuni maarufu ya bidhaa za kielektroniki kutoka Uingereza.Sarah alitamani na kuthubutu mara nyingi,kuwa mwanasheria wa kampuni hii lakini mara zote hakuweza kukubaliwa.Sio kwa sababu walikuwa na mashaka naye au taaluma yake ila kwa sababu ya ugumu wa mzee huyu wa cheocha Sir.Mzee Walters,alikuwa mgumu sana kuonana nae kama sio kupata namba zake za simu.

Mshangao huu ulimduwaza mpaka simu ikakata,Alikuwa akifikiria alivyotumia pesa zote alizolipwa katika kesi yake ya kwanza ili apate tiketi za ndege kujaribu kuonana na mzee Walters.Hakufanikiwa na akaamua kuomba walau namba yake ya simu,pia aligonga mwamba,alijaribu tena na tena hakufanikiwa.Hakukata tamaa aliamua kupanda ndege nyingine hadi nchini ufaransa katika jiji la Monaco kujaribu kupata mawasiliano ya mzee huyu,siku hii alimpata msaidizi wake aliyemkatisha tamaa.Alimwambia Simu ya mzee Walters ina namba tatu,moja ya mke wake,ya pili ya bintiye na yatatu ya waziri mkuu wa Uingereza.Hata yeye mlinzi mkuu wa mzee huyu hakuwa na namba zake za simu.Watu wote waliojaribu kumpigia mzee Walters ilikuwa lazima wapitie simu yake ya ofisini na kama kuna dharura yoyote ndipo huelekezwa kwa mzee Walters.


Mlinzi huyu alimuonea huruma Sarah akampa namba za binti yake ikawa bahati yake Sarah.Binti huyu wa Mzee Walters ndiye akaja kumpa namba za baba yake.Lakini akaambiwa habari zilizomkatisha tamaa zaidi.Mzee Walters hapigiwi simu akikuhitaji atakupigia.Hivyo leo ulikuwa mwaka wa nne na miezi tisa,na siku ishirini na saba baada ya tarehe ile jina la Sir Walters kwenye kioo chake alikaribia kuzimia kwa furaha kubwa aliyokuwa nayo.

Akaamua kuipokea,"Hello,Sarah",Sauti nzito ya mzee huyu ilimshtua .I am offering you an opportunity to be my legal representative in one of my cases,My personal secretary will call you for further information".Alimaliza na kukata simu yake bila ya Sarah kujibu,neno pekee alilolitamka ni "YES SIR".

STENDI YA MABASI -UBUNGO
Kijana Brian alilivuta begi lake dogo na kulipandisha katika Basi lililokuwa linaelekea mjini Bariadi,mkoani Simiyu.Huko angepanda lingine tayari kwa kwenda kijijini Ikungu yalipo makazi ya babu na bibi yake.Hakutaka kwenda nyumbani kwao jijini Mwanza ila aliamua kwenda kwa babu yake akiamini itakuwa ni sehemu salama ya kutuliza akili yake kwa kipindi hiki.

Maisha hutufunza mambo mengii,lakini mafunzo haya hutuachia maumivu makubwa.Ili kuyatumia mafunzo haya kufanikiwa tunatakiwa kubadilika,lakini mabadiliko huwa tunayapinga kwani yatabadilisha kila kitu tulichokizoea.Brian aliamua kuanza maisha upya ili ayasahau yaliyojitokeza huko nyuma.Safari iliendelea wakiivuka mikoa ya morogoro na Dodoma,Singida na Tabora,Shinyanga na Mwanza na hatimaye kama kila safari inavyofikia mwisho walifika mjini Bariadi.Alilazimika kulala pale na kusubiri hadi kesho yake ili kupata gari la kwenda kijijini kwa Babu yake.Alifika nyumbani kwa babu yake majira ya asubuhi na kupokelewa kwa shangwe na furaha.Mzee huyu alikuwa na busara nyingi,japo hakufanikiwa kwenda shule lakini alijua mambo mengi na alikuwa maarufu katika kijiji kile.

Baada ya salamu ,zikaanza mbio za hapa na pale kufukuza kitoweo rasmi cha mgeni wa kiafrika,Kuku.Sehemu nyingi za nchi yetu hasahasa maeneo ya vijijini mgeni hukaribishwa kwa kuchinjiwa kuku.Kijana alipewa majukumu hayo akiwasaidia Babu na bibi yake kumkamata.Japo lilikuwa saa la pili tu kwanzia afike mahali hapa aliiona furaha na amani ikiichukua nafasi ya huzuni aliyokuwa nayo.Hadithi za hapa na pale za mzee huyu machachari zilimsahaulisha hata maswahibu aliyokutana nayo.Jikoni nako bibi aliendelea na upishi,harufu nzuri iliwafikia wanaume wawili waliokuwa waki'yajenga'.Kwa kijana Brian ilikuwa ni zaidi ya siku kwake alitamani hata siku zote angekuwa na babu yake.

Watu huamini,au wamelazimishwa kuamini kuwa hela ndiyo kila kitu,hakunatena nafasi ya upendo,kuthaminiana imani,uaminifu.Hata makazini mtu akitumia matumizi inavyopaswa ataitwa anajipendekeza huku anayeiba akijiita anapiga 'dili' bila kujua kuwa bosi wake akifilisika atakosa kazi.Baadhi ya watu wachache wanatambua kuwa hela ipo kwa ajili ya kutimiza mahitaji yao lakini sio kila kitu.Babu yake aliyekuwa na miaka 75 sasa,alikuwa akionekana kama kijana wa miaka 40.Alikuwa mtu mwenye furaha wakati wake,nyumba yake iliyotengenezwa kwa miti imara,kitanda cha wastani ,zizi lenye ng'ombe wengi kiasi,akiishi na mjukuu wake mmoja tu hapa kijijini.Alikuwa na amani na kila mtu akiwa pia kiongozi wa kijiji hiki kwa miaka 15 sasa akipita mara zote bila kupingwa,alikuwa mtu wa watu.

Ukafika wakati wa jioni,kijana alimsaidia babu yake kuwasha moto kwa kutumia kinyesi cha ng'ombe,na baada ya chakula walipiga stori wakiota moto huu.Mzee huyu alimuuliza kijana swali fikirishi,"unajiona wapi katika miaka ijayo"?.Swali hili lililenga kupima ufahamu wa kijana wake.Kijana Brian,hakujua ajibu nini,Japo alikuwa muhitimu wa shahada ya masomo ya Biashara lakini hakujua atakuwa nani miaka ijayo,kwanini?.Kwa sababu hakuwa na uhakika ataajiriwa kama nani kwake yeye aliwaza ije siku apate ajira na hivyo alimjibu mzee yule sijui Babu,Sijui hata nifanye nini.

Babu alijiweka vizuri kwenye kiti na kumtazama kijana Brian,kisha akamwambia."Wakoloni walivyokuja ,walitukuta tukiwa na mfumo wetu wa maisha,waliingiza elimu yao na kuitumia kujinufaisha".Wakati huo watu walilima mazao ya chakula yaliyotosheleza mahitaji yao,walikuwa na elimu iliyosaidia kutatua matatizo yao,Mfano kijana wa kiume alifundishwa ujenzi wa nyumba ya kuishi.Au uhunzi wa kutengeneza,silaha na zana za kutumia katika shughuli mbalimbali.Hivyo,elimu kama haijatumika kusaidia matatizo ya jamii haina maana yoyote.Maneno ya mzee huyu wa miaka 75 yalimuingia barabara kijana Brian.Alizidi kumpenda mzee yule hata akathubutu kumfananisha na gwiji la sayansi Albert Einstein aliyewahi kusema "Kama huwezi kumueleza mtoto wa miaka sita akakuelewa basi hujui hicho unachokieleza".Japo mzee huyu hakusoma lakini aliweza kuiona hekima yake.Aliyahifadhi maneno ya mzee yule.

COLLOSEUM HOTEL
Leo Irene alikuwa na mzee wake,aliyempa "all of her" usiku wa jana,mahali hapa alikuwa akipata chakula cha mchana.Alikuwa amechangamka kwa mara ya kwanza maishani mwake akifanikiwa kunywa glass nzima ya Smirnoff X1.Alikuwa kavalia kaptula fupi na blouse iliyoonyesha sehemu kubwa ya kifua chake.Alionekana kupendeza sana.Wanawake wamejaaliwa upendo,lakini baadh yao hawajui hata mtu wa kupenda,kuna hulka ya watu kuona kilicho mbali kama chenye thamani zaidi kuliko ulichonacho ndiyo iliyomsumbua Irene,akiona Brian hakuwa na maaana yoyote kwake.Kwake yeye muda huu mzee huyu alikuwa ameiteka na kuiweka kusikojulikana akili ya binti huyu mrembo.

Baada ya chakula waliingia katika gari la mzee yule tayari kwa kurejea nyumbani kwa mzee yule maeneo ya Oysterbay.Gari hii ya Volkswagen Amarok,liliwafikisha katika geti kubwa nje ya jengo la ghorofa mbili yalipokuwa makazi ya mzee huyu.Kijana wa kazi alifika na kufungua geti lile,kuipisha gari hii kuingia.Mzee yule alilipaki gari likiungana na mengine matatu na kufikisha idadi ya magari manne yaliyokuwa ndani ya jumba hili kubwa.Walishuka kwenye gari wakiwa wamekumbatiana,japo ungewaangalia walivyotofautiana umri ungefikiri mzee huyu alikuwa na binti yake akimkaribisha kutoka masomoni,lakini alikuwa ni mpenzi wake.Labda tuite mmoja kati ya wapenzi wengi wa mzee huyu.

Walipandisha juu na kuelekea moja kwa moja chumbani kwao,Walivuana nguo kwa kasi ,huku wakitoa miguno ya kimahaba,Sasa mzee huyu alinyanyua mguu wa binti huyu na kuushikilia kwa mguu mmoja.kihisabati tungesema mguu huu ungekuwa umetengeneza angle ya 90 "to the horizontal' mzee huyu aliuvuta mmoja wa miguu yake usiovalishwa viatu kuisherehekea sherehe hii ya dharura.Lakini kabla ya kufanya chochote" mikono juu" ilisikika sauti nzito ya mamlaka ikiamrisha mzee yule.

"E1 nimekukosea nini" alisema mzee yule akitetemeka
"paaaaaaaaaah" Risasi moja kutoka bunduki hii ya kivita hii aina ya Daniel defense AR 15 Semi automatic ilikita katika paja la mzee yule.
Damu zilichuruzika na kukichafua chumba kile,binti Irene sasa alikuwa ameshafanya mojawapo ya sifa za viumbe haiyaani excretion,akitoa mkojo,macho yake yalitoa machozi alikuwa akilia sana.

Nini kimesababisha E1 Kuasi,je nini kitatokea? Nani unampenda katika hadithi hii usiache kucomment.
 
Big up sana mwanzoni sikuielewa vizuri ila sasa hivi nakuelewa vizuri sana, nakutabiria utakuja kuwa mtunzi bora sana, Mungu akubariki sana
Asante kaka,maoni ushauri 0785386036
 
Back
Top Bottom