Riwaya: Ant Ezekiel

SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE
Sasa leo ulipouleta ufunguo ulionisababishia majanga haya
nikakuona kuwa wewe naye ni mmoja wa watu wabaya
wanaofahamu siri yangu!! Sam kiuhakika nisingekutambua
basi ungekufa kifo kibaya sana leo.” Alimaliza mzee yule
kunieleza juu ya simulizi ile ya kutisha na kusisimua.
Mwili ulisisimka haswa nikijaribu kujenga picha juu ya
mwanadamu kung’olewa jicho na kukatwa mguu.
Watu ninaokabiliana nao walikuwa wanyama haswa!!!
Wakati nikiendelea kufikiria juu ya tukio hilo la maajabu.
Mara katika simu yangu ukaingia ujumbe!!
Hakuwa mwingine alikuwa ni Mama lao..
“SAM HALI SI SHWARI MZEE MATATA MATATANI”
Nilichoka!!!
Mzee akaishtukia hali ile ya hofu niliyokabiliana nayo, nami
sikuona hiyana kumshirikisha. Nikamweleza juu ya Jojina na
mkakati wetu. Na sasa amenasa huko jijini Dar.
“Mpigie simu tujue!! Kama ni hawa vijana niwaamnbie
wakusaidie.” Alinishauri, nami nikapiga namba za Jojina.
Simu ikapokelewa!!
“Sam, huu mtandao ni hatari. Nasi tupo katika hatari kubwa
sana. Mzee Matata amesimamishwa kazi, nyumba yake
inauzwa juma lijalo.” Jojina alinieleza hayo kwa sauti ya
chini tulivu!!
“Sikuelewi Jojina unamaanisha nini hata!!”
“Bosi wake mzee Matata ndo katoa tamko hilo la
kumsimamisha kazi eti anaandika habari za kichochezi!!...”
alijibu kinyonge.
Nikastaajabu, tangu zamani nilijua kuwa mzee Matata nd’o
mmiliki wa ile kampuni, kumbe na yeye ana bosi wake.
Nilistaajabu mno, kisha nikajenga picha ya huyo bosi wake na
kujiuliza iwapo namfahamu ama nimewahi kuona Matata
akiongozwa na mtu yeyote.
Hapakuwa na jibu la uhakika, na kama ningeamua kuwa na
jibu basi ni kwamba ofisi kuu ya gazeti lile ilikuwa ile ya
mzee Matata.
“Kwa hiyo sasa…” nilijikuta nikiuliza tu bila kuelewa kwa
nini nauliza.
“Hatuna hata senti tano, akaunti zake zote zimefungwa.
Mkewe tangu atoweke kwenda katika mambo ya vikao vya
wanawake hajarudi na simu haipatikani.” Alizidi
kunyong’onyea.
“Na mzee mwenyewe yupo wapi?”
“Nimemficha mahali Sam, hali si shwari na nimempa onyo
asitoke hata kidogo. Hilo si jambo la kawaida. Amenielewa na
ametii. Sam kiuhakika tunahitaji pesa kwa namna yoyote ile
huku si kwema tena. Hawa watu wapo Tanzania nzima.
Hakika ukiwajua ama ukitaka kuwajua tu unapotezwa!!”
mama lao alisihi.
Sikuona haja ya kumweleza lolote ambalo mimi binafsi
nilikuwa nimepitia, badala yake nilimuahidi pesa hiyo
aliyoihitaji kuwa nitamtumia. Mzee Sendeu alitikisa kichwa
kuunga mkono namna nilivyokuwa namjibu mama lao.
Jambo hilo likazidisha imani yangu kwake na mwisho
akatokwa na machozi na kuniambia neno lililonifanya
niingiwe uoga lakini na huruma vilevile.
“Natamani ningekuwa na miguu yangu yote miwili, natamani
wasingeharibu jicho langu hili. Leo hii ningeongozana na
wewe katika harakati hizi za kujua kuna nini kinafichwa
hapa. Lakini wameniwahi na kunitia ulemavu wa maisha na
bila shaka nikithubutu kutoka humu ndani wataniua kwanza
mimi kabla ya kuwatesa sana ninyi!! Hawa si wanadamu wa
kawaida Sam. Nakushauri kama ipo nafasi wewe jiweke mbali
nao. Kaa mbali tu haidhuru kitu.
Sikukatishi tamaa lakini elewa kuwa namna yangu ya kupona
na kuendelea kuwa hai si kila mmoja awezaye kupona hivi.”
Alimaliza huku akinikazia jicho lake moja.
Chumba kilikuwa kimya kwa sekunde kadhaa kabla simu yangu
haijaita tena!!
“Jojina..”
“Sam…. Nilisahau kukwambia kitu kimoja, katika
purukushani hizi za hapa na pale nimegundua kitu, sijui
kama ni chenyewe ama la!! Lakini hata kama ni chenyewe
Sam, sikushauri uende mbele zaidi. “
“nini tena jojina…”
“Ni ule ufunguo chakavu, sina uhakika sana lakini nimekuta
kitu kama hicho katika pochi langu!! Sijui kama ni wenyewe
na hata kama ni wenyewe Sam nakusihi, tusitishe kwa muda
kidogo harakati hizi hata pale tutakapoonana sote kwa
pamoja…” kauli ya funguo ilituliza jazba zangu maana
nilipanga kumkaripia mama lao kwa kuwa kigeugeu, mara
juzi aniite mimi muoga leo hii tena anasema tuahirishe.
Na hapo likanijia wazo la kucheza na akili ya Jojina.
“Jojina ni kama ulikuwa katika mawazo yangu!! Umoja ni
nguvu hakika, nitawangoja. Lakini nakusihi jambo moja
ulifanye. Uagizie huo funguo kwa njia nyepesi uweze
kunifikia huku. Nihakikishe kama ni wenyewe ili niachane na
haya mambo ya kuchonga kisha nawasubiri…..fanya hima
Jojina wakati hao wajinga wapo huko huko Dar.” Nikarusha
maneno, yakamwingia Jojina…
Akakubaliana nami.
Hakujua kichwani mwangu nawaza nini. Nilikuwa na hasira na
sikuwa na hofu tena.
Liwalo na liwe!!!!
Nikaagana na mzee Sendeu nikatoweka na kumwahidi
kurejea tena kwake kwa ushauri zaidi.
BAADA ya siku mbili nikapokea funguo zile zikiwa zimetumwa
kwa njia ya basi, ziliambatanishwa katika kitabu kikubwa
katika bahasha, jina lililoandikwa ni Jonhson Fortunatus.
Nami nikajitambulisha kwa jina lile nikapokea bahasha.
Swadakta!! Ulikuwa wenyewe, ufunguo alionipa Ezekiel
maeneo ya Ubungo. Kitu ambacho sikujua matumizi yake
lakini sasa natambua kuwa ni kitu muhimu sana
ninachokihitaji.
Nikiwa na munkari ya hali ya juu sana, nikaondoka muda
huohuo na kurejea nyumba ya kulala wageni. Huku nikaweka
mikakati sawa. Mikakati ya kumhadaa Masawe tena ili
nifanikiwe kutimiza jambo nililowaza!!
Kuingia katika hifadhi ile ya siri!!
Pombe!!
Ni hiki kitamfanya ahadaike na mimi niingie ndani!!
Nikasinzia na wazo hilo!!
*****
KINDO CHIZI
MASAWE alikuwa ameikubali ofa yangu, akaanza chupa ya
kwanza, mara ya pili hadi ya sita akili yake ikawa
imevurugika na akawa mcheshi sana. Mimi nilikuwa makini
sikunywa kwa pupa. Nilitaka yeye alewe mimi nifaidike,
wasiwasi ulikuwa kidogo maana nilishahakikishiwa kuwa watu
wabaya walikuwa Dar es salaam wakinitafuta.
Nilibeba bia za kutosha na kuzileta katika banda la Masawe!!
Wachaga kwa pombe!! Mbona nilimuweza.
Masawe alipopendeza kichwani nami nikajifanya nimelewa
nikaanza kumuuliza maswali hapa na pale.
Hatimaye akaanza kuropoka hapa na pale juu ya bosi wake.
“Bosi wangu mimi mpole sana lakini hataki tu kuchokozwa
yule, yaani kingine hataki kabisa ujue mambo yake
hovyohovyo, mimi sitaki kujua mambo yake kwa sababu
ananilipa lakini mbili yangu, nakula na kulala bure. Bosi
wangu mtu safi sana lakini watu wanamchokoza..” akasita
kidogo kisha akabeua, akapiga funda jingine kisha
akaendelea, “Mambo ya bosi ni ya bosi mimi hayanihusu, hata
Kindo nilimwambia aache kuwa na kiherehere akaniona mimi
----- wa mwisho, eti kisa tu aliwahi kufanya kazi sijui wapi
huko panaitwa eheee Michigani, nd’o huko na mimi
niliambiwa nakuja kufanya kazi lakini nikaishia hapa, hata
picha za hiyo hoteli sijawahi kuziona mimi. Kindo alikuwa
ananihadithia, mara Michigani sijui inafanya nini mara huko
Michigani nd’o kuna raha za dunia. Hebu tazama shehe
wangu mfano mimi umeniajiri wewe halafu tena naleta mtu
mwingine ndani ya duka lako, we utanielewa kweli. Sio mara
moja au mbili, Kindo anamleta ndugu yake humu ndani,
anaitwa nani vile sijui Alvin kitu kama hicho. Huyo Alvin
akifika mara wananiambia nitoke nje, mara wananiambia
mimi sijui mshamba.
Maneno yale yakanikera kweli ndugu yangu nikashindwa
kuvumilia nikamweleza bosi.
Siku hiyo Kindo akaitwa na bosi, sijui waliongea nini hata
lakini baada ya siku mbili akawa haji tena kazini, nikamkuta
akiwa chizi huko anaokota makopo mtaani. Mimi siwezi
kumchokoza mtu wa namna hii hata kidogo.”
“Na huyo Alvin wakasaidia kuokota makopo ama?”
nikamuuliza Masawe mlevi.
“Alvin hakuonekana tena, bosi alikuwa haijui hata sura yake
kwa jinsi alivyoniambia lakini alikuwa akimsaka sana.
Nikamuuliza kama kuna tatizo. Akasema kuna vitu fulani
havionekani mle ndani, huenda wameviiba…. Kuna kauli moja
aliisema nd’o nikaamini kuwa si mtu mzuri huyu bwana.
Akasema Kindo mwenyewe nshamtia uchizi hata hawezi
kunisaidia kitu!!. Kwa maana hiyo ni yeye aliyemtia
uhayawani yule jamaa. Wanadamu we acha tu…” alisikitika
kisha akafakamia tena pombe!!
