Riwaya: Chokoraa

Riwaya: Chokoraa

kumbe nlikua nimepitwa hivi!! ila leo nimeisoma yote,
mungu awasaidie wakina mwanaidi
 
RIWAYA: CHOKORAA
MTUNZI: George Iron Mosenya





SEHEMU YA THELATHINI


Kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu uso wake ulichanua na kutoa tabasamu japo hafifu. Tabasamu hilo liliambatana na maumivu ya kutoneshwa kidonda ambacho hakikuwa kimepona vizuri japo kilikuwa katika hatua hizo.
Aliimaliza siku hiyo huku akijiona mwepesi sana. Kichwa chake ambacho kilikuwa kinazidi kuwa kizito kadri siku zilivyosonga mbele na ukweli aliouhitaji kuzidi kuota mbaya sasa kichwa kilipata ahueni.
Mateso ya nafsi aliyokuwa anayapata yalimdhihirishia wazi kuwa alikuwa katika dimbwi la mapenzi na kiumbe yule ambaye alizikwa akiwa na kovu kubwa kabisa la kisu mgongoni.
Emiliana, mchumba wake ambaye walikuwa wanahesabu siku kadhaa waweze kuoana. Ndoto ikayeyuka baada ya binti huyu kukutwa amerupwa mtaroni akiwa mfu.
Wazazi wa upande wa mwanamke hawakuisha kumwaga lawama. Walimlaumu sana Kasuku kwa kushindwa kuwafichua wauaji wa mpenzi wake. Maneno hayakuishia hapo ilifikia wakati mama mkwe akamlaumu Kasuku kuwa huenda anawajua wauaji lakini anawaficha kwa kuwa amenufaika na mauaji hayo. Sasa alikuwa amerejewa kidogo na ari.


Furaha yake kidogo iliweza kurejea, kwanza kwa kuweza kuonana na mtu ambaye siku nyingi zilipita bila kuonana na hakujua kama yu hai ama amekufa tayari. Alikuwa mtu wa maajabu ambaye wameweza kuonana kwa kipindi kifupi wakazoeana sana kisha akatoweka machoni pake kwa mategemeo ya kuonana baada ya siku kadhaa lakini haikuwa hivyo hadi walipoweza kuonana katika hali ambayo Kasuku hakuitarajia
Wote walitabasamu huku wakikumbatiana, nyumba ilikuwa na upweke sana na binti aliyewasili hapo aliiona hali hiyo, mwenyeji wake alikuwa amekonda na alikuwa na uso wenye huzuni japo ulitabasamu. Tabasamu hafifu sana ambalo halikuweza kuificha huzuni iliyokuwa moyoni mwake.
Binti akauliza kulikoni kimya kikubwa. Majibu aliyopewa yalimsikitisha na kumfanya awe na huzuni kuliko mwenyeji wake.
Emiliana amekufa? aliuliza kwa sauti ya chini.
“Yaah wamemuua…….” alimalizia Kasuku huku akikwepesha macho yake yasitazamane nay ale ya yule binti.
Taarifa ya kifo cha mama mwenye nyumba hiyo ilimsikitisha sana Frida ambaye aliamua kuja kumtembelea bwana Kasuku baada ya Mwanaidi kukawia sana kurejea nyumbani na uwepo wa mama yao hospitali.
Kasuku hakupenda sana kukizungumzia kifo cha mkewe tena kwani aliamini kimejaa sintofahamu nyingi sana zisizokuwa na utatuzi, kimya kilipotanda Frida akaamua kuvunja ukimya, hakutaka naye kuzungumzia kifo cha mke wa bwana huyu bali akazungumzia yaliyomsibu katika mikono ya bwana Dembele. Alianza kusimulia akiwa anatabasamu kana kwamba anasimulia kisa cha kuchekesha. Lakini kadri alivyozidi kusimulia ndipo sauti ikazidi kwenda chini, hatimaye kwikwi. Frida akaanza kulia.
Ilikuwa lazima alie, tena kilio kikali. Unyama aliokuwa anaufanya bwana Dembele haukuwa wa kuchekesha wala kumshawishi mwanadamu yeyote yule kukenua meno. Frida alijieleza kwa uchungu mkubwa unyama anaoufanya bwana Dembele, unyanyasaji wa watoto na akina mama. Roho nyingi zinavyopotea kwa kumnufaisha yeye na familia yake.
Frida aliendelea kumsimulia Kasuku jinsi walivyookolewa na Mwanaidi. Ujasiri wa binti yule ulivyowaweka huru.
“Asingekuwa Mwanaidi, ningekuwa mfu tayari. Alitaka kunipasua tumbo nikalia sana nikimwambia kuwa mimi ni mjamzito. Kidogo akanielewa lakini kinyume na hapo……”
Frida alisimulia kila kitu. Kasuku akawa msikilizaji. Simulizi hii ilimgusa kwa kiasi kikubwa bwana Kasuku. Mazingira yaliyozungumzwa na Frida wakati wa kutoroka katika ngome ile yalifanana kabisa na kifo cha mkewe. Gari walilolikuta nje ya nyumba lilikuwa lilelile ambalo lilikutwa barabarani na mkewe kukutwa mtaroni.
“Kwa hiyo Dembele alimtaka mke wangu pia…” alijiuliza huku hasira kali zikimchemka kichwani.
Kasuku hakutaka kuonyesha wazi kuwa ana hasira juu ya Dembele, alijivika hali hiyo ili Frida awe huru kuzungumza.
Majira ya saa kumi jioni Frida alihitaji kuondoka, tofauti na awali ambapo alikuja kwa usafiri wa daladala sasa Kasuku alimpakia Frida katika gari lake akamrudisha nyumbani huku akiahidi kufika tena siku inayofuata ili aweze kuzungumza na mama George pamoja na Mwanaidi kisha zifanyike harakati za kuwapata George na Isha popote pale walipo.
“Bro…tunakutegemea sana……tupiganie….kama nilivyokueleza. Tunayo haki lakini nani wa kuitetea haki hiyo tuipate?? Kuwa sauti yetu kaka naamini kama ulivyoandika makala ile bado unaouwezo zaidi wa kutupigania. Lazima atakuwa anatusaka na lazima atafanikiwa kutupata maana sisi ni chokoraa na mtaa ndiyo makazi yetu. Atatuua.” Frida alizungumza kwa hisia kali. Hisia zilizomgusa Kasuku. Wakaagana kwa kukumbatiana.
Usiku huu baada ya kuachana na Frida. Bwana Kasuku alipita katika baa moja akajikita katika ulevi ili aweze kupunguza anachomuwazia Dembele. Tuhuma zote alizopewa kuwa anahusika na kifo cha mkewe alizihamishia kwa Dembele, kisha akamuona kuwa stahiki yake ni kifo. Tena kifo ambacho atajua wazi kwa nini anakufa.


Siku iliyofuata Kasuku aliwahi nyumba ambayo Frida alimueleza kuwa ndipo wanapoishi pamoja na Mwanaidi na yule mama ambaye alikuwa msafirishaji wa madawa ya kulevya bila hiari yake.
Maajabu, asubuhi yote ile hapakuwa na mmoja kati yao na majirani hawakuwa na taarifa yoyote.
Kasuku akahisi huenda Frida alimdanganya na wala si pale wanapoishi. Lakini kwanini amdanganye? alijiuliza bila kupata jawabu.
Akaiacha siku hiyo ipite. Na siku iliyofuata akajaribu tena, tatizo likawa lilelile, mlango umeegeshwa na hakuna mtu wala dalili ya kiumbe hai katika chumba kile.
Kasuku akachezwa na machale. Kuna jambo baya linawakabili watu hawa. Kasuku akajihisi kuwa analala tena na kama akilala na kuukosa ushahidi wa kumwadhibu Dembele basi lawama kutoka ukweni zitamfuata mpaka siku atakayofukiwa kaburini. Kasuku akaamua kujishughulisha. Kama Frida alivyomwezesha kwa kumpa habari ile naye akaamua kuwapigania chokoraa. Alijua wanamuhitaji sana.
Yale maneno aliyozungumza Frida, mara ya mwisho walipokuwa wakiagana yalimgusa na kumweka katika deni.
Zilipopita siku tatu bila Frida kuonekana huku majirani wakidai hawajui lolote zaidi ya kuwashuhudia wakiondoka na wanaume watatu usiku mmoja. Kasuku mpekuzi akaamua kupasua jipu.
Silaha ya mwandishi ni daftari na kalamu, silaha hii inaweza kuvunja maghorofa, na inaweza kuua na kuleta vita kubwa. Kasuku hakutaka kuleta vita bali alikuwa anaingia rasmi katika mapigano aliyoombwa na mwanadada Frida, kijana akainama chini na kuandika makala.
Makala nzito kupita zote zilizowahi kuandikwa na bwana Kasuku. Makala iliyomtambulisha tena Kasuku baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu.
Makala aliyoiandika haikuchapishwa gazetini mapema ili zifanyike hatua za kuwakomboa watoto na mama yao. Pia kutomuweka Dembele katika ufahamu unaoweza kumpa upenyo wa kutoroka.
Harakati zikaendeshwa kimya kimya.


****
Dembele alijisikia fahari sana kuwamiliki wabaya wake ambao maneno yao na uwepo wao katika maisha huru ilikuwa kikwazo cha usalama wake.
Mwanzoni baada ya kuwakamata alikuwa na ari ya kuziondoa roho hizi kwa mkono wake ilimradi tu awe huru bila hatia ya waziwazi. Lakini sasa akajikuta akiwaza mengine.
Mzigo wake. mzigo uliotakiwa kusafirishwa kuelekea ughaibuni.
Tatizo lilikuwa watu wa kubebeshwa mzigo huu. Dembele akaiona nafasi iliyopo mbele yake ni ya kipekee sana. Alikuwa na Mwanaidi, Isha, Frida, George, Suzi na mama George. Hakika alikuwa na matumbo mengi ya kupasua na kuweka mizigo yake bila kujali kama aliyepasuliwa ataendelea kuwa hai ama la. Cha msingi Punda afe lakini mzigo ufike.
Mzigo wa madawa ya kulevya.
Wazo hilo likamkatisha mipango yake ya kuwaua viumbe hawa. Kwanza aliona ni heri wakafie ughaibuni asipate ugumu katika kuwafukia ama kuwatupa baharini.
Dembele akaamua kuvuta subira bila kutambua kuwa kuna nyakati subira huvuta shubiri.
Laiti kama angejua……angechukua maamuzi mapema.


Wakati Dembele akihangaika kupitisha maamuzi sahihi kichwani mwake. Binti shujaa na jemedari wa vita hii alikuwa katika mahangaiko. Ni siku nyingi sana zilikuwa zimepita bila kukumbwa na tatizo hili ambalo lilimsababisha apotezane na Frida maeneo ya posta huku akiwa nusu mfu na nusu hai.
Mwanaidi aliwaza ni kifo gani ambacho bwana Dembele atawachagulia. Mawazo hayo yakapandisha shinikizo la damu. Shinikizo hili likaambatana na ugonjwa wake wa tangu kuzaliwa.
Pumu.
Mwanaidi akaanza kuikosa hewa murua. Akaanza kuhangaika huku na kule. Dawa yake ya kupuliza ilikuwa katika pochi yake.
Alijaribu kuita akiomba msaada lakini hakuna aliyesikia. Aliita kwa juhudi zote lakini ilikuwa sawa na bure.
Alijaribu tena na tena. Nguvu zikaanza kumuisha, akaanza kutapatapa. huku akipepesuka.
Roho ikalazimisha kuuaga mwili. Mwanaidi hakuwa radhi kuondoka. Hakutaka kuondoka kwa sababu aliamini alikuwa binti mdogo sana kupumzika wakati ana harakati kubwa za kufanya ili kuwakomboa wenzake.
Mwanaidi hakutaka kufa wakati anazo mbio ndefu za kuwapigania Chokoraa. Alimwomba Mungu amuache walau kidogo lakini alipangalo mola………
Mwanaidi shujaa wa machokoraa, Mwanaharakati aliyepigana kwa nguvu zake zote. Sasa alianguka chini, kiza kikatanda. Akatulia tuli.
Macho yakakutana na mkoba wake, mkoba wenye kile kichupa cha dawa yake ya kupulizia, ambayo humpa ahueni kila anapokuwa katika hali hii. Akili ikakiri kuwa ndani ya ule mkoba ipo dawa lakini haiwezi kutoka bila kutolewa. Nani wa kuusogeza ule mkoba? nani wa kuiokoa roho hii??


Viungo vyote vikasita kufanya kazi, yakabakia masikio ambayo yalisikia vishindo vya miguu kuelekea katika chumba kile. Vishindo hivyo vikaambatana na sauti zinazovuma mithili ya kelele. Mwanaidi hakuweza kutikisika.
Picha mbalimbali zikaanza kumpitia katika akili yake. Anazaliwa, anakulia mitaani, anachukuliwa na mjomba wake, anafukuzwa kwa kumsaidia Frida.
Anarudi kituo cha watoto yatima, anafukuzwa akiwa na Frida, anamsaidia Frida kutoa mimba, anakaribia kupoteza uhai kwa ugonjwa wa pumu, anaokolewa na mama mbaya muuza miili ya wasichana, anauzwa kwa mwanaume anayetaka kumlawiti, kwa mara ya kwanza anafanya mauaji, mara picha ya mama muuza miili akiuwawa nayo ikampitia, anakutana tena na Frida na Isha, wanaunganika na George, George anawekewa sumu, Frida na Isha wanakamatwa, anakutana na mama yake George akiwa mlemavu.
picha zinaendelea kwa kasi ya ajabu. Mwili unapatwa joto kali sana.
Jasho linatiririka.
Kiza kinazidi kutanda.




***Mwanaharakati HATARINI………..Kifo kinabisha hodi…..
Je ndio mwisho wa enzi….Mwanaidi anakufa kwa Pumu???


***KASUKU ameamua kuingia katika vita hii kimya kimya….je atawahi kabla matumbo yao hayajapasuliwa???


mangimeza Khantwe culbby Toplady Igunga Moja BPM
 
Last edited by a moderator:
RIWAYA: CHOKORAA
MTUNZI: GEORGE IRON MOSENYA
MAWASILIANO: 0655727325 au 0757727324


SEHEMU YA THELATHINI NA MOJA


Wakati Dembele akihangaika kupitisha maamuzi sahihi kichwani mwake. Binti shujaa na jemedari wa vita hii alikuwa katika mahangaiko. Ni siku nyingi sana zilikuwa zimepita bila kukumbwa na tatizo hili ambalo lilimsababisha apotezane na Frida maeneo ya posta huku akiwa nusu mfu na nusu hai.
Mwanaidi aliwaza ni kifo gani ambacho bwana Dembele atawachagulia. Mawazo hayo yakapandisha shinikizo la damu. Shinikizo hili likaambatana na ugonjwa wake wa tangu kuzaliwa.
Pumu.
Mwanaidi akaanza kuikosa hewa murua. Akaanza kuhangaika huku na kule. Dawa yake ya kupuliza ilikuwa katika pochi yake.
Alijaribu kuita akiomba msaada lakini hakuna aliyesikia. Aliita kwa juhudi zote lakini ilikuwa sawa na bure.
Alijaribu tena na tena. Nguvu zikaanza kumuisha, akaanza kutapatapa. huku akipepesuka.
Roho ikalazimisha kuuaga mwili. Mwanaidi hakuwa radhi kuondoka. Hakutaka kuondoka kwa sababu aliamini alikuwa binti mdogo sana kupumzika wakati ana harakati kubwa za kufanya ili kuwakomboa wenzake.
Mwanaidi hakutaka kufa wakati anazo mbio ndefu za kuwapigania Chokoraa. Alimwomba Mungu amuache walau kidogo lakini alipangalo mola………
Mwanaidi shujaa wa machokoraa, Mwanaharakati aliyepigana kwa nguvu zake zote. Sasa alianguka chini, kiza kikatanda. Akatulia tuli.
Macho yakakutana na mkoba wake, mkoba wenye kile kichupa cha dawa yake ya kupulizia, ambayo humpa ahueni kila anapokuwa katika hali hii. Akili ikakiri kuwa ndani ya ule mkoba ipo dawa lakini haiwezi kutoka bila kutolewa. Nani wa kuusogeza ule mkoba? nani wa kuiokoa roho hii??


Viungo vyote vikasita kufanya kazi, yakabakia masikio ambayo yalisikia vishindo vya miguu kuelekea katika chumba kile. Vishindo hivyo vikaambatana na sauti zinazovuma mithili ya kelele. Mwanaidi hakuweza kutikisika.
Picha mbalimbali zikaanza kumpitia katika akili yake. Anazaliwa, anakulia mitaani, anachukuliwa na mjomba wake, anafukuzwa kwa kumsaidia Frida.
Anarudi kituo cha watoto yatima, anafukuzwa akiwa na Frida, anamsaidia Frida kutoa mimba, anakaribia kupoteza uhai kwa ugonjwa wa pumu, anaokolewa na mama mbaya muuza miili ya wasichana, anauzwa kwa mwanaume anayetaka kumlawiti, kwa mara ya kwanza anafanya mauaji, mara picha ya mama muuza miili akiuwawa nayo ikampitia, anakutana tena na Frida na Isha, wanaunganika na George, George anawekewa sumu, Frida na Isha wanakamatwa, anakutana na mama yake George akiwa mlemavu.
picha zinaendelea kwa kasi ya ajabu. Mwili unapatwa joto kali sana.
Jasho linatiririka.
Kiza kinazidi kutanda.


****


Usilolijua ni sawa na usiku wa kiza kinene. Hali hii ilimkabili bwana Dembele pia, baada ya kuwa amewamiliki mateka hawa katika himaya yake akafikiri sasa yupo huru, hakutambua kuwa hakuna siri inayodumu milele, na sasa siri yake ilikuwa imetapakaa, na alikuwa ananuka hatia.
Tamaa zikamponza.
Amakweli mshika mbili moja humponyoka.
Dembele alikuwa anatamani kuua na wakati huohuo akatamani kuwatumia wale wafu watarajiwa katika biashara yake ya madawa ya kulevya.
Ngoja ngoja hii ikamponza. Hakuwa na mtu wa kumshauri, akahisi pombe pekee inaweza kuwa suluhu ya matatizo yake. Dembele akahamia katika baa iliyopo jirani na nyumbani kwake.
Chupa moja baada ya nyingine zikazidi kusalia chupa tupu mezani. Na ulevi nao ukaingia kichwani.
Katika meza yake awali alikuwa peke yake lakini sasa akaanza kuona kama wapo watatu hadi wanne lakini cha ajabu kila akiwashika anaambulia hewa.
Alitambua kuwa sasa amelewa. Akafanya tabasamu dogo. Kisha akamimina kilevi zaidi katika glasi yake.
Alipoanza kunywa mara wale watu wakaongezeka tena. Akajaribu kuwashika.
Maajabu. Mara hii walikuwepo kweli. Wakamkamata mkono. Akajaribu kufurukuta akaona wanaonyesha vitambulisho.
Ulevi mwingi uliokuwa umemkabili hakuweza kusoma maandishi. Akahisi ni wezi wanataka kumuibia.
Akajaribu kufurukuta akakumbana na pigo kali katika shavu lake. Bia kadhaa alizokunywa zikatoweka mwilini.
Alipoongezwa mapigo mengine mawili fahamu zikamrejea vyema. Ikabakia harufu tu.
Aliweza kuvisoma vile vitambulisho.
Walikuwa ni askari!!
Alhamdulilah!!
Dembele akapagawa. Wakamvuta pembeni, wakamuuliza iwapo alikuja na gari. Akasema hapana!!
Wakaingia naye katika magari yao.
Vumbi likatimka. Ving'ora vikipiga mayowe.
Dembele akasindikizwa kituoni.
Wakati anashuka, suruali yake ilikuwa tepetepe kwa mikojo.
Askari mmoja akamcheka.
Moja kwa moja katika chumba cha mahojiano. Mwanzoni Dembele alijifanya mbishi, askari wakawa wabishi zaidi yake.
Lile tipwatipwa lilipominywa kidogo likatiririka mistari zaidi ya George.
Dembele akasema kila kitu anachofahamu.
Kwa uoga aliokuwanao akakiri kuwa ni yeye aliyemuua mke wa Kasuku. Maajabu!!


Maelezo yake ya awali yalitosheleza kwa askari hawa wazoefu.
Upesi sana wakatoweka wakiwa wameambatana na Kasuku hadi nyumbani kwa Dembele.
Msako ukaanza.
Msako wa ukombozi.
Chumba hadi chumba.
Kamata mke wa Dembele, kamata watoto. Wote wakatupwa katika kalandinga.
Msako ukaendelea katika vyumba vya siri. Huku ndipo walipopatikana, George, Mama George, Suzi, Frida, Isha. Mmoja hakuonekana.
Kimya kikatawala.
Mwanaidi!! Walikumbuka, jina hili halikuwa katika orodha ya waliopatikana japo katika maelezo yumo.
Msako haukukoma, uliendelea hadi pale alipopatikana. Akiwa hawezi kusema neno. Alikuwa ametulia tuli uso wake ukitazama mkoba uliokuwa mbali naye, mikono yake ikiwa kama inayohitaji kuuchukua mkoba ule. Lakini haikuweza kuufikia.
Wakambeba katika gari ya wazi, akakimbizwa hospitali.
Wale wengine wakafikishwa katika kituo cha polisi kwa usalama wao.
Walihifadhiwa pale hadi majira ya saa kumi na moja jioni.
Kila mmoja akiwa ametoa maelezo yake juu ya chochote alichokuwa anafahamu kuhusiana na maovu ya Dembele.


