Riwaya: Ant Ezekiel

Riwaya: Ant Ezekiel

SEHEMU YA KUMI NA SABA
Kauli ya kwamba ukilijua jina la mbwa basi hakutishi
niliduwaa haikufanya kazi, niliita jina la Simba lakini mbwa
yule alionekana kuwa mwenye hasira kali zaidi,
aliunguruma kisha akaendelea kunisogelea. Mapigo ya moyo
yakazidi kwenda kasi na amani ikatoweka tena.
Mara akaanza kubweka, nikafanya kosa kutishia kuwa
naweza kupambana naye kwa kumtisha kama namfukuza.
Jibwa likatanua kinywa na bila shaka alitaka kufanya
shambulizi!!!
Nikaamini kuwa ng’ombe wa masikini hazai ni usemi sahihi
kabisa. Nikakiona kifo tena mbele yangu. Nguvu nazo
zilikuwa zimeniishia.
**UJUMBE! Kukata tamaa nd’o asili ya mwanadamu,
hasahasa akishafanya jitihada zake binafsi pasi na
kumshirikisha mtu!! Lakini je? Kukata tamaa ni suluhu ya
kujikwamua kimaisha, ama kufanikiwa lolote lile?
Wanadamu wengi hushindwa kutimiza ndoto zao kwa
sababu ya pepo hili la kukata tamaa.
Ili ufanikiwe katika maisha ni lazima ulishinde pepo la
kukata tamaa lakini vinginevyo katika kila vita ulimwenguni
wewe utakuwa wa KUSHINDWA TU!!
Utaishindwa vita ya kuupinga umasikini, utashindwa vita ya
kudharauliwa na mwisho kabisa utashindwa vita kuu ya
KUSHINDWA KUIONGOZA AKILI YAKO!!!
TAFAKARI!!
ENDELEA
. . “Acha simba!!!” ikaamrisha sauti kali. Nikapepesa macho
ili nijionee ni nani huyo!!
Na hapo akatokea MAMA LAO akiwa na tabasamu usoni na
rungu kubwa mkononi!!
Alikuwa anatokwa damu mdomoni lakini hakuwa na kitu
kinachoitwa wasiwasi tena, akaanza kutembea zaidi.
Alikuwa anachechemea!!
. . “Mama lao…” nikajikuta natokwa na sauti yenye
kitetemeshi.
. . “Tuondoke hapa Sam. Wajinga wana mtandao mpana
sana hawa. Simama Sam jikaze simama tupotee hapa.”
Alinisihi Mama lao, lile jibwa lilibaki kutikisa mkia, bila
shaka lilimjua vyema Jojina na mbwa akojuaye….
Hakuna kilichoharibika.
. . Nikajikaza nikasimama wima, mbwa huyu hakuwa na
madhara tena kwangu ilhali Jojina alikuwa amemkaripia
tayari.
. . Nikajikongoja huku nikiyasikia maumivu ya kiuno bado.
Lakini ilikuwa heri maumivu haya kuliko kuuwawa kabla
sijatimiza azma yangu.
. . Sikujua kama mwendo wangu ulikuwa mdogo kiasi cha
kumkwaza Jojina, hakusema na hata angesema isingesaidia
kuniongezea mwendo mgongo ulikuwa unauma sana, na si
hivyo tu hata nilipojaribu kukimbia yale maumivu ya kinywa
kilichopasuka yalisababisha kichwa kiwe katika maumivu
makali sana. Jojina alinitazama kwa huruma huku akizidi
kukaza mwendo.
. . Mara akasimama ghafla kisha akachuchumaa, nikamfikia
nikiwa nashangaa.
. . “Panda mgongoni Sam… panda upesi” aliniamuru, ni kitu
ambacho sikukitarajia hata kidogo lakini hakuwa na
masihara hata kidogo, akarudia kauli yake safari hii kwa
kuamrisha.
. . Nikajiweka mgongoni, Jojina akasimama kama kifaru
akaanza kutimua mbio mimi nikiwa mgongoni. Usiku wa
giza tukielekea anapopajua yeye. Niliyafumba macho yangu
kukabiliana na uchungu niliokuwa nikiusikia. Kichwa
kilikuwa kinauma haswa!! Lakini haukuwa wakati muafaka
wa kulalamika.
. . Mama lao akaendelea kutimua mbio.
. . “Taksiii….Taksiiii msaada tafadhali mgonjwaaa!!” aliita
kwa nguvu baada ya kuziona taksi kadhaa zikiwa
zimeegeshwa.
. . Dereva moja akawahi upesi akaufungua mlango wa teksi
yake. Hapo sasa nilikuwa nimefumbua macho nikishuhudia
filamu hii ya aina yake.
. . “Tupeleke Stendi ya mabasi…” aliamuru Jojina na hapo
nilikuwa siti ya nyuma na yeye akiwa pembeni yangu.
Dereva alibaki kuduwaa ni kama hakuwa akiamini kama
tulikuwa na pesa ya kumlipa, Jojina akaling’amua hilo, upesi
akajipekua na kutona na noti nyekundu akamlipa dereva.
Akatia gari moto tukatoweka…njia haikuwa mbaya sana
hivyo wakati huu nilipata fursa ya kutambua kuwa kinywa
kilipasuka japo si vibaya sana lakini shingo ilikuwa inauma
sana bila shaka yule bwana aliyenipiga mateke.
. . Stendi haikuwa mbali, tukapewa pesa yetu iliyosalia na
kutelemka, wakati huu nikijikongoja mwenyewe. Kila kitu
katika suala la maamuzi nikamuachia Jojina maana walau
yeye alikuwa na unafuu.
. . Sikujua alikuwa na maana gani usiku mnene kama ule
kuamua safari ya kuja stendi lakini hakuniacha niumie akili
kutafakari sana, mara akaita teksi nyingine.
. . “Tupeleke Gangilonga” akatajiwa bei akalipa.
Ukimya ukatawala kwa takribani dakika kumi na tano.
Tukatelemka mahali ambao Jojina aliamua yeye.
. . Teksi ilipoondoka tukatembea kwa mwendo wa miguu
hadi katika nyumba kubwa kiasi iliyozungukwa na majani
mengi, bila shaka ni kutokana na watu kutoishi eneo lile
kwa muda mrefu.
. . Jojina alivyofika pale geti lilikuwa limefungwa na
hakushtuka ni kama kitu alichokitarajia.
Akachumpa ukutani akatua upande wa pili. Kisha akafungua
geti dogo na kuniruhusu niingie ndani.
. . “Miezi sita sijakanyaga hapa aisee.” Alisema neno la
kwanza tangu tufike pale. Sikuchangia chochote.
Akaniongoza hadi ndani, uzuri wa Iringa hakuna vumbi kali
sana, badala yake vipindi vya baridi huchukua nafasi kubwa
zaidi hivyo hapakuwa na madhara ya vumbi.
. . “Hapa hakuna umeme wala nini Sam.” Alizungumza tena,
nikamuunga mkono kwa kumweleza kuwa hilo si tatizo cha
muhimu usalama wetu.
. . Akapapasa huku na kule akaibuka na mshumaa, kisha
akavuta kumbukumbu na kupapasa sehemu nyingine
akaibuka na kiberiti na kisha kutengeneza mwanga
hatimaye.
Nikaketi naye akaketi katika makochi chakavu yaliyokuwa
pale ndani.
. . “Baba yangu alikufa maskini lakini walau alijenga kibanda
hiki kwa taabu.” Akaanzia hapo, hili halikunigusa sana.
Nilitamani kusikia juu ya namna tulivyoweza kuokoka.
Nikaamua kumuuliza.
. . Akatabasamu kidogo kisha akaketi vyema!!
. . “Sam, yaani japokuwa huwa siendi katika nyumba za
ibada hata miezi sita ama mwaka lakini nimeamini kuwa
Mungu huwa hamtupi mja wake…. Lakini najiuliza iwapo
nami ama sisi ni waja wake. Maana nikiwa katika kile
chumba changu nikaisikia sauti ya baba mwenye nyumba
ikilalamika, na kuna watu walikuwa wakitoa karipio.
Nikasitisha nilichokuwa nafanya, simu yangu nilikuwa
nimeweka katika chaji. Nikainyofoa kwanza nikaiweka katika
mkoba wangu. Nikatuliza akili, mara nikaona mwanga wa
gari. Mwenye nyumba wangu hana gari, nikajishtukia na
kuheshimu machale yangu kuwa hapa mambo yanaanza
kuharibika, nikapitia dirishani mbiombio nikakimbia hadi
nyuma ya nyumba ambapo sauti hizo zilikuwa zinatokea.
Nikasikia wakimuuliza juu yangu iwapo nimerudi, kisha
wakamuuliza iwapo amewahi kuniona na mgeni. Nikasikia
wakimuuliza iwapo anaifahamu sura fulani katika picha
ambayo najua tu ni yako hakuna mwingine. Mwenye
nyumba akakiri kuwa nilikuwa nimerejea tayari. Lakini
hakukubali kiwepesiwepesi badala yake walimpa kipigo
kwanza nd’o akalainika.
. . Alipokubali kuwaongoza kuja upande wa kile chumba
changu na stoo pia ndipo nikashtuka na kuja mbiombio
upande ule, nikakuita hukuitika, nikawasha tochi nd’o pale
ukanipa ile bahasha!!! Wajinga wakavamia pale mimi haraka
nikadidimia chini.
. . Sam niliumia sana nilipowashuhudia wakikupa kipigo
kiasi kile, bahati nzuri ndani ya chumba changu tofauti na
simu nilichukua pia kile kirungu changu cha mgambo si
nilikwambia nilipita huko, kiukweli hicho kirungu
niliwadhulumu.
. . Nikajiuliza sasa mimi na kirungu nitakusaidia kitu gani
mie. Wakakutukana matusi mazito, nikatamani kukimbia
lakini ningeweza vipi kukuacha ufe hivihivi.
. . Nikatamani kupiga kelele lalini mwenzangu we, sisi
wahehe ni waoga sio siri, yaani unaweza kupiga kelele
asitokee hata mtu mmoja sasa hapo ni kipi kama si
kujitafutia kufa burebure.
. . Nikataka kuwakabili kwa kirungu lakini kweli wanaume
wanne kwa kirungu kimoja, si matusi hayo!!
. . Nikajikuta naketi chini, na hapo nikakumbuka jambo la
muhimu kupita yote na siajui tu niliwaza vipi kuhusu mbwa
wa kufugwa wa baba mwenye nyumba. Yule mbwa huwa
hana masihara, baba mwenye nyumba alipewa na wazungu
fulani hivi rafiki zake. Nikavamia banda nikalifungua, uzuri
ananitambua yule mbwa!!
. . Nikamvuta hadi nyuma ya nyuma, ghafla nakutana na
wanaume wawili kati ya wanne nikatambua kuwa kazi sasa
imeanza.
. . Nikamwachia mbwa akala sahani moja na bwana mmoja
halafu mimi na kirungu dhidi ya mwanaume asiyekuwa na
silaha, Sam nilimrukia, akanipiga teke mbavuni yule -----,
nikajikaza nikafyatuka na rungu nikalituliza hapa (akagusa
utosi wake) jamaa akalainika bila kupiga kelele, chini!!. Ile
nageuka namkuta mwenzake akitapatapa pale chini damu
inamruka, nikammulika nikahisia kuwa uhai ulikuwa
unafanya urafiki naye. Nikamrukia kwa ghadhabu, kabla
sijamfikia nikajikwaa nikaanguka chini, nilipoamka hasira
zote kwa yule bwana, na yeye nikamtandika rungu kwenye
paji la uso. Bila shaka kajifia yule we tungoje taarifa ya
habari tu. Kuja kusimama wima tena simwoni mbwa.
