Changalucha
JF-Expert Member
- Oct 19, 2011
- 508
- 594
Anaitwa Rehema au Ray?
Kwahiyo viongozi wa wizara ya afya wali teuwa DMO asiyekuwa na akili?Mkuu wa mkoa wa Singida, Rehema Nchimbi amedai alimueka ndani DMO ili apate akili baada kushindwa kutangaza mlipuko wa Kipindupindu japo amedai kuwa alimsikia DMO huyo akilalamika alikuwa hana jinsi ya kumfanya ila ilikuwa ni kumweka mahabusu hali uliopelekea DMO huyo kujiuzulu.
Kauli hii aliitoa jana wakati ni juzi tu Waziri Ummy kapiga marufuku wakuu wa Mikoa na Wilaya kuweka wataalam wa afya na madaktari ndani sasa sijui ni kutunishiana misuli au?
Kibri cha madaraka.Anasahau kwamba kuna siku atakuwa raia wa kawaida na kwamba bado anahitaji madaktari,kama si leo basi ni kesho.Huyu kalewa madaraka
ni ulevi mbaya sana kuliko hata wa ungaHuyu kalewa madaraka
hawa Marc ba madc walipaswa kupewa semina elekezi maana wanafanya vitu vya ajabu sanaKwa hiyo hapo rumande alimlipia na tuition fee kabisa?? Ma RC wa awamu hii vituko tupu!
Nikung'olewa meno yote ya nyuma.Huyo Rehema nchimbi ana wenge na kuweweseka! Jinamizi la yule DR bado analo! Pia ana wenge la kutofanya vizuri hapo Singida......ikitokea reshaffle ya ma RC basi ujue Rehema hatakuwemo! Then akiaj mtaan siku isiyo na jina ataenda hospital kutibiwa yeye au familia yake atakutana na yule Dr......sijui nini kitatokea!!
Utaua mkuuuanapewa flajiri halafu anawekewa dripu ya konyagi...

Kuna siku ataumwa... alaf madaktar watamgomea.. ndio atajua umuhim wao. Tatizo la Rc na ma DC Wa sasa wanafanya kazi kishabiki. Wanataka waonekane...Kibri cha madaraka.Anasahau kwamba kuna siku atakuwa raia wa kawaida na kwamba bado anahitaji madaktari,kama si leo basi ni kesho.
Sidhani kama waziri alipokemea hili la kuwatia ndani wahudumu wa afya kiholela allikuwa hajui atendalo,kwa haraka haraka waziri wa afya ametenda kwa weledi zaidi.
Sheria iko vizuri isipokuwa inatafsiriwa na kutumika vibaya na hasa na ma -RC, DC katika serikali ya awamu hii ya 5. Mambo haya ya kuwaweka mahabusu hovyo watendaji wa serikali hayakuwa hivi awamu zilizotangulia na sheria ni zile zile nafikiri hali hii pia inachangiwa na JPM kufuta semina elekezi kwa wateule wake.Sheria zetu bado ni za kikoloni japo kuwa tunajidai kuwa huru kwa miaka mingi. Hivi huu ujinga wa watanzania kuwa na nguvu ya kuwaweka watanzania wengine ndani bila makosa ya msingi bali utashi wa watawala hii kitu gani. Bora wakoloni walikuwa wanajihami dhidi ya weusi ambao kimsingi kutokana na kuwatawala kimabavu walikuwa maadui. Sasa watwambie uadui wetu na hawa watawala ni upi mpaka wawe na sheria za kujihami kama hizo za kuweka ndani weusi wenzao. Uhuru wa kweli bado sana.
Madaktari wanahitajika sana Kenya, Uganda, South Sudan, Angola Namibia Boswana Swaziland Canada USA lakini mkuu wa mkoa ni hapa tu!
aysee yaan sipati jibu!!...yaan km ndio mie nikitoka huko nitamsaka tu, hata uzeen then nampa vyakeSheria zetu bado ni za kikoloni japo kuwa tunajidai kuwa huru kwa miaka mingi. Hivi huu ujinga wa watanzania kuwa na nguvu ya kuwaweka watanzania wengine ndani bila makosa ya msingi bali utashi wa watawala hii kitu gani. Bora wakoloni walikuwa wanajihami dhidi ya weusi ambao kimsingi kutokana na kuwatawala kimabavu walikuwa maadui. Sasa watwambie uadui wetu na hawa watawala ni upi mpaka wawe na sheria za kujihami kama hizo za kuweka ndani weusi wenzao. Uhuru wa kweli bado sana.
Sheria imefafanua vizuri na ipo hata wakati wa serikali za awamu zilizotangulia na mambo hayakuwa hivi, tatizo lingine ni JPM kuteua watendaji wake na kuwaingiza kazini bila semina elekezi alizozifuta ili kubana matumizi.Majibu ya mlevi wa madaraka! Pamoja na mkwara wa Waziri kuwa Ma-RC/DC wasiwaweke ndani watumishi wa afya, haitasaidia lolote kwa sababu sheria inayowaruhusu kuweka ndani watu kwa muda wa masaa 48 bado ipo na itaendelea kutumiwa vibaya!
Shule ni shule tu, kama huna shule kwa kazi za taaluma, wee ni bure tu, na hapa unatuimbisha kwaya tu! Nyie wenyewe mmediriki kusema RC hahitaji cheti chochote kuteuliwa, ndiyo maana tunashuhudia maamuzi ya ajabu ajabu!Hata ukichukua miaka 10.lakini ukiwa mzembe na mla rushwa hufai