Majira ya saa mbili usiku yule diwani aliyenunua taarifa juu ya Dembele naye alikuwa mahabusu, kuingia kwake mahabusu kukaambatana na taarifa mbaya kupita zote katika riwaya ya CHOKORAA.
Yule mwanaharakati kijana kabisa, tena wa kike. Alikuwa amejaribu kuupigania uhai wake kwa namna zote lakini madaktari bingwa wakakiri kuwa hali si shwari na muda wowote anaweza kuiaga dunia. Ama la Mungu aweke mkono wake muujiza utendeke.
Kila mmoja aliumia kwa namna yake. Frida aliangua kilio.
Kwikwi ikamshika mama George.
George akaugulia kiume!!
Wote wakaomba kwa namna zao. Mwanaidi asipotee kirahisi hivyo katika uso wa dunia.


****


Makala ya Kasuku ilifanya vizuri sana katika magazeti.
Watu walibaki midomo wazi. Kwa wote waliomfahamu Dembele walibaki wakijiuliza? Maswali yasiyo na majibu.
Hakuna aliyetegemea anaweza kuwa bwana mbaya namna ile.
Lakini ilibaki kuwa hivyo.
Baada ya bwana Dembele, kila aliyemsoma mwanadada jasiri, yatima na chokoraa aliyewapigania wenzake. Bila kuwa na mhimili na kisha kuishinda vita hii, alitamani kumuona.
Umri wa Mwanaidi uliwashangaza wengi. Haukuendana na harakati alizokuwa anafanya.
Harakati zile zilihitaji mtu msomi.
Mwanaidi akasubiriwa anyanyuke kutoka kitandani aweze kupewa heshima yake. Lakini hakuamka mapema kama wanavyotaka.
Hadi usiku mchana fulani ambapo Frida alikuwa amelala. Alishtuliwa na ndoto mbaya. Ndoto ya maajabu. Alishtuka na kujikuta akiwa anatokwa jasho lakini jasho pekee halikuwa linamtia kero, kuna kitu alikuwa anahisi kinamtokea kwa mara ya kwanza katika maisha yake.
Maumivu !! maumivu makali sana. Frida akajikaza lakini yaliongezeka, akapiga kelele kubwa, kelele ikavuka mipaka ikawafikia walengwa waliopewa kazi ya kumtunza.
Wakafika na kugundua kuwa binti huyu alikuwa ameshikwa na uchungu.
Upesi zikachukuliwa hatua.
Baada ya masaa kadhaa Frida alikuwa hoi huku macho yake yaliyolegea yakimtazama mtoto wake. Mtoto asiyekuwa na baba.
Japokuwa alikuwa amechoka sana aliweza kuwasikia manesi wakimpa hongera ya kujifungua mtoto wa kike.
"Mwana….Mwanaiiiidi." alijitutumua akakiita kitoto kile jina hilo.
Kikalipuka kwa kilio cha kitoto.
Jina kubwa!! Mwanaidi.


Kwa sababu Frida alikuwa bado kitandani hakupewa taarifa yoyote mpya juu ya maendeleo ya Mwanaidi aliyekuwa anapumulia mipira.
Lakini ndoto yake ya kuota kuwa anajifungua mtoto anayefanana na Mwanaidi huenda ilikuwa sahihi. Alikuwa amejifungua Mwanaidi mpya na kumbatiza jina hilohilo.
Alipopewa taarifa juu ya umauti uliomkumba Mwanaidi, alifanya tabasamu hafifu kisha akasema.
"Ili itimie ile ndoto. Ndoto ya Mwanaidi kuishi maisha mapya ya furaha akiwa na mzazi wake ambaye ni mimi. Ni muda wa kumtunza aliyenitunza na kuniokoa." Maneno yale yaliamsha hisia, George akawa wa kwanza kudondosha chozi. Frida akalipuka na kilio kisichozuilika. Alikuwa anamlilia Mwanaidi.
Bahati nzuri alikuwepo Mwanaidi mwingine kichanga.
Isha akiwa mama mdogo, George baba mlezi, mama George bibi, Suzi shangazi, Frida akibaki kuwa mama mzazi wa Mwanaidi mpya.
Yule shujaa wa mapambano, asiyeogopa kufa wala asiyehofu kuua, ugonjwa wa pumu ukautwaa uhai wake.
Alikufa akiwa anapambana, hakuwahi kupumzika kamwe.
Kwa kifo chake akawaokoa wengi!!


****


Mali za bwana Dembele zilitaifishwa baada ya kuwa amehukumiwa kumalizia maisha yake yote jela huku akisindikizwa na diwani ambaye alivuliwa madaraka kutokana na kuficha siri kubwa kama ile baada ya kuuziwa na hayati Mwanaidi kisha kuhukumiwa kifungo cha miezi sita jela, mali zile zikawekwa mnadani. Zilikuwa mali nyingi sana. Mauzo yake yakawezesha kujengwa kituo kikubwa cha watoto yatima. Ili kuenzi harakati za mapambano yale ya siku nyingi. Kwa heshima ya yule mtoto aliyekufa akipigania watoto kituo kile kikaitwa jina lake ‘MWANAIDI'.
Ilikuwa huzuni wakati wa kukifungua kituo hicho.
Utepe ulikatwa na yule mtoto mdogo aliyezaliwa na chokoraa kisha akaitwa Mwanaidi.
Maisha yakaendelea.


****
Muonja asali haonji mara moja.
George Emmanuel. Alikuwa muonja asali, na ladha ya shubiri hakuitambua. Suluba walizopitia wenzake yeye alikuwa hajazipitia kwa kiasi kikubwa hivyo.
Starehe alizoendekeza baada ya kuwa amepata pesa za bwana Dembele akaendelea nazo tena baada ya kupata kazi katika kituo kile cha watoto yatima cha MWANAIDI.
Starehe yake aliyoendekeza zaidi ilikuwa wanawake.
Ukiyaendekeza mapenzi lazima uupoteze uelekeo, George aliyaendekeza huku akiisaka ile ladha aliyoipata kwa yule binti wa kitanga aliyemuingiza katika ulimwengu huu.
Alijisahau kuwa aliwahi kuwa chokoraa, alisahau kila kitu akavimba kichwa.
Machoni pa watu alijionyesha kuwa yu mwema sana tena mkarimu lakini ndani alificha mengi. Alikuwa zaidi ya mchafu.
Frida na Isha walijaribu kumshauri, aliwasikiliza kwa makini na kuahidi kubadilika lakini kamwe haikuwa hivyo.
Kila yatima aliyekuja katika kituo cha MWANAIDI ilimradi alikuwa ni mrembo George alifanya juu chini ili aweze kushiriki naye mapenzi.
Yote haya yalifanyika kimyakimya. Bila mtu yeyote kutambua.
George alitumia pesa!!
Kweli pesa mwanaharamu.


Tabia hii ilizidi kukomaa hadi pale alipotembelewa na binti nyumbani kwake. Binti mrembo lakini asiye na tabasamu usoni pake.
George alijiuliza kwa nini binti huyu anashindwa kutabasamu?
Binti akaketi katika moja ya viti pale sebuleni.
Hakuongea neno kwa muda akawa anamtazama George.
Baadaye uso wake ukaanza kumeremeta kwa hasira. George akashangaa, lakini mshangao haukudumu sana yule binti akamvagaa, George ambaye hakuwa amejiandaa kwa shambulizi hili, akaanguka chini.
Binti juu yake. Binti mwenye hasira kali. Binti ambaye hadi wakati huo hakuwa amesema neno lolote lile.
Hata salamu hakuwa ametoa!!


***MWANAIDI amefutika katika uso wa dunia….lakini amezaliwa Mwanaidi mwingine…….je kuna mapambano zaidi??


**GEORGE anaendekeza uasherati…anasahau alipotoka……
Sasa ametembelewa na mgeni wa kike..mgeni hajasema neno ila amezua balaa….JE HUYU NI NANI NA KWA NINI AMEZUA BALAA??


mangimeza Khantwe culbby Toplady Igunga Moja BPM showtie Samaya
 
Last edited by a moderator:
Lol!! Kweli mtunzi mueledi kama wewe, akili uliituliza...
Umeniacha kwenye kiwewe, uroho na uchu wa kutaka kilichompata George,....
Naomba ikate kiu hii ya kujua yaliyoendelea ndani ya riwaya hii yenye visa visivyoisha utamu.
 
RIWAYA: CHOKORAA
MTUNZI: George Iron Mosenya


SEHEMU YA THELATHINI NA MBILI


Muonja asali haonji mara moja.
George Emmanuel. Alikuwa muonja asali, na ladha ya shubiri hakuitambua. Suluba walizopitia wenzake yeye alikuwa hajazipitia kwa kiasi kikubwa hivyo.
Starehe alizoendekeza baada ya kuwa amepata pesa za bwana Dembele akaendelea nazo tena baada ya kupata kazi katika kituo kile cha watoto yatima cha MWANAIDI.
Starehe yake aliyoendekeza zaidi ilikuwa wanawake.
Ukiyaendekeza mapenzi lazima uupoteze uelekeo, George aliyaendekeza huku akiisaka ile ladha aliyoipata kwa yule binti wa kitanga aliyemuingiza katika ulimwengu huu.
Alijisahau kuwa aliwahi kuwa chokoraa, alisahau kila kitu akavimba kichwa.
Machoni pa watu alijionyesha kuwa yu mwema sana tena mkarimu lakini ndani alificha mengi. Alikuwa zaidi ya mchafu.
Frida na Isha walijaribu kumshauri, aliwasikiliza kwa makini na kuahidi kubadilika lakini kamwe haikuwa hivyo.
Kila yatima aliyekuja katika kituo cha MWANAIDI ilimradi alikuwa ni mrembo George alifanya juu chini ili aweze kushiriki naye mapenzi.
Yote haya yalifanyika kimyakimya. Bila mtu yeyote kutambua.
George alitumia pesa!!
Kweli pesa mwanaharamu.


