Ripoti ya Uchunguzi vifo vya watoto Tabora

............Kuhani tatizo lako ni kuwa........you don't think!..........unachukua kitu kizima kizima ....na kumeza..........sorry....im not here to baby sit any..........kwi kwi kwi kwi..................kusema kwangu "msanifu yeyote qualified angeweza kuwa consulted"..........haimaanishi taratibu husika zirukwe......nilichofanya ni kuongezea pale nilipoishia kuwa.........huwezi kukurupuka na ku-consult any qualified person........mambo kama hayo hayatakiwi kwenda kienyeji enyeji......and thats my point.........sasa kigumu kwako kuelewa ni kipi.........

...don't just jump onto my "nuktas".........na kumeza kitu kizima kizima......kwi kwi kwi kwi

Mkuu Ogah,

Respect mkuu, hapa tupo ukurasa mmoja mkuu, saafi sana.
 
lakini ES imekuwaje tena umeamua kuivunja ile ceasefire?

if thats the case basi bora tuambiane maana jamaa wananiuliza imekuwaje tena na FieldMarshall?
 
lakini ES imekuwaje tena umeamua kuivunja ile ceasefire?

if thats the case basi bora tuambiane maana jamaa wananiuliza imekuwaje tena na FieldMarshall?

Mkuu GT,

Heshima mbele, nilipokuwa ninalilia ceasefire, nilisema ninakubaliana na wazo kwamba ni muhimu tukatoa nafasi ili uchunguzi ufanyike na tusikie matokeo kwanza,

Kamati ya awali ya mkoa imefanya uchunguzi na imetoa matokeo ambayo ninaamini kuwa sio the final say ya hili tukio, lakini bado ninaheshimu matokeo waliyoyatoa, sasa kujitokeza kwangu hapa ilikuwa ni ku-aknowledge matokeo ya uchunguzi wa kamati ya mkoa, sidhani kama kwa kufanya hivyo ninavunja ceasefire tuliyokubaliana,

Sasa hao jamaa waliokuuliza kuhusu mimi sidhani kama wana nia njema, halafu ninapata ujumbe mwingi sana kuhusu watu, kila ninapoweka maoni yangu on any ishu ninaambiwa kuna watu na jamaa wanalalamikia watu flani humu huko pembeni kuhusu michango yangu, sasa na wewe mkuu kuna jamaa wamekuuliza huko pembeni,

Anyways, mimi ni mwananchi kama wengine wote na Tanzania ni nchi yangu, and I am proud to be a Tanzanian, msimamo wangu siku zote ni ule ule amani mbele na kuheshimiana, kutoa maoni hapa JF ni haki yangu kama mwananchi, hao jamaa wanaolalamika huko pembeni ni vyema wangeni-face mimi mwenyewe iwapo wana maswali ninaweza kuwasaidia kuyajibu,

Otherwise ilikuwa ni muhimu kwangu kutoa maoni kuhusiana na matokeo ya uchunguzi wa mkoa bila kumuogopa mtu yoyote hapa, kwa sababu ni haki yangu kama mwananchi.

Ahsante Mkuu Kwa Kunielewa!, na Amani mbele bro!
 
Wakuu Ogah na Kuhani.

Naamini wote mko sahihi. Hakuna sheria inayomlazimisha mshitiri kumtumia msanifu wake original kwa ajili ya mabadiliko yoyote atakayotaka kufanya kwenye jengo lake. Anachotakiwa kufanya ni kutafuta msanifu aliyekuwa qualified ambayo kwa Tanzania ni aliyekuwa registered na AQRB na mwenye leseni hai. Huyu msanifu mpya kama kweli ni competent ataweza kuwasiliana na msanifu original kupata maoni yake hasa kama mabadiliko yanayotarajiwa ni makubwa. Hii hawajibiki kufanya maana kama Ogah alivyoeleza, msanifu original alitakiwa kukabidhi kumbukumbu zote zinazohusiana na jengo (working drawings, michoro na hesabu za wahandisi wote, michoro ya mabadiliko yote wakati wa ujenzi, minutes za vikao vyote vya usimamizi wa jengo n.k.) kwa mshitiri mara mradi unapoisha. Hizi zinatosha kutoa mwongozo kwa msanifu majengo yeyote anayeijua kazi yake. Kama tena alivyosema, Ogah, kuna design liability kwa msanifu original kwa hiyo katika kukwepa kumpa loop-hole hapo yatakapotokea matatizo baadae ( kwa kudai yamesababishwa na msanifu mpya), mshitiri anaweza kuamua kumpa tena kazi za mabadiliko katika jengo. Hawajibiki lakini ni kuwa prudent hasa kama aliridhika na kazi ya msanifu original.

Kuhani yuko sahihi kuwa kwa kuingiza kipengele hiki cha kudai msanifu original ilibidi ashirikishwe kunaingiza dosari katika ripoti ya tume. Bila shaka msanifu original alikuwemo kwenye tume na angependa kujitengenezea mazingira ya kuendelea kupata ulaji kutokana na miradi yake yote ya awali. Hapa aliteleza na tume ilionyesha udhaifu wake kwa ku-entertain hilo. Ni mapungufu lakini si lazima yafanye ripoti nzima iwe batili.

Haya ni mawazo yangu Fundi Mchundo. Nawaachia waliopasua vitabu zaidi yangu, yaani, wahandisi na wasanifu majengo, walete michango yao.

Amandla..........
 
Je Ripoti ilisema nini kuhusu tukio kama hilo lililotokea huko nyuma na ripoti yake kutokuwasilishwa kwake? Je ilisema nini kuhusu Polisi kama walijua mahali hapo panauzwa bia kwa watoto wadogo na ya kuwa tukio kama hilo liliwahi kutokea? Je Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Polisi hawana chochote cha kuwajibika?
 
Je Ripoti ilisema nini kuhusu tukio kama hilo lililotokea huko nyuma na ripoti yake kutokuwasilishwa kwake? Je ilisema nini kuhusu Polisi kama walijua mahali hapo panauzwa bia kwa watoto wadogo na ya kuwa tukio kama hilo liliwahi kutokea? Je Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Polisi hawana chochote cha kuwajibika?

Morally, ndio. Lakini sidhani kama sheria inawabana. Hili la pombe kwa juveniles na watoto wadogo ni aibu kwa jamii nzima. Jamii tumekuwa wavumilivu mno kwenye suala hilo. Si adimu kuona mzazi akimwonjesha mtoto wake pombe. Si adimu kuona watoto wakighida pombe kwenye sherehe za harusi mbele za wazazi wao na watu wazima wengine. Mara ngapi tunawanunulia pombe under-age bar maids katika hizo sehemu za burudani? Kwenye hili, wote tunastahili kuwajibika.
 
Je Ripoti ilisema nini kuhusu tukio kama hilo lililotokea huko nyuma na ripoti yake kutokuwasilishwa kwake? Je ilisema nini kuhusu Polisi kama walijua mahali hapo panauzwa bia kwa watoto wadogo na ya kuwa tukio kama hilo liliwahi kutokea? Je Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Polisi hawana chochote cha kuwajibika?

jana niliipata hard copy ya summary ya report. kwa kuwa ilikuwa siku ya mapumziko sikuweza kuifanyia lolote. lakini sasa naibadilisha kuwa katika soft copy na nitaiweka hapa baada ya muda ili kila mmoja aone kilichomo
 
Hivi Tanzania kuna legal age ya kunywa pombe? Sijawahi kuona mtu akiulizwa kitambulisho au ushahidi wowote wa umri kwenye mabaa! Na tukizungumzia pombe, jee tunaunganisha na pombe za kienyeji? Maana kuna makabila mengine hawaoni ubaya kumwonjesha mtoto mchanga ulabu ili apate usingizi. Kama sheria hiyo haipo, watawashitaki vipi wahusika kwa kuuza pombe kwa watoto? Kama ipo, ni mahali gani ambapo inatumika?
 
Hivi Tanzania kuna legal age ya kunywa pombe? Maana kuna makabila mengine hawaoni ubaya kumwonjesha mtoto mchanga ulabu ili apate usingizi.

Wahehe hao Mkuu ndio wanatumia ulanzi kuwabembeleza watoto shambani ili wazazi wapige mzigo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!.
Sina hakika kuhusu sheria lakini nadhani sheria za vileo zinaelezea umri wa mtu kunywa pombe
 
Wahehe hao Mkuu ndio wanatumia ulanzi kuwabembeleza watoto shambani ili wazazi wapige mzigo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!.
Sina hakika kuhusu sheria lakini nadhani sheria za vileo zinaelezea umri wa mtu kunywa pombe

Je inakataza kuuziwa pombe mtu wa chini ya umri fulani kama kwa wenzetu? Sidhani, maana ni mara nyingi tu tunawatuma watoto sigereti na pombe kwenye groseri! Wengine hata tunawafundisha namna ya kutuwashia sigereti! Huu mzigo ni wetu wote!
 
Je inakataza kuuziwa pombe mtu wa chini ya umri fulani kama kwa wenzetu? Sidhani, maana ni mara nyingi tu tunawatuma watoto sigereti na pombe kwenye groseri! Wengine hata tunawafundisha namna ya kutuwashia sigereti! Huu mzigo ni wetu wote!

Nadhani kuna sheria. Ipo, lakini haionekani? Kwenye mabango yanayotangaza tusker, kilimanjaro na serengeti, nimeona imeandikwa: Ni marufuku kuuzwa kwa mtu aliye chini ya miaka 18.

Sina hakika kama hiyo ni sheria/sera ya kitaifa, au watengeneza ulabu wamejitungia.
 
Wakuu Ogah na Kuhani.

.........Kuhani yuko sahihi kuwa kwa kuingiza kipengele hiki cha kudai msanifu original ilibidi ashirikishwe kunaingiza dosari katika ripoti ya tume. Bila shaka msanifu original alikuwemo kwenye tume na angependa kujitengenezea mazingira ya kuendelea kupata ulaji kutokana na miradi yake yote ya awali. Hapa aliteleza na tume ilionyesha udhaifu wake kwa ku-entertain hilo. Ni mapungufu lakini si lazima yafanye ripoti nzima iwe batili...............


.........Mawazo yako mazuri.........naomba nikuulize swali....hivi design liability inaishia kipindi gani?...........
 
Wajamani,
Mie sipo Tabora mjini. Ila kwa kutembea kwangu haraka haraka pale Tabora mjini niligundua kuwa kazi nyingi za majengo ya pale ziko chini ya Mzee mchoraji na mzoefu wa siku nyingi aitwaye John Mlundwa (kaka yake Emanuel Mlundwa Boxer). Huyu Mzee namfahamu personal na kaanza kuwa na timu yake siku nyingi sana Dar. Nafikiri kwa sasa kaamua kurudi nyumbani maana ni mtu wa Tabora. Sidhani kama kuna Achitect mkali kama huyu Tabora. Hivyo ukichukulia na uzoefu wake, nafikiri unaona kuwa kazi nyingi zinaangukia mikononi mwake.
Nafikiri wamesema hivi kwani aliyefanya mabadiliko na kuwa ukumbi wa mkutano ni Mlundwa. Na kama sikosei aliyechora mwanzo ni Mlundwa. Mlundwa mwenyewe yupo hai na alishasema yake yafuatayo " .....Naye Msanifu wa Majengo aliyesanifu jengo hilo ambalo linamilikiwa na la Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF), John Mlundwa, alisema kuwa kumbi hizo zilijaza watoto kupita uwezo wake na kuongeza kuwa zilijengwa kwa matumizi ya mikutano na matumizi ya ofisi na si kwa matumizi ya sherehe za watoto, kwani wanatakiwa kustarehe katika maeneo ya wazi.
Mlundwa alisema kwamba uwezo wa ukumbi huo ni kuchukua watu 150 tu, kwenye mkutano. Alisema baada ya ukumbi huo kugeuzwa matumzina kuwa wa kupiga muziki madirisha yake yalifungwa na kuwekwa viyoyozi viwili tu.
Alisema kutokana na hali ya kufurika watu kupita kiasi na viyoyozi kuzimika ghafla, hali ya kukosekana kwa hewa ilijitokeza na kuwa chanzo cha maafa hayo ...."
Sasa anachosema KUHANI hapa ni kweli tu kama ingelikuwa ni BUNGE linaandika SHERIA. Nafikiri TUME wamechukulia hili kwa tukio hili tu hasa ukiangalia historia kuwa NSSF wamekuwa wakimshirikisha Mzee huyu huko nyuma na kushindwa kufanya hivyo wakati wanataka pawe DSCO. Tusibiri tuone litakalofuata.
 
Hamna litakalofuata; siku zitapita hili nalo litasahauliwa hadi watoto wengine wafe kwenye jengo jingine, tutalia, na kusonga mbele. Katika akili zetu timamu tunakubali ripoti ya Mkuu wa Mkoa kutoka tume iliyoongozwa na Mkuu wa Polisi.

Hapa Detroit wiki hii iliypita tukiwa na msiba wa kijana wa Kitanzania kuna msiba mwingine umetokea ambapo mtoto mmoja wa shule ya msingi amepigwa risasi na kuuawa na kikundi cha watoto wengine ambao pia walijeruhi wengine. Baadaye imekuja kugundulika kuwa mmoja wa watoto wanaotuhumiwa kushiriki mauaji ya mwanafunzi huyo ni mtoto wa Afisa wa Polisi wa Detroit.

Sasa baada ya kugundua hilo, Jeshi la Polisi likatangaza kujitoa kwenye uchunguzi huo na kuliachia kikosi cha Polisi cha State of Michigan ili kuondoa mgongano wa kimaslahi. Naye mwendesha mashtaka wa Tarafa hii ya Wayne Kim Worthy (aliyemfungulia mashtaka Meya wetu miezi michache iliyopita) naye alijitangaza kujitoa kuendesha mashtaka baada ya kugundua kuwa huyo mpelelezi amewahi kuwafanyia uchunguzi kwenye kesi nyingine mbalimbali.

Ninachosema ni kuwa inakuwaje Mkuu wa Mkoa ambaye ameshuhudia tukio kama hili mahali pale pale hadi kufikia kuunda tume (isiyotoa ripoti) aweze tena kuunda tume kuchunguza watu wengine wote isipokuwa yeye na ofisi yake? It boggles my mind.
 
Ninachosema ni kuwa inakuwaje Mkuu wa Mkoa ambaye ameshuhudia tukio kama hili mahali pale pale hadi kufikia kuunda tume (isiyotoa ripoti) aweze tena kuunda tume kuchunguza watu wengine wote isipokuwa yeye na ofisi yake? It boggles my mind.

Mwana Kijiji,
Nasikia kuna BOSS mmoja aliambiwa kuwa kutokana na uzembe katika sehemu yake ya kazi aandike watu wanaotakiwa kufukuzwa kazi. Jamaa alijitahidi kutafuta KONDOO WA KUTEKETEZWA na kuwapata. Akaawandika na kumpelekea BOSS wake. Boss kuona list akasema kuna mmoja kakosekana. Jamaa akaangalia na kusema wote wapo. Boss akasema, no mmoja hayupo. Itabidi umuandike sasa hivi kwenye orodha. Jamaa akashika kalamu na kusubiri jina. Boss akamwambia JIANDIKE JINA LAKO na unipe hiyo karatasi. Jina liliandikwa na karatasi ikapokelewa na BOSS akaifanyia kazi. Kikwete asingelikuwa kama ambavyo Mungu kamjalia kuwa, tungeliona kitu kama hiki. Lakini Thank you God kwa kumpa hiyo HURUMA aliyonayo. Mwanzo alituletea Ditopile pale Tabora. Sasa tunaye huyu nani sijui. Tabora tuna neema ya kupata ma RC Viwete wa uongozi!!!!!!!!
 
.........Mawazo yako mazuri.........naomba nikuulize swali....hivi design liability inaishia kipindi gani?...........

Sijui. Sijawahi kuiona kwenye consultancy agreement yeyote. Kwa mkandarasi kuna defect liability period ambayo inategemea aina ya jengo na mahitaji ya mshitiri. Zamani tulikuwa tunasema ni miezi sita au kipindi kimoja cha mvua (kama mvua haijanyesha katika hiyo miezi sita). siku hizi tunaenda mpaka miaka miwili. Lakini hii inahusu defects ndogo ndogo ambazo zinatokana na utendaji mbaya wa mkandarasi. Hizi zinaweza kurekebishwa katika wakati huo. Lakini kama kuna major structural au technical failure, inayofanya jengo lisiweze kutumika ipasavyo, kinyume cha maagizo ya mshitiri hii sifahamu lakini naamini inadumu kwa uhai wa jengo. Kwa mfano, kama kuna conference room ghorofani iliyotakiwa kuchukuwa watu mia lakini haijawahi kuchukuwa watu hao hadi miaka kumi kupita. Ikiwa baada ya miaka kumi, mshitiri akapata mkutano wa watu mia na jengo kuanguka kutokana na uzito wao, basi wataalam wote watakuwa liable (kuanzia msanifu majengo hadi mhandisi wa structures). Hasa ikiwa walikagua na kupitisha kazi ya mkandarasi kuwa ilifanyika kama walivyomuagiza.

Hivyo ndivyo ninavyoelewa. Labda nimekosea.
 
Back
Top Bottom