Revealing: TANESCO inaidai IPTL Tshs Bilioni 321...

Revealing: TANESCO inaidai IPTL Tshs Bilioni 321...

Wakuu,mimi ripoti haifunguki.naomba iwekwe live hapa
 
Sasa huu ni wakati wa sisi kuunganisha nguvu ya pamoja katika kadhia hii, tukishindwa itakuwa ni aibu sana kwasababu tumekuwa washabiki katika mambo hata yasiyokuwa na tija kama Miss TZ na megineyo. Pia itakuwa ni aibu sana kwa majirani zetu na hata hawa wazungu waliiona huu ufisadi tukinyamaza kimya.
 
Hivi vyombo vya dola mbona kimya havijaanza kamata kamata wezi hawa? Najua tu siku wakianza, 90% ya wahusika watakuwa nje ya nchi. Ila wakumbuke kitu kimoja -- wakikimbilia marekani au EU watarudishwa tu ku-face justice here!
 
Hivi vyombo vya dola mbona kimya havijaanza kamata kamata wezi hawa? Najua tu siku wakianza, 90% ya wahusika watakuwa nje ya nchi. Ila wakumbuke kitu kimoja -- wakikimbilia marekani au EU watarudishwa tu ku-face justice here!

hao wahusika unaowataja ni wepi?
 
Maswali magumu ninayojiuliza juu ya hili.


  1. Je watanzania tutakubali wanaohusika wajiuzuru bila kuchukuliwa hatua za kisheria? (Ref. Suala la Richmond)
  2. Je waliojigaia na kugaiwa fedha hizi watarudisha bila kuchukuliwa hatua zozote za kisheria? (Ref. Suala la Richmond)
  3. Waliozembea hadi suala hili likafika hapa wataachwa na kuzidi kulipwa posho za kuwa kule dodoma? (Ref. Suala la Richmond)
  4. Waliojaribu kuficha ficha, kukwamisha kwamisha na kujaribu suala hili lizimwe watanzania wataachwa bila kuchukuliwa hatua za kinidhamu?

Maswali haya hayana jibu rahisi kwa sababu sakata la hili lina reflect sakata la Richmod na kila lililotokea.
 
Duuh....hii kweli ni clue 1.

Wazungu huwa hawakurupuki asee. Mpaka wamechukua hatua nzito ya kusimamisha Budget support wameshafanya uchunguzi wao na wamejiridhisha uwepo wa ufisadi.

Ole wake sasa serikali wakijifanya kuingilia report hii na kuichakachua kama hawajaumbuka, watu wana facts zao siku nyiiingi.

Lakini ni aibu sana kwa Taifa hiki. Yaani mpaka mzungu ndo anakuja kuwa na uchungu na affairs za kwetu?. Sijui tumelaaniwa wapi hata hii nchi! Tanzania is tragedy country!

mkuu nilikuwa najiuliza kwanini Werema anauwa mkali kiasi kile kwa kulazimisha swala hilo lisiongelewe, wakishirikiana na Makinda wali jitahidi sana kumzuia Kafulila asiliongelee swala hili, hadi Werema akamwita "TUMBILI"
 
Sakata la IPTL likiwekwa wazi Kama lilivyokuwa nchi inaweza kusimama....
 
Asante mkuu kwa Taarifa, lazima serikali ivuliwe nguo kwa sababu imezoea ujinga kila siku na kila dakika yenyewe inawaza wizi tu wa pesa zetu.

Wenzetu Uganda wanatengeneza MAGARI kutuuzia sisi tunawaza kuiba na kuendeleza ujinga tu bila kuangalia maisha ya baadae ya TAIFA letu yatakuwaje.

Lazima Waziri Mkuu na wenzake wajiuzulu, nimechoka kusikia hizi habari za IPTL, RICHMOND, MEREMETA, EPA nk.

Yani ametoka ngedere wakamuweka nyani sasa wananchi wakikaa kimya mwisho atakuja tutaona anaingia sokwe asee wasituletee kamchezo kabisa juu ya hili kwa kweli.
 
Mkuu MANI itakuwa poa sana hili likiwezekana maana wahuni na mafisadi ndani ya hii Serikali dhalimu hawalali ili kuhakikisha ripoti hii inachakachuliwa au haiwasilishwi Bungeni ili ijadiliwe kwa kina.

Na yule muhindi mmoja wa wahusika wa wizi huu mkubwa aliyeanza kutoa rushwa nchini haonekani tena hadharani si ajabu kishatoroka nchini.

Ndio maana najiuliza huyu muhindi nilikua namuona kwenye tv Mara anakabidhi cheque za milioni 10 Mara ishirini za misaada nikawa najiuliza maswali yasiyokuwa Na majibu. Kumbee ametumwa ba magamba kusafisha njia yani funika kombe mwanaharamu apite. Hii sasa watoto WA mjini wanasema imekula kwao.....
 
Last edited by a moderator:
mkuu nilikuwa najiuliza kwanini Werema anauwa mkali kiasi kile kwa kulazimisha swala hilo lisiongelewe, wakishirikiana na Makinda wali jitahidi sana kumzuia Kafulila asiliongelee swala hili, hadi Werema akamwita "TUMBILI"

Mkuu, kuna kitu nyuma ya pazia ndo maana akina Tumbili wanashikia bango
 
Kwa nini wanaleta kila mara hii kinga ya kwamba hela siyo za umma - yaani hata EPA walisema siyo hela za umma. Haya, hata kama siyo za umma, basi ndiyo majizi machache wajichotee? Wizi wowote si wizi tu?

Wakiiba raia ndio wezi mkuu wao wana a.k.a wanajiita wala rushwa au mafisadi asee ila kwa hapa ni lazma pachimbike mkuu.
 
Wakiiba raia ndio wezi mkuu wao wana a.k.a wanajiita wala rushwa au mafisadi asee ila kwa hapa ni lazma pachimbike mkuu.

mwizi ni mwizi tu awe mkubwa au mdogo ilmradi kuna ushahidi wa hilo
 
Nawasoma Magamba kama Lizabon na Faiza naona mapovu yanawatoka maana tumewashika kwenye 18 zao tutawaumbua tu Mafisadi
 
Watetezi wa watawala na chama chao wana roho ngumu sana,Yaani kwa hizi kashfa zote hizi za Serikali na chama chao bado mtu unasimama kwenye hadhara kukinadi na kuhisifa serikali na chama chao?!
 
That not enough,this massive theft must go done with the government na chama chao,people this is it there is no tomorrow.

Tomorrow never come ni kweli mkuu.
 
mwizi ni mwizi tu awe mkubwa au mdogo ilmradi kuna ushahidi wa hilo


Kweli mkuu waturudishie fwedha zetu maana imedhihirika mabilioni yalilipwa ni ya umma maana IPTL waliwatoza TANESCO fedha zaidi ya kiwango walichostahili....

Sijui viongozi waliosema fedha zile so za umma watakuwa na jibu gani?
 
Back
Top Bottom