FANANI MTENZI
Senior Member
- Jul 4, 2017
- 106
- 95
- Thread starter
- #41
KOMBORA KIOTANI-23
BONIFACE BIRAGE
Rais Kilua akiwa kwenye ofisi yake anaingia mtu.Alienda moja kwa moja hadi alipoketi kwa heshma zote.Kilua aliinua macho nakumsikiliza kwa makini bwana huyu.
“Madam kuhusu kufanyiwa ushushushu kwa bwana Serambovu kwa mawasiliano yake.”alisema wakala huyo kwa umakini.Kilua alimwangalia huku akipitisha ulimi kwenye papi za midomo yake kwa haiba ya kike.Urembo wake ulikuwa umesimama dede na kila aliyemuona alihisi wivu kwa mwanaume aliyemuoa nakuona kama ananyimwa wasaa wa kufurahi na bibi huyu mwenye wajihi kama hurulaini.
“Mmegundua nini?”aliuliza Kilua.
“Jukumu hili nilipewa na bosi wangu bwana Masha.Na katika kupitiapitia nilIpata simu nyingi tu alizokuwa anapata bwana Serambovu kila mara nilijitahidi kuwa makini.Nanilichukulia kila mawasiliano kuwa ni makini sana nakuyapatiliza.Ila kuna simu moja ilinitatiza sana.Hii ilitoka hivi karibuni.Hii ilikuwa na mazungumzo yanayohusu kukamatwa kwa mwanausalama wa KISS.Simu hii iliuliza kwamba kama kuna oda yoyote kutoka ikulu kuhusu kufanyiwa ushushushu kwa meli ya mizigo iliyopo bandarini.Nilijaribu kufuatilia mazungumzo na hasa meli hiyo kwanini ifuatiliwe na kama kweli ilikuwa inafuatiliwa kwanini mfanyakazi wa ikulu atoe siri kwa wanaofuatiliwa?Nilichojua kupitia njia zangu meli hiyo inahusika kukamatwa kwa wanausalama waliokuwa katika operesheni zao.Idara ya usalama hadi sasa haijafanikiwa kuwaokoa watu wake.Hivi ni kwamba meli hiyo kama ina jeuri ya kuwaweka vizuizini watu wa usalama halafu hapohapo isifuatiliwe na bado kuna mtu kutoka ikulu anaongea nao inaonesha kuna mazito kuhusu uhusiano wa meli hii na Serambovu.”
Kilua alitumbua macho.Palepale alichukua simu nakumpigia Bwana Toti,”Halo bwana Toti?”
“Ndiyo mheshimiwa.”
“Kuna agent wako anaitwa Shuni?”
“Ndiyo na ndiye aliyekamatwa kwenye meli ile tulioishuku kuhusu madawa ya kulevya na hadi sasa bado hatujam-recover”
“Dame it!Nimeisha jua aliyemkamata ni nani?Njoo ofisini kwangu.”alisema rais Kilua kwa kujiamini bila kupepesa macho.
Alikata simu nakumuangalia kijana aliyepembeni yake,”Ulifanya kazi nzuri sana unastahili pongezi sana kijana wangu.’’
Kijana alishukuru kwa pongezi hizo.Zilikuwa pongezi za kuridhisha kutoka kwa mkuu wa nchi.Kilua alitilia shaka sana kuhusu Serambovu kuwa na mawasiliano na meli iliyohusika kuwaweka vizuizini watu wa idara ya usalama.Hilo lilikuwa kosa kubwa sana kuhusika kwake.Kilua alionganisha matukio kadhaa pamoja na lile la kupigiwa simu kwa yule mtu anayetaka file namba 13:14.Pia alikumbuka alizungumza naye na akaambiwa kuna wakala wa usalama amekamatwa na huyo wakala anaitwa Shuni!Aliongea na wakala huyo nakumthibitishia kwamba yupo mikononi mwao akiwa kwenye operesheni zao akatekwa na adui.Adui mwenyewe naye anahushwa na utekaji wa familia yake.Ina maana ni kweli Serambovu alijua watu hawa walimteka mwanaye?Anakumbuka siku fulani akiongea na Serambovu alimtajia kuhusu kutekwa kwa familia yake.Ni kweli Serambovu anajua.Ila alijuaje?Kilua hakuwa amemwambia na kwasababu hiyo aliweka ushushushu wa kuchunguzwa kwa Serambovu hadi sasa anapogundua wanaounganishwa na utekaji wa familia yake.Waliokuwa kwenye meli na yule anayempigia simu za vitisho kuhusu kuteka familia yake wanaushirikiano au kwa lugha nyepesi ni timu moja!Kama waliweza kuongea na chifu wake wa ushauri bila shaka walijua vyema nyendo zake.Hata walipomwambia wanajua hata akitema mate wanajua basi mvujishaji wa habari ni Serambovu!Kilua aliuma meno kwa hasira sana.Tena huyu mshenzi aliongea na watu hao wakiwa kitandani kwake!Kampa kila kitu na penzi lake lakini bado kafikia hatua ya kumsaliti?
Baada ya muda mfupi Toti na Masha waliwasili ikulu nakueleza walichogundua kuhusu faili nambari 13:14.Walimueleza yote waliyoyapata kutoka kwa bwana Pasha.Kilua aliwasikiliza kwa umakini nakuanza kupata picha kuwa ikulu iliingiliwa na sasa imengiliwa zaidi!
***
“Gentlemen kama mlivyoniambia basi na mimi nimegundua moja ya staff wangu alikuwa ana mazungumzo ya siri na kaptein wa meli hiyo na kwa mujibu wa ripoti niliyopata nikuwa kapteni wa meli anaitwa Mr Zungu.”
“Mheshimiwa pia kulingana na uchunguzi wa awali Shuni alikuwa akimpeleleza mtu anaitwa bwana Tufe huyu alikuwa na data zot kuhusu meli hiyo.”alisema bwana Toti.
“Kama huyo Tufe anahusika na meli basi anajua vyema alipo binti yangu na mume wangu!Namtaka huyo mtu atiwe nguvuni haraka sana.Alipo Shuni na familia yangu ipo.”
Kilua alikwisha waeleza watu hawa jinsi familia yake ilivyotekwa na watu na hadi Shuni kutekwa na ikatokea sadfa kwamba wote wamekutana sehemu moja!Hilo lilitosha kuwapa muelekeo kwamba adui alianza kuonekana ni nani.Kilua hakupenda kumuuza Serambovu kwa haraka kwa namna ile alitaka kumshtukiza.
“Na huyu stafu wako anatakiwa akamatwe.”alishauri Masha ambaye alionekana hampendi Serambovu hata kidogo.”
“Huyu tumuweke kwenye uangalizi wa hali ya juu.Tutamtumia kama chambo kuwapata hao wengine.Nikimshtukiza sasahivi itakuwa hasara kwetu.Huyu nitamshughulikia mwenyewe!”alisema Kilua hali iliyofanya Masha kuwaza mara mbilimbili kama ni kweli Serambovu na Kilua walikuwa na uhusiano wa mapenzi au la!Maana pozi la Kilua lilikuwa kama kuna uaminifu mkubwa kati yake na Serambovu hivyo kuwa na imani kwamba kwa uaminifu huo Serambovu atakiri kuhusika na wabaya wake.Hilo halikutosha kumpa lile jibu la swali gumu!
“Inatakiwa tuwe makini.Tukiweza kudhibiti watu hawa tutajua nani alilipua serikali nzima!”
“Kesho ni siku ya mazishi kwa mashujaa wetu waliofia kwenye ile ajali natumai iende vizuri.Kuna ujio wa wageni wengi kutoka nchi za nje.Naomba muweke vijana wenu ulinzi uwe wakutosha.”
Kilua aliinuka kuashiria kikao kimeisha.Kisha alienda moja kwa moja kwenye chumba cha mikutano.Humu kulikuwa na kamati ya ulinzi iliyokuwa inamsubiri kwa hamu kwa siku ile aseme nao.Waliketi walipomuona.Rais wao kafika.Kilua mwanzoni alikuwa amepitisha utaratibu wake wa ulinzi ambao ungetumika kwa siku ile.Kilichomleta pale ni kuhakikisha tu kwamba utaratibu alioupitisha upo sawa.Tofauti na mategemeo akakuta utaratibu umebadilishwa.
“Nani aliyebadili utaratibu huu?”
