Game Theory
Platinum Member
- Sep 5, 2006
- 8,545
- 835
Kuna kitu kimoja sikielewi labda wakuu mnaweza kunisaidia. Nimeipitia juu juu ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk. Mwakyembe. Naona watu wameongelea sana kutaka watu kujiuzulu, na wanaohusika kuchukuliwa hatua za kisheria.
Pia Dk. Mwakyembe amelalamika kuwa watu waliohojiwa hawakutoa ushahidi wa kutosha "officially" katika kiapo.Na wengine wametoa ushahidi nje ya kiapo.Sasa kama mtu hatoi ushahidi katika kiapo na anakuja kutoa ushahidi nje ya kiapo hapo hamna kesi ya "obstruction of justice" ili kuweza ku uphold rule of law?
Inawezekana hili ni swala dogo in the grand scheme of things na watu walifocus kumtoa Simba ndani ya nyumba kabla ya kupanga vikombe kwenye kabati, lakini inabidi tuweke standards za juu kuhusu utawala wa sheria ili kesho watu wajue kuwa ukiitwa na tume yenye mamlaka ya kisheria, inabidi utoe ushahid, utoe ushahidi wa kweli, na utoe ushahidi wote. Siyo mambo ya ma deal na ushahidi wa vichochoroni ambao unakosa nguvu.
[ame]https://www.jamiiforums.com/showthread.php?t=9687[/ame]