Labda tuwekane sawa hapa wazee. Nilikuwa naukodolea macho uzi lakini kutokana na comment yako imebidi nichangie tu.. Kwanza kabisa Side Lugumi aka Bilionea hajawahi kuwa mpambanaji kihalali hivyo hicho cheo mvue.
Saidi namfahamu toka Mwanza miaka ile akiwa mesenja kwenye kampuni ya Amrani Batenga. Kijiwe chake kilikuwa cha mamisheni town wa mwanza jengo la Atc pale chini. Saidi alikuwa anatumwa tu nenda hapa fanya hivi peleka huu mzigo kule kachukue hiki pale nk. Kiukweli jamaa alikuwa loyal kwa jamaa Amrani mpaka akaanza kutumwa mzigo nje ya mkoa na hata nje ya nchi kama Uganda. Mpaka hapa inabidi uelewe kuwa jamaa ni std 7 tu na sio zaidi ya hapo. Kwa waliofanya nae biashara hasa hapa dar watakuwa wanalielewa hili jamaa hajiamini kabisa dili yoyote yeye anahisi kupigwa la macho tu. Miaka ya 2000 Side alipotelea Kigoma baada ya kumpata mama mtu mzima aliyekuwa anafanya kazi kwenye mashirika kama sikosei ya UN. Kwa kifupi mr PUNKY shujaa wako Side alikuwa MARIOOO akiwa huko kigoma. Mchizi ndipo alipotokea huko maana jamaa tayari alikuwa na uzoefu wa mambo ya supplies ya vitu mbali mbali toka akiwa mwanza. Side kapiga dili kibao za supplies kwenye mikoa ya juu huko hasa kigoma kwenye mashirika ya maana kwa mkono wa mama. Huko ndio alikoanza kushika hela.
Side ana ugonjwa kama wasukuma wengine wengi tu ambao ni mabinti hasa weupe. Habari kutoka chanzo cha uhakika mama alishindwa tabia za Saidi walitemana.
Side alikuwa keshakichanga cha maana tu ndio akahamia Dar na wengi wamemjulia Saidi Dar background info yake wanaoijua ni kwa wachache hasa watoto wa mjini wa amwanza.
KUYATOA MAISHA
Saidi alisonteshwa na nani sijui mtoto wa IGP hapa ntakuwa muongo sijui ila kwa kifupi ilikuwa ni taarifa za mstuko wa kweli. Baada ya kuoa kwa Mwema ndio network ya kujuana na watu kama Riz na wengineo akaipatia hapo na uBilionea ukaanzia hapo. Ila kwa kifupi
1. Lugumi ni kampuni ya Saidi na si Ridhwani. Ridhwani anaitumia tu kama uchochoro wa kupata tenda na kuvuta chake simply because the guy is loyal na shule hana. Ni rahisi kutumia mtu ambae hajasoma he can be the puppet wewe ukawa puppet master unavuta tu strings.
2. Kwa taarifa tu mwenye pesa nyingi inayopitia kwa Side ni mke wa Mwamunyange na si Riz kama wengi wanavyofikiria. Mke wa Mwamunyange thru saidi wanaSupply pingu,boots, fummigation services,batons na mazaga kibao polisi na jeshini thru Lugumi kwa backup ya mume wake (wajanja wa mjini hili wanalifahamu).
3. Saidi ni kweli pesa anayo ila ndiyo hivyo mambo yakibadilika huko mbeleni yeye ndio scape goat na kwenye hilo hawezi kuchomoka riz na mrs mwamunyange there are just ghosts hawaja Appear kwenye paper work yoyote.
Hivyo wandugu mtu kama B.G TANTAWI wakiuliza mambo kama haya sio kama wana wivu wa kike bali ni wazalendo na wameamua kuhoji nchi yao ikitafunwa. Hii nchi inatafunwa kwelikweli na ndio maana huenda hata watoto wako we ulisema jamaa ana wivu wa kike hawana vitabu shuleni au madawati lakini badala ya kuhoji unapiga vijembe. Aisee mpaka bia yangu imepoa sasa..
Mapanya buku yanatafuna waya wa kupeleka power kwenye CPU ya nchi watu wanaponda wivu wa kike ebooooooo!