“Ni Serambovu pamoja na jenerali Lupogo.”alisema moja ya wajumbe wa kamati ya ulinzi.Jambo hilo lilimkera Kilua nakuona kama anaingiliwa kwenye maamuzi yake.Huo ulikuwa utaratibu ambao kuna maeneo uliacha mwanya na kama kuna mtu angetumia mwanya huo bila shaka angeingilia mzingo wa usalama jambo ambalo Kilua hakuwa tayari kulishuhudia hata kwa dawa.Mchoro mpya uliopitishwa na Serambovu na jenerali Lupogo haukumshibisha Kilua.Na aliupinga toka mwanzo lakini hawa wamepindua uamuzi wake nakumfanya aonekane kituko.Hicho kilimpeleka mbali ikiwa kweli Serambovu ndo anayemwendesha au kuna laziada linalotokea.Kilua alihisi mambo siyo sawa na hisia zake zikazidi kuwa za mashaka hasa jamaa alivyozidi kukumbwa na sakata la kuhisiwa vibaya.Yote haya yalimuweka Kilua katika wakati mgumu dhidi ya watendaji wake wawili muhimu sana.Jenerali Lupogo!
“Kwanini walibadili utaratibu?”
“Walipitia itifaki upya na kujiridhisha kwamba mchoro huu wa kiusalama ungekuwa mzuri zaidi kuliko ule tulioupitisha mwanzo na Serambovu alisema atazungumza na wewe kuhusu jambo hili.”alitaarifiwa.Kilua hakutaka kuonesha mashaka yake dhidi ya jambo hilo nakuona kweli kuna watu hawajajua sauti yake ni nini?
Kilua aliondoka katika kikao kile bila kumsemesha mtu.Alirudi hadi eneo jingine la ikulu.Kisha aliongea na walinzi wake kwamba anataka kudhuru eneo ambalo shughuli ya msiba wa kitaifa utafanyika.Hapo marehemu watapewa heshma zao za mwisho.Kulizuka mabishano kwamba asiende pale maana bado hawajafanya uhakiki wa barabara kwa rais kupita.Lakini alifanikiwa kuwashawishi walinzi wake.Ndani ya muda mfupi tofauti na utaratibu msafara wa rais uliandaliwa kwa yeye kwenda eneo lile.Kilua aliondoka na walinzi kadhaa.Magari yalianza mwendo huku Kilua akiwa amekasirika moyoni kwa jinsi Serambovu alivyomtenda!
Alijua akifika eneo hilo atamkuta jenerali Lupogo.Ving’ora vya msafara vilizidi kusambaa hivyo kuyafanya magari mengine kupisha njia.Kilua alikuwa anafikiria mambo sana ikiwemo hisia kali alizopata dhidi ya bintiye kwamba kuna mtu alitishia kumtenda unyama na toka wakati ule hadi sasa bado roho ya yake imekosa imani kama kweli mwanaye ana usalama huko alipo au kuna sintofahamu zinaendelea kati yao!
Baada ya dakika chache alikuwa amefika eneo lile.Kulizuka mshtuko mkubwa sana baada ya watu kugundua ujio wake rais Kilua ambao hakuna aliyemtegemea.Wengi walijua wangemuona siku ijayo atakuja akiwa na msafara wake kuwaongoza wananchi na wageni katika kutoa heshma za mwisho kwa mashujaa wa taifa walioaga dunia.Tofauti na vile Kilua ametokea eneo la tukio kwa kushtukiza sana!
Jenerali Lupogo alishtuliwa na ujio huo sana.Ilibidi awe wa kwanza kwenda kumlaki mkuu wake wa kazi.Kilua alijikuwa mpole.Aliwapa moyo wote waliokuwa wanafanyakazi kuandaa uwanja ule kwa shughuli ile maalum.Baada ya hapo aliomba kuongea na jenerali wake.
“Mheshimiwa nakushukuru sana kwa ujio wako hapa.Na…”jenerali alikatishwa na Kilua.
“Jenerali nafikiri tuna sahau mipaka yetu ya kazi?”Kilua alianza kwa jazba.Hilo halikutegemewa
“Kwanini mheshimiwa?”
“Inakuwaje mnabadili protokali niliyopitisha nakuweka mchoro wenu?”Kilua akawa mkali.
“Mheshimiwa unajua…n…”
“Jeneral nadhani hujui ni nani mwenye mamlaka?Sasa nasema hivi nakusimamisha kazi na kwaanzia hadi pale nitakapoamua vinginevyo.Agents mkamateni.”
“Ngoja hawa hawana mamlaka yakunikamata?”jenerali Lupogo alijitetea huku akibabaika.Lilikuwa jambo baya sana kwa mkuu wa nchi kukusimamisha kazi halafu anakuweka kizuizini!