Akaniachia nafasi ya kufanya tafakuri, juu ya Kindo na jina
hili la Alvini.
Sasa inamaana Alvin ndo Ezekiel kweli na hili ndo chimbuko
lake, na je yawezekana baadhi ya vitu alivyochukua na
ufunguo ulikuwa mmoja wa hivyo vitu? Pamoja na
makaratasi yale labda!!
“Masawe!! Kwa hiyo Kindo yupo bado hapa Iringa na je
akikuona hakukumbuki ama…”
“Hayupo yule, nilimsikia….. ujue bosi wangu ni rafiki yangu
sana na ananiamini, nilimsikia akijisemesha ili nimsikie
alisema kuwa hatimaye amemkamata huyo wa kuitwa Alvin,
kisha akajisifu kuwa ameua ndege wawili wa jiwe moja jijini
Dar yaani kindo na Alvin. Mimi kama unionavyo huwa
simuulizi maswali na nadhani nd’o kitu anapenda yaani niwe
bwegebwege hivi hivi.”
Majibu ya Masawe yakanitoa ukungu machoni!
Huyu bosi wake anajua kila kitu juu ya mkakati unaoisumbua
akili yangu na anajua pia juu ya sakata zito la anti Ezekiel.
Nikataka kumhoji zaidi lakini alikuwa anakoroma tayari kwa
usingizi.
“We Masawe wewe!! Masawe!!” nikajaribu kumtikisa lakini
hakujibu kitu zaidi ya kuendelea kukoroma, hakika alikuwa
amelewa!!
Ni hiki nilikuwa nahitaji, alewe sana ili aropoke mengi na
kisha asinzie kabisa niweze kufanya yangu!!
Yote yalikuwa yametimia.
Ni mimi tu niliyesalia kuchukua maamuzi!!!!
Nikasimama kwa tahadhari, nikajipekua na kukutana na ule
funguo kutoka jijini Dar es salaam.
Nikaingia hadi nikaufikia ule mlango wa siri, nikachomeka
funguo ule. Mlango ukafunguka ulikuwa na kuselelesha
kushoto na kulia. Nikauselelesha hivyohivyo. Nikapata
upenyo nikachungulia ndani, palikuwa na mwanga hafifu
sana, nikatega sikio nisikie kama kuna watu ndani yake
lakini hapakuwa .
Nikajipenyeza vyema na kuingia ndani nikapokelewa na hewa
murua si baridi sana lakini inayoburudisha. Nikashuka ngazi
moja baada ya nyingine huku macho yangu yakitazama huku
na kule, nilipoikanyaga ngazi ya tatu mara taa kali
zikawaka, na mlango huku nyuma ukajifunga.
Hofu ikatanda!!!
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO
Nikasimama kwa tahadhari, nikajipekua na kukutana na ule
funguo kutoka jijini Dar es salaam.
Nikaingia hadi nikaufikia ule mlango wa siri, nikachomeka
funguo ule. Mlango ukafunguka ulikuwa na kuselelesha
kushoto na kulia. Nikauselelesha hivyohivyo. Nikapata
upenyo nikachungulia ndani, palikuwa na mwanga hafifu
sana, nikatega sikio nisikie kama kuna watu ndani yake
lakini hapakuwa .
Nikajipenyeza vyema na kuingia ndani nikapokelewa na hewa
murua si baridi sana lakini inayoburudisha. Nikashuka ngazi
moja baada ya nyingine huku macho yangu yakitazama huku
na kule, nilipoikanyaga ngazi ya tatu mara taa kali
zikawaka, na mlango huku nyuma ukajifunga.
Hofu ikatanda!!!
***
Hofu ikaanza kutanda, nikageuka nilipotokea palikuwa na
mwanga mtupu sikuuona mlango.
Maajabu. Nikaendelea mbele huku nikitetemeka. Kwa mbali
nikajihisi kujutia kile kitendo cha kuzama katika mkasa huu
ambao mama lao alikuwa amenishauri tuungane pamoja
kuweza kuumaliza taratibu na kiuhakika.
Njia zilikuwa nyingi sana na sikujua njia ipi inaenda wapi,
kila njia ilikuwa na herufi zake tofauti!!
Jumba la maajabu!! Nikakiri hata kabla ya kuelewa kama
nitatoka salama ama la!!
Nikacheza pata potea nikachagua njia ya kuifuata.
Niliponyanyua uso wangu juu. Mara macho yangu yakaiona
ile picha fulani hivi, nikaamua kusogea taratibu ili niweze
kuitambua kama ni yenyewe ama la. Sikuhiotaji kutembea
sana kabla sijahakikisha kuwa ile picha ninayoiona mbele
yangu ilikuwa picha ya mtoto. Si mwingine ni ya mtoto
ambayo kwa mara ya kwanza niliiona katika makablasha ya
Ezekiel ambaye naaminishwa kuwa jina lake lilikuwa Alvin.
Picha hii haikuishia pale tu, pia Anitha alinitumia picha
ambayo inaonyesha picha hii, na akadai hajui wapi alipo.
Kisha akatekwa na wanaume waliovaa suti nyeusi!!
Hata mimi sijui nilipo!! Mungu wangu!!.. nikahanika
nisielewe kama nipo sahihi kuwa eneo lile ama sipo sahihi. Na
hata kama sipo sahihi bado nilitakiwa kuwa pale maana
mlango haukuwa ukionekana tena.
Nikajiuliza ilikuwaje Anitha akafika eneo kama lile na
nkupiga picha, ama kuna eneo jingine zaidi aliwahi kufika
maana picha ile ni kama ile aliyonitumia katika barua pepe.
Pangekuwa na hali ya kawaida kidogo tu jasho lingeweza
kunitoka lakini hali ya hewa ilikuwa baridi la kiyoyozi.
Ukimya ulitanda sana.
Hapakuwa na kelele hata kidogo!!
Nikaendelea mbele kidogo, mara nikasikia kama mchakato
fulani hivi, nikatega sikio vyema nitambue ni kitu gani
kinafurukuta ndani ya jingo lile. Sikuwa nimejiandaa kwa
majibu yoyote endapo nikikamatwa pale. Maisha yangu
niliyaweka rehani.
Mara ule mchakato ukaongeza kelele na nikasikia vishindo
nyuma yangu!! Macho yakanitoka nikataka kukimbia lakini
sikwenda mbali, nikakanyaga kamba za viatu vyangu na
kupiga mweleka chini!! Nikataka kusimama, macho yangu
yakakautana na viumbe wawili. Waliponiaona wakageuza na
kurudi walipotoka kwa mwendokasi wa kutisha. Nikasimama
na kutabasamu kidogo huku nikiunyoosha mkono wangu na
kusikitika sana kupiga mweleka nikiwakimbia panya buku!!
Wasiojua hata maana ya uwepo wangu ndani ya jumba lile la
siri kubwa!!
Hofu ikatoweka tena nikaendelea na njia ile hatimaye
upande wa kulia nikaiona njia iliyonyooka vyema nikaifuata
huku nikiwa na hofu juu ya uhai wangu, lakini nisingeweza
kurudi nyuma hata kidogo maana niliamini hiyo ilikuwa njia
ya kwenda kuikomboa familia yangu. Njia hii ilitia matumaini
kiasi fulani, ilikuwa imetandikwa zulia jekundu.
Sam, nikajikuta natembea katika zulia jekundu. Lakini
sikuwa na amani bali hofu na uoga tele. Kwa mbali nikamuona
mtu!!
Nikashtuka sana kwa mara ya kwanza kumuona mtu katika
kasri ile ya maajabu!! Nikataka kukimbia na yeye akataka
kufanya hivyo, nikaanza kurudi kinyume nyume na yeye
akaniiga, halafu na yeye alikuwa na hofu kubwa. Hili likanipa
matumaini ya kutomuogopa, nikaamua kwenda mbele. Na yeye
akaenda mbele ili tukutane.
Na hapo nikagundua kuwa nilikuwa naiona taswira yangu
katika chumba kilichojengwa kwa kutumia vioo.
Nikatabasamu na ile taswira nayo ikatabasamu!!
Mapigo ya moyo yakapungua mwendo kasi. Nikaacha
kuitazama ile taswira nikalitazama lile jengo la kuvutia.
Nikanyanyua macho juu ili nione urefu wake unafikia kimo
kipi, mwisho wa jingo lile nikakutana na maneno makubwa ya
kung’ara. Yaliyoniduwaza, nikayasoma mara mbili mbili.
“MICHIGANI HEAD OFFICE”
Moyo ukapiga kwa nguvu sana.Nikagutuka na kutaka
kukimbia, ile Michigani niliyokuwa naitafuta miezi kadhaa,
michigani inayosadikika kuchomwa moto ilikuwa mbele yangu.
Badala ya kufurahia nikahofia kukumbwa na mambo mabaya
katika jumba hilo la aina yake, nilikuwa ndani ya ile Michigan
niliyokuwa naitafuta siku zote kwa ajili ya kung’amua siri
juu ya Ezekiel.
Nikakisogelea kile kioo na kuangaza ndani kwa namna ya
kuchungulia.
Nikaona kiti cheusi cha kuzunguka kilikuwa wazi na kuna
koti lilitundikwa juu yake, bila shaka kuna mtu alikuwa hapo.
Nikaendelea kuangaza nyuma yake juu nikaona picha
iliyotundikwa, niliwahi kuiona mahali sura ile.
Nikajitahidi sana kutuliza akili nikatambua kuwa niliiona
nyumbani kwa Ezekiel, hiyo picha ya mwanaume wa kizungu,
na pia hiyo picha ilikuwa katika yale makablasha niliyokuwa
nimeyabeba kutoka nyumbani kwake ambapo nilikutana na
maiti yake. Lakini si hivyo tu hii picha kuna mahali pa ziada
kabisa nilipata kuiona kwa dharula sana, nikakifinyafinya
kichwa changu nikumbuke kama ni kweli niliona picha ama
mtu halisi mahali.
Hakuwa cheupe dawa, huyu alikuwa tofauti sana!!
Alikuwa anatabasamu!! Bila shaka ile ofisi ilikuwa yake na
yeye ndiye alikuwa kinara wa kasri hilo la Michigani.
Ile hali ya kuamini kuwa ndani ya hilo kasri kuna watu
wanaishi iliniletea wasiwasi mkubwa sana. Nikajitabiria kifo
iwapo nitagundulika kuwa eneo lile kiholela na si mwenzao
bali adui yao. Wazo likanijia la kuvujisha baadhi ya siri
ambazo zinaweza kuwawezesha mama lao na mzee Matata
kuweza kugundua kambi hiyo hata Kama nikiwa nimekufa
kinyama waweze kuyapata maiti yangu. Na ukweli uwe wazi.
Nikajiahidi kuwa nitapiga picha na kisha kama itawezekana
nizitume kwa njia ya email nikiwa humohumo Michigani. Na
litakalotokea baada ya hapo ni kuwaachia walio hai
walifikishe kwa walio hai wenzao. Sikuwa naogopa tena kufa
iwapo tu mama lao atanielewa.
Nikajipekua na kuitoa simu yangu nitazame uwezekano wa
kuwasiliana. Nikajaribu kubofya vitufe kadhaa nimpigie
Jojina lakini simu haikuwa na mtandao. Nikainyanyua huku
na kule lakini tatizo likabaki kuwa lilelile.
Hapakuwa na uwezekano wa kuzungumza kwa njia ya simu
ukiwa ndani ya ficho lile la ajabu!!
Nikaanza safari ya kurudi kutoka nje!! Nikajiapiza kuwa
nitauvamia mlango na iwe isiwe mpaka niufungue tena.
Nikajipekua na kuushika vyema ule ufunguo wenye kutu
ambao kwa tahadhari kuu niliuchomoa pale mlangoni baada ya
lango kukubali kufunguka. Sasa nilihitaji kufungua tena
niweze kutoa nje na kisha kufanya mawasiliano na mama lao
kisha nirejee tena kikamilifu. Nikajipa imani kuwa
nitakumbuka kila hatua niliyokuwa nimepita kabla kuingia
eneo la ofisi ile.
Hapa nilitamani kulia, maana nilipotea njia huku na kule,
nikajaribu kutuliza akili lakini sikuweza hata kidogo
kukumbuka ni wapi nilitokea hadi kufika humo ndani. Kila
upande niliojaribu kwenda ulikuwa mrefu kuliko mwingine,
na karibia kila kona ilifanana na kona nyingine.
Nikahaha huku na huko, bado hali ilikuwa tete, nikafikia
mahali nikakutana na ukumbi mwingine ukiwa umezungukwa
vioo pia. Nikiwa pale nikashangaa kuona watu kwa ndani,
kabla sijajua nifanye nini niliwaona wakinijia kwa kasi sana,
nikaanza kurudi kinyumenyume.
Nikagota katika vioo vingine, nikawa natazamana ana kwa
ana na wale watu! Walikuwa uchi na wote niliowaona kwa
harakaharaka walikuwa watoto wa kiume.
Walikuwa wakinisihi jambo fulani lakini sikuweza kuzisikia
sauti zao, nilitamani kuwasikiliza zaidi lakini hata mimi
nilikuwa matatani na sikuwa natambua ni wapi nimetokea na
wapi sahihi natakiwa kwenda.
Masaa yalikatika nisijue nimekaa humo ndani kwa muda gani.
Hali ya mule ndani haikubadilika ili kuwezesha kutambua
kama ule ni usiku sana ama ni mchana au asubuhi, hali
ilikuwa ileile, nilipanda na kushuka lakini sikuweza kuuona
mlango wa kutokea. Michigani ilikuwa Michigani haswa.
Nikaendelea kuhaha na hatimaye nikakutana na mlango
mwingine na huu nikaufungua baada ya kuona kitundu
kikifanana na ufunguo wangu, nikadhani kuwa hata ile
yaweza kuwa njia ya kutokea.
Looh!! Nikakutana na mwanaume akiwa amechoka sana na
bila shaka alikuwa amekata tamaa, nikastaajabu mambo
mawili. Ule ufunguo na yule bwana aliyefungiwa mle ndani ya
kile chumba kidogo. Alikosa nini hadi atendwe vile.
“Nisa….saidie..” aliongea sauti ya chini, alikuwa amekonda
na ngozi yake kubabuka kama aliyemwagiwa mafuta ya moto.
“Wewe ni nani….” Niliuliza kiuoga huku nikijiweka mbali
naye.
“Anti…..Anti…Ezekiel….” alijitambulisha kwa shida sana,
nikashangaa utambulisho huu. Kivipi hawa wa kuitwa Anti
Ezekiel wawe wengi kiasi hiki. Nikainama na kumtazama
vyema nikidhani kuwa ni yule aliyeniingiza matatani na
familia yangu kutokomea kwa sababu yake. Lakini hata kama
alikuwa amechakaa namna gani, hakufanania na yule Ezekiel
ninayeaminishwa kuwa anaitwa Alvin. Huyu alikuwa tofauti
kabisa.
Hawa jamaa vipi? Nilijiuliza huku nikihisi hasira kali
ikinitwaa kwa sababu ya fumbo ambalo nilidhani kwa kuwa
ndani ya michigani nitakuwa nimelifumbua badala yake hali
iliendelea kuwa tete.
“Sikuelewi…sikia wewe ni mwenyeji humu ndani? Niambie
niambie tafadhali natoka vipi ili niweze kukusaidia..”
nilimsihi kwa sauti ya chini kiasi.
“Ni ngumu … wanafunga kila upande wa jumba hili…wanaiita
nchi yao…” alilalama kwa sauti ya kunong’ona.
“Kina nani wanaoiita nchi yao eeh!! Ni akina nani hao.”
Nilihoji upesi upesi sasa nikiwa nimechuchumaa.
“Wazungu na vibaraka wao wa kiafrika….fungua ofisi
chukua nyaraka ukifanikiwa kutoka kaitangazie dunia… ”
“Ofisi ipi..na nyaraka ipi sasa eeh!!…” sikuelewa kabisa yule
bwana anajaribu kuniambia kitu gani. Kila aliochokisema
kilikuwa kipya.
“965901” alizitaja namba zile kwa tabu na hakuweza
kuongea tena akabaki kunitazama huku mikono yake
inayotetemeka ikinisihi kurejea nilipotoka.
Nikatamani kumbeba lakini ningempeleka wapi, nikarejea
njia niliyotoka, nikaifuata kwa muda na kukutana na tena
na ile ofisi kubwa ya vioo. Safari hii sikupotea sana.
Nikachungulia na kuona kablasha kubwa mezani.
Huenda ni hilo!!! Nikajiongeza!! Na hapo nikaona mahali pa
kufungua mlango kwa kutumia namba za siri.
Nikaanza kubofya!!
96…..59….. Mungu wangu!! nikasahau namba mbili za
mwisho. Nikajaribu kukumbuka lakini haikuwezekana, yule
bwana alizitaja mara moja, na hapo nikatambua kuwa
sikumsikiliza kwa makini na sasa niliuona umuhimu wa namba
zile.
Nikatimua mbio hadi kwa yule bwana tena, nikamkuta akiwa
bado amekodoa macho, hakuyapepesa hata kidogo.
“Nimesahau namba mbili za mwisho ndugu yangu….namba za
siri…TISA SITA TANO TISA…….” nikamtajia ili amalizie
lakini hakuwa akiweza tena kusema , akabaki kukodoa
macho, mkojo kidogo unitoke kwa kutamani aweze kusema ili
nijue ni nini katika makablasha yale.
Nikamtikisa lakini hakuonekana kupatwa na hisia zozote
zile!!
Mkojo ukachuruzika!! Sikuweza kuuzuia!!
Na hapo nikasikia vishindo kwa mbali!!!!
Hofu ikazidi.
 
Mwee sehemu ya 23 wapi jama??

Inaelekea ni kali maana wadau mnaifuatilia kweli, mie ilinipita, embu ni comment ili uzi huu uwepo kwenye profile yangu kama reference ili iwe rahisi kuutafuta na kesho jpili niusome nikiwa nimetulia
 
Inaelekea ni kali maana wadau mnaifuatilia kweli, mie ilinipita, embu ni comment ili uzi huu uwepo kwenye profile yangu kama reference ili iwe rahisi kuutafuta na kesho jpili niusome nikiwa nimetulia

inabidi uwe na akili kama james bond kuielewa, ila ni nzur sana
 
Inaelekea ni kali maana wadau mnaifuatilia kweli, mie ilinipita, embu ni comment ili uzi huu uwepo kwenye profile yangu kama reference ili iwe rahisi kuutafuta na kesho jpili niusome nikiwa nimetulia

Mkuu karibu sana, Tusaidie kumwita mzaramo aendeleze story katuga eti!
 
Last edited by a moderator:
SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU
“Kweli huo ni mtihani mgumu, lakini Sam unakumbuka kuwa
kila jaribu linalokuja kwa mwanadamu huwa linayo njia yake
ya kutokea? Basi amini kuwa hata kikwazo hiki tukakiruka.
Kama unaweza kwenda tena kwa huyo Masawe basi hakikisha
kuwa unachukua alama ya hilo tundu ili tuweze kuchonga
ufunguo wa bandia…….” Alianza kushauri Mama lao.
Nikaingilia kati na kumweleza kuwa kile kitasa ni cha aina
yake na hata ule funguo ulikuwa wa aina yake. Mama lao
akasihi kuwa ni heri kujaribu kuliko kupuuzia.
Nikakubaliana naye, lakini kila nilivyoujengea picha ule
ufunguo chakavu alionipatia Ezekiel na umbo lake la
kustaajabisha niliamini kabisa kuwa zile zilikuwa mbio za
sakafuni tulizokuwa tunajaribu kukimbia.
Lazima ziishie ukingoni tu!!
Tukaagana na mama lao, na kuahidia kupeana matokeo kwa
siku inayofuata.
Huo ukawa usiku wenye matumaini kiasi fulani, lakini
sikujua kama asubuhi ya siku inayofuata ingekuwa asubuhi
ya kustaajabisha ndani ya jiji la Dar es salaam na wakati huo
mjini Iringa!!!
Ni heri tusingefikia maamuzi yale!!
Lakini hatukujua!!!
***
ASUBUHI baada ya stafutahi ya wastani nilijongea katikati
ya mji huku na kule nikitazama hiki na kile na hatimaye
nikapata mahali ambapo wanachonga funguo. Nikawaeleza
shida yangu, wakanielewa na kunitaka nilete alama ya tundu
la kitasa ambacho nahitaji kuchonga funguo zake.
Wakanieleza kuwa alama sahihi nitaichukua kwa kutumia
kipande cha sabuni.
Nilipotoka pale moja kwa moja nikaenda dukani kwa Masawe.
Alinipokea kwa furaha zote, alikuwa anatabasamu pana
ambalo bila shaka lilionyesha dalili ya tumaini jipya!!
Akanisabahi kisha akanihoji kuhusu kutoweka kwangu siku
iliyopita bila taarifa.
“Kwanza nilivyokuagiza ulivipata?” nilipoteza uelekeo wa
swali lake.
“Sijakosa hata kitu kimoja ati! Vyote nimepata tena kwa bei
poa tu!” alinijibu huku akisahau kuwa sijamjibu swali lake la
awali!!
Nikataka kutia neno, Masawe akaendelea kuzungumza.
“Nikaona nom asana kuviweka humu ndani maana bosi
angevikuta ingekuwa kesi, hachelewi kusema kuwa namwibia.
Vipo hapo kwa jirani yangu mmoja…..”
Neno la mwisho la Masawe likanipa mwanga na akili
ikafunguka!! Huo ulikuwa mwanya mwingine wa kuweza
kufanya jambo.
Nikamsihi aende kuleta vitu baadhi alivyonunua niweze
kuvitazama.
Masawe akatoweka akiliacha duka lake wazi. Mguu wake
ukitokomea mimi nikaingia ndani ya kile kibanda, moja kwa
moja katika lile tundu la funguo. Nikailowanisha sabuni
kidogo kutoka katika duka la Masawe kisha nikagandamiza na
kuipata alama kama walivyonielekeza mafundi.
Nikaifunika ile sabuni na kuitia mfukoni.
Masawe aliporejea mimi sikuwa na habari, nilichokitaka
nilikuwa nimekitimiza tayari.
Mazungumzo kati yetu niliyaona kama kelele tu
zinazonisumbua masikio, nikamzuga Masawe kuwa nimepigiwa
simu fulani. Nikampa pesa kidogo na kumshukuru kwa wema
wake wote. Nikatoweka nikiwa katika haraka, nikapita huku
na kule nikachukua taksi.
Nikamwelekeza dereva wapi pa kunipeleka.
Akatia gari moto na kuanza kuitafuta sehemu.
Dereva huyu alikuwa muongeaji sana, akanieleza juu ya
jaribio la wizi wa taksi lililofanywa na shanta mmoja
akishirikiana na mteja wake. Akanielezea gari ilipokutwa!!
Nikatambua anaizungumzia gari ambayo niliitumia siku
iliyopita nikiwa na shanta aliyeingia matatani na kisha
kutoweka. Nikajifanya kushiriki katika maongezi yale lakini
nilikuwa katika kumchimba tu nipate mawili matatu
kuhusiana na na usalama wangu!!
Hali ilikuwa shwari hakuna hata mmoja aliyebahatika
kukumbuka walau nguo nilizokuwa nimevaa!!!
Alinifikisha nilipohitaji nikamlipa chake na kuingia katika
harakati za kuusaka ufunguo.
Nikawaonyesha wale mafundi alama ya tundu lile,
wakalitazama kwa makini na kukiri kuwa hawawezi
kutengeneza huo funguo na badala yake wakanielekeza kwa
mzee Sendeu. Mkongwe katika kuchonga funguo za kila aina.
Hata hao mafundi walikiri kuwa alikuwa kiboko yao na
walimkuta katika ufundi huo.
Nikaongozwa hadi katika kibanda chake kidogo!! Akanipokea
vyema na kisha tulipobaki wawili akabaki kunisikiliza. Wakati
nazungumza niligundua kitu, kuwa mzee yule hakuwa na
amani sana na ile miwani yake usoni haikuwa ya heri sana.
Nikajipa jibu kuwa huenda huwa anawachongea majambazi
funguo bandia maalum kwa shughuli zao, ama la yeye
mwenyewe si mtu mwema.
Lakini hayo yote hayakuwa yakinihusu hata kwa mbali,
kilichonihusu ni kuupata funguo wangu kwa ajili ya manufaa
yangu!!
Nikamweleza shida ileile na kisha kumpa ile sabuni yenye
alama.
Ama! Akaiachia ghafla ile sabuni!! Ikaanguka chini, akataka
kutoa miwani yake usoni akasita. Akapigwa na bumbuwazi la
waziwazi usoni!!
Nikaduwaa zaidi yake!! Na wala hakujishughulisha katika
kuiokota ile sabuni!!
“Wewe ni nani? Aliniuliza… nikakosa cha kumjibu na nisijue
nini maana ya swali lake. Nikiwa bado naduwaa niliona
akibonyeza namba za simu lakini hakuzungumza chochote
kile, uso wake ulitawaliwa na ghadhabu!! Nilitaka kuondoka
lakini nikajiuliza ni kwanini niondoke. Yawezekana kukutana
na mzee yule ni njia mojawapo ya kuifikia siri kuu!! Na
mbaya zaidi kuondoka kwangu kusingesaidia chochote kile.
Lakini kubaki na mtu nisiyemjua hili lilikuwa tatizo zaidi.
Nikaamua kusimama niweze kuondoka!! Akabonyeza tena
simu yake.
Milango ikajifunga tena!!
“Wewe ni nani nakuuliza??” sasa alikuwa ametoa miwani
yake usoni na alikuwa anakanisogelea!!! Nikajaribu kurudiu
nyuma.
Mzee alikuwa na miguu ya bandia na hata jicho lake moja!!
Hakuwa na jicho moja!!!
Alitisha kumtazama.
“Naitwa Dickson naitwa Dickson mzee wangu….” Nilijikuta
nalainika na kujibu alichouliza japokuwa nilikuwa
nadanganya.
Nilidhani jibu lake litamfanya aweze kutulia, lakini mara
akaurusha mkono wake. Nilikuwa sijajiandaa kwa tukio hilo,
kiganja chake kizito kikatua katika shavu langu.
Naam!! Maumivu makali haswa yakasambaa katika uso wote
na kichwa kikakumbwa na maumivu!!
Hakuishia pale yule mzee wa kutisha.
Mara akarusha gongo alilokuwa anatumia, hata hili pia
sikulitarajia lakini sijui ilikuwaje nikawahi kujikinga uso
wangu. Likanikung’uta mikononi. Maumivu mapya kabisa.
“Kwa hiyo nd’o mnataka kuniua eeh!!” akatokwa na kauli
hiyo. Sasa alikuwa ameikamata shingo yangu.
Uso wenye jicho moja ukawa unatisha zaidi ulipokuwa karibu
nami!!
“Nilitamani kusema neno lakini alikuwa amenikaba haswa!
Macho yakamsihi lakini ni kama hakutambua hilo.”
“Kindo na mwenzake wapo wapi?” aliniuliza swali lile huku
akiamini kuwa jibu ninalo basi tu ni kiburi.
Akaniachia ghafla nikawa nakohoa kwa fujo!!
Na hapo akatoa kisu kikali sana.
“Usipojibu maswali yangu nakufanya kama nilivyofanywa,
nang’oa jicho, nakata miguu na masikio, nakung’oa na hiyo
pua yako mwanaharamu wewe…” Akazungumza haya huku
akitetemeka.
“Naitwa Sam mzee wangu, hakuna nijualo kuhusu hayo
unayoniuliza niamini mzee wangu sijui lolote na mimi ni
mtafutaji tub ado sijapata chochote.” Nilizungumza huku
nikitokwa machozi.
Akanisogelea kwa kuchechemea, akanifikia.
“Unataka kufa eeeh!!” akasema kwa sauti ya chini inayosihi.
“Bonge waitio amekutuma kitu gani kwangu? Na nd’o nani
huyo bonge waiti…..” akaniuliza tena, ni kweli niliwahi
kuyasikia hayo majina mahali lakini sikuwa na maelezo
yoyote ya kuweza kujibu.
“Mzee wangu, nipe dakika tano tu za kujieleza kinaga ubaga
na baada ya hapo nitakuruhusu unifanye utakavyo iwapo tu
itakuwa ni haki yangu kuuwawa kinyama namna hiyo. Na
kama ikithibitika mimi ni mtu mbaya mzee wangu, usisite
kunisulubu. Lakini amini kuwa ukifanya suluba hiyo bila
kunisikiliza basin a kilio changu kiwe juu yako milele.”
Nikajitutumua na kutokwa na kauli ile ya mwisho ambayo
sikutarajia inaweza kuwa chachu ya kutuliza munkari ya
yule mzee mwenye jicho moja!!
Kwa ishara ya kichwa akanipa nafasi ya kuzungumza!! Kisu
kikiwa mikononi mwake imara.
Huo haukuwa wakati wa kuficha siri tena, nilikuwa katika
dakika za mwisho za uhai wangu.
Nikamweleza mzee juu ya uhalisia wa jina langu, wapi
natoka na kisha nikamweleza juu ya kukutana na kijana
shoga aitwaye Ezekiel jijini Dar es salaam, nikakumbuka
kumwelezea mwonekano wa Ezekiel na sikusahau tarehe za
kukutana kwetu.
Nikagusia juu ya utata wa Ezekiel wa Ubungo na yule maiti
wa Temeke Dar es salaam.
Sikuuyumbisha ukweli nikamweleza juu ya mke wangu
kupotea na kisha mimi kuanza kuzushiwa juu ya mambo kadha
wa kadha ikiwemo kifo.
“Wewe kumbe nd’o Samson….. Sam….” Alitokwa na maneno
yale mzee huku kisu kikiwa kimemtoka tayari. Alikuwa
ameduwaa haswa.
Mara akafungua makablasha kadhaa akatoka na magazeti
kadha wa kadha, akachomoa mojawapo. Akakutana nna
habari yangu, akaitazama ile sura na kujihakikishia kuwa
sikuwa nimemdanganya hata kidogo.
“Sam… umewakwepa vipi hadi sasa hawa watu wasijulikana
sura zao” aliniuliza huku akinisaili kwa chati.
Sikuamini kama uso wa yule mzee unaweza kulainika na kuwa
katika masikitiko kiasi kile.
Sikuwa na uwezo wa kujibu chochote kile. Ni kama nilikuwa
ndotoni tu!!
Mzee akajishughulisha zaidi akachukua pamba na kunifuta
damu mdomoni, kisha akaniomba niketi tuzungumze.
Mzee Sendeu!! Akanielezea juu ya mkasa wake. Mkasa
uliowahusisha Kindo na mwenzake ambaye hakuwa
akimtambua jina lakini alikiri kuwa sura yake na ya huyo
Ezekiel niliyemtaja ni kitu kimoja!!
“Wale vijana waliniletea tenda ya kutengeneza funguo,
hakuna funguo iliyonitia wazimu kama ile pale. Kila
nikijaribu kutengeneza wanaenda na kurejea wakidai
haifungui ule mlango. Natengeneza tena na wao wanalipa
pesa nzuri tu… nikakataa tenda zote nikabaki na tenda
moja tu ya kutengeneza ule funguo wa ajabu. Kila
nilipowasihi waende kunionyesha kitasa wakadai kuwa ni
mbali sana. Kwa sababu ni wao walikuwa wanasema basi mimi
nikaendelea kukuruka huku na kule nifanikishe
kuwafurahisha wateja wangu.
Mara ya mwisho kuonana nao wote kwa pamoja ilikuwa ni
siku ambayo walidai kuwa walau ule funguo unazo dalili za
kufungua japo kwa kulazimisha.
Baada ya hapo wakatoweka moja kwa moja!! Na hapo
nikaanza kuandamwa na watu nisiowajua wakinihoji juu ya
mambo nisiyoyajua vilevile.
Siku moja nikakamatwa na polisi, lakini sikupelekwa
rumande nikafungwa kitambaa usoni na kwenda kukutana na
mtu aliyeitwa bonge waiti. Alikuwa anazungumza kiingereza
na walitafsiri nami nikawa najibu.
Yule mtu akaniomba funguo! Nikasema sijui lolote juu ya
funguo. Ebwana walinishushia kipigo cha hali ya juu sana
ndugu yangu!!
Nakuja kupata fahamu nikiwa porini huko, mguu mmoja
haufanyi kazi, na jicho moja likiwa halioni, meno yote haya
ya mbele unayoyaona ni ya bandia sina meno Sam. Wale watu
ni zaidi ya majasusi na sijui niliweza vipi kupona kutoka
katika kifo kile.
Niliokotwa na mmoja kati ya majangili ambayo huwa
nayatengenezea funguo kwa ajili ya kwenda kuvamia
wanapojua wao. Tena waliniokota wakiwa katika shughuli
zao za kijangili.
Wakanichukua hadi katika machimbo yao.
Amakweli tenda wema uende zako bila kuangalia ni nani
ulimtendea wema. Wale watu walimtafuta daktari na
kunipatia tiba, mguu ulikuwa si mguu tena ukakatwa, jicho
haliukuwa jicho tena likang’olewa na kubaki na jicho moja.
Nilikuwa naitwa Masta key kabla sijatekwa na kupotezwa,
basi nikalazimika kufuga ndevu tele na kisha wale majangili
wakanitengenezea maficho haya niendelee na shughuli zangu
nikiwa katika usalama wa hali ya juu. Na hapo wakaniita
mzee Sendeu. Na hilo nd’o jina langu maarufu kwa sasa.
Watu wanaamini kuwa mimi ni mrithi wa Masta Key ambaye
wanadai alitoweka kishirikina.
Hawajui kuwa nd’o mimi hapa.
Sasa leo ulipouleta ufunguo ulionisababishia majanga haya
nikakuona kuwa wewe naye ni mmoja wa watu wabaya
wanaofahamu siri yangu!! Sam kiuhakika nisingekutambua
basi ungekufa kifo kibaya sana leo.” Alimaliza mzee yule
kunieleza juu ya simulizi ile ya kutisha na kusisimua.
Mwili ulisisimka haswa nikijaribu kujenga picha juu ya
mwanadamu kung’olewa jicho na kukatwa mguu.
Watu ninaokabiliana nao walikuwa wanyama haswa!!!
Wakati nikiendelea kufikiria juu ya tukio hilo la maajabu.
Mara katika simu yangu ukaingia ujumbe!!
Hakuwa mwingine alikuwa ni Mama lao..
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA
Nikatamani kumbeba lakini ningempeleka wapi, nikarejea
njia niliyotoka, nikaifuata kwa muda na kukutana na tena
na ile ofisi kubwa ya vioo.
96…..59….. nikasahau namba mbili za mwisho, maana ofisi ile
ilikuwa imefungwa kwa namba za siri. Nikatimua mbio hadi
kwa yule bwana, bado alikuwa amekodoa macho,
“Nimesahau namba mbili za mwisho ndugu yangu….namba za
siri…TISA SITA TANO TISA…….” nikamtajia ili amalizie
lakini hakuwa akiweza tena kusema , akabaki kukodoa
macho, mkojo kidogo unitoke kwa kutamani aweze kusema ili
nijue ni nini katika makablasha yale.
Nikamtikisa lakini hakuonekana kupatwa na hisia zozote
zile!!
Mkojo ukachuruzika!! Sikuweza kuuzuia!!
Na hapo nikasikia vishindo kwa mbali!!!!
Hofu ikazidi.
Nikageuka huku na kule kama kuna mtu yeyote anayekuja,
lakini nikaambulia kukutana na kiganja cha yule bwana
kikigongagonga chini!!
Mlio huu nikaupokea kama vishindo kutoka mahali pengine
Mara Nikauona mkono wake ukijitahidi kuchora chini!!
Nikaona SIFURI MOJA.
Nikatimua mbio hadi kule kwenye ile ofisi tena.
Nikaingiza namba zile!!
Mlango ukafunguka!! Nikaingia ndani upesi hadi katika meza
kuu.
“E.F.Kenton MANAGER!” meza ile ilipachikwa kibao kile,
nikaingia katika makablasha na kusaka hicho alichonambia
yule bwana.
Nikakutana na faili kubwa kabisa rangi yake nyeusi,
nikalichukua na kulifunua ndani kidogo.
Naam! Lilikuwa lenyewe ambalo nilikuwa nalihitaji kwa
ukombozi wa kizazi hadi kizazi. Maneno kadhaa yaliyoandikwa
yalinivutia sana na kutamani kujua mwandishi wake aliandika
nini cha ziada katika ukubwa wote ule.
Nikataka kutoka upesi ndani ya himaya ile na hapa nikakiri
kufanya kosa kubwa katika sehemu ya hatari kupita zote.
Nilikuwa nimesahau namba za siri tena huku mlango ukiwa
umejifunga kwa ndani!! Sikuwa nauwezo wa kumfikia yule
bwana wa kujiita anti Ezekiel anitajie tena kwa umakini,
nilichokumbuka ni ile SIFURI MOJA aliyoichora chini. Zile nne
za kwanza zilikuwa zimeyeyuka.
Mungu wangu!!
Nikakibinyabinya kichwa changu kiweze kukumbuka zile
tarakimu nne za mwanzo, lakini badala ya kuja tarakimu za
kufungulia mlango, likawa linarejea lile neno kubwa kabisa
katika faili nililokuwa nimebeba.
Hakika neno lile lilikuwa zito kuliko zile namba na lilikuwa la
kushtua sana, huenda nd’o lilinipagawisha na kunisahaulisha
juu ya namba za siri.
Nikatulia na kujifanya kuwa sina hofu ili nikumbuke zile
namba.
Nikakumbuka kuwa kuna namba tisa na nyinginezo lakini
mpangilio sikuukumbuka kabisa.
Nilijaribu mara kwa mara kubahatisha namba tofauti tofauti
katika kile kitasa kinachotumia umeme, mara ya kwanza, ya
pili hadi ya nne mambo bado yalikuwa magumu, na ilipofika
mara ya tano mara king’ora kikaanza kulia.
Huku ikiandika neno nililolielewa “PASSWORD ERROR”
Hatari kubwa!! Nikaanza kuhaha huku na kulke katika ile
ofisi nikitafuta namna ya kuweza kutoka nje kama ipo!!
Lakini ngome yote ilikuwa vioo vigumu tupu!!
Sikutaka kukamatwa nikiwa nimekaribia mwisho kabisa wa
mchakato wangu! Sikuwa tayari kukamatwa huku nikiwa na
ile nyaraka muhimu kabisa zaidi ya ile bahasha iliyopotea
awali katika mazingira ya kutatanisha.
Nikatazama huku na kule na kukutana na na chuma kubwa
ambalo sikujua matumizi yake lakini lilikuwa zito haswa.
Nikatua faili langu chini, nikakinyanyua kile chuma kizito
kabisa. Kama zinavyokuwa filamu za mapigano nami nikaamua
kuwa shujaa wa vita hiyo.
Navunja vioo!! Nikajiapiza, nikayauma meno yangu kwa
nguvu kisha nikatimua mbio, chuma likiwa mkononi,
nikajitosa kiume moja kwa moja hadi katika hifadhi hiyo ya
vioo, nikakitupa kile chuma kwa nguvu zote.
Nikasambaratisha vile vioo mbalimbali. Nikatua upande wa
pili kwa kujitupa baada ya kile chuma kuwa kimenitoka
mikononi mwangu.
Sikutaka kuyafikiria maumivu kwanza, nikainuka mbiombio
nikikanyaga vile vioo kwa viatu vyangu, nikakifikia
nilichokihitaji.
Faili likawa mkononi tena!!
Baada ya kulikamata lile faili mkononi ndipo nikayakumbuka
maumivu makali usoni, mikononi na mgongoni. Kisha nikaona
damu.
Vioo vilikuwa vimenitakata vibaya mno na kile king’ora
kilishanyamaza kimya!!
Ina maana hakuna walinzi humu ndani!!!! Nilijiuliza huku
nikistaajabu maajabu hayo ya Michigani.
Niliendelea kuzurura huku na huko, hatimaye nikayaona
mazingira hayo ya Michigan ambayo awali niliyaona katika
picha alizonionyesha mama lao.
Michigani!! Neno likanitoka!! Nikajisikia natabasamu kwa
ndani kuwa hatimaye nipo katika lile jumba la ahadi ya siku
nyingi.
Roho ya kinyama tayari ilikuwa imenikaba nikahakikisha
kuwa funguo wangu upo mfukoni. Nikatafuta kwa udi na
uvumba mahali pa kutokea. Miguu pia ilikuwa imekatwa na
vioo, kila nilipokanyaga niliacha damu, safari hii hata wale
watoto waliokuwa wakinililia katika vioo walinihofia.
Niliutumia ule ufunguo wa maajabu kufungua huku na kule!!
Chumba kimoja nilipokifungua kikatoka kipande cha mtu
ambacho kilikuwa bado kina nguvu!! Kikanirukia kwa
ghadhabu, nikapiga mweleka chini.
Akanifuata kwa kasi, nikahofia juu ya faili langu.
“Mimi ni mtu mwema tafadhali, mimi ni mtu mwema!!”
nilimsihi. Lakini hakuonekana kunielewa, akazungumza
kiarabu!!
Lugha gongana!
Nikaiona hatari waziwazi!! Nikajaribu kumkwepa nikaishia
kuegemea vioo. Akaja mbiombio nikaona isiwe tabu kwa
sababu ni heri mtu mmoja afe kuokoa taifa zima.
Nikajifanya kumkimbia huku nikiwa na wazo moja tu.
Akaendelea kufoka kiarabu nisichokielewa na mimi nikazidi
kukimbia, hadi nikalifikia lile jengo lililopalanganyikana,
nikatupa faili chini, nikatwaa kioo kikubwa kilichovunjika
upesi. Nikageuka na kukutana na jitu lile lenye nguvu
likinijia kwa kasi.
Nikamsukumia kile kioo.
Naam!! Kikazama tumboni huku kikinichanachana mikono
yangu vibaya sana. Nikaokota faili langu, likawa linaloa
damu lakini sikutakiwa kusimama wala kujiuliza. Nikasahau
kuhusu maumivu nikaweka riadha mbele.
Nikapenya huku na kule hadi nilipokutana na mlango
mwingine, nikaufungua ule kwa ufunguo wangu! Nikakutana
na mwanga hafifu kiasi fulani. Na ngazi kadhaa, nikazifuata
hizo hadi nilipofikia kizibo ambacho kilikuwa kinafunguka bila
ufunguo, nikasukuma juu, mwanga halisi wa dunia ukaingia
ndani, nikachungulia nje kabla ya kutoka mzima mzima.
Nikakutana na hali halisi ya Iringa, funguo mfukoni faili
langu mkononi. Nikawa duniani tena nisiamini kuwa nipo hai.
Hali ile ya hewa ilinifanya nishindwe kutabiri muda halisi.
Nikatumia shati langu kujifuta damu zilizokuwa zinatiririka,
kisha nikaanza kujiuliza hapo nilipokuwa ni wapi. Maana
lilikuwa eneo jingine kabisa.
Nikaangaza kwa utulivu hadi nilipoiona barabara! Nikaifuata
na kisha kuingia katika kichochoro kingine na kukutana na
mfano wa chemchem, nikatwaa maji na kujinawisha usoni na
popote palipoonyesha damu.
Hatimaye simu yangu ikanirejeshea fikra za msaada.
Kutazama ilikuwa ikilalamika kuwa betri imeishiwa chaji.
Nikafanya upesi kumpigia Jojina lakini hata simu haikuita
ikawa imezima.
Sikuwa na muda wa kupoteza. Nikaruka matuta kadha wa
kadha na hatimaye nikaupata uelekeo sahihi wa kuelekea
Michigani kwa Masawe! Sikuliacha faili langu na sasa likiwa
katika mfuko. Nilihitaji kujua nini chanzo cha haya yote.
Siku hii dukani pale umati ulijaa, nikastaajabu nini
kinaendelea. Nikaomba kupita lakini watu walikuwa wabishi
sana, nikajitahidi kupenya hivyohivyo. Hadi nikaufikia ukuta
wa polisi ambao haukuruhusu mtu yeyote kupenya pale, mimi
nikiwa na kihoro nikapenya huku nikiwa nusu nakimbia nusu
natembe, risasi ikafyatuka na kuchimba pembeni ya mguu
wangu, mara nikasikia napaishwa hewani. Sasa nikayasikia
maumivu!!
Risasi ilikuwa imenichuna!!
“Mimi raia mwema jamani, mimi raia mwema!!” nikapiga
kelele sana. Askari wakanisogelea wakiwa na hasira kali,
wakataka kuchukua kilicho mikononi mwangu nikawa mbishi
sana sikuwa nawaamini hata kidogo. Niliamini kabisa kwa
jinsi sura yangu ilivyokwanguka kwanguka hakuna ambaye
angeweza kunijua.
Kipigo kikazidi wakinisihi niachie na hapo nikamkumbuka mtu
wa kunisaidia. Lakini kabla sijajua nitamfikia vipi
nikakanyagwa teke mbavuni, mbavu za upande uleule ambao
nilikuwa nimeshikilia lile faili.
Naam! Nikalainika na kuliachia lile faili huku macho yakianza
kuona giza.
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA
Hatimaye simu yangu ikanirejeshea fikra za msaada.
Kutazama ilikuwa ikilalamika kuwa betri imeishiwa chaji.
Nikafanya upesi kumpigia Jojina lakini hata simu haikuita
ikawa imezima.
Sikuwa na muda wa kupoteza. Nikaruka matuta kadha wa
kadha na hatimaye nikaupata uelekeo sahihi wa kuelekea
Michigani kwa Masawe! Sikuliacha faili langu na sasa likiwa
katika mfuko. Nilihitaji kujua nini chanzo cha haya yote.
Siku hii dukani pale umati ulijaa, nikastaajabu nini
kinaendelea. Nikaomba kupita lakini watu walikuwa wabishi
sana, nikajitahidi kupenya hivyohivyo. Nilijihisi moyo
ukisaidiana na kiherehere ukinisukua kusonga mbele,
nilitaka kila mtu ajue kitu asichokijua nilitamani kila mmoja
awe shahidi. Ile dunia iliyokuwa imenitenga nilitaka iungane
nami huku ikiona aibu.
Nilijibana kinguvunguvu Hadi nikaufikia ukuta wa polisi
ambao haukuruhusu mtu yeyote kupenya pale, mimi nikiwa na
kihoro nikapenya huku nikiwa nusu nakimbia nusu natembe,
risasi ikafyatuka na kuchimba pembeni ya mguu wangu, mara
nikasikia napaishwa hewani. Sasa nikayasikia maumivu!!
Risasi ilikuwa imenichuna!!
“Mimi raia mwema jamani, mimi raia mwema!!” nikapiga
kelele sana. Askari wakanisogelea wakiwa na hasira kali,
wakataka kuchukua kilicho mikononi mwangu nikawa mbishi
sana sikuwa nawaamini hata kidogo. Niliamini kabisa kwa
jinsi sura yangu ilivyokwanguka kwanguka hakuna ambaye
angeweza kunijua.
Kipigo kikazidi wakinisihi niachie faili na hapo nikamkumbuka
mtu wa kunisaidia. Lakini kipigo kikaniweka gizani, huku faili
likinitoka mkononi.
Umuhimu wa faili lile ukanipa nguvu tena, nikazivuta pumzi
zangu ndani na nilipotoa nje niliuita msaada!!
“Mama laooooo!!” nikaita kwa nguvu zote nikiuona mgongo
wake.
Sauti yangu niliyoipaza kwa nguvu zote, labda nguvu za
mwisho kabisa za kunikomboa ilimfikia.
Jojina akageuka ghafla! Macho yetu yakagongana na hapo
nikaanguka chini kinywa changu kikiyauma majani machache
yaliyokuwa katika ardhi ile huku macho yangu yakimtazama
mwanamama yule akinijia kwa kasi ya ajabu. Jojina alikuwa
mwepesi sana, akatimua mbio na kunifikia pale nilipokuwa
akawasukuma askari wale huku na huko.
Wakamtisha na bunduki zao lakini hakutishika, hakuzitazama
zile bunduki bali alichokitazama ni mimi, mimi pekee!!
“Mwacheni mwachee!!” alikaripia huku akitapatapa, askari
wakastaajabu sana wakabaki wameduwaa wasijue la
kufanya.
Wakati wakiendelea kupigwa na bumbuwazi, macho yangu
yakaona kiatu ninachokifahamu, kiatu ambacho hakikuwa
kigeni hata kidogo machoni mwangu!!
Nikajitutumua na kutazama ni kiatu chake ama nilikuwa
nimemfananisha!!
Huku nikiyasikia maumivu makali nilifanikiwa kugonganisha
macho yangu na mtu aliyekuwa amevaa kiatu hicho.
Naam!! Hakuwa mwingine, alikuwa ni yule bosi aliyenisalitiu
na baada ya kashkash mtoto wake akaamua kuungana nami
lakini hakudumu sana akatoweka kimaajabu.
Mzee Matata alikuwa amesimama mbele yangu.
Hakika alikuwa amekongoroka kama Jojina alivyonieleza kwa
njia ya simu, tukatazamana akawa anaona haya!
Nikamsalimia kwa shida. “Shkamoo bosi.” Akanijibu kiaibu
aibu. Wakati huo Jojina alikuwa akiwaeleza jambo askari
ambao walikuwa wananishushia kipigo.
Huduma ya kwanza waliokuja na polisi wakafika pale
nilipokuwa wakitaka kunichukua, nikawasihi wangoje kidogo
nimalize kazi. Maana huo haukuwa muda muafaka wqa
kutulia kitandani nikipata huduma.
Wahudumu walilazimika kunielewa hasahasa baada ya
kuwaeleza kuwa eneo lile si salama sana. Kuna jambo lazima
liwekwe sawa. Nikaeleweka!!
Na hapo nikasimama tete japo nikiwa nayumbayumba,
wakaniwekea dawa mguuni nilipokuwa natokwa damu.
Nikawauliza akina Jojina nini kinaendelea hapo.
Wakadai kuwa mlango ule haufunguki hata kwa kuvunjwa na
inaonekana ni miaka mingi tangu ufunguliwe hivyo kuna
uwezekano mkubwa kuwa hapana lolote hapo.
Nikatabasamu kidogo na kisha nikawaeleza kuwa ule mlango
unafunguka tena mara kwa mara tu! Na iwapo wanadhani
hakuna lolote linalofanyika pale wanakosea sana.
Wakati huo faili lilikuwa limerejeshwa mikononi mwangu,
wale askari wasijue kuna nini ndani ya nyaraka ile muhimu!!
“Sam, hapana si kweli mpenzi wangu hakuna haufunguki
maana kila jitihada imefanyika huenda ulikuwa unaota siku
hiyo!!” alinijibu Jojina.
Tukiwa katika maongezi, akatokea ofisa wa polisi kanda ya
Dar es salaam ambaye aliongozana na msafara huo,
nilimuuliza Jojina kwa kunong’ona iwapo anamuamini huyo
ofisa, akadai wanamuamini sana. Na hapo akanieleza kuwa
baada ya mambo kuwaendea mlama na mzee Matata
kufukuzwa kazi basi huyu ndiye alikuwa kimbilio la mwisho na
ni huyu aliyewawezesha kufika Iringa na kama hiyo haitoshi
aliwawezesha kuwakamata baadhi ya wahusika ambao
waliwatia mashaka. Hawa walikuwa ni wale wanaume wawili
ambao nami niliwahi kuwaona hapo kabla.
“Sam, kama hiki kilichotuleta huku hakipo basi utawajibika.”
Alinikaripia yule bwana, nikayatazama macho yake na kuona
hatia ikimtawala.
Walewale!! Nilijisemea.
Nikapiga hatua mbili mbele na kufanikiwa kuwaona wale watu
wawili waliomkamata Shanta siku kadhaa nyuma, wote
walikuwa wameunganishwa mikono yao kwa pingu!! Na askari
wababe walikuwa wamewazunguka na bunduki zao.
“Sam kama hauna uhakika, tusifike mbali na mambo haya!!”
Jojina akanieleza wakati najongea taratibu huku umati
ukisubiri kujua kuna nini hapo.
“Jojina, si wewe uliyenisihi nisiwe nakata tamaa, si wewe!!
Ama umekuwa pamoja nao.” Nikamkaripia. Akajirudi.
Nikaufikia ule mlango wa siri. Nikazuga kuuvuta kwa nguvu.
“Tumetumia nguvu nyingi zaidi ya hiyo uliyojaribu
kutumia!!” alinipa angalizo askari mmoja, huku akionekana
kama anayekejeli!!
“Na nd’o maana haukufunguka maana mlitumia nguvu bila
akili!!” nikawajibu kimoyomoyo.
Nikawatazama wale waliopigwa pingu na wao walikuwa
wakicheka kwa dharau. Bila shaka waliamini kuwa sitaweza
kufanya lolote lile, na waliamini kuwa siri ambayo
hakuitambua Masawe basin a mimi ni mbumbumbu vilevile.
Nikajipekua mifukoni na kutoka na funguo! Kabla ya
kufungua nikawaonyesha wale wanaharamu waliobadili
historia ya maisha yangu kuwa mbaya nay a mashaka.
“Hukumu yenu imewadia!!” nikawaambia kwa lugha ya
kiingereza.
Macho yakawatoka pima!
Sikuwajali, nikaingiza ule funguo na kuufungua mlango!!
Kila mtu akaduwaa!! Kama nilivyoingia awali bado palikuwa
na mwanga!!
Wale askari waliokuwa wameduwaa wakaamrishwa kuingia
ndani na mbwa wao, mbwa wa kwanza tu alipoingia ndani ya
sekunde kadhaa yakasikika mayowe.
“Angalia asijekuwa yeye…tafadhali..”
“Hatujaziruhusu kuuma… usijali.” Wakanieleza.
Yule ofisa niliyemuhisi kuwa ana hatia ina mkabili
akanifuata na kunivuta kando, alibaki kutikisa kichwa
asiseme neno na kisha akasema.
“Jeshi letu linahitaji roho za paka kama wewe. Kuanzia
ulipokuwa mwandishi hadi harakati hizi nakupa heshima
yako!!”
Nikajikuta natabasamu! Aliyeniona wa nini sasa
ananithamini!!!
Zile hekaheka zikanichangamsha mwili, nikayasahau maumivu
na mimi nikaingia katika mtafutano huu wa aina yake.
*****
MTU wa kwanza kutolewa mle ndani alikuwa ni swahiba wangu
Masawe, alikuwa amejikojolea tayari huku akiwa haelewi
kama analia ama anajaribu kulia. Askari walikuwa
wanamgombania huyu akivuta huku huyu anavuta kule
ilimradi kumtia wazimu Masawe!!
“Jamani mi sijui kitu mnanionea bure asee” kwa lafudhi ya
kichaga Masawe alilalamika. Nilitamani kucheka lakini
haikuwepo sababu ya kunifanya nicheke mambo yalikuwa bado
sana.
Masawe akarushwa katika karandinga na kupigwa pingu!!
Nikamfuata yule afsa ambaye sasa alikuwa rafiki
nikamweleza juu ya Masawe nikamsihi kuwa simfundishi kazi
lakini yule bwana hajui lolote na ametumiwa tu! Akanielewa
na kwenda kusema naye.
Baada ya nusu saa akanieleza alichosema Masawe. Ni kwamba
alipigiwa tu simu ya ghafla na kusisitizwa achukue funguo
mahali na kufungua kile kitasa na kuingia ndani kisha afunge
kabisa. Masawe akadai kuwa ilikuwa mara yake ya kwanza
kuingia na kukijua chumba hicho.
Nikamweleza afisa pia juu ya Masawe. Akaahidi kumsaidia!!
Mzee Matata alikuwa mstari wa mbele kuhangaika huku na
kule, mimi walinisihi nipumzike lakini niliamini bila nguvu
yangu wasingefanikisha lolote, nikaamua kuungana nao.
Vioo vikavunjwa pale pasipoweza kufunguka, watoto zaidi ya
themanini wakatoka wakiwa uchi. Hii ilistaajabisha sana,
hakuna aliyejua maana ya watoto hawa kuhifadhiwa katika
maficho ya namna ile.
Vyumba vyote vikafunguliwa, wakatoka watu wazima wakiwa
hoi kwa vipigo, wengine walikuwa maiti tayari.
Shanta alitoka akiwa hai!! Kumbe naye walimuingiza humo?
Nilistaajabu!!
Hatimaye akatoka yule mwanamke nimpendaye kupita wote
Mama Eva, alikuwa na majeraha makubwa sana mwilini
mwake, macho yake yalikuwa wazi lakini ni kama hakuwa
anaona lolote mbele yake. Nilimuita lakini hakuitika, nguo
zake zililowa damu na uso wake ulikuwa umevimba
hovyohovyo!!
Niliuma meno yangu kwa uchungu mkubwa, nikajenga hasira
maradufu kwa yeyote yule ambaye amehusika na mpango huu
hadi kumuingiza mke wangu katika mateso asiyohusiana nayo
hata kidogo. Nilitamani kufuata msafara wa wauguzi
waliombeba mke wangu, lakini nikajionya kuwa uwepo wangu
hautamsaidioa lolote lile, nikaamua kuwaachia jukumu lile
wanaohusika.
Nikiwa nataka kurejea shimo mara macho yangu yakawa
kama yananidanganya, ama la yalikuwa yanasema ukweli.
Nikayapikicha vyema, huku miguu ikigoma kupiga walau hatua
moja mbele. Nikataka kuita lakini koo nalo lilikuwa
limekauka.
Macho yangu yalikuwa yanatazamana na kiumbe cha ajabu
sana, kiumbe ambacho labda ni mimi mwenyewe kiliniogofyua
maana waliokibeba hawakuwa na hofu hata kidogo, kasoro
mimi t undo mapigo ya moyo yalikuwa yakiongeza kasi yake.
Nilikuwa natazamana na mzimu wa ajabu sana!!!
Mzimu ulioniingiza katika maswaibu haya, mzimu uliotoweka
kishja ukaonekana, ukatoweka tena na sasa nauona tena
mzimu wa Anti Ezekiel wa Temeke!!
Nikiwa napitiwa na mambo lukuki kichwani mara mzimu ule
ukajitutumua na kuyafumbua macho yake wakati huo ukiwa
katika machela ya kubebea wagonjwa!!
Mzimu ukatabasamu. Maajabu!! Si alikufa na akazikwa huyu,
na niliyaona maiti yake kitandani…. Sio Ezekiel huyu?
Wakati najiuliza hayo, Anti Ezekiel alinyanyua mkono wake
na kunifanyia ishara ya dole gumba. Bado alikuwa
anatabasamu
Ezekiel hakufa?
Sasa ile maiti ndani ya chumba chake alikuwa nani yule?
Au ushirikina? Nilijiuliza wakati huo Ezekiel akizidi
kutokomea katika machela aliyokuwa amepakizwa!!
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE
Nikiwa nataka kurejea shimo mara macho yangu yakawa
kama yananidanganya, ama la yalikuwa yanasema ukweli.
Nikayapikicha vyema, huku miguu ikigoma kupiga walau hatua
moja mbele. Nikataka kuita lakini koo nalo lilikuwa
limekauka.
Macho yangu yalikuwa yanatazamana na kiumbe cha ajabu
sana, kiumbe ambacho labda ni mimi mwenyewe kiliniogofyua
maana waliokibeba hawakuwa na hofu hata kidogo, kasoro
mimi t undo mapigo ya moyo yalikuwa yakiongeza kasi yake.
Nilikuwa natazamana na mzimu wa ajabu sana!!!
Mzimu ulioniingiza katika maswaibu haya, mzimu uliotoweka
kishja ukaonekana, ukatoweka tena na sasa nauona tena
mzimu wa Anti Ezekiel wa Temeke!!
Nikiwa napitiwa na mambo lukuki kichwani mara mzimu ule
ukajitutumua na kuyafumbua macho yake wakati huo ukiwa
katika machela ya kubebea wagonjwa!!
Mzimu ukatabasamu. Maajabu!! Si alikufa na akazikwa huyu,
na niliyaona maiti yake kitandani…. Sio Ezekiel huyu?
Wakati najiuliza hayo, Anti Ezekiel alinyanyua mkono wake
na kunifanyia ishara ya dole gumba. Bado alikuwa
anatabasamu
Ezekiel hakufa?
Sasa ile maiti ndani ya chumba chake alikuwa nani yule?
Au ushirikina? Nilijiuliza wakati huo Ezekiel akizidi
kutokomea katika machela aliyokuwa amepakizwa!!
Wakati nikitingwa na fikra juu ya walakini wa huyu
mwanadamu wa kuitwa Ezekiel, kufa, kuoza na kufufuka na
sasa namuona tena akiwa hai. Ghafla nilivamiwa na wazo na
hili lilikuja baada ya macho yangu kuona kitu ambacho
nilikiona hapo kabla. Niliona mchoro ambao nimewahi kuuona
na ukanikumbusha mengi.
Mchoro wa mtoto akiwa anatabasamu.
Mchoro huu ukanikumbusha mambo mawili mazito.
Kwanza ni huyu Ezekiel… makablasha niliyoyatoa nyumbani
kwake yaliambatana na picha iliyomuyonyesha mtoto yule, na
baadaye nikaikuta picha hiyo katika anuani yangu ya barua
pepe ikiwa imetumwa na mtu ambaye sasa alizivamia fikra
zangu maradufu!!
Anitha!!
Binti huyu alikuwa hajaonekana bado, mapigo ya moyo
yaliongeza kasi yake. Sikutaka akili yangu ikubaliane na
ukweli kuwa Anitha aligundulika kuwa aliwasiliana na mimi
hivyo akauwawa kinyama kama baadhi ya wanadamu
tuliowakuta wakiwa wafu bila hatua zozote kuchukuliwa.
Nikaamua kumsahau Ezekiel wa maajabu na nikajikita katika
shimo lile tena kwa lengo la kumsaka Anitha. Msichana wa
muhimu kabisa kabita maisha yangu.
Nilizikuta vurugu zikiendelea hapa na pale katika jitihada za
ukombozi kutoka Michigani, chimbo ambalo hadi wakati huo
sikuwa najua linahusika na nini.
Sikuwa katika tahadhari juu ya kitu nilichokuwa nimepakata
katika mikono yangu. Jambo ambalo nililitazama kwa wakati
huo ni jibu la Anitha yu hai ama la!!
Nilitapatapa huku na kule nikipishana na mizoga, nilijivika
ujasiri na kuitazama vyema. Haikuwa ikifanania na sura ya
Anitha. Hili jambo lilizidi kunipa matumaini kuwa huenda
nitamkuta Anitha akiwa hai nimwonyeshe kuwa nilimpigania.
Nikiwa katika kuangaza macho huku na kule mara nilihisi
kitu cha baridi kabisa kikipenya katika kiuno changu.
Nikageuka upesi kutazama kulikoni.
“Sam, it takes a second to kill!! (Sam inachukua sekunde
moja tu kuua)” sauti ilitoka kwa mwanaume aliyevalia
mavazi rasmi ya jeshi la polisi. Sikuweza kuiona sura yake
kwani nilivyojaribu kufanya hivyo alinilazimisha nitazame
mbele kana kwamba hakuna kitu kilichotokea.
“Kwa heshima zote ili usije kunichafua na damu yako chafu
naomba kwa urafiki mkubwa liachie hilo faili lidondoke chini
kisha utafuata maelekezo yangu.” Sauti ile iliendelea
kunong’ona na haikuwa nha utani bali ilikuwa ni sauti
ambayo inaashiria mauti tu.
Watu walipita huku na kule wakinipita, nilitamani sana
ajitokeze mmoja wa kugundua kuwa nipo katika tatizo lakini
ndo kwanza kila mmoja alikuwa akijishughulisha na mambo
yake hasahasa katika zoezi zima la kujikomboa.
Sikutaka kuuweka uhai wangu rehani katika dakika hizo
ambazo kila mmoja alikuwa katika kuutetea uhai wake, roho
ikaniuma sana kuchelewa kusoma kila mstari katika faili lile.
Sasa lilikuwa linahitajika!!!
“Weka faili chini Sam ama la nakusambaratisha kiuno chako
na faili unaliachia.” Sauti ikazidi kunikanya.
Akili iligoma kabisa kunipatia njia mbadala, na hatimaye
nikalegeza mkono wangu ili faili liweze kwenda chini.
La haula!! Hawa jamaa walikuwa makini katika kila jambo
walilokuwa wanafanya. Wakati nawaza kuwa faili likianguka
chini yule bwana akijaribu kuliokota nimvamie na kumrusha
mbali. Haikuwa kitoto kama vile, wakati faili linatoka katika
mkono wangu ni kama alikuwa ameandaliwa mtu mwingine
kwa ajili ya kulichukua lisipate bughudha yoyote.
Kama vile kipanga akiwanasa vifaranga vya kuku, ndivyo lile
faili lilikwapuliwa.
Wakati naduwaa sauti haitoki na sijui cha kufanya faili
likitokomea, bunduki haikuwa tena katika kiuno changu.
Fahamu zinanirudia na kupiga kelele, tayari nilikuwa
nimechelewa. Nikakabiliwa na maaskari waliokuwa na sare
wakaniuliza kulikoni. Jasho lilikuwa linawatoka kwa sababu
ya shughuli pevu ya kufanya ukombozi sasa nawaeleza kuwa
mwenzao amenitishia bunduki na kulinyofoa faili kutoka
katika mikono yangu!!
Mwenzao? Kila mmoja aliduwaa nilipowaeleza kuwa kuna
mmoja wao amenitenda vile na ametokomea pasi nami kujua
ni wapi ameelekea. Walitazamana wao kwa wao na kisha kwa
pamoja wakakiri kuwa ninawafitini na hakuna kitu kama
hicho kimetokea.
Hakika ilikuwa ngumu kuamini kuwa limenitokea tukio hilo,
nani angeamini sasa zaidi yangu mimi niliyeetendwa?
Msako wa faili ukaanza tena!!
Kila kona ikatazamwa nikawaelezea rangi na ukubwa wa lile
faili, msako ukapitishwa kwa makini sana lakini hakuna
kilichoonekana!!
Mungu wangu!! Siri imepotea ikiwa mikononi mwangu, zaidi
ya kichwa cha habari nilichokisoma kimawengewenge sikuwa
najua lolote lile ndani ya faili lile.
Faili kupotea na Anitha kutoonekana nikajiona sina lolote
nililofanya katika harakati hizo!!
Mzee Matata naye alikuwa amekata tamaa.
Kwa kupoteza faili na kutompata Anitha sikutaka kupoteza
jingine.
Anti Ezekiel!!!
Huyu ndiye aliyeniletea matatizo yote haya, ni huyu wa
kunitoa katika matatizo hay ail hali yupo hai ni lazima
anieleze kwa kina juu ya tamthilia hii ya maajabu!!
Hasira zikanipanda maradufu na nikaamua kuzi8malizia kwa
Anti Ezekiel wa Temeke.
Nikatoka katika kundi la watu na kumtafuta Ezekiel, popote
pale alipo.
Nikamuona nesi ambaye awali nilimuona akimuhudumia
Ezekiel. Nikamvaa
“Ezekiel yupo wapi?” hili lilikuwa swali la kwanza,
akababaika kidogo, nikamshangaa ni kwanini ababaike.
“Ezekiel nd’o nani?” akaniuliza, nikamweleza nilichojua
akanijibu kuwa kuna askari watatu walikuwa wanamuhoji.
Shenzi type!! Askari wanamuhoji ili iweje na ni askari gani
huyo awezaye kufanya jambo kama hilo wakati hata
ukombozi haujakamilika. Nikafura kwa hasira na kuelekea
mahali ambapo alinielekeza yule kijana.
“Lakini wamesema asiende mtu yeyote huko nyuma….”
Alinikatisha kwa kauli ile iliyojaa uoga.
Shit!! Askari gani hawa wa kuzuia watu muda huu, kwanza
msafara huu ulikuwa chini ya yule ofisa wa ngazi za juu za
mkoa. Yeye alikuwa mbali, sasa ni kwa namna gani
anajitokeza mtu mwingine wa kutoa amri hizo??
Maswali haya yakaipandisha hasira yangu maradufu!!
Nikapenya huku na huko, nikafanikiwa kuiona machela
iliyokuwa imembema Ezekiel ikiwa imezungukwa na watu
watatu. Walikuwa wamevaa sare za jeshi la polisi la
Tanzania!!!
Nikawatazama kwa mbali sana hadi akili yangu ilivyokuja
kushtuka kuwa Ezekiel alikuwa ameniona.
Akauchukua mkono wake nami nikaufuata kwa makini, na
hapo akajishika kiunoni.
Sikujua anamaanisha kitu gani. Lakini hakuutoa na alitaka
nielewe kitu.
Kiuno chake kina tofauti gani sasa na viuno vingine??
Nilijiuliza!!!
Na hapo nikapata wazo la kutazama viuno vingine!!
Viuno vya askari wale!!
Asalalee!!! Mikanda iliyokuwa katika viuno vyao haikuwa
mikanda yenye bendera ya taifa!!
Ezekiel anamaanisha kuwa wale ni polisi feki!!!
Nikarudi kinyumenyume, nikajipa ujasiri zaidi nisitetemeke,
huku nikijua maana ya askari wale kunishangaa nilipodai
wenzao wamenipokonya faili.
Kumbe kuna kenge katika msafara wa mamba!!
Nilipotokomea katika eneo lile, moja kwa moja nikamnkabili
yule ofisa wa ngazi za ju, kwanza nikamtazama kiunoni.
Alikuwa na mkanda halali kabisa wenye utepe uundao rangi
za bendera ya taifa.
Njikamvuta kando na kumweleza juu ya hatari tuliyonayo ya
kuzungukwa na maadui!!
Maadui wanaojifanya nao ni kati yetu.
Ofisa alitaharuki baada ya kupokea taarifa hii, na hapo
nikamuhakikishia kuwa hata aliyenipokonya faili atakuwa
mmoja kati yao.
Macho yake makali yakapepesa huku na kule, na mara
akawachukua vijana wake wawili ambao walikuwa wamevaa
kiraia. Akazungumza nao kisha nikaongozana nao kwenda
kushuhudia yale ambayo huwa nayaona katika sinema.
Hawakuwa na msalia mtume!!
Askari feki watatu walivunja miguu ndani ya sekunde
kadhaa!! Bomba la sindano likamtoka mmoja wao huku akipiga
mayowe!!
Nikabaki kuwa shuhuda wa mpambano huu ambao uliwageukia
maaskari halali baada ya kufanya kosa la kizembe la kudhani
kuwa wale waasi wapo watatu tu!!
Wakamwinamia Ezekiel na kuanza kumuhoji kwa sauti zao za
pupa na maswali yasiyokuwa na mbele wala nyuma.
Kiwiliwili kingine katika mavazi ya kiaskari kikavamia na
kufanya mzunguko wa aina yake, askari wawili waklaanza
kugumia chini kwa chini.
Na hatimaye ana kwa ana na askari mmoja!!
Askari feki akarusha teke kali likakumbana na mbavu za yule
askari halali, akatokwa na mguno wa maumivu huku akiyumba
chini!!
Nikajiona ----- ninayetazama hali hii kama filamu. Lakini ni
kitu gani ningeweza kufanya na mwili wangu dhaifu dhidi ya
skari wale feki ambao bila shaka wamehitimu mnafunzo yote?
Liwalo na liwe!!
Nikatoka mbio mbio pasipo na tahadhari.
Nikaokota jiwe kubwa. Huku nikitokwa na kelele nyingi
nikaenda kumvamia yule bwana.
Teke zito likatua katika paji la uso wangu, sijui hata kama
nilirusha lile jiwe kwa urefu wa mita moja, lakini nilihisi
kama nimetua katika mguu wangu!! Maumivu yake yalikuwa
ya kawaida sana, kulinganisha na maumivu katika paji la
uso!!
Nilijikuta naona nyotanyota, nuru ilikuwa inatoweka na
kurejea!!!
Kwa mbali niliweza kumwona askari feki akimnyonga askari
halali wa jeshi letu. Na wakati akimnyonga alikuwa
akinitazama usoni!!
Bila shaka azilikuwa salamu kuwa baada ya yule ni mimi
ninayefuata!!
Nilijaribu kupiga kelele lakini sijui kama kelele zile zilitoka.
Naam!! Ni kama nilivyowaza. Alipomaliza nikamuona
akijongea kunifuata.
Akanifikia!! Akanitazama kwa jicho bay asana ambalo
lilitangaza chuki tele!! Mikono yake ilikuwa inatetemeka.
Nakufa!! Nilipitiwa na wazo hilo huku nikijaribu kufurukuta
huku na kule bila kujua kama ni kweli nafurukuta ama
nawaza tu kuwa nafurukuta!!
Nilihamisha macho yangu kutazama kama kuna msaada
kutokana kona yoyote!!!
Na huku nikakutana na askari mwingine feki akinijia na
bunduki mkononi!!
Nimekwisha!!! Niliapa……
Na baada ya kiapo kweli nikajikuta nakuwa kama mpira wa
kona.
Nilikuywa nagombaniwa!!!
Nilivutwa huku na kule. Sasa sikuweza kumtazama yeyote,
kila kiungo katika mwili wangu kilikuwa kinauma, huyu
akivuta mkono huyu anavuta mguu, huyu ananipiga teke
mbavuni, huyu anavuta kichwa changu!!
Kisha mlio mkali sana ukasikika!!! Mamivu yakapenya
barabara, maumivu makali kupita yote niliyowahi kuyasikia.
Sikuweza kufumbua macho!!
Masikio yakausikia mlio mwingine mkali zaidi, na hapo sikujua
nini kinaendelea tewna duniani!!!
 
Mzaramo umetisha ndugu, yaani wewe ni moto tena sijui mwiba ambao unachoma kwenye maaumivu(yaani pale watu wanapokua na hamu ndo wewe una dondosha haja yao), uko vizuri sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom