Wanajamvi,
Naona kuna kuchanganyikiwa kwa aina fulani. Ningependekeza Mod watenganishe taarifa hizi ili watu waelewe.
1. Kuna taarifa ya kamati iliyoundwa na MCT na Jukwaa la habari(TEF). Ipo katika kiingereza na kiswahili.
2. Kuna taarifa ya 'kamati' ya Nchimbi kama ilivyoletwa katika post# 129.
Maoni yangu
Taarifa ya MCT imeeleza kwa ufasaha yale tuliyokuwa tunayajua. Tofauti ni kuwa upo mpangilio maalumu wa tukio muda na wahusika. Taarifa hiii ilizama kwa kina katika kutoa habari za nini kilitokea.
Licha ya kina cha habari taarifa ya MCT na TEF ina mapungufu katika eneo la majumuisho (conclusion)
Eneo hilo halikuwa na mkazo wa nini wanapendekeza. Ukisoma taarifa utaona wametumia neno 'cover up' kuonyesha kuwa kuna 'kulindana'. Ukisoma jedwali utaona linaonyesha majina ya wahusika waliotoa taarifa potofu ili kufanya hiyo cover up.
Nilidhani walitakiwa waende moja kwa moja kwa akina nani wawajibishwe na kwasababu zipi.
Taarifa ya kamati ya Nchimbi
Hii taarifa ni ya kupuuza sana, siamini kuwa umeandaliwa chini ya usimamizi wa jaji mstaafu Ihme.
Hii inaonyesha tatizo kubwa kwa wataalam wa mambo ya kisheria.
Tatizo linalofanana na hilo ni la Theophil Makunga. Tulitahadharisha sana hapa JF kuwa, ili jamii ya wanahabari ipate heshima ni wajibu wa Theophil kujitoa.
Kwanza kutoshiriki kamati inayofanana na ya harusi kwa vile haina meno na imeundwa kisiasa zaidi.
Tulisema hii ilikuwa mbinu ya Nchimbi kufunika kombe. Kwa bahati mbaya Theophil Makunga akaamua kuwatosa na kuitosa taaluma pengine kwa ujira kidogo. Nasema hivi kwasababu ukisoma taarifa ni ya kiwango cha chini, cha ajabu na cha kusikitisha. Kama Theophil ameshiriki vema basi tuna tatizo kubwa katika fani ya habari pia kama ilivyo ya sheria.
Ukisoma utaona kuwa taarifa hiyo ilikwenda kukusanya maoni ya watu na si uchunguzi. Sikutegemea taarifa hiyo ichukue nukuu za akina Shibuda na watu wengine mitaani tena kwa kuchagua ili iwe sehemu ya taarifa.
Taarifa inaonyesha wazi kuwa kifo cha Mwangosi kilitokana na uelewa mdogo wa kuandika habari katika maeneo ya hatari. Inapoandikwa kuwa waandishi wapewe mafunzo ni dhahiri taarifa inaonyesha tatizo kwao.
Hapo ndipo Theophil Makunga anapojikuta akiwasaliti wenzake na taaluma
Taarifa imejikita katika kutupa lawama kwa CDM. Eti mikutano ya siasa inawapunguzi watu muda wa kufanya kazi!
Inaongeza kuwa vyama vya siasa viache siasa za kibabe.
Hakuna nguvu kubwa iliyotumika
Kuwanukuu akina shibuda wa CDM kama ushahidi wa CDM kuwa chanzo cha mauaji
n.k.
Nitashangaa sana kama CDM watakaa kimya dhidi ya tuhuma wazlizotupia ili kukwepa ukweli wa mauaji ya Mwangosi.
Hakuna tulichotarajia na kama tulivyowahi kusema, Nchimbi kwanza alitakiwa aondoke ili apishe uchunguzi huru.
Tume ya Nchimbi ni ya kisiasa, haikuja na jipya, imepoteza pesa za uma na kutuletea taarifa ya kipuuzi sana.
Tutaendelea kubabaishwa hadi pale tutakaposiamama kwa pamoja na kudai haki zetu.
Kwa mara nyingine tumefanywa wendawazimu na Nchimbi, Jaji Ihema, Theophili Makunga, Chagonja, Kaumhanda, Mwema na kundi lao. Tutairejea taarifa ya Nchimbi aya moja hadi nyingine ili muone ujuha na uhayawani uliofanyika
Sasa tukae kimya kwasababu ndio njia tuliyochagua.
Inasikitisha sana!