ITAENDELEA WIKI IJAYO
BONIFACE BIRAGE
Rais Kilua akiwa kwenye ofisi yake anaingia mtu.Alienda moja kwa moja hadi alipoketi kwa heshma zote.Kilua aliinua macho nakumsikiliza kwa makini bwana huyu.
“Madam kuhusu kufanyiwa ushushushu kwa bwana Serambovu kwa mawasiliano yake.”alisema wakala huyo kwa umakini.Kilua alimwangalia huku akipitisha ulimi kwenye papi za midomo yake kwa haiba ya kike.Urembo wake ulikuwa umesimama dede na kila aliyemuona alihisi wivu kwa mwanaume aliyemuoa nakuona kama ananyimwa wasaa wa kufurahi na bibi huyu mwenye wajihi kama hurulaini.
“Mmegundua nini?”aliuliza Kilua.
“Jukumu hili nilipewa na bosi wangu bwana Masha.Na katika kupitiapitia nilIpata simu nyingi tu alizokuwa anapata bwana Serambovu kila mara nilijitahidi kuwa makini.Nanilichukulia kila mawasiliano kuwa ni makini sana nakuyapatiliza.Ila kuna simu moja ilinitatiza sana.Hii ilitoka hivi karibuni.Hii ilikuwa na mazungumzo yanayohusu kukamatwa kwa mwanausalama wa KISS.Simu hii iliuliza kwamba kama kuna oda yoyote kutoka ikulu kuhusu kufanyiwa ushushushu kwa meli ya mizigo iliyopo bandarini.Nilijaribu kufuatilia mazungumzo na hasa meli hiyo kwanini ifuatiliwe na kama kweli ilikuwa inafuatiliwa kwanini mfanyakazi wa ikulu atoe siri kwa wanaofuatiliwa?Nilichojua kupitia njia zangu meli hiyo inahusika kukamatwa kwa wanausalama waliokuwa katika operesheni zao.Idara ya usalama hadi sasa haijafanikiwa kuwaokoa watu wake.Hivi ni kwamba meli hiyo kama ina jeuri ya kuwaweka vizuizini watu wa usalama halafu hapohapo isifuatiliwe na bado kuna mtu kutoka ikulu anaongea nao inaonesha kuna mazito kuhusu uhusiano wa meli hii na Serambovu.”
Kilua alitumbua macho.Palepale alichukua simu nakumpigia Bwana Toti,”Halo bwana Toti?”
“Ndiyo mheshimiwa.”
“Kuna agent wako anaitwa Shuni?”
“Ndiyo na ndiye aliyekamatwa kwenye meli ile tulioishuku kuhusu madawa ya kulevya na hadi sasa bado hatujam-recover”
“Dame it!Nimeisha jua aliyemkamata ni nani?Njoo ofisini kwangu.”alisema rais Kilua kwa kujiamini bila kupepesa macho.
Alikata simu nakumuangalia kijana aliyepembeni yake,”Ulifanya kazi nzuri sana unastahili pongezi sana kijana wangu.’’
Kijana alishukuru kwa pongezi hizo.Zilikuwa pongezi za kuridhisha kutoka kwa mkuu wa nchi.Kilua alitilia shaka sana kuhusu Serambovu kuwa na mawasiliano na meli iliyohusika kuwaweka vizuizini watu wa idara ya usalama.Hilo lilikuwa kosa kubwa sana kuhusika kwake.Kilua alionganisha matukio kadhaa pamoja na lile la kupigiwa simu kwa yule mtu anayetaka file namba 13:14.Pia alikumbuka alizungumza naye na akaambiwa kuna wakala wa usalama amekamatwa na huyo wakala anaitwa Shuni!Aliongea na wakala huyo nakumthibitishia kwamba yupo mikononi mwao akiwa kwenye operesheni zao akatekwa na adui.Adui mwenyewe naye anahushwa na utekaji wa familia yake.Ina maana ni kweli Serambovu alijua watu hawa walimteka mwanaye?Anakumbuka siku fulani akiongea na Serambovu alimtajia kuhusu kutekwa kwa familia yake.Ni kweli Serambovu anajua.Ila alijuaje?Kilua hakuwa amemwambia na kwasababu hiyo aliweka ushushushu wa kuchunguzwa kwa Serambovu hadi sasa anapogundua wanaounganishwa na utekaji wa familia yake.Waliokuwa kwenye meli na yule anayempigia simu za vitisho kuhusu kuteka familia yake wanaushirikiano au kwa lugha nyepesi ni timu moja!Kama waliweza kuongea na chifu wake wa ushauri bila shaka walijua vyema nyendo zake.Hata walipomwambia wanajua hata akitema mate wanajua basi mvujishaji wa habari ni Serambovu!Kilua aliuma meno kwa hasira sana.Tena huyu mshenzi aliongea na watu hao wakiwa kitandani kwake!Kampa kila kitu na penzi lake lakini bado kafikia hatua ya kumsaliti?