Nikataka kumwita kwa sauti ya juu lakini nikahofia usalama
maana nilitambua fika kuwa wale wanaume wawili wapo
bado kule mbele. Nikaanza kunyata taratibu gizani ili
nitambua kulikoni, nd’o hapo nikaisikia sauti ya baba
mwenye nyumba ikimwamrisha mbwa kushambulia!! Walau
amani ikarejea japo niliendelea kunyata, hadi wakati
nafanikiwa kufika ndipo namuona yule mbwa akitaka
kukushambulia nikamzuia…Sam Mungu ametupangia jambo
fulani amini!! Hili tukio halikuwa la kuokoka kirahisi namna
hiyo hata kidogo.” Jojina alimaliza na kushusha pumzi kwa
nguvu, nami nikashusha pia kama tuliambizana kufanya vile
kwa pamoja.
. . “Sam nadhani tunatakiwa kupumzika halafu kesho
twende Makanyagio. Lazima tuanzie huko.”
. . “Makanyagio? Nd’o wapi huko??”
. . “Kweli wewe mgeni Iringa nimeamini. Huko ni sehemu
maarufu sana kuna makaburi kule, kama unakisikia chuo cha
Mkwawa basi ndo kuelekea hukohuko.” Alimaliza kisha
akasimama, lakini mimi sikuwa na usingizi. Jojina akaleta
godoro la pamba ambalo lilikuwa linatoa harufu ya uvundo
akalitandika pale sebuleni.
. . “Tutalala hapa maana huko chumbani hapalaliki kuna
harufu sana.”
. . “Popote tunalala Jojina.” Nilimuunga mkono.
Akajitupa na baada ya muda alikuwa anakoroma, nilijaribu
kujilazimisha kulala lakini hata usingizi haukujileta jirani
nami.
Nikapata wazo la kujishughulisha na bahasha na yaliyomo.
Maana swali juu ya hawa watu walikuwa wanatafuta nini na
mbona wameacha ile bahasha lilikuwa linanisumbua.
Nikaichukua bahasha kutoka katika kiti alichokuwa ameketi
Jojina.
. . Nikashtuka na mapigo yangu ya moyo yakaongeza
mwendo kasi. Bahasha ilikuwa nyepesi sana tofauti na
ilivyokuwa awali wakati inabeba picha na makorokoro
mengineyo.
. . Nikaanza kutetemeka nikiamini kuwa ule ushahidi
nilioupigania kwa muda mrefu umetoweka, nikaingiza kwa
uoga mkono ndani ya ile bahasha. Hapakuwa na makaratasi
mengi sana.bali karatasi moja tu!!
. . Nikalichomoa upesi. Lilikuwa karatasi tofauti kabisa na
yale ambayo yalikuwa ndani ya bahasha ile awali.
Nilianza kumwamsha Jojina awe shahidi lakini bahati mbaya
hakunisikia hata kidogoa alikuwa amezama katika dimbwi la
usingizi.
. . Nilijaribu kuiweka akili sawa labda si bahasha
ninayoitazamia, lakini ilikuwa ni ile na sasa haikuwa na kitu
ndani yake.
. . Nikafungua ile karatasi kwa makini nitambue kama nayo
ni moja kati ya zile za awali lakini hapana hii ilikuwa
tofauti.
Nikajongea katika mshumaa, nikaanza kuisoma.
Hofu ikatanda maradufu, ulikuwa mwandiko wa kike.
. . “Sam kama huu ujumbe utakufikia, fanya kila uwezalo
uniokoe Sam. Nimefanya kila jitihada nijitoe katika mikono
ya watu hawa lakini jitihada zimegonga mwamba.
Nakuandikia ujumbe huu nikiwa nimekata tamaa kabisa ya
maisha na sina uhakika kamaq utaupata ujumbe huu, Sam
yanayotokea huku hayasimuliki hata kidogo kwa maandishi,
ninayoyashuhudia huku nilipo ni mazito mimi na wewe
hatuyawezi bila msaada wa watu wengine, lakini hao watu
wengine ambao nawasema wote wapo katika upande wa
watu hawa. Sam kama ukiona ni ngumu sana kuniokoa,
amini kuwa nimeridhia kufa. Wewe funga safari ondoka
katika nchi hii, nenda mbali Sam maana ukiingia huku
hautatoka Sam. Jiondokee uende mbali labda utapata
msaada kutoka kwa watu wengine huko wasiokuwa wenyeji
wa ardhi hii.
Natamani sana walau ningejua huku nilipo ni wapi lakini
bahati mbaya sina hata kitu kimoja cha kufananisha eneo
hili. Na bora ningekuwa natulia sehemu moja, hawa jamaa
wananihamisha kila leo. Nimeuza utu wangu Sam na
nimeshiriki penzi na huyu bwana ambaye kama ni mkweli
atakufikishia ujumbe huu, ameshindwa kabisa kunivujishia
siri za humu lakini amesema kuwa hapendezwi na mambo
ya humo na atakushirikisha. Nimeamua kumwamini kwa
sababu sina namna na hata nisipomwamini mimi ni wa kufa
tu Sam wangu!!! Sama kama itakuwa sawa naomba
umsikilize huyu bwana, macho yake hayadanganyi hata
kidogo, na laiti kama pasingekuwa na vifaa vya kurekodia
humu ndani angeweza kunieleza jambo nami nikakuandikia.
. . Sina thamani yoyote zaidi ya uhai nilionao,
nimejirahisisha kimapenzi mara kadhaa ili niweze kuokoka
lakini haijasaidia. Nimejirahisisha kwa huyu bwana pia, sijui
kama nitafanikiwa ame nimeshindwa!!!
. . Samahani kwa mwandiko huu mbaya, nimeyaandika haya
nikiwa katika giza, narudia tena kama huyu bwana ni
mkweli basi alifanya hila ya kuzima taa na kuzuia kamera
kuweza kunirekodi, nikafanikiwa kukuandikia haya.
Sam, kama sitafanikiwa kupona nifikishie salamu hizi kwa
mama yangu mwambie nampenda sana, pia mwambie mzee
Matata katika maisha yake ajifunze kumsikiliza mtu kabla
hajaamua kumuhukumu. Hii itasaidia kuokoa wengi.
. . Akupendaye!!!
. . Anitha
 
SEHEMU YA KUMI NA NANE
. . Samahani kwa mwandiko huu mbaya, nimeyaandika haya
nikiwa katika giza, narudia tena kama huyu bwana ni
mkweli basi alifanya hila ya kuzima taa na kuzuia kamera
kuweza kunirekodi, nikafanikiwa kukuandikia haya.
. . Sam, kama sitafanikiwa kupona nifikishie salamu hizi kwa
mama yangu mwambie nampenda sana, pia mwambie mzee
Matata katika maisha yake ajifunze kumsikiliztu kabla
hyajaamua kumuhukumu. Hii itasaidia kuokoa wengi.
. . Akupendaye!!!
. . Anitha
. . Barua ilimalizika nisijue kama imemaridhika, maneno
yaliyoandikwa ndani ya barua ile yalikuwa mazito sana.
Nikamkumbuka yule bwana aliyekuwa akinibinyia macho
kila mara nilipofanikiwa kutazamana naye, sikuweza kupata
jibu la moja kwa moja iwapo ni yeye aliyeagizwa na Anitha
kunifiikishia ujumbe ule.
. . Nikakumbuka pia jinsi yule mbwa alivyomng’ata shingoni
na labda kuondoka na uhai wake.
. . Labda alikuwa mtu mwema!!! Macho yake yalijawa na
huruma yule mtu!!!
. . “Jojina….” Sasa nikamkanyaga kwa nguvu, akaamka.
Nikamshirikisha juu ya nilichokutana nacho katika bahasha
tuliyosadiki kuwa ina nyaraka zetu za kutuongoza.
. . Kama nilivyoduwaa na yeye akaduwaa vilevile. Akaisoma
barua na kuimaliza.
. . “Sam, hawajatuchezea akili hawa tujiingize mkenge!!!”
. . “Hapo n’do pagumu pa kuamini na pagumu zaidi
kukataa.” Niliishia kujibu kwa sauti ya chini.
. . “Inawezekana kumbe Anitha yupo hapahapa Iringa eti!”
akaniuliza swali la kizembe kabisa. Sikumjibu badala yake
nikabetua midomo.
. . Hakuna aliyelala tena!!!
. . Bahasha iliyokuwa na zile takwimu nyingine za muhimu
ikawa imepotea katika namna ile ya kustaajabisha.
. . . . . . ****
. . SAA MBILI asubuhi tulikuwa maeneo ya Makanyagio,
Jojina alikuwa kiongozi kama kawaida. Kwa mtazamo
alionekana kuipoteza kumbukumbu ya nyumba ambayo
alikuwa anataka twende, mbaya zaidi alilisahau hata jina la
mzee wa makamo ambaye alihitaji twende kuonana naye.
. . “Ujue nimekuja huku mara ya mwisho mwaka juzi ule,
sasa watu wamejenga majumba yao huku, siikumbuki
nyumba hata kidogo. Na jina nd’o limenitoka sasa.”
Alilalamika, tayari ilikuwa saa saba.
. . Hadi majira ya saa kumi na mbili hatukuwa tumefanikiwa
kwa lolote.
. . Tukarejea Gangilonga kisirisiri usiku mnene.
. . Jojina alijituliza peke yake akivuta kumbukumbu hii mara
ajaribu kubinyabinya kichwa chake. Nilimsikitikia sana
maana macho yake makubwa yalikuwa mekundu, akachukua
kipande cha mkaa na kuandika chini herufi A hadi Z
akidhani kwa kuiona herufi fulani atakumbuka jina la mzee
huyo ambaye sikujua alihitaji nini kutoka kwake.
. . Bado hakulikumbuka jina!!
. . Angeweweza kukumbuka hata majina ya watoto wake
lakini bahati mbaya hakuwahi kuwa na mtoto wa kumzaa.
. . “Sam…Sam….. “ Ghafla Jojina aliniita, nikiwa nimeduwaa
akanishika mkono na kunivuta kuelekea chumbani.
. . “Baba alikuwa anaandika namba za simu katika kitabu
fulani hivi…..” alizungumza huku akianza kupekuea maboksi
kadha wa kadha na mimi nikamsaidia. Haikuwa kazi nyepesi
kulikuwa na harufu kali sana isiyostahimilika. Lakini
tulilazimika kujikaza.
. . Saa nane usiku na dakika kadhaa nikafanikiwa kupata
kijitabu kidogo rangi ya kijani. Jojina akapiga kelele
kushangilia. Kilikuwa chenyewe, upesiupesi akapekua
majina.
. . “Mzee Madati huyu hapa!!!” akakutana na jina ambalo
alilihitaji.
. . Tukalala tukiwa na jina hilo vichwani mwetu!!!
. . Mzee Madati!!!
. . . . UTATA MPYA WA ANTI EZEKIELI
. . KAMA ilivyokuwa siku iliyopita maeneo ya Makanyagio,
tulihangaika kuuliza huku na huku hatimaye tukaipata
nyuma iliyojificha sana tukaelezwa kuwa hapondipo
anapatikana mzee Madati. Ajabu sasa kila ambaye
alituelekeza alitutazama kwa mashaka, wakati mimi
nilikuwa na kofia ya pama na miwani kichwani na Jojina
naye alijifunika vyema na wigi lake asiweze kuonekana.
. . Tuliwakuta akinamama watatu wakiwa wanatwanga
majani ambayo mimi sikuyafahamu. Nikawasalimia kwa
Kiswahili lakini hawakunijibu.
