RC Singida: Nilimuweka DMO rumande ili apate akili

RC Singida: Nilimuweka DMO rumande ili apate akili

Mwaka jana nilitembelea Botswana nikakuta madaktari wengi ni kutoka Tanzania na tunaheshimiwa sana huko. Sekta ya afya asilimia kubwa ni wataalamu wa kitanzania.
 
kwa serikali hii nivigumu kumwamini hata anaesema "wasiwekwe ndani" maana kila siku ina lake.
 
Hana Akili District Medical Officer (DMO?
Kwa hivyo tuamini kwamba
Amekuwa DMO kwa miujiza.
Naamin kada ya Udaktar ndio moja ya kada unayosota mpaka.
Siasa za Bongo na nam mamlaka ya Mkuu wa Mkoa shida tupu
 
me sijaona cha maana alinachonacho mpaka wampe nafasi iyo na ukifatilia mikoa yote aliyopitia kavuluga ukianzia dodoma,,njombe hata cngida
 
Acha kuchekesha,akili ni uwezo wa kujua,je jiulize kama elimu yako inaendana na daktari? Mkiambiwa mlikimbia umande ina maana hisabati,physics,Chemistry,Biology ni mali hadimu
 
Haya ndiyo maajabu ya viongozi katika utawala wa awamu ya 5,mtu kasoma sayansi masomo magumu ambayo watu wengi wanayaamukia shikamo pengine hata Mkuu mwenyewe wa wilaya yalimshinda kutokana na ugumu wake,mtu kasomea Udaktari kwa miaka kadhaa na akafanya kazi za udaktari mpaka akafikia ngazi ya u DMO,eti Mkuu wa wilaya ana kuja kumuweka lock up ili lock up impe akili,mtu kama huyo akiambiwa Hana akili mwenyewe atakuwa ametukanwa wakati kajitukana mwenyewe?.
 
Mkuu wa mkoa wa Singida, Rehema Nchimbi amedai alimueka ndani DMO ili apate akili baada kushindwa kutangaza mlipuko wa Kipindupindu japo amedai kuwa alimsikia DMO huyo akilalamika alikuwa hana jinsi ya kumfanya ila ilikuwa ni kumweka mahabusu hali uliopelekea DMO huyo kujiuzulu.

Kauli hii aliitoa jana wakati ni juzi tu Waziri Ummy kapiga marufuku wakuu wa Mikoa na Wilaya kuweka wataalam wa afya na madaktari ndani sasa sijui ni kutunishiana misuli au?
Na huyu naye asiudhi watu! Atalipuliwa aombe poo.
 
Kwa sisi wenye field za afya mtaani tuna fulsa nyingi mno, hata mimi ukinizengua narudi kitaa najipanga tu,alichokisema waziri ni sahihi sometimes rumande hazitusaidii sana kuleta ufanisi kwenye kazi.
 
hoja ni hiyo tu uliyoona kwani hauafahamu kuwa kusomea udakitari wa medicine si kuwa na akili kama ulivyodai hapo awali bali unakuwa na akili ya dawa tu au haujui
ukweli unao mwenyewe.....mbona zote gari Ila kuna lorry na sedan....hujui
 
Sio ajabu huyu naye ana kabashite.

Hata ningekua Mimi, ningeweza kutamba kwa kuitambua nafasi yangu na mipaka yangu ya kazi kua hakuna wa kunigusa.

Sasa huyu mkuu kakalia ze majunguzzz.
Anamuweka ndani kwasababu ya maneno.
Haki iko wapi sasa?

Kuna wamama wako na stress sana. Kama huyu.
Hawafai kupewa kazi kama hizi...
Bora wawe mayaya tu.
Huyu mama hana Bashite wewe
 
Kuna dc mmoja tulipishana kibiashara,akaniambia!nisingehamishwa mkoa lazima ningekuweka lockup hata mwezi,wana jeuri hawa wakuu sana kwa sasa,wameota MENO.
 
Sheria zetu bado ni za kikoloni japo kuwa tunajidai kuwa huru kwa miaka mingi. Hivi huu ujinga wa watanzania kuwa na nguvu ya kuwaweka watanzania wengine ndani bila makosa ya msingi bali utashi wa watawala hii kitu gani. Bora wakoloni walikuwa wanajihami dhidi ya weusi ambao kimsingi kutokana na kuwatawala kimabavu walikuwa maadui. Sasa watwambie uadui wetu na hawa watawala ni upi mpaka wawe na sheria za kujihami kama hizo za kuweka ndani weusi wenzao. Uhuru wa kweli bado sana.
Hakuna sheria inayofuatwa zaidi ya watu kutaka kuabudiwa mtu anasoma 5years wewe unateuliwa wengine ndo hao hata vyeti wamenunua unasema unamweka ndani hiki kitu kimeniudhi sana yani na madactari yako kimya hata kutoa sauti sijui wameparalize shame kabisa i wish ningekuwa huyo doctor. I like Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ana hekima na anasikiliza kila mtu hana uchama hata kidogo big up sana. Eti nalimweka ndani ili apate akili wakati yeye kateuliwa
 
Now nimeelewa y ccm wanataka kila mahali waweke makada wao chama cha madactari utakuta wameweka boya, vyama vya wafanyakazi, vya sheria every where so that they can do wat they want without any question. Chama cha sheria wamesikia tu Lisu akili zote zimepata joto asiiiiii y tanzania tunakuwa hivi nani katuloga au umaskini
 
Back
Top Bottom