Revealing: TANESCO inaidai IPTL Tshs Bilioni 321...

Revealing: TANESCO inaidai IPTL Tshs Bilioni 321...

Jesus....Akaunti ilikuwa na bilioni 306 ......good enough hizi zilikuwa ni fedha za umma.....mbaya zaidi Tanesco inaidai IPTL bilioni 321.......hakika nawaambia....hii ngoma italeta historia mpya nchi hii.........kama bado kuna Watanzania waliobaki na chembe za uzalendo lazima tusimama pamoja sasa kuliko wakati wowote......

So kifupi tun adai Bilioni 618. Je ile mitambo na asset zingine za Singa singa zinafika gahrama hiyo?
Inabidi tuchukue kile kitalu cha mafuta kufudia deni letu.

CC: Pasco

Ndugu yangu vipi Ushabadilisha maoni yako?
 
Last edited by a moderator:
Walidanganganya mwanzoni na wakawa wanalipwa zaidi ya walichostahili, kama kawaida ya wasomi wetu wapumbavu, wanaoingia mikataba fake hawakuliona hilo. Mbaya zaidi mwishoni wameshirikiana kuiba hata kile ambacho kingerudishwa.
Muda mrefu IPTL ilikuwa haizalishi umeme, walikuwa wanalipwa capacity charge.
kwani mitambo ilisimikwa mwaka gani na ikaanza production mwaka upi?
 
Niliwahi kumwambia rafiki yangu mmoja, kaa mbali na wazungu hawakurupuki kwa vile source zao za habari ni beyond na tunavyofahamu. Hatuelewi kuwa, hizo tunazoita siri zetu na kuwasiliana kwenye mitandao inayomilikiwa na hao watu, ndio bayana yao.

Ukiona jambo wamelishupalia jua wana hakika nalo. Mbaya zaidi, haya maviongozi yetu malafi bila kufikiria, wanataka kujitia kitanzi zaidi kwa kuchakachua kitu hiki.
 
Eti Ame ni nabii?

Lord of glory I bow before you, you are a convenant keeping God!
 
Bei ya umeme uniti 1= tsh.306.56/-
posho za ewura 1% = tsh. 3.07-
mchango REA 3% = tsh. 9.20/-
VAT 18% maVX = tsh. 55.18/-
tozo kila mwezi = tsh. 5,520/- (unalipa kila mwezi hata kama hujatumia)
JUmla LUKU Bei ya uniti 1 = tsh. 680/-

Kadirio la chini kabisa kwa nyumba ya familia ya watu watano walau wanahitaji uniti 1.5 kwa siku, gharama yake ni tsh.1020/- kwa siku.

Sababu ya gharama za uzalishaji umeme kuwa kubwa;
1.kila kukicha wakurugenzi wa TANESCO wanapiga dili, mfano Mhando.
2.kulipia tsh.5,520/- kila mwezi kwa ajili ya kukamilisha mikataba kama IPTL, Songas, RICHMOND, PAP, Dowans, Symbion

WANANCHI TUTAUTUA MZIGO HUU SIKU TUTAKAPOAMINI BILA CCM INAWEZEKANA, kama tutaendelea na CCM tutapigwa danadana na habari zisizo rasmi TANESCO wanaandaa DODOSO LA KUPANDISHA BEI UMEME. wakipandisha tu posho ya ewura, REA, VAT zote zitapanda kwa sababu upatikana kupitia bei itakayopandishwa na TANESCO. mfano bei ikipanda hadi kufikia 450/- mtumiaji wa umeme utalipia uniti moja kwa tsh. 927 tena hapo tsh.5,520/- ambayo unalipia kila mwezi ibaki kama ilivyo.

bila vurugu za ufisadi bei ya umeme ni tsh. 373/- kwa unit ka elfu kumi kako ungepata uniti 26.8

Mkuu upo sahihi kabisa! tuendelee kupinga Magamba tutapona. Nadhani walivyoona makelele yamezidi wamesitisha hizo 5,520/- mana jana nimenunua umeme wa 50,000 nimepata units 133.9 na sijanunua tangu October mwanzoni kwahio nimeuziwa unit moja sh. 373.412..... Nakumbuka kuna kipindi mzee unaenda luku na ka shilingi 10,000 kako unaambiwa hii hupati umeme kaongeze, sasa kama ndio yote ulonayo unaamua kununua mshumaa na chenji inabaki ndeeeefu....tuamkeni jama hii mijamaa itatuzikia humu
 
imebainika kuwa ripoti ya iptl ni nyeupe na wala haijakaa katika mfumo wa kumuadhibisha mtu kwa kuwa imekaa kihasibu zaidi.

Source;Gazeti la Mtanzania
 
Kihasibu inakaaje??!!
Haioneshi mapato na matumizi wala activities za mafungu husika???!!!

By the way repoti ya fedha haiwezi kuwa nyeusi na ya ki famasia lazima iwe ya kihasibu!!
 
Maskini watanzania wenyewe bado hawajitambui kama wangejitambua saa hizi majambazi yote ya ccm yangekuwa yameshaikimbia nchi hata yule aliyepasuliwa busha angechukuwa ukimbizi huko huko hospitalini ili akamuliwe vizuri busha lake. Lakini bado hawajajitambua kama walivyojitambua Burkina Faso, wanatiwa vidole vya macho na Magamba bado yamelala fofofo wala hayajitambui yamebakia umbea na udaku tu ndio wanayojua wao

Au naye angefanya kama BALALI.
 
Hivi inawezekanaje mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila alijua uchafu huu wa IPTL pasipo raisi kujua?

Kama raisi alijua,mbona alikaa kimya?Na kama raisi hakupewa taarifa,mpaka leo amechukua hatua gani kwa waliopaswa kumwarifu?

Kwa wenye kumbukumbu nzuri mtakumbuka kauli/ahadi ya JK kwa waandishi wa habari mwaka 2005 wakati anatangaza baraza lake la mawaziri kwa mara ya kwanza kuwa atatumia hata ushahidi wa kimazingira kuwawajibisha wateule wake na akatao mfano wa mtu kuwa na mali nyingi ndani ya muda mfupi tangu ateuliwe.

Sasa swali langu ni mbona imekuwa kinyume chake kabisa?

Hivi kweli tunahitaji kuendelea na katiba inayotoa kinga ya raisi kutoshitakiwa popote pale kwa makosa atayofanya akiwa madarakani na hata baada ya kustaafu?

Aliondoka Lowassa,sasa ni zamu ya Pinda.Vipi kiranja mkuu hagusiki?

Only in Tanzania!

Think twice mtanzania.
 
Back
Top Bottom