Tabia hii ilizidi kukomaa hadi pale alipotembelewa na binti nyumbani kwake. Binti mrembo lakini asiye na tabasamu usoni pake.
George alijiuliza kwa nini binti huyu anashindwa kutabasamu?
Binti akaketi katika moja ya viti pale sebuleni.
Hakuongea neno kwa muda akawa anamtazama George.
Baadaye uso wake ukaanza kumeremeta kwa hasira. George akashangaa, lakini mshangao haukudumu sana yule binti akamvagaa, George ambaye hakuwa amejiandaa kwa shambulizi hili, akaanguka chini.
Binti juu yake. Binti mwenye hasira kali. Binti ambaye hadi wakati huo hakuwa amesema neno lolote lile.
Hata salamu hakuwa ametoa!!




George hakutegemea shambulizi la ghafla kutoka kwa binti yule ambaye walikuwa wanaheshimiana sana na waliwahi kupeana ahadi za kuja kuoana siku moja japo kwa kipindi hicho kila mmoja alikuwa akiishi kivyake.
George akaduwaa, wakati huo tayari alikuwa amekabwa koo na binti yule. Akataharuki huku akijaribu kujilazimisha kutabasamu.
"We Suzi wewe ni nini kwani?" akauliza huku akijaribu kujing'atua kutoka katika mikono ile.
Yule binti hakujibu kitu chochote. Aliendelea kumkaba kwa nguvu George, sasa alikuwa anatetemeka na alitokwa jasho.
Sasa George akaamua kutumia nguvu za ziada, akafanikiwa kujiondoa katika dhahama ile. Binti hakukoma akamkabili tena George, George akajitetea kwa kurusha vibao viwili, vikampata barabara Suzi, hapa morali ikashuka kiasi, George akacharuka akamkabili tena akamnasa vingine viwili mgongoni. Suzi akapiga mayowe. George akatulia lakini ndita zikiutawala uso wake.
Suzi akaugulia kwa dakika kadhaa kisha akaunyanyua uso wake ulioiva kwa hasira na uchungu wa kunaswa vibao, akamtazama George.
George akawa wa kwanza kukwepesha macho yake wasiweze kutazamana.
Suzi bila kusema neno akamkabidhi George kipande cha karatasi kisha akatoweka akiubamiza mlango kwa nguvu sana.
George akasonya.
Baada ya Suzi kutoweka, George alifungua kile kikaratasi, akakitazama kwa makini.
Kiliandikwa jina la Suzi kwa usahihi kabisa kisha ukafuata mwandiko usioeleweka. Lakini ulifikia mahali ukaeleweka.
Kijasho chembamba kikaanza kumtoka George, akajiuliza endapo yu sahihi ama la. Akavuta kumbukumbu na kujiuliza ‘Chanya na hasi' zina maana gani.
Hakuwahi kulipenda somo la baiolojia hapo awali, hii ilikuwa ni sababu tosha ya yeye kutatizwa na mambo hayo. Akajaribu kuvuta kumbukumbu kama aliwahi kusikia mahali vitu vilivyoandikwa katika karatasi ile. Akajiaminisha kuwa aliwahi kusikia lakini ni nini hicho.
Alitamani kumuuliza mtu lakini cha kusikitisha alikuwa peke yake katika himaya hiyo. Akachanganyikiwa.
Alichungulia nje endapo Suzi bado hajafika mbali, lakini binti hakuwepo kabisa.
Kizungumkuti.


****


Msichana mkiwa alikuwa chumbani akitathimini juu ya maneno makali aliyotoka kuelezwa na msichana mwenzake. Picha iliyokuwa inaonekana katika luninga ilifanana na kivuli kisichotazamika na kueleweka. Macho yake yalitawaliwa na ukungu na hatimaye chozi likamdondoka.
Kadri alivyokuwa analia alijenga picha ya maisha yake ya nyuma.
Akahisi huenda amelaaniwa.
Ndio. Amelaaniwa, maana matatizo hayamuishi na inapojaribu kuja amani, tatizo jipya linajitokeza na amani inatoweka.
Matatizo yaliyotokea kipindi cha nyuma yalikuwa na ahueni kwani yalikuwa na suluhu lakini hili la sasa ni janga. Janga litakaloteketeza kizazi kikubwa.
Isha alikuwa amepewa taarifa juu ya hati hati ya kuwa katika msafara wa kifo.
Licha ya kupitia magumu mengi lakini Isha hakutaka kufa. Alichukia kutangulia.


Akiwa kama mzimu ama roboti linaloongozwa na mitambo, Isha alisimama, akaufunga mlango wa chumba chake huku akiiacha luninga ikipiga kelele bila mtazamaji.
Akaongoza njia akachukua usafiri. Akamuamuru dereva akampeleka anapohitaji kwenda.
Mwanzoni alihisi itakuwa jambo dogo tu kufanya alichopanga lakini kadri alivyozidi kukikaribia chumba alipatwa na mfadhaiko ambao ulimfanya ajifikirie kughairi. Lakini kabla hajafanya maamuzi ya kughairi alisikia akishinikizwa. "We dada si uingie ametoka mtu tayari"
Isha akaingia, ana kwa ana na mwanaume mnene aliyevalia mavazi ya kawaida tu ya vijana yaliyomuweka katika unadhifu.
"Shkamoo." alisalimia.
"Marahaba, karibu…"
"Asante….nahitaji kuchukua vipimo….vipimo vya …vya UKIMWI."
"Ok. Chumba cha tatu kutoka hapa, utaona mlango umeandikwa ‘USHAURI NASAHA NA KUPIMA' ingia hapo utapewa maelekezo." Alijibu daktari na kutoa maelekezo nyoofu.
Isha akaaga na kuelekea sehemu husika.
Huko akafuata maelekezo na baada ya nusu saa alikuwa ana kwa ana na mshauri wa kike, sauti yake ilikuwa inabembeleza lakini ikiongea mambo ya kumtisha Isha. Kabla ya kumweleza majibu yake ni mazuri ama mabaya alisisitizwa kula vizuri iwapo atakuwa ameathirika.
Maneno hayo yaliupondaponda moyo wa Isha.
Na mwisho wa siku majibu yakafanana na aliyotabiriwa na Suzi alipomtembelea nyumbani kwake na kumueleza hali halisi.
Isha alifanya igizo la kisasa. Mshauri hakujua kama ana hasira kali ndani yake, akahisi Isha ameelewa vyema na hatafanya kitu chochote kibaya.
Isha aliaga kwa miadi ya kufika tena hapo baada ya juma moja.
Safari hii hakurudi nyumbani bali alielekea katika soko dogo pembeni kidogo na hospitali akanunua kisu kipya. Akakitia katika pochi yake.
Akachukua taksi ambayo ilimpeleka moja kwa moja mahali alipohitaji. Akashuka kituoni na kuanza kutembea hima kwa miguu, ni kama alikuwa haoni mbele na alikuwa ametaharuki.
Yule roho wa mauaji aliyedhaniwa amefukiwa kaburini pamoja na marehemu Mwanaidi alikuwa hai tena katika kifua cha Isha. Isha alijenga chuki kuu dhidi ya George.
Isha akiwa na asilimia mia za kuwa muaminifu katika maisha yake na George, lawama zote zilimwangukia kijana huyu mtanashati.
Akayakumbuka machungu ya mimba yake kutoka kisa kikiwa ni George, kwa hilo alimsamehe. Sasa amemwambukiza UKIMWI kwa hili hapakuwa na dalili ya msamaha.
Maneno ya Suzi yakajirudia kichwani mwake, "Amenipiga sana hakutaka kunisikiliza lakini nimemwachia majibu mezani kwake. George si mwanadamu!!" Suzi aliyazungumza haya akiwa analia, isha naye akaanza kutokwa machozi.
"Amewaua wengi sasa ni zamu yake." aliapa wakati anaukaribia mlango. Ujasiri usio kifani uliitawala nafsi yake.
Alipokaribia katika makazi ya George, alipatwa na wazo.
Kuua kwa kisu!! Hili likaonekana kuwa jambo gumu sana.
Mwanaidi pekee anayaweza mambo haya!! Isha alikiri kimya kimya.
Ghafla akaubadili uelekeo na kulitafuta duka.
Huku akafanikiwa kuipata sumu kali ya panya.
Isha akaamua kumtokomeza George kwa kutumia sumu ya panya.
Akanunua na maji akanawa uso wake ili asionekane kama alikuwa anatoka kuangua kilio muda mfupi uliopita.
Zile dakika zilizopotea kwa kwenda kununua maji na kununua sumu ya panya zilikuwa dakika za kujutia maisha yote kwani George naye alikuwa katika maandalizi ya mwishomwisho ya kuelekea anapojua yeye. Begi dogo begani, akatoweka akikiacha chumba katika upweke.
Isha alipofika alipokelewa na chumba kisichokuwa na uhai.
Alingoja sana lakini hakuna kilichobadilika.


Alijaribu na siku iliyofuata lakini hali ilikuwa vilevile. Hatimaye taarifa rasmi ikasambaa kuwa George kiongozi wa kituo cha watoto yatima cha MWANAIDI haonekani nyumbani kwake.
Hofu ikatanda.
Msako ukapita, lakini hali bado ilibaki vilevile.


****


**GEORGE hajulikani alipo….ISHA na SUZI wameathirika….mtuhumiwa wao namba moja ni GEORGE……


***ISHA ana nia ya kuua….je atafanikiwa…na nini kipo kichwani mwa SUZI???


ITAENDELEA

muuza ubuyu culbby betrecious23 Jullie Z
 
Last edited by a moderator:
George bana.... umalaya weee mwishowe umeukwaa, haya ngoja tuoone umekimbilia wapi
 
Janga juu ya janga ... wengi husahau magumu yaliyopita
 
RIWAYA:CHOKORAA
MTUNZI:George Iron Mosenya
CONT:0655 727325

SEHEMUYA THELATHINI NA TATU

Viungovyote vikasita kufanya kazi, yakabakia masikio ambayo yalisikiavishindo vya miguu kuelekea katika chumba kile. Vishindo hivyovikaambatana na sauti zinazovuma mithili ya kelele. Mwanaidi hakuwezakutikisika.
Picha mbalimbali zikaanza kumpitia katika akili yake.Anazaliwa, anakulia mitaani, anachukuliwa na mjomba wake, anafukuzwakwa kumsaidia Frida.
Anarudi kituo cha watoto yatima,anafukuzwa akiwa na Frida, anamsaidia Frida kutoa mimba, anakaribiakupoteza uhai kwa ugonjwa wa pumu, anaokolewa na mama mbaya muuzamiili ya wasichana, anauzwa kwa mwanaume anayetaka kumlawiti, kwamara ya kwanza anafanya mauaji, mara picha ya mama muuza miiliakiuwawa nayo ikampitia, anakutana tena na Frida na Isha,wanaunganika na George, George anawekewa sumu, Frida na Ishawanakamatwa, anakutana na mama yake George akiwa mlemavu.
pichazinaendelea kwa kasi ya ajabu. Mwili unapatwa joto kali sana.
Jasholinatiririka.
Kiza kinazidi kutanda.



****

Ishaalikuwa amemlilia Mungu pasina kupata dalili zozote za majibu yaupesi, hali ya upweke ilimkosesa amani kabisa na alipofikiria juu yakubakwa akazidi kufadhaika.
Aliyafikiria maisha yake yalivyozongwana sintofahamu ndani ya juma moja tu. Tayari alikuwa amesalitiwakatika mapenzi, katika kuifuatilia haki yake hiyo anakumbana nakimbembe cha kupigwa na wasichana watatu. Anapoteza fahamu,anapozinduka anapokea taarifa kuwa mimba yake iliharibika kutokana nakipigo kile. Anabaki hospitali kwa matibabu, anapopata ruhusa yakurejea nyumbani hata bila kutulia zaidi anakutana na balaa lakutekwa na sasa yu mpweke katika chumba kipweke.
Ghafla akaijiwana wazo tena lililomghafirisha, Isha akayakumbuka maneno mazitokutoka kwa mama George usiku ule wa kwanza na wa mwisho kuwa pamoja.Mama Yule alizungumzia juu ya bwana huyu ambaye anahusika katikakusafirisha madawa ya kulevya.
Kumbe ametuteka ili atutumiekusafirisha madawa!! Isha alijiuliza na kujikuta akiwa anapingana naukweli.
Lakini atafanya nini? Hili likabakia kuwa swali zito na laaina yake.
Kifo!! Hili likasafiri katika akili yake. Isha akaaminikuwa ni heri kufa kuliko kufanyishwa kazi zile zilizoliharibu kabisatumbo la mama George. Isha hakuwa tayari kukabiliana na maumivuyale.
Sasa atakufa vipi? Hili nalo likaingia katika mfululizo wamaswali aliyokuwa anajiuliza, akatamani itokee sumu aweze kunywalakini muujiza huo haukuwa mwepesi, akatamani walau kijitokeze kisu,ama kamba ajinyonge. Bado haikuwezekana.
Macho yaliyokata tamaayakainuka na kukutana na ule ukuta mweupe katika kile chumba. Wazo laujasiri usiokuwa kifani likaandamana katika fikra zake, akasimamawima na kuamua kujiua katika namna ya ajabu namna isiyotamanishakusimulia.
Isha aliyebakwa akaamua kuuvamia ukuta ule kwa kutumiakichwa chake, lengo likiwa moja tu kukikutanisha kichwa chake na uleukuta ili aweze kutokewa na lolote ambalo litatokea. Aidha kifo amalolote lile.

Ni heri kukumbwa na wazimu kuliko kukutana nayule mwanaharamu kwa jina Dembele. Ambebeshe madawa ya kulevya kishaamuue, ama la wale wabakaji waendelee na ile tabia yao katika mwiliwake…..
Wakati akitegemea kukutana na kishindo kikubwa kwakichwa chake kukutana na ukuta, hali haikuwa hivyo. Ule mwendo wakeakajikuta amesukuma kitu ambacho kilizidiwa uzito na kuachana Ishaakapenya.
Lahaula! Hakuwa amekufa wala kurukwa naakili……alipofumbua macho alikuwa katika chumba kingine….alionatundu la mahali ambapo alikuwa amepenya, kumbe ule haukuwa ukuta kamaalivyodhania awali.
Mara akahisi kitu kingine tena, hakuwa pekeyake katika kile chumba. Wazo likamjia kuwa yu katika chumba kimojana wale wabakaji wasiokuwa na huruma hata kidogo. Akageuza shingoyake taratibu aweze kukabiliana na ukweli, maajabu mengine alikutanana macho yakiwa yamekodolewa katika namna ambayo hakuwahi kuona hapokabla, hakuhitaji dakika ya ziada kuhisi jambo. Hapana hazikuwa hisiailikuwa ni kweli…..alikuwa yeye……
Mwanaidi shujaa wa kikeasiyeogopa lolote alikuwa taabani. Alikuwa anahangaika, alikuwaamenyoosha mkono wake bila kutikisika, midomo ilikuwa wazi kabisa najicho lilikuwa limekodolewa kuelekea mahali…..kulikuwa kuna kitu.Ni hapa Isha alipoikumbuka ile siku ambayo alikutana na Frida maeneoya posta akiwa amepotea, alimueleza kuwa rafiki yake aitwaye Mwanaidialikuwa amekumbwa na ugonjwa wa ajabu alipoenda kumtafutia dawaakapotea. Kwa wakati ule hakuwa na mahali pa kwenda. Ni siku hiyoIsha alivyoanza kuishi rasmi na Frida.

Sasa anakutana naMwanaidi akiwa na ugonjwa uleule ambao Frida aliwahi kumweleza.Ugonjwa wa Pumu.
Kumbe mtu akitaka kufa n'do anafanania hivi!!!Alijisemea Isha katika namna ya kustaajabu. Lakini hakutaka mfano wamtu kufa mbele yake uwe Mwanaidi….
Upesi Isha akatazama tenajicho la Mwanaidi, lilikuwa limekodoa kutazama mahali, akalifuatishana kukutana na kitu mfano wa mkoba mdogo.
Kwa nini anautazamamkoba huo. Isha hakutaka kumuuliza yeyote maana alijua hatakuwepo wakumjibu. Kwa mara ya kwanza akashukuru kwa hali ile aliyokuwa nayo,laiti kama angekuwa mjamzito huenda asingeweza kuthubutu kujirushanamna ile. Isha alizirukia mbao moja baada ya nyingine hadi akaufikiamkoba ambao ulitupwa kule juu wakati Mwanaidi anasulubiwa. Ulikuwamkoba mdogo ambao Mwanaidi hutembea nao mara kwa mara, Isha akajivutazaidi na sasa alikuwa akitembea katika ‘kenchi' kwa kunyata…….
Nihuku alipokutana na jambo ambalo lilimfanya afanye kitendo ambachohakutarajia na mwisho kuleta mikikimikiki.

****

BADALAya kumtumia pesa yote kwa njia ya simu, Zainabu aliamua kukutana naMeja faragha kidogo ili waweze kuzungumza zaidi japo hakumweka wazianahitaji wazungumze jambo gani jingine. Meja aliendesha gari upesikuelekea nyumbani kwa Mama Sakina kama ambavyo alikuwaameelekezwa.
Baada ya saa zima walikuwa wakizungumza juu yatukio ambalo Meja alikuwa amelishuhudia. Hapakuwa na neno jipyalililoongezeka katika maongezi yale, maswali ya Zainabu na maelezoyake n'do yalimuweka Meja mdomo wazi. Hakutegemea hata kidogo Yulemama wa kiislamu anaweza kufanya kitendo alichokifanya na kijanaGeorge wakati yupo ndani ya ndoa….
"Meja nilijikuta tu nafanyahivyo usinilaumu…"
"Ona sasa umemtakia balaa mwenzio..mtotomdogo Yule umemuingiza katika kash kash kama hiyo. Utamtoaje sasapale." Alilaumu Meja.
"N'do maana nipo na wewe hapa nahitajimsaada zaidi, nahitaji kufahamu kwa nini anampa vitisho hivyo na pianahitaji kujua huko ndani anafanywa nini na pia Meja anampango ganina mimi." Alizidi kuelezea. Meja akatikisa kichwa kumaanisha kuwaamemuelewa.
Zainabu akatoa kiasi cha pesa bila kuhesabu,"Ukimaliza hiyo kazi nitakuongezea" akasindikiza na manenohayo.
Meja akazipokea bila kusema lolote. Wakaagana.

****

MEJAalianzia upesi eneo la Mchikichini, huko akafanya upelelezi wa harakasana na kugundua ni wapi George alikuwa anaishi. Bila kuhitajikusindikizwa yule mwarabu akatuliza akili na kufahamu fika mahaliambapo George alikuwa anaishi. Huku akakutana na neno la ziada kuwaGeorge alikuwa anaishi na mwanamke aitwaye Isha, pia akafahamu kuwaGeorge alikuwa Chokoraa ambaye n'do kwanza anaanza kujikwamuakimaisha…..
Kama hiyo haitoshi Meja anasimuliwa mkasa wakuonekana kwa mama mmoja akiwa na mkewe George wakihangaika kumtafutaGeorge bila mafanikio kisha katika hali ya kushangaza nyumbani kwaGeorge wakatokea wageni wa ajabu, wageni ambao waliwalazimisha yulemama pamoja na mke wa George kuondoka nao.
Huo ukawa mwisho wakuwaona hadi wakati ule waliokuwa wanazungumza na Meja.
"He!Wamempeleka wapi tena ticha wangu dah!! Ujue nasoma elimu ya watuwazima….siu unajua mambo ya elimu tena hizi…" akasita hukuakijichekesha kama ambaye ameona aibu kusema jambo lile la kuwa yeyeni mwanafunzi.
"…kwa hiyo n'do ananipiga msasa kidogo."Meja akamalizia kuteka akili za majirani wawili waliokuwa wamechotwaakili zao bila kujua.

Hata alipoondoka tayari alikuwa na jambola ziada. Kumbe George ni yatima na mke wake naye ni yatima, na huyomama ni nani haswa? Na kwa nini watoweke baada ya Georgekutoweka.
Hapa kuna jambo la ziada huenda ambalo hata mama Sakinahalijui na halimuhusu!! Meja alijisemea kwa sauti ya juu kidogo hukuakiingiza gia katika gari na kutoweka.
Alipoyafikia mataa,aliyatazama kwa makini kisha katika yale mataa ya barabaranialijikuta akirejea akili zake nyuma miaka mingi sana ya msoto nchiniSudani, alipoishi maisha ya kutomjua baba wala mama, aghalabu hatandugu mmoja. Wote hakuwajua.
Maisha yaliyomkutanisha nawasaliti na vizingiti…akaishi kila aina ya maisha magumu nakujikuta akiwa na mi8aka kumi na tatu akijua vyema matumizi yabunduki.
Alishikishwa bunduki huku akisisitizwa kuwa ni vyemaakamate mtutu na kulipiza kisasi kwa watu waliowaua wazazi wake, ilesumu ikamwingia yatima yule akatenda waasi walivyotaka….
Kadrialivyozidi kuwasiliana na wenzake ndivyo alivyozidi kubaini kuwa ulemtutu aliokuwa anaushika ni kwa manufaa ya watu kadhaa na si kwakulipa kisasi., akaamua kuitupa Bunduki na kurejea mtaani akiwayatima vilevile kama awali.
Huku akakutana na vijana wenginewaliomwonyesha njia na kumwingiza katika biashara haramu ya kuibasilaha na kuuza kwa kwa wageni wanaotembelea nchi hiyo kwa sababu zaobinafsi. Ni huku alipokutana na mzee Barghash, mwarabu kutokaTanzania. Wakaanza urafiki, mara ya kwanza wakiuziana silaha, mara yapili akimsaidia kuijua mitaa kadhaa ya Sudan na mipaka na namna yakupenya kwa njia za panya. Ilikuwa rahisi kwa wawili hawa kuwasilianakwa sababu msudani huyu alikuwa anafahamu baadhi ya maneno yaKiswahili.
Damu zao zikaendana na hatimaye siku moja akaamuakurejea Tanzania akiambatana naye…..huu ukawa mwanzo wa kuitambuamaana ya amani isiyokamilika…amani inayokosa watu muhimu wakuifanya iitwe amani.
Amani bila ndugu wa damu yako hasahasawazazi, inakosa maana.
Honi za magari mengine zilimfumbua macho nakugundua kuwa mataa ya kijani yalikuwa yamewaka. Akarejesha akiliyake barabarani na kukanyaga mafuta. Gari ikapepea kuelekea kulealipokuwa anaenda.

Mawazo yaliyopenya katika kichwa chake kwakipindi kifupi yakamfanya ajengeke kihisia fulani. Akahisia anatakiwakujua jambo kutoka kwa yatima wenzake. Japokuwa umri ulikuwa umeendawa kujiita yatima lakini bado alikuwa ana kumbukumbu ya kuzaliwayatima na kuishi kiyatima.
Gari lake akaliegesha katika baa fulanimita nyingi kidogo kutoka katika nyumba ya Dembele. Akaagiza mchemshowa kuku, akaanza kujilia taratibu huku akitegea muda fulani ufikeaweze kufanya kile alichotakiwa kufanya.
Saa mbili usikuakajikongoja kwa mwendo wa miguu, umri wake wa miaka 40 haukufananiahata kidogo na umbo lake, alikuwa amekomaa na haikushangazwa kamaungeweza kumkadiria kuwa na miaka 28. Alikuwa mkakamvusana.
Alilifikia geti la ile nyumba. Akabofya kengere ya mlangoakangoja kwa dakika tano mlango ukafunguliwa.
Jambo la kwanza Mejaakawahi kumtazama mtu aliyefungua geti. Hakuwa mlinzi na ni mtuambaye alionekana kuwa na wasiwasi na hakutarajia ujio wa mtu yeyotekatika nyumba ile.
"Samahani eti Ndesamburo yupo…" aliulizakwa kitetemeshi kana kwamba anahofia umaridadi wa yulekijana.
"Hakuna mtu kama huyo hapa aisee…." Alijibu kwaghadhabu kisha akafunga geti kwa nguvu. Meja akajifanya kuduwaa,wakati alikuwa anatafuta sababu ya kuweza kuchungulia ninikinaendelea ndani.
Kupitia tundu dogo akamwona yule kijanaakirejea ndani.
Hapakuwa na mlinzi!! Meja akapata jibu.Akajipapasa kiunoni mwake akakisikia kitu kigumu ambacho huwahakitumii mara kwa mara isipokuwa kwa shughuli nyeti tu anazofanya namzee Barghash. Mafia asiyejitangaza hadharani….

Kwa wepesiakasogea nyuma biula kupoteza muda, alijua kuwa kwa muda ule kamakuna watu wengine ndani basi watakuwa wakisimuliana juu ya ujio wakekatika himaya n ile. Jambo ambalo litawapumbaza na kushindwa kutiliamaanani jambo jingine geni. Meja akanyata na kuona kipande cha ukutaambacho kilikuwa kirefu lakini kikipokelewa na mti wa mwembeuliochungulia nje. Meja akafaya tabasamu hafifu. Kisha akarudi hatuakadhaa nyuma na kujirusha akanasa alipotaka, akajitutumua hadiakafika juu, kwa uangalifu kabisa akanasa katika ule mwembe.
Akatuliakwa sekunde kadhaa kisha akaanza kushuka. Wakati anashuka akakutanana kitu kilichomtia faraja nyingine. Akaliona tundu……vioo vyakuingia katiuka choo cha ndani vilikuwa wazi, Meja akashuka hadichini kisha akasogea hadi katika kile choo, akatulia kama kivulikusubiri matokeo yoyote. Hakikutokea kitu.

Akajirusha na kutuandani ya kile choo kama aliyepita kimiujiza tu na kuwa pale ndani.Akaangaza huku na kule, kisha akajituliza kiakili kwanza. Akatakakuufunga mlango wa chooni ndipo aliposikia hatuazikisogea kuelekeakatika choo hicho.
"Oya mi nalala kabisa nyie mafala endeleenina filamu yenu hiyo." Sauti ilisikika, haikuwa mara yake ya kwanzakuisikia. Na hakuhangaika sana kutambua kuwa ni yule bwanaaliyemfungulia geti na kumjibu kwa dharau.
Meja akaendelea kutuliavile vile akamsikia akipiga mluzi, bila shaka kabla ya kulalaalihitaji kuanzia chooni. Maana mluzi ulielekea sana kule.
Hakikailikuwa hivyo. Mlango ukatikiswa, Meja akajiweka nyuma ya mlango ule.Yule kijana akiwa uchi wa myama akaingia bila shaka alikuja kwa ajiliya kuoga. Akiwa kama ----- alianza kupiga miluzi huku akikata viuno.Mara akaanza kuongea mwenyewe.
"Lile ----- kwenye ile filamulinapiga aisee, yaani mfano pale hivi ndo ningekuwa mimi daah yuledemu simuachi, yaani nimemsaidia vile halafu nimwachie aahwapi….halafu karembo aisee…..wanafaidi sana hawa jamaa. Hapoukute baada ya filamu wanaenda kumalizana aah….kudadeki usikunamzamia yule demu chumbani kwake nambaka kama hataki kwaniatanifanyaje….halafu siwaambii hawa mabwege maana watakomaa tupigewote…." Kadri alivyozidi kuzungumza ndivyo maungo yake yalizidikuwa magumu kisha yakasimama wima……

Mara akachezwa na kitukama machale kuwa nyuma yake kuna mtu anamtazama. Alitaka kugeukalakini akahisi kuwa ni mawazo yake hafifu tu. Akabaki kujitazamajinsi maungo yake ya uzazi yalivyokakamaa. Hakika jamaa alikuwakwenye uhitaji.
Na wazo alilokuwa nalo ni kwenda kumbaka tenaIsha.
Machale yalivyomcheza kwa mara ya pili, alifungua bombalinalotoa maji kwa juu. Yalipoanza kummwagikia akageuka aweze kutwaasabuni, ni hapo alipokuta na kituko.
Yule mgeni mshambaaliyemwacha solemba getini. Sasa alikuwa pale bafuni.
Uumeukasinyaa ghafla kana kwamba haukuwahi kuwa wima hapo kabla.
Akatakakupiga mayowe. Meja akamuwahi kooni.

Akamnyanyua juujuu. Akahakikisha kuwa analegea vilivyo.
"Ni maelezo yako pekeeyanaweza kukutoa huru humu ndani ili ukafanye huo ubakaji wako kwaamani kijana." Mwarabu mweusi alizungumza kwa utulivu na kwa sautiya chini sana.
Yule kijana sasa akajikuta akitokwa na kojolisilotarajiwa. Ni kama alikuwa anaona mauzauza ya ajabu sana.
"Weweni nani na unafanya nini katika jumba hili la bwana mdogo."Alimuuliza huku akiwa amemdhibiti kiuhakika.
"Sikwambiichochote." Alijaribu kuweka jeuri lakini Meja alikuwa jeuri wamajeuri.
Akamnyanyua juu kisha akakunja mguu wake na kuliweka gotikatika hatamu. Akaanza kumpiga na goti lile tumboni. Mapigo matatupekee. Kisha Meja akakiachia kichwa chake kikubwa kilichokomaakikatua katika paji lake la uso huku akiwa amemkaba koo asiweze kutoakelele zozote.
. .E bwana eee! Palepale haja kubwa ikamtoka yulebwege……na kuanzia pale akasema kila kitu alichokuwa anajua.
Kumbealikuwa ni daktari kabisa aliyeajiriwa na serikali na anapokeamshahara mkubwa tu lakini nje ya hapo alikuwa anapasua matumbo yaraia wema na kutia madawa ya kulevya ndani yake. Na pale ndaniwalikuwa wanangojea kuwapasua wanawake wane na mwanaume mmoja. Usikuhuo walitarajiwa kumtoa mimba muhusika mmoja ili zoezi liweze kwendakama lilivyopangwa.
Huyu muhusika aliitwa Frida. FridaGereza.

Kujieleza huku kukamkera zaidi na kumtia hasira kuumzee Meja. Akaghafirika na kutokwa na tusi zito la nguoni kwa lughaya kiarabu.
Kisha akafanya kitendo ambacho hapo zamani kwakeilikuwa kawaida sana kukifanya hasahasa akikasirika.
Akaikamashingo ya yule daktari muuaji. Akaizungusha kwa nguvu, akatulia hivyokwa sekunde kadhaa.
Ile zawadi ya uhai ambayo daktari alikuwaamepewa na mwenyezi Mungu ikaondoka zake hata kabla hajajisafishakutokana na tendo la kutokwa na haja kubwa na ndogo kwa pamoja.
"Wefala ndo kuoga huko au unapiga masterbation…" ilisikika sautikutoka nje ikiuliza lakini haikutilia maanani kuhusu jibu.
Mejaakacheka kwa sauti ya chini kidogo ili azidi kuwahadaa kabla yakuwavamia kiaina nyingine.

BAADA ya kuhakikisha pametulia tenaalipanda juu kidogo akasukuma kiubao kilichokuwa kinaziba tunduambalo nyumba inatumia kupumua. Ni hapa alielekezwa kuwa pana njia yakuingia katika dari.
Alipohakikisha kuwa hakudanganywa. Alishukatena akaufunga vyema mlango wa choo kile kisha akapanda juu. Kwaustadi wa hali ya juu akaanza kutambaa akivitafuta vyumba ambavyowamehifadhiwa binadamu waendao kwa majina ya George, mama George,Isha,Mwanaidi, na Frida.
Meja alikiri kauli yake ya awali kuwaanaenda kukutana na jambo ambalo hata Mama Sakina pekee halijui. Hiiilikuwa zaidi ya wazo lake kuwa amefumaniwa. Hii ilikuwa kivinginekabisa.
Ulikuwa ni ukiukwaji wa haki za binadamu.
Alipitishamawazo hayo huku akinyata kwa umakini wa hali ya juu sana. Maraakakutana na tukio la ajabu zaidi na lililomshtua na kufikia hatua yakutoa bunduki yake aweze kuitumia.
Ana kwa ana na kiumbe kama pakamkubwa wa kutisha akiwa anahaha kutembea katika dari. Upesi akatoabunduki yake kiunoni. Mara ghafla yule paka akapiga kelele akisema‘mamaaaa' hii ilishangaza sana paka anasema mama? Haya yalikuwamaajabu ya pekee.
Haiwezekani……

Kishindo kikasikika!Meja akataka kukimbia kurejea chooni lakini akajipa imani kuwabunduki yake ipo kumpa ulinzi.
Akanyata tena hatua kadhaa kishaakatazama chini, huku sasa akawaona wanadamu wawili.
"He! Inamaana yule paka amegeuka kuwa mwanadamu ama sikuona vizuri. Tenamsichana tazama…" Meja aliyasema haya huku akimtazama Isha naMwanaidi waliokuwa wametulia tuli sakafuni.

**ISHA katikaharakati za kumwokoa MWANAIDI lakini anakumbana na MEJA juu yadari…je nini kitaendelea…..

***MEJA Amemuua daktarichooni, je? Siri hii itadumu kwa muda gani? Na je ikifichuka Mejaataweza kupambana hadi mwisho??

NI KIZAAZAA CHA UHAKIKA!!!!
mlyn ram Khantwe muuza ubuyu culbby BPM Jullie Z
 
Sehemu hii kama imenichanganya vile, naona tumerudi nyuma tena, sehemu iliyopita mwanaidi alishafariki na isha alikuwa ana mtafuta George akiamini amemwambukiza ukimwi na George ametoweka, sasa mtunzi sijui hapa inakuwaje?
 
Sehemu hii kama imenichanganya vile, naona tumerudi nyuma tena, sehemu iliyopita mwanaidi alishafariki na isha alikuwa ana mtafuta George akiamini amemwambukiza ukimwi na George ametoweka, sasa mtunzi sijui hapa inakuwaje?

Hii yaitwa flashback
 
Yee bh'agosha utoro huu!! ila hii 33 naiona kama chips makande vile, sijapata ladha kabisa mkuu Casuist
 
Last edited by a moderator:
RIWAYA: CHOKORAA
MTUNZI: George Iron Mosenya




SEHEMU YA THELATHINI NA NNE


Meja alikiri kauli yake ya awali kuwa anaenda kukutana na jambo ambalo hata Mama Sakina pekee halijui. Hii ilikuwa zaidi ya wazo lake kuwa amefumaniwa. Hii ilikuwa kivingine kabisa.
Ulikuwa ni ukiukwaji wa haki za binadamu.
Alipitisha mawazo hayo huku akinyata kwa umakini wa hali ya juu sana. Mara akakutana na tukio la ajabu zaidi na lililomshtua na kufikia hatua ya kutoa bunduki yake aweze kuitumia.
Ana kwa ana na kiumbe kama paka mkubwa wa kutisha akiwa anahaha kutembea katika dari. Upesi akatoa bunduki yake kiunoni. Mara ghafla yule paka akapiga kelele akisema ‘mamaaaa' hii ilishangaza sana paka anasema mama? Haya yalikuwa maajabu ya pekee.
Haiwezekani……
Kishindo kikasikika! Meja akataka kukimbia kurejea chooni lakini akajipa imani kuwa bunduki yake ipo kumpa ulinzi.
Akanyata tena hatua kadhaa kisha akatazama chini, huku sasa akawaona wanadamu wawili.
"He! Ina maana yule paka amegeuka kuwa mwanadamu ama sikuona vizuri. Tena msichana tazama…" Meja aliyasema haya huku akimtazama Isha na Mwanaidi waliokuwa wametulia tuli sakafuni.






Usilolijua ni sawa na usiku wa kiza kinene. Hali hii ilimkabili bwana Dembele pia, baada ya kuwa amewamiliki mateka hawa katika himaya yake ya siri akafikiri sasa yupo huru, hakutambua kuwa hakuna siri inayodumu milele, na sasa siri yake ilikuwa imetapakaa, na alikuwa ananuka hatia. Hatia mbaya zaidi ya ambavyo angeweza kudhani.
Tamaa zikamponza.
Amakweli mshika mbili moja humponyoka.
Dembele alikuwa anatamani kuua na wakati huohuo akatamani kuwatumia wale wafu watarajiwa katika biashara yake ya madawa ya kulevya.
Ngoja ngoja hii ikamponza. Hakuwa na mtu wa kumshauri, akahisi pombe pekee inaweza kuwa suluhu ya matatizo yake. Dembele akahamia katika baa iliyopo jirani na nyumbani kwake.
Chupa moja baada ya nyingine zikazidi kusalia chupa tupu mezani. Na ulevi nao ukaingia kichwani.
Katika meza yake awali alikuwa peke yake lakini sasa akaanza kuona kama wapo watatu hadi wanne lakini cha ajabu kila akiwashika anaambulia hewa.
Alitambua kuwa sasa amelewa. Akafanya tabasamu dogo. Kisha akamimina kilevi zaidi katika glasi yake. Kasha akaitwaa simu yake akapiga namba Fulani.
"Fanyeni kazi yenu usiku huu..hakikisha mzigo wote unaondoka kesho kutwa asubuhi…..yule mwenye mimba naye ahusishwe hakuna kubakiza hata mmoja. Nimemaliza!!!" alizungumza huku akitokwa na matemate hovyo. Dalili tosha ya ulevi. Akaitua simu yake kisha akaitwaa tena pombe yake. Akagida mfululizo kabla ya kuitua chini chupa tupu.
Akatikisa chupa nyingine ambayo ilikuwa imefunguliwa tayari akataka kuifanyia ukatili ibaki tupu kama ile nyingine. Alipoanza kunywa mara wale watu aliowahisi mwanzo kisha akawashika na kuambulia patupu wakaongezeka tena. Akajaribu kuwashika kama awali.


Maajabu. Mara hii walikuwepo kweli. Wakamkamata mkono. Akajaribu kufurukuta akaona wanaonyesha vitambulisho.
Ulevi mwingi uliokuwa umemkabili hakuweza kusoma maandishi. Akahisi ni wezi wanataka kumuibia.
Akajaribu kufurukuta akakumbana na pigo kali katika shavu lake. Bia kadhaa alizokunywa zikatoweka mwilini kwa kasi ya ajabu.
Alipoongezwa mapigo mengine mawili fahamu zikamrejea vyema. Ikabakia harufu tu mdomoni.
Aliweza kuvisoma vile vitambulisho.
Walikuwa ni askari!! Askari wa jeshi la polisiTanzania.
Alhamdulilah!!
Dembele akapagawa. Wakamvuta pembeni, wakamuuliza iwapo alikuja na gari lake. Akasema hapana!!
Wakaingia naye katika magari yao.
Vumbi likatimka. Ving'ora vikipiga mayowe.
Dembele akasindikizwa kituoni. Hapo akiwa hajaulizwa kitu chochote kile.
Wakati anashuka, suruali yake ilikuwa tepetepe kwa mikojo, jicho likiwa limemtoka pima zaidi ya mjusi aliyebanwa na mlango.
Askari mmoja akamcheka.
Moja kwa moja katika chumba cha mahojiano. Mwanzoni Dembele alijifanya mbishi, askari wakawa wabishi zaidi yake.
Lile tipwatipwa lilipominywa kidogo likatiririka mistari zaidi ya George alivyofanya baada ya kutogwa sikio.
Dembele akasema kila kitu anachofahamu.
Kwa uoga aliokuwanao akakiri kuwa ni yeye aliyemuua mke wa Kasuku. Maajabu!! Hakuna aliyetarajia taarifa ile hata kidogo.
Kumbe hayawani anahusika!!!


Maelezo yake ya awali yalitosheleza kwa askari hawa wazoefu.
Upesi sana wakatoweka wakiwa wameambatana na Kasuku hadi nyumbani kwa Dembele.
Msako ukaanza.
Msako wa ukombozi.
Chumba hadi chumba.
Kamata mke wa Dembele, kamata watoto. Wote wakatupwa katika kalandinga.
Msako ukaendelea katika vyumba vya siri. Hakuna kilichopatikana huko.
Wakayakumbuka maneno ya Dembele kuwa mateka walikuwa katika nyumba yake nyingine, Kasuku alikuwqa anaifahamu akawaongoza maaskari katika jambo hilo.
Huku kikazuka kitimtim kingine cha aina yake ambacho kilinyamazisha mtaa kwa muda mrefu.
Hali ilikuwa imetulia kama kwamba eneo lile hakuna mtu hata mmoja. Askari hawakubabaika kutokana na hali ile wakaweka umakini katika kuendesha ule msako. Wakiwa na nguo zao za kiraia wakaizingira nyumba ile waweze kupenya.
Kupitia katika ukuta jicho moja kali ajabu kutokea katika eneo lisilofikirika liliona kiwiliwili kikihangaika kumalizia kupanda ule ukuta. Bunduki makini ikiwa katika kiwambo cha kuzuia sauti ilifyatuka na kutua katika chemba ya moyo barabara.
Yowe la hofu likasikika kutokea nje, mshambuliaji alikuwa na uhakika kuwa hajaikosa shabaha ile hivyo bila shaka kuna maaduio wengine walikuwa wamemtanguliza mwenzao kama chambo sasa ametua kama maiti. Muuaji akaweka hadhari ya hali ya juu. Macho yake yakafanya mzunguko mwingine mkali, akakutana na kichwa kikimangamanga huku na kule. Mara macho yao yakagongana, yule askari alikuwa hajategemea kukutana na macho yale gizani. Akatokwa na yowe la hofu lakini hilo lilikuwa neno lake la mwisho kusema kabla hajasukumwa kwa nguvu kurudi nyuma mapande ya damu yakaruka huku na kule.
Alikuwa amekufa.


Mshambuliajni akiwa makini kabisa alididimia chini tena kwa uangalifu akarejea mahali ambapo alimwacha msichana mwingine akimuhudumia mwenzake…akiwa katika hatua za kunyata mithili ya paka anayewinda panya, aliendelea kutembea katika ‘kenchi' ile hadi akafikia kile chumba.
Jicho lake likakutana na kitu cha ajabu kingine. Mwanaume mmoja alikuwa akimuhangaisha msichana ambaye muda mfupi uliopita walikutana katiuka dari kisha akaporomoka na kuanguka chini. Huyu alikuwa ni Isha na mwanaume alikuwa katika jaribio la kumbaka.
Macho ya Isha yaliyokuwa yamekata tamaa kutokana na kubanwa vilivyo na yule mwanaume yalikutana ana kwa ana na macho angavu ya Meja. Tumaini likarejea upya, japo hakutambua yule mwanaume ni nani lakini alifarijika kutambua kuwa alikuwa upande wao.


Ni mwanaume huyu ambaye alifanikiwa kuitoa ile dawa ya kupuliza katika mkoba wa Mwanaidi na kuurejesha uhai wake tena. Na ni huyu ambaye alikuwa anatazamiwa kutoa msaada baada ya sekunde kadhaa.
Wakati Isha akijiuliza ni wakati gani atatoa msaada Alishangaa mwanaume yule mweusi lakini mwarabu akijiachoa kutoa juu.
Akatua mgongo ukiwa umejikunja. Kishindo kikatoka.
Isha alitarajia kuwa mtu yule asiyekuwa na jina atafanya papara, haikuwa hivyo yule mwarabu alitua kama vile ameanguka bahati mbaya. Mara ghafla chumba kikawa na watu wanne. Yule mbakaji ambaye alikuwa amevua nguo zake tayari alitaharuki akajaribu kujirusha pembeni lakini Isha alikuwa habari nyingine. Mnyanyase akiwa peke yake lakin kuna mwanaume pembeni yake…usithubutu.
Upesi akamdaka yule mwanaume kama ambaye anamsihi aendelee na zoezi la kujaribu kumbaka. Mwarabu mweusi bado alikuwa wima kama anayesubiri kitu fulani kitokee. Jinsi alivyosimama alifanania na mwendawazimu ambaye hata ule wazimu hana tena ni kama roboti linalopumua tu lakini akili haiku pale. Yule mbakaji ambaye alikuwa ametaharuki akaanza kushangaa kiumbe kile, sasa alitaka kujing'atua kutoka kwa Isha. Isha alipozidi kumng'ang'ania akamshushia ngumi nzito tumboni.
Binti akatokwa na yowe…yowe kali lililosafiri katika masikio ya Meja na kumkumbusha juu ya vifo vya wanawake katika vita walikuwa wanalia lakini hakuna wa kuwasaidia.
Mara akaunganisha meno yake kwa ghadhabu. Hata wakati akifanya hivi yule mwanaume alikuwa amesimama.
Akiwa hajajua afanye nini na kile kiumbe mara, kiligeuka na kumpa mgongo.


Mwendawazimu kamili!! Isha na yule mbakaji ambaye pia ni daktari walifikiria hivyo. Lakini mara miguu ya yule mwendawazimu ikarushwa katika mtindo wa sarakasi ya aina yake ya kuzunguka.
Lile korodani lisilokuwa na nguo likakutana na dhahama ya ajabu mguu wa kuume ukalitandika kwa uzito wa ajabu. Yowe kubwa likatoka na halikuweza kutoka tena Suleiman Meja alikuwa amegeuka na kumkaba tena shingo yake.
Kama alivyomjaza mateke yule marehemu wa bafuni sasa alikuwa anamshambulia huyu mbakaji mwingine…..
Ni kama jamaa alikuwa mwendawazimu kweli, alimrukia katita staili hii mara akaruka huku na kumng;ata sikio yule mbakaji mara akamtwisha ngumi nzito, kisha akamwangusha chini na kuzidi kuthibitisha kuwa yeye ni mwehu. Akaanza kumkanyaga kanyaga pasipo na utaratibu maalumu hadi pale kiliposikia king'ora cha polisi na matangazo yao yakisihi kila mmoja atoke ndani ya nyumba hiyo.
"Mpo wangapi?" kwa mara ya kwanza mwarabu alizungumza.
"Wapi? Aah wawili lakini…..na wengine wapo lakini…sij…" kabla hajamaliza yule mwarabu aliruka juu na kukwea kurejea darini.


Akina Kasuku waliendelea kungoja na kusihi kuwa kila aliye hai katika chumba kile ajitokeze nje. Kimya hakuna aliyejitokeza.
Tangazo lilirudiwa tena na tena. Na kimya kikaendelea kutanda. Askari wawili walikuwa wamepoteza roho zao. Bila shaka mtandao wa Dembele ulikuwa mkubwa na hatari sana.


Tangazo lililotolewa nje n'do lilimshtua akili Meja na kutambua kuwa badala ya kupambana na maadui alikuwa amepambana na maaskari na kwa jinsi alivyokuwa akiiamini bunduki yake hakuwa na shaka kuwa kuna roho alikuwa amezitawanya tayari. Sasa alihitaji kufanya namna yoyote ile kuwasaidia maaskari katika kazi iliyopo mbele yao.
Akiwa darini alitambaa huku na kule kwa umakini kabisa bila kufanya vurugu yoyote ile. Alipita chumba kwa chumba kwa umakini. Alitambua fika kuwa watu wale wabaya kwa kusikia tangazo lile kutoka kwa maaskari lazima watafanya namna ya kufuta ushahidi wa mchakato mzima. Na ushahidi huu ulikuwa unatoka kwa hawahawa wahanga.
Meja alikuwa hajaridhika kabisa kutoiona sura ya yatima ambaye alimtia hasira na chuki na kumfanya achukue maamuzi haya bila kumshirikisha mtu yeyote. George! Bado alikuwa hajaonekana.
Meja akazidi kutambaa kwa kasi na hatimaye akafikia chumba kingine……
Wazo lake lilikuwa sahihi kabisa, sasa aliweza kumuona mama mtu mzima!!
Mama George huyu. Alijisemea……mama huyu alikuwa amekodoa macho yake huku kijana mwenye jaketi jeupe akiwa anajiandaa kumdfunga sindano. Kijana huyu alionekana kufanya jambo hili kwa haraka kupita kawaida.
Meja mwarabu mweusi mzoefu wa mapambano ya aina mbalimbali na sehemu za kila aina akatambua kuwa yule mama alikuwa katika dakika za mwisho za uhai wake. Ni heri angemkuta amedungwa sindano tayari angesikitika tu na kusahau, lakini kumkuta akiwa katikia mchakato wa kudungwa sindano na yeye ashuhudie hakika asingeweza kusahau maishani na angejiweka katika kundi la wauaji.
Wakati huu hakutaka kupoteza muda kushuka chini na kukabiliana naye, japo aliamini kuwa anaweza. Akaitoa bunduki yake na kuiweka vyema mkononi. Akajikohoza kidogo, yule daktari akasita, akajikohoza tena. Daktari akatazama juu.
Hapakuwa na nafasi ya kuulizwa alikuwa anataka kufanya nini. Risasi ikapenya mahali palipostahili. Daktari akarushwa kwa nguvu kuelekea ukutani…..maajabu ule ukuta ukabomoka.
Lilifanana na tukio la Isha aliyedhani kuwa ule ni ukuta.
Chumba kilichofuatia alikuwemo Frida.
George akashuka upesi, hakusema neon na yule mama. Akajirusha kwa nguvu kuvamia chumba kingine, humo akamkuta George Emmanuel. Alikuwa na majeruhi ya kipigo kikali. Akawatazama jinsi walivyotaharuki, akaamua kusema nao neno.
"Mkiulizwa semeni kuna yatima mwenzetu, yatima wa kiarabu alikuja kutukomboa." Kila mmoja alimsikia. Lakini hakuna aliyeelewa kwa wakati ule.
Aliporuka darini tena. Huo ukawa mwisho wa kumuona mazingira yale.


*****


Askari walifanikiwa kupenya na kuingia ndani bila kukutana na kikwazo kipya, ulinzi ulikuwa umeimarishwa vyema sana na yule mshambuliaji alikuwa hashambulii tena. Jambo hili liliwaduwaza askari. Waliweka tahadhari ya aina yake tahadhari kubwa sana…..
Ndani walikutana na miili mitatu ikiwa haina uhai tena, maiti moja ikiwa na kovu la risasi huku nyingine zikiuwawa katika namna ya kustaajabisha zikiwa uchi wa mnyama.


Walifanikiwa kuwatoa watoto na mama yao. Huku Mwanaidi akiwa bado na hali tete. Licha ya Meja kufanikiwa kumpulizia ile dawa yake ya pumu lakini mambo yalikuwa bado.
Wakambeba katika gari ya wazi, akakimbizwa hospitali.
Wale wengine wakafikishwa katika kituo cha polisi kwa usalama wao.
Walihifadhiwa pale hadi majira ya saa kumi na moja jioni siku iliyofuata wakiwa chini ya ulinzi maalum.
Kila mmoja akiwa ametoa maelezo yake juu ya chochote alichokuwa anafahamu kuhusiana na maovu ya Dembele. Pia walifafanua juu ya mwanaume mweusi wa kiarabu jinsi alivyowafikia kama muujiza na kuwakomboa, George, mama yake pamoja na Frida kwa pamoja waliyakariri maneno aliyosema nao kabla hajatoweka na wasiweze kumuona tena.
Katika maelezo yao akapewa jina la ‘Mwarabu wa kuchovya' kwa sababu hakuna aliyemtambua jina lake.
Walitarajia pia kumuhoji mke wa Dembele ambaye naye alikuwa mahabusu waweze kutambua kama anajua lolote juu ya maasi ya mumewe ama kwa namna moja au nyingine wanashirikiana.


Majira ya saa mbili usiku yule diwani aliyenunua taarifa juu ya Dembele naye alikuwa mahabusu, kuingia kwake mahabusu kukaambatana na taarifa mbaya kupita zote katika riwaya ya CHOKORAA.
Yule mwanaharakati kijana kabisa, tena wa kike. Alikuwa amejaribu kuupigania uhai wake kwa namna zote lakini madaktari bingwa wakakiri kuwa hali si shwari na muda wowote anaweza kuiaga dunia. Ama la Mungu aweke mkono wake muujiza utendeke.
Kila mmoja aliumia kwa namna yake. Frida aliangua kilio.
Kwikwi ikamshika mama George.
George akaugulia kiume!!
Wote wakaomba kwa namna zao. Mwanaidi asipotee kirahisi hivyo katika uso wa dunia.
Kimya kikatandaaa....


****


****HALI ya MWANAID bado si shwari…….
***DEMBELE mikononi mwa polisi…..

mlyn ram Khantwe muuza ubuyu culbby BPM Jullie Z
 
Back
Top Bottom