Baada ya muda mfupi Toti na Masha waliwasili ikulu nakueleza walichogundua kuhusu faili nambari 13:14.Walimueleza yote waliyoyapata kutoka kwa bwana Pasha.Kilua aliwasikiliza kwa umakini nakuanza kupata picha kuwa ikulu iliingiliwa na sasa imengiliwa zaidi!
***
“Gentlemen kama mlivyoniambia basi na mimi nimegundua moja ya staff wangu alikuwa ana mazungumzo ya siri na kaptein wa meli hiyo na kwa mujibu wa ripoti niliyopata nikuwa kapteni wa meli anaitwa Mr Zungu.”
“Mheshimiwa pia kulingana na uchunguzi wa awali Shuni alikuwa akimpeleleza mtu anaitwa bwana Tufe huyu alikuwa na data zot kuhusu meli hiyo.”alisema bwana Toti.
“Kama huyo Tufe anahusika na meli basi anajua vyema alipo binti yangu na mume wangu!Namtaka huyo mtu atiwe nguvuni haraka sana.Alipo Shuni na familia yangu ipo.”
Kilua alikwisha waeleza watu hawa jinsi familia yake ilivyotekwa na watu na hadi Shuni kutekwa na ikatokea sadfa kwamba wote wamekutana sehemu moja!Hilo lilitosha kuwapa muelekeo kwamba adui alianza kuonekana ni nani.Kilua hakupenda kumuuza Serambovu kwa haraka kwa namna ile alitaka kumshtukiza.
“Na huyu stafu wako anatakiwa akamatwe.”alishauri Masha ambaye alionekana hampendi Serambovu hata kidogo.”
“Huyu tumuweke kwenye uangalizi wa hali ya juu.Tutamtumia kama chambo kuwapata hao wengine.Nikimshtukiza sasahivi itakuwa hasara kwetu.Huyu nitamshughulikia mwenyewe!”alisema Kilua hali iliyofanya Masha kuwaza mara mbilimbili kama ni kweli Serambovu na Kilua walikuwa na uhusiano wa mapenzi au la!Maana pozi la Kilua lilikuwa kama kuna uaminifu mkubwa kati yake na Serambovu hivyo kuwa na imani kwamba kwa uaminifu huo Serambovu atakiri kuhusika na wabaya wake.Hilo halikutosha kumpa lile jibu la swali gumu!
“Inatakiwa tuwe makini.Tukiweza kudhibiti watu hawa tutajua nani alilipua serikali nzima!”
“Kesho ni siku ya mazishi kwa mashujaa wetu waliofia kwenye ile ajali natumai iende vizuri.Kuna ujio wa wageni wengi kutoka nchi za nje.Naomba muweke vijana wenu ulinzi uwe wakutosha.”
Kilua aliinuka kuashiria kikao kimeisha.Kisha alienda moja kwa moja kwenye chumba cha mikutano.Humu kulikuwa na kamati ya ulinzi iliyokuwa inamsubiri kwa hamu kwa siku ile aseme nao.Waliketi walipomuona.Rais wao kafika.Kilua mwanzoni alikuwa amepitisha utaratibu wake wa ulinzi ambao ungetumika kwa siku ile.Kilichomleta pale ni kuhakikisha tu kwamba utaratibu alioupitisha upo sawa.Tofauti na mategemeo akakuta utaratibu umebadilishwa.
“Nani aliyebadili utaratibu huu?”
“Ni Serambovu pamoja na jenerali Lupogo.”alisema moja ya wajumbe wa kamati ya ulinzi.Jambo hilo lilimkera Kilua nakuona kama anaingiliwa kwenye maamuzi yake.Huo ulikuwa utaratibu ambao kuna maeneo uliacha mwanya na kama kuna mtu angetumia mwanya huo bila shaka angeingilia mzingo wa usalama jambo ambalo Kilua hakuwa tayari kulishuhudia hata kwa dawa.Mchoro mpya uliopitishwa na Serambovu na jenerali Lupogo haukumshibisha Kilua.Na aliupinga toka mwanzo lakini hawa wamepindua uamuzi wake nakumfanya aonekane kituko.Hicho kilimpeleka mbali ikiwa kweli Serambovu ndo anayemwendesha au kuna laziada linalotokea.Kilua alihisi mambo siyo sawa na hisia zake zikazidi kuwa za mashaka hasa jamaa alivyozidi kukumbwa na sakata la kuhisiwa vibaya.Yote haya yalimuweka Kilua katika wakati mgumu dhidi ya watendaji wake wawili muhimu sana.Jenerali Lupogo!
“Kwanini walibadili utaratibu?”
“Walipitia itifaki upya na kujiridhisha kwamba mchoro huu wa kiusalama ungekuwa mzuri zaidi kuliko ule tulioupitisha mwanzo na Serambovu alisema atazungumza na wewe kuhusu jambo hili.”alitaarifiwa.Kilua hakutaka kuonesha mashaka yake dhidi ya jambo hilo nakuona kweli kuna watu hawajajua sauti yake ni nini?
Kilua aliondoka katika kikao kile bila kumsemesha mtu.Alirudi hadi eneo jingine la ikulu.Kisha aliongea na walinzi wake kwamba anataka kudhuru eneo ambalo shughuli ya msiba wa kitaifa utafanyika.Hapo marehemu watapewa heshma zao za mwisho.Kulizuka mabishano kwamba asiende pale maana bado hawajafanya uhakiki wa barabara kwa rais kupita.Lakini alifanikiwa kuwashawishi walinzi wake.Ndani ya muda mfupi tofauti na utaratibu msafara wa rais uliandaliwa kwa yeye kwenda eneo lile.Kilua aliondoka na walinzi kadhaa.Magari yalianza mwendo huku Kilua akiwa amekasirika moyoni kwa jinsi Serambovu alivyomtenda!
Alijua akifika eneo hilo atamkuta jenerali Lupogo.Ving’ora vya msafara vilizidi kusambaa hivyo kuyafanya magari mengine kupisha njia.Kilua alikuwa anafikiria mambo sana ikiwemo hisia kali alizopata dhidi ya bintiye kwamba kuna mtu alitishia kumtenda unyama na toka wakati ule hadi sasa bado roho ya yake imekosa imani kama kweli mwanaye ana usalama huko alipo au kuna sintofahamu zinaendelea kati yao!
Baada ya dakika chache alikuwa amefika eneo lile.Kulizuka mshtuko mkubwa sana baada ya watu kugundua ujio wake rais Kilua ambao hakuna aliyemtegemea.Wengi walijua wangemuona siku ijayo atakuja akiwa na msafara wake kuwaongoza wananchi na wageni katika kutoa heshma za mwisho kwa mashujaa wa taifa walioaga dunia.Tofauti na vile Kilua ametokea eneo la tukio kwa kushtukiza sana!
Jenerali Lupogo alishtuliwa na ujio huo sana.Ilibidi awe wa kwanza kwenda kumlaki mkuu wake wa kazi.Kilua alijikuwa mpole.Aliwapa moyo wote waliokuwa wanafanyakazi kuandaa uwanja ule kwa shughuli ile maalum.Baada ya hapo aliomba kuongea na jenerali wake.
“Mheshimiwa nakushukuru sana kwa ujio wako hapa.Na…”jenerali alikatishwa na Kilua.
“Jenerali nafikiri tuna sahau mipaka yetu ya kazi?”Kilua alianza kwa jazba.Hilo halikutegemewa
“Kwanini mheshimiwa?”
“Inakuwaje mnabadili protokali niliyopitisha nakuweka mchoro wenu?”Kilua akawa mkali.
“Mheshimiwa unajua…n…”
“Jeneral nadhani hujui ni nani mwenye mamlaka?Sasa nasema hivi nakusimamisha kazi na kwaanzia hadi pale nitakapoamua vinginevyo.Agents mkamateni.”
“Ngoja hawa hawana mamlaka yakunikamata?”jenerali Lupogo alijitetea huku akibabaika.Lilikuwa jambo baya sana kwa mkuu wa nchi kukusimamisha kazi halafu anakuweka kizuizini!
ITAENDELEA WIKI IJAYO