Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

January hii apa tuna fanya usajiri tuna fukia mapengo mwendo mdundo ktk miaka zaid ya kumi hatuja wahi kua na team bora zaidi ya hii Benz asepe zake ila kwa Zizu bado cja kubaliana na ww makosa mengine cio ya coach ni mchezaji binafisi na bahati pia jana tume gonga besela mara tatu kumbuka

Ok!...ngoja tuone Board ya team itaafanya usajili upi hapo january, ila kwangu mie kama zidane atabakia pale bernabeu inabidi abadili mwenendo na mbinu za mchezo wa madrid na sio kwa dizaini hii tunayokwenda nayo ila mbali na hapo kutakuwa na tatizo tena kubwa tu, pia ningefurahi kuona tunasajili KIPA Na BEKI WA KATI MMOJA...Maana ukiangalia vizuri katika beki zetu za kati yani varane na Ramos...ni ukweli ulio wazi na utagundua tayari Ramos kiwango chake kimeshuka yani anaacha mashimo mengi sana eneo lake hadi varane yanamshinda kufukia...kama uliona moja jana kuna shuti moja kaliblock varane pale kati ya goli kabisa ata kipa alikuwa keshapotea kabisa.
 
Pambana na hali yako mama, kwn team yako haina thread JF? kinacho kuleta huku n nn.

mkuu achana nao hao jamaa nafikiri hapa ni thread maalumu ya madrid fans...twende tujadili mambo chanya kwa timu yetu na sio vijembe vyao!, muache maana anatumia MB zake na zikiisha hutaona usumbufu wake humu jukwani...unless otherwise ajiunge bando tena na tena.
 
Mbinu zimewaishia!!!!!!
Hii man to man marking mara ya mwisho cjui niliona inatumika wapi
Huu ni uoga wa hali ya juu

Hawa majamaa wanasingizia wamechoka eti mechi nyingi!!!! Mechi nyingi zipi hizo walizocheza?? Last season uefa tumeshiriki wote,la liga hata copa der ley walilotolewa asubuhi kbs
Haya walifika fainali ,mbona juve hajateteleka bado??? Au yeye aliruka tu akakutana nao????

Madridiots hawataki kukubali ukweli kuwa this season washakabwa koo.Timu zishawasoma na makrosi yao
Eti wanalalamika wanataka kunyanyua kwapa!!!!!!
MADRI
Halafu sijui kwanini wanapiga cross,mbona flanks za Barca zinaingia na mpira mpaka ndani ya 18-na ku cut back mpira
 
Pambana na hali yako mama, kwn team yako haina thread JF? kinacho kuleta huku n nn.
Avatar yako tu inaonyesha what kind of a person you are
Naona unafurahia tu jibu nikujibu baina yetu. Sijaona pointi kutoka kwako yakueleweka. Kiufupi huna hoja
 
Halafu sijui kwanini wanapiga cross,mbona flanks za Barca zinaingia na mpira mpaka ndani ya 18-na ku cut back mpira
Makrosi ndo mbinu yao hawa
Wanategemea waviziaji wa pale mbele wapige heda

Skills zakuwatoka mabeki solid ka wa barca zilishawatoka
Ndo maana uliona jana strikers wao wanaanguka ovyo wakijaribu kupenya na mpira katikati ya mabeki wa barca
Wanategemea krosi,mikona na ma freekick

Mwisho,hawana players wakucheza ka style yetu ya uchezaji.
 
On the seventh day GOD took a rest,on day eight he created Messi
Mundo_Deportivo.jpg
 
Hili timu limekuja kuwa libovu sana.

Kma spurs alipita hapa kirahirisi, Barca atashindwaje kwa mfano.

Eti naskia mna mtaka na king Conte. pambaneni na hali zenu
 
Mbappe amekiri kwamba alifanya mazungumzo na Real Madrid wakati wa usajili
 
Tetesi
REAL YASAKA MNUNUZI WA RONALDO


Real Madrid ipo tayari kumuuza Cristiano Ronaldo ikiwa itatokea timu yenye dau nono Diario Gol .
Licha ya kuendelea kuongeza mataji kwenye klabu hiyo ya Hispania, kuna hisia ndani ya Santiago Bernabeu kuwa Mreno huyo nguvu zake zinaanza kufifia.
 
Tetesi
SALAH ANATAKA KWENDA REAL


Mohamed Salah anatamani kuihama Liverpool ili aweze kujiunga na Real Madrid, kwa mujibu wa habari kutoka Don Balon .
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Misri amekuwa kwenye kiwango cha kutosha tangu alipotua Anfield majira ya joto, na timu nying kubwa za Ulaya zimeona na kuvutiwa na jitihada zake.
Miamba wa La Liga Real Madrid inaaminika ni miongoni mwa timu zilizopanga foleni kuiwania saini ya nyota huyo wa Kimisri.
 
Back
Top Bottom