. . Jojina akawasalimia kikabila, mimi nikabaki kimya
nisiambulie neno hata moja.
. . Hata yeye hawakumjibu vilevile.
. . “Tunahitaji kuonana na mzee Madati….” Alizungumza
Kiswahili hatimaye. Bado wale wanawake hawakujibu kitu.
Mmoja wao akaingia ndani, na baada ya hapo akatoka kijana
moja mrefu mwenye macho mekundu.
. . “Samahani tunahitaji kuonana na mzee Madati!!” alisema
kwa unyenyekevu Jojina lakini yule kijana hakuguswa na
unyenyekevu huo.
. . Akatutazama na kutuuliza ni ipi shida yetu.
. . Jojina alishindwa aanze vipi kujielezea shida yake kwa
mtu baki kiholela namna ile, nikamwona akianza kukunja
ndita nikatambua anataka kuzua zogo. Nikamkanyaga
mguu, akatambua dhima yangu. Akatulia
. . “Kaka tuna shida kubwa sana ambayo ni yeye tu wa
kuisikiliza.” Alisema Jojina kwa sauti ya chini kabisa.
. . “Mnatoka wapi.”
. . “Gangilonga!!”
. . “Mbona unajibu wewe tu mwenzako yupo kimya, we
jamaa unatoka wapi?” alikoroma yule kijana. Mara
nikamwona Jojina akitokwa na tabasamu na hapo akatokwa
na kauli iliyoleta urafiki.
. . “We Geza wewe yaani ujue nilikuwa nimekusahau kabisa,
mwone mtoto mdogo unakoroma hivyo!!!”
. . Yule kijana akashtuka kuitwa jina lile.
. . “Ndema mie!!” Jojina akajitambulisha kwa jina jipya.
Kumbe lilikuwa jina lake la ukoo.
. . Sura ya yule kijana ikajawa na tabasamu si yeye tu na
wale akinamama wakaanza kuzungumza, wakamsemesha
Jojina kikabila naye akawajibu. Wakakiri kuwa alikuwa
amebadilika sana.
. . Tukakaribishwa ndani!!
. . Mzee Madati alikuwa mahututi kitandani!!!
. . Ilisikitisha kumtazama, lakini nd’o ilikuwa hali yake
haswa.
. . Jojina akazungumza kwa muda mrefu sana na ile familia
kwa kikabila. Baadaye akaninong’oneza.
. . “Ile homa ya Ezekiel inamwondoa mzee Madati.” Kauli
fupi lakini nzito sana.
. . Nikatamani kuuliza lakini hatukuwa huru kiasi kile.
. . Jioni hiyo tukapata fursa ya kuzungumza na mzee Madati
alipokuwa ameamshwa kwa ajili ya kunywa uji pamoja na
dawa.
. . Alichukua muda sana kumkumbuka Jojina, lakini
alipomkumbuka ilikuwa shangwe tele. Alizungumza naye
juu ya baba yake ambaye alikuwa marehemu tayari.
. . Akatuelezea namna alivyochukuliwa na watu
asiowafahamu wakamlaghai kuwa wanataka kununua
shamba lake hivyo aende kuzungumza na bosi wao.
. . “Nilipofika wakaniuliza iwapo nafahamiana na mzee wako
Ndema, mimi nikakubali upesi tu na hapo ili kufanya
biashara iende haraka nikawaeleza kuwa nauza kipande
changu kwa sababu ya kusimamia kesi ya mzee wako.
Wakanipongeza sana kwa utu wangu kisha wakaniuliza
matumaini ya kushinda kesi. Ndema unajua jinsi gani mimi
na baba yako….(akasita akakohoa sana) kisha akaendelea…
mimi na baba yako tangu utoto ni chanda na pete. Kwanini
nimwombee mabaya, nikawaeleza ukweli kuwa naamini
kuwa ile kesi kuna watu wenye fitina wameitengeneza.
. . Ndema, awali nilikuwa nimekataa kata kata kunywa
kahawa yao, niliikataa kata kata lakini baada ya sote
kuchangamka na kuonekana kufahamiana. Nikanywa ile
kahawa yao ya moto nyeusi.
. . Nd’o nikajipa tiketi ya maswaibu haya, nakufa najiona na
mzee wako wakamuua wajinga wale….. Ndema na wewe
kijana kaa mbali kabisa na Anti Ezenaninani sijui, Anti nani
yule…msijihusihe kabisa na hao…mi wameniua na ninyi
watawaua ”
. . “Baba usiseme hivyo!! Hautakufa hata tafadhali, kwani
wenyewe wanapatikana wapi ili tuangalie uwezekano wa
kuwachukulia hatua.” Jojina aliuliza kwa upole kabisa.
. . “Akina nani tena jamani?” mara mzee Madati aliuliza kwa
sauti ya kukoroma.
. . “Si hao watu wabaya waliokuwekea hiyo kahawa. Na huyo
Ezekiel ni nani tena maana…” Aliuliza Jojina huku
akimpoozea uji mzee Madati.
. . “Kahawa gani tena?” alihoji huku akiwa katika kubung’aa.
. . Na hapo wale wanawake wakatueleza kuwa mzee Madati
ana tatizo la kusahau na hapo hawezi kukaa sawa tena
ilikuwa bahati kubwa sana kwetu amesema nasi kwa muda
mrefu.
. . Hawakuwa katika utani!!
. . Tulijaribu zaidi ya mara kumi lakini mzee Madati alikuwa
haonyeshi ushirikiano, na baadaye akasinzia.
. . Akaondokea kuwa katika hali ile hata siku iliyofuata na
nyingine tena, hakuonyesha ushirikiano nasi tukabaki katika
utata mtupu.
. . Mzee Madati naye anamtambua huyo Ezekiel.
. . Kulikoni? Ama ni mzimu huu unatuzunguka kwa ajili ya
kuja kuyavuruga maisha yetu? Niliwahi kujiuliza.
. . Lakini kuna kitu mzee Madati anajua kuhusu Anti Ezekiel.
. . SIKU YA NNE hatukwenda tulibaki mafichoni. Lakini
tukifanikiwa kununua gazeti mjini.
. . Hapakuwa na habari yoyote ile mpya. Sikuzungumziwa
hata kidogo katika kurasa za mbele, bila shaka walitaka
kuwaaminisha watu kuwa nimeuwawa.
. . Wakati najiaminisha hivyo, mara nikakutana na habari
ambayo bila shaka katika siku kadhaa nyuma ilikuwa
ikiunda vichwa vya habari lakini sasa ilibakia kuwa habari
ya kawaida.
. . “Mama aliyefukua kaburi la mwanae na kuutoa mwili
kisha kuuchoma amegundulika kuwa na matatizo ya
akili……..” habari ile ilitaja jina la mama yangu mzazi!!
. . Nilichoka!!
. . Mama yangu amefukua kaburi langu akautoa mwili na
kuuchoma?? Haya yalikuwa maigizo kabisa tena yaliyokosa
waigizaji wazuri.
. . Hawa watu walikuwa wanatumia pesa!!
. . Waligundua kuwa Dulla aliuwawa mjini Morogoro.
Wakajiaminisha kuwa mama lao hawezi kuwa muhusika.
. . Wakati huo wakijua fika kuwa mimi bado nipo hai. Kile
kifo wakakihusisha na uwepo wangu, bila shaka walimbana
mama awaambie kama tuliwasiliana, mama akagoma.
. . Wakatumia pesa kumuuzia kesi nzito, kisha wakatumia
pesa tena kumhonga daktari ampime mama akili na kisha
wakayanunua majibu kwa pesa zao.
. . Daktari akalipa fadhila kwa kuandika kuwa mama yangu
mimi ana matatizo ya akili.
. . Akatolewa rumande na kutupwa hospitali ya vichaa
Mirembe.
. . Hakika ilistaajabisha.
. . Machozi yakanitoka!!!
. . Jojina akasogea karibu yangu na kuanza kunibembeleza!!!
. . “Jojina, wamemchukua Mama Eva, wamemchukua mama
Eva, Anitha ndo huyu anatoka kutuandikia barua hajui kama
atapona ama atakufa, wametaka kukuua Jojina, sasa
wamemchukua mama yangu, walimuua baba yako,
wamemchukua mtoto wako.. ni kipi sasa wanataka. Mi
siwezi kuishi hivi kwakweli siwezi kabisa.si bora nife sasa
eeh bora nife” nilijikuta nakaribia kufanya kufuru. Jojina
akaingilia kati.
. . “Ufe wewe ili mama ateseke huko bila kuwa na msaada
wowote, kufa kwako ni kumkimbia Eva mtoto wako, aibu
ilioje Sam. Unawaza kufa, basi sikuwa na haja mimi ya
kumuua yule askari kule porini, sikuwa na haja yoyote ya
kujiingiza katika utata huu, ni heri ungeniacha nikiwa nauza
bajia na sambusa zangu kuliko huku uliponileta. Ungeniacha
sasa. Haya si unataka kufa!!!
. . Naomba unirudishe uliponitoa, nirejeshe stendi na kapu
langu la bajia na sambusa lakini usisahau kitu kikubwa
kabisa. Naitaka amanmi yangu ambayo umeipoteza!!!”
Mama lao Jojina alikuwa amekasirika haswa. Lakini sio
hasira zilizozungumza, aliyoyasema yote yalikuwa kweli
tena kweli tupu. Nikakumbwa na aibu nikatamani kuomba
msamaha lakini Jojina hakuwa tena pembeni yangu!!!
Alikuwa ameelekea chumbani.
. . Nililazimika kumfuata, ikawa zamu yangu kumbembeleza
kutoka katika kilio chake.
. . Nilimsihi sana, hatimaye akanikumbatia miili yetu
ikagusana na kila mmoja kujikuta akivuta pumzi ya
mwenzake. Baridi kali la Iringa likatusababisha tutamani
kuendelea kukumbatiana.
. . Kilichotokea baada ya hapo hakuna aliyekitazamia kuwa
kitatokea.
. . Tulikurupuka asubuhi kila mmoja akiwa utupu!!!
. . Hakuna aliyeanzisha mazungumzo juu ya ajali iliyotokea
usiku.
 
SEHEMU YA KUMI NA TISA
“Ufe wewe ili mama ateseke huko bila kuwa na msaada
wowote, kufa kwako ni kumkimbia Eva mtoto wako, aibu
ilioje Sam. Unawaza kufa, basi sikuwa na haja mimi ya
kumuua yule askari kule porini, sikuwa na haja yoyote ya
kujiingiza katika utata huu, ni heri ungeniacha nikiwa nauza
bajia na sambusa zangu kuliko huku uliponileta. Ungeniacha
sasa. Haya si unataka kufa!!!
Naomba unirudishe uliponitoa, nirejeshe stendi na kapu
langu la bajia na sambusa lakini usisahau kitu kikubwa
kabisa. Naitaka amanmi yangu ambayo umeipoteza!!!”
Mama lao Jojina alikuwa amekasirika haswa. Lakini sio
hasira zilizozungumza, aliyoyasema yote yalikuwa kweli
tena kweli tupu. Nikakumbwa na aibu nikatamani kuomba
msamaha lakini Jojina hakuwa tena pembeni yangu!!!
Alikuwa ameelekea chumbani.
Nililazimika kumfuata, ikawa zamu yangu kumbembeleza
kutoka katika kilio chake.
Nilimsihi sana, hatimaye akanikumbatia miili yetu
ikagusana na kila mmoja kujikuta akivuta pumzi ya
mwenzake. Baridi kali la Iringa likatusababisha tutamani
kuendelea kukumbatiana.
Kilichotokea baada ya hapo hakuna aliyekitazamia kuwa
kitatokea.
Tulikurupuka asubuhi kila mmoja akiwa utupu!!!
Hakuna aliyeanzisha mazungumzo juu ya ajali iliyotokea
usiku.
****
SIKU yetu ilianzia nyumbani kwa mzee Madati, tulikuwa
tunajaribu bahati yetu kama akili zake zitakuwa zimekaa
mkao aweze kutueleza ni kitu gani anafahamu kumuhusu
huyo Ezekiel.
Utulivu pale nyumbani uliniweka katika wasiwasi, kitu cha
kwanza kuhisi ni kwamba mzee Madati anauwezekano
mkubwa wa kuwa marehemu ama mahututi zaidi ya awali.
Majirani wakatueleza kuwa familia nzima imealikwa katika
kituo kimoja cha redio pale Iringa mjini kwa ajili ya
mahojiano juu ya utata wa afya ya mzee wao. Wakatutajia
na jina la kituo hicho cha redio. Jojina alikuwa anakifahamu,
tukataka kwenda huko lakini wazo la kujiingiza matatani
likatuingia.
Tukafikia maamuzi ya kurejea kule Gangilonga mafichoni,
kama kawaida tukiwa na tahadhari kubwa kabisa.
Tukanunua magazeti mbalimbali kwa ajili ya kujipatia
taarifa zozote kuhusiana na mkasa wetu ili tujue adui
amejipanga vipi kutuangamiza ili tuzidi kujihadhari.
Majira ya saa moja usiku, tukiwa na amani kabisa tukarejea
tena nyumbani kwa mzee Madati ili tuweze kujua ni kitu
gani wamehojiwa redioni, na pia kama hali ya mzee ni njema
tuweze kuzungumza naye.
Umati wa watu ukatuvutia na kutuweka katika umakini
mwingine.
Askari!! Ndo kitu cha kwanza nilichowaza na kumshirikisha
Jojina, tukaishi kimashaka eneo lile. Taratibu kwa kupitia
upande usiokuwa na watu wengi tukafanikiwa kufika jirani
na umati.
Kweli tulikuwa sahihi, walikuwa ni maaskari lukuki
wameizunguka ile nyumba. Umati wa watu ukifanya
minong’ono mingi kila mmoja na lake.
Mnong’onaji mmoja akanivutia zaidi kumsikiliza.
Akawa anamtuhumu mama Sadiki, mama nisiyemfahamu
kuwa ni yeye ameyafanya haya. Lakini mwenzake
akampinga na kusema kuwa mama Sadiki amesafiri kwenda
Mbeya hiyo ikiwa siku ya nne.
“Kwani kila sumu lazima ikuue hapohapo wewe jamaa
yangu vipi wewe.” Alizidi kusimamia msimamo wake.
Akili ikafyatuka kusikia kauli ya huyo bwana ambayo
ilionekana kuwa tatanishi lakini yenye kuaminika katika
kichwa chake.
“Sikieni jamani, kama kuna anayemjua muuaji askari wale
pale akawaeleze sio kutusumbua huku sisi tusiokuwa na
msaada wowote.” Mzee mmoja wa makamo akatoa karipio,
yule mnong’onaji akatulia kimya asiseme kitu lakini
akirusha mikono huku na kule kama anayenyimwa haki zake
za msingi.
Jojina alikuwa kama hasikilizi lolote lakini ghafla akamvuta
yule bwana aliyekuwa akirusha mikono huku na kule.
Kisha akanivuta na mimi. Tukawa tumejitenga!!
Jojina akajifanya na yeye anaamini kuwa mama Sadiki
anaweza kuwa nyuma ya haya, yule bwana akafurahi
kupata wanaomuunga mkono.
“Yaani mimi nimewasikiliza redioni wote wakiwa na afya
tele hata huyu mzee Madati aliweza kuongea, sawa alikuwa
haeleweki na maneno yake hayo ya Ezekiel sijui kitu gani
lakini alikuwa mzima wa afya, sasa wanafika nyumbani
mzee anafia kitandani, mke wa kwanza anafia bafuni,
mwingine akaanguka ghafla tu uani. Mama Sadiki hayupo!!
Na hao wanaodai amesafiri, safari gani ya ghafla hivyo
kama sio kujitafutia sababu za kuonekana hausiki?
Tangu mwanzo mimi nilisema kuwa huyu mama kisa ana
mtoto wa kiume anataka arithi mali za mzee Madati
kinguvu. Mtoto mwenyewe sio wa Madati wala nini!!!
Ameiteketeza familia ya watu jamani!!!” alilalama bwana
yule kwa uchungu. Hakujua kama anatupa faida kubwa sana
kujua ni kitu gani kinaendelea.
Kulisikia jina Ezekiel hapohapo nikaikumbuka kauli ya siku
ya kwanza kabisa aliponiambia.
UKIMJUA EZEKIEL NA WEWE UNAPOTEA.
Mzee Madati na familia yake ikawa imepotea kwa kumtaja
Ezekiel.
Huyu mtu ni nani hadi awe amesambaa kila mahali, na
kwani yeye ni nani hadi asitajwe?
Sura yake ipoje kama si yule aliyejifia kitandani Dar es
salaam.
Swali gumu kupita yote kati ya yale tuliyowahi kujiuliza.
Miili mitatu ikaondolewa usiku ule na kupelekwa katika
hospitali ya wilaya.
Tukajiondokea mapema sana ili kukwepa kuanza kuhojiwa
iwapo kuna lolote tunalojua, maana kuna baadhi ya watu
walianza kututambua kama ndugu wa karibu wa familia ile.
Ndani ya chumba chetu cha kule mafichoni kila kitu
kilionekana kuwa shaghalabaghala. Jojina alikuwa amechoka
na mimi nikiwa hoi vilevile. Adui yetu alikuwa ametupiga
mapigo makali mfululizo bila sisi kujibu lolote.
Mbaya zaidi ni kwamba hata sisi tuliojua kiasi juu ya Ezekiel
tulitakiwa kuuwawa kama ni kweli kila anayetaka kumjua
lazima apotee.
Jojina alijaribu kuweka mezani mikakati kadhaa ya kujaribu
kukabiliana na huyo bwana wa kujiita Ezekiel ma lolote lile
kuhusu Michigani. Tukaamua kujisahaulisha juu ya Anti
Ezekiel ambaye niliamini kuwa alikuwa mtu mwenye utata
zaidi kupata kuonekana machoni pangu na kisha kutoweka
ghafla.
Akiwa mzima, akiwa kitandani maiti na kisha akiwa muuaji
Iringa!!
Muuaji asiyeonekana.
SALAMU KUTOKA DAR ES SALAAM
MAAMUZI aliyoyapitisha Jojina ni kugawana majukumu,
kujificha Iringa tu haina maana yoyote ile. Kwa sababu mimi
nilikuwa nasakwa sana jijini Dar es salaam na yeye akiwa
anajulikana Iringa, akaamua kuniacha mimi Iringa na yeye
akimbilie Dar es salaam kuangalia iwapo mpango aliokuwa
ameupanga utaweza kuleta mafanikio yoyote.
Niliibariki safari yake, kama kawaida akajiweka katika
mavazi ambayo yataubadilisha muonekano wake.
Akajihifadhi katika baibui jeusi!!
“Sam, ishi kwa tahadhari, usikae hapa kila siku,
watakusoma na mwisho watakudaka kama kuku. Nadhani
sina haja ya kukukumbusha juu ya hatari inayotukabili
mbele yetu, usilemae. Pesa unayo lala hotelini, ikibidi
wakati mwingine nenda Mbeya huko, kimbia Morogoro
kidogo.
Wewe na mimi ni wakimbizi. Tusikae kama watu huru kiasi
hicho!!” alinisihi mama lao, Jojina alfajiri wakati akiondoka
kuelekea Dar es saalam kujaribu kutimiza mipango aliyoiita
mipango makini.
Jojina akaniacha mpweke katika ardhi ya Iringa, ardhi
inayosadikika kuwa ina mahali panaitwa Michigani ambapo
nd’o kuna utata unaotakiwa kutatuliwa.
****
MAJIRA ya saa nne usiku nikapokea simu ya kwanza kutoka
kwa Jojina, akanielezea kuwa amefika salama na muda ule
naongea naye tayari alikuwa hotelini.
Wakati nataka kumpa pole juu ya safari yake, akanicheka
kidogo kisha akaniambia nimpe pole ya mizunguko maana
tangu saa kumi na moja jioni alikuwa jijini Dar.
Mizunguko ipi tena huyu mwanamke ama kwa mahawara
zake tena.
“Sam, nilikuja Dar es salaam kufanya kazi na sio kulala.
Niliposhuka Ubungo kitu cha kwanza kama ulivyonielekeza
kuwa mzee Matata anaishi Shekilango, niliamua kuitafuta
nyumba yake muda uleule. Bahati nzuri kama
ulivyonielekeza kuwa huyo mzee ni maarufu sikuhangaika
sana kuipata nyumba anayoishi. Nadhani umaarufu wake
umekuwa maradufu!! Kisa kilichokuza jina lake zaidi ni
kuchanganyikiwa na kuwa anaongea peke yake barabarani
baada ya mtoto wake wa kike anayempenda kupotea katika
mazingira ya kutatanisha. Wamemtafuta kwa kila namna
lakini hawajampata!! Kesho nitaenda kuitembelea familia
hiyo ili niweze kuanza ule mkakati ambao nilikwambia…..”
Anitha alimaliza kuongea, nilishangazwa sana na uchapaji
kazi wake mkubwa kiasi kile. Wakati mtu mwingine
angefika na kupumzika yeye alikuwa ameingia moja kwa
moja katika jambo lililompeleka huko.
“Jojina, naogopa kukupoteza tena naogopa sanma. Ujue ni
wewe uliyebaki katika maisha yangu ambaye naweza
kukuamini. Niite muoga niite mdhaifu lakini nasema ukweli
kuwa naogopa sana kusikia jina Matata. Asije kukuingiza
matatani Jojina, yaani usiporudi huku nikwambie kitu
kimoja tu. Sitajali kama umekufa ama nini. Mimi ni heri
nijiue Jojina. Sitakuwa na nguvu tena za kupambana….”
Kabla sijamaliza akanikatisha, “Sam, ukinitia uoga basi
yatakuwa kama usemavyo, acha niende na ule mkakati.
Kumbuka ni mkakati ambao nimetumia masaa manne
kukuelezea na ukakiri kuwa umenielewa Sam. Kama
hukunielewa ulimaanisha nini kunibariki nikaondoka huko.
Sasa Sam ni hivi kitu kimoja naomba nikwambie, mkakati
huu sitaachana nao, na kama nikishindwa na kuingia
matatani, tambua kuwa ni wewe upo nyuma ya haya yote.
Wakiniua jua kuwa na wewe kwa maneno ya mdomo wako
umechangia, wakinitesa na kuninyima uhuru basi upo pia
katika shutuma hizi.
Na pia kama simulizi hiyo ya mwanangu Justin kuwa yu hai
mafichoni pia ni kweli basi baya lolote watakalomtenda ni
juu yako wewe na si mimi Sam….
Kitu unachotakiwa kufanya kwa sasa ni kuniombea tu
yasitokee hayo yote…..nadhani umenielewa vyema kabisa
Sam… na usinipigie simu tena kuniambia mambo yako ya
kipuuzi puuzi….hujui thamani ya mama yako, mkeo na
mtoto wako wa kumzaa Sam… hivi umerukwa akili Sam
eeeh!!” Jojina alizungumza haya kwa hisia kali na baada ya
hapo akakata simu.
Nilibaki katika zizimo nisijielewe ni mkasa gani huu
unaoendelea kunikabili katika maisha yangu. Nikabaki
kuumia nisitambue kama siku moja maumivu haya yataisha
ama la!! Maana sikuwa naupata unafuu badala yake
nilikuwa mtu wa janga hili likiondoka linaibuka jingine!!
Sasa nikaziona dalili zote za kumpoteza Jojina.
Jojina alikuwa katika mlango wa kutokea na kisha
kukaribisha maumivu makali katika moyo wangu!!
Jojina alikaribia kabisa kuufunga ukurasa wa mwisho wa
maumivu yangu huku nikiamini kuwa bila yeye basi tena
sitakuwa na thamani zaidi.
Wakati huu ni moyo tu ulibaki kuuma, machozi yalikuwa
mbali nami.
Nikasimama imara tena na kuilazimisha akili yangu kuwa
machozi si tiba ya mkasa huu ninaopitia, ni lazima
nichakarike ili niweze kuupata mwanga. Kumtegemea Jojina
kwa asilimia mia ni kujitafutia msongo wa mawazo pale
mambo yatakaposhindikana.
Nikazikumbuka harakati za Anitha punde tu baada ya
kuwasili Iringa kisha nikayakumbuka na maneno yake. Na
mwisho nikajionya kuwa nikilemaa nitapoteza kila kitu.
Nikalala nikiwa na wazo moja tu!! Jojina anapiga hatua Dar
es salaam nami napiga hatua Iringa!!
Haba na haba hujaza kibaba!!
 
asante, naomba uweke tena kama mbili kama inawezekana
 
SEHEMU YA ISHIRINI
MSAKO
Niliamini nikimshirikisha Jojina juu ya harakati zangu za
kwenda kwenye kile kibanda atazidi kuniona wa ajabu na
nisiyejua kitu gani ambacho ninafanya.
Kibanda hicho hakuwa akikipa nafasi hata kidogo kuwa
kinaweza kuwa na mwqanzo wowote wa kutufumbua macho
juu ya siri hii. Hata mimi binafsi sikuwa na imani tele juu
ya kibanda kile lakini ningeendelea kulala ndani kila siku?
Ningeendelea kumtegemea Jojina kwa kila jambo!
La!! Ni heri mtembea bure kuliko mkaa bure, wengi
wamewahi kutembea bure na mwisho wakaokota pesa.
Nikajionya pia kuwa wapo wanaotembea bure na mwisho
kujikwaa barabarani huko na kupoteza kucha za vidole
vyao!!!
Nikaamua kuwa mtembea bure!!
Saa tatu asubuhi ilinikuta nikiwa natazamana ana kwa ana
na kile kibanda kilichoandikwa Michigan, sikujua ni kipi
kitafuata baada ya mimi kuwasili pale lakini nilienda
nikiamini yawezekana ni harakati za kuusogelea ukweli.
Ukweli ambao utaniweka huru mimi na watu kadhaa
wanaonizunguka!!
Hapakuwa na mabadiliko kama tulivyokiona siku ya awali,
kwa mbali nilimuona bwana Massawe ambaye ndiye
tulimwona siku ya kwanza akiwa amejikita katika kufagia
eneo lililopo mbele ya kibanda chake, nikapiga hatua moja
baada ya nyingine hadi nikakifikia kibanda kile,
nikalitazama vyema lile neno Michigan. Hakika mwandishi
alikuwa anatania ama la! Hakulipwa pesa ya kutosha aweze
kulisanifu jina lile.
Halikupendeza kulitazama!! Ni kama liliandikwa ilimradi tu
limeandikwa
“Karibu aiseee!!” alinikaribisha huku akiutupa fagio kando
na kujongea katika kibanda nikiwa nimeduwaa bado.
Akafungua mlango wa mbao na kuingia dukani, akatega
sikio kunisikiliza.
“Za asubuhi shehe wangu!!” alinisabahi kwa lafudhi yake ya
kichaga, nami nikamjibu kwa utulivu!!
“Kuna maziwa fresh!!” nilijikuta nikimuuliza ilihali macho
yangu yaliyofanikiwa kupepesa pale ndani hayakuona hata
mfano wa maziwa.
“Hamna maziwa bosi wangu, hapa hata friji sina.
Unavyoviona n’do vitu pekee humu dukani.” Alinijibu huku
akiufungua mlango tena na kutoka nje. Hitaji langu
lilikuwa limemkera kiasi fulani.
“Masawe! Njoo unipatie sigara, samahani kwa usumbufu!!”
Hakujibu kitu akajongea kibandani na kunipatia sigara
niliyokuwa nimeagizia. Akataka kunipatia kiberiti,
nikamweleza kuwa hicho nilikuwanacho!!
“Yaani tumbo limenisumbua jana Masawe. Hapa sijui hata
maziwa nt’ayapatia wapi? Lakini licha ya hayo Masawe
wewe hunikumbuki nd’o maana hata hujanichangamkia…
hata hivyo siku ile giza lilishaanza kutawala…” nikaingiza
maongezi ya kulifikia lengo. Akanitazama akijaribu
kuitafuta sura yangu bila mafanikio.
“Nilikuja hapa na mke wangu usiku mmoja hivi, tukanunua
pipi na vocha…. Ni siku kadhaa nyuma, halafu kigiza
kilishaanza kuingia usingeweza kunitambua, halafu siku ile
sikiwa na miwani hii….” Nilizidi kumuundia mazingira huku
nikiupuliza moshi wa sigara juu.
Kumbe Masawe naye alikuwa mvutaji, akachomoa sigara na
kuanza kuivuta.
“Hivi Masawe una uzoefu sana na biashara ya duka kwa
huku Iringa hasahasa hapa mjini?” nikamuuliza swali lile
huku nikijifanya sitilii maanani sana chochote
atakachonijibu.
“Nina miaka minane nauza duka, Moshi huko na hapa pia
japo si muda mrefu lakini ninaifahamu vyema Iringa”
alinijibu huku tukiendelea kushindana kuvuta sigara.
“Masawe na ujanja wako huo hadi leo unavuta SM shehe
wangu…” nilihama nikarejea katika utaniii.
“Hapana hataaa ‘sports huwa navuta sema leo nabadilisha
ladha” jibu lake likaleta matabasamu na vicheko
hatimaye!!!
Urafiki ulianza kujengeka!!
“Masawe mimi ni mgeni huku Iringa, na kitu kikubwa
kilichonileta huku ni kufanya biashara ya duka katika mtaa
fulani huko karibu na chuo sijui wanakiitaje. Mwanzoni
nilitarajia kumweka mke wangu asimamie lakini bahati
mbaya ameugua na hali ya huku imemkataa kabisa, sasa
natafuta mtu mwingine wa kumweka pale. Wewe nakuona ni
mzoefu sana, waweza kunisaidia mawazo kidogo.” Nikatupa
karata yangu kubwa zaidi niliyokuwa nimeiandaa.
Masawe akatabasamu kidogo kisha akaingiza utani.
“Mbona mimi nipo waweza kuniajiri tu shehe wangu!!
Ilimradi masilahi tu” tukacheka pamoja lakini nikausimamia
ule utani wake ili uniongoze zaidi.
“Aaah Masawe mtu mzito kama wewe nitakulipa bei gani,
maana utalazimika kuiacha ofisi yako. Sasa ndugu si
utanifilisi wewe….. yaani mtaji ukiongezea na mshahara
wako n’do nafilisika kabisa.” Nilifanya utani kimalalmiko.
Masawe akacheka kabla ya kuleta jibu langu la kwanza
kabisa.
“Bora hata kingekuwa kibanda changu asee. Cha wenyewe
hiki bwana, kila nikilalamika bidhaa ziongezwe bosi anadai
ningoje kidogo, hiyo kidogo huu mwezi wa sita tangu nianze
malalamiko!!. Tazama sasa mfano tangu umefika wewe
hapa bado hajafika mteja mwingine tena. Eneo lenyewe hili
halijakaa kibiashara kabisa na bosi hashauriki hata
kidogo!”
“Aah Masawe yaani unataka kuniambia wewe umetoka
Arusha na kuja kuajiriwa huku kwenye hiki kibanda kikiwa
hivi hivi ama amehamishia bidhaa nyingine mahali. Mbona
unanitisha bwana ama huku Iringa maduka hayalipi, niweke
wazi bwana Masawe.” Nilifanya udadisi, wakati huu sigara
ilikuwa imemalizika.
“Ni stori ndefu shehe wangu, ila bosi wangu aliponitoa
Moshi kunileta huku yalikuwa makubaliano mengine kabisa.
Alinileta kufanya kazi mahali lakini mwisho wa siku
nikaishia hapa dukani. Sema ninachoshukuru nikiwa na
shida ananisaidia..” alijibu kwa ufupi lakini nikatambua
kuwa kuna mengi sana anayo na si wa kumwendea kwa
pupa.
“Aisee Masawe pole ndugu yangu, basi ngoja niingie hapo
stendi Masawe nikitoka nitakuja tubadilishane mawazo
bwana Masawe. Maana mimi shemeji yako bwana, nimeoa
hukohuko kwenu!!” nilijenga undugu wa kilazima huku
nikiamua kuonyesha kuwa sihitaji sana kujua kuhusu hicho
kibanda.
Laiti kama Masawe angejua kila neno lake lilivyo la muhimu
kwangu asingethubutu kuzungumza nami!!
Niliondoka pale na kujizungusha mjini, nikanunua nguo
nyingine mpya, kisha nikatafuta nyumba ya kulala wageni
nikalipia, nikaoga na kubadili nguo.
Nikatoka na kurejea kwa Masawe tena, kama kawaida
kofia kichwani na miwani usoni. Sikutaka Masawe
anitambue maana angejua tu kuwa ni mimi yule
ninayetafutwa basi mambo yangeharibika. Na
nilichoshukuru zaidi magazeti hayakuwa na habari na mimi
tena baada ya kuthibitishiwa kuwa nimekufa.
Masawe alinichangamkia baada ya kuniona tena kwa mara
nyingine, sasa nilikuwa nadhifu kabisa tofauti na awali.
Shida yangu kucheza na akili ya Masawe, nilitambua ni kiasi
gani watu kutoka Moshi na Arusha walivyo makini
linapokuja suala la kutumia nafasi.
“Haya sasa tazama tangu wewe uondoke wamekuja wateja
wawili tu mmoja kununua kibiriti na mwingine mtoto
amekuja kununua pipi kifua. Unaweza kuiita hii biashara
shehe wangu!! Mimi nataka kuchakarika yaani.” Alianza
kujivutia upande wake. Nikaipenda hali hii.
“Kwa makadirio mfano, samahani lakini. Wanakulipa milioni
ngapi hapa ili nijipange na mimi nikitaka kukunyofoa.”
Akacheka sana kabla ya kunijibu, “Yaani uuze pipi na sigara
ulipwe milioni!! Hata laki mbili haifiki sema nina sehemu ya
kulala ya bure.”
Nikatikisa kichwa kisha nikawalaumu mabosi wake ambao
sijawahi kuwaona, kuwa ni wanyonyaji sana. Nikalaani na
mwisho nikajisemea.
“Mimi siwezi kumlipa mfanyakazi wangu chini ya laki tatu
na nusu. Nimesota katika maisha na ninaujua ugumu wa
hizi kazi na maisha yako juu pia Masawe.”
Masawe akafanya tabasamu kisha akacheka kibwege huku
akiona aibu. Bila shaka lile dau langu lilimkamata akili.
Nikaamua kuendelea kumkamata.
“Ujue wakati mwingine unapompa mfanyakazi mshahara
kidogo ndo mwanzo wa kuanza kukuibia, mara leo hiki kesho
kile. Anakuwa hawezi kujikimu, lakini ukimlipa mtu vizuri
akikuibia huyu ni mwizi wa tabia tu!!”
Masawe akatikisa kichwa kuunga mkono hoja!!
“Sasa kwa hii biashara bosi wako anaweza vipi kukulipa
mshahara kama leo umeuza pipi na sigara na kibiriti?”
“Inashangaza sana, ananilipa hivyo hivyo, tena
anaendesha magari yule ya kifahari. Kuna kipindi zinapita
hata wiki mbili sifungui duka, yaani ana maamuzi ya ajabu
sana anaamka tu Masawe leo hakuna kwenda dukani mpaka
nitakapokwambia. Zinapita hata siku kumi nd’o nafungua
tena…. Sijui ana wazimu?” alijiuliza Masawe, mimi
nikapata faida nyingine.
Kumbe Masawe hata yeye hajui kwanini bosi wake
analing’ang’ania hilo duka. Nikayakumbuka maneno ya
Anitha aliponisisitiza kuwa huyu aliyepo dukani si lolote si
chochote yupo mwingine mdosi zaidi.
“Looh!! Kwa hiyo ukifunga nd’o hakuna kinachoendelea
tena dukani, kumbe nd’o maana mnafukuza wateja.”
“Aaah!! Bosi wangu wa ajabu mno, kuna kipindi alikuja
ghafla mimi nikaambiwa kutoka nje, walikuwa wawili.
Nilipokuja kuchungulia ndani sikuwaona hata. Baadaye
kabisa wakatoka, hata sikuuliza lakini nilipowashirikisha
watu kadhaa wakaniambia kuwa hayo ni mambo ya
ushirikina tu hakuna la ziada.. nikapuuzia na kusahau.”
“Dah!! Inasikitisha sana!!” nilimaliza maongezi hayo,
lakini moyo ukinienda mbio, ni kama kulikuwa kuna kitu cha
ziada nilitakiwa kukitambua kutoka katika himaya ile. Kitu
cha msingi zaidi!!
Siku hiyo maongezi yakaishia pale nikaaga!! Kwa
makubaliano ya kufika tena siku nyingine.
“Bosi wangu wewe ukiwa tayari niambie tu mimi nafanya
kazi kama kawaida.” Alinisihi, nikaondoka!!
****
USIKU huo nikiwa nyumba ya kulala wageni nilikuwa
nikiunganisha mambo kadha wa kadha, kubwa zaidi
kuhusiana na utata wa kile kibanda kilichoitwa Michigani.
Nilitaka kujua kiundani zaidi kuhusu mmiliki na mengine ya
ziada. Nikajipanga kikamilifu kwa ajili ya kumkabili tena
Masawe kwa lugha nyingine ili niambulie mengi zaidi.
Nikaamua kujipa siku tatu mbele zaidi ili niweze
kumtembelea tena yule bwana muuza duka.
Wakati huo niliendelea kupokea jumbe kadha wa kadha
kutoka kwa Jojina akinijulia hali huku akidai kuwa
anaendelea na harakati kwa kasi kabisa. Jambo ambalo
lilinitia nguvu na mimi kuendelea
CHEUPE DAWA.
BAADA ya siku tatu kama nilivyojipangia majira ya saa nne
asubuhi nilifunga safari kwenda kuonana tena na bwana
Masawe. Siku hii nilijipanga kumchukua tukae mahali
tuzungumze kwa kina, maswali niliyoyaandaa kutokana na
taaluma yangu ya uandishi wa habari niliamini kuwa hata
awe mjanja vipi bwana Masawe hawezi kuchomoka!!
Maswali yale nilikuwa nikiyatumia katika matukio
magumumagumu hasa hasa kujua ukweli juu ya jambo
fulani kutoka kwa mtu mbishi na mjanja mjanja!!
Niliamua kutumia usafiri wa taksi ili niweze kuidhihirisha
hadhi ambayo tayari nilianza kuijenga kwa Masawe, tena
safari hii nilitaka niendeshe mwenyewe hadi mahali ambapo
Masawe ataniona vizuri kabisa.
Nikajivuta hadi katika kijiwe cha taksi nikazungumza na
‘shanta’ juu ya shida yangu!! Yeye hakuwa na kikwazo
baadaye akamuita mmiliki halali.
Wakadai nilipe zaidi ya kawaida nikakubaliana nao.
Nikaingia katika usukani, shanta (deiwaka) akawa ameketi
kiti cha nyuma!! Nikaanza kunyonga kuelekea kwa Masawe
huku Shanta akiniongoza kila nilipotaka kupotea njia.
Ni wakati nataka kukata kona ili gari iweze kutazamana
moja kwa moja na duka la Masawe ndipo nikaona gari
nyingine ya kifahari ikiwa katika harakati aidha za
kuegesha ama kuondoka kutoka eneo lile. Akili ya haraka
ikajirusha katika kichwa changu!!
Sikukata kona badala yake nikanyoosha moja kwa moja!
Shanta akadhani nimekosea njia, nikamsisitiza kuwa
nilikuwa sahihi kabisa. Nikaegesha gari kwa mbele kabisa,
tukakubaliana na Shanta kuwa ataningojea palepale.
Akatoa pakiti ya sigara na kuchomoa moja!!
Nikaondoka na funguo za gari huku nikitembea kimadaha,
katika namna ya kuridhika sana kana kwamba ni mdosi
kutoka nje ya nchi!! Kwa nje ningeweza kuonekana
nimeridhika sana lakini macho yangu yalijikita katika
kuitazama Nissan Patrol ilivyokuwa inajaribu aidha
kuondoka ama kuendelea kuwa eneo lile. Na hapo
nikagundua kuwa ile gari haikuwa ikiondoka bali ilikuwa
imewasili.
Akili ikanicheza upesi!! Kwa mbali kabisa nikaangaza
sikufanikiwa kuiona sura ya Masawe wala dalili yoyote ya
uwepo wake!! Upesi nikatoa simu yangu mfukoni,
nikaitazama kana kwamba ilikuwa inaita nikapokea wakati
si kweli kuwa ilikuwa inaita.
Nikajizungusha huku na kule kama ninayetafuta mtandao.
Nia yangu ikiwa kutazama kama naweza kuona chochote
kitu kinachoendelea!!
Mlango wa duka ukafungwa!! Upesi nikaikumbuka kauli ya
Masawe kuwa aliwahi kuchungulia ndani baada ya kutolewa
nje! Nami nikajitia jeuri tena nisiyekuwa na hatia
nikajisogeza mbele kwa kujiamini funguo zangu zikiruka
hewani huku na kule.
Nikakifikia kile kibanda.
“Masaweee!!” nikaita kwa sauti ya chini!!
Kimya! Nikaita tena kwa sauti ya chini bado hapakuwa na
jibu. Nikalisogelea lile gari niweze kuangaza kulikoni,
nikajifanya natazama kama kuna mtu ndani yake niweze
kumuulizia kulikoni mbona Masawe hajafungua duka.
Nilipolikaribia gari nikakutana na vioo vilivyovikwa utando
mweusi ‘Tinted’ nikatamani kujua ni nini kinaendelea
ndani!!
Nikachungulia!!
Nikaona kitu mfanowe bahasha, bahasha kama ile yangu
iliyokuwa na nyaraka zangu kutoka kwa yule bwana wa
kuitwa Ezekiel. Nikazidi kukisogelea kioo ili nijihakikishie
zaidi juu ya ile bahasha katika kile kiti.
Lahaula!! Pua yangu ikagusana na kile kioo. Ving’ora vya
dharula vikaanza kulia, ile gari ikawa inapiga makelele kwa
fujo, hofu ikanitanda. Nikapagawa na kuamini kuwa
wakati wa kuumbuka na kukamatwa ulikuwa umewadia,
nikataka kukimbia lakini nikagundua kuwa ni upuuzi
uliopitiliza. Sijaiba cha mtu, nimevaa kofia na miwani
machoni, nikimbie nini. Lakini nafsi nyingine ilikuwa
inanisihi nikimbie, maana kama ni kweli hiyo bahasha ni ile
nilikuwa naisaka basi hao watu lazima watakuwa watu
wabaya.
Na hivyo watakuwa wananifahamu fika!!!
Maswali mawilimawili, nikimbie ama nisikimbie!!
Nikakosa maamuzi na kubaki kama zezeta nikingoja
kuumbuliwa!!
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA
Akili ikanicheza upesi!! Kwa mbali kabisa nikaangaza
sikufanikiwa kuiona sura ya Masawe wala dalili yoyote ya
uwepo wake!! Upesi nikatoa simu yangu mfukoni,
nikaitazama kana kwamba ilikuwa inaita nikapokea wakati
si kweli kuwa ilikuwa inaita.
Nikajizungusha huku na kule kama ninayetafuta mtandao.
Nia yangu ikiwa kutazama kama naweza kuona chochote
kitu kinachoendelea!!
Mlango wa duka ukafungwa!! Upesi nikaikumbuka kauli ya
Masawe kuwa aliwahi kuchungulia ndani baada ya kutolewa
nje! Nami nikajitia jeuri tena nisiyekuwa na hatia
nikajisogeza mbele kwa kujiamini funguo zangu zikiruka
hewani huku na kule.
Nikakifikia kile kibanda.
“Masaweee!!” nikaita kwa sauti ya chini!!
Kimya! Nikaita tena kwa sauti ya chini bado hapakuwa na
jibu. Nikalisogelea lile gari niweze kuangaza kulikoni,
nikajifanya natazama kama kuna mtu ndani yake niweze
kumuulizia kulikoni mbona Masawe hajafungua duka.
Nilipolikaribia gari nikakutana na vioo vilivyovikwa utando
mweusi ‘Tinted’ nikatamani kujua ni nini kinaendelea
ndani!!
Nikachungulia!!
Lahaula!! Pua yangu ikagusa na kioo. Ving’ora vya dharula
vikaanza kulia, hofu ikanitanda. Nikapagawa na kuamini
kuwa wakati wa kuumbuka na kukamatwa ulikuwa
umewadia, nikataka kukimbia lakini nikagundua kuwa ni
upuuzi uliopitiliza. Sijaiba cha mtu, nimevaa kofia na
miwani machoni, nikimbie nini.
Nikaamua kungoja atakayetoka niweze kumuuliza
kulikoni!!!
Maajabu!!
Hakutoka mtu hadi king’ora cha dharula cha kwenye hiyo
gari kilipokoma kulia.
Ina maana wapo mbali sana hao watu!! Ama ndo mambo ya
ushirikina? Nilijiuliza mwenyewe huku nikisogea ule upande
ambao Masawe aliutumia kuchungulia ndani siku ile
aliyonisimulia!! Nilikuwa natetemeka sana lakini kitu
ambacho sikutaka kufanya ni kupiga hatua nyuma!!
Kupiga hatua walau moja tu nyuma ningejidhihirishia ni
kwa namna gani mimi ni muoga tena nisiyekuwa na uchungu
na nafsi zilizopotea kimasihara!!!
Pia ningekuwa si mzalendo hata kidogo!! Kama Anitha
alipotea akinipigania, mimi nikipotea kuna tatizo??
Nikajipa moyo na kupata nguvu mpya!!
Hakika! Hapakuwa na mtu ndani ya chumba kile, nikasogea
karibu zaidi nikachungulia kwa ukaribu. Nikaangaza huku
na kule bila mafanikio. Hapakuwa na mtu, wala dalili ya
kitu chochote chenye uhai.
Wachawi hawa! Nikafikiria, kisha nikaanza kuondoka,
nikajiweka mbali kabisa na eneo lile. Nilimwona Shanta kwa
mbali alikuwa analalamika akitupa mikono huku na kule ma
ajishike tumbo ma ra kichwa. Nikajua ni njaa
zinamsumbua, nikachomoa pesa mfukoni na kumwonyeshea
kuwa nitamwongezea nyingine akaendelea kulalamika huku
akiniita kwa kutumia viganja vyote viwili vya mikono yake!!
Kuna jambo alikuwa anamaanisha natakiwa kulifanya labda
hasahasa nikiwa karibu yake lakini sikujali sana sikudhani
kama lingeweza kuwa na umuhimu wowote ule kwangu kwa
wakati ule ambao kila dakika ilikuwa na umuhimu wake.
Nikaenda upande mwingine ili nipate eneo zuri la kuweza
kuona kila kona.
Nikalipata jumba bovu lisilotumika tena, baada ya aidha
kubomoka ama ujenzi wake kuishia njiani.
Au ndo magofu ya Michigani haya!!! Nikajiuliza.
Nikajiweka pale na kuchungulia nini kinatokea kwa hao
watu waliopotea kimaajabu ndani ya duka lile dogo kabisa
la Masawe! Nilivuta subira bila kupepesa macho kona
nyingine. Nilitaka kukata tamaa baada ya kungoja sana
lakini nikakumbuka kitu!!
Subira yavuta heri!
Naam ile heri ikawadia hatimaye!! mlango wa kibanda cha
Michigani ukafunguliwa!!
Wakatoka wanaume wawili, mmoja akiwa amevaa suti
nyeusi, huyu alikuwa mweusi, na mwingine alikuwa…….
Hakika alikuwa ni yeye, haikuwa mara ya kwanza kuonana
naye.nisha kichwa chaka kama niliwahi kukiona mahali.
Hatimaye akageuka na hisia zangu hazikuwa potofu hata
kidogo!!
Alikuwa yule mzungu, cheupe aliyehusika katika kumkamata
mke wangu!!
Alikuwa ni cheupe dawa! Mtu ambaye niliamini kabisa kuwa
anahusika katika kuniachia ujumbe wa ‘UTAMFUATA
MWENYEWE’.. hakika alikuwa anajua, maana siku
aliyomteka mke wangu ndo siku hiyo hiyo yule mtoto
mtukutu Selemani alinambia kuna ujumbe upo ndani ya
nyumba yangu. Na nilipomwagiza na yeye akakamatwa!!
Sijui walimpeleka wapi watu hawa wabaya!!!
Nilijihakikishia kuwa sijakosea, wakati nikiamini kuwa
eneo lile wapo watu wawili, mara nikawaona wawili wale
wakigeuka ghafla, na mimi nikageuka nao. Ana kwa ana na
shanta wa ile gari. Alikuwa anaangaza huku na kule, bila
shaka alikuwa katika harakati za kunifuata nilipokuwa!!
Cheupe dawa akamuita!! Shanta akababaika, lakini
alivyoitwa na yule mwafrika akaenda huku dalili za uoga
zikiwa bayana. Alifika nan kuzungumza nao kuna jambo
walimuuliza lakini sikuweza kulisikia. Shanta akawa
anaangaza huku na kule, bila shaka akinitafuta mimi. Sijui
walimuuliza mimi nipo wapi ama?
Wakaongozana naye hadi jirani kabisa na gari yao.
Ghafla yule mzungu akamkwida, huku akitazama huku na
kule, dereva akawa anarusha miguu huku na kule.
Nilijisikia kutetemeka miguu, shanta aliyekuwa mkarimu
kwangu alikuwa matatani sasa.
Nikataka kupiga mayowe lakini nikatambua kuwa nitakuza
tatizo badala ya kulipunguza. Na ugumu zaidi ungekuja
upande wangu!!!
Punde akamrusha ndani ya gari. Milango ikafungwa wote
wakiwa ndani kisha ikatimua vumbi, kutoweka eneo lile
ikiipita taksi yetu.
Nilibaki nimebung’aa nisijue nini cha kufanya.
Funguo mkononi!! Shanta katoweka, maskini labda
walidhani kuwa alikuwa anawafuatilia!!
Kumbe na mimi wangenikuta ningeambulia kipigo na
kukamatwa!!.....
Nusu saa baadaye nikiwa katika kuhakikisha kuwa wale
watu wametoweka kabisa, na Masawe naye aliwasili,
niliusikia mluzi wake kwa mbali kisha akatokea akiwa
katika mwendo wake wa kusuasusa na hapo nikatambua
kuwa alikuwa ana ulemavu mguu mmoja ulikuwa mfupi.
Kabla ya kufungua duka, alichukua kipande cha fagio na
kuanza kusafisha eneo linalozunguka duka, huku
akiendelea kupiga mluzi. Baada ya kuhakikisha kuwa
Masawe hana walau muonekano wa kujua ama kutaka
kujua kilichotokea humo ndani nikatokea mafichoni na
kumkabili na asijue ni wapi nimetokea.
“Aisee nimekuja asubuhi sijakupata shehe wangu!!”
nilimsemesha kwa lafudhi ya kichaga, akacheka kabla ya
kunieleza kama nilivyoona. Kuwa bosi alikuwa na mambo
yake!!
“Kwa sasa yupo wapi?” niliuliza ili nipate kujitoa mashaka
na usalama wangu!!
“”Wameenda Mbeya huko, hapo safari maana huwa
wanaondoka na ndege!!” alinijibu. Amani ikarejea kiasi
lakini kuna mambo mawili yalikuwa ya msingi zaidi.
Kujali muda nilimalize hili tukio upesi na pili nitambue juu
ya siri iliyopo katika kibanda kile.
“Kwa hiyo akiwa hayupo nani sasa anakusimamia hapa!!”
“Hata akiwepo hakuna wa kunisimamia” alinijibu bila
wasiwasi.
“Maana mguu wangu hapa kwako nia yangu unisaidie
kuingia mjini kunilangulia vifaa kadha wa kadha vya kazi.
Si unajua mimi mgeni wasije kunipiga bei kali…”
nilidanganya. Masawe akafurahi kuona kuwa ninamthamini,
akazungumza mawili matatu kisha akaniuliza
tunaongozana ama aondoke peke yake!!
Nikamwomba aondoke peke yake na mimi kama kuna
uwezekano nijilaze kidogo, Masawe akaniruhusu kuingia
katika kile kiduka ambacho thamani yake haikuwa ya
kumwogopa mwizi.
Masawe akatoweka baada ya kumpa mahesabu ya uongo!
Aliponipa mgongo, nami nikaanza kufanya kilichonipeleka,
nikatazama huku na kule bila mafanikio. Nikaituliza akili
yangu na hatimaye nikaona kitu.
Tundu la funguo katikati ya makablasha ya kuwekea
bidhaa, nikajaribu kuvuta pakawa pagumu kufunguka,
nilijaribu tena na tena lakini bado hali ilikuwa ileile.
Nikachukua funguo zilizokuwa pale ndani lakini
hazikufanania na tundu lile!!
Nguvu zikaniishia tena, nilitamani dakika za mwisho za uhai
wangu ziishie ndani ya huo mlango ilimradi nijue tu ni kitu
gani huwa kinaendelea katika maficho yale. Nilitaka kujua
kitu kimoja tu, hiyo Michigani ni Michigani kweli? Na je
inahusiana vipi na Anti Ezekiel??
Wakati nawaza juu ya ufunguo.. nikakumbuka kuwa kuna
funguo nilipewa na Ezekiel Ubungo na kunisihi mambo kadha
wa kadha. Nilipotazama kile kitasa hakika kiliendana na ule
ufunguo!! Walau matumaini yakajengeka upya huku
nikimshukuru Ezekiel kimoyomoyo!!
Lakini mara nikafadhaika!! Na ilikuwa lazima nifadhaike
kutokana na kilichopita kwa kasi kichwani mwangu!!!
Nikakumbuka kuwa ufunguo ulipotea ukiwa ndani ya
bahasha nyumbani kwa mama lao!!
Kazi ikawa ngumu zaidi!! Tena mpya!!
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI
Aliponipa mgongo, nami nikaanza kufanya kilichonipeleka,
nikatazama huku na kule bila mafanikio. Nikaituliza akili
yangu na hatimaye nikaona kitu.
Tundu la funguo katikati ya makablasha ya kuwekea
bidhaa, nikajaribu kuvuta pakawa pagumu kufunguka,
nilijaribu tena na tena lakini bado hali ilikuwa ileile.
Nikachukua funguo zilizokuwa pale ndani lakini
hazikufanania na tundu lile!!
Nguvu zikaniishia tena, nilitamani dakika za mwisho za uhai
wangu ziishie ndani ya huo mlango ilimradi nijue tu ni kitu
gani huwa kinaendelea katika maficho yale.
Wakati nawaza juu ya ufunguo.. nikakumbuka kuwa kuna
funguo nilipewa na Ezekiel Ubungo na kunisihi mambo kadha
wa kadha. Nilipotazama kile kitasa hakika kiliendana na ule
ufunguo!!
Nikakumbuka kuwa ufunguo ulipotea ukiwa ndani ya
bahasha!!
Kazi ikawa ngumu zaidi!!
****
Nilirejea kimaficho katika nyumba ya kulala wageni
niliyokuwa nimefikia, lakini9 nikakumbuka kununua
magazeti kadha wa kadha, nikatilia maanani gazeti la yule
mzee Matata, mzee ambaye kwangu mimi alikuwa kama adui
tayari.
“MZIMU WA SAM WAONEKANA DAR UKIZURURA”
Nilishikwa na hasira kuiona picha yangu tena katika kurasa
za mbele za magazeti. Nikajikuta nakabiliana na donge la
hasira kooni, nikakumbuka kuwa funguo nimepoteza
tayariu ambazo zingenisogeza karibu na ukweli na sasa
gazeti la kipuuzi la mzee Matata linaandika ujinga tena
kuwa nimeonekana Dar.
Huyu mzee na shahada zake za kutosha bado anashikiliwa
akili na wajinga wajinga hawa. Haoni uchungu mwanaye
amepotea? Ama nd’o upendo uliopoa?
Ghafla nikavamiwa na wazo kuwa huenda Anitha
alirejeshwa nyumbani kwao, na huu msala umebaki kuwa
mzigo wangu mwenyewe!!
Wazo hili halikutaka kutoka kichwani mwangu hata kidogo!!
Nikajiaminisha kuwa namuwaza mtu ambaye yu huru!!
Nd’o maana baba yake anaendelea kufanya upumbavu huu!!
Nilijihisi kutetemeka mwili mzima, huku lile gazeti mkononi
mwangu nikiliona kuwa mzigo mzito sana tena mzigo wa
miiba unaochoma kwa hasira.
Mwendo mfupi wa kuifikia ile nyumba ya kulala wageni
niliona ni sawa na kilometa kumi. Nilitamani kukifikia
chumba nikivamie kitanda na kujilaza. Sikuwa na la ziada.
Hatimaye nikafika chumbani, nikalifunua lile gazeti. Kama
ilivyo kawaida ya wasiojiamini, akaandika kuwa habari ile
imeandikwa na ‘MWANDISHI WETU’
Nikasonya kwa ghadhabu na kulichana vipande vipande
gazeti lile, kisha nikalala! Bila hata kuvua viatu vyangu!!
HARAKATI ZA JOJINA DAR
Nilikuja kushtuka masaa kadhaa mbele, usiku ulikuwa
umeingia tayari na sikuwa nimepata walau hamu ya kula,
niliumiza sana kichwa nisijue ni wapi pa kuweza kuanzia
tena ili niufungue mlango ule, nikajiuliza mara mbili zaidi
na kukosa majibu. Nikaingia bafuni na kujimwagia maji
huenda kuna jambo jipya limezibwa na uchovu wa mwili
litajitokeza.
Hakuna kilichojitokeza. Nilishika hiki na kuacha kile labda
nitapata ufumbuzi lakini sikuwa na ujanja wowote,
nikafikiria juu ya kuchongesha funguo za bandia lakini
ajabu hata ramani ya tundu lile sikuwanayo na
haikuonekana kuwa kazi nyepesi kuchonga funguo zahali
pale. Funguo za maajabu.
Simu yangu ya mkononi ambayo namba yake alikuwanayo
Jojina pekee ilipatwa na uhai na kuanza kuimba!
Nikaisogelea kwa hofu maana sikutarajia simu kutoka Dar
es salaam niliamini Jojina alikuwa mwenye ghadhabu na
labda hakutaka kusema nami lolote.
Naam hakuwa mwingine aliyepiga simu ile.
Alikuwa Jojina!
“Nambie Mama lao…” nilimuanza kiutani ili kama ana jazba
azitulize kidogo
“Safi tu Sam vipi ulikuwa umelala tayari.” Alinijibu kwa
uchangamfu, ile saauti yake ya kimahaba ikanituliza woga
wangu.
“Hapana nilikuwa bafuni ….”
Nikajirusha kitandani na kujilaza simu sikioni niweze
kusikia Jojina ana lipi jipya!!
Alinieleza mambo kadha wa kadha kuhusu uwepo wake jijini
Dar na mimi nikamweleza juu ya hali ya hewa ya Iringa,
kisha akachukua nafasi kuel;ezea nia ya kunipigia simu
usiku ule pasi na matarajio.
JOJINA.
SAM, kwanza sahau kuhusu yaliyopita, nadhani tulipishana
lugha tu, nilipokukosea nisamehe nami nishasamehe
uliponikwaza. Sam ni siku kadhaa hatujazungumza na ni
kama siku yangu ya nne ama ya tano huku Dar es salaam.
Kubwa zaidi la kukupigia hii simu ni kwamba hatimaye
nikafanikiwa kuonana na mzee Matata. Sam yaleyale ya
mzee Madati kurukwa akili ndo huku pia lakini afadhali huyu
hajawekewa madawa lakini kupotea kwa mtoto wake
kumemchanganya sana. Nilipofika kule mara ya kwanza
nilizuiliwa kuingia eti kwamba mzee hatakiwi kuonana na
watu madaktari wamekataza.
Nikaondoka kapa siku hiyo! Lakini sikufa moyo.
Sikukata tamaa Sam. Mara ya pili nikajieleza kuwa shida
yangu kuonana na mzee ni kuhusu mwanaye. Wacha wee!
Hapo sasa nikaonekana lulu mchangani, kila mtu ananiuliza
kulikoni. Nikagoma kusema lolote hadi niongee na mzee.
Kama yeye atawaeleza ni juu yake! Lakini mimi simwelezi
mtu tofauti na yeye, na kama sitaruhusiwa siku hiyo basi
tena hawataniona mimi kukanyaga pale nyumbani kwao.
Sam niliyasema haya huku natetemeka, maana najua kuwa
maaskari watakuwa wameshirikishwa juu ya jambo hili,
hivyo wakisikia kuna mtu anajua wanaweza kumweka
kizuizini ili asaidie upelelezi. Nikaamua kujitoa muhanga
huku nikiamini kuwa Mungu anamshika mkono mwenye haki.
Ama kweli damu nzito kuliko maji!!
Mzee akaelezwa nikakubaliwa kuingia japo walinionya kuwa
ana tatizo la kubadilika badilika yule. Sikujali kuhusu hilo
nilichotaka kuonana naye kwanza.
Sam, yule mzee amekwisha na hapa sasa naamini alikuwa
akimpenda sana mtoto wake, yaani amekuwa dhaifu sana.
Akanikodolea macho nami nikajiweka sawa, tulikuwa wawili
tu, nikaanza kumweleza kilichonileta hadi pale,
nikamsimulia baadhi ya matukio hadi ujio wa Anitha Iringa,
sikukutaja wewe hata kidogo kwanza, nikadanganya kuwa
alikuwa amekuja kufanya biashara huko.
Nikamwelezea juu ya mikasa ya ajabu ya Anti Ezekiel mjini
Iringa. Mikasa ambayo inasemekana kuwa ni ya kishirikina
ama mauzauza mengine!
Hapo akakodoa macho yule mzee, na kwa mara ya kwanza
akasema na mimi. Kumbe na yeye ni mtu wa Iringa ni Mbena
yule mzee. Hapa tukabadili lugha tukahamia katika kabila,
nikasema naye kibena. Ushirikiano ukawa mkubwa sana
tukawa marafiki.
Nikamweleza kuwa nauhitaji sana msaada wake maana
hata mimi nimepoteza mtoto na kuna mwenzangu familia
yake yote inateketea. Kufikia hapa nikaona hakuna haja
yoyote ya kuendelea kuficha siri hii ilhali mzee ameonyesha
ushirikiano na nilichokisema hakikuwa katika maandishi
ningeweza kukibadili muda wowote ule!!!
Nikamtajia jina lako, sikumpa nafasi ya kusema lolote bali
nikamlaumu kwa kutotaka kukusikiliza nikamweleza juu ya
tuhuma unazozushiwa na watu wabaya na nd’o haohao
wamemchukua mtoto wake. Kufikia hapo nikamweleza kuwa
Anitha alikuwa katika harakati za kukusaidia wewe na wao
wakagundua nd’o wamemshikilia.
Macho yakamtoka mzee na akatoa ushirikiano!!
Akakiri kuwa kuna watu walikuwa wakileta taarifa zile
ofisini, na hakujua kama ni watu wabaya. Nikamuonya
asithubutu kumweleza mtu yeyote juu ya hili maana hao
watu ni hatari, wakigundua umewajua tu wanaanza
kukuonya kimatendo, mzee akakiri kuitambua skendo hiyo
ya UKIMJUA UNAPOTEA. Akajionya!!! Aliwahi kuisikia Iringa
miaka hiyo!!
Kumbe ni mchezo wa miaka mingi tu huu Sam!! Na bado
umefumbiwa macho. Anti Ezekiel ni nani hadi alibabaishe
taifa letu!! Yeye ni nani katika ardhi hii huru??
Baada ya mazungumzo marefu tukapanga mikakati
kabambe! Mkakati wa kumvumbua huyo Anti Ezekiel.
Mzee alichangamka na hakuna hata ndugu mmoja aliyeweza
kuamini kuwa yule alikuwa mzee wao.
Leo asubuhi mikakati hiyo imeanza kufanya kazi!
Gazeti la mzee Matata limeandika taarifa zako kuwa
umeonekana maeneo ya Dar es salaam mjini ukizurura.
Nia yetu kubwa ni kuwavuta hawa watu waje huku ili
tuweze kushughulika nao vyema. Baada ya taarifa hiyo
ofisi ya mzee Matata ikapokea simu kutoka kwa watu
wanaojiita wapelelezi kutoka Iringa, mmoja akazungumza
Kiswahili na mwingine akasema kiingereza. Wakadai
wanahitaji kuonana na huyo mtu aliyekuona wewe waweze
kujua wapi pa kuanzia ili kuujua ukweli, walilalamika kuwa
wao wanaamini umekufa hivyo uzushi kama huo unashusha
thamani ya utendaji kazi wao.
Kufikia hapo mzee Matata ameniamini sana na kujua ni
kweli kuna jambo linafichwa nyuma ya pazia..
Hao mabwana wakawasili kutoka Iringa na kukutana na
watu wa mzee Matata, ni mzungu mmoja na muafrika na
wamekuja na gari binafsi aina ya Nissan patrol! Kwa leo
wametoa tu salamu, kesho watakuwa ofisini kwa mzee
Matata, japo mzee hatakwenda amewaambia wakitoka huko
wamtembelee nyumbani kwake.
Kwa hiyo Sam hapo nd’o tumefikia!!
JOJINA AKAMALIZA.,
Nilikuwa natetemeka sana, ilikuwa ni sababu ya baridi
pamoja na uoga tele huku kihoro cha matumaini
kikinipagawisha. Mwanzoni nilikuwa na hasira wakati
namsikiliza mama lao kwa sababu nilihisi mzee Matata ni
mnafiki na anamhadaa lakini kumbe ile habari gazetini
imepikwa maksudi ili kuwaweka karibu maadui kuwa
marafiki ili shambulizi likifanyika wawe katika taharuki bila
matarajio wala maandalizi ya kujikinga!!
Watu waliotajwa nilikuwa nimewaona asubuhi hiyohiyo
katika kijumba cha Michigan!!
Cheupe dawa na yule mwenzake wapo Dar tayari.
Nikamweleza Jojina juu ya mkasa wangu kwa ufupi sana,
nikamwelezea juu ya watu hao na jinsi wanavyoishi
kimaajabu katika kibanda cha Michigan. Nikamwelezea kila
nilichofanya hadi kufikia hatua ya kukuta tundu la
kufunguliwa na funguo. Sikusita kumhakikishia kuwa
cheupe dawa huyo ndiye aliyemkamata mke wangu jijini
Dar…
“Jojina, tumekaribia kulipata jibu lakini kuna kitu kimoja
ambacho kinanipa utata na kuniumiza kichwa, sehemu ya
kufungulia geti la kuingia katika maficho yao imeonekana
tayari na ninaweza kujua namna ya kupaingia tena. Lakini
Jojina funguo hakuna Jojina, ile bahasha tuliyopoteza
katika chumba chako kwenye operesheni mbwa okoa, ndani
yake kulikuwa na funguo!!
Ni hizo na ninao uhakika kuwa Ezekiel alimaanisha kitu
aliponipatia zile funguo!!
Nilimaliza kuongea nikamsikia Jojina akishusha pumzi zake
kwa nguvu sana. Ni kama alikuwa ameungana nami katika
kukata tamaa.
“Kweli huo ni mtihani mgumu, lakini Sam unakumbuka kuwa
kila jaribu linalokuja kwa mwanadamu huwa linayo njia
yake ya kutokea? Basi amini kuwa hata kikwazo hiki
tukakiruka. Kama unaweza kwenda tena kwa huyo Masawe
basi hakikisha kuwa unachukua alama ya hilo tundu ili
tuweze kuchonga ufunguo wa bandia…….” Alianza
kushauri Mama lao. Nikaingilia kati na kumweleza kuwa
kile kitasa ni cha aina yake na hata ule funguo ulikuwa wa
aina yake. Mama lao akasihi kuwa ni heri kujaribu kuliko
kupuuzia.
Nikakubaliana naye, lakini kila nilivyoujengea picha ule
ufunguo chakavu alionipatia Ezekiel na umbo lake la
kustaajabisha niliamini kabisa kuwa zile zilikuwa mbio za
sakafuni tulizokuwa tunajaribu kukimbia.
Lazima ziishie ukingoni tu!!
Tukaagana na mama lao, na kuahidia kupeana matokeo kwa
siku inayofuata.
Huo ukawa usiku wenye matumaini kiasi fulani, lakini
sikujua kama asubuhi ya siku inayofuata ingekuwa asubuhi
ya kustaajabisha ndani ya jiji la Dar es salaam na wakati
huo mjini Iringa!!!
Ni heri tusingefikia maamuzi yale!!
Lakini hatukujua!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom