Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,820
- 4,572
Katika mwaka 2023/24 Serikali iliendelea kuchukua hatua za kuimarisha uzalishaji na upatikanaji wa umeme nchini ambapo hadi kufikia Machi 2024, uwezo wa mitambo ya kufua umeme iliyounganishwa katika mfumo wa Gridi ya Taifa ulifikia jumla ya megawati 2,138 ikiwa ni ongezeko la asilimia 14.2 ikilinganishwa na megawati 1,872.1 za Mei 2023. Katika kiasi hicho megawati 836.3 sawa na asilimia 39.1 ni umeme unaotokana na nguvu ya maji, megawati 1,198.8 sawa na asilimia 56.1 ni gesi asilia, megawati 92.4 sawa na asilimia 4.3 ni mafuta mazito na megawati 10.5 sawa na asilimia 0.5 ni umeme wa tungamotaka (biomass)”- Dkt. Biteko.
Ongezeko la uwezo wa uzalishaji wa umeme limetokana na kuanza kwa uzalishaji wa umeme katika Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Julius Nyerere (megawati 2,115) ambapo megawati 235 zimeanza kuzalishwa kupitia mtambo namba 9 pamoja na kukamilika kwa mradi wa kuzalisha umeme wa Rusumo ambao unachangia megawati 26.7 katika Gridi ya Taifa.
Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Machi 2024, uwezo wa mitambo ya kuzalisha umeme ambayo haijaungwa katika Gridi ya Taifa ni megawati 33.4 ambazo zinajumuisha mitambo inayomilikiwa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) yenye uwezo wa kufua megawati 28.4 na megawati 5 zitokanazo na nguvu ya jua kutoka kwa mzalishaji binafsi.
TANESCO na kununua Umeme
Wizara kupitia TANESCO inanunua umeme wa megawati 31 kati ya hizo megawati 21 kutoka Uganda kwa ajili ya Mkoa wa Kagera na megawati 10 kutoka Zambia kwa ajili ya Mkoa wa Rukwa.
PIA SOMA
- TANESCO: Umeme tunaozalisha ni mwingi mahitaji ni madogo nchi nzima, hakuna mgawo kwa sasa
- Waziri Mkuu Majaliwa: TANESCO imezalisha umeme zaidi ya mahitaji