RC Singida: Nilimuweka DMO rumande ili apate akili

RC Singida: Nilimuweka DMO rumande ili apate akili

Sheria zetu bado ni za kikoloni japo kuwa tunajidai kuwa huru kwa miaka mingi. Hivi huu ujinga wa watanzania kuwa na nguvu ya kuwaweka watanzania wengine ndani bila makosa ya msingi bali utashi wa watawala hii kitu gani. Bora wakoloni walikuwa wanajihami dhidi ya weusi ambao kimsingi kutokana na kuwatawala kimabavu walikuwa maadui. Sasa watwambie uadui wetu na hawa watawala ni upi mpaka wawe na sheria za kujihami kama hizo za kuweka ndani weusi wenzao. Uhuru wa kweli bado sana.
Binafsi ninafikiri kuna haja saana ya kutafakari katika nchi huru, wanahitajika viongozi au watawala.
 
huyu mkuu wa mkoa magu awasaidie medical students amlete vyuoni aweweke med students mahabusu akili ziongezeke🙂🙂🙂🙂🙂🙂🙂
 
Mkuu wa mkoa wa Singida, Rehema Nchimbi amedai alimueka ndani DMO ili apate akili baada kushindwa kutangaza mlipuko wa Kipindupindu japo amedai kuwa alimsikia DMO huyo akilalamika alikuwa hana jinsi ya kumfanya ila ilikuwa ni kumweka mahabusu hali uliopelekea DMO huyo kujiuzulu.

Kauli hii aliitoa jana wakati ni juzi tu Waziri Ummy kapiga marufuku wakuu wa Mikoa na Wilaya kuweka wataalam wa afya na madaktari ndani sasa sijui ni kutunishiana misuli au?

Kwa hiyo kama ni utafiti Daktari hana ruhusa ya kutangaza matokeo, lakini ikitokea kuna kipindupindu ndio daktari anaruhusiwa kutangaza hali ya hatari hapa sio mwenyekiti tena wa kamati ya ulinzi na usalama. Ebu acheni tukae kimya kwanza muda wa kazi huu.
 
Awamu hii ya Viwonder ili uonekane mtendaji mzuri lazima usweke watu ndani.
 
!
!
daktari anaweza kuwa mkuu wa wilaya au mkoa hata kesho tu rais akitaka, ni swala la uteuzi tu kama vile mimi ninavyoteua flana gani nivae leo. Ila hata raisi apende vipi Mkuu wa wilaya au mkoa hawezi kuwa Daktari mpaka na mpaka tu aende shule miaka kadhaaaa. Wateule wajifunze kuheshimu kazi za wenzao
 
Kama ni kweli katamka hivyo atumbuliwe haraka
 
Mpaka uwe daktari inachukua miaka mitano chuo ukisoma, mpaka kuwa mkuu wa mkoa inakuchukua miaka mingapi chuo? Ukipata jibu utajua nani hana akili

Akili za darasani au zipi hizo?

Kazi zote anazo fanya DMO alisomea miaka hiyo yote?
 
Ma DC na Ma RC hawana KAZI ndio maana wanatafuta sana kuonekana kwenye TV.
Kumuweka mtaaalamu kama dr lupango ni sawa na kucma wanasiasa hawataugua milele, bila kwenda kutibiwa, vinginevyo umejenga wingu nene na madaktari wote tanzania, tafakari kabla hujatenda faida na hasara
 
!
!
kwa kigezo cha kupata akili kama RC angekuwa na akili, angejiweka yeye kwanza kwasababu nadhani ana vikeibii tu apsteaz
 
Mpaka uwe daktari inachukua miaka mitano chuo ukisoma, mpaka kuwa mkuu wa mkoa inakuchukua miaka mingapi chuo? Ukipata jibu utajua nani hana akili
Kuwa RC inahitaji kuwa na kadi ya chama, elimu hata ukifoji sawa
 
Unataka kuniambia waziri mkuu hana power dhidi ya mkurugenzi kisa wote wameteuliwa na mtu mmoja?
Hana power ya kumfukuza kazi,labda kumsimamisha wakati anamshitaki kwa bosi.
 
Hapo ndipo nawashangaa wanawake wanaomba haki sawa waaminiwe kwenye madaraka matokeo yake mikurupuko naona mwendelezo wa yule dc wa njombe kumpiga kibao diwani unaendelea ngoja muwekwe benchi sijui mtaficha wapi hizo sura
 
Huyo Rehema nchimbi ana wenge na kuweweseka! Jinamizi la yule DR bado analo! Pia ana wenge la kutofanya vizuri hapo Singida......ikitokea reshaffle ya ma RC basi ujue Rehema hatakuwemo! Then akiaj mtaan siku isiyo na jina ataenda hospital kutibiwa yeye au familia yake atakutana na yule Dr......sijui nini kitatokea!!
Anacheza na taaluma, nakumbuka Dr. Baki aliwahi kumfanyinzia RPC aliyemletea pesa za moto. Mbona jamaa alikuwa mdogooo kama kapiriton.
 
Kumuweka mtaaalamu kama dr lupango ni sawa na kucma wanasiasa hawataugua milele, bila kwenda kutibiwa, vinginevyo umejenga wingu nene na madaktari wote tanzania, tafakari kabla hujatenda faida na hasara
Wanatibiwa India
 
wanalewa madaraka hawa wanasiasa, mpuuzi kabisa huyu RC anazadi udaktari ni sawa na kazi kubwabwaja kama yake
 
Back
Top Bottom