Regia Mtema is No More!

Regia Mtema is No More!

Status
Not open for further replies.
There are currently 512 users browsing this thread. (176 members and 336 guests)
 
mkuu weka maelezo kamili basi!

maiti ipo hospital ya tumbi, majeruhi wengine wanapewa huduma ya kwanza tayali kwa kupelekwa muhimbili. mama yake wanamficha kumwambia kama mwanae kafa. naye ni mmoja ya majeruhi. Mia
 
Mkuu mizizi inabidi kuamini2 mi pia nikajua ni siku ya wjinga leo lakini hapana dah! inauma sana!
 
Duuu!!! Ni ngumu kuamini.........nimeishiwa nguvu kabisa! Poleni ndugu wote, Poleni JF members! Mungu awatie nguvu na kuwafariji wote.
 
?????????????????????????????????????!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Ee Mungu eeeeeeeeeeeee!!!!!!!!!!!!!!!!
Nasikia kizungu zunguuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
R.I.P Regia Mtema

nimejifunza mengi na ujasiri wako utasimuliwa vizazi hata vizazi!
 
Habari hii imenishitua sana na nimeiona kwa post za Mh. Heche kule facebook...Inauma sana coz I spoke with her majuzi kama sikosei na ilikuwa nionane...Lol...R.I.P Hon Mtema...

Sijawahi kuonana na Hayati Regia Mtema ana kwa ana katika uhai wake lakini siku zote nilimwona kuwa ni mtu ninayemfahamu sana. Misiba hutokea mara nyingi, tunapoteza ndugu zetu, tunapoteza marafiki zetu, na wengine wengi LAKINI kifo hiki cha Regia Mtema ni mshtuko wa pekee. Muumba wetu, kazi yako haihojiwi wala haipingwi lakini kama tungepewa nafasi ya kusema lolote kabla ya kifo hiki, tungepiga magoti maelfu kwa maelfu, kukuomba utuepushe na msiba huu. Muumba wetu, tunapoyapokea yote kwa moyo wa unyenyekevu, tunakuomba umpokee katika ufalme wako Regia Mtema, uwape uvumilivu na nguvu ya kuyapokea haya, familia yake na ndugu wote wa karibu. Sote tumehuzunika sana lakini tunatambua kuwa familia yake itakuwa imehuzunika zaidi. Pole sana familia ya Regia, poleni sana viongozi wa CHADEMA, poleni sana Watanzania na hasa wale wanaopigania mabadiliko kama alivyokuwa Regia.
 
Mungu wangu! yawezekana mafisadi wamevuka mipaka wanafatilia hata wapinzani ili wachukue nchi kilaini!

Acha ujinga wewe, nyie ndio hamuishi shiriki ata katika mambo ya wazi.Hii ni ajali kama ajali nyingine na alikuwa anaendesha mwenyewe na abiria ni ndugu zake pamoja na mama Mzazi.
 
Habari za kuaminika nikuamba yule mbunge na member maarufu wa JF amepata ajari akiwa njiani kwelekea kibaha majira ya saa 5 asubuhi na kusababisha majeruhi 7. Alikuwa aki Overtake lorry na akakutana na Lorry jingine kwa mbele na alipojaribu kulikwepa akapoteza direction na kupata ajari na amepoteza maisha palapale.
RCO wa Mkoa wa Pwani amedhibitisha tukio hili.

Mungu ailaze mahali pema peponi Amen

Munu alitoa na mungu ametwaa,Jina lake libarikiwe
 
Ni kweli wanajf kamanda kafariki, source Itv breaking news muda mfupi uliyopita
RIP kamanda Mtema, Mungu ailaze mahali pema peponi, Amin
 
Jamani ni kweli imetangazwa na Radio One Breaking News
Ooh God............................
 
tutamkumbuka sana kamanda REGIA,,
mungu ametoa na mungu ametwaa, jina lake libarikiwe..amen
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom