Riwaya: Ant Ezekiel

Riwaya: Ant Ezekiel

Safi sana mzaramo stori imefikia mahali ambapo inatia hamasa zaidi na zaidi kutaka kujua kilichoko nyuma ya pazia. Nasubiri sana muendelezo
 
Duuuh... aiseee bonge la story... ila mbona kama naona inaelekea ukingoni vle?
 
Safi sana mzaramo stori imefikia mahali ambapo inatia hamasa zaidi na zaidi kutaka kujua kilichoko nyuma ya pazia. Nasubiri sana muendelezo

yeah mkuu inazidi utamu kudoga
 
Mzaramo umetisha ndugu, yaani wewe ni moto tena sijui mwiba ambao unachoma kwenye maaumivu(yaani pale watu wanapokua na hamu ndo wewe una dondosha haja yao), uko vizuri sana

ahaa ahaa ndio raha ya kuwa mtoto wa Dar Es Salaam mkuu
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA
Mikono yake ilikuwa inatetemeka.
Nakufa!! Nilipitiwa na wazo hilo huku nikijaribu kufurukuta
huku na kule bila kujua kama ni kweli nafurukuta ama
nawaza tu kuwa nafurukuta!!
Nilihamisha macho yangu kutazama kama kuna msaada
kutokana kona yoyote!!!
Na huku nikakutana na askari mwingine feki akinijia na
bunduki mkononi!!
Nimekwisha!!! Niliapa……
Na baada ya kiapo kweli nikajikuta nakuwa kama mpira wa
kona.
Nilikuywa nagombaniwa!!!
Nilivutwa huku na kule. Sasa sikuweza kumtazama yeyote,
kila kiungo katika mwili wangu kilikuwa kinauma, huyu
akivuta mkono huyu anavuta mguu, huyu ananipiga teke
mbavuni, huyu anavuta kichwa changu!!
Kisha mlio mkali sana ukasikika!!! Mamivu yakapenya
barabara, maumivu makali kupita yote niliyowahi kuyasikia.
Sikuweza kufumbua macho!!
Masikio yakausikia mlio mwingine mkali zaidi, na hapo sikujua
nini kinaendelea tena duniani!!!
NILITAMANI kuendelea kuwa shuhuda wa kile kilichokuwa
kinatokea lakini milango yangu mitatu ya fahamu iliyokuwa
imesalia nayo ikafunga na kiza kinene kikatanda.
***
Mivumo ilisikika mara nuru ikachomoza tena nilikuwa
nimevaa mavazi meupe huku kila mtu aliyenizunguka akiwa
na mavazi meupe pia. Tulikuwa tunatembea kuelekea mahali
peupe pasipokuwa na doa lolote. Wenzangu walisemezana
wao kwa wao, nilijaribu kuwasikiliza kwa umakini ni kitu
gani wanamaanisha lakini sikuambulia kitu walikuwa
wanaongea lugha nisizozielewa hata kidogo.
Walinong’onezana kisha wakanitazama na kunifanyia ishara
za mikono kuwa niendelee mbele, nilisita kidogo na
kuwauliza kwanini mimi niende mbele na wao wabaki nyuma.
Niliwauliza kwa Kiswahili, wakatazamana na kuanza
kucheka, walicheka sana na mara vicheko vilipowaisha
wakachomoa mapanga na marungu.
Hawakuwa wakicheka tena, hapo nikalazimika kuanza
kutimua mbio, walikuwa wakinifuata nyuma kwa kasi ya
ajabu, nilizidi kukimbia huku nikipiga kelele za kuomba
msaada, njia nzima ilikuwa nyeupe na hapakuwa na jengo
hata moja, nilikimbia zaidi na wao nikawasikia nyuma yangu
wakinikaribia, hatimaye nikaona nyumba kwa mbali.
Ni hapa nitapata msaada!!! Nilijisemea na kuendelea kutimua
mbio. Nilipoifikia nyumba niliyotarajia msaada niliwaqsikia
waliokuwa wakinikimbiza wakitokwa na vicheko.
Nilipoitazama nyumba ile nikakaribishwa na maandishi
makubwa yaliyoandikwa MICHIGAN EMPIRE. Mapigo ya moyo
yakaongeza kasi, wale watu wenye mapanga wakiwa
wanacheka walizidi kunisogelea na miguu ilikuwa mizito
kukubali kuingia katika jingo lile ambalo niliamini kwa namna
yoyote ile kuwa nitauwawa baada ya kuteswa vibaya!!
Nikiwa bado sijapata maamuzi sahihi ya nini cha kufanya
mara watu wawili wakatoka katika lile jengo la MICHIGAN,
mmoja sikumtambua lakini mwenzake nilimfahamu fika.
Akanitazama kwa jicho lililojaa chuki.
Alikuwa ni cheupe dawa!! Yule mzungu ambaye alimteka mke
wangu na baadaye nikamwingiza matatani!!
Kumbe walikuwa watu watatu!! Yule mwingine alikuwa mfupi
sana na sikuwa nimemuona hadi alipozungumza.
“Babaaa!!!” sauti ikapenya masikioni mwangu, jicho
likafumbuka upya.
Alikuwa ni Eva!!!
Nikataka kumsogelea Anitha, yule mzungu akatoa Bunduki na
kuilengesha katika kichwa cha Anitha!! Nilipiga kelele bila
kujua ni kitu gani ninasema!! Yule mzungu hakujali, akazidi
kuigandamiza katika kichwa cha Eva, mtoto wangu wa
pekee!!.
Na mara akafyatua!!!
Nikalegea macho yakitazama mwili wa Eva ukiwa hauna
kichwa ukirukaruka huku na kule. Nikatua kwa magoti kisha
nikaanguka tena nikitanguliza kichwa chini!!! Nilikuwa
nimeshuhudia mauaji ya mtoto wangu kwa jicho langu…….
Sauti za kiarabu ama kichina kutoka kwa wale watu
zikageuka kuwa za Kiswahili sanifu, lakini Kiswahili chenye
hofu ndani yake.
“Ametulia, ametuliaaa…” sauti ilizikika. Ilikuwa sauti ya
kike. Maajabu, sikukumbuka kumwona walau msichana mmoja
katika kundi lile la watu waliovaa nguo nyeupe.
Nikafanikiwa kufumbua macho yangu!!!
Nikaona maluweluwe, nikafumba na kisha kufumbua tena.
Nikakutana na tabasamu hafifu kutoka kwa mwanadada. Ni
kama nilikuwa namfahamu, lakini nfikra zilikuwa mbali.
Ina maana na yeye alikuwa katika kundi la wale wauaji
wenye mapanga walionifukuza hadi Michigan kwenda
kumshuhudia yule fedhuli akiutoa uhai wa mwanangu, sasa
anatabasamu wakati mwanangu amekufa.
Nikakunja ngumi zangu ili niweze kumshambulia, nikamngoja
anisogelee zaidi.
Naam!! Akanisogelea!! Nikaikaza mikono na kisha kwa nguvu
zote nikarusha ngumi huku nikitokwa na maneno makali.
“Anitha nawe u muuaji… unataka kuniua Anithaaa….
Umeshiriki kumuua mwanangu Anitha…” nilibaki kupiga
kelele, mikono na miguu ilikuwa imefungwa vilivyo!!
Anitha hakushtuka badala yake alitokwa na machozi huku
akitikisa kichwa kuonyesha kusikitika, nilipepesa macho huku
na kule. Akajifuta machozi kisha akatokwa na neno kwa
sauti ya chjini.
“Sam u hai tena mpenzi wangu!!!”
“Nani mpenzi wako muuaji mkiubwa wewe, Anitha
mwanaizaya wewe mwanaharamu mkubwa unashirikia na
watu wabaya kumuua Eva, wamekulipa shilingi ngapi hao
mabwana zako wa kizungu… wamekulipa shilingi ngapi Yuda
msaliti wewe……” niliwaka kwa hasira zote nikitamani
mikono na miguu yangu iwe huru lakini haikuwezekana.
“Sam…..” sauti nyingine ikaniita ikitokea upande mwingine,
nikajaribu kuigeuza shingo yangu lakini maumivu makali
yakanizuia sikuweza kugeuka. Nikangoja hadi yule mtu
akafika mbele yangu.
“Sam wewe ni mwanaume asee!! Yaani wewe ni mwanaume
haswa!!!” ilikuwa sauti ya kichaga, sauti ya Masawe!!!
Nikazidi kuchanganyikiwa!! Masawe naye anashirikiana vipi
na Anitha sasa. Na mbona hawana nguo nyeupe kama
nilizowaona nazo hapo awali, hata mimi sikuwa na nguo
nyeupe, maajabu haya.
“Sam….iruhusu akili yako kufikiri yaliyopo sasa!! Yote
unayoyaongea ni maluweluwe tu katika kuzimia kwako…”
Anitha alitokwa na kauli ambayo ilirejesha amani.
Akanikumbusha jinsi gani nipo hapo.
“Sam.. hatuna mud asana hapa lazima tuondoke lakini
napenda kukukumbusha ili uwe na imani nami tena. Sam…
nilikutana nawe ukiwa katika dakika za mwisho za
kukabiliana na umauti, nilivaa nguo za kiaskari ambazo
nilizipata kutoka kwa askari mnoja feki aliyeuwawa katika
mapambano, sikuwqa na nguo siku zote nilizokuwa
Michigani, nilikuwa uchi. Nilikuona kupitia tundu la mlango
wakati unahangaika ndanmi ya Michigani, lakini nilikuwa
nimefubgwa midomo yangu nisiweze kupiga kelele zozote,
nilitamani unione uweze kunifungulia ule mlango lakini
bahati mbaya Sam hukuweza kuhisi lolote, ulikuwa
umetaharuki. Baada ya maaskari kuingia katika chimbo hilo
na kuvunja milango ndipo nilipotoka lakini nikiwa uchi.
Askari aliyeuwawa, nikamvua nguo na kuzivaa huku
nikumbuka kuichukua na bunduki yake. Bunduki ambayo
haikuwa tofauti kabisa na bunduki ndogo ya baba yangu
ambay7o nilijua namna ya kuitumia.
Nilitembea kwa kuchechemea, sikuwa nafanya lolote lile
zaidi ya kukutafuta wewe Sam. Nilitamani kukuona ukiwa
hai.
Baada ya hekaheka zote za hapa na pale huku nmaaskari feki
wakifanikiwa kuwadhibiti vilivyo askari halali mimi nikiachwa
wakidhani mimi ni mwenzao ndipo nikakukuta ukikabiliana na
askari feki na hapo nikaingilia kati bila yeye kujua kama mimi
si mmoja wao. Tulikugombania Sam tukikuvuta huku na kule,
akitaka kukuua nami nikijaribu kukutetea kwa kila namna.
Mwisho wewe ukawa sadaka baada ya yule bwana kutoa
bunduki na kudai kuwa anakuua. Akili yangu ikazinduka yule
bwana akiwa amefyatua risasi katika paja lako na alitaka
kufyatua kichwa chako ukiwa tayari umepoteza fahamu, ni
hapo nilipomfyatulia risasi na kusambaratishas kifua chake
bila uoga wowote. Mateso ya Michigani, kubakwa na
kudhalilishwa kwa kila namna kulinifanya niwe mnyama,
lakini si mnyama awezaye kuwa mkali na mwenye chuki mbele
yako.
Ni mnyama awezaye kupigania haki!!
Nilijaribu kukuburuta lakini ulinizidi uzito na hapo ndipo
nikafanikiwa kuonana na huyu bwana akiwa na pingu
mikononi, nikaisambaratisha ile pingu kwa risasi kisha
nikamweka chini ya ulinzi kwa lugha moja tu, akubebe hadi
mahali ambapo mimi nahitaji.
Akatii amri hiyo!! Lakini njiani alijaribu kuelezea kuwa
anakufahamu haswa, akanisihi sana nimuamini, naam
nikamwamini baadaye kabisa. Baada ya kuusoma uso wake na
pia kumtishia kuwa nina wenzangu, akijaribu kuleta fitina
yoyote ile. Bahati nzuri hakuleta ujanja wowote na badala
yake alinisimulia namna ambavyo uliingia Iringa na hatimaye
kufanikisha kulifungua lango kuu la kuingia Michigani. Sam!!
Siwezi kukuficha na unajua kabisa huwa siwezi kuficha hisia
zangu, niliuona mwili wako kama dhahabu, nikangoja upate
uhai nikwambie maneno haya.
Sam wewe ni mwanaume kati ya mwanaume, uwe hai ama ufe
leo. Jina lako litabaki katika vichwa vya watu wengi na
maandishi uliyoandika hayatafutika kamwe kizazi hadi
kizazi.” Anitha alimaliza kusimulia kila kilichotokea, na
kadri alivyokuwa anasimulia nilizidi kurejewa na fahamu
zangu.
Anitha alikuwa mwanamke wa aina yake!!
“Mama lao yu wapi!?” nilijikuta nauliza hatimaye…. Kabla
hajajibu nikaijiwa na swali juu ya swali, “Mzee Matata je?
Na faili lipo wapi … faili lipo wapi Anitha…” kila swali
nililouliza Anitha hakuwa na jibu nalo, akaningoja nitulie
ndipo alipozungumza nami tena.
“Sam, hayo maswali ni magumu sana baadhi hata mimi
nimejiuliza lakini nadhani kwa sasa tuchukue alichosema yule
kijana kabla hawajamchukua…” alisema Anitha kwa sauti ya
chini sana.
“Kijana yupi tena….”
“Mh! Sijui kama nipo sahihi, lakini macho yangu yalidai kuwa
ni Alvin sijui na mimi nilikuwa naota. Maana Alvin si ndo yule
alikufa na magazeti yakadai kuwa wewe ndo umemuua…..
lakini nimekutana naye…..”
“Ndo Anti Ezekiel huyo….kasemaje?”
“Geti namba saba….funguo zilezile….”
“Geti namba saba?.. yupo wapi huyo Alvin….”
“Nalijua hilo geti tatizo ni funguo alizosema……sizijui wala
sijawahi kuzisikia.”
Neno la Anitha likanikumbusha funguo nilizokuwanazo lakini
sikukumbuka ni wapi zilipokuwa kwa mara ya mwisho, iwapo
ni Michigani ndani ama eneo la shambulizi ambapo nilipoteza
fahamu…
“Pia amesisitiza juu ya kitu fulani ambacho kimenitatiza
sana… amekuwa akirudiarudia neno Kenton. Amelisema mara
kwa mara na ni kama nimewahi kulisikia jina lile mahali.
E.F.Kenton…….” Anitha alisema kama mtu anayekariri
jambo.
“Nini E.F.Kenton? unamjua? Ni nani? Nimeliona jina hilo
ndani ya Michigani wewe umelijulia wapi…..”
“Dar es salaam Mlimani City. Nimewahi kukutana naye….”
Alinijibu Anitha na kuzidi kunichanganya. Sasa ikawa zamu
yangu kuamini kuwa Anitha ndiye anayeota. Atakutana vipi
na bosi wa Michigani ambaye anayo ofisi kubwa kabisa chini
ya ardhi, anadai amekutana naye Dar, hapana huyu anaota.
“Anitha unaota wewe…” nilimweleza na kutoa tabasamu kwa
mara ya kwanza…..
“Sam, nimewahi kukutana naye, niamini!!!” alisisitiza
Anitha.
Nikabaki katika viulizo kadha wa kadha!!!
 
Kama kawaida mzaramo kazini ila leo umetupa kwa ufupi haha. Asante sana tunadhamini kazi yako
 
Patamu hapo,Anitha is back twende kazi@Mzaramo
 
SEHEMU YA MWISHO
“Umeyajuaje yote haya…” nilimuuliza hatimaye.
“Kuna bwana nilimuagiza akuletee barua, ndo huyo alinieleza
kila kitu juu ya Michigani, akanisemelea juu ya geti namba
saba pia. Niliwahi pia kuletwa huku, na huu mlango wa
dharula ni kwa ajili ya walinzi japo huwa hautumiki mara
kwa mara mpaka hatari kubwa ikiwepo…..” alisema kwa
ufupi na hapo wakaanza kusukumwa watu kuingia katika
uwazi mkubwa.
Asilimia kubwa walikuwa ni wale waliokuwa nje tayari
wamekombolewa, mzee Matata alikuwa amelegea, Mama lao
alikuwa amefungwa kamba mikono yote. Nikajisikia hasira
kali sana.
Vikashushwa vitanzi upesi na hapo baadhi ya askari feki
wakaanza kuwasukuma raia katika vitanzi.
Na hapa ndipo ikafuata VITA YA MWISHO CHINI YA ARDHI
MICHIGANI………Ni aidha kufa ama kupona lakini siri lazima
ifichuke.
**JIFUNZE kuwa hakuna marefu yasiyokuwa na ncha!!!
Usikate tamaa!!
Risasi zilimiminika kuwaendea wale mahayawani takribani
watano wa kiafrika ambao walitaka kuwaweka katika kitanzi
waafrika wenzao.
Kambi yetu ilikuwa imara haswa!!
Kuangushwa kwa watu wale wabaya kukazua tafrani mpya,
mateka wao wakaanza kukimbia huku na kule. Wao wakabaki
katika sintofahamu. Wakiwa katika taharuki kali zaidi.
Walijaribu kuwazuia huku wakikishambulia kwa risasi kile
kibanda cha dharula ambacho tulijihifadhi ndani yake. Lakini
hawakuwa na shabaha murua.
“Adui katika kambi hii… adui katika kambi hii, bomu la mkono
linatupwa katika maficho yenu ndani ya dakika moja. Kwa
usalama wenu na wenzenu jisalimisheni, la sivyo ninyi
pamoja na wenzenu wote mtapoteza uhai. Angalizo ni
kwamba hakuna njia yoyote ya kutoka Michigan ukiwa hai,
njia zote zimefungwa.” Ilikuwa ni sauti kubwa ikielezea kwa
ufasaha juu ya usalama wetu na wenzetu. Sauti hii ilirudia
mara ya pili na wakati ikirudia haya mara Michigani ilianza
kupanda juu tena. Kambi yetu iliingiwa na kiwewe baada ya
tangazo lile ambalo mtangazaji wake hakuonekana na wala
kinasa sauti na kipaza sauti vyote havikuonekana.
Majambazi yakiwa na silaha mkononi yalishindwa kufyatua.
Hatimaye Michigani iliyokuwa imezama chini ikarejea usawa
wa kile kibanda chetu cha dharula!!!
Na wakati huu yule mtangazaji alikuwa akihesabu namba
kadhaa kwa ajili yetu kujisalimisha.
Tulikuwa tumepatikana!!
Heka heka za kule chini za mateka ziliendelea huku wakikosa
mahali sahihi pa kukimbilia, kwani kila mahali palikuwa
pamefungwa!!
Kambi yetu ilikuwa na bunduki mkononi bado kwa lolote
litakalotokea mbele yao. Mimi, Masawe na Anitha tukiwa
tumepigwa butwaa tu.
Na mara kikatokea kisa cha kushangaza. Ukaanza kuvuma
upepo mdogo kiasi na mara majambazi wakaanza kuhamanika,
wakionekana kuvutana na kitu kisichoonekana, na hata
walipozidiwa nguvu wakaziachia bunduki zikivutwa kwa kasi
na kutokomea na upepo ule.
“Shit! Magnetic wind…..” alilalamika Anitha akionekana
kujua nini kinatokea pale.
Sasa wakatokea watu wanne!!
Cheupe dawa na yule mwafrika mwenzake wakiwa katika
jopo. Walikuwa wanacheka kwa dharau na namna fulani ya
kuridhika sana.
Cheupe alikuwa amebeba faili mkononi.
“Unaanza vipi kutoka Michigan ukiwa hai… we ----- wewe
ulibahatika kutoka umejileta tena eeh..” aliongea huku
akinitazama, nikakwepesha macho nisimtazame.
“Salim!! Hakuna kupoteza muda tena….” Alikaripia yule
mzungu. Na hapo akatokea bwana mmoja mwenye ndevu
ndefu haswa.
Akapiga miluzi wakatokea wengine wawili. Wakawakwida
mashati raia wawili wakiwa uchi na dhaifu, wakawaingiza
katika kitanzi kisha wakabonyeza mahali, ardhi yao
ikafunguka.
Wakawanyonga wale watu wasiokuwa na hatia.
Ilisikitisha kuwatazama. Nilifumba macho kwa uchungu na
uoga ukanitawala nikiyafikiria maisha mafupi katika kitanzi
kile.
“Bonge waiti amesema kuwa wao wameua watano sijui sita,
sisi tunaanza na sitini na sita kama mfano tu… na wale
vichwa ngumu kama Sam na baba yake huyu Matata ni adhabu
takatifu kabla ya kifo..” cheupe dawa alimweleza mwenzake
kimadaha na majigambo.
“Sam… Sam….” Anitha aliniita huku akitazama mbele
asijulikane kama anasema nami.
“Wanamuua baba Sam…..” Anitha alinieleza kana kwamba
nilikuwa sijasikia lolote. Niliuma meno yangu kwa uchungu
nisijue nafanya nini.
Wakati huo raia wengine sita walikuwa katika kitanzi.
Na hawa wakauwawa katika namna ileile.
Mbona watoto hawauwawi ama!! Nilijiuliza baada ya kuona
kuwa ni watu wazima pekee waliokuwa wananyongwa.
Awamu ya tatu ya kunyonga haikwenda kama ilivyopangwa
badala yake ikaingia doa.
Cheupe dawa aliyekuwa mwenye tabasamu muda wote, akiwa
na tabasamu lake vilevile ghafla alirushwa nyuma kimyakimya
akitua katika umati mkubwa wa mateka, na doa jekundu
likaonekana katikati ya kifua chake kimyakimya.
Yule muafrika kibaraka wa yule mzungu akafanya kosa
kugeuka upesi kutazama nini kinamtokea mwenzake.
Akauachia mgongo wake wazi, ghafla akarushwa mbali
akifunuka kifua chake na kutokwa na yowe kubwa kabisa.
Akaungana na mzungu katika safari ya milele.
Kimya kikatanda asijulikane ni nani anayeshambulia,
majambazi hawakusogea mbele kwa sababu hawakujua ni nani
aliyefanya shambulio hilo, na wenyeji wa humo wakapigwa na
bumbuwazi.
Mluzi ukasikika katika namna ya kuvutia masikioni,
majambazi kwa pamoja wakasema.
“Kigulu……” nikalikumbuka jina hilo kuwa ni la mzee Sendeu.
Yule fundi makufuli.
“Hakuna bunduki, vamia…. Hakuna bunduki magnetic wind
imepita….” Anitha aliyasema hayo huku akiongoza mbio
kumkabili yule bwana aliyekuwa anawanyonga mateka. Lakini
kabla hajamfikia alijikuta katika mikono yenye nguvu sana.
Alikuwa ni mzee Matata!!!
“Baba…..” Anitha akamuita lakini hakujibiwa na badala yake
mzee Matata akamrukia yule mnyongaji na kumkaba koo yake
huku akipiga mayowe hadi pale alipotulia tuli.
Alikuwa ameua!!
Niliendelea kuwa shuhuda na miguu yangu mibovu, majambazi
wakipambana ana kwa ana na maadui.
Mzee Matata akazifungua kamba zilizomfunga afisa wa jeshi
la serikali. Akiwa kama mbogo na yeye akafanya mashambulizi
makubwa tena ya upesi upesi. Makabiliano ya ana kwa ana
maana upepo uliokuwa umewashwa haukuruhusu bunduki
wala chuma yoyote kuwa pale, ilisafisha kila kitu pale.
Afisa aliambatana na mama lao. Kipigo alichokuwa anatoa
mama huyu sikuwahi kukidhania lakini kilinifanya
nitabasamu, nilitabasamu kwa sababu niliwahi kuwa pembeni
ya shujaa huyo.
“Michigani mini office Geti namba saba, yupo huko…. Yupo
na faili..” sauti ikaniambia kwa shida sana, nikageuka na
kukutana tena na ule mzimu wa maajabu.
Ezekiel!!!
Alikuwa anatabasamu tena.
Nikaanza kupiga kelele nikitafuta wa kumwelewesha juu ya
hili!!
Afisa akanisikiliza, akawatambua baadhi ya vijana wake wa
kazi ambao walikuwa na nguvu bado. Wakaunda jeshi la
dharula, msako wa geti namba saba ukafuata…..
Niliungana na msako huu nikiwa nachechemea, hatimaye
tukalifikia geti hilo la vioo.
Amri ikatoka na kundi lote la ukombozi na mateka wetu
kutoka kwa wapinzani wakazingira geti namba saba.
Kisha ufumbuzi wa kufungua pale ukafanyika, kwa sababu
palifungwa kwa utaalamu, basi ni nguvu pekee ingeweza
kufungua, kila kitu kizito kisichokuwa chuma kilitumika
kuponda vile vioo. Hadi vilipovunjika vipande vipande.
“Bosiiiiiiii…” alipiga kelele mzee Matata. Huku akiiziba
midomo yake. Watu hawakugeuka kumtazama bali walimkazia
macho kiumbe aliyekuwa ananing’inia katika mkono wa koti
la kuvalia suti, ulimi ukiwa umemtoka nje.
Mzee Matata anamuitaje bosi wake sasa? Nilijiuliza!!
“Sam…… ni huyu…. Ni huyu Kenton!!!” Anitha naye alipiga
kelele.
Sikumsikiliza tena baada ya kuliona faili mezani!!
Nikatimua mbio kwa kusuasua hadi nikaifikia meza na
kulikwapua faili lile. Faili lenye siri nzito.
Afisa alitoa wazo kuwa tutafute namna ya kutoka nje ya
Michigan lakini Ezekiel, yule mwanadamu wa ajabu
alininong’oneza kuwa anahitaji kusedma neno kabla hajaaga
dunia kwani hali aliyonayo anaijua mwenyewe tu na si vyema
akifa huku ameacha utata. Kubwa zaidi aliongezea kuwa
kufikia hatua ya bosi yule kuuwawa basi hakuna hofu tena
katika chimbo hilo la Michigan.
Upesi nikaisambaza ile taarifa, na nilikuwa nasikilizwa sana.
Mimi, Mama lao pamoja na Anitha tulisikilizwa zaidi. Na
tuliheshimiwa kama mashujaa hata kabla hatujaimaliza vita
hiyo.
Umati ukamzunguka Ezekiel ukimya ukairuhusu sauti yake
kupenya. Askari watiifu wakiwa makini kutulinda.
ALVIN….
Niliishi na kufanya kazi michigani kabla haijawaka moto na
kuteketea na nikiwa kama mfanyakazi mtiifu sana
nililazimika kuyafumbia macho mabaya ili niendane na sera za
mkuu wangu wa kazi, ambaye kwa wakati ule nilimtambua
kama cheupe (akamwonyeshea mkono yule mzungu mwenye
upara niliyemzoea kama cheupe dawa)… lakini baada ya
kugundua mambo kadha wa kadha ndani ya jumba la Michigani
hasahasa suala la kukamata watoto wasiokuwa na hatia.
Nikajisikia nipo hatiani na kuamua kupingana kabisa na
mfumo huo, nilijaribu kuwahamasisha wenzangu lakini baadhi
walinisaliti na mwisho kunichomea utambi. Bahati nzuri kuna
mkuu mmoja alinishtua kuwa nilikuwa hatarini. Nd’o
nikatimua mbio mapema kabla ya dhahama. Siku nne baada ya
mimi kutoka Michigani, ilichomwa moto na kupotea kabisa
huku watanzania wasiokuwa na makosa wakitupwa jela na
serikali ikiendelea kumkumbatia mmiliki wa Michigani kisa tu
anaongeza pato la taifa kwa sana.
Niliishi kama digidigi ndani ya mji niliozaliwa. Baada ya
Michigani kuchomwa ndipo kwa usiri ikaanzishwa Michigani
nyingine miezi kadhaa baadaye, niliamini kuwa nimesahaulika
tayari hivyo nikaendelea na harakati zangu za kusanua
mpango kabambe wa mmiliki wa Michigani. Bwana aliyekuwa
muuzaji katika duka la Michigani alikuwa ni jamaa yangu wa
karibu na niliwahi kufanyanaye kazi Michigani ya zamani
huyu anaitwa Kindo, ni yeye aliyekuwa akinieleza kila
kilichokuwa kinaendelea katika duka dogo la Michigani.
Alifanikiwa kunipatia picha kadha wa kadha ambazo aliamini
kuwa zinaweza kunisaidia, mimi pia nilikuwa na picha zangu
zinazoionyesha Michigani. Masawe alikuwa muuzaji
mwenzake na Kindo japo yeye hakuwa akifuatilia mambo
yetu, kama ilivyo kwamba Ng’ombe wa masikini hazai wakati
tunakaribia kufanikiwa kuingia katika himaya ya chini kwa
chini ya Michigani ndipo mkuu akashtukia na nikaanza
kusakwa huku kindo akitiwa uchizi. Nilifanikiwa kuchukua
nyaraka kadhaa muhimu pia funguo chakavu. Funguo ambao
niligundua kuwa unaingia karibia kila kitasa. Na ni huu
funguo ambao ulifungua jumba hili.
Maisha ya udigidigi yalivyonishinda nikaamua kuelekea Dar es
salaam nikiwa na nyaraka zangu.
Ili nisiishi kama digidigi nikaamua kuishi kama Alvin mwingine
kabisa, nikalikuta neno Anti likitumika kuwaita mashoga
jijini Dar es salaam, na huku nikijua mashoga wanachukiwa
sana na mimi nikahitaji kuchukiwa na jamii ili nifanye mambo
yangu kimya kimya!!
Na hapo nikajitambulisha rasmi kama Anti Ezekiel, wao
wakidhani jina la anti kwangu linasimama kama shoga, kumbe
ninamaanisha Mpinga Ezekiel (ANTI-EZEKIEL kwa
kiingereza)
Akanyamaza kidogo akivuta pumzi!!
Akaelezea namna tulivyokutana mara ya kwanza na ya pili
kisha akaendelea
“Sikuwa na mtu mwingine wa kumuamini basi ule funguo
nikamkabidhi yeye, nilitaka kumkabidhi Sam funguo huo
usiku mmoja baada ya kutumiwa ujumbe wa kurejea Michigan
lakini nikamkuta katika faragha na mkewe, nikasikia kuwa
atasafiri siku inayofuata, nikaamua kwenda kuonana naye
Ubungo, na nikafanikiwa japo nilikuwa chini ya uangalizi
mkali, nilitumia mbinu ya yeye kuupata tu funguo na kwa
kuwa ni mwandishi wa hadithi za kipelelezi nikajua lazima
atapeleleza tu na sasa yu hapa. amefanikisha” alizungumza
haya huku akitokwa na machozi ndani ya tabasamu.
Machozi ya furaha
“Na ni kwa nini unachanganya majina, mara Alvin mara Anti
Ezekiel…” afisa alimuuliza swali ambalo alikuwa amelijibu
tayari….
“Mimi naitwa Alvin, Anti Ezekiel, hili sio jina bali neno Anti
ni la lugha ya kigeni na linamaanisha Mpinga ama kuwa
kinyume, yaani mpinga Ezekiel ama mkataa Ezekiel, hivyo
mimi namkataa na kumpinga Ezekiel na maisha aliyotaka
kuyaleta Tanzania hasahasa Iringa.” Alijibu swali hilo
nikastaajabu. Yaani siku zote namtafuta Anti Ezekiel kumbe
hata mimi mwenyewe ni Anti Ezekiel!!
Jojina naye akacheka kidogo!! Na yeye alikuwa akimchukia
Anti Ezekiel kumbe alikuwa akijichukia?
Na hapo nikatambua kuwa lile jina E.F.Kenton, ile E
inasimama badala ya Ezekiel!!
Kufikia hapo sasa nikaamua kulitoa lila faili, mbele ya umati
haya yote yalifanyika maana yalikuwa mambo muhimu kwa
ajili ya watanzania.
“E.F.Kenton kumbe ndo bosi wa haya yote!!” Mzee Matata
alitahamaki, masikio yakageukia kwake wakati akimuelezea
Ezekiel Kenton kama mmiliki wa gazeti ambalo alikuwa
anafanyia kazi huko!!
Aliezea zaidi hatua ya yeye kufukuzwa kazi na kufungiwa
kazi baada ya kuandika makala kuwa Sam ameonekana mjini!!
“Kumbe nilikuwa namtumikia shetani!!!” alimalizia mzee
Matata kwa masikitiko.
Nami sikungoja tutoke nje ya ngome ile, nikaamua kulifunua
lile faili na kuumakinisha umma ukatulia na kunisikiliza
nikielezea
MKAKATI WA KUDUMU KUIFANYA TANZANIA NCHI TEGEMEZI.
Hicho kilikuwa kichwa cha habari kikubwa zaidi.
Ndani ukaelezewa ule mkakati kwa urefu!
Nchi zilizoendelea ama nchi za dunia ya kwanza zilikuwa
katika mkakati wa kuua nguvu kazi ya taifa kwa
kuwapunguza vijana na kiasi cha kuzaana.
Mkakati huu ulikuwa na dhima ya kuzifanya nchi masikini
kuwa masikini zaidi ili kuwezesha uhuru linapokuja suala la
uwekezaji. Kama wakishindwa kujizalishia mali zao wenyewe
basi kwa namna yoyote watakuwa tayari kuruhusu nchi za
kigeni kuwekeza kwa kadri ziwezavyo jambo ambalo
litaongeza pato kwa nchi zilizoendelea. Na kuongeza tatizo
la umasikini katika mataifa masikini, Tanzania ikiwa
mojawapo.
Mkakati nambari wani waliouanzisha ulikuwa ni kuongeza
idadi ya ndoa za jinsia moja hasahasa wanaume kwa
wanaume.
Mkakati ambao waliamini utazaa matunda sana, maana kwa
wanaume kuoana basi vijana watapungua na si kupungua tu,
ndoa zaj insia moja hazizai mtoto hivyo, idadi ya watu
ingepungua pia. Kupitia mkakati huu ilimaanisha kuwa
mwanaume aliyeolewa nd’o mwisho wa utendaji kazi wake!!
Mkakati huu ukaenda mbali zaidi na kuhamasisha maandamano
ya kuomba haki kwa wanaume wanaotetea ndoa za jinsia
moja. Maandamano haya yasingewezekana ikiwa idadi ya
wanaounga mkono ndoa hizi ikiwa ndogo!!
Mkakati huo ukaanzia kwa watoto, yaani wanakamatwa
wakiwa wadogo kisha wanafunzwa vitendo vya kishoga na
wakishakomaa wanaachiwa huru wakachafue hali ya hewa
mtaani. Hii ingewasaidia kuwa na idadi kubwa sana ya
wanaounga mokono upuuzi huo.
Na iwapo yangetokea maandamano basi nchi zenye sauti
duniani ambazo tayari zimeyaruhusu mambo haya zingeingilia
kati na kufanya ziara za kuhoji juu ya maandamano hayo
yanayohatarisha amani.
Kwa sababu nchi hizo zina sauti kubwa sana na pia zikiwa
zimewekeza mamilioni katika ardhi ya Tanzania basi mkuu wa
nchi hatakuwa na sauti na badala yake atasikiliza ni kitu
gani wao wanataka!!
Na hapo ndoa za jinsia moja zitaanzishwa rasmi na
kuruhusiwa!!
Huu unakuwa mwisho wa mkakati huu thabiti!! Katika namna
ya mafanikio makubwa!!
Mwanzo wa mkakati huu ukawa kuanzisha kambi ya kwanza
ambayo itaanzishwa kama hoteli kubwa ya kifahari lakini
lengo kuu likiwa kuwa kambi ya kuanzia mkakati.
Na hapo ikaanzishwa MICHIGANI ya juu ambayo ilitoa ajira
kwa wananchi wengi hasahasa wakazi wa Iringa!!
Hoteli ilivyokamilika, likaanza tatizo la watoto kupotea
kimyakimya!! Ili lengo lisijulikane wakawa wanawachukua
watoto wa kike na wa kiume!!
Vilio vikasikika na kupotea bila msaada wowote ule kutoka
serikalini.
Akina mama wakasahau juu ya watoto wao!! Hawakujua
kama wanapelekwa Michigani kuandaliwa kuwa mashoga!
Wazee wa kimila na wakongwe wa mji wakalitilia mkazo
tatizo la watoto kupotea mara kwa mara tena kwa wingi na
wasionekane tena.
Mzee mmoja akatilia mashaka Michigani, mwanzoni
akapingwa lakini mwishowe akakubaliwa, malalamiko
yakapelekwa kituo cha polisi, polisi wakaenda kufanya
upelelezi bila mafanikio.
Kikafuata kipengele cha mkakati wa kuitokomeza Michigani.
Nakala ile ikaelezea vikao kadhaa vilivyokaa na hatimaye
kuamua Michigani iteketezwe!
Kambi ya juu ikateketezwa makusudi, wale wazee walioleta
malalamiko wakashukiwa kuhusika katika uteketezaji.
Sheria ikachukua mkondo wake!
Wengi wao wakafia jela! akiwemo baba yake Anitha.
Kambi ya chini kwa chini ikaanzishwa kwa siri baada ya ile ya
Michigan juu kuonekana ipo wazi sana na muda wowote
itafichuka.
Baada ya vipengele vingi ambavyo vilihitaji umakini sana
kuvielewa hatimaye nikakifikia kipengele cha muhimu
ambacho tuliwahi kukitafsiri kama UKIMJUA UNAPOTEZWA.
“Yeyote atakayepingana na sera za Ezekiel lazima aidha
auwawe ama kuteswa hadi afe….(For any Anti- Ezekiel side
.…..)” ilijieleza hivyo! Nilijikuta najiuliza kama niliewahi
kukubaliana na sera yake!
La! Sijawahi hata siku moja kukubaliana na sera ile kwa hiyo
nikajitambua rasmi kama Anti Ezekiel. Kumbe wakati wote
huo nahangaisha akili yangu kumtafuta Anti ezekiel nilikuwa
najitafuta mimi mwenyewe, kumbe hata mama lao ni Anti
Ezekiel pia na Anitha vilevile ni Anti Ezekiel. LABDA HAYA
WEWE!!
Ilistaajabisha.
Kumtafuta mtu asiyekuwepo na baadaye kugundua kuwa
unajitafuta mwenyewe!!
WATOTO wadogo walielezea walichokuwa wanafundishwa
ndani ya jengo lile kubwa!! Walikuwa wanafundishwa uchafu
tupu lakini ilikuwa bahati kubwa sana walikuwa hawajabobea
katika mambo hayo. Ilisikitisha sana kumsikiliza mtoto
mmoja kwa jinsi alivyoweza kujieleza vyema jinsi
alivyokamatwa kwa kulaghaiwa kisha kuingizwa katika ngome
ile. Akaelezea namna walivyoanza kufundishwa kuishi kama
wanawake!!..... aliongea sana na waliomsikia walitokwa
machozi.
Akiwa bado anaendelea kuongea nilimwona mwanamke
akimkimbilia na kumkumbatia. Na hapo nikabaini kuwa
alikuwa ni Jojina!! Akamtoa yule mtoto pale alipokuwa
amesimama na kusogea naye kando.
“Justin….” Niliita, yule mtoto akanitazama.
Naam! Alifanania vyema kabisa na Jojina!!
Alikuwa ni mtoto wake wa pekee ambaye alitekwa miezi
kadhaa nyuma na kuhisiwa kuwa alipotea katika mambo ya
kishirikina.
Tayari askari watiifu walikuwa wameongezeka kwa wingi na
eneo lote lilikuwa katika ulinzi wa hali ya juu.
Mwisho tukatoweka bila kipingamizi chochote, Michigani
ilikuwa wazi hapakuwa na wa kutuzuia, tukawatoa majeruhi
wetu wote, simu zikapigwa na kupata msaada wa haraka
kutoka serikalini.
Afisa aliamuru watuhumiwa wote waingizwe katika
karandika na baada ya hapo mashahidi tulioonekana kuwa
tuna ulazima wa kuhudhuria katika mlolongo wa kesi hiyo
tuliambatana nao pia!
KIHITIMISHO!
MAKABURI ya Morogoro mjini yalinipokea kwa simanzi kubwa
sana, mama lao na Anitha walinisindikiza. Anitha akiwa
amembeba Eva ambaye alikabidhiwa kwangu kutoka katika
hifadhi ya serikali muda wote ambao nilikuwa natafutwa…
Nilipiga hatua za kinyonge sana hadi nikalifikia kaburi la
kwanza.
Hili lilikuwa la mama yangu! Nikazungumza naye kwa kina.
“Mama mwenye upendo na msimamo, mama uliyekuwa radhi
kunipigania mwanao, mama ambaye umeniamini hadi nukta ya
mwisho, mama ambaye umeteswa mpaka kifo chako huku
neno lako la mwisho likiwa ‘nakupenda Sam’.. ulazwe pema
peponi mama. ” machozi yalikuwa yakinichuruzika,
nikamgeukia Anitha naye alikuwa analia kwa uchungu, Jojina
alikuwa anaonekana dhahiri kuwa anajikaza tu lakini
alikuwa kwenye uchungu mkubwa sana!!
Nikahama kutoka pale na kujumuika na familia ya mama Eva,
tukasogea hadi katika kaburi alilopumzika mke wangu
mpenzi. Niliyebahatika kumwona akiwa hai lakini hoi sana
akitolewa katika chimbo la Michigani, jitihada zikazidiwa na
uwezo wa Mungu. Akaamua kumtwaa.
“Wewe mwanamke ambaye ulinibadilisha mitazamo yangu,
ukautwaa utoto na ujana wangu na kunifanya mtu mzima.
Hukufaidi sana matunda ya harakati hizi lakini amini kuwa
bila wewe huenda hata nisingefanikisha zoezi hili gumu,
asante sana kwa mtoto uliyeniachia, najua atalia sana lakini
hatuwezi kubadili ukweli huo kuwa haupo nasi tena.
Ulazwe pema peponi mama Eva!!
Nikatoweka pale, sasa Jojina na anitha wakiwa wamenishilia
mikono yangu, tukarejea garini alipokuwa amelala Eva,
nikaingia na kumpakata. Jojina akashika usukani, safari ya
kuelekea Dar es salaam.
Huko tukakutana na taarifa katika vyombo vya habarai!!
Watumishi wa marehemu Ezekiel ambao wote waliutumikia
mkakati wa kudumu walihukumiwa vifungo vya maisha jela.
Hili lilikuwa jema sana kwa kila mpenda amani na mzalendo
katika nchi yake.
Bwana Masawe aliachiwa huru baada ya kukosa hatia!!
Hilo lilinifurahisha pia.
Na mwisho majina kadhaa likiwemo jina langu yalitajwa kwa
ajili ya kwenda ikulu kuonana na mheshimiwa raisi.
Baada ya siku kadhaa!!
Anitha akarejea chuoni huku akipewa heshima kubwa ya
kuwa mwanaharakati, heshima hiyo pia ilituzwa kwa Jojina,
na mimi pia! Si tu kwa nishani alizotuvika raisi la!!
Nilimsamehe mzee Matata na mkewe kwa imani waliyopoteza
kwangu, Enock na mkewe pia waliupata msamaha wangu pasi
na kinyongo!!
Kwa jiji la Dar es salaam, mama lao akiwa amerejea Tanga,
Anitha akabaki kuwa mtu wangu wa karibu zaidi.
Mazoea yakazaa tabia, tukawasiliana kwa ukaribu zaidi hadi
Eva akalitambua hilo. Akampenda Anitha naye Anitha
akampenda haswa.
Mzee Matata na mkewe ni kama walitarajia kuwa itakuwa
hivyo. Walisema kiutani wamkidai kuwa tunaendana sana….
Naam kweli ikawa!! Na wao wakabariki.
ANITHA AKAGEUKA KUWA MAMA EVA!!!
JIFUNZE: DUNIA ina mapito mengi, ukijikwaa na kuanguka
amini kuwa haujaanguka moja kwa moja, zipo njia zaidi ya
milioni moja za kusimama tena. Usijaribu njia moja tu na
kusema nimeshindwa kusimama nami nitakuwa wa kulala
milele. Jaribu njia zote.
Amini hazitafika njia kumi bila ya wewe kusimama tena!!
Mungu anaziona jitihada zetu kwa jicho la huruma, jaribu
kufanya ukishindwa yeye yupo kusaidia!! Yapinge yale
yasiyopendeza kwa taifa na usoni mwake pia……
Naupinga USHOGA na tabia zote za zinazofanania hivyo.
Mimi ni ANTI - EZEKIEL…. WEWE JE?
MWISHO!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom