Riwaya: Barua Kutoka Jela

Riwaya: Barua Kutoka Jela

Mbona unahamishia comments pasipo husika nini shida?

Sorry, hii kitu huwa inantokea na mpk sasa sijaweza kujua huwa napress button gn, Evelyn Salt kama una idea naomba msaada wako! Mwenye kujua tafadhali?
 
Last edited by a moderator:
RIWAYA: BARUA KUTOKA JELA
MTUNZI: IBRAHIM GAMA


SEHEMU YA TISA

"Hapana mwanamke, siwezi kuondoka hapa bila kuonana na Dokta Masawe ambaye wewe unamuita Bosi. Lakini pia sikutishii kukukamata, bali nitakukamata kweli usipokuwa makini. Kwani kwa kauli hiyo ni kupuuza agizo halali la Jeshi la Polisi na huyo bosi wako hawezi kunifundisha kazi akafanya kwa utaratibu anaoutaka yeye! Sasa mwambie hivi Inspekta Jamila anasema hataondoka hapa hadi unaongea naye. Vinginevyo anaweza kutumia PLAN, B!"
Inspekta Jamila aliongea bila kuifafanua hiyo "PLAN, B".

Kufikia hapa yule dada akataharuki kupita maelezo, akainua tena mkono wa simu na kubonyeza namba kadhaa, akasubiri kwa muda kisha simu ile ikampa maelezo SIMU YA MTEJA UNAYEMPIGIA HAIPOKELEWI!
Akarudia tena na tena kuipiga simu ile, huku Inspekta Jamila akishuhudia lakini bado ulikuja ujumbe kama wa mara ya kwanza.

Yaani ilikuwa inaonyesha kwamba simu aliyokuwa akiipiga yule dada, mkono wake wa simu haukuwekwa katika sehemu yake.
Inspekta Jamila akamwambia yule dada, "Nipe namba ya simu yake ya mkononi."
Yule dada akamjibu "siyo utaratibu kutoa namba ya simu ya mtu ya mkononi bila ridhaa ya mwenyewe!"
Hivyo Inspekta Jamila akawa haelewi kwa wakati ule nini amfanye dada yule kwa majibu yale.
Inspekta Jamila akatoka nje ya hospitali ile hadi katika gari yake akatoa simu yake kwenye mkoba akabonyeza nambari kadhaa na simu yake ikawa inaita.

"Dokta Zahala tafadhali naomba unipatie namba ya simu ya mkononi ya Dokta Masawe, kwani nipo kazini kwake na napata usumbufu kiasi kumuona".
"Sawa shoga nitakutumia katika meseji sasa hivi."
Alijibu Dokta Zahala na Inspekta Jamila akakata simu.
Kiasi cha kama sekunde ishirini simu ya Inspekta Jamila ikaingia ujumbe na kwa wahka mkubwa Inspekta Jamila akaufungua ujumbe ule uliotoka kwa Dokta Zahala, na kukuta namba zenye
tarakimu kumi, ilikuwa niyamtandao wa Voda Com.
Naye bila Ajizi akaipiga namba ile akawa anasubiri. Jibu alilolisikia kutoka katika simu ile lilimkatisha tamaa.
"Simu unayopiga kwa sasa haipatikani, tafadhali jaribu tena baadae."
Inspekta Jamila alilewa bila ya kunywa!. Mara akakata shauri kuwa siku hizi watu huwa wana namba moja kwa mitandao tofauti.

Basi alichofanya ni kuipiga namba ile katika mitandao mingine. huku akiiseti simu yake katika mfumo wa "PRIVATE NUMBER" Alipoipiga namba ile katika mtandao wa Airtel ikawa inaita na Inspekta Jamila pumzi zikampaa.
Moyo wake ukaanza kwenda mbio kama saa mbovu kwa mchecheto mkubwa uliomjaa. Huku akiombea isiwe simu ya mtu mwingine!

