Ridhiwani Kikwete, Hii kampuni ni yako?

Ridhiwani Kikwete, Hii kampuni ni yako?

Hivi huyu Ridhiwani Kikwete kila biashara kubwa Tanzania ni yake?.

Ukisoma mabandiko mengi kwenye mitandao utagundua anahusishwa na biashara zote nzuri na mbaya na zenye faida kubwa nchini.

Kuna mlolongo wa madai kuanzia kwenye madawa ya kulevya, usafirishaji wa mizigo na abiria (buses, trucks, plane, boat), mafuta, uanasheria, minerals, Fumigation, politics, n.k.

This is beyond belief kwa mtu mwenye upeo mkubwa katika uchambuzi na hasa ikichuliwa kuwa evidence ni moja ya kikamilisho katika madai.

Is this political placebo au ndiyo yale ya waswahili wasemao, 'lisemwalo lipo' kama halipo linakuja.
 
Ridhiwani ni kijana maarufu sana hasa hapa Jukwaani. Average ya kutajwa katika thread na comment ni zaidi ya kawaida
 
Haya ni majungu ya kukosa kazi, hii ka mpuni ipo miaka mingi kabla hata riz hajaenda jando
 
Daaaah! Unampinga sana jamaa lkn kitu usichokijua ni kama usiku wa giza. Au kuna kitu unakijua ndio unajitahidi kumpinga mleta mada ili akate tamaa?

Msukuma-shemeji wa Mwema-BOT-EPA.......Endelea kupinga tutatoa vyote

Mimi simpingi jamaa Kama unavyosema. Ila napinga Uongo na upotoshaji UMMA kwa kuleta habari za kichochezi. Ridhiwani ni Mtanzania Kama Watanzania wengine...imetokea Baba yake ni Rais kwa hiyo muacheni atumie fursa aliyonayo ili mradi tu havunji sheria na taratibu za nchi yetu tukufu. Kwani kuwa shemeji ya Mwema ndio nini!!??? ACHENI MAJUNGU. Kama una hoja za msingi zitoe zote na utajibiwa accordingly....Hii ni JF na sio Facebook.

Wewe Kijana, hebu acha kuugua huo ugonjwa wa husda na majungu,, acha kabisa mdogo wangu maana hautakusaidia na haujengi picha nzuri ya JF,, Njoo huku Midle east tupige kazi, wenzetu wakenya , waganda, na matatifa mengine kibao wako huku Dubai, Iraq, Iraq Lebanon, Jordan wanapiga kazi, wanasaidia familia zao, sisi tumekalia politik tu,, sasa maneno ya vijiweni tunayaleta mpaka huku.... huu ugonjwa hujaugua wewe peke yako hata enzi zetu tuliugua ugonjwa huu ndo maana nakushauri kwa sababu naujua vizuri,, hatima ya ugonjwa huu ni wewe kwenda barababrani ukisemea hovyo!! Nakumbuka miaka ya 80s kuna watu walishamzushia mzee wetu Nyerere eti yeye ndo mmiliki wa KUGIS transport compay enzi hizo iko juuuu,,, mara nyerere ameonekana Geneva amekwenda kuficha hela,,, mzee wa watu kafa mweupe!! mapaka tunaona aibu.... na kwanza nani kakwambia ukiwa mtoto wa mkubwa basi ujikalie tu home usifanye biashara!!! kutoka moyoni nakupa pole

Mkuu Msumeno,
Umenikumbusha mbali sana kwa hii issue. Wengi hawa wapiga Majungu hawaijui hata KUGIS.
Tatizo letu kubwa baadhi ya Watanzania ni Majungu na Unafiki tu. Hatutaki kuchapa kazi na kujenga Taifa. Wakiambiwa ukweli wanakimbilia "Ooooh ninayajua mengi lakini Sitaki kusema".

Haya ni majungu ya kukosa kazi, hii ka mpuni ipo miaka mingi kabla hata riz hajaenda jando

Mkuu Gama,
Waeleweshe hawa wakurupukaji waelewe. Hiyo Kampuni iko miaka mingi.
 
Nisaidieni picha ya Riz nikimuona nimuombe ya chai. Namsikia tu
 
Ss km umeweza kuyajua yt Haya Hilo la kodi limekushinda nini.
 
Ridhiwani muacheni dogo afanye biashara mbona mabaniani pale kariakoo hamuulizi kama wanalipa pango kwa NHC?Au kwa vile mzawa ndio mna shoboka Mnawanyenyekea wageni huku mkiwaponda wazawa Hii nchi ngumu
 
Tuwe tunafanya utafiti (research) kidogo tu kabla hatujaleta Mada hapa jamvini na kuanza kutaja watu majina.
Huyo jamaa anaitwa LUGUMI ni Msukuma fulani ana hela zake na biashara hajaanza jana wa juzi. Uliza vizuri au watakuja watu wanaomfahamu hapa JF watakuelewesha. Mwisho wake mtasema AZAM ni ya Riz na amemuweka Bakhresa tu pale na watoto wake.

Nadhani thread ilikuja kimfumo wa swali.
 
RIZ ni mtanzania jamani anahaki pia ya kufanya biashara mradi iwe halali, wabaya ni wale wanaokwapua na kwenda kuficha mabilioni ya pesa za watanzania nje ya nchi, ni afadhali wakawekeza nchini watoto wetu japo waambulie ajira na kodi kwa nchi kwa ajili ya maendeleo.
 
Kijana mwenzetu, mtanashati na mzalendo wa nchi hii na mwanasheria na wakili msomi wa mahakama kuu Nd. Ridhiwani kikwete ametajwa kumiliki kampuni kubwa iitwayo LUGUMI, kampuni hii ipo maeneo ya hapa POSTA mpya jengo la ATC HOUSE, jengo hili ni mali ya watanzania wote na ndo ofisi kuu ya shirika la Ndege za serikali. Kampuni hii inajihusisha pamoja na mambo mengine na maswala ya Unyunyiziaji wa dawa za kuulia wadudu yaani Furmigation katika ofisi mbalimbali za umma na binafsi hapa nchini.

Katika kuficha ili asifahamike, kijana huyu amemuweka mtu pale ili awe msimamizi tu, ili yeye awe anatafuta tender kupitia kofia ileeee.

Swali ni je, analipa kodi serikalini? kwa sababu wana magari mengi sana pale, sasa je alilipa kodi ya serikali wakati anayaingiza? na je, Shirika la Ndege la ATC linapata kodi yake?

Nadhani thread ilikuja kimfumo wa swali.
Hapo kwenye RED huo mfumo wa Swali unaozungumzia ni UPI!!??? Tusiwe na tabia ya kukurupuka Watanzania wenzangu...soma habari au mada kwa undani,chukua ya mleta mada na ya Kwako changanua...halafu ndio upinge au kuunga mkono mada kwa vielelezo na sio UNAFIKI,MAJUNGU NA MATUSI.
 
Tuwe tunafanya utafiti (research) kidogo tu kabla hatujaleta Mada hapa jamvini na kuanza kutaja watu majina.
Huyo jamaa anaitwa LUGUMI ni Msukuma fulani ana hela zake na biashara hajaanza jana wa juzi. Uliza vizuri au watakuja watu wanaomfahamu hapa JF watakuelewesha. Mwisho wake mtasema AZAM ni ya Riz na amemuweka Bakhresa tu pale na watoto wake.

Kama haujui kaa kimya nani alikwambia mali za Bakhresa zote zake? stuka wewe!! Unalijua lile ghorofa la Fire pale karibia na yard? Ukimcheck mwenyewe amechoka kinoma,nikamuuliza ndugu yake inakuwaje ndugu yako ana mali hivi lakini hasomeki akaniambia kaka we acha tu,sio lake kiini macho tu yeye....wenyewe wapo!!! Riz1 anakaba kila kona huyu dogo kuanzia kuzoa taka ECO hadi kuua sisimizi LUGUMI
 
Jamani jamani!vya Riz ndio vya kuuliza tu!?hebu tuambie kwa upande wako ili wana jf tuanze kukufuatilia.
 
Kama haujui kaa kimya nani alikwambia mali za Bakhresa zote zake? stuka wewe!! Unalijua lile ghorofa la Fire pale karibia na yard? Ukimcheck mwenyewe amechoka kinoma,nikamuuliza ndugu yake inakuwaje ndugu yako ana mali hivi lakini hasomeki akaniambia kaka we acha tu,sio lake kiini macho tu yeye....wenyewe wapo!!! Riz1 anakaba kila kona huyu dogo kuanzia kuzoa taka ECO hadi kuua sisimizi LUGUMI
Kama sijui nini sasa? Mimi huwa sikuRupuki. Nimechangia hii thread kwa kuwa naifahamu au kumfahamu LUGUMI. Hayo ya Bakhresa unayajua wewe...mimi nilitoa mfano tu. Kwa hiyo wewe Kwa akili yako timamu Kama mtu anamiliki Mali au Ghorofa na amechoka atakuwa anatumiwa na watu sio!!??? Duuuuuuuuh:shocked:!!!! Kweli wabongo tuna safari Ndefu bado. Mmeshazoea kuona mtu akiwa na vishilingi vya kula kavaa mipete na micheni ya dhahabu na ufahari mwingiiii. Kuna watu wana hela zao wametulia mkuu,ndio Kama hao unaosema hawasomeki.
 
kijana mwenzetu, mtanashati na mzalendo wa nchi hii na mwanasheria na wakili msomi wa mahakama kuu nd. Ridhiwani kikwete ametajwa kumiliki kampuni kubwa iitwayo lugumi, kampuni hii ipo maeneo ya hapa posta mpya jengo la atc house, jengo hili ni mali ya watanzania wote na ndo ofisi kuu ya shirika la ndege za serikali. Kampuni hii inajihusisha pamoja na mambo mengine na maswala ya unyunyiziaji wa dawa za kuulia wadudu yaani furmigation katika ofisi mbalimbali za umma na binafsi hapa nchini.

Katika kuficha ili asifahamike, kijana huyu amemuweka mtu pale ili awe msimamizi tu, ili yeye awe anatafuta tender kupitia kofia ileeee.

Swali ni je, analipa kodi serikalini? Kwa sababu wana magari mengi sana pale, sasa je alilipa kodi ya serikali wakati anayaingiza? Na je, shirika la ndege la atc linapata kodi yake?

kabla ya kuuliza hili nenda kwenye yale magari ukaangalie yana road.l kwanza uje kuniambia
mwanzoni nilihisi magari ya state na ile tinted zao kumbe zinakazi maalum
napita tu jamani msisnimalizie kucha zangu mbili zilizobaki mie
 
Back
Top Bottom