Reincarnation...nazidi kupata uhakika binadamu hatufi

Reincarnation...nazidi kupata uhakika binadamu hatufi

nzalendo

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2009
Posts
12,673
Reaction score
14,052
Naam hili jambo nilikuwa nalichukulia poa...lakini baada ya kuamua kufuatilia kidogo naanza kupata uthibitisho pasi kuwa na shaka juu ya mzunguko wa maisha ya viumbe sisi bin adamu.

Kwa kifupi sana tafiti ni nyingi lakini......nilipata kuishi nyanda za juu kusini mwa Tanzania nikiwa kijana mdogo miaka mingi sana iliyopita.

Nilikuwa nina rafiki yangu Mbulushi...rafiki yangu huyu kwa bahati mbaya alifariki.

Siku ya siku sina hili wala lile nikiwa katika nchi ya mbali sana nikakutana na kijana mmoja amefanana na yule rafiki yangu kwa zaidi ya asilimia 90%...nikabaki namshangaa...kitu cha ajabu na yeye kama alikuwa ananishangaa...nikamuuliza ulishawahi kuishi.

Tanzania...akasema hapana hata Neno Tanzania ndio leo analisikia.
Ajabu zaidi anasisitiza kwamba ananifahamu lakini hakumbuki ni wapi tulisha wahi kuonana
Mahali ambapo nilipata mshituko niliona alama katika mkono wake wa kulia sawasawa na yule rafiki yangu,,,(alama hii naikumbuka kwa sababu alianguka na baiskeli akachanika na kushonwa katika hospitali ya Aga khan)....sasa huyu jamaa anasema hiyo alama amezaliwa nayo hivyohivyo.

Nikijaribu kumuuliza yeye asili yake ni wapi anasema ni Afganistan na hana ndugu wala jamaa Afrika.

Kwa kifupi sana 1.Sauti yake 2.Ongea yake 3.Namna anavyotembea ni yule marehemu kabisa kabisa.

Yule Marehemu leo angekuwa na miaka kama 70 hivi na huyu niliyekutana nae yuko kwenye miaka ya 30 katikati.
 
Hata mimi nahisi hatufi mazima
Lakini kuna dhana ambayo naona ipo sahihi zaidi. Nayo ni kwamba ukifa ndio unapotea mazima, haurudi tena duniani na ndio inakuwa imeisha hiyo
Hii naiamini kwa asilimia nyingi zaidi, japo kuna muda nikiwaza hata hiyo ya kwamba ukifa unazaliwa tena inamake sense kuliko hizi habari za kwenda motoni na peponi
 
Huwezi ukajua maana ya MUNGU ni mengi. Ni jambo linafkrisha pia, hv vip kama kweli mtu unapofariki kumbe unazaliwa nchi nyingne na tayal umepoteza kumbukumbu yoyote, yaan upo kama mtu aliyepata ajali kichwa kikaathirika kwa kupoteza data yoyote, hapo hata mama ako humkumbuki tena, in short hukumbuki chochote hata jina lako hulijui na hujui wew ni nan! Inafkrisha sana, huenda hata mm niliwah kuish kabla sijafa huko na kuzaliwa tena bongo! Mm sijui
 
nzalendo

Ukishaondoka duniani haurudi tena mkuu utabakia kwenye kizuizi kaburini mpaka siku ya kufufuliwa kwaajili ya kulipwa wema kwa wema na ubaya kwa ubaya, najua ni mtu mzima sasa, punguza haya matumaini na ujiandae na mauti yako.
Hiyo unayosema wewe ni imani ya Kikristo au ya Kiislamu
Mleta mada anajaribu kuextend akili yake kwenda kwenye imani nyingine tofauti na hizi tulizozizoea. Na hakuna hata moja iliyothibitishwa kwa hiyo muache watu wawe free kufikiria beyond
 
Naam hili jambo nilikuwa nalichukulia poa...lakini baada ya kuamua kufuatilia kidogo naanza kupata uthibitisho pasi kuwa na shaka juu ya mzunguko wa maisha ya viumbe sisi bin adamu.

Kwa kifupi sana tafiti ni nyingi lakini......nilipata kuishi nyanda za juu kusini mwa Tanzania nikiwa kijana mdogo miaka mingi sana iliyopita.

Nilikuwa nina rafiki yangu Mbulushi...rafiki yangu huyu kwa bahati mbaya alifariki.

Siku ya siku sina hili wala lile nikiwa katika nchi ya mbali sana nikakutana na kijana mmoja amefanana na yule rafiki yangu kwa zaidi ya asilimia 90%...nikabaki namshangaa...kitu cha ajabu na yeye kama alikuwa ananishangaa...nikamuuliza ulishawahi kuishi.

Tanzania...akasema hapana hata Neno Tanzania ndio leo analisikia.
Ajabu zaidi anasisitiza kwamba ananifahamu lakini hakumbuki ni wapi tulisha wahi kuonana
Mahali ambapo nilipata mshituko niliona alama katika mkono wake wa kulia sawasawa na yule rafiki yangu,,,(alama hii naikumbuka kwa sababu alianguka na baiskeli akachanika na kushonwa katika hospitali ya Aga khan)....sasa huyu jamaa anasema hiyo alama amezaliwa nayo hivyohivyo.

Nikijaribu kumuuliza yeye asili yake ni wapi anasema ni Afganistan na hana ndugu wala jamaa Afrika.

Kwa kifupi sana 1.Sauti yake 2.Ongea yake 3.Namna anavyotembea ni yule marehemu kabisa kabisa.

Yule Marehemu leo angekuwa na miaka kama 70 hivi na huyu niliyekutana nae yuko kwenye miaka ya 30 katikati.
Unaongelea kuzaliwa upya wa mwili au roho
 
Hiyo unayosema wewe ni imani ya Kikristo au ya Kiislamu
Mleta mada anajaribu kuextend akili yake kwenda kwenye imani nyingine tofauti na hizi tulizozizoea. Na hakuna hata moja iliyothibitishwa kwa hiyo muache watu wawe free kufikiria beyond
Aliyetueleza ametuumba kwa utaratibu huu na huu, na sayansi imethibitisha ndio yeye ametueleza tukifa tunaenda wapi, na uhalisia ni shahidi mzuri, umeona mtu amekwepa kifo?! hata uwe Buddha wa nyota 70 siku ikifika unaenda na maji kirahisi sana, so na wewe ukiuza simu punguza kujipa matumaini jiandae na mauti yako.
 
Back
Top Bottom