"Dokta Masawe hapa nani mwenzangu?" ilisikika sauti baada ya kupokelewa ile simu.
Inspekta Jamila aliguna kwa kihoro aliposikia sauti nzito ya mtu aliyehitaji kuonana naye, hatimaye amefanikiwa kuisikia sauti yake.
"Ohoo! Dokta Shikamoo. Mimi ni Jenipha niko Mwenge nataka kukuona nina mgonjwa wangu. Je upo kazini kwako au upo nyumbani?"
Inspekta Jamila aliongopa huku akitoa heshima ya shikamoo pia akisikiliza uongo wake kama utaleta jibu gani!
"Wewe nani aliyekupa namba hii? Kwani hakuna mtu zaidi ya mke wangu na baadhi ya watu wangu muhimu ndiyo niliowapa namba hii."
Dokta Masawe alipatwa na mshituko kwani aliyepiga namba ile lazima jina lake litokee kwenye kioo cha simu yake, Kwa sababu wote aliowapa namba ile alihifadhi namba na majina yao katika simu ile. Lakini pia namba ile ilikuwa katika simu yake inayojitegemea, hakuiweka katika mfumo wa kuidivert ingawa ilikuwa inafanana na namba yake ya voda ambayo watu wengi aliwapa namba hiyo. Na alifanya hivi kwa sababu zake maalum!
Inspekta Jamila akajibu.
"Aliyenipa namba hiyo ni katika hao watu wako muhimu na wakaribu." Kisha akaendelea.
"Dokta sasa simu inakwisha pesa naomba unijibu basi kama leo inawezekana kukuona ili tuonane kwanza tuzungumze ili nijue gharama kabla sijamleta mgonjwa. Pia tutapoonana tutapata wasaa mzuri wa kunihoji chochote upendacho, kwani kutakuwa hakuna gharama yoyote itakayosababishwa na maongezi hayo kwangu".
Inspekta Jamila alijibu huku akiilegeza sauti yake kidogo.
"Sawa, sasa muda huu nina kikao kidogo, wewe unaweza…"
Dokta Masawe hakumalizia kauli yake akamuuliza swali.
"Kwa nini simu yako umeiweka katika mpango wa Private Namba?"
Dokta Masawe kama aliyegutuka, alitaka kufahamu.
"Jamani Dokta simu yangu haina pesa ya kutosha bwana, inaweza kukatika muda wowote."
Inspekta Jamila aliongea kwa sauti ya mapozi iliyotokea puani.
"Simu yangu ipo katika hali hii muda mrefu sana kiasi miezi mine, miezi miwili baadae ndiyo itakuwa katika hali ya kawaida. Kwani nimeongea na huduma kwa wateja wa kampuni yangu ya Vodacom na kuwataka waniwekee simu yangu katika hali hii, kwani mimi ni mfanyabiashara nina watu wengi niliowakopesha bidhaa zangu, nilipokuwa nawapigia katika kufuatilia madeni yangu, walipokuwa wanaona namba ya simu yangu, walikuwa hawapokei simu au huwapa watu wengine na wakanijibu majibu ya utumbo. Ndipo nilipoamua kutumia mtindo huu."
Inspekta Jamila alitumia uongo unaofanana na ukweli na Dokta Masawe akaingia katika mtego.
"Okey sasa nimekuelewa kwani nilifikiri ni askari mmoja wa kike anayeitwa Jamila alikuwa analazimisha kuongea na mimi muda mfupi uliopita. Hivyo nilidhani labda ndiyo wewe unanichezea. Samahani sana kwa usumbufu uliojitokeza."
Dokta Masawe alijibu kisha akatoa majibu ambayo Inspekta Jamila hadi anaondoka katika eneo lile alikuwa katika tabasamu pana, akaiwasha gari yake na kuondoka eneo lile taratibu, huku moyoni akiwa na matumaini ya kushinda kesi ile kwa kishindo baada ya mtego wake kunasa muda mfupi ujao.
Inspekta Jamila aliendesha gari yake hadi Magomeni Mwembechai, akaegesha gari yake na kushuka nje katika Mgahawa wa Mwembechai Plazza.
Akaenda katika viti vya mgahawa ule na mara baada ya kukaa tu muhudumu akamfuata na kutaka kujua mteja wao anataka kula au kunywa nini.
Inspekta Jamila akaagiza maziwa ya moto ya Ng'ombe na mayai mawili ya kuchemsha pamoja na juice ya parachichi.
Alipoletewa vitu hivyo akawa anaburudika taratibu akiwa anavuta muda wa kwenda kuonana na Dokta Masawe kama walivyopanga. Hiyo ilikuwa ni saa tano ya asubuhi.
Inspekta Jamila akawa anatafakari mambo aliyokutana nayo toka muda ule alipotoka nyumbani kwake asubuhi hadi kwenda ofisini kwake, na alipokwenda kwa Dokta Zahala namna alivyokuta waraka uliyopenyezwa ndani ya gari yake na yote yaliyotokea kwa Dokta Masawe. Alipokuja kutahamaki, Hamad! Maziwa yalikuwa yameishapoa.
Inspekta Jamila akapiga tarumbeta maziwa yale na kisha akawa anakunywa juice na mayai kwa taratibu.
Ilipotimu saa tano na dakika ishirini, Inspekta Jamila akalipa bili yake na kuiendea gari yake ili aende katika mtego wake.
Alifungua mlango wa gari na kuondoka eneo lile, akielekea kwenye mtego wake, kwani zilikuwa zimesalia kama dakika thelasini na tano, ili kuonana na Dokta Masawe ana kwa ana!
Inspekta Jamila aliwasha gari yake na kuondoka eneo lile kwa mwendo wa taratibu, akielekea maeneo ya Manzese. Dakika tano baadae, Inspekta Jamila alikuwa ameegesha gari yake katika Hoteli ya Friends Corner pale Manzese Arjentina.
Akajichoma ndani ya hoteli ile,huku wateja wachache waliokuwa pale kwa ajili ya mlo wa mchana, na wale wanywaji wa pombe wasiokuwa na muda maalumu wa kunywa, walikuwa wakimtumbulia macho Inspekta Jamila toka alipoingia hotelini pale hadi sehemu aliyokwenda kukaa!
*******
Inspekta Jamila alikuwa amekaa katika eneo ambalo, alikuwa akimuona kila anaeingia na kutoka. Alipokuja muhudumu akamuagiza amletee kinywaji kisichokuwa na kilevi cha Malta Guness, na yule muhudumu akadai pesa yake kabisa, na Inspekta Jamila akamlipa kabisa muhudumu yule.
Kiroja kilikuja yule muhudumu alipokuja, alileta chupa tatu badala ya ile moja aliyoagizwa!
Inspekta Jamila alifikiri labda ni "Order" ya watu wengine wameagiza. Lakini tofauti na mawazo yake, muhudumu yule aliweka mezani kwake zote zile chupa tatu! Na akasema.
"Dada uliagiza chupa moja ya Malta Guness, ila kuna Buzi moja pale limejipendekeza limekupa ofa hizi chupa mbili hivyo usilaze damu."
Inspekta jamila alishangaa sana kwa kitendo kile, pia akichukia kufikiriwa labda ni Malaya aliekwenda pale kutafuta wanaume!
"Poh, mungu anipishie mbali", alisema Inspekta Jamila huku akimalizia kwa msonyo hafifu.
Inspekta Jamila akiwa anapata kinywaji chake taratibu mara wakaingia watu wanne wanaume katika Hoteli ile na mara moja moyo wa Inspekta Jamila ukapiga chemba kifuani mwake!
Kwani aliweza kumuona Dokta Masawe akiwa na jamaa wengine watatu, moja kwa moja wakatafuta sehemu wakakaa.
Inspekta Jamila alipowaangalia wale jamaa kwa makini zaidi ndipo sasa alipopigwa na Butwaa zaidi!
Kwani katika wale jamaa watatu waliongozana na Dokta Masawe, kuna jamaa mmoja sura yake ilikuwa si ngeni machoni mwa Inspekta Jamila, alimtambua kuwa ni Geradi Mwaipopo! Yule mtu aliyepata kuwa askari katika Jeshi la Polisi kisha akafukuzwa kazi!
"Ndiyo yeye huyu," alijikuta akiongea mwenyewe huku akiwaangalia wale watu kwa macho maalum!
"Hawa jamaa wana uhusiano na Dokta Masawe bila shaka Dokta Masawe atakuwa anahusika katika maswala yao," alijikuta bado akiongea peke yake Inspekta Jamila!
"Sasa huyu Dokta Masawe nimfuate pale alipo au nimuache kusudi niwafatilie watakapoondoka ili nijue nyendo zao?!"
Alikuwa anapanga na kupangua Inspekta Jamila kwani aliona kuwa mambo sasa yameiva!
Na hata pale alipokuwa anaongea kimoyomoyo, aliangalia saa yake nakuona ni saa sita kasoro dakika kumi! Ikiwa ni tofauti ya dakika kumi tu iliyosalia ili kutimia ahadi ya kuonana na Dokta Masawe pale FRIENDS CORNER HOTEL kama alivyopendekeza Dokta Masawe!
Inspekta Jamila akajipongeza kwa kuweza kuificha namba yake ya simu alipompigia Dokta Masawe, kwani sasa hatoweza kumtambua kwa kuwa hawajawahi kukutana ana kwa ana kabla ya sehemu ile, ila yeye anamtambua Dokta Masawe kutokana na tukio moja la ajali iliyotokea pale Kibaha, na jopo la madaktari kutoka Muhimbili na hospitali zingine walipokwenda kutoa msaada ili kuokoa maisha ya watu, Dokta Masawe ndiyo alikuwa kiongozi wa msafara ule wa Madaktari!
Hivyo mara kwa mara alipokuwa anaongea kupitia vyombo vya habari, kuelezea maendeleo ya wagonjwa, Inspekta Jamila alikuwa anamuona kupitia kwenye Luninga!
Ndiyo maana hata alipoiona picha yake katika Albam ya marehemu Hamida, mara moja alimtambua!
Lakini kabla hajaongea na Dokta Masawe, kimaajabu na kiulaini anamuona pia Geradi Mwaipopo ambaye yeye alikuwa akimtafuta kwa Udi na Uvumba! Ambaye picha ya sura yake ilinaswa kwenye macho ya marehemu Kiyarwenda Mwemezi Baada ya kufanyika vipimo vya kitaalam.


***JAMILA anazidi kugundua jambo moja bada ya jingine…….je nini mwisho wa mchezo huu…..


Jagarld Jullie Z Sangomwile Khantwe Mr Rocky Gunda66 Himidini VAN HEIST BPM ABUBAKAR SHEKAU NYIRO mamsapkhan born again pagan princetx Ennie mcubic jonnie_vincy slim5
 
Mh kila part ni nzuri kuliko ilopita. Simulizi nzuri sana hii casuits
 
Nahisi inspector ataipotezea ahadi na kufuatilia nyendo za hao maharamia kwa siri......Thanx Casuist......endelea kutupa burudani
 
Last edited by a moderator:
mkuu Casuist hongera sana, utunzi bora sana ktk zama hizi!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Casuist shukrani kwa kuniita, hii story ipo poa mno inanifanya napunguza stress za ofisini!
 
Last edited by a moderator:
í-½í¸Ší-½í¸Š This story kwa kweli ni nzuri and always naiona very short. Waiting for another episodes. í-½í³–
 
Hadithi inaviwango vya ubora kabisa, Naifanisha na hadithi za JORAMU KIANGO.

Usisahau kunitag mara ubandikapo mkuu.
 
mkuu hongera san

mi nataka vitabu vyako tu.nielekezen nitavipata wapi
 
Mii mzima wangu, wapita corridor gn? mbona hatuonani?

Humu humu, sema majukumu yamenizidi tu naonekana kwa nadra, kuiweka episode mpya uwe unaniita manake casuist hata haniiti siku hizi
 
Back
Top Bottom