Ndugu yangu
Pasco naona umekuja kutetea hata visivyo weza kutetewa.
Watu wengi sana humu JF tunafahamu vizuri sana Legal System inavyo-operate hususani katika Common wealth countries.
Watu wanahoji ni Experience na competence ipi aliyonayo Ridhwan mpaka awe recognised kama Successful young Legal Experty?
Hata watu waliosoma naye pale UDSM bachelor of Law wanamjua vema Ridhwan kama Kilaza mchovu kabisa aliyepita kwa kubebwa sana mpaka kuhitimu, wakati wenzie wanakula nondo kavu kavu za sheria yeye alikuwa kutwa anashinda akiwinda na kutafuna vibinti tu lakini akiwa na uhakika mwisho wa siku atafaulu bila kupingwa kwa mgongo wa influence ya baba yake!!
Inawezekanaje fresh from Law school graduate anatoka moja kwa moja na kuwa Senior International Legal opinion Personnel?
Kama mambo ndio hivi nina uhakika ikifika 2015 Ridhwan ataapishwa kuwa jaji na kutangazwa kuwa ndio jaji mdogo kabisa kuwahi kutokea katika nchi za jumuiya ya madola!!!
Mkuu Tanganyika Tanu, life ina opposites nyingi tuu ambapo not all first runners win the race!, kuna akili za darasani, akili za maisha, vipaji na bahati!.
Pale UD wanafunzi vipanga kabisa hubakisha kufundisha!, hata Mkono aliondoka pale na Pass tuu!. Waliopata 1st class ya sheria tangu chuo kikuu cha Dar es Salaa kianzishwe miaka 50 iliyopita, hawafiki 15!, Mpaka sasa 4 kati yao ni walimu pale mlimani, kiukweli ni mmoja tuu ndio nimemsikia akiendesha kesi!. Hivyo hiyo hoja ya mtu ambaye alikuwa kilaza darasani kuwin life, its immaterial!. Hata katika maisha ya kawaida, vichwa ndio wanaokwenda kuchukua medicine, engeneering au computer sciences, vilaza ndio waopiga B com na hatimaye MBA, tukija kwenye ajira, vichwa wanaajiriwa kama technicals na wale vilaza ndio kwenye menejimenti na wanaopiga pesa ndefu ni vilaza na sio vichwa!.
Hili la fresh from school to rise into siniority overnight nalo linategemea umeanzia wapi!, kama umetoka shule ukaanzia vichochoroni, lazima usote kwanza ndipo upande!. Kama umetoka shule ukaanzia top law firm IMMA, then ukaenda ulaya kusoma na kupata exposure!, ukirudi ni halali kabisa kuwa kuwa senior international legal opinion personel!.
Imetokea tuu kijana anafahamika ndio maana mnamsakama sana!, hivi mtu akiwa mtoto wa rais, kama ana uwezo wa kufanya hili au lile, asifanye eti kwa sababu baba ni rais?!. Kijana kasoma sheria kwa uwezo wake, kamaliza kapata kazi sehemu nzuri, kaenda ulaya kuongeza ujuzi, karudi kafungua law firm yake, mlitaka afanye nini?!.
Kwani Karume alifanya nini kustahili urais wa Zanzibar, au Bush jnr, au Kenyata?, ikitokea mtu ni mtoto wa mfalme, umezaliwa kwenye royal familiy, how are you expected to live, or is it your fault?!. Mtu ukizaliwa presideantial family, you live presideantial, hata mimi ningekuwa yeye, 2015 ndio ningechukua ubunge wa Chalize na ten years letter at the top office!, na sio peke yake, tumeyaona kwa kina Gadhi, Kennedies, Bushes, Karumes na sasa Kenyattas etc.
Natoa tuu angalizo, kuweni makini na baadhi yetu humu, wao wamejaa chuki tuu dhidi ya wenzao, wao ni kila siku kulalamika tuu kuhusu kila kitu na kushutumu always!. We have lots of hate preachers as well well as prophets of the doom!.
Pasco.