BJB FC
JF-Expert Member
- Aug 25, 2015
- 2,169
- 2,487
Spot on mkuu. Baadhi ya wapumbavu humu, hawaumii kwa kupoteza game, bali wanaumia kupoteza dhidi ya Arsenal.Ni Madrid wenyewe kuleta vyuma vya kazi, Jana Saka na Martinelli wote walikuwa wakirudi Hadi chini kabisa kukaba na imekuwa hivyo Kila siku Kwa arsenal, Sasa hivi mido ya Rice, Partey na Odegaard Iko compact sana na akili nyingi, Arsenal walikuwa hawatembei tu uwanjani Kila movement waliyofanya hata kama hawakuwa na mpira ilikuwa na maana.
Kilichoamua ni ubora wa Arsenal, hata mechi ingerudiwa mara kumi Bado Madrid angefungwa tu... Arsenal msimu huu Yuko Bora sana hivyo mara nyingi hufungwa Kwa ujanja ujanja na mpira wa kihuni huni, ukisema uende nao toe to toe kama ni mchovu hutoboi, mfanyie uhuni basi unamfunga...Subirini muone ikitokea Arsenal akakutana na Inter Milan, utaona jinsi mpira wa kihuni ulivyo na unavyochezwa.
Kwao wakisia Arsenal, basi picha ya kwanza inakuja ni Manchester United 8-2 Arsenal. Wanashindwa kukubali zama zimebadilika.