RIP Emmanuel Mwaikasu- MBEYA DAY 1987-IFUNDA TECH 1988-90

RIP Emmanuel Mwaikasu- MBEYA DAY 1987-IFUNDA TECH 1988-90

Huyo mwingine aliyefariki anaitwa Fredrick Otieno, alikua mkenya ambaye aliishi hapa kwa muda, alikua mwalimu wa michezo, yeye aligongwa na pikipiki ya marehemu Imma baada ya Imma kugongwa, Imma alifariki on the spot ila Fred alifia njiani, pikipiki iliruka baada ya kugongwa na RV4 na kumgonga kiunoni na kumchana na kumvunja mguu alikua amesimama pembeni anasubiri kuvuka barabara, Fred kasafirishwa jana kwenda Nairobi atazikwa on 1st January makaburi ya Lang'ata. RIP Fred and Imma
 
atakumbukwa the day alipoteremshwa pale round about ya sinza na mkwawa kuelekea kwa mama(vizib0), darajani utawala na kushuka kule down chabruma!! The real man from mbeya akajikuta anakabidhiwa mkulu jimmy by then chairman wa chabu akatupwa pale e6 uso kwa uso na miaka vallery luwi akisaidiwa na mzee francis mulungu na membi kileo na vijana fulani wa dodoma na morogoro, inafurahisha kuzikumbuka zama zile mpaka pale alipojiunga na jopo la wazee wa dojo kilemile na njagamba lawrence huku wakisaidiwa na kijana toka kigoma bitozi mtanashati wa kuuzoa kitwana, hahahaaaaaaaaaa!!! Imma akahamia seuta just to enjoy maisha ya msolopagaz akiwa karibu sana na kilemile na njagamba, he will always be bro,friend, binadamu. Jana nilifarijika sana kuona vijana wa lyandembela na pale sinza wakimuombeleza mtumishi wa mungu imma. Bwana alitoa na bwana ametoa, jina la bwana lihimidiwe
rip imma
Mkuu, nilipigwa butwaa na ule umati uliojitokeza jana. nilijitahidi kuchukua picha kadhaa ingawa kamera yangu ilikufa charge (TANESCO). Inshallah nitaiweka hapa jamvini ili marafiki na nduguze wa mbali waweze kuona safari ya mwisho ya mpendwa wetu.

Ama niwashukuru TRA kwa niaba ya familia kwa kujitoa kwa hali na mali kushughulikia na kugharimikia maziko ya Imma. Lile kaburi lilikuwa la mfano mpaka nikatamani lingekuwa ndo kaburi langu.....

Amekufa akiwa na miaka 36 to 7 lakini ameacha jina kama mzee wa miaka 90 kwa umaarufu, ukarimu na wema wake...
 
Imma alikuwa mcheshi, mtu wa watu na anayependa utani!!!! Sikumbuki kuona amekasirika, kweli watu wazuri hawadumu. Hapa nilipo nakumbuka tabasamu lake. Imma tulikupenda lakini mungu kakupenda zaidi. Tutakukumbuka daima kaka yetu. Nenda kapumzike, mwenyezi mungu aiweke roho yako mahali pema peponi, Amen!!!!
 
Ahsante sana aise!!! Maana sisi tulio mbali tulikuwa tunataka kujua au kuona kaka yetu Imma ameagwa vipi. Inafurahisha kusikia kwamba watu walijitokeza kwani Imma alikuwa mtu wa watu!!! Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina la bwana libarikiwe!!!! Kapumzike rafiki na kaka yetu Emmanuel!!!!
 
rip mwaikasu

NB:kuna umuhimu wa jf members kufahamiana.....!mimi na asprin tulikuwepo msibani na tumeshiriki ibada na mazishi ya mshikaji wetu.sasa ninachoshangaa ni uwepo wa MKUU MSANII na huyo FRD JNR.i wish tungeonana ninyi watu
 
rip mwaikasu

NB:kuna umuhimu wa jf members kufahamiana.....!mimi na asprin tulikuwepo msibani na tumeshiriki ibada na mazishi ya mshikaji wetu.sasa ninachoshangaa ni uwepo wa MKUU MSANII na huyo FRD JNR.i wish tungeonana ninyi watu
wow coincidence.....
nipo darasani mda huu lakini nitawawekea picha zilizosalia. kabla ya new year....
 
rip mwaikasu

NB:kuna umuhimu wa jf members kufahamiana.....!mimi na asprin tulikuwepo msibani na tumeshiriki ibada na mazishi ya mshikaji wetu.sasa ninachoshangaa ni uwepo wa MKUU MSANII na huyo FRD JNR.i wish tungeonana ninyi watu

MIMI NDO Nashangaa kumbe kuna marafiki(huenda ni ndugu pia) tulikua pale(nilikuepo tangu tar 25 hadi 30)
Tunawashukuru ndugu,jamaa na rafiki wote walioshiriki nasi katika kipindi hiki kigumu. Upendo mliotuonesha ni zaidi ya yote.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.
 
DSC01517.JPG
DSC01518.JPG
DSC01520.JPG
DSC01515.JPG
DSC01522.JPG
DSC01524.JPG
DSC01503.JPG
DSC01519.JPG
DSC01516.JPG
DSC01506.JPG
DSC01521.JPG
DSC01514.JPG
DSC01512.JPG
DSC01513.JPG
DSC01525.JPG
DSC01523.JPG
DSC01499.JPG
Nimetimiza ahadi.
Da Sophy, pole sana kwa msiba mzito. Tupo amoja always.
 
Tunashukuru kwa picha!!! Tuta mmiss Imma. Tulikuwa sote Arusha Tech!!! Kapumzike rafiki na ndugu yetu Emmanuel!!! Ilikuwa vigumu kukubali ila sasa nasema kazi ya mungu haina makosa. Tutakumbuka tabasamu lako na jokes zako!!!!
 
Msibani kulikuwa na watu wengi na makaburini pia.
Nilivutiwa na speech ya mwalimu wake CBE kuwa jamaa alikuwa kiungo na problem solver. Ucheshi na bashasha zake havitasahaulika kamwe.

Ameacha watoto wa kutosha kulibeba jina lake kama kumbukumbu njema. Najua kwa namna alivyokuwa kwenye jamii basi amewarithisha watoto au baadhi tabia yake ya kujali na utu. Nduguze niliowaona hawatofautiani sana na marehemu yaani uchangamfu na ucheshi.
 
R.I.P Imma,He was my primary school,class mate..Nyanza,Mwanza...
 
Back
Top Bottom