RC Mtwara: Hali ya Mtwara ni shwari kabisa!

RC Mtwara: Hali ya Mtwara ni shwari kabisa!

licha ya vurugu na patashika iliyotokea leo na inayoendelea katika viunga mbalimbali vya mji wa mtwara, mkuu wa mkoa huo bw.joseph simbakalia amezungumza na wapo radio jioni ya leo akisema kwamba kwa siku nzima ya leo mtwara hali ilikuwa,
shwari kabisa na changamoto zilizotokea ni za kawaida tu.

Source: Wapo radio.
huu ndiyo ujinga wa serikali yetu.
Sasa huyu rc bado anajua kuna watu wa kudanganywa leo hii?


tatizo ni hapo kwenye red kaka.
 
Mabomu yanapigwa hadi usiku huu yeye anasema hali shwari??

Hana maana kabisa
 
Kauli Yake inafanana na sahafi wa Iraq uongo mwingi usio na tija
 
Licha ya vurugu na patashika iliyotokea leo na inayoendelea katika viunga mbalimbali vya mji wa Mtwara, Mkuu wa Mkoa huo Bw.Joseph Simbakalia amezungumza na Wapo Radio jioni ya leo akisema kwamba kwa siku nzima ya leo Mtwara hali ilikuwa,
shwari kabisa na changamoto zilizotokea ni za kawaida tu.

SOURCE: Wapo Radio.
Mkuu usipotoshe.......kama ulisikiliza hadi mwisho wa mahojiano...hakusema kama hali ya Mtwara ni shwari....Tuwe wa kweli........
 
RC anadhani bado tupo enzi za RTD pekee.Hajui kuwa kwa sasa nchi chombo pekee unachoweza kupata habari kwa uharaka ni JF.Ndio maana wana Mtwara wakaamua kuchoma moto nyumba ya TBC Kasim Mikongoro.Mwache afumbe fumbe tu watu tunajua kinachotokea just immediately.
 
Mkuu usipotoshe.......kama ulisikiliza hadi mwisho wa mahojiano...hakusema kama hali ya Mtwara ni shwari....Tuwe wa kweli........
Hebu iweke taarifa vizuri wewe uliyesikia hadi mwisho alisemaje?
 
Waongo utawajua jinsi wanavyojicanganya. Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mtwara, Edward Gontako amethibitisha kutokea ajali iliyoua askari wanne wa JWTZ, 41KJ Nachingwea na askari wengine 20 kujeruhiwa wakati wakielekea Mtwara ili kusaidia kutuliza vurugu hizo.

Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Ligula, Dk Mohamed Kodi amethibitisha kupokea maiti moja na kuomba apewe muda kutaja idadi ya majeruhi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Linus Sinzumwa anadai hakuna mtu aliyefariki dunia wala majeruhi.

Nae Mkuu wa Mkoa Bw.Joseph Simbakalia anadaiwa kusema siku nzima ya jana Mtwara hali ilikuwa
shwari kabisa.

Hawa wote wako Mtwara na wanatakiwa wafanye kazi ka timu moja.

Full kujichanganya.
 
Kauli Yake inafanana na sahafi wa Iraq uongo mwingi usio na tija

Jamani mbavu zangu, msinikumbushe mambo ya Mohammed Saeed al-Sahhaf aka Baghdad Bob, aka Comical Ali, aka Alì il Comico.

<strong>
 
Last edited by a moderator:
Hayo ndio matokeo ya kuwa na Rais dhaifu anayeunda Serikali dhaifu, kusihia kuzungukwa na mkusanyiko wa Viongozi dhaifu. Viongozi wamejijenga mazoea ya kuendesha nchi kwa njia za propaganda.

Wanashindwa kujitambua na kuelewa kuwa siku hizi hata vijijini watu wana cellular phone na wanapata internet.Lakini kama bosi mkuu anapiga propaganda na danganya toto nyingi kwa nini kiranja mdogo kama mkuu wa mkoa asiendeleze chorus the same tunes....
 
Huyu RC Simbakalia si ndie alipewa zawadi na Papa Benedict wa 16 huyo ? Kwa kazi nzuri ya kulifanya kanisa listwani mkoani kwake enzi zile yupo Kigoma ?

Wenye kumbukumbu zaidi, Please !
 
Haa mkuu wa mkoa na mjumbe wa kamati ya siasa ya ccm ya mkoa wa mtwara analinda unga wake usimwagwe kwa kuchonga habari kuhusu mtwara! Duh hatumsahau jk kwa vitimbi vyake!
 
..hivi CDM ndiyo waliosababisha kusini ya Tanzania isitawalike?

..zile propaganda kwamba "wakaskazini" wanataka kujitenga sijui kama zina mashiko tena ukizingatia yanayotokea mikoa ya kusini.

..zaidi, tuliambiwa CDM ni chama cha "kikiristo" na wanamchukia JK kutokana na dini yake. sasa hawa wananchi wa kusini wanampenda JK?


cc: Jasusi, Pasco, Ritz, ZeMarcopolo, THE BIG SHOW
 
Last edited by a moderator:
Huyu RC Simbakalia si ndie alipewa zawadi na Papa Benedict wa 16 huyo ? Kwa kazi nzuri ya kulifanya kanisa listwani mkoani kwake enzi zile yupo Kigoma ?

Wenye kumbukumbu zaidi, Please !
Mkuu,
Maelezo yako yana nusu ukweli na nusu uwongo kabisa.

Ni kweli kwamba Simbakalia alipewa nishani na Papa Benedict wa 16 mwaka jana. Sababu ya kupewa nishani haikuwa kwaajili ya kustawisha kanisa Mkoani kwake, huu ni upotoshaji miongoni mwa wanajamvi.
Ni hatari sana kuandikia au kuelezea kitu usichojua kabisa, ambapo ni sawa na kumwaga sumu kwenye reservoir-tank la mji, maana utaua watu wengi kama si wote.

Kanali Simbakalia alitunukiwa nishani na Papa kutokana na kuwa Mlei Bora wa Mwaka.
Mlei ni Mkristo Mkatoliki ambaye hayuko kwenye daraja la Utume au upakwa mafuta, au kwa maana ingine si Padri au Sista na madaraja mengine ya juu...ni Mkatoliki wa kawaida kabisa.
Vatican ina utaratibu wa kutoa nishani kwa Mlei popote duniani endapo ataonekana kuishi maisha yanayompasa mlei, ikiwa ni pamoja kujitoa kwa ziada katika huduma kwa kanisa. Simbakalia alichaguliwa kwa vigezo hivyo, na si kwa kustawisha kanisa Mkoani Kigoma kama ambavyo post ya hapo juu inavyotaka kuwapeleka watu chakani.

Nadhani nimeeleweka!
 
Aseme ukweli aondolewe huo ukuu wa mkoa? Ndo tz yetu kila kitu ni kusifia tuu nae et mwanaume na ana familia, hiv unaogopa nini kusema ukweli kama kumenuka si unasema? Mi nawachukia watu kama hao watu wanakufa unasema hakuna akiyekufa, lema kasema dhambi kubwa kuliko zote ni uoga, magamba wakamuona mwongo leo tunayaina live. Polen watu wa mtwara na lindi tuko pamoja sana katika hili

Kwao ndo siasa safi! wameendelea kuwaaminisha watanzania ktk siasa za uongo. Wamesahau dunia/tnz ni kijiji. wanaficha uso viuno vinaonekana. Thanks to Lema ' uoga dhambi mbaya sana'.... hata ivyo wenye woga hawataiona mbingu...my bible says.
 
Licha ya vurugu na patashika iliyotokea leo na inayoendelea katika viunga mbalimbali vya mji wa Mtwara, Mkuu wa Mkoa huo Bw.Joseph Simbakalia amezungumza na Wapo Radio jioni ya leo akisema kwamba kwa siku nzima ya leo Mtwara hali ilikuwa,
shwari kabisa na changamoto zilizotokea ni za kawaida tu.

SOURCE: Wapo Radio.

Inawezekana ikawa ni hivyo, na ndo maana bunge jana jioni liliakhirishwa kwa ajili ya kwenda kujadili suala la hali ya utulivu unaendelea kule Mtwara.
 
Wana JF,

Naomba kupewa haki ya kikatiba kwa kupewa habari za huyu Bwana ambae kwasasa ni mkuu wa mkoa wa Mtwara Joseph Simbakalia

Juu ya ;
Uwezo wake kiutendaji kwa wale waliowahi kufanya nae kazi

Imani yake kwa MUNGU na watu wake kwa wale waliowahi/ wanaeishi nae kwenye pwani ile ya Mtwara

Wakubwa wa Magogoni wanamuonaje kuwa ni mtetezi wao ama ni mtetezi wa Taifa zima ?

ANGALIZO;
Alishawahi kuwaita wana Mtwara Wahaini na Wahuni juu ya namna wanavyodai haki zao.

The Fixer,

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom