SEHEMU YA KUMI NA TANO
ILIPOISHIA
. . Sam wanayo picha sijui ni picha ya nani, hawakagui
tiketi mafala hawa wanakagua sura Sam. Ni hatari Sam
Jojina akazidi kunitia hofu.
. . Niliendekea kudumu katika hali ile bila kujitingisha wala
kukohoa. Hofu niliyokuwanayo katika mazingira haya
ilikuwa mara kumi ya hofu ya siku moja iliyopita nilipokuwa
kabatini nikiwasubiri akina Dulla, na hofu hii ilizidi ile hofu
ya kumuona Jojina akiua mtu.
. . Wakati naitafakari hali inayonikabiri nmara nikaisikia
sauti ya Jojina tena, safari hii ilizungumza kwa uoga zaidi.
. . Sam
tumekwisha
.mafala wana picha yangu aisee
kumbe wananitafuta mimi!! Jiweke safi Sali sala zako za
mwisho, wanatuua hawa!! Hawatuachi Sam
. . Kauli hii haikuwa kavu, iliambatana na mkojo!!
. . Yule mwanamama jasiri alikuwa anajikojolea, ule mkojo
wa moto kutoka kwa Jojina ukatua vyema katika uso
wangu!! Nikataka kujitikisa lakini nikahofia kuharibu zaidi.
. . Hakika Jojina alikuwa ameogopa sana.
. . Na kama alivyosema kuwa tumekwisha ni kweli
alimaanisha, maana jasiri akifikia hatua ya kujikojolea basi
ujue amenyanyua mikono juu
. . ***KUMBUKA!! MUNGU alitumia ubunifu wa hali ya juu
sana kuliko ubunifu wowote uliowahi kutokea popote pale,
kipindi anamuumba mwanadamu. Alimpa kila kitu, lakini
akamnyima uwezo wa kujua nini kitatokea katika sekunde
moja ijayo mbele yetu.
. . Kwa sababu hatujui lijalo, ni vyema kujiweka tayari kila
muda ikiwa hatujui siku wala saa!!!
. . ENDELEA
. . Sikukarahishwa na ile mikojo ya mama lao badala yake
fikra zangu ziligandiana maneno ya Jojina ambaye ndo
alikuwa shuhuda wa kila kinachoendelea.
. . Alikuwa amekiri kuwa hatuna ujanja na tumekamatika.
Niliisikia na kuiona vyema mikono yangu jinsi ilivyokuwa
ikitetemeka, nilijaribu kujiimarisha lakini sikuweza.
. . Wewe kaza uso wako nitazame!!! niliisikia sauti ya
askari ikiamrisha, Jojina akazidi kutetemeka, sasa hakuwa
akijikojolea tena, bila shaka mikojo ilijiishia katika kibofu!! .
.Mimi ndo nilikuwa kwenye mashaka zaidi.
. . Niliiona miguu ya yule askari ikiwa imesimama imara
mbele ya siti ya mwisho kabisa, bila shaka alikuwa
akiwakagua akina Jojina.
. . Niliusikia mkono wa Jojina ulishuka kwa kasi na kuanza
kunipapasa, alinishika sikio mara anishike kichwa!!
Nikajiuliza kulikoni na bado sikufanya jitihada za kumzuia
asinipapase. Sikujua anachokihitaji ni kipi. Mara akanishika
pua na hatimaye akapanda juu kidogo akainyofoa miwani
katika macho yangu.
. . Nilistaajabu nisijue kama hii ni hofu inasababisha ama ni
kipi kinamsibu mwanamama huyu!! Nilikuwa namwomba
Mungu afanye muujiza wowote ule na ile iwe ndoto. Tatizo
ni moja tu!
. . Mungu hapangiwi kazi!! Yeye huombwa tu. Nami
nikalazimika kuomba huku nikitarajia majibu ya haraka
haraka.
. . Hatimaye miguu ile ikageukia upande aliokuwa ameketi
Jojina. Hofu ikaongezeka maradufu.
. . Kwani kuna nini hapa jamani!!! nniliisikia sauti ya Jojina,
sikujua anamuuliza nani.,
. . Tiketi yako ipo wapi mwanamke?? sauti kali ya kiaskari
ilijibu.
. . Tiketi
tiketi yangu mimi
.. Joshua, we Joshua
.. mpe
kondakta tiketi yake. Jojina alijibu nikabaki kuduwaa kule
chini nisijue nini kinaendelea baina yao.
. . Jojina aliendelea kusema maneno maneno, bila shaka
aliyajua mwenyewe mimi nikabaki katika fumbo!!!
. . Kimya kikatanda, nikamsikia yule askari akisonya na mara
akageuza na kuondoka zake. Nilistaajabishwa sana na
muujiza huo.
. . Usitoke
vumilia huko huko!!! alinongona Jojina, nami
nikajizi kujikaza. Gari likawashwa!! Safari ikaendelea na kile
kilichotokea kikabaki kuwa cha kutetwa ndani ya basi.
Baada ya dakika kadhaa Jojina aliniruhusu nitoke kule chini,
hii ni baada ya abiria kadhaa kuwa wameuchapa usingizi
wasijue kama nilitokea kule chini.
. . Jojina umewalaghai kitu gani wewe mwanamke!!
nilimuhoji kwa sauti ya chini.
Akaanza kwa tabasamu kisha akanieleza kitu kilichonifanya
niamini kuwa si lazima uende shule ndipo uwe na uwezo
mkubwa wa kimaamuzi kama wa mama lao.
. . Yaani nilikuwa najua kuwa sitaweza kuchomoka hapa,
yaani kitu nilikuwa nimesahau ni kwamba Dulla huwa ana
picha zangu tena nyingi tu, na wale jamaa waliniona
nikiwanaye na mbaya zaidi aliwatambulisha kwangu. Hivyo
ule mzoga kwa namna yoyote ile lazima skendo za kuua
ziwe juu yangu. Sasa nikajibweteka kimawazo nikiaqmini ni
wewe wanakusaka. Alikuwa pale hivi siti ya nne ndo
nikaiona picha, wacha nichachawe mtu mzima!! Yaani
nikajua tumekwisha. Aliponikaribia zaidi nikaamua kama ni
kufaacha nife kishujaa, ndo pale nikakupapasa nikakutoa
miwani yako harakaharaka nikaitundika katika uso wangu.
Aliponifikia nikaanza kujisemesha, jamaa akaniondoa
miwani, aisee kitu nilichofanya najua mwenyewe,
nikabenjua macho yangu, hii bolti nyeusi ikapotea ikabaki
hii nyeupe, hii michezo naijua sana tangu zamani, wakati
nabenjua nilikuwa napapasa huku na kule na mara
nimkamate mkono, mara nimshike kifua. Nadhani unajua
kilichotokea hapo, wasafiri bila kutumia aki;li wakaanza
kukoroma kuwa mimi sina uwezo wa kuona tena wakitumia
lile neno kali kabisa, kipofu!! Askari akaishiwa hamu,
akanirejeshea miwani yangu machoni, nikayaweka macho
yangu sawa na kumwona jinsi alivyokuwa na wasiwasi.
Lakini nadhani ile picha nikiwa na kipara na uhalisia huu
nikiwa na wigi umemwacha hoi. Kipofu mwenye wigi, wakati
picha ni mtu anayeona akiwa na kipara.
. . Akasonya na kuondoka zake!! Sam siamini hata kidogo
kama
. Akasita kuzungumza, akaniegemea na
kunongona, kuna ----- anatuchora
. Aliniambia na
kisha akanionya kuwa nisifanye jitihada zozote za kupepesa
macho.
. . Pita upesai nenda kamwombe kondakta,,, mwambie
ninaumwa tumbo
.pameharibika Sam hapa nenda haraka.
Akanisihi, upesi nikasimama na kupita nikafanya hima na
kumfikia kondakta. Nikamsihi kama nilivyoelekezwa,
nikalalamika sana juu ya mgonjwa wangu asiyeweza kuona
anaumwa tumbo.
. . Kondakta akanielewa, nikarejea na kumchukua Jojina
katika namna ileile ya kumwongoza mimi mbele yeye
nyuma, akiigiza kuwa hana uwezo wa kuona. Wakati huu
niliweza kumtilia mashaka yule mtu ambaye Jojina alidai
kuwa hana nia nzuri, nilimwona akinongona na mwenzake.
Nikajifanya sijui lolote linaloendelea.
. . Tulipoufikia mlango mimi nikiwa mbele kama kawaida
mara tukasikia sauti kali ikiamrisha.
. . Ninakutilia mashaka wewe mama usiyeweza kuona.
Simama hapo hapo ulipo!! Nayaongea haya kwa mamlaka
niliyopewa na jeshi la polisi Tanzania. Niliskia miguu
ikiishiwa nguvu, nikaanza kutetemeka. Lakini haikuwa hivyo
kwa mama lao.
Ghafla akanisukuma nikatangulia nje.
. . Saaaam poteaaaaa!!! ndo neno pekee alilotoa, akatupa
miwani huko, akaikunja sketi yake. Akili ikafanya kazi
vyema sikulemaa, mwanamama anakimbia sijapata kuona,
kumbe ule unene ni gelesha tu.
Nikaanza kufuata nyuma, huku nyuma zikawa zinasikika
kelele za abiria. Yule askari sikuisikia sauti yake. Na niisikie
ili iweje tena.
. . Nikapenya kila alipopita Jojina, mimi nyuma.
. . Simama la sivyo nafyatua risasi!!! ilisikika sauti kwa
mbali, almanusura nisimame kama yasingekuwa maneno ya
Jojina.
. . Sam usisimame hakuna kitu hapo Sam kimbia.
Alinisisitiza pasipo kugeuka nyuma. Maneno yake yakanitia
wazimu wa kukimbia nikakazana zaidi. Hakika hatukujua ni
wapi tunakwenda!!
. . Taratibu nilianza kuchoka, na bado nilisikia vishindo kwa
nyuma. Jojina alikuwa ameniacha tayari na vile tulikuwa
tukipenya katika majani sikuweza kumwona kabisa. Hofu
ikaanza kutanda, dalili za kukata tamaa zikanikumba.
. . Jojinaaa
..Jojinaaa.. nilianza kuita lakini sikujibiwa.
. . Simama kimburu Kenge, shenzi kabisa simama. Sauti
iliamrisha kwa nyuma. Nilikuwa nimechoka, nikasikia miguu
ikigongwa kwa nyuma, nikayumbayumba kisha kama mzigo
nikatua chini.
. . Meno yangu yakauma nyasi!!! Nikajitahidi kugeuka
nikakutana na mwanaume akiwa ameshikilia pingu. Alikuwa
anahema juu juu, ni yuleyule mwanaume ambaye
tulikuwanaye ndani ya gari. Alikuwa ananitazama kwa jicho
kali.
. . Shetani mkubwa!!! nikasikia sauti nyingine ikasikika
ikitokea katika majani!!! Mimi na yule mwanaume mwenye
pingu tukatahamaki, lakini hatukudumu sana mara yule
mwanaume akaaguka chini akijishika kichwa, nikaona jiwe
kubwa pembeni yake. Na hapo akatokea yule mama
aliyejikojolea ndani ya gari.
. . Jojina kwa mara nyingine!!!
. . Mshenzi mkubwa wewe ukipona nenda kamweleze mkuu
wako wa kazi kuwa kuna watu wabaya anawafuga huko.
Alikoroma mama lao. Lakini huyo mtu aliyepewa nafasi ya
kupona akataka kuleta ujanja, ambao Jojina aliutegemea
kumbe, akasimama na kurusha teke, mama lao akaingiza
mkono wake katika sketi yake, akatoka na jiwe jingine
kazuga kama analirusha yule askari akajificha kwa kutumia
mikono miwili huku akiruka kando.
. . Jojina akatabasamu wakati yule bwana anaitoa kinga
yake usoni, hapohapo akalivurumisha lile jiwe.
. . Nilibahatika kuona meno kadhaa yakitoka katika kinywa
cha yule bwana. Kufikia hapo mama lao hakuwa akizuilika.
. . Auaye kwa upanga
alisema huku akitua juu ya mwili
wa yule bwana anayevuja damu, Atauwawa kwa upange
vilevile akamalizia huku akiishika ile pingu na kuanza
kumcharaza nayo yule bwana usoni.
. . Kila alipoituliza paliumuka kisha damu!!
. . Akapiga kwenye taya, akapiga paji la uso!! Akapiga kila
kona!!!
. . Kisha mbio zikaendelea. Kidogo nilikuwa nimepumzika.
Nikaweza kukimbia zaidi, wakati huu tukiwa sambamba na
mama lao Jojina.
. . Niliwahi kuwa mwanariadha shule!! alisema bila
kunitazama.
. . Sikumjibu.
. . Hapakuwa na mtu anayetufuatilia kwa nyuma!!!
. . Hivi unajua tunapoelekea lakini? Jojina aliniuliza, hapo
tukajikuta tunapunguza mwendo taratibu huku kila mmoja
akikumbwa na kiwewe.
. . Hata sijui ndugu ujanja wangu mimi Morogoro mjini tu
Msamvu, Kihonda basi!! nilimjibu na hatimaye tulikuwa
tumesimama.
. . Jojina akajipekua na kutoka na simu yake katika koba lake
ambalo hakuwahi kulitua hata mara moja tangu tuliposhuka
garini na kuanza kutimua mbio.
. . Simu imezima chaji aisee tungeweza hata kutumia
ramani ya simu kama ingeweza kufaa. Akasonya kisha
akairudisha simu yake mkobani.
. . Tukaendelea kutembea kuelekea mbele bila kufahamu
kama ni salama ama hatari.
. . HIFADHI YA TEMBO MIKUMI Kibao kikatukaribisha
baada ya mwendo mrefu.
. . Mungu wangu tupo mbugani Sam!! Mbugani Mikumi
hapa
aliweweseka Jojina nami nikapagawa. Hapakuwa na
ngojangoja zaidi tukaanza kukimbia kuelekea uelekea
mwingine, tukapishana na makundi ya Swala, na kwa mbali
kabisa tukaiona barabara. Tukaukaza mwendo zaidi hadi
tulipoifikia ile barabara.
. . Ilikuwa barabara ya vumbi, na ilikuwa bahati yetu tena
tukaonana na wanadamu. Tukauliza na kupewa uelekeo wa
barabara ya kuelekea Iringa, tukakaza mwendo, miguu
yangu ilikuwa hoi sana lakini sikukubali kuonekana
lelemama.
. . Sam hawa jamaa tunaopambana nao hawa
wananikumbusha hekaheka za Tunduma huko. Jojina
akaanzisha maongezi, walau mwendo na maongezi
wapunguza uchovu.
. . Tunduma? Harakati zipi tena huko.
. . Wakati ule wa uchunaji ngozi bwana!! Yaani kuna mdogo
wangu fulani hivi kidogo achunwe ngozi, mwanamama
nikaingia front kutetea damu aisee, yaani mafunzo ya
mgambo niliyopitia yananibeba sana mara kwa mara.
Nikamjua jamaa anayewafahamu mabwana waliomteka
dogo, aisee akajifanya mbishimbishi, nilimpiga ngumi mbili
akalegea huko nikamkamata, nikamuwasha vibao ka vinne
hivi wacha apagawe!! Nikamzuga kama nampiga teke
akasema atanipeleka, nikamshika ile staili inaitwa
Tanganyika jeki, yaani nikamkamata suruali yake huku
nyuma nikamyanyua akawa anatembelea vidole. Moja kwa
moja hadi eneo la tukio, saa nane usiku hiyo mwanamke
barabarani. Nimeficha kisu huku kwenye pindo la sketi,
tumbili yeyote ajiweke mbele yangu nafyeka korodani zake
namtia uhanithi mimi!!, nikafika pale, nikatia mkwara na
jamaa akiwasihi, mbona walimtoa ndani, walikuwa ndo
wanajiandaa na safari ya kwenda Zambia wakamchune
ngozi
.nikaondoka naye mabwege wananishangaa tu!!
Chezea mama lao wewe!!! alimaliza simulizi hii kwa
majigambo, nikamkodolea macho wakati huo tukiwa
barabarani tayari.
. . Kichwani nikakiri kuwa huyu Jojina alikuwa na mengi zaidi
ya nilivyomtambua.
. . Baada ya muda tukafanikiwa kuelewana bei na lori la
mbao lililokuwa linaelekea Mafinga, Jojina akawa siti ya
mbele mimi nikawa nyuma huku na vijana wengine.
. . Safari hii haikuwa na mushkeri wowote ule.
. . Tukafika Iringa mjini majira ya saa nne usiku!!
. . Tukatembea kwa miguu kuitafuta nyumba ya Jojina.
. . Tukaifikia nyumba vyema, lakini mazingira haya yalikuwa
tofauti kidogo!! Ni kama kuna aidha ukarabati ulikuwa
umefanyika ama la yale makazi kuna mtu aliongeza ama
kupunguza kitu.
. . Naam!! Tulipoufikia mlango palikuwa na kufuri!!
. . Nani amefunga sasa? Wakati sisi tulikuwa tukitumia
kitasa cha kawaida!!
. . Hatukungoja usiku ule upite, tukazunguka kwa nyuma na
kuifikia nyumba ya mmiliki wa nyumba zote pamoja na
chumba alichokuwa amepanga mama lao!!
. . Mwenye nyuma alikuwa hajalala, kuna mambo ya faragha
alikuwa anashughulika nayo na mkewe na bila shaka ujio
wetu ulimshtua sana!!!
. . Kulikoni Jojina
aliuliza kwa sauti tulivu.
. . Mimi ndo niulize kulikoni kama ni kodi yako nilimaliza
mapema tu vipi tena kufuli jipya mlangoni kwangu!!
. . Mwennye nyuma akaduwaa kabla hajauliza.
. . Wewe mwanamama wewe mbona mnataka kunivuruga
sasa. Si wamekuja kaka zako hapa na dada zako wengine
kudai kuwa unahama wewe, tena wamekuja na simu yako
wewe kuwa haurudi tena hapa. Tena kizuri zaidi walikuja na
mwenyekiti wa mtaa na mjumbe, mimi nikawaruhusu
wakachukua mizigo yako kuwa wanakuletea huko ulipo,
sijui kwa mume wako wewe!! Mi hayo sijui na hapa
wakaacha vitu vichache tu!!! alijibu kwa kujiamini baba
mwenye nyumba.
. . Mungu wangu weeeee!! Bahasha!!! ndicho kitu cha
kwanza kabisa kukumbuka kuwa tulikiacha ndani ya
chumba kila kabla ya kusafiri!!!
. . Jojina akalegea na kushuka chini.
. . Akakaa!!
. . Nikaungana naye katika fedheheko hili!!!
. . Bila kithibitisho kile ni wapi zaidi pa kujitetea?
. . Tumekwisha!!!!
. . Nilikiri kimoyomoyo!!!